Title June 2020

SHETANI ANAITHAMINI HATA MAITI YAKO.

Biblia inatupa mwangaza wa jinsi shetani alivyomaanisha kweli kuwaangamiza wanadamu japokuwa sisi hatulijui hilo.. Unaweza ukadhani siku ukifa tu, ndio basi shetani anakuwa amemalizana na wewe. Huo mtazamo ni wakuuondoa kabisa kichwani..

Embu jaribu kifirikia kile kisa cha Musa, baada ya Kufa, ni nini kilitokea baadaye?..

Utasoma kwenye kitabu cha Yuda, Malaika Mikaeli alikuwa akihojiana naye sana na juu ya mwili wa Musa.. Tusome..

Yuda 1:9 “Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee.

Kumbuka hiyo ni baada ya Mungu kumuona Musa ni mwaminifu na amevipiga vita vyema, mwendo ameumaliza, na Imani ameilinda, Na sasa baada ya kufa Mungu anampa maagizo malaika Mikaeli amchue aende kumzika mahali pa siri pasipojulikana na watu (Soma Kumbukumbu 34:5-6).. Lakini shetani kwa kulijua hilo kuwa hawezi kumpata Musa tena, hawezi kumletea tena jaribu ili atende dhambi amshinde kwani roho yake tayari haipo pale ilishamtoka na kwenda sehemu nyingine siku nyingi..

Lakini yeye bado aliona fursa ya kuushitaki na mwili wa Musa pia, alitaka Mungu auache tu ardhini, alitaka usizikwe kipekee vile na Mungu, au alitaka aupate yeye kwa shughuli zake za kuwapotosha watu waabudu mahali alipozikwa, au mifupa yake….shetani japokuwa alijua ni muozo tu ule, na mavumbi, lakini hata hilo alililia apewe, bado anashughuli nao.

Alikuwa anahojiana na Mikaeli, pengine kwa kumwonyesha ubaya wake aliokuwa anaufanya duniani au madhaifu yake, kama alivyokuwa anamshitaki Ayubu ili tu Mungu aghahiri asizike mwili wake kipekee..Lakini tunasoma alishindwa kwasababu Musa alikuwa ni mtakatifu wa Mungu.

Sasa tujiulize, ikiwa maiti tu ya mtakatifu, ibilisi anaigombania, mfano tu wa wale askari walioligombani vazi la Yesu pale msalabani, ambalo walijua halikuwa na faida yoyote kwao,..Sisi je tutawezaje kumkwepa kirahisi huyu adui wa roho zetu ikiwa hatutakuwa milki ya YESU KRISTO?

Shetani haitaki tu roho yako, ingekuwa heri aishie hapo ..Lakini Akishaipata bado atataka na familia yako pia, atataka na afya yako, atataka na watoto wako, atataka na nyumba yako, na mali zako ulizozitaabia… pengine, atapelekea mashitaka mbinguni kuwa hata hizo nguo unazovaa ni mali yake.. Na siku ile ukifa hata huo mwili wako, pia atautaka kwa Mungu..Sasa jiulize ikiwa wewe ni mwenye dhambi ni nini kitamshawishi Mungu asimpe vyote hivyo?

Ndio hapo Kaburi lako badala lilindwe na Mungu, ndio shetani analifanya kuwa VILINGE VYA WACHAWI WAKE, mwili wako uliozikwa kwa heshima na wabunge wenzake, unafukuliwa na wachawi ili kuchukuliwa viungo ambavyo vitawasaidia katika shughuli zao za kiganga..Si ni kwasababu wewe ni mali yake?..shetani kashinda hoja mbinguni juu yako…anazo point za kutosha za kupewa mwili wako, na Mungu ni Mungu wa haki, anahojiana na shetani na vile vile pia anampa haki zake kama anastahili.

Hata sasa bado ukiwa hai, hivyo vyote ulivyonavyo shetani anavijengea hoja kwa Mungu, kwanini visiwe vyake?….Umetoka kuzini, na umeshajua Neno la Mungu linakataza kufanya hivyo, unatoka asubuhi unakwenda kazini..wakati upo njiani shetani kashafika mbele za Mungu na kusema…mwangalie Yule mtu ambaye unasema ni mtumishi wako ametoka kuzini..na masaa chache tu alitoka kulisoma neno lako linalomwambia usizini..hivyo huyu ni wangu, nataka nimtumie majeshi ya mapepo nimuue!…na malaika wa Mungu wanapojaribu kutafuta hoja mbili tatu za kukutetea wanapokosa..shetani anapewa haki yake, na wewe unakabidhiwa chini ya mikono yake..kwasababu ni wake yeye…

hivyo unajikuta unapata matatizo ambayo si ya kawaida..

Ndugu haya mambo sio hadithi za kutunga ni vitu vinavyoendelea katika roho kabisa…Je unajua tafsiri ya jina “shetani”?…Shetani maana yake ni “mchongezi/mshtaki” biblia imetoa tafsiri yake hiyo…Hivyo kazi yake ni kukuchongea mbele za Mungu..hata unapochukia tu, tayari kashafika mbele za Baba kupeleka mashtaka..Hivyo sio wa kujiungamanisha naye kabisa.

Unaweza kuona tupo hatari kubwa kiasi gani ndugu yangu.. Ulimwengu huu ni wa mashaka na hofu ikiwa tu Yesu Kristo sio kimbilio lako. Aliposema pale Yohana 17:15 “Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu” . Alimaanisha kweli wale wanaomkimbilia watalindwa na Yule mwovu shetani, mshitaki wao.

Hivyo yasalimishe maisha yako leo kwa Kristo, ndani ya hichi kipindi kifupi tulichobakiwa kabla Kristo hajarudi. Dalili zote zinathibitisha Unyakuo ni wakati wowote,..Na shetani hilo analijua na ndio maana na yeye anafanya kazi sana kwasababu anajua muda wake ni mchache..

Hivyo ingia zizini mwa Bwana kama bado upo nje. Tubu dhambi zako kwa kumaanisha kweli kuziacha, nenda kabatizwe kama ulikuwa hujafanya hivyo katika ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu Kristo ambalo ndio jina la Baba, mwana na Roho Mtakatifu. Kisha utapokea Roho Mtakatifu ambaye ndiye atakayokusaidia na kukulinda hadi siku ile ya mwisho.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MTU ASIYE PAMOJA NAMI YU KINYUME CHANGU.

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?

 

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

Kwanini Kristo hakuitwa Imanueli badala yake akaitwa Yesu?

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.

Mathayo 17:21 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]

Kuna mambo ambayo kamwe hayawezi kutokea bila kufunga…Neno “kufunga” maana yake ni “kutokuruhusu kitu kiingie wala kitoke sehemu fulani”…..kwamfano kuku ili aweze kuwa na Watoto hana budi kupitia kipindi cha mfungo wa siku 21, kutaga mayai sio kuwa na Watoto, bado kuna kazi nyingine ya ziada…itambidi, ajizuie kula, ajizuie kuzurura-zurura mitaani…ajizuie kucheza na wenzake..ili asilipoteze lile joto, vinginevyo akiwa mzembe mayai yatakuwa viza..na ndege wote wa angani ni hivyo hivyo, upo wakati itawabidi waliache anga kidogo, wajifungie ndani kutamia mayai yao.

Na sio tu mfungo wa kutokujizuia kula unahitajika ili kuumba jambo jipya…bali pia mfungo wa Maisha…kwamfano ili mwanafunzi aweze kufanya vizuri katika mitihani yake…hana budi kufunga milango fulani fulani…atakwenda shule ya bweni (huko tayari ni kifungoni)..atakaa huko miezi hata 6 bila kutoka hata nje ya uzio wa shule, mbali na wazazi wake na ndugu zake, na mafariki zake wa mtaani…ni kama tu kuku aliyeko bandani, sio hilo tu peke yake, itamlazimu aache matumizi ya simu, tv, aache kuangalia tamthilia hizi au zile, movie, aache kabisa kuzurura…itambidi kila siku za muda wake wa masomo aishi Maisha ya kuitumikia elimu..ataamka mapema asubuhi, atachelewa kulala…Sasa anafanya hayo ili asilipoteze lile joto…

Kwasababu anajua akishika mambo mawili au Zaidi kwa wakati mmoja…hatafaulu…kichwa hicho hicho kimoja akikijaza tamthilia, movie na miziki na wakati huo huo masomo…HATAFAULU!…Kwahiyo ni bora aache kimoja afuate kingine…Na Zaidi ya yote anakuwa radhi kuvumilia vyakula vibovu vya shuleni mpaka anahitimu ili tu apate anachokitafuta…

Vivyo hivyo…na katika Imani…hatuna budi kufunga baadhi ya mambo ili TUPATE YALIYO BORA!…Utasema mimi miaka yote nimeshindwa kuushinda uasherati…ni kwasababu haujaamua kuutoa maishani mwako…bado hujafunga baadhi ya milango!…Mbona wengine waliookoka wanaweza kwanini wewe ushindwe?..maana yake tatizo lipo kwako sio kwa Mungu wako!….Hujafunga hiyo milango ya uasherati…bado kuna vimelea vinavyokuchochea wewe kuendelea kuwa hivyo ulivyo…na hivyo si vingine Zaidi ya kampani ulizonazo, au picha unazoziangalia, au mazungumzo unayoyazungumza kila wakati yenye maudhui ya kizinzi, au mitandao unayoitembelea, au mtu unayeishi naye…Kama ukifunga kweli kweli na ukamaanisha kuutafuta uso wa Mungu…hayo mambo hayatakuendesha kamwe!!…

Kwanini hulielewi Neno la Mungu unapolisoma na huku umeshaokoka?… ni tabia tu uliyonayo!…na sababu zake ni zile zile za kwanini mwanafunzi haelewi anaposoma…Ni kwasababu hajaamua kuacha kila kitu na kuongeza umakini kwa kile anachokisoma….Utaona anafungua tu kitabu na kusoma Mada iliyopo katikati ya kitabu, halafu analalamika haelewi…sasa ataelewa vipi?..na wakati mada za kwanza zilipokuwa zinafundishwa darasani yeye alikuwa anacheza huko nje wakati wenzake wanasoma?…

Hali kadhalika utaelewa vipi kitabu cha Yeremia wakati madarasa ya biblia yanayofundishwa makanisani huudhurii??..Hujawahi hata kukisoma kitabu cha Mwanzo peke yako na kukimaliza…utakielewa vipi kitabu cha kutoka?…wakati wa asubuhi au jioni wa utulivu ambao ungetakiwa kukaa chini kwa bidii yako mwenyewe kusoma Biblia…wakati huo ndio unafungua whatsapp na facebook?, kusoma Habari za kidunia??…halafu unalalamika hulielewi neno?…Nakuambia ukweli biblia ni kitabu kirahisi sana kukielewa kuliko vitabu vyote endapo tu, tutaamua kumtii Mungu na kuzingatia kulisoma Neno lake kwa bidii…

kwasababu Roho Mtakatifu yupo kutusaidia kulielewa, kwahiyo kazi inakuwa rahisi sana…

Lakini kama Maisha yako hutajishughulisha kutenga muda kusoma Neno lako mwenyewe, angalau kuanzia kitabu cha Mwanzo, ukatulia, ukasoma hatua kwa hatua..bila kutegemea kufundishwa na mtu…utajikuta ufahamu wako unakuwa kwa haraka sana…na KUZALISHA KITU KIPYA KATIKA MAISHA. Lakini ukipalilia tabia ya kutolisoma kwa bidii Neno, hautazalisha chochote…

Hivyo funga leo vitu ambavyo ulikuwa umeviachia mlango wazi katika Maisha yako, ambavyo vinazuia wewe kutoivisha kitu chochote kipya!…matamthilia ya Kikorea, ya ki-Nigeria, ya-Kifilipino, ya Ki-hindi na mamovie yote pamoja na MIPIRA!…ni mambo yanayoondoa joto la Maisha yako ya kiroho, Jitenge achana nayo Jiondokee..…Wewe utaona unajifurahisha tu, lakini katika roho mayai uliokuwa unayatamia yanazidi kupoa na kuwa viza!…kwasababu tulivyoumbwa hatuwezi kushikilia mambo mawili kwa wakati mmoja.

Je Umewahi kuwasikia watu wanaosema “Ngoja nikatazame tamthilia fulani nipoteze mawazo au ngoja nikatazame movie au mpira nipoteze mawazo au kupunguza stress?”…. umewahi kujiuliza kwanini wanahusisha na neno “kuondoa stress au kupunguza mawazo”?….Ni kwasababu ni kweli wanapokwenda kutazama hayo mambo yanasababisha kile kitu ambacho kilikuwa kimeingia ndani ya mioyo yao kipotee, hivyo kama wakiendelea kujiburudisha hivyo kwa kipindi fulani hatimaye kile kitu ambacho kilikuwa kinawaumiza kichwa kinamezwa na zile burudani….Hali kadhalika kama mtu alikuwa ametoka kusoma Neno vizuri na kulielewa…ile ni mbegu inakuwa imepandwa ndani yake….Lakini sasa anapotoka na kwenda kutazama vichekesho, au mipira, au movie, au tamthilia wakati wote au kuhudhuria hudhuria party party zisizo za muhimu, kidogo kidogo kile kilichopandwa ndani yake kinaanza kujizika….hata kama hapendi! Kitapotea tu!..na baada ya kipindi kupita atajikuta kakisahau kabisa….

Hivyo tunajukumu zito la kulinda kile kilichowekwa ndani yetu na Mungu ili tupate kile tunachokitafuta kumbuka biblia tena hili Neno.

“namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga”.

Nyakati hizi ni za mwisho. Tukaze mwendo tuufikie mwisho mwema wenye mafanikio.

Kwani biblia inasema.. “Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako. (Ufunuo 3:11) ”…

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

JIEPUSHE NA MASHINDANO YA DINI.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

DUNIANI MNAYO DHIKI.

ALIYOKUTANA NAYO YESU, YERIKO.

WANA JUHUDI KWA AJILI YA MUNGU, LAKINI SI KATIKA MAARIFA.

MIJI YA MAKIMBILIO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.

Ndoto ni eneo ambalo watu wengi wanadanganywa na kupotoshwa Na hiyo yote ni kutokana na kukosa maarifa ya kutosha. Wapo watu wengi mitandaoni, wanaowaeleza watu tafsiri za ndoto mbalimbali zao na mwisho wanaambatanisha na dawa zao za kibishara wakiwadanganya watu kuwa hizo zitaleta suluhisho la matatizo yao.

Wengi wa hao watu kama si wafanyabiashara basi ni waganga wa kienyeji na hawana lolote la kukusaidia zaidi ya kukuongezea matatizo. Kumbuka Ndoto si tatizo la kimwili hivyo hakuna tiba yoyote ya kimwili kama vile dawa ya kunywa au ya kumeza itakayoweza kuleta suluhisho la ndoto zako.

Kwa ufupi Zipo ndoto za aina tatu, 

  1. Zinazotokana na Mungu:
  2. Zinazotokana na shetani
  3. Zinazotokana na mtu mwenyewe.

Ndoto zinazotokana na Mungu zinachukua sehemu ndogo sana ya ndoto zote mtu anazoota kila siku naweza kusema hata asilimia 5 tu ya ndoto zote ulizowahi kuota,..

Vivyo hivyo na za shetani nazo hazina asilimia kubwa ya ndoto unazoziota mara kwa mara.

Lakini ndoto zinazotokana na mtu mwenyewe hizi ndizo zinazochukua sehemu kubwa ya ulimwengu wa ndoto za wanadamu. Na hapa ndipo watu wengi wanapokosa shabaha, wakidhani kila ndoto tu wanayoita ni lazima iwe na tafsiri, au ni lazima iwe imebeba ujumbe maalum.

Sasa hizo aina mbili za kwanza, (yaani ndoto za Mungu, na za Shetani) huwa zinabeba maana kubwa sana rohoni, ili kufahamu jinsi ya kuweza kuzitambua aina hizi za ndoto  fungua hapa..>>> Tofauti kati ya ndoto za Mungu na Shetani

Leo hii nitajikita kuorodheshea baadhi ya ndoto ambazo watu wengi wanaota na hawajui nyingi kati ya hizo zinatokana na mwili wenyewe..

Ukiota Hizi  uzipuuzie, wala usihangaike kutafuta maana zake, kwasabu hizi huwa zinakuja aidha kutokana na shughuli nyingi..

  • Kwamfano wewe ni mkulima, hivyo kila siku kuota upo shambani unalima, au unaota pembejeo au mazao, hilo ni jambo la kawaida…

Soma..

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;..”

  • Au kama akili yako muda wako wote kutwa kuchwa ilikuwa unafikiria masomo tu, basi jua kuota unafanya mitihani litakuwa  ni jambo la kawaida,
  • Vilevile ndoto za namna hii zinakuja kutokana na mabadiliko ya mwili. Kama ulilala una njaa, basi tarajia usiku kuota unakula kula hushibi, kama ulikunywa maji mengi na hivyo kibofu kimejaa, tarajia usiku kuota unakojoa kojoa mkojo hauishi, n.k.

Isaya 29: 8  “Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo, kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu; na kama mtu mwenye kiu aotapo, kumbe, anakunywa; lakini aamkapo, kumbe, anazimia, na nafsi yake inatamani; hivyo ndivyo utakavyokuwa huo wingi wa mataifa waletao vita juu ya mlima Sayuni”.

Hivyo watu wengi wanaota ndoto nyingi za namna hiyo, na nyingine ubongo unazitengeneza wenyewe. Kwamfano utakuta mtu anatafuta kufahamu Tafsiri za ndoto mbalimbali kama hizi:

  1. Kunyonyesha mtoto: Wanaoota ndoto hizi asilimia kuwa ni wanawake, kwasababu wao ndio akili yao sehemu kubwa ilishajengeka katika mazingira ya kuwa na Watoto hata kama hajazaa..Hivyo kuota unaonyenyesha haliwezi kuwa ni jambo la ajabu
  2. Vivyo hivyo kuota mbwa:
  3. kuota  panya,
  4. Wengine wanatafuta kujua ndoto za magari zinamaanisha nini: Magari tunakutana nayo kila siku barabarani.
  5. ukiota unaswali, .
  6. Maana ya ndoto nyevu,
  7. kuota una nywele ndefu,
  8. ndoto ya kufua nguo,
  9. tafsiri ya ndoto ya harusi.
  10. kuota unavua samaki, na za  kuogelea,
  11. Kuota umegeuza nguo
  12. Ndoto za kuogelea
  13. Kuota ajali
  14. Kuota umeua mtu
  15. Kuota upinde wa mvua
  16. Ndoto za meli
  17. Kuota unanyeshewa na mvua
  18. Maana ya ndoto za kuolewa
  19. Unachuma matunda
  20. Unakunywa pombe
  21. Umevaa nguo nyeupe, 
  22. Ndoto za mayai
  23. Ndoto ya Nyama
  24. Ndoto za asubuhi
  25. Kuota unaoga
  26. Kuota Wanyama, kama mbuzi, sungura, kinyonga, kobe, ngamia, tembo, mamba, kiboko, nyani,paka, mbwa, ng’ombe.N.k. Zote hizi zipuuzie tu.Hazina maana yoyote kwako.
  27. Kuota wadudu kama sisimizi, siafu, konokono, mchwa, mbu, nge, mjusi, mende,tandu
  28. Kuota mapacha.
  29. Kuota jirani, ndugu yako,
  30. Kuota unakula mkaa.
  31. Kuota unatapika.
  32. Watu wanavuna.
  33. Ndoto za kutembea peku.
  34. Unafagia, Unalia,
  35. Kumuota raisi, waziri mkuu, makamu wa raisi, mbunge. Hawa kila siku unawaona kwenye Tv, au unawasikia kwenye Radio, ni lazima utawaota tu usiku siku moja.
  36. Ndoto Juu ya mpenzi wako.
  37. Kuota kabati.
  38. Unafua nguo,
  39. Unaosha vyombo, Maiti,
  40. Kuota jeneza
  41. Ukiota karanga, vitunguu, nyanya, pilau, sherehe,
  42. Kuota Unauza duka

Nakadhilika, Nakadhalika..zipo nyingi, nyingine unazijua wewe mwenyewe, hatuwezi kuziorodhesha zote hapa.. Lakini zote hizo hazina umuhimu wa kutafuta kujua maana zake. Kwasababu ukienda kwa mtindo huo utachanganyikiwa mwilini na rohoni.

Kikubwa ni kufahamu kuwa njia Kuu  ambayo Mungu aliichagua kuzungumza na wanadamu ni kupitia Neno lake (Biblia tu)

Ikiwa wewe ni mwenye dhambi nataka nikuambie hizi ni nyakati za mwisho, Mafundisho mengi ya uongo, na ya mashetani yamezaa kila mahali, Usipotaka kusimama, shetani ni lazima akuzombe kwenye aina ya mafundisho hayo ya mashetani na kukupa tafsiri ya kila ndoto unayoita….

Tubu mgeukie Mungu wako, dalili zote zinathibitisha hilo kuwa tunaishi katika siku za mwisho. Maisha yako yapo hatarini sana, kwani hujui siku yako ya kuondoka ni lini, na hata kama hutaondoka leo au kesho, lakini UNYAKUO upo karibuni sana.. Yesu yupo mlangoni kuja kuwachukua wateule wake.

Angalia hali halisi ya ulimwengu ulivyo sasa halafu niambie ni dalili ipo Yesu aliyosema kuhusu siku za mwisho haijatimia, angalia magonjwa ya mlipuko, angalia tetesi za vita, angalia matetemeko, angalia kuongozeka kwa maasi duniani,..yote hayo yalitabiriwa.

Huu si wakati wa kuangalia mambo mengine Zaidi ya wokovu wako. Nani ajuaye leo hii Mungu kakupitisha kwenye ukurasa huu ni ili Akuokoe? Kwasababu anaompango mkubwa na wewe maishani mwako?

Hivyo kama wewe ni mwislamu usiogope kumkabidhi YESU Maisha yako leo, fungua tu moyo wako mruhusu atende kazi, nawe utaona badiliko la ajabu atakalolileta ndani yako.

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana.

Bofya chini kwa kujiunga na magroup yetu ya Whatsapp, kwa  mafundisho ya kila siku.

Mada nyinginezo:

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UNYAKUO.

MIJI YA MAKIMBILIO.

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAKATI WA JUA KALI NDIO WAKATI WA KAZI:

Hebu tuchukue muda kidogo kuisoma habari ifuatayo naamini tutajifunza kitu,

1Samweli 11: 1 “Ikawa, kama baada ya mwezi mmoja, Nahashi, Mwamoni ,akakwea na kupanga marago juu ya Yabesh-gileadi;na watu wote wa Yabeshi wakamwambia Nahashi, Fanya mapatano nasi,na sisi tutakutumikia.

2 Huyo Nahashi, Mwamoni, akawaambia, Kwa sharti hii mimi nitapatana nanyi, kila mtu ang’olewe jicho la kuume; na kwa jambo hilo nitawashutumu Waisraeli wote pia.

3 Basi wazee wa Yabeshi wakamjibu, Tuachie siku saba, ili tutume wajumbe waende mipakani mwote mwa Israeli; kisha, ikiwa hakuna atakayetuokoa, tutakutokea.

4 Hivyo wajumbe wakafika Gibea ya Sauli, wakasema maneno hayo masikioni mwa watu; na watu wote wakainua sauti zao wakalia.

5 Na tazama, Sauli akaja akifuata ng’ombe kutoka kondeni; naye Sauli akauliza, Watu hawa wana nini, hata wakalia? Wakamwambia maneno ya watu wale wa Yabeshi.

6 Na roho ya MUNGU IKAMJILIA SAULI KWA NGUVU, hapo alipoyasikia maneno yale, na hasira yake ikawaka sana.

7 Naye akatwaa jozi ya ng’ombe, akawakata-kata vipande, kisha akavipeleka vile vipande mipakani mwote mwa Israeli kwa mikono ya wajumbe, kusema, Ye yote asiyetoka nyuma ya Sauli na Samweli, ng’ombe zake watatendwa vivi hivi. Basi utisho wa Bwana ukawaangukia wale watu, wakatoka kama mtu mmoja.

8 Naye akawahesabu huko Bezeki; Waisraeli walikuwa mia tatu elfu, na Wayuda thelathini elfu.

9 Nao wakawaambia hao wajumbe waliokuja, Waambieni watu wa Yabesh-gileadi, Kesho, WAKATI WA JUA KALI, mtapata wokovu. Basi wale wajumbe wakaenda, wakawaarifu watu wa Yabeshi; nao walifurahiwa.

10 Kwa hiyo watu wa Yabeshi walisema, Kesho tutawatokea, nanyi mtatufanyia yote myaonayo kuwa ni mema.

11 Ikawa, kesho yake, Sauli akawapanga watu katika vikosi vitatu; nao wakaingia katikati ya marago kwenye zamu ya asubuhi, wakawapiga Waamoni hata WAKATI WA JUA KALI; kisha ikawa wale waliosalia wakatawanyika, hata wasiachwe wawili wao pamoja”.

Biblia inasema taa ya mwili ni jicho, maana yake mtu akitolewa macho anakuwa kipofu, giza linaingia katika mwili wake wote, hebu fanya utafiti wa kufunga macho yako uone utakachokiona…bila shaka ni giza tupu…

Mathayo 6:22 “Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote utakuwa na nuru.

23 Lakini jicho lako likiwa bovu, mwili wako wote utakuwa na giza. Basi ile nuru iliyomo ndani yako ikiwa giza; si giza hilo!”

Kwahiyo kwa tukio hilo hapo juu, kuna wakati Mfalme wa Moabu alitaka kuingia katika ardhi ya Israeli inayoitwa Yabeshi, na alipoingia kwasababu ya wingi wa majeshi yake akawatishia Israeli vikali, nao wakaogopa, wakanyenyekea chini yake wakamwambia fanya mapatano nasi (maana yake kama unataka kitu chochote kutoka kwetu hata kama ni kodi tutakupatia)..lakini Yule mfalme kwa kiburi akasema hatataka kitu chochote bali kumng’oa kila mtu wa mji huo wa Yabeshi jicho la kuume…Na lengo la kuwaambia hivyo ni ile awaaibishe na pia aliingize giza katika mji ule, kwasababu alijua jicho la mtu ndio mwangaza wake..mtu hakuna chochote anaweza kufanya.

Jambo hilo liliwahuzunisha watu wa Yabeshi, mpaka kufikia hatua ya kwenda kuomba msaada wa ndugu zao waisraeli walio kwenye majimbo mengine, na wakati huo Israeli walikuwa wameshajitakia mfalme, na walimteua Sauli…lakini kila mtu alikuwa anamdharau Sauli kwa kuwa walimwona kama ni kijana laini asiye na uwezo wa kutawala wala wa vita. Lakini biblia inasema ROHO YA MUNGU ilimjia Sauli kwa nguvu na kumpa moyo wa ujasiri na ushujaa, na kutoka kwenda kuwapiga wamoabu na kuwaangamiza wote kabisa…Lakini jambo pekee ni kwamba hawakuwapiga wakati wa jioni, au wakati wa asubuhi, bali waliwapiga wakati wa JUA KALI linaloangaza…Kuashiria kuwa wao sio WANA WA USIKU bali wa Mchana.. Na kamwe Nuru ya macho yao haiwezi kuzimwa…wala giza haliwezi kuingia kwao.  Hivyo kwa imani waliwaua wakati wa jua kali..

Kama tujuavyo wakati wa jua kali, ndipo watu wanazimia nguvu, ndio wakati watu wanachoka haraka, ndio wakati ambao mwili unapungukiwa maji….Lakini kwa majeshi ya Bwana, hicho ni kinyume chake…wakati wa mchana ndio wakati wa kushinda na kupambana…

Wakati wa mchana(jua kali) ndio wakati wa kuingia vitani, wakati wa mchana ndio wakati wa kwenda kuyavamia majeshi ya adui, wakati wa mchana ndio wakati wa kwenda kuteka nyara, ndio wakati wa kumnyang’anya shetani mateka, wakati wa jua kali ndio wakati wa kuhubiri injili..

Bwana Yesu alisema…

Yohana 9:4 “Imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenipeleka maadamu ni mchana, usiku waja asipoweza mtu kufanya kazi

5 Muda nilipo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”.

Wakati huu wa jua kali ndio wakati adui yetu kukosa nguvu, ndio wakati anaoungua, ndio wakati ambao anakimbilia kivulini na mafichoni…hivyo ndio wakati wa kumfuata huko kwa vishindo kama Sauli alivyofanya, na kumwangusha na kumnyang’anya mateka sio wakati wa sisi kulitafuta giza au kivuli kama wao.. “Na Yesu ndio Nuru yetu, ndio jua letu..na sisi ni wana wa Nuru, jua lake halituchomi wala halituumizi wala halituchoshi, wala halitumalizi maji mwilini”..linawadhoofisha maadui zetu lakini si sisi.

Isaya 18:4 “Maanaa Bwana ameniambia hivi, Mimi nitatulia, na kuangalia katika makazi yangu, kama wakati wa mwangaza mweupe wa JUA KALI, mfano wa wingu la umande katika hari ya mavuno”.

Ifanye kazi ya Mungu wakati huu wa Neema, wakati huu wa jua kali…usiku unakuja ambao hutaweza…wakati adui atakuwa na nguvu…na wakati huo ni kipindi cha dhiki kuu…wakati ambao neema ya Yesu itafungwa…huo ndio wakati wa mamlaka ya nguvu za giza kutenda kazi..kutatokea dhiki isiyo ya kawaida!. Yule joka atakapopata nguvu…..Bwana atuepushe na hiyo dhiki, ili wakati huo utakapofika utukute tuwe tumeshanyakuliwa na watakatifu wengine kwenda mbinguni kwa baba na tumeshaimaliza kazi yake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?

USIHUZUNIKE.

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

Nuhu alipataje ujuzi wa kuwatambua wanyama wale wote na kuwaweka ndani ya Safina?

JE! UMEFUNDISHWA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

WANA JUHUDI KWA AJILI YA MUNGU, LAKINI SI KATIKA MAARIFA.

Shalom,

Jina la mwokozi wetu, Mfalme wa Wafalme na Bwana wa mabwana, Yesu Kristo libarikiwe daima. Ni siku nyingine tena hivyo Nakukaribisha tuyatafakari pamoja maandiko.

Neno linasema..

Warumi 10:1 “Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe.

 2  Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa”.

Kama tunavyoweza kuona hapo kuwa “Juhudi” tu peke yake hazitoshi, kama hatuna maarifa ya kutosha ya kumwabudu Mungu, tutakuwa tunafanya kazi bure.. Na hapa ndipo kundi kubwa la sisi wanadamu tunaposhindwa kumfikia Mungu, tunaishia kuona kama vile Mungu hayupo na sisi japokuwa tunajibidiisha kwake..

Leo tutayatazama makundi mawili  ya watu wa namna hii katika biblia ambao kweli yana bidii kwa ajili ya Mungu lakini sio katika maarifa:

Kundi la kwanza ni lile la watu walio ndani ya Imani ya Kikristo.

Na Kundi la Pili ni lile lililo nje Ya Imani ya Kikristo, lakini linadai kuwa linamtafuta Mungu wa kweli na linampenda.

Tutayatazama yote mawili kibiblia, na ikiwa mimi au wewe, au sote  tunaangukia kwenye mojawapo ya makundi hayo basi tujithamini mapema na kugeuka haraka sana kabla ya kupotea kwetu.

Tukianzana na hili kundi la kwanza ambalo ni la wale walio ndani ya Kristo…

Sasa Katika biblia Kuna mtu anaitwa Martha. Huyu Siku moja alimkaribisha Bwana Yesu kwake. Lakini yeye hakujua Kristo anataka nini, badala yake akawa anajitaabisha na mambo mengine yasiyo na maana sana machoni pa Bwana, mara anakwenda kuosha vyombo, mara anakwenda jikoni kuandaa chakula, mara anachota  maji kwenye majagi kwa ajili ya wageni,  mara anafanya hiki mara kile,..Na kibaya zaidi kilichokuwa kinamkasirisha ni pale anapomwona mdogo wake, Miriamu hajisumbui kwa lolote ameketi tu pale miguuni pake akimsikiliza Bwana..

Martha kuona vile akidhani ni utomvu wa nidhani, akamsemelea kwa Bwana ili aondoke pale..Lakini Bwana akasema..

Luka 10:41 “…. Martha, Martha, unasumbuka na kufadhaika kwa ajili ya vitu vingi;

42  lakini kinatakiwa kitu kimoja tu; na Mariamu amelichagua fungu lililo jema, ambalo hataondolewa”.

Sasa huyu ni mfano wa watu ambao wanaobidii kweli kwa ajili ya Mungu lakini si katika maarifa..Wanadhani Mungu anapendezwa na taabu zao na masumbufu yao na huku maagizo ya msingi ya rohoni wanayaacha yawapite..

Leo hii lipo kundi la wakristo, ambao, hawana muda wa kuyatafakari maneno ya uzima ya Kristo, hawana muda wa kusali, hawana muda wa kumwomba Roho Mtakatifu awafundishe mapenzi ya YESU, hawana hata muda wa kuutafuta ubatizo sahihi, lakini kwenye kwaya wapo na wana bidii sana, kwenye ujenzi wa kanisa wapo, na wanajitoa kwa bidii, kwenye michango yote wapo haiwapiti, wako tayari kufanya hiki au kile kwa ajili tu ya Mungu hawaachi, wanajitoa kweli hata usafi wa kanisa ni wenye bidii sana, lakini tukirudi kwenye bible-study tu, huwaoni,..

Ni kweli wanachokifanya si kibaya, wanajuhudi kwa ajili ya Mungu lakini si katika maarifa kama vile Martha..Hivyo mbele za Mungu wanaonekana hawajafanya chochote haijalishi bidii yao ni kubwa kiasi gani. Kwasababu mambo ya msingi wameyaacha. Kwasababu ni heri usiwe unaimba kwaya, ni heri ukawa hufanyi mambo mengine lakini Neno la Mungu unalishika kwa bidii na unalisoma sana na kulichunguza, na umebatizwa, na umepokea Roho Mtakatifu, unaweza ukakosa kitu cha kuchangia lakini ukawa ni mtu wa kusali sana, ukawa ni mtu ambaye haiwezi kupita siku hujajifunza biblia na kuisoma peke yako pasipo kusubiria mtu fulani akuelezee, huku ukimtegemea Roho Mtakatifu akufundishe n.k.

Kundi la Pili: Ni la watu ambao si wakristo, lakini wapo ulimwenguni kote wanadai kuwa wanamuheshimu Mungu.. Na wengi wao ni kweli wanao nia nzuri, na wanaweza wakawa na juhudi kubwa kwa ajili ya Mungu kuliko hata wewe, lakini mwisho wake, watu wa namna hii, huwa ndio wanakwenda mbali kabisa na mpango wa Mungu, na wakati mwingine wanaiharibu kabisa kazi yake.. Na hiyo yote ni kutokana na kukosa maarifa ya kumwabudia Mungu.

Mfano wa watu hawa ni Mtume Paulo mwenyewe. Yeye kabla ya kumpokea Kristo alikuwa ni mtu mwenye bidii kwa Mungu kweli, lakini kwasababu alikosa maarifa matokeo yake akawa anawaua mpaka wakristo akidhani anamtolea Mungu sadaka (Wafilipi 3:6-7)..Na wayahudi wengine wote ndio walikuwa vivyo hivyo kama yeye.

Wengine walio katika kundi hili ni waislamu..Sio wote unaowaona wanawachinja watu kule Syria na Iraq na Somalia ukadhani hawampendi Mungu..hapana, wengine wanafanya vile kwasababu wanadhani ndio wanamuheshimu Mungu, kama mtume Paulo, kumbe juhudi zao si katika maarifa na hivyo inawafanya wazidi kupotea Zaidi na kwenda kinyume na Mungu, na hata kuwa adui wa Mungu kabisa..Kama vile Neno linavyosema..

Hosea 4:6 “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa..”

Lakini maarifa sahihi yanapatikana wapi?

Ndugu, ni kwanini tunasisitiza sana YESU, YESU, YESU,? Nikwasababu maarifa yote na hekima yote zinapatikana kwake tu (Wakolosai 2:3). Huyo tu, ukimpata, au ukimjua katika usahihi wote, basi ujue kuwa utamwabudu Mungu katika maarifa na sio katika ujinga.

Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo”

Na Yesu yupo wapi? Jibu ni kuwa Yupo katika NENO lake(biblia)..Hivyo kama wewe ni muislamu au upo katika dini nyingine yoyote, mgeukie Yesu sasa, mwamini yeye, ayaongoze Maisha yako. umwabudu Mungu katika maarifa anayoyataka, ili akufurahie..kwasababu anasema..

Yohana 14:6  “…Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”… Hakuna njia nyingine ya kumfikia Baba isipokuwa kwa kupitia Yesu.

Vilevile na wewe kama ni mkristo lakini bado unasua sua, unaishi kidini dini tu,..kwaya kwako ni muhimu kuliko kulisoma Neno, kutoa sadaka nyingi kwako ni muhimu kuliko kuutafuta ubatizo sahihi na Roho Mtakatifu, Huu ni wakati wako wa kujihurumia, na kugeuka na kuanza kumwabudu yeye katika Roho na Kweli, kwa kujifunza mapenzi yake katika Neno lake (biblia).

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?

Chapa zake Yesu ni zipi hizo?

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

MTANGO WA YONA.

SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UTAPATAJE RAHA NAFSINI?

Mathayo 11: 28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”

Kama ukiutafakari huo mfano Bwana Yesu alioutoa….utagundua kwamba aliwafananisha watu aliowaona mbele yao na punda wa kubeba mizigo ambao Bwana wao hao punda kawafunga NIRA shingoni na kuwabebesha mizigo waivute huko nyuma. Na kitu kingine Bwana Yesu alichokiona kwa hao punda ni kwamba wamefunga NIRA shingoni ambayo ni ngumu sana, pengine inachubua ngozi ya shingo sana…na sio hicho tu, aliona pia mzigo wanaobebeshwa na Bwana wao ni mkubwa sana, kuliko uwezo wao…Na lililobaya kuliko yote, ambalo naamini ndilo lililomfanya azungumze ni “tabia ya bwana wa hao punda”…kwani alikuwa ni mkali sana na sio mnyenyekevu…pengine alikuwa anawatandika viboko, na alikuwa anawaendesha kwa ukali, na awapi pumziko ni kazi tu mwanzo mwisho..

Hivyo Bwana Yesu kuona vile akawahurumia….akasema maneno yafuatayo..

“Njooni kwangu ninyi nyote(maana yake mwacheni huyo Bwana wetu mje kwangu mimi) msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha…..zingatia hilo neno “nitawapumzisha”..maana yake huko walipokuwepo walikuwa hawapumzishwi, lakini hapa wanaahidiwa Pumziko…Lakini hajaishia hapo tu anaendelea kusema…jitieni nira yangu mjifunze kwangu (maana yake vueni hiyo nira ngumu ya Bwana wenu mvae ya kwangu)..na pia mjifunze kwangu (maana yake mchukue mafunzo yangu ya namna ya kufanya kazi hizo za mizigo)…kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo (sio kama huyo Bwana wenu ambaye anawatumikisha kwa ukali na hana unyenyekevu)..Na Bwana Yesu anamalizia kwa kusema NANYI MTAPATA RAHA NAFSINI MWENU.

Hebu tafakari hilo tukio…Ni sawa na wewe unafanya kazi mahali Fulani ambapo boss wako anakupa mshahara mdogo sana, halafu anakufanyisha kazi nyingi kuliko hata uwezo wako, halafu pamoja na hayo yote, anakuwa mkali kwako na kukunyanyasa…Na kisha anatokea mtu mwingine anakuhurumia anakwambia njoo fanya kazi kwangu, nitakupa mshahara mzuri, nitakupa kazi za wastani, kwakuwa mshahara wangu mimi ni mzuri na kazi zangu si nyingi…na zaidi ya yote mimi ni mpole na mnyenyekevu…nawe utapata raha maishani mwako?…Je utakataa kwenda???..Bila shaka utaondoka kwa miguu yote miwili pasipo kutazama nyuma..

Na ndivyo hivyo hivyo tunapokuwa dhambini…Biblia inasema atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi…maana yake kila ambaye hajampokea Yesu anakuwa chini ya utumwa wa shetani penda asipende…na shetani ni bwana anayetesa, asiye mnyenyekevu, mkali, na nira yake ni ngumu na mzigo wake ni mzito kwa ufupi ni muuaji, yupo kwa maslahi yake akutumie wewe kupata watu wengi wa kuwapeleka jehanamu na mwisho wa siku akumalizie na wewe…

Lakini Bwana Yesu anatokea leo mbele yako na kukwambia mwanangu…utumwa uliotumikishwa na shetani..unatosha, vua hiyo nira, tua huo mzigo…njoo kwangu UTAPATA RAHA NAFSINI..Je hutaki raha??

Hivyo kama hujampokea Kristo leo..huu ndio wakati wa kutua mzigo wako Kalvari…hupendi raha?..kama hupendi sawa unaweza kuendelea kubaki kwenye dhambi…lakini kama unataka raha nafsini mwako..sio wakati wakuichezea hiyo fursa..vua leo hivyo vimini, tupa hizo hereni, hizo lipstick zitupe, hizo suruali ulizokuwa unazivaa acha kuzivaa kuanzia leo…sigara na pombe ulizokuwa unakunywa, uasherati uliokuwa unaufanya wote uweke chini ni mzigo mzito…mfuate Yesu leo..na hakuna haja ya kuhadithiwa wala kusimuliwa baada ya kuviacha hivyo vyote..utaona mwenyewe raha itakayoingia ndani yako…utaona kama ulikuwa umechukuliwa msukule sasa umerudia akili yako timamu…utakuwa huru kuliko maelezo, wala hutatamani kumrudia shetani tena..utajilaumu kwanini hukumgeukia Kristo tangu zamani. Hata sisi tulikuwa hivyo, lakini raha hii tumeionja tukaona ni kweli.

Shetani atakuonea wivu baada ya kumkimbia, atakutishia hivi na vile, lakini usiogope utakuwa chini ya Bwana ambaye si mkali kama shetani wala si mkorofi maisha yako yote…

Bwana akubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU

TABIA YAKO NI YA MNYAMA GANI?

AMEFUFUKA KWELI KWELI.

JE WAKRISTO TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA VALENTINE’S DAY?

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

NINI TOFAUTI KATI YA KARAMA, UTENDAJI KAZI NA HUDUMA.

Rudi Nyumbani:

Print this post