Hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao;

Hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao;

SWALI: Biblia ina maana gani kusema maneno haya kwa habari ya mitume?

Matendo 5:13 “hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao; ila watu waliwaadhimisha;”

JIBU: Tusome habari hiyo tena;

Matendo ya Mitume 5:12-16

[12]Na kwa mikono ya mitume zikafanyika ishara na maajabu mengi katika watu; nao wote walikuwako kwa nia moja katika ukumbi wa Sulemani;

[13]na katika wote wengine hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao; ila watu waliwaadhimisha;

[14]walioamini wakazidi kuongezeka kwa Bwana, wengi, wanaume na wanawake;

[15]hata ikawa katika njia kuu hutoa nje wagonjwa, na kuwaweka juu ya majamvi na magodoro, ili Petro akija, ngawa kivuli chake kimwangukie mmojawapo wao.

[16]Nayo makutano ya watu wa miji iliyoko kandokando ya Yerusalemu wakakutanika, wakileta wagonjwa, nao walioudhiwa na pepo wachafu; nao wote wakaponywa.

Japokuwa Mungu alidhihirisha uweza mwingi na maajabu kwa mikono ya mitume, lakini kulikuwa na aina maisha/ mwenendo ambao haukuwa mwepesi kwa watu wengine kuufuata kama wao.

Na ndio maana maandiko yanasema hapo “hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao, japokuwa walikuwa  wanawaadhimisha, yaani wanawaonea fahari kama maaskari wa Bwana, waaminifu.

Na mwenendo wenyewe ambao uliwafanya watu wasiweze kufuatana nao, ndio huo wa kutokuogopa vifo, mapigo, mabaraza ya makuhani, mashutumu, na sura za watu.

 Ikumbukwe kuwa mitume walipoitwa hawakutumwa kwanza nchi za mbali bali waliagizwa waanzie kwanza pale pale Yerusalemu ambapo palikuwa na ukinzani mkubwa sana kutoka kwa wafalme na viongozi wa kidini,

na cha hatari zaidi mitume walikuwa wanaongozwa kwenda kuhubiri katika hekalu lile lile ambalo, Kristo alipindua meza zao, hata baadaye tena Petro na Yohana walipofungwa, kwasababu ya kuhubiria watu, mule hekaluni..utaona malaika aliwatoa na kuwaaagiza warudi kule kule hekaluni kuhubiri.

Matendo ya Mitume 5:18-21

[18]wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza;

[19]lakini malaika wa Bwana akafungua milango ya gereza usiku, akawatoa, akasema,

[20]Enendeni mkasimame hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya Uzima huu.

[21]Nao waliposikia wakaenda alfajiri hekaluni, wakaanza kufundisha.

Akaja Kuhani Mkuu nao waliokuwa pamoja naye, wakawakutanisha watu wa baraza, na wazee wote wa wana wa Israeli, wakatuma watu gerezani ili wawalete.

Unaona, Hata wakati kanisa linapitia dhiki Yerusalemu, na kuwafanya  watakatifu wote watawanyike, ni mitume peke yao waliendelea kubaki Yerusalemu.

Matendo ya Mitume 8:1

[1]Siku ile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume.

Hivyo kwa utumishi wa namna hiyo wa kuhatarisha maisha, haikuwa vyepesi kwa watu wengi, kuufuata..japokuwa watu walikuwa pamoja nao bega bega, wakifurahia ushujaa wao, wakitamani waendelee kumtumikia Mungu kwa ujasiri, injili ienee.

Jambo kama hilo tunaliona pia katika huduma ya  Bwana Yesu..

Biblia inasema wengi wa wakuu wa kidini walimuamini lakini hawakuweza kumkiri kwasababu ya hofu wa watu..

Yohana 12:42

[42]Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi.

Watu wengi hawakuweza kuambata na Yesu katika mapito yake lakini aliaminiwa na wengi.

Hii ni kufunua nini kwa watumishi wa Mungu?

Ikiwa umeitwa kama mtumishi wa Mungu..Ni lazima maisha yako yajikite katika utumishi wa Mungu kwelikweli, yaani viwango vyako vya kujikana lazima viwe juu zaidi ya watu wengine..

Ndivyo Mungu atakavyokutumia na ndivyo watu watakavyokuadhimisha kama ilivyokuwa kwa mitume.

Chachu yetu ni lazima izidi ya watu wengine. Bwana atusaidie sana.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

THAWABU ZA SIRI, ZA WATAKATIFU MBINGUNI.

SIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, BALI MAFARAKANO.

KWANINI MITUME WAMUULIZE BWANA FARAGHANI?

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

Ulafi ni nini kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments