Neno Kupatiliza maana yake nini katika biblia?

Neno Kupatiliza maana yake nini katika biblia?

Kupatiliza ni neno lenye maana ya “kupiga/kuadhibu ”..mfano badala ya kusema “fulani, kapigwa na Mungu, unaweza kusema fulani kapatilizwa na Mungu”

Lakini swali la kujiuliza ni je!..Mungu huwa anapiga watu (anapatiliza)?

Jibu ni ndio!. Huwa anatoa adhabu, anawapatiliza waovu vile vile na wema endapo wakitoka nje ya mstari.

Lakini siku zote adhabu za Mungu lengo lake ni ili sisi tutubu na si kutukomoa au kutukomesha, kama sisi wanadamu tunavyokomeshana.

Tunapopatwa na majanga tofauti tofauti, ni ili tutubu tuache njia zetu mbaya na tulitafute kusudi la Mungu juu ya maisha yetu. Na pale tunapopata ufahamu na kugeuka kuiacha ile njia mbaya tuliyokuwa tunaiendea basi moja kwa moja, Bwana anaondoa yale mapatilizo na kutupatia mema.

Mfano wa mtu aliyepigwa baada ya kuliacha kusudi la Mungu ni nabii Yona.
Yeye alidhani kuacha kuitii sauti ya Mungu ataendelea kuwa salama!…kumbe kinyume chake ndio anazidi kuielekea ile hatari.

Akajikuta amekaa tumboni mwa samaki siku 3, bila kula wala kunywa.

Vile vile Bwana anawapatiliza Waovu hata kizazi cha tatu na cha nne..

Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; NAWAPATILIZA wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao”.

Umeona?..ukiabudu sanamu, kama babu yako au kama baba yako au bibi yako au mama yako…Bwana atakupatiliza wewe mzao wake kama na wewe utaendelea na kuabudu sanamu kama wao.

Vile vile na wakristo wote waliomwamini Yesu wamepewa mamlaka na nguvu za kuvamia kambi za adui katika ulimwengu wa roho na kupatiliza (kupiga) kila kazi zote za giza, na kuyaacha huru mateka..

Tunaweza kuyasoma hayo katika…

2 Wakorintho 10:3 “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;

4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;

6 tena TUKIWA TAYARI KUPATILIZA maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”.

Na tunazipiga/patiliza Ngome za Adui kwa KUOMBA, KUHUBIRI na KUSOMA NENO.

Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp group:
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Nini maana ya kupiga Kite! Katika biblia.

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

KWANINI UPIGE MISHALE CHINI?

NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.

Ngome ni nini?  Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments