Title November 2021

MFANYE BWANA YESU MWENYEJI MAISHANI MWAKO.

Ipo tabia moja  ya kipekee ya wageni waliostaarabika. Kikawaida wageni walio wastaarabu huwa wanaonyesha tabia fulani baadhi ambazo wenyeji wanapaswa wazijue ili waweze kuchukuliana nao na kuendana nao.

Kikawaida mgeni sio mtu wa kuonyesha moja kwa moja kwamba anajitaji jambo fulani kutoka kwa mwenyeji, mgeni akija kukutembelea bila shaka hawezi kukuomba chakula hata kama ana njaa sana, utaona atakaa na wewe kimya, na  tena utakapofika wakati wa kuondoka, utaona anaondoka bila hata kukukumbusha suala la chakula, tena utaona anaondoka kwa furaha sana, na wakati mwingine hata kwa kukupa asante nyingi. Lakini moyoni, hajafurahishwa sana!.

Hivyo ni wajibu wako wewe kupambanua ni nini mgeni anahitaji kwa wakati huo. Kama ni chakula, au makazi au malazi.. Ili ajisikie yupo nyumbani kadhalika awe huru kuzungumza nawe zaidi..

Ukiona mgeni kakutembelea asubuhi jua kuna kitu anakihitaji kwako kwa asubuhi hiyo usimfanye akae mpaka jioni, wala usijifanye huelewi, ukiona mgeni kafika kwako mchana wakati wa kupata riziki, ujue ana nafasi pia katika hicho chakula, ukiona anashinda kwako mpaka jioni, ujue pengine anahitaji kulala kwako, mwekee mazingira ya kulala kwasababu pengine kuna jambo na atakapoona umemwelewa hali yake na umemruhusu ale chakula chako, au alale kwako, basi ni rahisi zaidi kusikia mengi kutoka kwake, au kukufunulia mengi.

Lakini ukimnyima riziki, au makazi, au malazi.. utafikiri kweli umemkomoa lakini hutasikia mengi, ambayo angetaka kukuambia..

Kadhalika Kristo naye kuna wakati anakuja kwetu kama Mgeni, au anatukaribia kama mgeni, na anakuwa anaonyesha tabia zote kama za mgeni. Atakuwa ana njaa, lakini atajifanya kama hana njaa, atakuwa anatamani kuja kulala na sisi lakini atajifanya kama anapita tu!. Ndicho kilichowatokea wale watu wawili waliokuwa wanakwenda Emau.

Hebu tuisome habari hiyo vizuri katika kitabu cha Luka.

Luka 24:13 “Na tazama, siku ile ile watu wawili miongoni mwao walikuwa wakienda kijiji kimoja, jina lake Emau, kilichokuwa mbali na Yerusalemu kama mwendo wa saa mbili.

14 Nao walikuwa wakizungumza wao kwa wao habari za mambo hayo yote yaliyotukia.

15 Ikawa katika kuzungumza na kuulizana kwao, Yesu mwenyewe alikaribia, akaandamana nao.

16 Macho yao yakafumbwa wasimtambue.

17 Akawaambia, Ni maneno gani haya mnayosemezana hivi mnapotembea? Wakasimama wamekunja nyuso zao.

18 Akajibu mmoja wao, jina lake Kleopa, akamwambia, Je! Wewe peke yako u mgeni katika Yerusalemu, hata huyajui yaliyotukia humo siku hizi?

19 Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, aliyekuwa mtu nabii, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote;

20 tena jinsi wakuu wa makuhani na wakubwa wetu walivyomtia katika hukumu ya kufa, wakamsulibisha.

21 Nasi tulikuwa tukitumaini ya kuwa yeye ndiye atakayewakomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu yalipotendeka mambo hayo;……………..

25 Akawaambia, Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii!

26 Je! Haikumpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake?

27 Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe.

28 Wakakikaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, NAYE ALIFANYA KAMA ANATAKA KUENDELEA MBELE.

29 Wakamshawishi wakisema, Kaa pamoja nasi, kwa kuwa kumekuchwa, na mchana unakwisha. Akaingia ndani kukaa nao”.

Hapo katika mstari wa 29 maandiko yanasema.. “NAYE ALIFANYA KAMA ANATAKA KUENDELEA MBELE.” Yaani baada ya kuzungumza nao muda wote huo, umefika wakati wa kuingia ndani, yeye anajifanya kama anataka kuendelea na safari!.. Hebu jiulize endapo wale watu wangekuwa wachoyo, na kusema kile chakula chetu kule ndani kinatutosha tu sisi wawili, huyu mtu mwache aendelee zake, je wangekosa mangapi?..au wangesema kile kitanda chetu kule ndani kinatutosha tu sisi wawili na si mwingine watatu, wangekosa mangapi?..Lakini tunaona walielewa hali ya mgeni kwamba kamwe hawezi kusema naomba jambo fulani kama anaona wenyeji hawana huo moyo.. Sasa hebu tuone wangekosa nini endapo wangemruhusu Bwana aende zake.. Tuendelee mbele kidogo katika mistari hiyo…

Luka 24:29 “Wakamshawishi wakisema, Kaa pamoja nasi, kwa kuwa kumekuchwa, na mchana unakwisha. Akaingia ndani kukaa nao.

30 Ikawa alipokuwa ameketi nao chakulani, alitwaa mkate, akaubariki, akaumega, akawapa.

31 Yakafumbuliwa macho yao, wakamtambua; KISHA AKATOWEKA MBELE YAO.

32 Wakaambiana, Je! Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, na kutufunulia maandiko?

33 Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao”,

Umeona, kumbe sio kila mgeni ni mgeni wa kawaida tu!, si kila anayekuomba ni kwasababu anashida, si kila anayetaka kuja kukaa na wewe ni kwasababu yake yeye, wengine wanataka kuja kwako kwa faida yako wewe, wengine wanataka kula chakula chako kwa faida yako wewe… Unyonge wa Kristo kwako ni kwasababu anataka wewe upate faida.

Hivyo hata leo hii, Kristo anakuja mioyoni mwetu kama mgeni, hivyo hatuna budi tumpe nafasi.

Jambo moja wengi wasilolijua ni kwamba Kristo sio dikteta, kwamba tunapompokea basi ataanza kututumikisha kama maroboti, siku zote anakuwa kama mgeni..maana yake unapompa nafasi zaidi ndivyo anavyojifunua kwako zaidi, unapomkataa anakuacha na kukupita..wala hakulazimishi, ingawa atakuonyesha kila dalili za kutamani kuendelea kukaa na wewe…

Na sio tu katika hatua ya kumpokea yeye, bali hata baada  ya kumpokea Yeye, endapo tukijitenga naye..na kujikuta tumezama kwenye mateso au majaribu hatakuja kutulazimisha atusaidie, atasogea karibu na sisi, kuonyesha ishara ya kutaka kutusaidia, lakini kama hatutampa basi hatatupa msaada..

Utasema hilo tunalithibitisha vipi kimaandiko…Hebu tusome kile kisa cha Bwana kutembea juu ya maji ni nini kiliwatokea mitume, na kwa jinsi gani Bwana aliwasaidia.

Marko 6:48 “Akawaona WAKITAABIKA kwa kuvuta makasia, kwa maana upepo ulikuwa wa mbisho; hata ilipopata kama zamu ya nne ya usiku akawaendea, akitembea juu ya bahari; AKATAKA KUWAPITA.

49 Nao walipomwona anatembea juu ya bahari, walidhani ya kuwa ni kivuli, wakapiga yowe,

50 kwa kuwa wote walimwona, wakafadhaika. Mara akasema nao, akawaambia, Changamkeni; ni mimi, msiogope”.

Ukisoma habari hiyo sehemu nyingine utaona, Baada ya Bwana kuingia chomboni, ule upepo ulikoma!.

Lakini nataka tuone hapo kwenye mstari wa 48, maandiko yanasema “AKATAKA KUWAPITA”.. Umewahi kujiuliza kwanini alikuwa anataka kuwapita?.. Ni kwasababu bado alikuwa hajaona kibali cha yeye kutoa msaada…ndio maana akataka kuendelea mbele

Sasa kama Kristo aliweza kufanya hivyo kwa wanafunzi wake!, ambaye aliwachagua yeye mwenyewe, atashindwaje kufanya kwangu na kwako?.

Huu ni wakati wa kumpa Kristo nafasi na kumfanya mwenyeji ndani yetu…

Unajua kabisa huelewi maandiko unapoyasoma, lakini bado humpi Yesu nafasi katika maisha yako, bado kwako ni mgeni mnyonge!.. Kwenda kanisani kwako ni jambo la kusukumwa na kulazimishwa!, kujikana nafsi kwako ni jambo zito.. ukiambiwa uache kuvaa suruali tu! Ni shida, uache vimini na mavazi yasiyo na heshima ni shida.. Kristo atajifunuaje kwako!.. Hawezi kwasababu akiangalia huku na huko anaona milango kila mahali imefungwa!… Unapitia tabu lakini hata kumtolea Mungu huwezi, zaidi sana unapinga matoleo, pasipo kujua kuwa wakati mwingine ni kwa faida yako si ya Kristo.

Je! Kristo ni mgeni au mwenyeji kwako?

Bwana Yesu anasema..

Mathayo 25:41“Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;

43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya ya kila siku kwa njia ya Whatsapp  basi waweza kujiunga kwa kubofya hapa >>> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

YESU NI MFALME WA AINA GANI KWAKO? 

Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

“Si watu wa kutumia mvinyo sana”, je tunaruhusiwa kutumia mvingo kidogo?(1Timotheo 3:8).

Hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao;

Tarshishi ni mji gani kwasasa?

Rudi nyumbani

Print this post

NI KIZAZI KIPI WEWE UPO?

Kibiblia  Kizazi ni kundi la watu linalozuka ghafla lenye tabia zinazofanana, linaweza kuzuka aidha kutokana na mabadiliko ya nyakati, au mabadiliko ya mazingira. Kwamfano, Wana wa Israeli walipokuwa Misri, chini ya Yusufu, waliishi kwa raha sana, Lakini Yusufu alipokufa pamoja na Yule Farao, kilinyanyuka kizazi kingine kisichokumbuka wema wa Yusufu, na hapo ndipo utumwa mgumu ulipoanza.

Vilevile, Wana wa Israeli walipofika katika nchi yao ya  Ahadi, mwanzoni waliishi maisha ya kumcha Mungu sana, lakini wakati ulipopita mrefu kilinyanyuka kizazi kingine kisichomjali Yehova, hapo ndipo Israeli ilipoanza kuingia katika matatizo mengi sana.(Waamuzi 2:10)

Na katika hichi kipindi cha Siku za mwisho, tunapaswa tuwe makini sana, Zipo tabia ambazo utaziona kwa watu wengi sana, lakini kiuhalisia hazikuwepo huko nyuma. Hivyo ni vizuri ukafahamu aina ya vizazi vilivyopo duniani sasa hivi  kulingana na biblia ili ujue wewe upo wapi na jinsi gani unapaswa ujiupeshe navyo.

  1. Kizazi cha uzinzi na zinaa:

 Bwana Yesu alisema..

Mathayo 12:39 “Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona”.

Ni kizazi cha watu kinachozuka kinapenda tu usherati na uzinzi kuliko kitu kingine chochote ulimwenguni. Leo hii tazama  mawazo ya vijana wengi yalivyo, sikiliza mazungumzo yao,  mambo wanayoyafanya kwa siri,vitu wanavyotazama mitandaoni, video za ngono, ni jambo la kawaida kwao, na kibaya zaidi sio tu vijana, hadi wazee na watoto wamo katika kundi hili. Jambo ambalo hapo zamani halikuwepo. Hiyo ni kuthibitisha kuwa ni hiki ni kizazi kingine kimezuka, ambacho ni hatari sana.

Bwana Yesu alisema..

Marko 8:38 “Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika KIZAZI HIKI CHA UZINZI na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.

Ndugu, jiupeshe, na mkondo huu, si lazima uishe kama ulimwengu unavyotaka, kizazi hiki kimeshahukumiwa na Mungu.

     2) Kizazi cha nyoka:

Kipo kizazi cha Nyoka.

Mathayo 3:7 “Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?

8 Basi zaeni matunda yapasayo toba;

9 wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto”.

10 Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.

Soma pia..Mathayo 12:34

Nyoka, alikuwa mwerevu sana kuliko wanyama wote mwituni, lakini alikubali kuwa chombo teule cha shetani. Uzao wake, ndio uliendelea mpaka kwa Kaini, na ndio maana watu wale walikuwa hodari sana , wagunduzi na wavumbuzi wakubwa, lakini waovu waliopindukia (Mwanzo 6:4). Ni watu ambao walikuwa hawana muda na Mungu, lakini kwa upande wa pili uzao wa Mungu, ulikuwa ni mnyenyekevu unaomtafuta Mungu usiku na mchana, vilevile na usio na masumbufu mengi ambao ulipitia kwa Sethi. (Mwanzo 4:26).

Inafunua hadi sasa, kwamba kizazi hiki kipo, Angalia dunia ya sasa, imestaarabika kuliko ile ya zamani, watu wanaelimu kubwa sana, wanagundua mambo makubwa  sana, wamekwenda mpaka mwezini, lakini ukiwagusia habari za Mungu, wanakuambia  hayo ni mawazo yako tu, hakuna Mungu,dini imetengenezwa na watu, wamejikita katika mambo ya mwilini, tu, elimu, utajiri, uvumbuzi basi, Mungu hayupo.

Ndugu, ikiwa na wewe upo katika jopo hili la watu, jiangue haraka sana, hichi ni kizazi, ambacho kipo ulimwenguni sasa.

   3) Kizazi cha watu wasiowatii wazazi wao.

Mithali 30:11 “Kuna kizazi cha watu wamlaanio baba yao; Wala hawambariki mama yao”.

Kuporomoka kwa maadili na nidhamu unakokuona leo, hakukuwepo huko nyuma. Leo utasikia mtoto anajibizana na mzazi wake, mwingine anampiga, mwingine anamzungumzia vibaya, wengine wametengeneza mpaka uadui na wazazi wao.. Kesi hizi ni nyingi sana sikuhizi..Wewe kama mtoto, wewe kama kijana, kuwa makini sana, kizazi hiki kimezuka ulimwenguni sasa. Unapoona, wenzako hawawaheshimu wazazi wao, na wewe usiwe mmojawapo.

Katika agano la kale mtu aliyejaribu kuonyesha utomvu wa nidhani kwa mzazi wake, sheria yake ilikuwa ni kifo. Jitathmini unawatii wazazi wako, Unawapenda?, unawabariki? Unawanenea mema? Unawaombea?.. Hata kama mzazi anakuudhi, huna ruhusu ya kurudisha baya kwa baya kwake. Vinginevyo upo chini ya laana ya kizazi hiki.

4) Kizazi cha watu wanaojiona siku zote wapo sawa:

Mithali 30:12 “Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao wenyewe; Ambao hawakuoshwa uchafu wao”.

Hili kundi ni kubwa sana, Mtamuhubiria mtu na kumwambia pasipo kumwamini Kristo, huwezi kuokolewa, yeye atakuambia, mimi naamini matendo yangu ni safi, ninaamini Mungu hiyo inatosha, siwezi kuhukumiwa. Atakuwa radhi, kujihesabia haki, hata kama ni mzinzi, au mlevi..Haoni hatia yoyote kwa anayoyafanya. Yeye anachoamini ni kuwa Mungu hawezi kumchoma motoni milele,.Nimeshakutana na watu wa namna hii wengi sana. Wanaodhani kuwa kwa kile wanachokiamini, ndio tiketi ya Mungu kuwaokoa siku ile.

Ndugu kama upo katika hili kundi jiepushe nalo, Ikiwa bado hujaokoka, mkimbilie Yesu, yeye pekee ndiye mwenye uwezo wa kukusafisha dhambi zako, na sio kile unachokiamini.

 5) Kizazi cha watu wenye kiburi:

Mithali 30:13 “Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka kama nini! Na kope zao zimeinuka sana”.

Wapo watu ambao, kujishusha hakupo ndani yao. Wanajiona kuwa hakuna chochote kinachoweza kuwa msaada kwao, Mungu si kitu kwao, kwanini wakaombe, kwanini waende ibadani. Wapo radhi hata kuutukana wokovu, au kazi ya Mungu. Wanatumaini, mali zao, au ujuzi wao.

Kama tabia hizo zimeanza kuonekana ndani yako, geuka upesi.

  6) Kizazi wa watu wasio na huruma.

Mithali 30:14 “Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga; Na vigego vyao ni kama visu. Ili kuwala maskini waondolewe katika nchi, Na wahitaji katika wanadamu”.

Utu umeondoka duniani, Yupo radhi kufanya biashara haramu, bila kujali kinaleta madhara mangapi kwa jamii, anauza madawa ya kulevya, anauza bidhaa zilizoisha ubora, wanadhulumu haki za wajane na mayatima kwa faida zao wenyewe. Anaua, ili apate mali, n.k.

Tunayoyaona, hayakuwepo zamani, tusiwe watu wenye tamaa ya mali.

  7) Kizazi cha wenye adili:

Lakini pamoja na kuwepo kwa vizazi hivi vyote, vya watu waovu.. Biblia inasema pia, kitakuwepo kizazi cha watu wenye adili, wanaomcha Mungu, wanaotenda mapenzi yake.

Zaburi 112:1 “Haleluya. Heri mtu yule amchaye Bwana, Apendezwaye sana na maagizo yake.

2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa”.

Na ndio maana unaona pia wapo watakatifu wa Mungu leo duniani. Hawa ndio Bwana anaowatazama, na siku moja itafika Kristo atawahamisha kutoka katika huu ulimwengu kwa tukio la UNYAKUO na kuwapeleka mbinguni. Swali ni je wewe upo katika kizazi kipi?

Matendo 2:40 “Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi”.

Jibu unalo moyoni mwako.

Kumbuka Unyakuo upo karibu sana, dalili zote zimeshatimia, huna haja ya kuendelea kutangatanga na huu ulimwengu tena. Mgeukie Kristo akuokoe, ili uwe mmojawapo wa kizazi cha watu waadilifu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp yanayotumwa kila siku basi bofya hapa >>>  WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA?

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

Marago ni nini? ( Waamuzi 10:18)

Rushwa inapofushaje macho?

Rudi nyumbani

Print this post

Is a woman allowed going to the altar when she is in her menstruation?

The word of God which shows that a woman must be abandoned when she is in her menstruation if from

Leviticus 15:19-33

19 And if a woman have an issue, and her issue in her flesh be blood, she shall be put apart seven days: and whosoever toucheth her shall be unclean until the even.

20 And every thing that she lieth upon in her separation shall be unclean: every thing also that she sitteth upon shall be unclean.

21 And whosoever toucheth her bed shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the even.

22 And whosoever toucheth any thing that she sat upon shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the even.

23 And if it be on her bed, or on any thing whereon she sitteth, when he toucheth it, he shall be unclean until the even.

24 And if any man lie with her at all, and her flowers be upon him, he shall be unclean seven days; and all the bed whereon he lieth shall be unclean.

25 And if a woman have an issue of her blood many days out of the time of her separation, or if it run beyond the time of her separation; all the days of the issue of her uncleanness shall be as the days of her separation: she shall be unclean.

26 Every bed whereon she lieth all the days of her issue shall be unto her as the bed of her separation: and whatsoever she sitteth upon shall be unclean, as the uncleanness of her separation.

27 And whosoever toucheth those things shall be unclean, and shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the even.

28 But if she be cleansed of her issue, then she shall number to herself seven days, and after that she shall be clean.

29 And on the eighth day she shall take unto her two turtles, or two young pigeons, and bring them unto the priest, to the door of the tabernacle of the congregation.

30 And the priest shall offer the one for a sin offering, and the other for a burnt offering; and the priest shall make an atonement for her before the LORD for the issue of her uncleanness.

31 Thus shall ye separate the children of Israel from their uncleanness; that they die not in their uncleanness, when they defile my tabernacle that is among them.

32 This is the law of him that hath an issue, and of him whose seed goeth from him, and is defiled therewith;

33 And of her that is sick of her flowers, and of him that hath an issue, of the man, and of the woman, and of him that lieth with her that is unclean.

Remember we have to know that not everything that took place on Old Testament is not the must to take place too in New Testament, Other things were just as a symbol in order to present the spiritual message to the New Testament.

For example for the issue of food Jesus came and correct by saying what enters a person doesn’t make a person unclean but from what’s comes out from a person because it comes from the heart, that’s why in anyways food doesn’t make a person to do mistakes before God if the food will be eaten by gratitude. But in the past animals who didn’t ruminate they were known as unclean,Which currently revealed in spiritual that people who chew spiritual food which they have been fed, they don’t have time to meditate on what they have been taught or what God has done for them or to work on the things which they have been taught.

Even in women issue when they are in menstruation normally the blood as blood doesn’t have a problem but ask yourself why that blood which comes out from reproductive organs seems to be unclean. This reveal that the dirt that produced due to adultery known as gross uncleanness to the person.

That’s why the bible tells us and the bed undefiled…(Hebrews 13:4)

That’s why we have to keep our body far from fornication.

But this doesn’t mean that bleeding make you unclean because that is automatically issue and it is not planned by a women. So it doesn’t come from the spirit to make one unclean. God use such example to show that things are much worse which comes from committing adultery . So when a women is bleeding that doesn’t make her to do not serve on altar or pray to God.

What she supposed to do is to make herself and her environment clean.

God bless you.


Related Topic:

What is the difference between flesh and spirit uncleanness?

JONAH’S VINE.

DO NOT BE CONCEITED.

Home:

Print this post

WITO WA MUNGU HAUVUKI NENO LAKE.

Bwana Yesu atukuzwe ndugu yangu. Karibu tuyatafakari maneno ya uzima pamoja..

Tunaposoma biblia..tujue kuwa tunausoma ufahamu wa Mungu. Mtu asiyeitafakari biblia halafu anakimbilia kwenda kumtumikia Mungu.. Ajue kuwa anajiweka katika hatari kubwa sana ya kuangamizwa na Mungu.

Ni sawa na mtu anayekimbilia kufanya biashara ambayo hajaifanyia utafiti kujua changamoto zake.faida zake na hasara zake..

Leo tutatazama ni kwa namna gani.

Ndugu usipumbazwe hata kidogo kuona Mungu anasema nawe..anakuonyesha maono makubwa..anakusifia..anakutokea..anakutuma ukawahubirie watu injili.. Usipumbazwe kabisa na jambo hilo. Kama maagizo yaliyopo katika Neno lake huyatii..Kufa unaweza tu kufa.

Jambo kama hilo tutaliona kwa Musa. Kila mtu anafahamu kuwa alitokewa na Mungu mwenyewe katika mwali wa moto. Mungu akampa ishara kubwa..akamtuma aende Misri kwenda kuwaokoa mamilioni ya watu..Lakini cha ajabu tunashangaa Mungu alitaka kumuua njiani..

Yaani kama sio mke wake Sipora,kumsaidia habari ya Musa ingekuwa imeishia pale na maono yake na wito wake.

Kutoka 4:21-25

[21]BWANA akamwambia Musa, Hapo utakaporudi Misri, angalia ukazifanye mbele ya Farao zile ajabu zote nilizozitia mkononi mwako; lakini nitaufanya mgumu moyo wake, naye hatawapa ruhusa hao watu waende zao.

[22]Nawe umwambie Farao, BWANA asema hivi, Israeli ni mwanangu mimi, mzaliwa wa kwanza wangu;

[23]nami nimekuambia, Mpe mwanangu ruhusa aende, ili apate kunitumikia, nawe umekataa kumpa ruhusa aende; angalia basi, mimi nitamwua mwanao, mzaliwa wa kwanza wako.

[24]Ilikuwa walipokuwa njiani mahali pa kulala, BWANA akakutana naye akataka kumwua.

[25]Ndipo Sipora akashika jiwe gumu na kuikata govi ya zunga la mwanawe, na kuibwaga miguuni pake akasema. Hakika wewe u bwana arusi wa damu kwangu mimi.

Sasa ni kwanini Mungu alitaka kumuua ni kwasababu alipuuzia maagizo ya msingi ya kuwatahiri watoto wake..Mambo ambayo Mungu alikuwa ameshawaagiza  wana wa Israeli wote wafanye hivyo kulithibitisha agano lake..Lakini yeye hakuona umuhimu huo..kisa tu Mungu amemtokea..amemtuma kama nabii mkuu Misri..hivyo hakuna sababu ya kuhangaika na yale mengine..

Ni wangapi leo hii wamepatwa na kiburi cha kukataa maagizo ya Mungu kama vile ubatizo sahihi wa maji..kwa kisingizio kuwa Mungu anazungumza na wao..Mungu kawatokea..Mungu kawaagiza waende kutumika..ubatizo hauna maana yoyote ukishamkiri tu Kristo inatosha..Wewe si zaidi sana ya nabii  Musa..Mungu hashindwi kukuua.

Unaweza kusema ni Musa tu peke yake yalimkuta haya..Yupo nabii mwingine huko mbeleni anaitwa Balaamu.. Yeye naye alitokewa na Mungu katika safari yake ya kwenda kuwalaani Israeli.

Mara ya kwanza Mungu akamuonya lakini hakusikia.. Akataka zaidi kufanya hivyo..baadaye Mungu akamruhusu na akamuhakikishia kuwa atakuwa pamoja naye..Lakini njiani Mungu alikuwa ameshamweka malaika wake tayari amuue. Kama si yule Punda kumsaidia habari yake ingekuwa naye imeisha pale…

Ni kwanini sasa iwe vile ni kwasababu alipuuzia maagizo ya awali ya Mungu “..amlaaniye Israeli na yeye atalaaniwa”(Mwanzo 12:3)..hivyo yeye akataka kulipindua hilo Neno kwa maono yake..au mitazamo yake mwenyewe. Akawa katika hatihati ya kufa..

Hesabu 22:12-13

[12]Mungu akamwambia Balaamu, Usiende pamoja nao; wala usiwalaani watu hawa, maana wamebarikiwa.

[13]Balaamu akaondoka asubuhi akawaambia wakuu wa Balaki, Enendeni zenu hata nchi yenu; kwa maana BWANA amekataa kunipa ruhusa niende pamoja nanyi….

Lakini baada ya kushurutishwa sana na wale wakuu wa Balaki..utaona alijifanya tena kwenda kumuuliza Mungu..hichi ndio kitu alichoambiwa mara ya pili

Hesabu 22:20-22

[20]Mungu akamjia Balaamu usiku, akamwambia, Kwa kuwa watu hawa wamekuja kukuita, enenda pamoja nao; lakini neno lile nitakalokuambia ndilo utakalolitenda, basi.

[21]Balaamu akaondoka asubuhi, akatandika punda wake, akaenda pamoja na wakuu wa Moabu.

[22]Hasira ya Mungu ikawaka kwa sababu alikwenda; malaika wa BWANA akajiweka njiani, ili kumpinga. Basi alikuwa amepanda punda wake, na watumishi wake wawili walikuwa pamoja naye.

Ndugu..tuzifahamu tabia za Mungu..wapo watu wengi wameonyeshwa mambo makubwa sana katika wito wao. Lakini unashangaa hakuna hata moja limetimia..hadi siku anakufa..Ni kwanini?

Nikwasababu alikwenda pasipo kujua kanuni za Mungu. Tuishi kwa Neno la Mungu na sio kwa ndoto au sauti au maono. Haijalishi wito huo utakuwa mkubwa kiasi gani..hauwezi kuzidi Neno lake.. Neno linasema mwanamke hana nafasi ya kufundisha kanisani (palipo na mchanganyiko wa wanaume na wanawake) 1Timotheo 2:12..Lakini mwingine atasema Mungu kaniita kuwa Mchungaji..kanitokea kabisa na kunitia mafuta..

Mama kuwa makini..kasome biblia yako kwanza umwelewe Mungu ndipo ukatumike..

Hivyo ili tuwe salama.. kabla ya kuitii sauti yoyote ya nje..Tuitii kwanza Sauti ya Mungu iliyo katika Neno lake.  Ndio hayo mengine yafuate.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp ya kila siku basi jiunge kwa kubofya hapa >>> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

JE UNAIFANYA KAZI YA MUNGU?

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

TAFUTA MSAMAHA HALISI, NA SI MSAMAHA TU!

UTAWALA WA MIAKA 1000.

Nini maana ya “wazimu” katika biblia?

JINSI PAULO ALIVYOPAMBANA NA UJINGA WA ROHONI.

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Bwana Yesu alikuwa na mchoro (tattoo) katika paja lake?

Tusome..

Ufunuo 19:16 “Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA”

Mstari huu unatumika na wengi wanaohalalisha uchoraji wa tattoo katika miili yao, kuwa hata Bwana Yesu mwenyewe alijichora tattoo katika paja lake.

Je ni kweli hiyo ndio maana ya huo mstari?
Jibu ni la! Katika Maono hayo Yohana aliyoyaona, hakuona nyama ya paja la Bwana Yesu ikiwa limeandikwa hayo maneno, bali alichokiona ni vazi lililofunika paja limeandikwa maneno hayo, BWANA WA MABWANA na MFALME WA WAFALME.

Kwamfano kuna andiko linasema jifunge upanga pajani mwako..

Zaburi 45:3 “Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari, Utukufu ni wako na fahari ni yako”.

Je kwa mstari kwa huo biblia imemaanisha, kuchua upanga na kuubandika kwenye nyama ya paja?..

Bila shaka haikumaanisha hivyo bali ilimaanisha funga upanga katika ghala iliyopo viununo mwetu.

Au labda mtu akupe maagizo ya kubeba kiroba cha mzigo Begani, je atakuwa anamaanisha uvue nguo ubaki bega wazi ndio ubebe mzigo huo?.

Au mtu akwambie vaa mkanda kiunoni, atakuwa amemaanisha uvue nguo zote halafu ujifunge mkanda kwenye nyama ya kiuno chako? Jibu ni la!..bali amemaanisha katika vazi lililopo kiunoni kama ni suruali au nguo nyingine yoyote, ifungwe kwa mkanda.

Vile vile katika mwonekano mwingine wa Bwana kuna mahali, maandiko yanasema alionekana kafungwa mshipi wa dhahabu “matitini”.

Ufunuo wa Yohana 1:13 “na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa Mwanadamu, amevaa vazi lililofika miguuni, na kufungwa mshipi wa dhahabu matitini”.

Bila shaka mstari huo haukumaanisha ndani ya kifua cha Bwana kuna mshipi umedungwa wa dhahabu, bali biblia imemaanisha kwenye vazi lake la nje, sehemu ya kifua palikuwa na mshipi (yaani mkanda).

Kadhalika katika mstari huo,wa Ufunuo 19:16, biblia haijamaanisha kuwa kuna maneno yaliyoandikwa kwenye nyama ya paja, bali imemaanisha maneno yaliyoandikwa katika vazi lililofunika paja.

Hakuna mahali popote maandiko yanaagiza wala kutufundisha kujichora tattoo.

Kujichora kwa aina yoyote ile, ikiwemo kupaka hina ni dhambi kibiblia, Na wote wanaojichora hawataurithi uzima wa milele (Kwa maelezo marefu kuhusu kujichora na kujichanja kibiblia unaweza kufungua hapa Kujichota ni dhambi

Je umempokea Yesu?..je umebatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jinala Yesu?, Mambo haya mawili ndio msingi wa wokovu, na kila mtu lazima ayafanye ili awe mkristo.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp ya kila siku basi jiunge kwa kubofya hapa >>> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JE! WEWE NI MFUNGWA WA BWANA?

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

WAKAMCHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE.

HAPANA MFUPA WAKE UTAKAOVUNJWA.

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?

USO WAKE ULIKUWA UMEHARIBIWA SANA ZAIDI YA MTU YE YOTE.

Rudi nyumbani

Print this post

What is the difference between flesh and spirit uncleanness?

QUESTION: I need to know what is the difference between flesh and spirit uncleanness?? As we read in 2 Corinthians 7:1

2 Corinthians 7:1 “Having therefore these promises, dearly beloved, let us cleanse ourselves from all filthiness of the flesh and spirit, perfecting holiness in the fear of God”.


ANSWER: In order for us to be perfection that we can approach God’s promises, we have to know that God wants us to be holy both in spirit and flesh.

As Paul said that we have to cleanse ourselves from all filthiness of the flesh and spirit, he means to keep away from all the sin that inherent in us, For example of those sins is as follows Adultery, alcoholism, theft, smoking, insults, unnecessary clothes such as mini-skirts for women, color body transformation, applying make-up, abortion,tattoo marks,homosexuality, the use of drugs and other similar things whose origin is in the flesh.

And where Paul said let us set aside spirit uncleanness he meant all the sins that comes from within a person which are not related to the flesh an example of these sins is as follows jealousy, anger,lust,bad thoughts, hypocrisy, greed,envy,arrogance,rude,idolatry,lie. These are sins that God hates very much as he hates that which are produced by people through flesh.

So let us know that God is watching both flesh and spirit. There are people who know that God is only watching in our spirit and he never look towards our flesh.

Brethren! Your flesh is worth as much as your spirit before God,because in that last days not only your spirit that will be saved but your flesh also must be saved. (Read your Bible you will prove it). So glorify God in your flesh, dont be deceived with doctrine of false prophets which tells you that God only judge your spirit and not your flesh.

The Word of God is more than the words of men .Because that is what will protect you that day and it’s the same Word that will judge you that day, because the Word of God is the sword .
So be afraid of God’s word.

Hebrews 4:12 “For the word of God is quick, and powerful, and sharper than any two edged sword, piercing even to the dividing asunder of soul and spirit, and of the joints and marrow, and is a discerner of the thoughts and intents of the heart.

13 Neither is there any creature that is not manifest in his sight: but all things are naked and opened unto the eyes of him with whom we have to do”.

God Bless you.

Please kindly share this good news with others.


Other Topics:

UNDERSTAND HOW CHRIST HEALS PEOPLE’S SOULS.

THERE’S POWER WHICH DRAWS US TO CHRIST, VALUE IT!

DO NOT BE CONCEITED.

WHAT DOES IT MEAN TO LIVE WHILE REDEEMING THE TIME?

WE HAVE A RESPONSIBILITY TO LEAD CAPTIVITY CAPTIVE.

Home

Print this post

NA ABARIKIWE KILA AKUBARIKIYE, NA ALAANIWE KILA AKULAANIYE.

SWALI: Nini maana “nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani;”..Je! Ni kwa namna gani tunapaswa tulibariki taifa la Israeli.  Je! Ili tubarikiwe tunapaswa, tufunge na kuliombea Taifa la Israeli usiku na mchana, au tuwe na bendera za taifa lile makanisani kwetu au majumbani mwetu?.

Ni kwa namna gani tutapokea Baraka kwa kulibariki tu taifa hilo?


JIBU: Maneno hayo, kwa mara ya kwanza tunaona Mungu akiyatamka kwa Ibrahimu katika;

Mwanzo 12:1 “Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;

2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;

3 nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa”.

Maandiko hayo hayatupi tafsiri ya kwamba tukeshe kuliombea taifa la Israeli usiku na mchana ili tubarikiwe, hapana utaona maneno hayo, Mungu alisema akilenga wakati ambapo watu wanapanga kuliangusha, au kuliporomosha au kuliletea vitisho taifa hilo, aidha kwa kulivamia, au kuliloga, n.k. kwa namna yoyote ile, hapo ndipo anayejaribu kufanya hivyo anakumbushwa,kuwa aibarikiye Israeli, atabarikiwa, na ailaaniye Israeli atalaaniwa.

Jambo kama hilo tunalithibitisha kwa Yule Balaamu mchawi, ambaye aliajiriwa na Balaki, ili aende kuwalaani Israeli, (yaani kuwaloga) kwa ushirikina ili wasifanikiwe kuvuka katika nchi ya Balaki. Lakini Ilikuwa nusura Mungu amuue Yule Balaamu, kwa kitendo tu hicho cha kujaribu kuliloga taifa teule. Kinyume chake ikabidi alibariki ili tu awe salama..Mpaka yeye mwenyewe akakiri,na kusema hapana uchawi katika Israeli wala uganga..

Hesabu 23:21 “Hakutazama uovu katika Yakobo, Wala hakuona ukaidi katika Israeli. Bwana, Mungu wake, yu pamoja naye, Na sauti kuu ya mfalme i katikati yao.

22 Mungu amewaleta kutoka Misri, Naye ana nguvu kama nguvu za nyati”.

Hiyo ni kuonyesha kuwa, hata sasa yapo mataifa mengi ambayo yameshatangaza uadui na Israeli, mojawapo ni Somalia, na Libya, embu yaangalie mataifa hayo leo hii yapoje., na hiyo yote ni kwasababu yamejaribu kuleta vita na vitisho kwa taifa teule la Mungu, na matokeo yake ni kuwa yamepigwa, kila kukicha ni vita. Na mengine yanalitamkia maneno ya laana kama vile Palestina,, na mengine kuliwekea vikwazo.  Embu Yatazame ustawi wao hayo mataifa au hao watu leo hii walivyo.

Halikadhalika, taifa ambalo halitaki shari na Israeli, bali linalitakia mema amani na mafanikio daima, basi taifa hilo au Mtu huyo Mungu  atambariki. Hivyo  umeona hapo, inalenga katika habari ya amani na shari, yaani pale ambapo unalazimishwa utamke mabaya, uwalaani, uwatukane,  au upigane vita kinyume chao, hapo unapaswa uende kinyume chake, uwabariki, na kuwatakia amani. Ndipo utakapobarikiwa.

Lakini sio kuacha kufuata kanuni za Mungu za kimaandiko na kukesha kuliombea taifa la Israeli ili tubarikiwe. Mpaka tunasafiri kwenda kule Yerusalemu, kupokea Baraka hizo, Mungu havutiwi sana na sisi tunapofanya hivyo, anavutiwa na sisi pale tunapoishi kulingana na Neno lake, hivyo tu. Kwahiyo, usipeleke fikra zako sana Israeli, bali zipeleke kwenye maisha yako, vilevile maombi yako, yaelekeze kwa watu wenye dhambi leo hii ulimwenguni. Kesha kuwaombea hao, na kuiombea Injili.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp  yanayotumwa kila siku basi fungua bofya hapa ujiunge >>> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

ALAMA ZA BENDERA YA ISRAELI ZINAWAKILISHA NINI?

Israeli ipo bara gani?

Mataifa ni nini katika Biblia?

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “yamfaa afungiwe shingoni jiwe kubwa la kusagia, na kutoswa katika kilindi cha bahari?”

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

Je Mkristo kutembea na walinzi (Bodyguards),ni sawa?

Rudi nyumbani

Print this post

ALAMA ZA BENDERA YA ISRAELI ZINAWAKILISHA NINI?

Wakati Mungu anawatoa Israeli kutoka Misri, Mungu hakuwapa bendera kuwa kama Ishara ya Taifa hilo, Hivyo bendera kwa Israeli ni kitu kilichokuja kuzalika miaka mingi baada ya Kristo kuja duniani katika harakati za kutafuta uhuru.

Sasa swali, ni je zile rangi katika bendera hiyo zinawakilisha nini?, Na ile nyota iliyopo katikati ya bendera inawakilisha nini?.

Bendera ya Israeli ina rangi mbili tu! Nyeupe na Blue (kwa kiswahili Samawi).
Rangi nyeupe inawakilisha utakatifu wa Mungu. Na Blue inawakilisha utukufu wa Mungu.

Tukitazama juu mbinguni, anga linaonekana la rangi ya Blue(Samawi).

Kufunua utukufu wa Mungu.Hata vitu vingine vya asili kama milima, bahari utaona vina mwonekano wambwa wa rangi hii ya blue kufunua utukufu wa Mungu.

Lakini kitu cha mwisho katika bendera ya Israeli, ni ile alama kama ya Nyota, yenye pembe sita, iliyopo katikati ya bendera hiyo.
Alama hiyo inajulikana kama Nyota ya Daudi au Ngao ya Daudi.

Imejulikana hivyo, kwasababu inaaminika Ngao ya Daudi ilikuwa na umbile hilo mfano wa hiyo nyota, na inaaminika ngao hiyo ilikuwa ina nguvu fulani ya kiungu.
Vile vile zile pembe sita katika hiyo ngao zinawakilisha zile tabia sita za Roho wa Mungu katika Isaya 11.

Isaya 11:2 “Na roho ya BWANA atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha BWANA”.

Na vile vile kama ilivyokuwa na pembe tatu mbili, moja inaangalia juu na nyingine chini, inawakilisha uhusiano wetu sisi na Mungu.

Ingawa hakuna mahali popote katika torati wala biblia nzima, nyota hiyo ilitajwa kwa sifa hizo, lakini wayahudi wa karne ya 17, walishawishika kuamini hivyo na kuitumia hiyo kama ishara ya Nembo ya Taifa lao, na hata kuitumia katika bendera yao.

Lakini katika jicho lingine, nyota hiyo inaaminika kama ishara ya Masihi, yaani Yesu Kristo, yeye ndiye Uzao wa Daudi, na ndiye ile nyota ing’aayo, ambaye Mataifa yote watamtumainia.

Ufunuo 22:16 “Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi”.

Lakini swali ni je! Bendera hiyo kwetu sisi wakristo, ina manufaa yoyote kiroho?, Kwamba tunapokuwa na bendera ya Israeli katika makanisa yetu, au katika vyombo vyetu vya usafiri, au katika nyumba zetu, tunakuwa tunajiongezea baraka??.

Jibu ni la!. Bendera ya Taifa la Israeli haituongezei chochote, zaidi sana mtu anapoiweka ndani kwake, na kuifanya kama mungu wake atakuwa anajizombea laana badala ya baraka. Kwasababu kwake yeye ni kama mungu.

Baraka pekee tunayoweza kuipata sisi ni kuishi kulingana na Neno lake na kanuni zake, utakatifu sawasawa na Waebrania 12:14, ndiyo bendera yetu, na alama ya kukubaliwa na Mungu..na sio bendera ya Israeli ndani kwetu.

Hivyo hakuna ulazima wowote wa Mkristo au mhubiri kutembea na bendera kana kwamba ndio kitovu chake cha baraka, labda atembee nayo kwa lengo lingine lakini sio hilo la kutafuta baraka kupitia hiyo.

Maandiko yaliposema “ambarikiye Israeli amebarikiwa” hiyo sio maana yake..Maana yake ni nyingine kabisa.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kama utapenda uwe unafikiwa na masomo ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP basi bofya hapa ujiunge moja kwa moja  >>>> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU

WEKA KUMBUKUMBU YA MAMBO BWANA ANAYOKUFANYIA KWASABABU YATAKUFAA MBELENI.

Neno Kupatiliza maana yake nini katika biblia?

Babewatoto ni nani katika biblia?(Isaya 34:14).

Ni kosa gani Daudi alilolifanya katika kuwahesabu watu, mpaka kupelekea vifo vya waisraeli wengi?

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Rudi nyumbani

Print this post

Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;

SWALI: Nini maana ya huu mstari..

Mithali 15:27

[27]Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;

Bali achukiaye zawadi ataishi.


JIBU: Mstari huo ni mgumu kueleweka kidogo kwasababu kiswahili kilichotumika hapo ni kile cha zamani..

Ukiangalia tafsiri nyingine..mstari huo unamaana hii.. Atamaniye kupata vingi kwa njia isiyohalali huifadhaisha nyumba yake mwenyewe bali achukiaye rushwa ataishi.

Jambo ambalo ni kweli..kwamfano Mtu anayejiingiza katika biashara ya madawa ya kulevya kwa tamaa tu ya kupata fedha nyingi..hajui kuwa mwisho wake ni kujibomoa yeye mwenyewe na pamoja nyumba yake yote.

Habakuki 2:9

[9]Ole wake yeye aipatiaye nyumba yake mapato mabaya, ili apate kukiweka kioto chake juu, apate kujiepusha na mkono wa uovu!

Mwingine utakuta anatoa rushwa ili bidhaa zake zisilipishwe kodi..lakini hajui mwisho wake utakuwa mbaya siku moja.

Lakini kinyume chake biblia inasema atakayeyakwepa hayo yote ataishi..

Sikuzote tamaa ya  za haraka haraka mwisho wake huwa ni mitegoni..

Mhubiri 4:6

[6]Heri konzi moja pamoja na utulivu,

Kuliko konzi mbili pamoja na taabu;

na kujilisha upepo.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kama utapenda uwe unafikiwa na masomo ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP basi bofya hapa ujiunge moja kwa moja  >>>> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Maana ya huu mstari ni ipi? Mithali 14:4 ‘Zizi ni safi ambapo hapana ngombe;bali nguvu za ngombe zaleta faida nyingi’.

UMEDI NA UAJEMI ZILITAWALAJE?

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

HUANGUA MAYAI YA FIRA, NA KUSUKA WAVU WA BUIBUI;

Print this post

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

Tusome,

2Wakorintho 1:15 “Nami nikiwa na tumaini hilo nalitaka kufika kwenu hapo kwanza, ili mpate karama ya pili

Sio wakati wote neno “karama” linapotumika kwenye biblia linamaanisha “karama ya roho kama vile unabii, uchungaji, ualimu n.k”. Bali karama pia ni neno linalomaanisha “Zawadi au Baraka”.

Kwamfano kuna andiko linasema “karama ya Mungu ni uzima wa milele”.

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

 Sasa hapo haimaanishi kwamba Mungu karama yake ni “Uzima wa milele” kama sisi karama zetu zilivyo kutoa unabii, au Kunena kwa lugha, au kutabiri nk.

Mungu yeye hana kipawa fulani maalumu, kwasababu vyote vinatoka kwake.

Bali hapo biblia imemaanisha kuwa “Zawadi ya Mungu ni uzima wa milele”..au “Baraka ya Mungu kwetu ni uzima wa milele”

Kadhalika Mtume Paulo aliposema  kuwa “nalitaka kufika kwenu hapo kwanza, ili mpate karama ya pili” hakumaanisha kuwa kuna karama nyingine ya pili tofauti na hiyo ya kitume aliyokuwa nayo,  au nyingine mpya  hivyo anataka kwenda kuwapa, au kuwanufaisha katika hiyo, hapana!, bali alimaanisha “Baraka ya Pili”.

Ni sawa mhubiri aliyeko Dar es Salaam, aende kuhubiri Morogoro, kwa wiki moja na kisha arudi Dar, na ghafla apate tena safari ya kwenda Dodoma kuhubiri baada ya wiki moja wakati kasharudi Dar, bila shaka hawezi kufika Dodoma bila kupita Morogoro, hivyo Mhubiri huyu akawasiliana na wale aliokwenda kuwahubiria hapo kwanza  (Watu wa Morogoro) kwamba atapita tena kuhubiri kwa siku moja na siku inayofuata atakwenda Dodoma.. Hivyo watu wa Morogoro wakawa wamepata Baraka mara mbili. Ndicho Mtume Paulo alichomaanisha hapo!.

Kwamba alishapita kwao (watu wa Korintho) na kuwabariki kwa Mafundisho akaondoka, lakini alitaka tena kupita kwao kwa mara nyingine ya pili wakati anaelekea Makedonia ili wapate Baraka mara mbili.

Maisha ya Paulo yanatufundisha kuwa na bidii na jitihada katika kuifanya kazi ya Mungu, ijapokuwa Paulo alikuwa anapitia vita vikali katika kuhubiri, lakini mara zote alitafuta kurudia kuhubiri mahali ambapo ameshapita kuhubiri.

Matendo 15:36 “Baada ya siku kadha wa kadha Paulo akamwambia Barnaba, Haya! Mrejee sasa tukawaangalie hao ndugu katika kila mji tulipolihubiri neno la Bwana, wa hali gani”.

Bwana atusaidie na sisi tuwe kama watakatifu hawa wa kanisa la kwanza.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kama utapenda uwe unafikiwa na masomo ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP basi bofya hapa ujiunge moja kwa moja  >>>> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Rudi nyumbani

Print this post