Category Archive Wanawake

JE UNAMTUMIKIAJE BWANA?

Mafunzo maalumu kwa Wanawake.

Karibu tujifunze Biblia,

Je Bwana alishakufanyia muujiza wowote katika maisha yako?..Na ukaufurahia?.. Je baada ya hapo ulimfanyia nini Bwana?.. Je uliishia kushukuru tu na kuendelea na mambo yako? Au kuna lingine la ziada ulilifanya?, kama hukufanya chochote au hukujua nini cha kufanya basi leo fahamu yakupasayo kufanya!

Hebu tujifunze kwa baadhi ya wanawake katika biblia ambao hawakuwa Mitume, wala Waalimu, wala Maaskofu wala wachungaji lakini walikuwa wakimtumikia Bwana Yesu.. na kisha tutazame walikuwa wakimtumikia kwa namna gani?

Mathayo 27:55  “Palikuwa na wanawake wengi pale wakitazama kwa mbali, HAO NDIO WALIOMFUATA YESU TOKA GALILAYA, NA KUMTUMIKIA.

56  Miongoni mwao alikuwamo Mariamu Magdalene, na Mariamu mama yao Yakobo na Yusufu, na mama yao wana wa Zebedayo”.

Hawa wanawake walikuwa wakifuatana na Bwana Yesu kila mahali.. Lakini je! Walikuwa wanafuata naye kumtazama uso?, au kumsikiliza tu anayoyahubiri?..Jibu ni La! Biblia inatuambia walikuwa pia WAKIMTUMIKIA!!.. Sasa swali wakimtumikia kwa nini?..tusome mistari ifuatayo..

Luka 8:1  “Ikawa baada ya hayo alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu; na wale Thenashara walikuwa pamoja naye,

NA WANAWAKE KADHA WA KADHA ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,

3  na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, WALIOKUWA WAKIMHUDUMIA KWA MALI ZAO”.

Umeona hapo?.. Walikuwa wakimhudumia kwa MALI ZAO!. Ikiwa na maana kuwa gharama kubwa za kuipeleka Injili zilikuwa zinabebwa na hawa WANAWAKE!..  hata ule mkoba ambao Yuda alikuwa anaushika, huenda sehemu kubwa ilijazwa na hawa wanawake!.

Na kwanini wanawake hawa walipata msukumo huo mkuu wa kumhudumia Bwana kwa mali zao?.. Jibu ni kwasababu walitendewa miujiza na Bwana, walitolewa pepo waliokuwa wanawatesa, waliponywa magonjwa  yao yaliyokuwa yanawatesa, walipewa wokovu ndani yao ambao uliwapa Amani na tumaini la maisha..Hivyo wakaona si sawa kumtazama Yesu kwa uso tu na kumshukuru kwa maneno tu!, bali pia kwa vitendo.

Ndipo wakaona wavunje vibweta vyao ili Bwana akaende miji mingi Zaidi kuhubiri, wakaona watoe hazina zao ili wanafunzi wa Bwana wasipungukiwe wanapokwenda kuhubiri miji na miji. Na hivyo wakawa mashujaa wa Imani ambao mpaka leo tunawasoma.

Na sio hao tu, bali pia tunamwona na Mkwe wake Petro, (Mama yake mkewe) ambaye alikuwa anaumwa homa, biblia inasema baada ya Bwana kumponya, alinyanyuka na kuanza KUMTUMIKIA BWANA!.

Mathayo 8:14 “Hata Yesu alipofika nyumbani kwa Petro, akamwona mkwe wa Petro, mamaye mkewe, amelala kitandani hawezi homa.

15  Akamgusa mkono, homa ikamwacha; NAYE AKAONDOKA, AKAWATUMIKIA”

Je na wewe Mama unamtumikia nani?, Na wewe binti unamtumikia nani?…Je umemtumikia Bwana kwa kipi tangu alipokuponya?, tangu alipokufungua?, tangu alipokuinua?, tangu alipokupa wokovu bure?.. Je unamtumikia kwa maneno tu, au pia na vitendo?.

Ni kweli wewe sio Mchungaji, wala Mwalimu, wala Mhubiri, wewe ni kama tu Mariamu Magdalena, au Susana..basi fanya kama hao!.. Na kumbukumbu lako litadumu kama la hao wanawake lilivyodumu, Bwana atakuheshimu na kukuona wewe ni mtumishi wake kama tu walivyo Mitume kwasababu na wewe pia unamtumikia kwa mali zako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?

WANNE WALIO WAONGO.

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

Rudi nyumbani

Print this post

MWANAMKE ABIGAILI ANAFUNZO GANI KWA WANAWAKE?

Abigaili.

Huu ni mwendelezo wa mafundisho maalumu yahusuyo wanawake.

Na Leo tutaisikia sauti ya Mungu iliyokuwa nyuma maisha ya huyu mama aliyeitwa Abigaili.

Abigaili ni mwanamke aliyeolewa na mwanaume ambaye halikuwa chaguo la Mungu kwake, ijapokuwa mwanaume huyo alikuwa tajiri, hatujui ni nini kilimsukuma Abigaili katika ujana wake kukubali kuolewa na mwanaume yule, labda pengine Nabali hakuanza vile, alikuja kubadilika baadaye, au pengine wazazi wake walimshurutisha aolewe naye kwasababu ya utajiri aliokuwa nao.

Lakini mwanaume huyo halikuwa chaguo sahihi la Abigaili Kutoka Kwa Mungu, kwani Nabali hakuwajali watu wa chini kabisa, Wala hakuwa mtu wa kurudisha fadhila. Utakumbuka wakati ambapo Daudi anakimbizwa na Sauli, akiwa kule  maporini, alikutana na kundi kubwa la mifugo wa huyu Nabali, hivyo Daudi alichofanya ni kuwapa hifadhi watumwa wake, kuwahakikishia ulinzi, dhidi ya wavamizi wa mifugo ya wachungaji,kwasababu Nabali alikuwa na mifugo mingi sana na kipindi ambacho wanakwenda kuwakata manyoya kondoo wao, waporaji wenye silaha Huwa wanawavamia sana wafugaji..hivyo walidumu na Daudi Kwa muda wote huo mpaka walipomaliza shughuli zao.

Lakini siku moja Daudi alipungukiwa chakula yeye na jeshi lake hivyo wakaona mtu wa karibu atakayeweza kuwasaidia ni huyu Nabali. Ndipo Daudi akatuma wajumbe kwake kumuomba chochote alichonacho awasaidie.Lakini badala ya kupokea fadhili akapokea matusi. Ndipo Daudi akakasirika sana akataka kwenda kumuua Lakini mke wake alipopata habari akafanya kinyume chake akaaanda vyakula na kumpelekea Daudi, ndipo hasira yake ikageuka.

Embu tukisome kisa hichi Kwa ufupi;

1 Samweli 25:9-38

[9]Basi walipofika vijana wake Daudi, wakamwambia Nabali sawasawa na maneno hayo yote kwa jina la Daudi, kisha wakanyamaza.

[10]Naye Nabali akawajibu wale watumishi wa Daudi, akasema, Huyu Daudi ni nani? Na mwana wa Yese ni nani? Siku hizi kuna watumwa wengi wanaomtoroka kila mtu bwana wake!

[11]Basi mimi je! Nitwae mkate wangu, na maji yangu, na machinjo yangu niliyowachinjia hao watu wangu wakatao manyoya kondoo zangu, na kuwapa watu ambao siwajui wametoka wapi?

[12]Basi vijana wake Daudi wakageuka, wakaenda zao, wakarudi, nao wakaja wakamwambia sawasawa na maneno hayo yote.

[13]Kisha Daudi akawaambia watu wake, Haya! Jifungeni kila mtu upanga wake. Nao wakajifunga kila mtu upanga wake; Daudi naye akajifunga upanga wake; nao wakapanda nyuma yake Daudi, wapata kama watu mia nne; na watu mia mbili wakakaa na vyombo vyao.

[14]Lakini kijana mmojawapo alimpasha habari Abigaili, mkewe Nabali, kasema, Tazama, Daudi alituma wajumbe kutoka nyikani waje ili kumsalimu bwana wetu, naye akawatukana.

[15]Walakini watu hawa walitutendea mema sana, wala hatukupata dhara, wala sisi hatukupotewa na kitu cho chote, wakati wote tulipofuatana nao, tulipokuwako mavueni;

[16]watu hao walikuwa boma kwetu usiku na mchana, wakati wote tulipokuwa nao tukiwachunga kondoo.

[17]Basi sasa ujue na kufikiri utakayotenda; kwa sababu yamekusudiwa mabaya juu ya bwana wetu, na juu ya nyumba yake yote; kwa kuwa yeye ni mtu asiyefaa kabisa, hata mtu hawezi kusema naye.

[18]Ndipo Abigaili akafanya haraka, akatwaa mikate mia mbili, na viriba viwili vya divai, na kondoo watano waliofanyizwa tayari, na vipimo vitano vya bisi, na vishada mia vya zabibu, na mikate ya tini mia mbili; akavipakia vitu hivi juu ya punda.

[19]Akawaambia vijana wake, Haya! Tangulieni mbele yangu; angalieni, mimi nawafuata. Ila hakumwambia mumewe, Nabali.

[20]Ikawa, alipokuwa amepanda punda wake, na kutelemka penye sitara ya mlima, tazama, Daudi na watu wake walikuwa wakishuka kumkabili; naye akawakuta.

[21]Basi Daudi alikuwa amesema, Hakika ni bure nilivyokuwa nikilinda nyikani yote aliyo nayo mtu huyu, asipotewe na kitu cho chote cha mali yake yote; naye amenilipa mabaya badala ya mema.

[22]Mungu naye awafanyie hivyo adui za Daudi, na kuzidi, nikimwachia katika wote walio wake hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi.

[23]Ndipo hapo Abigaili alipomwona Daudi, alifanya haraka kushuka juu ya punda wake, akamwangukia Daudi kifulifuli, akainama mpaka nchi.

[24]Akamwangukia miguuni pake, akasema, Juu yangu, bwana wangu, juu yangu mimi na uwe uovu; tafadhali mjakazi wako na anene masikioni mwako, nawe uyasikilize maneno ya mjakazi wako.

[25]Nakusihi, bwana wangu, wewe usimwangalie huyu mtu asiyefaa, yaani, Nabali; kwa maana kama lilivyo jina lake ndivyo alivyo yeye; jina lake ndilo Nabali, na upumbavu anao; lakini mimi, mjakazi wako, sikuwaona hao vijana wa bwana wangu aliowatuma.

[26]Basi sasa, bwana wangu, aishivyo BWANA, na iishivyo nafsi yako, kwa kuwa BWANA amekuzuia usimwage damu, tena usijilipize kisasi mkono wako mwenyewe, basi sasa adui zako, na hao wamtakiao bwana wangu mabaya, wawe kama Nabali.

[27]Na sasa zawadi hii, mjakazi wako aliyomletea bwana wangu, na wapewe vijana wamfuatao bwana wangu.

[28]Nakuomba ulisamehe kosa lake mjakazi wako, kwa kuwa hakika BWANA atamfanyia bwana wangu nyumba iliyo imara, kwa sababu bwana wangu anavipiga vita vya BWANA; tena uovu hautaonekana ndani yako siku zako zote.

[29]Na hata ijapokuwa binadamu angeinuka akuwinde, na kuitafuta nafsi yako, hiyo nafsi ya bwana wangu itafungwa katika furushi ya uhai pamoja na BWANA, Mungu wako; na nafsi za adui zako ndizo atakazozitupa nje, kama kutoka kati ya teo.

[30]Tena itakuwa, hapo BWANA atakapokuwa amemtendea bwana wangu sawasawa na mema yote aliyoyanena juu yako, na kukutawaza juu ya Israeli;

[31]hili halitakuwa kwazo, wala chukizo la moyoni kwa bwana wangu, ama ya kuwa umemwaga damu bure, ama ya kuwa bwana wangu amejilipiza kisasi mwenyewe; tena hapo BWANA atakapokuwa amemtendea bwana wangu mema, ndipo umkumbuke mjakazi wako.

[32]Naye Daudi akamwambia Abigaili, Na ahimidiwe BWANA, Mungu wa Israeli, ambaye amekuleta hivi leo kunilaki;

[33]na ibarikiwe busara yako, na ubarikiwe wewe, uliyenizuia hivi leo nisimwage damu, wala kujilipiza kisasi kwa mkono wangu mwenyewe.

[34]Kwa kuwa ni kweli, aishivyo BWANA, Mungu wa Israeli, aliyenizuia nisikudhuru, kwamba hungefanya haraka kuja kunilaki, hakika huyu Nabali asingaliachiwa hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi.

[35]Basi Daudi akapokea mkononi mwake vitu vile alivyomletea; akamwambia, Haya! Kwea kwa amani kwenda nyumbani kwako; tazama, nimeisikiliza sauti yako, nami nimeukubali uso wako.

[36]Kisha Abigaili alimjia Nabali; na tazama, alikuwa amefanya karamu nyumbani mwake, kama karamu ya kifalme; na moyo wake huyo Nabali ukafurahiwa ndani yake, kwa maana amelewa kabisa. Kwa sababu hiyo hakumwambia neno, dogo wala kubwa, hata kulipopambazuka.

[37]Ikawa asubuhi, divai ilipokuwa imemtoka Nabali, mkewe alimwambia mambo hayo, na moyo wake ukafa ndani yake, akawa kama jiwe.

[38]Tena ikawa, yapata siku kumi baadaye, BWANA alimpiga huyo Nabali, hata akafa.

Ni nini mwanawake wanapaswa wajifunze kuhusiana na maisha ya Abigaili.

  1. Mwanaume Bora si yule mwenye Mali:

Kundi kubwa la wanawake wengi wa sasa wanaotaka kuolewa kigezo wanachokitazama Kwa wanaume ni Mali, wanasahau kuwa hata shetani hutoa Mali. Nabali alimsumbua sana Abigaili katika maisha yake ya ukamilifu, na kama asingekuwa na bidii katika busara yake angeshauliwa mbali na Daudi pamoja na Mali zao. Kufunua kuwa Kristo kama mfalme wetu, Huwa anaziadhibu familia Kwa makosa ya wanandoa wasiowajibika kiroho. Haijalishi wingi wa Mali walizonazo. Wewe kama mwanamke unayekaribia kuolewa kumbuka mwanaume anayemcha Mungu ndio chaguo sahihi kwako, na si vinginevyo.

  1. Pili Abigaili analiwakilisha kundi la wanawake ambao, wameshaingia katika ndoa za watu wasiosahihi.

Wanawake wengi wapo kwenye ndoa, lakini baadaye sana ndio wanakuja kugundua kuwa waume walionao hawakuwa Kutoka Kwa Bwana. Wengine ni wazinzi, wengine ni walevi kama Nabali, wengine hawajali kazi za Mungu Wala Roho zao wenyewe, wengine majambazi, wengine wanawatesa n.k.

Lakini utaona busara ya Abigaili haikuwa kwenda kutafuta mwanaume mwingine aolewe naye, kisa mume wake ni mpumbavu, ila aliendelea kudumu katika haki na ukamilifu, aliendelea kumwombea rehema mume wake hata Kwa maadui zake. Ijapokuwa alikuwa mjinga, lakini hakujaribu kujitenga na mumewe, alimwachia Mungu amfanyie wepesi. Na tunaona Mungu mwenyewe ndio alikuja kushughulika na Nabali akamuua, Kisha Abigaili akawa mke wa Mfalme Daudi. Pumziko la ndoa yake likaja.

Hata sasa wewe kama mwanamke ambaye upo katika ndoa chungu. Huitaji kuizira ndoa hiyo, badala yake omba rehema, na wokovu Kwa mume wako kwa Yesu. Naye ataugeuza moyo wake. Bwana hatatumia njia ya kumuua, lakini ataua uovu na ubaya ulio ndani yake. Na atakuwa tu mume Bora, lakini  usichoke kuomba ukasema nimeomba sana sijaona mabadiliko.yoyote… wewe endelea kuomba hata kama itapita miaka 20, ujue Mungu anaona na kusikia maombi Yako tu, atatenda jambo. Huyo atakuwa mume Bora zaidi ya unavyodhani, usipozimia moyo.Hivyo iga busara ya Abigaili.

Anza sasa kuijenga ndoa Yako. Bwana akubariki.

Shalom.

Je! Umeokoka? Je unafahamu kuwa hizi ni nyakati za mwisho na Mlango wa neema unakaribia kufungwa? Unasubiri nini usiokoke? Itakufaidia nini uupate ulimwengu wote halafu upate hasara ya nafsi Yako? Ikiwa upo tayari kumkabidhi Leo Bwana Yesu maisha Yako. Basi wasiliana nasi Kwa namba zetu hizi Kwa ajili ya mwongozo huo Bure.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MASOMO MAALUMU KWA WANAWAKE.

NI KITU GANI TUNAJIFUNZA KWA RISPA, BINTI AYA?

Je! kuna mwanamke mwingine aliyempaka Bwana marhamu (manukato) zaidi ya Mariamu ndugu yake Lazaro?

Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo; Nayo hushukia pande za ndani za tumbo

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inasemaje kuhusu Nywele?

Biblia imetoa maelekezo kuhusu Nywele kwa jinsia zote mbili (Ya kike na Kiume).

JINSIA YA KIUME:

Biblia inasema Mwanaume hapaswi kuwa na Nywele ndefu.. kwasababu kichwa chake yeye ni Utukufu wa Mungu..

1Wakorintho 11:3 “Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu

Hivyo kwa Mwanaume kuziweka Nywele zake kuwa ndefu ni aibu kwake na ni kukiaibisha Kichwa chake hicho ambacho ni  Kristo.

Tusome..

1Wakorintho 11:14  “Je! Hayo maumbile yenyewe hayawafundishi ya kwamba mwanamume akiwa na nywele ndefu ni aibu kwake?”

Na sio tu hatakiwi kuwa na Nywele ndefu, bali hata “Kufunika kichwa” awapo ibadani, maana yake ni kwamba  mwanaume anapokuwa ibadani hapaswi kuvaa kofia, au kuweka kitu chochote kichwani kinachoashiria kufunikwa kwa kichwa chake (maana yake kichwa chake siku zote kinapaswa kiwe wazi).

Na vile vile Mwanaume hapaswi kusuka Nywele, wala kuweka mitindo mitindo kichwani kwasababu kichwa chake ni utukufu wa Mungu.

JINSIA YA KIKE:

Katika jinsia ya Kiume tumesoma kuwa ni aibu kwa mwanaume kufunika kichwa, lakini tukirudi katika jinsia ya kike ni kinyume chake. Kwamba ni Aibu mwanamke kuwa na Nywele fupi na ni FAHARI MWANAMKE KUWA NA NYWELE NDEFU.

1Wakorintho 11:15 “Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni fahari kwake. Kwa sababu amepewa zile nywele ndefu ili ziwe badala ya mavazi”.

Wanawake wote ni sharti waache nywele zao ziwe ndefu kulingana na biblia, kuzikata Nywele au kuzifanya fupi, pasipo sababu yoyote ya msingi kama vile magonjwa, au udhaifu wa mwili, ni kwenda kinyume na maagizo ya Mungu.

Ndio maana Upara (Ulaza) huwa hauwapati wanawake, bali wanaume tu!!..Hiyo ni kuonyesha kuwa wanawake wamekusudiwa kuwa na Nywele vichwani mwao wakati wote wa maisha yao, na wanaume ni kinyume chake.

Na zaidi sana biblia inazidi kuelekeza kuwa hata kama Mwanamke atakata nywele zake kutokana na matatizo Fulani Fulani, labda magonjwa au kutokana udhaifu wa nywele kukatika zenyewe basi hapaswi kutembea nje akiwa na nywele zake hizo fupi, bali anapaswa afunike kichwa chake kwa kitambaa au kwa kitu chochote kile.

1Wakorintho 11:6  “Maana mwanamke asipofunikwa na akatwe nywele. Au ikiwa ni aibu mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa, na afunikwe.

7  Kwa maana kweli haimpasi mwanamume kufunikwa kichwa, kwa sababu yeye ni mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume”.

Na mwanamke anapokuwa ibadani awe na nywele ndefu au fupi, ni Agizo la Bwana kwamba afunike kichwa chake, kwasababu kuu 2

Sababu ya Kwanza ni ili asikiabishe kichwa chake ambacho ni MWANAUME. Na sababu ya pili ni kwaajili ya MALAIKA. Tunapokuwa ibadani Malaika wa Bwana wanahudumu pamoja na watakatifu. Malaika hawa Bwana aliowaweka kwaajili yetu wana uhusiano mkubwa sana sisi katika kutuhudumia Soma Mathayo 18:10.

Kwahiyo tunapokuwepo katika ibada na ndani yake kukawa kunafanyika mambo ambayo ni kinyume na Neno la Mungu, malaika hawa wanaondoka, na hivyo kufanya ibada kupoa na utukufu wa Mungu kupungua.

Na pia Wanawake hawapaswi kusuka nywele zao, au kuvaa wigi, au kuzibadilisha maumbile nywele zao aidha kwa kuziweka kemikali, au dawa za kuzifanya zilale, Biblia haijawapa maagizo ya kuzifanya nywele zilale au zing’ae au ziwe kama za jamii ya watu Fulani, Hapana!.. imesema “ZIWE NDEFU!!” Basii!!..

1Timotheo 2:9  “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;

10  bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.

11  Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)

Je kuchonga Nywele na Ndevu ni dhambi?

MSHAHARA WA DHAMBI:

FUVU LA KICHWA.

NGUVU YA MNADHIRI WA BWANA.

Rudi nyumbani

Print this post

Walakini ataokolewa kwa uzazi wake.

SWALI: Biblia inaposema mwanamke ataokolewa kwa uzazi wake, inamaanisha nini?

1Timotheo 2:14 “Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa.

15 Walakini ataokolewa kwa uzazi wake, kama wakidumu katika imani na upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi”.


JIBU: Tofauti na inavyotafsiriwa na watu wengi, kwamba andiko hilo linamaanisha kuwa mwanamke yeyote ambaye atakuwa na watoto wa kulea, basi mwisho wa siku ataokolewa kwa kutimiza tu kusudi hilo.  Mtazamo ambao sio sahihi na unakinzana na maandiko, Kwasababu kama kila mwanamke angekuwa anaokolewa kwa namna hiyo, hata wanawake wachawi nao wangeokolewa kwasababu na wao pia wanao watoto wa kulea.

Lakini biblia ilimaanisha nini kuandika hivyo? 

Mtume Paulo aliandika maneno hayo, kuonyesha jinsi gani huduma ya mwanamke ambaye ana watoto jinsi ilivyo na nguvu hata kusababishia wokovu kwake mwenyewe IKIWA atawalea watoto wake katika misingi ya imani, upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi kama ilivyoainishwa hapo..Na sio kwa kuzaa tu basi.

Kwasababu atakuwa ameifanya huduma ya kuokoa kizazi kingine.. Tengeneza picha kama wanawake wote ulimwenguni wangekuwa wanatimiza wajibu wao huu wa kuwalea watoto wao katika misingi ya imani, leo hii, kusingekuwa na haja ya kuhubiri injili kwasababu watoto wote wangekuwa tayari wanamjua Mungu. Lakini injili imekuwa ngumu kwa kizazi cha sasa kwasababu jambo la kwanza mzazi analolithamini kwa mtoto wake ni elimu tu, Mungu ni ziada, mtoto akifaulu darasani ndio furaha yake kubwa, wakati hajui hata mstari mmoja wa biblia. Hajui hata pambio moja la kumsifu Mungu. Mzazi haoni aibu hata mtoto wake anakuwa hadi mtu mzima hajui biblia ina vitabu vingapi.

Kwahiyo hapo mtume Paulo alikuwa anaonyesha nguvu iliyopo katika mwanamke kulea watoto wake vema, ambayo mwisho wa siku itampelekea hata na wokovu wake mwenyewe. Kwamfano Mungu akiona mtoto Yule ambaye alilelewa katika misingi kama Samweli, amekuwa sababu ya wokovu kwa Israeli, unategemea vipi Mungu amwache mama aliyemlea?. Ni sawa tu na yule anayewavuta watu kwa Kristo, ambao biblia inasema kitendo hicho kina nguvu ya kuokoa roho ya mhubiri na kufunika wingi wa dhambi zake.

1Petro 5:20 “jueni ya kuwa yeye amrejezaye mwenye dhambi hata atoke katika njia ya upotevu, ataokoa roho na mauti, na kufunika wingi wa dhambi”.

Kwahiyo ikiwa wewe ni mwanamke na Mungu kakujalia watoto ujue jukumu lako la kwanza, la injili ni kwa watoto wako, hakikisha hao wanakuwa katika misingi ya kumcha Mungu, wafundishe, na pale wanapokosea Mungu kakupa ruhusu ya kuwaadhibu, lengo ni kuwaweka katika mstari wa kumcha Bwana, na sio kuwatesa. Ukifanya hivyo matokeo yake utakuja kuyaona baada ya haya maisha hapa duniani.

Tito 2:4 “ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao;

5 na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

Raheli aliwalilia vipi watoto wake?

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

Rudi nyumbani

Print this post

MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 3)

Hii ni sehemu ya tatu ya mfululizo wa masomo kwa wanawake, katika sehemu ya kwanza  na ya pili tumeona, ni kwanini Bwana aliwatambua baadhi ya wanawake, kwa jinsia zao, na sio kwa majina yao, kwa kuwaita “wanawake”, na sehemu nyingine kuwatambua kwa mionekano yao kwa kuwaita “Binti” na sio labda kwa majina yao..ipo sababu, ikiwa hujapata bado, chambuzi zake, basi tutumie msg inbox tukutumie..

Lakini leo tutasonga mbele tena, kuona ni kwanini baadhi ya wanawake, aliwatambua kwa majina ya “MAMA”.

Mama ni cheo cha ukomavu, kwasababu mpaka uitwe mama ni wazi kuwa lazima utakuwa na watoto uliowazaa au unaowalea chini yako. Sasa tukirudi kwa Bwana Yesu, kuna wanawake aliwaona ni “Wamama rohoni”, sio mwilini, kwasababu kulikuwa na wanawake wengi, lakini si wote aliwaita “Mama” kama tu vile si wote aliwaita “Binti yangu”, bali baadhi tu.

Sasa embu twende tukasome baadhi ya Habari katika biblia kisha tuone, ni nini Bwana anatufundisha katika Habari husika. Mwanamke wa kwanza tutakayemtazama ni yule mkananayo. Tusome;

Mathayo 15:21 “Yesu akaondoka huko, akaenda kando pande za Tiro na Sidoni.

22 Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.

23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.

24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.

25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.

26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.

28 Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, MAMA, IMANI YAKO NI KUBWA; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile”.

Angalia asili ya huyu mwanamke, hakumtafuta Bwana kwa shida zake mwenyewe, au kwa matatizo yake mwenyewe, bali alimtafuta Bwana Yesu kwa shida za mwanawe.. Japokuwa mwanzoni hakujibiwa chochote, hata baada ya pale alipewa na maneno ya kukatishwa tamaa ya kuitwa mbwa, lakini bado hakuacha kuomba kwa shida ya mtu mwingine, kwasababu uzito wa mwanae ulikuwa kama wakwake.

Hiyo ni kuonyesha ni jinsi gani asivyojali vya kwake tu, bali hata vya wengine…

Mwanamke mwingine ni Mama yake Yesu mwenyewe, ambaye tunamsoma katika Yohana 2:1-4 siku ile alipoalikwa katika Harusi..

Yohana 2:1 “Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.

2 Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.

3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai. 4 Yesu akamwambia, MAMA, TUNA NINI MIMI NAWE? Saa yangu haijawadia”.

Angalia tabia yake alijali shida za wengine, aibu za wengine, akazifanya kama ni za kwake. Na kumpelekea Kristo, na muda huo huo akamwita “mama”

Mwingine ni Mariamu Magdalena, asubuhi ile ya kufufuka kwa Bwana, alikuwa akilia pale makaburini ndipo Yesu akamtokea na kumwambia “Mama unalilia nini?” Saa hiyo hiyo Yesu akamtuma kwa ndugu zake kwenda kuwatangazia injili. Akawa mtu wa kwanza kupewa neema ya kuwahubiria watu wengine Habari za kufufuka kwa Bwana Yesu. (Yohana 20:11-18)..

Neema hiyo si kila mwanamke atapewa, bali ni wale “wamama rohoni tu” Wanawake waliokomaa kiroho,ambao wanajua wajibu wao kwa Bwana, wanajua kuwaongoza wengine katika njia za Mungu, haijalishi umri wao Rohoni watu kama hawa, wanawekwa kundi moja na akina Sara, na Rebeka, na Mariamu, na Elizabeti na wengineo. Kwasababu wamevuka viwango cha utoto, hadi kufikia hatua ya utu uzima ya kuzaa na kulea.

Swali ni je! Wewe, dada upo katika kundi gani? Bwana anapokuona anakutambuaje? msichana? Au Mtu? Mtoto? Au Mama?. Kabla hujafikiria kuyatazama Maisha ya mitume wa Yesu mfano wakina Petro waliishije, embu tafakari kwanza, Maisha ya wanawake wacha Mungu katika biblia waliishije. Hiyo itakusaidia sana mwanamke.

Tamani sana, Kristo akutambue kama “Mama” Ni heshima ya juu sana, Kristo anaweza kumpa mwanamke, iliyosawa na ya “Kitume”. Kua kiroho timiza wajibu wako wa kuitangaza injili na pia kuwasaidia wengine kumjua Mungu rohoni.

Bwana akubariki.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 2)

Hii ni sehemu ya pili ya mfululizo wa masomo kwa wanawake, katika sehemu ya kwanza tumeona, ni kwanini Bwana alipokutana na yule mwanamke mwenye dhambi, alimtambua kwa jinsia yake (Yaani “mwanamke”) na sio kwa mwonekano wake wa kike pengine wa kiumri au  wa kimaumbile. Hiyo ni kufunua kuwa ujumbe alioubeba yule mwanamke ulikuwa ni wa kijinsia.. yaani maalumu kwa wanawake. Hivyo kama hukupata maelezo yake, unaweza kunitumia ujumbe inbox nikakutumia.

Leo tutaenda katika sehemu ya pili: ya BINTI.

Mahali pengine, Bwana Yesu, aliwatambua wanawake wengine kama, binti zake.. Na cha ajabu ni kuwa, wengine walikuwa pengine wana umri mkubwa kuliko yeye, lakini bado aliwaita BINTI zake, akifunua kuwa kutazama kwake hakukuwa katika jicho la kimwili bali la rohoni. Embu tusome, kisa hiki kimoja..kisha tuone ni ujumbe gani Bwana alitaka kuupitisha kwa ulimwengu kupitia mwanamke huyu.

Mathayo 9:20 “Na tazama, mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, alikuja kwa nyuma, akaugusa upindo wa vazi lake.

21 Kwa maana alisema moyoni mwake, Nikigusa tu upindo wa vazi lake nitapona.

22 Yesu akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, BINTI YANGU; imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile.”.

Swali la kujiuliza ni kwanini alimtambua mwanamke huyu kama binti na sio pengine kama Mama, au bibi?

Ni kwasababu ya Imani yake ya kipekee aliyokuwa nayo kwake..Ambayo hakuiona kwa watu wengine wote waliomfuata, ijapokuwa alihangaika kwa miaka 12 kutafuta suluhu la matatizo yake asipate, lakini alipofika kwa Yesu kwa mara ya kwanza tu hakumuhesabia kama mmojawapo wa wale matapeli aliokutana nao, huko nyuma, waliomchukulia fedha zake.

Bali alimwamini moja kwa moja kwa asilimia 100, akasema, nitakapoligusa tu pindo la vazi lake, muda huo huo nitakuwa mzima, kumbuka hakusema sio “naamini nitapona, au pengine nitapona” hapana, bali alisema “NITAPONA” kuonyesha kuwa alikuwa na uhakika wa yule aliyekutana naye sio mbabaishaji au tapeli…. Na ndio maana akaona hata hakuna sababu ya kwenda kumsumbua kuzungumza naye, au kumwomba aje kumtembelea, Bali aliona pindo la vazi lake, tu linatosha yeye kuwa mzima..

Na Yesu alipoiona Imani yake saa ile ile akamgeukia na kumwita “Binti yangu”.. Akampa nafasi ya kipekee sana Kama Mtoto wa kike aliyemzaa yeye mwenyewe, ambaye ana haki zote za kupokea mema yote ya Baba yake.

Tujiulize ni wanawake wangapi leo Bwana anaweza kuwaita binti zangu? Usidhani Kristo kukuita binti yake, kwasababu ya umri wako mdogo, au mrembo wako, au utanashati wako, hilo halipo, yeye hana jicho la mwilini, kama sisi tulilonalo, haangalii umri wala umbile.

Kama wewe ni mwanamke lakini unafika kwa Kristo ili kujaribu jaribu tu, uone kama Bwana atakujibu au la!,atakusaidia au la! unamlinganisha na wale waganga wa kienyeji uliowahi kuwatembelea huko nyuma.. uone kama atajibu au la!. Ujue kuwa wewe sio binti wa Yesu.

Mabinti wa Yesu, tangu walipokutana na Yesu utawakuta wametulia kwa Bwana hadi sasa, wanaouhakika na waliyemwendea, hawahitaji kusaidiwa na mtu, kuelewa kuwa Yesu ni muweza, wanafanya mambo yao wakiwa wame-relax, huwezi kuwakuta leo kanisani Kesho, disco,  leo wamevaa magauni, Kesho wanakatiza barabarani na visuruali na vikaptura, leo kwa nabii huyu Kesho kwa yule..huwezi kuwakuta wapo namna hiyo.

Hao ndio binti za Mungu. Na faida yao ni kuwa kwasababu wameshaitwa binti za Mungu, tayari wanaourithi kutoka mbinguni. Jambo ambalo wengi hawajui wakidhani kila mtu atakuwa mrithi wa kila baraka ya Mungu mbinguni.

Dada/mama/bibi tambua ni nini Kristo anatamani kuona kwako, acha kutangatanga na huu ulimwengu, Acha kujaribu jaribu, maanisha kumfuata Kristo.. Yeye mwenyewe anasema.

2Wakorintho 6:17 “Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.

18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu WANANGU WA KIUME NA WA KIKE”,

Kumbuka hizi ni siku za mwisho, Kristo anarudi siku yoyote. Bado tu hujatulia kwa Bwana? Injili tuliyobakiwa nayo sasa hivi sio ya kubembelezewa tena wokovu, ni wewe mwenyewe aumke usingizini, umtafute Mungu wako. Kwasababu muda umeshaisha.

Maran atha..

Usikose sehemu ya tatu na ya mwisho ya Makala hii, ambayo, tutaona pia ni kwanini Bwana Yesu aliwatambua wanawake wengine kama MAMA.

Bwana akubariki..

Maran atha

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu katika sehemu ya kwanza ya  mfululizo wa masomo ya wanawake.

Yapo masomo mengine kwa wanawake yameshapita nyuma , ikiwa yalikupita na utapenda kuyapata, basi utanitumia msg inbox nikutume.

Lakini leo tutatazama, namna ambavyo Bwana Yesu alivyowatambua wanawake aliokutana nao, katika kipindi chote cha huduma yake alipokuwa hapa duniani.

  • Kuna wakati alipokutana na mwanamke Fulani, alimtambua kama BINTI
  • Kuna wakati tena alipokutana na mwanamke Fulani, alimtambua kama MAMA
  • Na kuna wakati pia alipokutana na mwanamke Fulani alimtambua kama MWANAMKE.

Haya ni mambo ambayo unapaswa uyaelewe, na kuyazingatia sana unaposoma biblia. Kwasababu kila utambulisho ulibeba ujumbe maalumu kwa kundi husika.

1) Leo tutaangazia Utambulisho wa kwanza wa Bwana ambao ni  MWANAMKE.

Unajua mpaka mtu akuite “mwanamke” ni wazi kuwa halengi kitu kingine Zaidi ya “jinsia” yako, halengi umri wako, au ukubwa wako, au umbo lako, hapana bali jinsia. Ndicho alichokifanya Bwana Yesu alikupokutana na baadhi ya wanawake, hakuwa na nia ya kuwaita kwa vyeo vyao au kwa  mionekano yao labda ni wadogo au wakubwa, au wazee au vijana hapana bali aliwaita “mwanamke” kulenga jinsia yao Zaidi..

Kufunua kuwa, ujumbe ulio nyuma yake, ni mahususi kwa watu wa jinsi hiyo. Hivyo, embu tusome kwa pamoja habari ya yule mwanamke aliyekuwa na dhambi nyingi, tuone ni nini alikifanya mpaka ikampelekea Bwana Yesu kumtambua kama mwanamke na sio, kitu kingine..

Tusome..

Luka 7:37 “Na tazama, mwanamke mmoja wa mji ule, aliyekuwa mwenye dhambi, alipopata habari ya kuwa ameketi chakulani katika nyumba ya yule Farisayo, alileta chupa ya marimari yenye marhamu.

38 Akasimama nyuma karibu na miguu yake, akilia, akaanza kumdondoshea miguu machozi yake, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake, akiibusu-busu miguu yake na kuipaka yale marhamu.

39 Basi, yule Farisayo aliyemwalika alipoona vile, alisema moyoni mwake, Mtu huyu kama angekuwa nabii, angemtambua mwanamke huyu amgusaye, ni nani, naye ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi.

40 Yesu akajibu akamwambia, Simoni, nina neno nitakalo kukuambia. Akasema, Mwalimu, nena.

41 Akasema, Mtu mmoja mkopeshaji alikuwa na wadeni wawili; mmoja amwia dinari mia tano, na wa pili hamsini.

42 Nao walipokuwa hawana cha kumlipa, aliwasamehe wote wawili. Katika hao wawili ni yupi atakayempenda zaidi?

43 Simoni akajibu akasema, Nadhani ni yule ambaye alimsamehe nyingi. Akamwambia, Umeamua haki.

44 Akamgeukia yule mwanamke, akamwambia Simoni, Wamwona mwanamke huyu? Niliingia nyumbani kwako, hukunipa maji kwa miguu yangu; bali huyu amenidondoshea machozi miguu yangu, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake.

45 Wewe hukunibusu; lakini huyu tangu nilipoingia hakuacha kunibusu sana miguu yangu.

46 Hukunipaka kichwa changu mafuta; bali huyu amenipaka miguu yangu marhamu.

47 Kwa ajili ya hayo nakuambia, Amesamehewa dhambi zake ambazo ni nyingi, kwa kuwa amependa sana; lakini asamehewaye kidogo, huyo hupenda kidogo.

48 KISHA ALIMWAMBIA MWANAMKE, UMESAMEHEWA DHAMBI ZAKO”.

Unapoitafakari habari hiyo unaona nini kwa huyu mwanamke aliyekuwa gwiji wa dhambi, aliyefahamika mji mzima..? Utagundua kuwa Toba au kibali chake hakikuja katika maneno yoyote? Bali katika vitendo ambavyo Bwana Yesu aliona hata wakuu wa dini waliomwalika karamuni, hawakuvitenda.

Mwanamke huyu alitoa mafuta yake yenye thamani nyingi sana, akaanza kuusafisha mwili wa Kristo, ambao aliouna umechafuka sana, alianza kujitoa bila kujali ni nini anapoteza, na kikubwa Zaidi akatumia na nywele zake za thamani, jambo ambalo si la kawaida kwa wanawake wa kidunia wapendao urembo kufanya, kama tu mvua ikimdondokea atatafuta kibanda ajifiche ili tu nywele zake zisiharibike, sembuse kupangusa miguu michafu kwa nywele zake?

Lakini huyu mwanamke alikuwa radhi kufanya hivyo..Na kwa kitendo kile, moyo wa Bwana uliguswa sana, hadi kumsamehe dhambi zake, japokuwa hakutoa Neno lolote kinywani mwake…akasema “mwanamke” umesamehewa dhambi zako.

Na wewe kama mwanamke kabla hujafikiria kujifunza kwa akini Petro, embu chukua muda kwanza, ujifunze kwa wanawake kama hawa, ambao mpaka sasa tunasoma habari zao, ambao Bwana Yesu aliwaona wanathamani kubwa kuliko hata yule Farisayo tajiri (Simoni), aliyemwalika nyumbani kwake, kula chakula..

Mwanamke Ikiwa utatamani, Kristo akusamehe, au akupe kibali, au akufungue, au akuponye,  Maisha yako. Basi Jibidiishe, kuusafisha mwili wa Kristo, kwa kumaanisha kweli, kweli. Tukisema mwili wa Kristo, tunamaanisha, Kanisa lake, na kazi yake. Jitoe kwa hali na mali zako. Hata kama huna chochote, kapige deki, kasafishe hiki au kile.. Lakini usiwe mwombaji tu wa maneno.

Hichi ndicho Bwana alichokiona wa wanadamu wa jinsia hii, (wanawake). Kumjali Kristo ni sehemu ya wito wao hapa duniani, na unathamani kubwa kama tu karama nyingine za kitume zilivyo mbele ya Kristo.

Muhudumie Bwana mwanamke..

Luka 8:2 “na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,

3 na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao”.

Bwana akubariki.

Maran atha

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Mwendelezo wa sehemu ya pili unakuja…ambapo tutaona kwanini Bwana aliwatambua baadhi ya wanawake na kuwaita binti zake, na sio, kwa vyeo vyao au ukubwa wao..

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

SOMO no.02 (BINTI WA YEFTHA).

Karibu katika mwendelezo wa masomo yawahusuyo wanawake wa kwenye biblia,  Leo tutamtazama mwanamke mmoja/binti mmoja aliyekuwa mtoto wa pekee wa Mwamuzi wa Israeli.

Binti huyu alikuwa alikuwa ni mtoto wa pekee wa mtu aliyeitwa Yeftha, ambaye alikuwa ni Mwamuzi wa taifa la Israeli. Nafasi ya mwamuzi katika Israeli nyakati hizo, ilikuwa inakaribia sana kufanana na ile ya Mfalme, ingawa sio ya kifalme.  Hivyo mtu aliyekuwa mwamuzi katika Israeli katika nyakati hizo, alikuwa ni Mkuu sana, na mwenye kujilikana na kuheshimiwa katika nchi nzima.

Lakini tunasoma katika biblia alitokea Mwamuzi mmoja aliyeitwa Yeftha, ambaye huyu alikuwa ni shujaa sana..Na hakuwa na mwana wa kiume katika nyumba yake bali wa kike tu, tena mmoja. Lakini tunasoma wakati Fulani alipokwenda vitani, alimwekea Bwana nadhiri kubwa, kutokana na ukubwa wa vita iliyoko mbele yake, alitazama mbele yake akaona hiyo vita anayotaka kwenda kukumbana nayo, sio ndogo!, na endapo ikitokea kashinda basi ni muujiza wa Mungu tu umefanyika, na si kingine, kwasababu katika hali ya kawaida ni ngumu kushinda…kwasababu wanaokwenda kupigana nao ni wengi kuliko wao na wenye nguvu kuliko wao.

Kwahiyo ili kujihakikishia ushindi zaidi, alimwekea Mungu nadhiri, kwamba endapo Mungu atampa ushindi, basi kile cha kwanza, kitakachotoka kumlaki wakati anarudi vitani atakitoa kiwe sadaka ya kuteketezwa mbele za Bwana. Na katika mawazo  yake pengine alilenga mtumwa wake mmoja, au ndugu mmoja aliye katika nyumba yake, ndiye atakayekuja kumlaki (kwani nyumba yake ilikuwa na watu wengi, kwasababu yeye alikuwa ni Mkuu katika Israeli). Lakini cha kushtusha ni kwamba alitokea Binti yake wapekee kuja kumlaki, kinyume na matarajio yake. Na alipomwona akahuzunika sana, lakini akawa hana cha kufanya…(Hawezi kuitangua nadhiri yake)

Hebu tusome kidogo habari yenyewe kisha tusonge mbele..

Waamuzi 11:28 “Lakini mfalme wa wana wa Amoni hakuyasikiza hayo maneno ya Yeftha aliompelekea.

 29 Ndipo roho ya Bwana ikamjilia juu yake Yeftha, naye akapita katika Gileadi na Manase, akapita na katika Mispa ya Gileadi, na kutoka hapo Mispa ya Gileadi akapita kuwaendea wana wa Amoni.

30 NAYE YEFTHA AKAMWEKEA BWANA NADHIRI, AKASEMA, KWAMBA WEWE UTAWATIA WANA WA AMONI MKONONI MWANGU KWELI,

31 ndipo itakuwa ya kwamba, kile kitakachotoka katika milango ya nyumba yangu kunilaki, hapo nitakaporudi na amani kutoka kwa hao wana wa Amoni, kitu hicho kitakuwa ni cha Bwana, nami nitakisongeza kiwe sadaka ya kuteketezwa.

 32 Basi Yeftha akavuka kuwaendea wana wa Amoni ili kupigana nao; naye Bwana akawaua mkononi mwake.

33 Akawapiga kutoka Aroeri hata kufikilia Minithi, miji ishirini, na mpaka Abel-keramimu, akawapiga kwa machinjo makuu mno. Basi hivyo wana wa Amoni walishindwa mbele ya wana wa Israeli.

34 Kisha Yeftha akafika Mispa nyumbani kwake, na tazama, binti yake akamtokea kumlaki, na matari na machezo; naye alikuwa ni mwanawe pekee; hakuwa na mwingine, mwana wala binti, ila yeye.

35 Ikawa alipomwona akayararua mavazi yake, akasema, Ole wangu! Mwanangu, umenitweza sana, nawe u mmoja miongoni mwa hao wanisumbuao; kwa kuwa mimi nimemfunulia Bwana kinywa changu, nami siwezi kurejea nyuma.

36 BINTI YAKE AKAMWAMBIA, BABA YANGU, WEWE UMEMFUNULIA BWANA KINYWA CHAKO; BASI UNIFANYIE SAWASAWA NA HAYO YALIYOTOKA KINYWANI MWAKO; KWA KUWA YEYE BWANA AMEKULIPIA KISASI JUU YA ADUI ZAKO, HAO WANA WA AMONI.

  37 Kisha akamwambia baba yake, Basi na nifanyiwe neno hili; niache peke yangu muda wa miezi miwili, ili nipate kwenenda milimani, na kuombolea uanawali wangu, mimi na wenzangu.

  38 Akamwambia, Haya, enda. Akampeleka mbali muda wa miezi miwili; naye akaenda zake, yeye na wenziwe, akauombolea uanawali wake huko milimani.

 39 Basi ikawa mwisho wa hiyo miezi miwili, akarudi kwa babaye, aliyemtenda sawasawa na ile nadhiri yake aliyokuwa ameiweka; naye alikuwa hajamjua mtu mume. Kisha ikawa desturi katika Israeli,

 40 kwamba binti za Israeli waende mwaka baada ya mwaka ili kumkumbuka huyo mwana wa Yeftha, Mgileadi, siku nne katika mwaka”

Leo nimetamani tujifunze kuhusu huyu binti, Kwasababu alikuwa ana roho ya Ushujaa ndani yake!..

Dada/Mama/ binti siku zote kumbuka hili: ni vizuri kwanza kujifunza kwa wanawake waliopo katika biblia kabla ya kuwatafuta wanaume.

Wanawake wengi wanapenda sana kujifunza kwa Isaka!.. Jinsi alivyonusurika kifo!, cha kuchinjwa na kutolewa sadaka ya kuteketezwa, lakini hawajui kuwa Isaka alinusurika tu!!, hakuchinjwa, wala hakutolewa sadaka… Yupo Shujaa mmoja katika biblia ambaye Alikubali mwenyewe kuchinjwa na nyama yake kukatwa katwa vipande na kisha kutolewa kama sadaka ya kuteketezwa!.. Ambaye pengine tutakapofika mbinguni tutamkuta ni mkuu kuliko ISAKA!..Na tutajilaumu sana kwanini hatukujifunza kutoka kwake!

Na huyo si mwingine zaidi ya huyu binti wa Yeftha!!. Binti huyu baba yake alimwambia dhahiri kabisa kwamba atakwenda kutolewa sadaka ya kuteketezwa!.. Jambo ambalo kiuhalisia ni gumu sana mtu kukubaliana nalo, lakini Binti huyu baada ya kupewa hizo taarifa!, wala hazikumwazisha.. wala hakuogopa kufa!, wala hakuogopa makali ya visu katika mwili wake, wala moto.. badala yake alisema maneno haya..

“36 BINTI YAKE AKAMWAMBIA, BABA YANGU, WEWE UMEMFUNULIA BWANA KINYWA CHAKO; BASI UNIFANYIE SAWASAWA NA HAYO YALIYOTOKA KINYWANI MWAKO; KWA KUWA YEYE BWANA AMEKULIPIA KISASI JUU YA ADUI ZAKO, HAO WANA WA AMONI”.

Bila shaka maneno kama haya, Isaka mwana wa Ibrahimu asingeweza kusema, pale alipokuwa anapelekwa mlimani kuchinjwa! Na Baba yake. Si ajabu, Ibrahimu hakumwambia Isaka chochote, kwamba anakwenda kumchinja na kumtoa sadaka!..pengine ingekuwa kitimtimu pale!, pangekuwa hapatoshi!, pangetokea vurugu kubwa sana!…Ndio maana Ibrahimu alimficha, kwasababu alimwona pengine hana huo utayari wa kujitoa kufa!!.

Mwanzo 22: 6 “Basi Ibrahimu akazitwaa kuni za hiyo sadaka, akamtwika Isaka mwanawe; akatwaa moto na kisu mkononi mwake, wakaenda wote wawili pamoja.

 7 Isaka akasema na Ibrahimu baba yake, akinena, Babangu! Naye akasema, Mimi hapa, mwanangu. Akasema, Tazama! Moto upo, na kuni zipo, lakini yuko wapi mwana-kondoo kwa sadaka ya kuteketezwa?

 8 Ibrahimu akasema, Mungu atajipatia mwana-kondoo kwa hiyo sadaka, mwanangu. Basi wakaendelea wote wawili pamoja”.

Huyo ni Isaka anaulizia sadaka ya kuteketezwa ipo wapi!, maana yake yeye haimwingii akilini kujiweka katika hilo kundi!, kwamba yeye anaweza kuwa hiyo sadaka!.. Lakini alikuja kutokea Shujaa mmoja!, binti mdogo, ambaye taarifa za msiba si kitu kwake!, ambaye visu shingoni si kitu kwake, ambaye moto juu ya mwili wake si kitu kwake.. Zaidi ya yote alikuwa mtoto, tena ni binti, na tena ni BIKIRA!.. Lakini alikuwa na Imani kubwa kuliko ya Isaka!!. Huyu taarifa za kuchinjwa zilipomjia hakupepesuka wala hazikumshutua, alianza kuufikiria mambo mengine kabisa (Ubikira wake!!..na kwenda kuomboleza kwaajili ya huo, na alipomaliza kwa miezi miwili), kama vile kondoo apelekwavyo machinjoni, alikwenda mwenyewe na akachinjwa na kufa na kuteketezwa..

Labda inawezekana hujui vizuri!, sadaka ya kuteketezwa inakuwaje.

Sadaka ya kuteketezwa ambayo Mungu alimjaribu nayo Ibrahimu amtoe mwanawe , ilikuwa ni kwamba.. mtoto Yule anakamatwa, anafungwa kamba na kisha kisu kinapitishwa shingoni, anachinjwa kama ng’ombe, damu inachuruzika, na baada ya kuchinjwa, mwili wake unakatwa vipanda vipande, kisha vile vipande vinawekwa juu ya kuni, zilizopo juu ya mawe, na moto unawashwa na ile nyama inateketea kabisa mpaka inakuwa jivu!.. Hiyo ndiyo sadaka aliyokusudiwa Isaka!, ambayo Mungu alimwepusha nayo haikumpata, lakini ikatimia kwa shujaa huyu mmoja Binti wa Yeftha!, yeye alikubali mwenyewe kwenda kuchinjwa!.

Waebrania 11:35  “Wanawake walipokea wafu wao waliofufuliwa. Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora”

Isaka aliibeba picha ya Yesu tu!, lakini huyu binti alilibeba tukio zima la Yesu!.. alionja kile Bwana alichokipitia pale Kalvari.. Na baada yake hatuoni mtu mwingine, awe mwanaume au mwanamke aliyefanya jambo la kishujaa kama hilo!, wengine wote kwenye biblia waliingia kwenye dhiki bila idhini zao, walishikwa wakakatwa vichwa na kuchinjwa, lakini si kujipeleka wenyewe kuchinjwa!…

Jambo hilo tunaliona kwa watu wawili tu! Kwenye biblia nzima, wa kwanza ni MKUU WA UZIMA MWENYEWE, MWAMBA-YESU KRISTO..Na mwingine ni huyu “Binti wa Yeftha”.

Dada/Binti /mama umeona ni jinsi gani una mashindano makubwa mbele yako??… Siku ile utajitetea vipi, kwamba umeshindwa kujitoa kwake!, na kumtumikia  kwasababu tu wewe si mwanaume??..Leo hii unaogopwa kuchekwa!, wenzako walikufa kabisa!..jambo ambalo hata mwanaume hawakuweza kulifanya!.. Bado huoni tu! Siku ya hukumu binti wa Yeftha atasimama kuhukumu mabinti wengi??..Bado huoni tu hilo!..fahamu kuwa!..hukumu ya wanawake itakuwa ni kali kuliko ya wanaume.. kwasababu katika biblia wapo wanawake waliofanya makubwa kuliko wanaume.  Eliya alimkimbia Yezebeli, ili ayanusuru maisha yake, lakini huyu binti wa Yeftha, yeye anakifuata kifo mwenyewe!..jiulize kati ya hao wawili ni yupi mwenye imani kubwa!..Wanawake kama hawa pamoja na mfano wa Yule Malkia wa Sheba Bwana Yesu aliyemtaja, watasimama kuhukumu vizazi vyetu..

Mathayo 12:42 “Malkia wa kusini atasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, naye atawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu yeye alikuja kutoka pande za mwisho za dunia ili asikie hekima ya Sulemani, na hapa yupo aliye mkuu kuliko Sulemani”.

Hivyo, wewe kama Mwanamke, simama itambue nafasi yako!.. kama Dada simama!, kama binti simama!.. usiogope kufa!, badala yake uwe tayari kufa hata kwaajili ya imani, usiogope kupitia dhiki,badala yake uwe tayari kukumbana nazo kwaajili ya imani yako, usiogopwe kuonwa mshamba unapoacha mambo yote ya kidunia, na fashion zote!..Badala yake uwe tayari kuonekana umerukwa na Akili, Fahamu kuwa thawabu yako ni kubwa mbinguni.. Kuanzia leo anza kupiga mbio, ukijifunza kwa wanawake mashujaa katika biblia..

Vile vile usiutamanie  udunia, ukasema ngoja uule ujana, ndio utamtumikia Mungu, siku ile huyu binti wa Yeftha atasimama kukuhukumu, kwasababu yeye alikufa katika ubikira wake bila mume, angeweza kumwambia baba yake amruhusu akaolewe kwanza miezi miwili ndipo, amtoe sadaka!..lakini hakufanya hivyo, aliuthamini ubikira wake, akafa hivyo hivyo..

Vile vile hakuwa mtoto wa maskini, labda tuseme amechoka maisha ndio maana kakubali kujitoa afe!.. hapana!, alikuwa ni mtoto wa Mwamuzi wa Israeli..Ni tajiri sana!, kwasababu waamuzi walikuwa ni kama wafalme, lakini hakuutumainia utajiri wake, wala ubikira wake, wala uzuri wake.. Alikubali kuondoka!, kwasababu alijua, anao mji unao mngojea huko mbele. Yeru salem mpya. Alijua ufufuo unakuja na atakuwa mkuu katika ufalme wa mbinguni.

Kumbuka Mungu aliwachagua tu wanaume kwenye biblia wawe kama mwonekano tu!.. ndio maana utaona kila mahali wanatajwa wanaume..kama Isaka, Yakobo, Eliya n.k Lakini hiyo haimaanishi kuwa wao ndio wa kwanza katika ufalme wa Mbinguni.. Kwaufupi ni kwamba Mbinguni watakuwepo wanawake watakaopata thawabu kubwa hata kuliko hata wakina Ibrahimu, Isaka na akina Eliya na Musa. Kwasababu Mungu siku zote hana upendeleo.

Hivyo unaposoma biblia, anza kutafuta matendo ya wanawake mashujaa, ujifunze kwao, na vile vile, jifunze kwa wale waliojiharibia njia zao pia, ili uchukue tahadhari.

Mwisho wa muhtasari huu kumhusu “binti wa Yeftha” shujaa wa Bwana. Usikose mwendelezo wa wanawake wanaofuta!.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Sadaka ya kuinuliwa ni sadaka ya namna gani?

FUNGUO WALIZOKUWA NAZO MABINTI WATANO WA SELOFEHADI!

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji zilikuwaje?

Rudi nyumbani

Print this post

SOMO no. 01 (HAWA)

HAWA

Karibu katika mfululizo wa masomo yawahusuyo wanawake wa kwenye biblia, katika mfululizo huu, tutajifunza mengi yahusuyo majukumu ya wanawake kibiblia.

Katika biblia kulikuwepo na wanawake waliokuwa mfano mzuri wa kuigwa, na ambao hawakuwa mfano mzuri wa kuigwa, vile vile walikuwepo wanawake waliokuwa ni manabii wa kweli, na vile vile walikuwepo manabii wa uongo.

Kama mwanamke ni vizuri kujifunza kwa wote hawa, kabla ya kuanza kujifunza kwa Manabii na watumishi wa Mungu wa kiume katika maandiko.

Kwasababu mbio za wanaume ni tofauti na za wanawake. Katika tuzo na thawabu mbinguni hawatalingalishwa wanaume na wanawake.. bali wanaume kwa wanaume, na wanawake kwa wanawake..

Hata katika mbio za kidunia, wanawake wanapewa tuzo kulingana na mbio zao wao, na wanaume vivyo hivyo.. huwa hawachanganywi katika mbio, vinginevyo tuzo zote zingeenda kwa wanaume tu!, kwasababu ni ngumu wanawake kuwazidi mbio wanaume..

Hivyo ili kulitatua hilo, ndipo wanawatenga wanaume na wanawake.. Na Yule anayeibuka kidedea kwa wanawake anapewa tuzo sawa na yule aliyeibuka kidedea kwa wanaume..

1Wakorintho 9:24“ Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.

25  Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika.

26  Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa; ”

Hivyo leo tutaanza kwa kujifunza kutoka kwa mwanamke wa kwanza, aliyeitwa Hawa. Kwa Hawa yapo mazuri ya kujifunza lakini pia yapo mabaya tusiyopaswa kujifunza kwayo..

Hawa ndiye mwanamke wa kwanza kuumbwa, na biblia inasema aliumbwa kama Msaidizi kwa Adamu (Mwanzo 2:20). Amsaidie katika majukumu yote ambayo Mungu alimpa Adamu. Hivyo HUDUMA ya kwanza ya Hawa aliyopewa na Mungu ilikuwa ni USAIDIZI!.. Na si “mke” Au “Mama”  Mungu hakumuumbia Adamu mke!, suala la mke lilikuja baadaye!.. Hakumuona Adamu na kumwona Yupo mwenyewe hivyo anahitaji mke wa kumliwaza!, au anahitaji mama wa kumlelea watoto wake!, ..Hapana!.. bali aliona anahitaji msaidizi wa kumsaidia shughuli alizompa..Hilo! ndilo la kwanza.. hayo mengine yalikuja baadaye.

Mwanzo 2:20 “Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; LAKINI HAKUONEKANA WA KUMSAIDIA ADAMU ALIYEFANANA NAYE”

Na usaidizi huo Hawa aliopewa si wa kutumia nguvu, ndio maana hakuumbwa na misuli, zaidi ya yote aliumbwa mwororo na mwenye umbo la wastani. Mungu angetaka awe msaidizi wa kutumia nguvu bila shaka angemuumba mwenye nguvu na mkubwa kuliko Adamu, lakini tunaona hakuwa hivyo.

Ikimaanisha kuwa usaidizi wake sio wa kutumia manguvu, bali hekima na akili. Wanyama kama ng’ombe, punda, farasi hao ndio waliumbwa kama wasaidizi wa Adamu kwa kutumia nguvu ndio maana waliumbwa wenye nguvu kuliko Adamu, ili ngamia amsaidie Adamu safari yake, hana budi awe mkubwa na mwenye nguvu kuliko Adamu. Lakini si Hawa!, usaidizi wa Hawa ulikuwa ni wa tofauti..

Hivyo USAIDIZI ndio huduma ya kwanza HAWA aliyopewa, Na hiyo hiyo huduma ya usaidizi Mungu alianza kuiweka kwa mwanamke wa kwanza anayeitwa Hawa, na wazao wote wa kike wanaofuata baada yake, wanayo hii HUDUMA ndani yao..Ndio maana wanaendelea kuzaliwa wakiwa kama Hawa, kimwonekano, wasio na misuli kama Hawa wa kwanza.

Hivyo hilo ni jambo la kwanza ambalo kila mwanamke anapaswa alijue, na shetani asilopenda walijue. Mungu anapomwangalia mwanamke yeyote duniani, anamwangalia kwanza kama MSAIDIZI kabla ya kumwangalia kama mke au Mama!. Hivyo kitu cha kwanza mwanamke anachopaswa kukifikiri na kukitafuta si Mume ili kumpendeza Mungu..bali Ile huduma ya usaidizi iliyopo ndani yake!, namna atakavyoivumbua na kuitumia ipasavyo.

Mwanzo 2:18 “Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye”

Hivyo kama mwanamke ni lazima ujue!.. Usaidizi wako ni nini katika mahali ulipo!…Kibali ulichopewa unakitumiaje!.. ukienda mahali unapoona ni rahisi mwanamke kuaminika, na kukubalika kuliko mwanaume ni lazima ujiulize ..Ni kwanini iwe hivyo?..Ni lazima ujue kuwa kuna jambo la kusaidia pale, ambalo haliwezi kufanywa na wanaume!.. na jambo hilo si la kutumia nguvu bali akili, na hekima..Hivyo ni vyema uwe mshapu wa kulivumbua na kulitekeleza..

Labda tuchukue mfano pale katika Edeni.

Pengine wakati Adamu anawapa majina wale wanyama.. Hawa alipokuja akaweka mfumo bora wa kuwakumbuka, kwa kuwagawanya katika makundi au kwa kazi zao wanazozifanya!..ambao pengine kwa Adamu peke yake ingekuwa ni ngumu au asingeweka utaratibu mzuri..(Huo ni mfano tu).. Maana yake ni kwamba Hawa alipewa akili ya ziada, ambapo ikichanganyikana na ile ya Adamu, basi kazi ingefanyika vizuri zaidi!..

Vile vile katika kanisa, yapo mambo mengi hayapo sawa, ambayo yanahitaji usaidizi!.. Hayo yamefichwa kwenye macho ya wanaume, lakini yamewekwa wazi kwa wanawake werevu.

Katika kanisa ipo mifumo mingi ambayo kweli ni ya kiMungu, lakini endapo ikiendelea kwa namna hiyo hiyo, inaweza kuchukua muda mrefu zaidi kutekelezeka, au hata kama ikitekelezeka basi isitekelezeke kwa ufasaha.. Ni wajibu wako wewe kama mwanamke wa kikristo kutafuta namna ya kulitatua hilo.

Umeona kuna jambo Fulani linakwenda kupotea, haraka sana unaingia kwenye maombi, au unakusanya wenzako wachache na kuingia kwenye maombi kuliombea,  au kuna jambo umeona halijafanyika vizuri chukua nafasi hiyo wewe kulifanya lifanyike vizuri zaidi ili mambo yasiharibike,  usisubiri mwingine afanye!, kila jambo unaloona ni tatizo au linaelekea kuwa gumu unatafuta namna ya kulitatua haraka sana, …Na hulitatui kwa kumuagiza mtu mwingine akalifanye! Bali kwa wewe mwenyewe kulifanya!… vinginevyo wewe hutakuwa tena msaidizi, bali ndiye unayesaidiwa kutekelezewa majukumu yako.

Kumbuka Sifa moja ya msaidizi sio yeye kusaidiwa!, bali ni yeye kusaidia. Kwahiyo kila kitu mwanamke anachokiona kinahitaji marekebisho na msaada, hana budi kukifanya yeye kabla ya kumwambia mwingine, ili akidhi vigezo vya kuwa msaidizi..

Na hekima ya kuona mambo ambayo yanahitaji msaada katika kanisa au katika maisha inatoka kwenye Neno la Mungu. Huwezi kukaa hulijui Neno la Mungu, halafu uwe na jicho la kuona marekebisho!.. Itakuwa ni ngumu sana, zaidi utaishia kudanganywa na Yule mwovu na kufanya uharibifu mkubwa kwasababu wewe ni lango!

Hawa alianza vizuri kazi ya usaidizi, lakini alipoanza kutoka nje ya mpango wa Mungu, na kwenda kutafuta maarifa kinyume na maagizo ya Mungu, akajikuta badala ya kumsaidia Adamu kuujenga ufalme, akajikuta anamsaidia kuubomoa!.. Na anguko lake likawa kubwa ambapo madhara yake mpaka leo hii yapo!!.

Vile vile mwanamke yeyote asipolijua Neno la Mungu na kudumu katika hilo, basi kazi yake au macho yake yatakuwa hayaoni kujenga bali kubomoa (Na hatajua kama amepofushwa macho). Na mwanamke ndiye shabaha ya kwanza ya adui kutafuta kupitishia uharibifu wake kabla hata ya mwanaume.

Hivyo kama mwanamke hauna budi kutafuta kujifunza Neno kwa bidii..usiku na mchana, ili hekima iingie ndani yako, ili macho yako yaone madhaifu sahihi, na uweze kuyarekebisha. Hilo ndio jukumu lako la kwanza ulilopewa, hayo mengine ya kuwa Mama, au mke hayana umuhimu sana zaidi ya hilo la USAIDIZI!.

Ukifanyika kuwa msaada mkubwa katika kazi ya Mungu na kuifanya ikue na kustawi, basi fahamu kuwa Mungu anakuheshimu sana na una thawabu kubwa sana mbinguni, kwasababu ndiyo huduma ya kwanza Mungu aliyompa mwanamke. (Unakuwa umetii agizo la Msingi na la awali)

Hata Bwana Mungu wetu, alipoona kutakuwa na kasoro nyingi baada ya Bwana wetu Yesu kuondoka duniani, alituachia msaidizi, ambaye ndiye Roho Mtakatifu. Kazi ya Roho Mtakatifu sio sisi kumsaidia yeye, bali ni yeye kutusaidia sisi..

Warumi 8:26  “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.

27  Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu”

Je na wewe unachunguza mambo?, na kuchukua udhaifu wa wengine, na hata wa kazi ya Mungu, na kuwa msaidizi bora?..kama bado!.. anza leo kwa bidii, na utaona jinsi Mungu atakavyotembea na wewe kwa viwango vingine!

Bwana akubariki.

Huu ni msingi wa kwanza tuliouweka,kuhusu huduma ya kwanza ya Mwanamke!..Tutazidi kusonga mbele kutazama, wanawake wengine, na mambo ya kujifunza kuhusu wao, hivyo usikose mwendelezo.

Bwana akubariki.

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

KIKWAZO CHA EUODIA NA SINTIKE.

Rudi nyumbani

Print this post

FUNGUO WALIZOKUWA NAZO MABINTI WATANO WA SELOFEHADI!

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo litukuzwe daima, karibu katika kuyatafakari maandiko.

Katika biblia tunasoma Kisa cha mabinti wa tano wa mtu mmoja, wa kabila la Manase, waliokuwa mashujaa katika Imani, hata kuibadilisha taratibu ambazo zilikuwepo.

Zamani wakati wana wa Israeli wanatoka Misri, kuelekea Kaanani. Mungu alimpa Musa maagizo ya kuigawanya hiyo nchi watakayoiendea.. Kwamba kila kabila, lipate sehemu ya ardhi katika hiyo nchi ya kaanani wanayoiendea. Lile kabila lenye watu wengi, basi litapewa sehemu kubwa ya ardhi, na lile lenye watu wachache basi litapewa sehemu ndogo ya ardhi.  Na kabila la Yuda ndio kabila lililokuwa na watu wengi kuliko kabila zote za Israeli, na kabila la Manase ndilo lililokuwa dogo kuliko yote (yaani lenye watu wachache).

Hivyo wakati wa kugawa urithi, walikuwa wanaangaliwa wale wazee wa ukoo ambao ndio vichwa vya ukoo, wanaomcha Mungu, hao ndio wanaopewa labda tuchukue mfano, hekari elfu moja, na hao ndipo wanagawa hizo ekari elfu kwa watoto wao wa kiume, kufuatia kila familia iliyopo chini yao. Hivyo mwisho wa siku kila familia ilikuwa inapata urithi wa ardhi katika hiyo nchi ya Kaanani waliyokuwa wanaiendea.

Lakini sasa katika hilo kabila lenye watu wachache kuliko kabila zote, yaani kabila la Manase, kulikuwepo na mtu mmoja ambaye alikuwa mashuhuri katika kumcha Bwana, ambaye naye pia alihesabiwa kama kichwa, ambaye aliandikiwa urithi katika hiyo nchi waliyokuwa wanaiendea.. Mtu huyo aliitwa SELOFEHADI.

Lakini kwa bahati mbaya mtu huyo alikufa kabla ya kuzaa mtoto wa kiume ambaye angerithi sehemu ya urithi huo, akawa anao mabinti tu!. Hivyo kutokana na jambo hilo, wana wa Israeli wakalitoa jina lake miongoni mwa watakaopata sehemu ya ardhi katika hiyo nchi ya ahadi wanayoiendea..Kwasababu wanawake hawawezi kupewa urithi!..

Lakini tunasoma jambo moja la kipekee lililotokea..kwa mabinti wa huyo Selofehadi, hatujui Baba yao aliwafundisha nini, lakini tunasoma kwamba walifanya jambo la kipekee kugeuza sheria na taratibu za Israeli kwa IMANI. Kwani walipoona tu! Baba yao amekufa na sehemu yake ya urithi imeondolewa, hawakuridhika, wakasema watamwendea Musa na kudai haki ya baba yao.. Kwamba sehemu ya urithi wa baba yao wapewe wao!.. jambo ambalo ni kinyume na utaratibu, kwani wanawake hawana ruhusa ya kurithi mali..Lakini wanawake hawa watano wa familia moja!, walishindana mpaka wakapata haki yao hiyo.

Hebu tusome kidogo..

Hesabu 27:1 “Wakati huo wakakaribia hao binti za Selofehadi, mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, wa jamaa za Manase mwana wa Yusufu; na majina ya hao binti za Selofehadi ni haya; Mala, na Noa, na Hogla, na Milka, na Tirsa.

 2 Nao wakasimama mbele ya Musa, na mbele ya Eleazari kuhani, na mbele ya wakuu, na mkutano wote, mlangoni pa hema ya kukutania, wakasema,

 3 Babaetu alikufa nyikani, naye hakuwamo katika mkutano wa hao waliojikutanisha kinyume cha Bwana katika mkutano wa Kora; lakini akafa katika dhambi zake mwenyewe; naye alikuwa hana wana wa kiume.

 4 Kwa nini basi jina la babaetu kufutwa katika jamaa zake kwa sababu alikuwa hana mwana wa kiume? Tupe sisi urithi pamoja na ndugu zake babaetu.

5 Basi Musa akaleta neno lao mbele ya Bwana

6 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

 7 HAO BINTI ZA SELOFEHADI WANANENA LILILO HAKI; KWELI UTAWAPA MILKI YA URITHI PAMOJA NA NDUGU ZA BABA YAO; NAWE UTAWAPA URITHI WA BABA YAO.

8 Kisha utanena na wana wa Israeli, na kuwaambia, MTU AKIFA, NAYE HANA MWANA WA KIUME, NDIPO UTAMPA BINTI YAKE URITHI WAKE.

9 Tena ikiwa hana binti, mtawapa nduguze urithi wake.

 10 Na ikiwa hana ndugu, mtawapa ndugu za babaye huo urithi wake.

  11 Tena ikiwa babaye hana ndugu, utampa huyo aliye karibu naye katika jamaa zake huo urithi wake, naye atakuwa nao; na neno hili litakuwa ni amri ya hukumu kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Musa”.

Kabla ya hapo hakukuwa na sheria kwamba mtu akifa, kama hana mtoto wa kiume urithi wake uende kwa mabinti wake, lakini Mabinti hawa watano, WALILIFUNGUA HILO KWA IMANI. Laiti wangeendelea hivyo, labda mpaka leo Israeli, mabinti wasingekuwa wanapata urithi wowote. Lakini kwa Imani ya hawa mabinti watano wa mtu mmoja ambao majina yao yalitajwa kama MALA, NOA, HOGLA,  MILKA, na TIRSA, waliweza kubadili majira kwa Imani..na kuwafanya mabinti wengine wote wa Israeli wafurahi.

Mwanamke au binti, unayesoma haya…kabla ya kwenda kujifunza kwa akina Eliya, na Elisha, na Paulo walio wanaume, hebu jifunze kwanza kwa wanawake hawa!, jinsi gani walivyopata urithi wao!, hawakwenda kwa waganga!..wala hawakwenda kwenye vikundi vya kijamii, wala hawakuanzisha mgomo!, wala vurugu.. bali walikimbilia kwa Musa, aliye mtumishi wa Mungu pekee wakati huo, huku wakiwa na hoja zilizo shiba,  ambaye huyo Musa alilipeleka hoja zao kwa Baba wa mbinguni, na Baba wa mbinguni akatoa majibu..

Lakini sasa aliyesimama kama Musa, ni Bwana Yesu, huyo ndiye wa kukimbilia ili kudai urithi wako..Ukienda na hoja zenye nguvu mbele zake, utapata haki yako.. Na hoja zenye nguvu tunazipata katika Neno la Mungu..

Isaya 41:21 “Haya, leteni maneno yenu, asema Bwana; toeni hoja zenu zenye nguvu, asema mfalme wa Yakobo”.

Isaya 43: 26 “Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, UPATE KUPEWA HAKI YAKO”

Jambo linguine la kujifunza juu ya mabinti hawa watano ni UMOJA!. Hakutoka binti mmoja na kumfuata Musa.. hoja yake isingekuwa na nguvu.. Lakini walipojiunga mabinti wote watano na kuwa kitu kimoja..Ndipo hoja yao ilipokuwa na nguvu. Ni vile vile hata sasa, ili Hoja zetu ziwe na nguvu mbele za Mungu, ni lazima tuungane watu wa familia moja, ambao imani yetu ni moja, Baba yetu ni mmoja, na ndipo tukamsogelee.. Tukienda kwa umoja kama huo, basi nirahisi sana kupokea majibu kuliko kwenda mmoja mmoja..

Mathayo 18:19 “Tena nawaambia, ya kwamba WAWILI WENU WATAKAPOPATANA duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni”.

Umeona hapo, anasema “wawili wenu”.. maana yake ni zaidi ya mmoja.. watakapopatana… maana yake kinachotangulia ni kupatana na kukubaliana… na baada ya kupatana, wakiliomba hilo jambo watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.

Bwana atusaidie tuwe Umoja na imani kama ya mabinti wa Selofehadi pamoja na Umoja, ili tuweze kufungua milango iliyofungwa mbele yetu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

Je! Israeli wote wataokolewa siku ya mwisho kulingana na Warumi 11:26?

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

Kwa jina lake Ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.

NGUVU YA MNADHIRI WA BWANA.

Rudi nyumbani

Print this post

UTAPENDA KUCHANGIA HUDUMA HII?

Tutamshukuru Mungu kwa ajili yako, kwa mchango wako, ili kuifanya injili hii isonge mbele Tuma sadaka yako kwa namba hizi:
Airtel:+255789001312 -Devis Magembe
Mpesa: +255767992434-Denis Magembe