Title June 2020

MALIPO YA UPOTEVU.

Upotevu una malipo. Pale mtu anapoufahamu ukweli, lakini hataki kuufuata, pale mtu anaposikia kila kukicha acha dhambi, mpe Yesu Maisha yako, dunia hii inakwenda kuisha, dalili zote zinaonyesha, magonjwa ya Tauni Bwana Yesu aliyoyazungumzia kuwa yatatokea nyakati za Mwisho yanaonekana sasa, watu kupenda pesa, watu kupenda anasa kuliko kumpenda Mungu yanaonekana sasa ulimwenguni kote, tetesi za vita, manabii wa uongo kuzuka, Injili kuhubiriwa ulimwenguni kote, Israeli kama mtini kuchipuka tena, yote hayo yameshatimia lakini ni kama kelele kwake..

Mpaka sasa hakuna mtu anayejiita mkristo ajiyejua kuwa tunaishi katika siku za kumalizia, dakika za majeruhi, majira ya parapara kulia, na lakini mtu huyo huyo anayeyafahamu hayo yote hataki kuchukua hatua yoyote rohoni mwake, anaposikia injili anaona ni kama ya watu fulani hivi waliokata tamaa ya Maisha wajulikanao kama walokole, kila siku anasema moyoni “nita”….“nita” nitaacha siku moja, nitatubu siku moja, na huku bado anatazama picha za ngono mitandaoni, anazini, anajijua kabisa yupo upotevuni, lakini bado anaendelea kufanya hivyo, na kusahau kuwa Upotevu huo ulio ndani yake unao malipo yake..

Na malipo yenyewe, sio yale ya kwenda motoni hapana, kabla hujafika huko, Mungu anachofanya kwanza katika Maisha haya ni kukuacha..Ni heri ukaachwa na ulimwengu mzima lakini sio kuachwa na Mungu..ukishaachwa tu wakati huo huo maroho mengine mabaya ya kuzimu yanakuingia, na ndio hapo unajikuta kiwango chako cha kufanya maasi kinaongezeka mara mbili Zaidi, kama ulikuwa ni mwasherati hutaishia kufanya na jinsia tofauti tu, utafika kutamani hata jinsia ya aina yako, au viumbe vingine, au vitu vingine,..hayo ndio malipo ya uovu wako..

Warumi 1:26 “Hivyo Mungu ALIWAACHA wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili;

27 wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, WAKAPATA NAFSINI MWAO MALIPO YA UPOTEVU wao yaliyo haki yao”.

Hapo mstari wa 27 unasema.. wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao..Unadhani walioishia kuwa mashoga walianzia wapi? Walianzia kwenye dhambi ya uzinzi na uasherati lakini wakakataa kumtii Mungu alipokuwa anaugua ndani ya mioyo yao, wakapata malipo ya upotevu wao..Vivyo hivyo na dhambi nyingine zote, huwa zinakwenda hatua nyingine iliyo ovu Zaidi, kama mtu huyo hatataka kumtii Mungu na kubadilika..

Biblia pale inaendelea kusema..

“28 Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.

29 Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya,

30 wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao,

31 wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema;

32 ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao”.

Ndugu tumtii Yesu Kristo ambaye alituokoa bure kwa damu yake. Anatuwazia mawazo yaliyo mema, ikiwa tutamwamini na kutubu dhambi zetu kwa kumaanisha kuziacha yeye mwenyewe atatusafisha na kutusamehe kabisa na kutufanya kuwa wapya tena haijalishi tulimkosea namna gani..

Hivyo Ikiwa leo hii utahitaji kumpa Yesu Maisha yako, basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu katika roho na kweli, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Fanya hayo yaliyo ya msingi na yaliyosalia Bwana atashughulika nayo maishani mwako.

Ubarikiwe sana

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

NDUGU,TUOMBEENI.

MTANGO WA YONA.

HAKI HAIMWACHI KUISHI.

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

MAOMBI YA YABESI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

IMANI NI KUWA NA UHAKIKA WA MAMBO YATARAJIWAYO.

Waebrania 11:1 “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana”.

Hebu tujifunze kitu kuhusu milango mitano ya ufahamu tunayoijua…ambayo ni Pua, ngozi, ulimi, macho na masikio…milango hii kazi yake ni kukupa uhakika au kukujulisha mambo yanayoendelea katika mazingira yanayokuzunguka hata kabla hujayakufikia..

Hebu tuchukue mfano unatembea barabarani kwa miguu na mbele yako umbali wa kama  mita 100 kuna moto mkubwa umewashwa….Sasa kwa kutumia macho yako mawili unaweza kuuona ule moto na kuepukana nao kabla hata hujaufikia…maana yake ni kwamba macho yamekupa uhakika ya hatari itarajiwayo kabla hujaifikia..

Hali kadhalika unaweza ukafumbwa macho lakini kwa kutumia masikio yako ukasikia sauti ya moto ukiteketeza kitu kwa mbali na hivyo ukachukua tahadhari katika hiyo njia unayoiendea kabla hata hujafika eneo la tukio…hapo napo masikio yamekupa uhakika wa hatari uliyopo mbele yako kabla hata hujaifikia.

Sio hilo tu!..unaweza kufumbwa macho na ukazibwa masikio lakini kwa kutumia pua yako unaweza kuunusa moto mita kadhaa mbele kabla hata hujaufikia…ukasikia harufu ya moshi na vitu vinavyoteketea na hata ukajua ni nini kinaungua kama ni takataka au miti au vitu vya plastiki n.k…Lakini ukajua kabisa kuwa kuna moto mkubwa mbele na hivyo ukajihadhari kabla hata hujafika eneo la tukio..

Na pia sio hilo tu peke yake…unaweza ukafumbwa macho, ukazibwa masikio na pua zako zisifanye kazi lakini kwa kutumia ngozi ukapata majibu yale yale ambayo pua, macho na masikio yaliyapata..kwa kutumia ngozi unaweza ukahisi joto linaongezeka kila unapozidi kukaribia tukio na hivyo ukachukua tahadhari aidha ya kusimama au kubadili njia au kuahirisha safari…Na hivyo ukapata uhakika wa hatari inayokuja…

Sasa huo ni mfano tu mmoja  mwepesi ambao umetumia hisia nne..ipo inayotumia hisia zote tano..sasa mfano huo ni unaonyesha ni namna gani inawezekana kabisa kulitambua jambo hata kabla halijafikiwa…ni utashi wa mwili ambao Mungu kamwekea kila mwanadamu kwamba kabla mabaya hayajamfikia kwa ghafla achukue tahadhari…na kama umechunguza Mungu hajamzuia mtu kuifuata hatari..alichofanya ni kumpa hisia za kuihisi kabla haijamfikia au hajaifikia…kujamzuia mtu kuingia kwenye moto unaowaka mbele yake…huo ni uchaguzi wa mtu binafsi…(ukikuta moto unawaka mbele yako na wewe ukajitupa juu yake, huo ni uchaguzi wako). Ukikaa kwenye reli na unaiona Treni inakuja kwa kasi na honi inapiga tangu mbali lakini hutaki kutoka pale, ni uchaguzi wako.

Hali kadhalika biblia imeyafananisha maisha yetu na safari…katika safari yetu ya maisha…Ni roho zetu ndizo zinazosafiri…Miili yetu ipo hapa hapa duniani, inazunguka katika shughuli za kila siku za maisha, lakini roho zetu zinasafiri…Na mbele ya safari yetu (yaani huko tunakoelekea) kuna mambo makubwa mawili 1) MOTO na 2) MBINGU.

Kama vile mwili ulivyo na hisia na Mungu kaziwekea roho zetu hisia vivyo hivyo…Na hisia hizo naamini pia zipo nyingi kama vile hisia za mwili zilivyo nyingi….Hizi hisia za roho ni kutusaidia tujue hatari au baraka zilizopo mbele yetu…na kuchukua uamuzi wa kuziendea au kuzikwepa.

Ndugu mbeleni kuna ziwa la moto…kama hujapewa macho ya kuiona kuzimu katika maono/ndoto, basi Mungu atakujulisha kwa masikio ya rohoni..katika maisha yako utasikia tu habari za kuzimu na ukali wake na zitakupa uhakika kabisa kwamba kuzimu ipo…Hiyo sauti ni lazima utaisikia katika maisha yako….Hali kadhalika kama hutaisikia sauti inayokupa uhakika ya kwamba unalisogelea ziwa la moto…basi utaisiki harufu ya kulikaribia ziwa la moto…na ndio maana katika Maisha yako ya ulevi, ya wizi, ya uasherati, ya kutomcha Mungu, kuna alamu fulani ndani inakuambia kabisa ukiendelea kuishi hivyo utaishia pabaya, hapo ni hisia ya harufu inafanya kazi yake katika roho yako..n.k N.K.

Lakini ukizipuuzia hizo hisia ndugu yangu..na kusema mimi siamini kama kuna kuzimu kwasababu sijawahi kuiona kwa macho…nakuambia ukweli hujawahi kuiona kweli kwa macho yako lakini umeisikia na kuihisi…macho yako yamefumbwa kweli lakini bado hisia nyingine zinakupa uhakika kwamba unaliendea ziwa la moto!…kwasababu huwezi kuuhisi moto mbele yako na kusikia harufu yake na kisha kuzama huko..na kujitetea kwamba hukuuona kwa macho!…ulipaswa uchukue tahadhari kwa kutumia hisia nyingine..ambazo zilikuwa zinakutahadharisha kwamba huko unakoelekea sio!

Ndugu KUZIMU IPO!..Na MBINGU pia IPO!..Ukisubiri uone ndipo uamini utapotea…

Nakushauri kama hujampa Kristo maisha yako au kama bado ni VUGUVUGU hebu chukua muda kasome mistari hii (Ufunuo 3:15-17)...na usiseme nitampa Kristo maisha yangu kesho au nitafanya mabadiliko kesho!…biblia inasema hujui yatakayozaliwa ndani ya siku moja…(Mithali 27:1)..maana yake ni kwamba hata leo unaweza ukafa ghafla au parapanda ya mwisho ikalia..Je utakuwa wapi??..Macho yako hayajaiona mbingu bado…lakini hisia nyingine zilikuambia mbingu ipo….Jiulize Unaposoma ujumbe huu hisia nyingine inakuambia nini?..Je utamlaumu nani siku ile utakapojikuta kwenye ziwa la moto milele?..

Dhambi inavutia sana..na shimo la kuzimu ni kama mtego…hata kabla hujaufikia vizuri ukisema utajikuta limekuvuta ghafla na kuzimu haishibi watu biblia inasema hivyo…Shetani hakupendi hata kidogo..anachokifanya ni kupeleka wengi kuzimu kwasababu anajua yeye hawezi kuokolewa tena!..hivyo anaona wivu kukuona wewe binti/kijana uliyezaliwa tu juzi kukuona utaishi milele..Hivyo geuka leo kwa dhati kama hujageuka, na ukatubu na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu kabla wakati wa hatari haujafika. Mbinguni tumeandaliwa mambo mazuri sana, hata hisia zetu zimeshaanza kuzihisi.

Kumbuka aliyekabidhiwa mamlaka yote ya mbinguni na duniani (yaani Yesu Kristo) anakuja upesi…na anasema maneno haya…

Ufunuo 22.12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.

14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.

15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.

16 Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi.

17 Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye”

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

 Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako,katika kufanya maombezi?

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

USIPUNGUZE MAOMBI.

JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI NI LAZIMA TUFE KWA HABARI YA DHAMBI?.

Tunapaswa tufe kwa habari ya dhambi kwasababu kitendo hicho ni kitendo  kinacholazimisha UHAI wetu kuhamishwa toka pale ulipokuwa kwanza na kwenda sehemu nyingine..

Kama vile tunavyojua siku zote kitu pekee kinachoweza kuuhamisha uhai wa mtu ni Kifo. Ukifa leo hii  Moja kwa moja uhai wako unatoka na kwenda kwingine.., Na hiyo inapelekea watu kutokutujua mahali ulipoelekea, haijalishi watakutafuta vipi kamwe hawatakaa wajue mahali ulipo isipokuwa Mungu peke yake.

Na ndivyo ilivyo pale mtu anapokufa kwa habari ya dhambi, kwa kuzaliwa mara ya pili, Uhai wake unahamishwa na kwenda kuficha na Mungu mwenyewe, mbali na shetani au kitu kingine chochote, kiasi kwamba hata ibilisi akutafuteje rohoni  hawezi kukupata kamwe…

Biblia inasema..

Wakolosai 3:3 “Kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu”.

Unaona, pale tunapokufa ndipo uhai wetu unapofichwa.  Ikiwa tutasema tumeokoka, lakini bado tunaendelea kuyaishi maisha yale yale ya kale, tuwe na uhakika kuwa Mungu hata hana shughuli na uhai wetu..Ikiwa hatutakuwa tayari kuacha uzinzi wetu, uasherati, disko, fashion, matusi, ulevi, ambayo tunafanya mara kwa mara n.k. basi tujue bado shetani anayo mamlaka makubwa sana juu ya uhai wetu..

Anao uwezo wa kututumia vyovyote apendavyo, anao uwezo wa kuyashinda maamuzi yetu, anao uwezo wa kutuletea majaribu ya ajabu ajabu, ikiwemo vifo visivyo vya wakati, anao uwezo wa kuyazuia maombi yetu, anauwezo wa kutufanya tusiyaelewe maandiko. Na zaidi ya yote anakuwa na uwezo wa kuyaingilia maisha yetu kwa viwango kikubwa sana kwa kwa kutumia majeshi ya mapepo yake.

Na ndio hapo utaona, mtu anasema siwezi kushinda dhambi Fulani, siwezi kuacha kuishi maisha Fulani ya dhambi, siwezi kuacha kujichua , Ni kwasababu hakukubali kufa kwanza ili uhai wake uchukuliwe na kwenda kufichwa kwenye moyo wa Mungu.

Mtu aliyefichwa uhai wake, shetani anakuwa haelewi chochote Mungu alichokipanga juu yake, shetani anachofanya ni ku-kisia kisia tu, pengine kesho yake itakuwa hivi au itakuwa vile, lakini haelewi chochote uhai wake unaendelea kuwa moyoni mwa Mungu mbinguni daima, umefichwa huko, ukisubiria wakati maalumu wa kufichuliwa tena.. Kwasababu kitu kinachofichwa ni sharti siku moja kifichuliwe/kifunuliwe.

Na utafunuliwa lini? Biblia inaendelea kusema..

Wakolosai 3:3 “Kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.

4 Kristo atakapofunuliwa, aliye uhai wetu, ndipo na ninyi mtafunuliwa pamoja naye katika utukufu”.

Ipo siku ambayo, watu wote wa Mungu watafahamu kusudi halisi la Mungu kuwaumba ni nini?.. siku watakapoona mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia, siku ambayo watakavikwa miili mipya isiyoharibika na kutawala na Kristo kama wafalme na makuhani milele.. Ni siku isiyokuwa na mfano, Hatupaswi kuikosa hata mmoja wetu.

Na ndio maana biblia inazidi kutuambia..katika

Mithali 4:23 “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima”.

Lakini kama utausoma  tu ujumbe huu au mwingine wowote mfano wa huu, kwa desturi na mazoea ya kila siku, kujitimizia tu ratiba yako, na huku hutaki kufanya badiliko lolote ndani yako, uhai wako bado hauuthamini  upo mikononi mwa ibilisi, ufahamu kuwa kila unalolisikia shetani naye analihesabu na kuliandika,  ili siku ile utakapojikuta katika mitego yake ya hatari ya kukumaliza, awe na hoja za kutosha za kumwambia Mungu ni kwanini hupaswi kupewa msaada.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je! shetani anaweza kuyajua Mawazo ya mtu ,hata kama mtu huyo hatayatamka?

JIWE LA KUKWAZA

KABLA YA MAANGAMIZI, KRISTO HUWA ANAONYESHA KWANZA NJIA YA KUTOROKEA.

KABLA YA MAANGAMIZI, KRISTO HUWA ANAONYESHA KWANZA NJIA YA KUTOROKEA.

CHEMBE YA NGANO ISIPOANGUKA KATIKA NCHI, IKAFA,

Rudi Nyumbani:

Print this post

MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.

Bwana Yesu ndiye Mkuu wa Uzima (Matendo 3:15) Kwasababu alitabiriwa kuwa atakuwa Mkuu Zaidi ya wote..(Luka 1:15)..Na kwasababu hiyo basi Mungu alimpaka Mafuta ya Ukuu kuliko wote (Waebrania 1:9)..na uweza wa ajabu aliuweka juu yake….”Uweza wa kuwaweka huru waliofungwa na uteka wa shetani.(Luka 4:18).. Na kwa jina lake ametupa sisi wote tulio mwamini, mamlaka ya kuzitenda kazi zake zote…na utukufu ule aliokuwa nao ametupa sisi (Yohana 17:22)..Hivyo tuna nguvu kama za Simba zisizokuwa na mwisho, za kufanya makubwa kama aliyoyafanya Mkuu wa Uzima Yesu.

Kwasababu alisema..

Marko 16:17 “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;

18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya”.

Kwasababu hiyo basi mimi kama mmoja wa waliomwamini yeye, na kupewa mamlaka hayo…

  •  Nakuombea Bwana akupe afya katika jina la Yesu Kristo,
  •  Nakuombea Bwana akulinde na yule mwovu, katika kila kitu unachokifanya kinachompendeza yeye.
  • Nakuombea Bwana akufanikishe katika yote katika Jina la Yesu Kristo. 
  • Kama wewe ni mgonjwa, na una ugonjwa ulioshindikana, kuanzia leo ukuondoke na usikurudie tena, katika Jina la Yesu.
  • Kama umefungwa na nguvu za giza, na Kamba za mauti, na roho za mapepo, kuanzia sasa Bwana akufungue katika jina la Yesu.
  • Bwana akupe kibali kila uendako, na kila ufanyacho chenye manufaa kwako na kwa wengine kikafanikiwe wiki hii na mwezi huu unaoanza.
  • Bwana akakupatanishe na maadui zako, na kukupa furaha na amani na watu wote katika Jina la Yesu.
  • Bwana akakuondolee Mashaka yote na hofu na wasiwasi na huzuni..akakupe furaha, utulivu, raha, na akujaze Roho wake Mtakatifu katika Jina la Yesu.
  • Bwana akupe kibali katika yote uliyomwomba na ufanikiwe katika jina la Yesu.
  • Nakuombea neema ya Mungu ya kumjua yeye Zaidi, na kumfahamu na kumfuata yeye ishuke juu yako kwa wingi katika kipindi hichi katika Jina la Yesu.
  • Kila mpango wa Ibilisi uliopangwa dhidi yako, katika mwili wako na dhidi ya wale uwapendao..uondoke saa hii katika Jina la Yesu, na wala usiusikie hata dalili jaribio lolote la kishetani juu ya Maisha yako.

Amini kuwa Ameyafanya hayo yote…Na yatakuwa kama ulivyoamini.

ZABURI 18: 1 “WEWE, BWANA, NGUVU ZANGU, NAKUPENDA SANA; BWANA NI JABALI LANGU, NA BOMA LANGU, NA MWOKOZI WANGU, MUNGU WANGU, MWAMBA WANGU NINAYEMKIMBILIA, NGAO YANGU, NA PEMBE YA WOKOVU WANGU, NA NGOME YANGU”

Maran atha!

Mada Nyinginezo:

MAOMBI YA VITA

YESU MPONYAJI.

KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.

USITOKE NJE YA HIFADHI YA MUNGU.

WAZAZI WA YOHANA NA YAKOBO.

Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?

VITA VYA IMANI NI VITA ENDELEVU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Mtume Paulo alikuwa ni Mrumi, Myahudi au raia wa Tarso?

Je! Mtume Paulo alikuwa ni Mrumi, myahudi au raia wa Tarso? Nachanganyikiwa kusoma pale Paulo anajitaja kama raia wa Rumi tena wa kuzaliwa wakati yeye ni myahudi?…


JIBU: Tukisoma katika matendo tunaona Mtume Paulo akijitambulisha kama yeye ni mwenyeji wa Tarso mji wa Kilkia..

Matendo 21:39 “Paulo akasema, Mimi ni mtu wa Kiyahudi, mtu wa Tarso, mji wa Kilikia, mwenyeji wa mji usiokuwa mnyonge. Nakuomba, nipe ruhusa niseme na wenyeji hawa.

Kama tunavyoweza kusoma hapo ni wazi kuwa mtume Paulo hakuzaliwa Israeli wala Rumi(Italia) Bali alizaliwa mji wa Tarso sehemu ijulikanayo kama Kilikia ambao kwasasa ungekuwepo maeneo ya kusini kidogo mwa Uturuki”.

Hivyo uraia wake wa Rumi aliutolea wapi?

Ifahamike kuwa enzi zile Mtu kuwa Mrumi ulikuwa ni mtu wa daraja la juu sana kuliko raia mwingine wowote chini ya jua, na pia ulikuwa na haki kuliko watu wengine. Kwasababu enzi hizo Ngome ya Rumi ndio iliyokuwa inatawala dunia, hivyo ukiwa raia wa Rumi ulikuwa na raia wa daraja la juu sana.

Kwanza ilikuwa hauruhusiwi kupigwa au kufungwa bila kushtakiwa, tofauti na raia wa mataifa mengine..Kitendo cha kumpiga tu raia waki-Rumi bila kumshitaki adhabu yake ilikuwa kali sana iadha kifungo au kifo wakati mwingine.

Pili raia wa Rumi alikuwa na uwezo wa kukata rufaa, ikiwa hajaridhika na mashtaka aliyohukumiwa nayo, anao uwezo wa kukata rufaa. Tofauti na raia wengine hukumu ikitolewa imetolewa, kama ni kufa utakufa tu, kama adhabu basi utaadhibiwa tu! hakuna cha rufaa. Na hiyo ndio iliyokuwa inawafanya mitume wengi, na watakatifu wengi wauawe wakati wa kanisa la kwanza kwasababu hawakuwa warumi.

Vilevile kwa Rufaa hiyo anao uwezo wa kufikisha mashitaka yake hata kwa kaisari mtawala mkuu mwenyewe kule makao makuu Rumi, ana akasikilizwa na kupewa haki yake.

Na katika nyaraka zao za historia ya Rumi inayonyesha kuwa raia wa Rumi alikuwa anapewa vipaumbele vya kwanza kuingia mikataba mingi ya kisheria pasipo kuwa na vizuizi vingi tofauti na wale wengine..

Hivyo enzi zile kuwa raia wa Rumi ilikuwa ni bahati sana,ni Zaidi ya sasahivi labda mtu kupata uraia wa mataifa makubwa yaliyo endelea.

Vilevile uraia huo ulikuwa unapatikana aidha kwa kuzaliwa au kwa fedha nyingi..Soma.

Matendo 22:27 “Jemadari akaja, akamwuliza, Niambie, u Mrumi? Akasema, Ndiyo.

28 Jemadari akajibu, Mimi nalipata wenyeji huu kwa mali nyingi. Paulo akasema, Na mimi ni Mrumi wa kuzaliwa”.

Sasa tukirudi katika swali Paulo alitolea wapi Uraia wa Rumi wa kuzaliwa angali yeye hakuwa Mrumi wala hakuzaliwa katika taifa la Rumi(Italia) wakati ule?

Biblia inatupa mwanga juu ya mji wa Tarso Paulo aliozaliwa kwamba ulikuwa ni mji USIOKUWA MNYONGE..

Matendo 21:39 “Paulo akasema, Mimi ni mtu wa Kiyahudi, mtu wa Tarso, mji wa Kilikia, mwenyeji wa mji usiokuwa mnyonge. Nakuomba, nipe ruhusa niseme na wenyeji hawa”.

Unaona mji huo wa Taso ambao ulikuwa Upo Kilkia ni mji ambao haukuwa kama miji mingine iliyokuwa chini ya ngome ya kirumi, bali huu ulifanywa kuwa Huru, japo biblia haielezi ni kwasababu gani uliachwa huru, lakini ni mji ambao raia wao waliachwa huru kuchagua uraia wao wenyewe (Ndio maana ya kutokuwa mnyonge)…Na ndipo huko huko Paulo alijipatia uraia wa Rumi wa kuzaliwa.

Jambo lingile la kujifunza ni kuwa japo mtume Paulo alikuwa na uraia wa Rumi na kwamba alikuwa na haki zote za kukataa mashtaka yoyote ya mapigo na vifungo yaliyomkuta, lakini aliruhusu wakati mwingine kupigwa hadi kutoka damu na kutupwa gerezani.. Na mwishoni ndio anajitambulisha kwa waliomshitaki, kuwa yeye ni Mrumi, nao wanaogopa sana.. (Soma Matendo 16:16-40)

Lakini kwa kufanya vile utaona alipata faida mara mbili, kwanza alijiongezea thawabu kwa Mungu kwasababu alipigwa kwa ajili ya ushuhuda wa Kristo, na pili, alimwokoa yule askari wa magereza na familia yake yote.

Hivyo na sisi wakati mwingine tunaweza tukawa na nguvu za kuzuia mashtaka yetu aidha kwa vyeo vyetu au kwa ukubwa wetu, au kwa mamlaka yetu, au kwa kujua kwetu sheria lakini hatupaswi kufanya hivyo kila wakati, isipokuwa tu pale inapopasa tukiwa na sababu maalumu kama ilivyokuwa kwa Paulo wakati walipotaka kumshtaki wampige tena wamuue alipokwenda Yerusalemu, lakini alikataa na kusema mimi ni Mrumi, na akakata rufaa ya kwenda Rumi, si kwa lengo la kwenda kujitetea bali kwa lengo la kwenda kuwafikishia injili watu wa Rumi.(Soma Matendo 22-26 )

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Mtume Paulo alimwabudu malaika aliyetembea naye?

Mtume Paulo alioa?

Mtume Paulo alikuwa na maana gani kusema katika 1Wakorintho 15:31″…NIKAKUFA KILA SIKU?

SIRI YA KUFANIKIWA KWA MTUME PAULO.

Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UTASIMAMA PEKE YAKO SIKU ILE.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe..karibu tujifunze mambo ya msingi katika safari ya haya maisha ya hapa duniani..biblia inasema dunia inapita, pamoja na tamaa zake zote, (1Yohana 2:17). Na siku ya hukumu siku moja itafika na kila mmoja atatoa habari zake mwenyewe…(Warumi 14:12).

Wengi hawajui kuwa siku ya hukumu itakapofika kila mtu atasimama mbele ya kiti cha hukumu akiwa peke yake pasipo mtu mwingine pembeni yake…utakuwa peke yako pasipo mzazi wako pembeni yako, wala dada yako, wala kaka yako, wala ndugu yako yoyote..Wala mzazi wako au ndugu yako hatakuwa na wewe pembeni yake..Kila mmoja atakuwa mwenyewe, na kutoa habari zake mwenyewe.

Kama uliishi maisha yanayostahili hukumu utahukumiwa kivyako, na kuzimu kule ni pa kubwa mno..nafasi ya mtu mmoja hadi nyingine haielezeki…Kuzimu ni kubwa kuliko hii dunia.. sasa hebu tafakari pamoja na idadi yetu yote tuliyopo bado haijajaa hata theluthi ukisafiri tu kilometa kadhaa kutoka hapo ulipo, tayari unakutana na mapori, yasiyo na watu…sasa kuzimu ni kubwa mara nyingi kuliko hii dunia..kiasi kwamba hata idadi yote hiyo inayoingia huko na watakaoingia hata nusu ya robo watakua hawajaijaza…ina nafasi ya kutosha..Biblia imesema kuzimu haishibi wala haitosheki kwa inayoyapokea…

Mithali 30:15 “Mruba anao binti wawili, Waliao, Nipe! Nipe! Kuna vitu vitatu visivyoshiba kamwe, Naam, vinne visivyosema, Basi!

16 KUZIMU; na tumbo lisilozaa; Nchi isiyoshiba maji; na moto usiosema, Basi!”

Kumbuka jambo moja unapokuwa katika mkutano wa Neno la Mungu na katika mkutano huo kuna watu elfu..kumbuka neno hili kwamba Mungu hazungumzi pale na nyie watu elfu kwa pamoja bali anazungumza na wewe binafsi. Huwa anapotoa onyo ni kama anaongea na mtu mmoja na si wengi.. Hebu tuzitafakari kidogo zile amri 10, ambazo Mungu alimpa Musa awape wana wa Israeli… Kila amri utaona ni kama Mungu anazungumza na mtu mmoja. Hebu tusome..

Kutoka 20: 2 “Mimi ni Bwana, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.

3 Usiwe na miungu mingine ila mimi”….

Hapo hasemi Mimi niliyewatoa katika nchi ya Misri..bali mimi “niliyekutoa”…maana yake anazungumza na mtu mmoja na si wengi..

Tukiendelea amri ya pili anasema..

“4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia”…

hapo tena ni vile vile hasema “msijifanyie sanamu za kuchonga”..bali anasema “usijifanyie”..kuonyesha kwamba anazungumza na mtu mmoja na si wengi…kwahiyo unapoona wengi wanasujudia sanamu usiwaige na kusema mbona tupo wengi..ina maana Mungu atatuhukumu wote?…Atakuhukumu wewe peke yako, kwasababu katika amri hii anazungumza na wewe na si wao..Siku ya hukumu hao hawatakuwepo na wewe…wewe utasimama peke yako..

Na amri nyingine zote zilizobakia ni hivyo hivyo…zinasema USIZINI, USIIBE, USIUE…na sio msizini, au msiibe, au msiue….Leo hii unapozini, siku ya hukumu hutasimama na yule uliyekuwa unazini naye….wala hutamwona…Utahukumiwa wewe binafsi na kutupwa kwenye lile ziwa la moto na huko pia utakuwa peke yako..yule uliyekuwa unazini naye hutamwona tena hata huko kuzimu hutasikia sauti yake…utakuwa peke yako.

Shetani lengo lake kubwa ni kuwapeleka watu kuzimu…kwa kuwatumainisha katika wingi wa watu…Kwamba kwasababu tupo wengi tunaofanya hivyo basi Mungu hawezi kutuhukumu wote..siku ile kwa pamoja ataturehemu…ndugu usidanganyike…ikumbuke ile gharika ya Nuhu, pengine wapo waliodhani hivyo kwamba Mungu hawezi kuihukumu dunia na kuifadhi familia mmoja tu ya Nuhu…lakini gharika iliposhuka wote walipotea na sasa hivi wapo kuzimu wakisubiria hukumu ya mwisho na kutupwa katika ziwa la moto..biblia inasema hivyo.

Na pia shetani anapenda kuwafariji watu kuwa hata mtu akifa na kwenda kuzimu leo basi kuna uwezekano wa kuombewa na watakatifu huku duniani na Mungu akakutoa kutoka kule kuzimu na kukuingiza paradiso… huo pia ni uongo wa Adui, usidanganyike!..ukifa leo katika dhambi na ukijikuta kuzimu huko hutoki tena, milele na milele utakuwa umepotea. Utauliza ni wapi imeandikwa hiyo?

Ayubu 7: 9 “Kama vile wingu likomavyo na kutoweka, NI VIVYO HUYO ASHUKAYE KUZIMUNI HATAZUKA TENA KABISA.

10 Hatarudi tena nyumbani kwake, Wala mahali pake hapatamjua tena”.

Binti wa Mungu lisikie hili Neno la Mungu linalokuonya leo..suruali unazovaa, vimini unavyovaa, hereni unazizovaa, ngozi unayojichubua, kwasababu unahisi tu mbona mpo wengi mnaofanya hivyo? Mbona hata mhubiri wako anavaa hivyo?…Sikia leo neno la Mungu…siku ile itakuwa peke yako!! Hatakuwepo mhubiri wako pembeni, wala ndugu yako ambaye alikuwa anavaa kama wewe…wala mimi sitakuwepo!..utakuwa wewe na yeye na kitabu chake cha maneno yake…na kitabu cha maisha yako.

Kijana ambaye unabet, unayeshabikia mipira na kuifanya ndio miungu yako..unapata dakika 90 za kuitazama mpaka inaisha lakini kulitazama neno la Mungu dakika kumi macho yanafumba…Neno linasema “usiwe na miungu mingine ila mimi”..sio msiwe na miungu mingine…Ni wewe ndio unayeambiwa hapo…na pia ni mimi ndiye ninayeambiwa…lakini si wote wawili tunaoambiwa kwa pamoja…

Hivyo tubu leo kama hujatubu…siku ni chache sana zimebaki za kuondoshwa watakatifu wa Mungu ulimwenguni…na saa yoyote ile parapanda ya mwisho italia na watakatifu wataondoshwa kupelekwa mbinguni, kitakachosalia ulimwenguni ni dhiki kuu ya mpinga-kristo na hukumu ya siku ya Bwana inayotisha.

Tubu leo ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, upate ondoleo la dhambi zako na Bwana atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu.

Kuzimu ipo!!

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE WAKRISTO TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA VALENTINE’S DAY?

USISUBIRI MPAKA MUNGU AKUAMBIE, NDIO UFANYE!

Jehanamu ni nini?

NI NANI ALIYEIDHARAU SIKU YA MAMBO MADOGO?.

KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU NA ZA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KAMA MMOJA TU NDIO HIVI! SI ZAIDI 153?

Jina la Bwana wetu Yesu yeye atupendae upeo libarikiwe daima. Nakukaribisha katika kuyatafakari maandiko kama vile tulivyopewa maagizo kwenye biblia kwamba tunapaswa tumjue yeye sana mpaka tufikia kimo cha cheo cha utimilifu wake, ili tusiwe watoto wachanga wa kuchukuliwa na kila aina ya upepo wa elimu (Efeso 4:13-14)

Kuna swali unaweza kujiuliza kwanini Bwana alipowatokea wanafunzi wake siku ile walipokuwa wanavua, tunasoma wanafunzi walivua samaki wengi na wakubwa, ambao jumla yake ilikuwa ni 153. Kwanini idadi itajwe pale? Na kwanini Bwana abakie na samaki mmoja tu kule ufukweni?

Embu tusome ..

Yohana 21:3 “Simoni Petro aliwaambia, Naenda kuvua samaki. Nao wakamwambia, Sisi nasi tutakwenda nawe. Basi wakaondoka, wakapanda chomboni; ila usiku ule hawakupata kitu.

4 Hata asubuhi kulipokucha, Yesu alisimama ufuoni; walakini wanafunzi hawakujua ya kuwa ni Yesu.

5 Basi Yesu akawaambia, Wanangu, mna kitoweo? Wakamjibu, La.

6 Akawaambia, Litupeni jarife upande wa kuume wa chombo, nanyi mtapata. Basi wakatupa; wala sasa hawakuweza kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa samaki.

7 Basi yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akamwambia Petro, Ndiye Bwana. Naye Simoni Petro, aliposikia ya kwamba ni Bwana, akajifunga vazi lake, (maana alikuwa uchi), akajitupa baharini.

8 Na hao wanafunzi wengine wakaja katika mashua; maana hawakuwa mbali na nchi kavu; ila yapata dhiraa mia mbili; huku wakilikokota lile jarife lenye samaki.

9 Basi waliposhuka pwani, wakaona huko moto wa makaa, na juu yake pametiwa samaki, na mkate.

10 Yesu akawaambia, Leteni hapa baadhi ya samaki mliowavua sasa hivi.

11 Basi Simoni Petro akapanda chomboni, akalivuta jarife pwani, limejaa samaki wakubwa, mia hamsini na watatu; na ijapokuwa ni wengi namna hiyo, jarife halikupasuka.

12 Yesu akawaambia, Njoni mfungue kinywa. Wala hakuna mtu katika wale wanafunzi aliyethubutu kumwuliza, U nani wewe? Wakijua ya kuwa ni Bwana.

13 Yesu akaenda akautwaa mkate, akawapa, na samaki vivyo hivyo”.

Kama tunavyoiona habari, Bwana alipowapa maagizo ya kutupa jarife upande wa pili, na kufanikiwa kutoka na samaki wengi vile, Lakini waliporudi pwani walimkuta Bwana pia akiwa na samaki na mkate lakini cha kushangaza zaidi, alikuwa ni samaki MMOJA TU!.

Unaweza kujiuliza ni kwanini awe mmoja tu na si wengi? Halafu utaona pale samaki huyo huyo ndio Bwana aliyewapa wanafunzi wake, pamoja na mkate, soma pale mstari wa 13 vizuri utaona..

Yesu ambaye aliwapa mbinu wanafunzi wake wa kuvua samaki wengi na wakubwa ambao hata nyavu zao hazikuweza kusapoti kwa uzito wa samaki wale ambao walikuwa 153, Huyo huyo ndiye aliyekuwa na samaki mmoja tu pwani akimwandaa vizuri juu ya makaa, huku akiwangojea wanafunzi wake aliowaagiza wakatupe nyavu.

Ni nini Bwana alikuwa anawafundisha wanafunzi wake?

Alikuwa anataka kuwafundisha samaki mmoja jinsi alivyo na thamani kubwa kuliko wao wanavyoweza kudhani.. Mitume walipomla Yule samaki aliyeandaliwa na Bwana mwenyewe utamu waliouona najua ulikuwa ni wa kipekee sana wa kuwaburudisha wao wote, wa kuwafurahisha wao wote,wa kuwabariki hao wote.. Sasa kama ni hivyo si zaidi wale 153 waliowavua?.

Ni zaidi sana watakuwa furaha kwao mara 153. Hivyo Bwana alikuwa anawaonyesha thawabu watakayoipata katika kuifanya kazi yake siku ile mbinguni, na ndio maana Baada ya pale akaanza kumuuliza Petro ambaye ndiye aliyekuwa kiongozi wao..Petro Je! wanipenda? Petro Akasema ndio nakupenda, Bwana akamwambia, Lisha kondoo zangu..Chunga kondoo zangu..

Hata sasa Bwana Yesu anatufundisha sisi, kuifanya kazi yake aliyotuitia hapa duniani ya kuwavua watu kwake waliopotea katika ulimwengu, kazi hiyo sio ya bure bali inayo malipo makubwa sana katika ufalme wa mbinguni.. Laiti kama Bwana angetuonjesha thawabu aliyotuandalia katika mtu mmoja tunapomvuta kwake, tusingetamani kuacha kufanya hivyo usiku na mchana.

Tunapaswa tujiulize karama zetu tulizopewa na Mungu tunazitumiaje kama wakristo..Je! Zinawavuta watu kwa Kristo au zinawaburudisha tu? Tunapoimba hizo nyimbo za injili Je zinawageuza watu au tunazitumia tu kwa ajili ya kupata kipato, na kutafuta umaarufu..Je! Mahubiri yetu yanawaelekeza watu kwa Bwana, au katika biashara na uchumi?..Je! Uchungaji wetu ni wa kulichunga kundi la Mungu au kulitapanya?..

Bwana na yeye anakuliza wewe, Je! wanipenda?? Kama unampenda Basi fahamu kuwa Kristo anahitaji umvulie samaki wengi kwa kadiri alivyokukirimia karama, kama mitume walivyofanya kwa wale 153..Kwasababu thamani ya kondoo mmoja kwa Kristo, inawafanya malaika waruke ruke kule mbinguni kwa furaha na shangwe.

Bwana atubariki na kutushika mkono.

Maran Atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Mariamu Magdalene ni nani. Na hilo jina amelitolea wapi?

VITA VYA IMANI NI VITA ENDELEVU.

MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.

ROHO ZILIZO CHINI YA MADHABAHU:

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIFIKIRI FIKIRI.

Udhaifu shetani anaoupenda kwa mtu ni kufikiri fikiri…Tabia ya kufikiri fikiri inasababisha kupoteza ujasiri, na hata Imani…Kwamfano ukitaka kwenda kukutana na mtu, ukianza kutumia muda mrefu kufikiri fikiri itakuwaje utakapokutana naye …ni rahisi sana kuingiwa na woga na hata kupoteza shabaha ya kile ulichokuwa unakwenda kukifanya au kukisema.

Na katika Imani, kuna vitu vichache vidogo vidogo ambavyo ni vya kuvizingatia vinginevyo utajikuta unakosa ujasiri na utulivu kila mahali na kushindwa kumtumikia Mungu. Roho Mtakatifu anafanya kazi katika utulivu.

Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi maneno haya…

Mathayo 10:16 “Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.

17 Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga;

18 nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa.

19 Lakini hapo watakapowapeleka, MSIFIKIRI-FIKIRI JINSI MTAKAVYOSEMA; maana mtapewa saa ile mtakayosema”.

Hapo Bwana alizungumzia katika eneo la kusimamishwa mbele za washitaki…kwamba hatupaswi kuogopa na kuanza kufikiri namna ya kujitetea au namna ya kujibu…badala yake TUTULIE!! Roho Mtakatifu afanye kazi yake…kwani wakati huo huo ukifika atatupa kinywa cha hekima ambacho kitategua mitego yao yote…

Hali kadhalika wakati wa kuhubiri ni hivyo hivyo..Unapotumwa na Roho Mtakatifu kwenda kusimama na kuhubiri…sio wakati wa kuanza kufikiri fikiri utakwenda kusema nini, nitawezaje kuhubiri muda wote huo uliopangwa, nitawezaje kupangilia maneno, nitawezaje kuombea, nitaaanzaje anzaje kuelezea mstari huu na ule. Ukishaanza kuruhusu hayo mawazo basi jua ni rahisi sana kumzuia Roho asitiririke vizuri ndani yako…

Unachopaswa kufanya baada ya kuliandaa somo, kwamba kuna ufunuo Roho Mtakatifu kakupa, kupitia katika roho yako mwenyewe au kupitia mtumishi wake…na hivyo unasikia kuongozwa kwenda kuwashirikisha wengine…moja kwa moja andaa mistari michache ambayo inashikilia somo lako..baada ya hapo muda uliobakia endelea kuombea mambo mengine…na subiri huo muda ufikie…na utakapofika anza kuzungumza…wakati unazungumza Roho Mtakatifu ataungana na wewe na utajikuta unatiririka kwa namna ambayo hata wewe mwenyewe utajishangaa.

Lakini ukianza kuogopa..na kufikiri fikiri…yule mchungaji anajua kuliko mimi, itakuwaje nikihubiri mbele zake, fulani anajua biblia kuliko mimi itakuwaje…nikikosea itakuwaje, nikiishiwa na maneno katikati itakuwaje…nitaweza kweli kumaliza lisaa lizima nikihubiri?..na sauti yangu hii ya kigugumizi itakuwaje?..nianze na mstari gani nimalize na mstari gani?

Usiwaze yote hayo…wala usiruhusu hivyo vikao vya maswali kuzunguka kichwani kwako…Roho Mtakatifu atakupa kinywa cha hekima saa ile ile utakayokuwa unahubiri. Na baada ya kuhubiri tu utajiona umerudia hali yako ya kawaida…Na kujishangaa umemalizaje lisaa haraka hivyo, umewezaje kupangilia maneno hivyo na si kawaida yako, utashangaa na lile Neno linawageuza watu, na wengine kufunguliwa na kuponywa…ukiona hivyo jua ni Roho Mtakatifu alikuwa kazini…wewe ulitumika tu kama chombo.

Sasa nguvu hiyo ya Roho Mtakatifu huwa inajaa na kupungua ndani ya mtu…lakini haiondoki ndani ya mtu…Mtu anapokuwa katika hali ya shughuli zake za kawaida au amelala inakuwa inapungua…lakini likitokea tu jambo! Huwa inashuka ndani ya mtu kwa nguvu…kwamfano mtu anaposimama kuhubiri, huwa inashuka ndani yake…hapo ndio mtu anajikuta anapata ujasiri wa kipekee, yale mambo aliyokuwa hawezi kuzungumza au kuyafanya anajikuta uwezo fulani umemwingia ghafla wa kuyafanya…au mtu wa Mungu anaposimamishwa mbele ya washtaki mahakamani au penginepo na hajui la kusema…ghafla anashangaa amepata hekima ya kujibu. Nk.

Ndio maana Bwana alisema “tusifikiri fikiri” maana yake ni kwamba upo wakati ambao utajiona huwezi wala hustahili kufanya kitu fulani, ni wakati wa kujiona mdhaifu…wakati huo sio wakati wa kufadhaika, kwasababu yupo Roho Mtakatifu atakayeshuka kukutia nguvu..Kama Mtume Paulo alivyosema kwa uweza wa Roho mahali fulani…

2Wakorintho 12:9 “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana UWEZA WANGU HUTIMILIKA KATIKA UDHAIFU. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu”

Kama ni msomaji wa biblia utakuwa unazijua Habari za Samsoni…Mtu huyu si wakati wote alikuwa na nguvu..na wala biblia haisemi kwamba alikuwa ni mtu mkubwa kuliko wote, au kama Goliathi…alikuwa ni mtu wa kawaida tu…pengine hata alikuwa na misuli ya wastani tu, kama ya wanaume wengine ndio maana ilikuwa ni ngumu watu kujua asili ya nguvu zake ni nini?..kwasababu alionekana kama wengine tu..Sasa kilichokuwa kinatokea kwa Samsoni ni kwamba lilipokuwa linatokea jambo fulani ndipo zile nguvu zilimshukia…Sio wakati wote alikuwa nazo…wakati mwingine wowote alikuwa kama watu wa kawaida mwenye nguvu za wastani…Ila linapotokea jambo aidha maadui wamemzunguka ndipo zile nguvu za Roho Mtakatifu zinamshukia na kumpa uwezo wa ajabu wa kuwaangamiza…na baada ya hapo zile nguvu zinapungua na kurudia kuwa mtu wa kawaida…Mpaka tena wakati mwingine wa tukio..(Kasome habari za Samsoni kwa makini utaligundua hilo).

Sio yeye tu…hata baadhi ya wafalme na Waamuzi katika biblia…Kwamfano Mfalme Sauli, wakati kulipotokea vita katika Israeli na watu wanakosa ujasiri wa vita…ndipo Roho wa Mungu alikuwa anamshukia kwa nguvu na kumpa ujasiri wa ajabu wa kwenda vitani…ambao ulikuwa unawashangaza wengi.

Hivyo kuanzia leo usifikiri fikiri wakati wa kwenda kuifanya kazi ya Mungu kama ulikuwa una tabia hiyo..na sio tu kazi ya Mungu bali hata kazi yoyote ile..maadamu umempa Kristo Maisha yako na umezikabidhisha njia zako kwake..Kwasababu huko unakokwenda yeye atakuwa na wewe, kukupa kinywa, kukupa hekima, kukupa akili, kukupa ufahamu, kukupa uwezo, kukupigania, kukuongoza…Usijipime hapo ulipo akili uliyo nayo, utaishia kupaniki na kuishiwa nguvu, usijipime hekima hapo ulipo sasa…subiri mpaka utakapofika huko ndipo utaona Mkono wa Mungu…na utajua kuwa Mungu yupo na pasipo yeye wewe huwezi kufanya lolote…Hivyo endelea mbele usiangalie kushoto wala kulia..

Kutoka 14:14 “Bwana atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.

15 Bwana akamwambia Musa, Mbona unanililia mimi? Waambie wana wa Israeli waendelee mbele”

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

KWARESMA IPO KIMAANDIKO?

KUWA WEWE.

JE KUHUDUMU KWA NYIMBO ZA INJILI KUKOJE?

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

YEZEBELI ALIKUWA NANI

Rudi Nyumbani:

Print this post

UFALME WAKO UJE.

Shalom,

Bwana Yesu alituambia tusalipo tuseme hivi..

Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, UFALME WAKO UJE,..

Ni kweli, tunajua kuwa siku moja ufalme wake utakuja duniani..Lakini upande wa pili wa shilingi yaani sisi tunaousubiria ufalme huo unadhani tungepaswa tuwe katika hali gani?..Nadhani ulishawahi kujikuta katika hali ya kumsubiria mtu au kitu mahali Fulani halafu kwa bahati mbaya kikachelewa/akachelewa kidogo, ile hali unatakayokuwa nayo wakati ule bila shaka si ya kawaida, dakika tano tu utaziona kama ni lisaa limoja limepita, na ndio maana kila sekunde utampigia simu kumuuliza umefika wapi? Mbona sikuoni? Fanya haraka bwana!, Kimbia au chukua pikipiki,, nimesimama hapa muda mrefu nakungoja tu sikuoni? Ni nini kimekukumba? Umekwama wapi? ..n.k.. Unaona Hiyo yote ni kumuharakisha ili tu afike, kwasababu kusubiri kunaumiza.

Lakini haiwezekani ukasema unamsubiria mtu, halafu masaa matatu yanapita, na bado huna hata wasiwasi, humpigii simu kumuuliza hata amefika wapi, au huna hata mpango wa kuulizia atafika saa ngapi, wewe umesimama tu unasema unamngoja, ni wazi kuwa hilo jambo haliwezekani vingenevyo utakuwa na shughuli zako nyingine za kando.

Na ndicho hicho Mungu anachotaka kuona kutoka kwetu, sisi tunaosema tunamngojea Bwana, ni lazima tuwe tunamkumbusha juu ya siku ile ya kuja aihimize ifike haraka, UFALME WAKE UJE HARAKA! (upesi)..Ndugu hichi ni kipengele muhimu sana ambacho Mungu anatazamia kila mkristo wa kweli aliyezaliwa mara ya pili awe anamwomba yeye daima, na ndio maana Bwana Yesu alikiweka katika sala hiyo ya msingi.

Kipimo kizuri cha kujitambua kama kweli umejiweka tayari kwa ajili ya kwenda mbinguni au La, basi ni kwenye kipengele hichi, Jipime je! Ndani yako ipo ile shauku ya kutamani siku ile ya mwisho ifike au La?. Kama haipo basi ujue hata unyakuo ukipita leo hii huendi popote, utabaki tu hapa duniani.

Ni kama tu Mwanafunzi shuleni, yule aliyejiandaa vizuri na mtihani wa mwisho, pale anapokumbuka tu mtihani wa taifa unakuja, huwa anatamani siku hizo zifike haraka amalize zake akapumzike, lakini yule ambaye hajajiandaa, utaona yeye ni kinyume chake, atatamani hata muda uzidi kuongezwa tu wa kuendelea kubaki shule…kwasababu hakujua kilichompeleka shuleni.

Na sisi kama wakristo wapitaji hapa duniani Bwana anatazamia, kila siku tunapoamka tunapolala tunapaswa tumwombe, tutamani na tumkumbushe jambo hilo, kuwa siku ile ya kwenda zetu kwa Baba mbinguni ifike haraka. Aharikishe neema ya wokovu ya kuwaokoa watu wake, mambo yaishe haraka tukapumzike kwake milele. Siku ya unyakuo, siku ile ambayo tutamwona Bwana wetu Yesu uso kwa uso mawinguni ifike!, Tukaile ile karama ya mwanakondoo na malaika mbinguni tuliyoandaliwa tangu zamani.

Siku ambayo tutaiona mbingu mpya na nchi mpya, kwa mara ya kwanza ikishuka ambayo haitakuwa na machozi tena, wala misiba, wala magonjwa, wala vita, wala matetemeko, wala chuki, wala mashindano, wala mahangaiko ya dunia hii, wala umaskini, wala ubaguzi.. siku hiyo tunaiomba na tunaitamani ifike.

Hili ni jambo ambalo kila siku tunatakiwa tumwombe Mungu, Unaweza ukaliona halina thamani machoni pako, lakini mbele za Mungu lina maana sana.. Lakini sisi tukiwa kila mara tunapomwendea Mungu ni kuomba tu magari, nyumba, biashara, wake, kila siku mambo ya kiduniani tu ndiyo tunayompelekea yeye….Hatuna muda wa kutafakari kuwa hii dunia inafika mwisho, na dunia inapita (1Yohana 2:17) Tujue kuwa Mungu anatuona kama hatujastahili kuurithi ufalme wake. Tupo tu.

Anza leo kujijengea desturi hii, ya kumhimiza Mungu, juu ya ufalme wake, aliotuahidia tangu zamani uje haraka ulimwenguni, Na hiyo ni ndio inayothibitisha kuwa kweli tunatamani unyakuo ufike haraka, kweli tunatamani kufutwa machozi, Hizo ndizo hoja zenye nguvu kwa Mungu wetu.

Kama tu viumbe vyenyewe (swala, twiga, mbwa, tausi, punda, ng’ombe n.k.) wanatazamia kwa shauku siku hiyo ya sisi kutukuzwa, inakupasaje wewe na mimi? Ambao ndio warithi wenyewe..Tunapaswa macho yetu yaelekee kule Zaidi.

Warumi 8:18 “Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu kama utukufu ule utakaofunuliwa kwetu.

19 Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu.

20 Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili; si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye atiyevitiisha katika tumaini”.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JIFUNZE KUELEWA MAANA YA KUOA/KUOLEWA KABLA YA KUINGIA HUKO.

JINSI DHAMBI INAVYOMGHARIMU MTU SANA.

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?

JIBU: Mungu anaweza kuzungumza na mtu moja kwa moja, au akatumia malaika wake kumpa mtu ujumbe au akamtumia mwanadamu…na mara chache sana anaweza kutumia hata wanyama (Hesabu 22:30). Au vitu vya asili (Ayubu 12:7-9).

Sasa wanadamu na wanyama ni viumbe wa mwilini, Mungu hawezi kuzitumia roho zao kuzungumza na sisi…kwamfano Mungu hawezi kutumia roho yangu au ya mtu fulani kuzungumza na roho ya mtu mwingine…akitaka kuzungumza na mtu, atampa ujumbe katika roho, mtumishi wake, kisha huyo mtumishi atautoa huo ujumbe kwa mhusika. Ni Roho Mtakatifu pekee na Malaika watakatifu ndio wenye huo uwezo wa kuzungumza na sisi kwa njia hiyo ya rohoni kwasababu wao ni wa rohoni..

Malaika anaweza kuonekana kama mtu na kumpa mtu ujumbe na vile vile anaweza kuzungumza na mtu moja kwa moja kwenye roho yake bila kutumtokea wala kuonekana.

Jambo la muhimu la kufahamu ni kwamba…Malaika wa Mungu hawazungumzi kitu kama watakavyo wao…kila wanachokisema au kila ujumbe wanaotupa ni ujumbe kutoka kwa Roho Mtakatifu kama ulivyo (haujaongezwa wala kupunguzwa). Kwahiyo sauti zao ni sauti za Roho Mtakatifu mwenyewe…Ikiwa na maana kuwa Malaika anapozungumza na wewe rohoni, ujue kuwa ni Roho Mtakatifu anazungumza na wewe, kwasababu Malaika anazungumza kitu alichoambiwa na Roho Mtakatifu akiseme vile vile.

Kwamfano hebu tusome mistari michache ifuatayo..

Mwanzo 22:10 “Ibrahimu akanyosha mkono wake, akakitwaa kisu ili amchinje mwanawe.

11 Ndipo MALAIKA WA BWANA AKAMWITA KUTOKA MBINGUNI, AKASEMA, IBRAHIMU! IBRAHIMU! NAYE AKASEMA, MIMI HAPA.

12 Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee.

13 Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.

14 Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire,kama watu wasemavyo hata leo,Katika mlima wa BWANA itapatikana.

15 MALAIKA WA BWANA AKAMWITA IBRAHIMU MARA YA PILI KUTOKA MBINGUNI

16 akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,

17 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao”

Umeona katika tukio hilo…hapo ni Malaika wa Bwana anazungumza na Ibrahimu kama Mungu mwenyewe…kiasi kwamba ni ngumu kujua kama huyo ni Malaika au Mungu anayezungumza hapo..

Tusome tena..

Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu.

2 MALAIKA WA BWANA AKAMTOKEA, KATIKA MWALI WA MOTO uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea. 3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei

4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.

5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.

6 TENA AKASEMA, MIMI NI MUNGU WA BABA YAKO, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu”.

Wengi wetu tunaijua hii habari ya Musa kuona kijiti kilichokuwa kinaungua lakini hakiteketei, na wengi wetu tunajua kwamba ni Mungu ndiye aliyemtokea Musa…lakini kiuhalisia sio Mungu aliyemtokea Musa…Bali ni Malaika wa Mungu ambaye alibeba maneno ya Mungu kama yalivyo, ndiye aliyemtokea Musa katika kile kijiti kilichokuwa kinawaka lakini hakiteketeiSiku zote Malaika anapotoa ujumbe ni kama tu msemaji wa Raisi anayesoma waraka wa Raisi mbele ya watu..atasoma mpaka sahihi ya mwisho iliyoandikwa (mimi Raisi nimesema haya yote yaafanyike)!…

Tusome tena..

Waamuzi 2:1 “Kisha malaika wa Bwana alikwea juu kutoka Gilgali kwenda Bokimu. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi”.

Umeona na hapo? Malaika anasema “Mimi nimewatoa Misri na kuwaleta katika nchi niliyowaapia baba zenu,…milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi”. Ukitafakari hakuna mahali popote Malaika alishaingia agano na wana wa Israeli, ni Mungu ndiye aliyeingia agano na wana wa Israeli..Kwahiyo hapa ni Malaika anazungumza ujumbe wa Mungu, ni kama vile anarudia kuzungumza kile kitu Mungu alichomwambia azungumze..(Ni kama vile anasoma waraka).

Malaika mara nyingi hawana hichi kitu cha “Mungu kasema”…wenyewe wanarudia kuzungumza kile Mungu alichokisema…Hivyo hiyo inafanya kuwa ngumu sana kuitofautisha sauti ya Roho Mtakatifu na ya malaika…Kwani Malaika atakapozungumza nawe katika roho yako hatasema…Mungu kasema fanya hivi au vile….utasikia tu sauti inasema “Mimi Bwana nimesema”..na wewe unaweza kudhani ni Bwana kazungumza nawe kumbe ni Malaika wake.

Sasa kilicho cha muhimu sio kutafuta kujua kuzitofautisha hizi sauti kwasababu haisaidii chochote…kilicho cha muhimu ni kujifunza kutii kile unachoambiwa…iwe ni Roho Matakatifu kazungumza kupitia kinywa cha malaika au kazungumza yeye mwenyewe moja kwa moja…kilicho cha muhimu na maana kwetu ni kukitii kile tulichokisikia maadamu tumehikiki ni Ujumbe kutoka kwa Mungu…

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Je! kuchora tattoo ni dhambi?

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

USIPUNGUZE MAOMBI.

SHETANI ANAITHAMINI HATA MAITI YAKO.

IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

Rudi Nyumbani:

Print this post