Title February 2024

Kwanini Mungu alimkataa Sauli? (1Samweli 15:23)

Swali: Kwanini Mungu alimkataa Mfalme Sauli na tunapata funzo gani?


Jibu: Sauli alikataliwa na Mungu kwasababu ya mambo makuu mawili, 1) UASI na 2) UKAIDI WA MOYO.

Hayo ndio mambo mawili yaliyomkosesha Sauli, na biblia imeweka wazi..

1Samweli 15:22 “Naye Samweli akasema, je! Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya Bwana? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya beberu.

23 Kwani KUASI ni kama dhambi ya uchawi, Na UKAIDI ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme”.

     1. KUASI

Kuasi maana yake ni kuondoka katika njia sahihi na kuwa adui wa hiyo njia. Ndicho kilichomtokea Sauli, Moyo wake ulianza kuondoka kwa MUNGU kidogo kidogo, na akaanza KWENDA KINYUME na sheria ya MUNGU huku akijua kabisa kuwa anachokifanya si sawa.

     2. UKAIDI

Dhambi ya pili ya Sauli ni “Ukaidi”. Mkaidi ni mtu asiyeshaurika wala hakubali kubadili mawazo yake…anachokiamini amekiamini!!,…anachokishikilia amekishikilia!..

Na Mfalme Sauli alikuwa mkaidi kwa BWANA!, Kwani utaona alipofanya kosa la kwanza la kutoa dhabihu kinyume na sheria ya Mungu katika 1Samweli 13:18 na kukemewa na Bwana, lakini utaona anakuja kurudia kosa linalofanana na hilo katika 1Samweli 15:14 pale alipoleta dhabihu haramu kutoka kwa waamaleki na kutaka kuzitoa kwa Bwana.

Alileta kondoo na Ng’ombe (walionona) kutoka Taifa la Amaleki, ili amtolee Mungu dhabihu… Kwa jicho la Haraka inaweza kuonekana kuwa alifanya jambo la busara…lakini kwa jicho la ndani SAULI alifanya machukizo makubwa sana.

Kwani kitendo cha kutwaa Ng’ombe za watu wanaoabudu miungu, ambao wanaitolea miungu yao, na tena hajui hizo ng’ombe zina historia gani..na kuzichukua hizo kisa tu zimenona kisha kumtolea Mungu, ilikuwa ni kitendo cha dharau kubwa sana (1Samweli 15:14-15)!!.. Ni sawa tu na kutwaa msharaha wa kahaba na kumletea Bwana ule alioukataza katika Kumbukumbu 23:18..

Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”.

Hivyo Sauli alikuwa mkaidi kwa  Mungu.. kwani sheria inasema Usimchinjie Bwana Ng’ombe wala kondoo aliye na kilema au MWENYE NENO OVU! (Kumbukumbu 17:1)..Na hapa Sauli analeta Ng’ombe walionona lakini waliojaa maovu ya Waamaleki kama sadaka kwa Bwana. (1Samweli 15:14-15)!!.. Huo ni UKAIDI MKUU..

Na hata leo, Mambo haya mawili (UASI na UKAIDI) yanamchukiza Mungu.

Yeremia 5:22 “Je! Hamniogopi mimi? Asema Bwana; hamtatetemeka mbele za uso wangu; mimi niliyeweka mchanga kuwa mpaka wa bahari, kwa amri ya daima, isiweze kuupita? Mawimbi yake yajapoumuka-umuka, hayawezi kushinda nguvu; yajapovuma sana, hayawezi kuupita.

23 Lakini watu hawa wana moyo wa KUASI NA UKAIDI; wameasi, wamekwenda zao.

24 Wala hawasemi mioyoni mwao, Basi, na tumche Bwana, Mungu wetu, aletaye mvua, mvua ya mwaka, na mvua ya vuli, kwa wakati wake; na kutuwekea juma za mavuno zilizoamriwa.

25 Maovu yenu yameyageuza haya, na dhambi zenu zimewazuilia mema msiyapate”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

ROHO MBAYA KUTOKA KWA BWANA.

DHABIHU ZA ROHO NI ZIPI? (1Petro 2:5)

Dhabihu ni nini?

Gudulia ni nini? (1Samweli 26:11).

Habari ile ya Pilato kuchanganya zile damu za wayahudi na pamoja na dhabihu zao,(Luka 13) ilihusu nini?

Rudi nyumbani

Print this post

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

Hizi ni sababu kuu nne (4), ambazo zinampa sababu mwaminio yoyote kuihubiri injili kwa nia yote kutoka moyoni.

1) Kwasababu ni agizo kuu la Bwana.

Marko 16:15  “Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. 16  Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”

Bwana wetu alituagiza, na kutupa jukumu la kufanya sisi kama wakristo. Sio tu kusema sisi tumeokoka halafu basi, hapana bali ni pamoja na kuwafanya wengine kuwa kama sisi, kuwafanya kuwa wanafunzi wa Kristo.

2) Kwasababu ya ushuhuda wako mwenyewe.

Mitume walikuwa na ujasiri wa kumuhubiri Kristo, kwasababu ya ushuhuda wao wenyewe kwa mambo waliyoyaona kwa  Bwana Yesu akiwatendea.

Matendo 4:18  Wakawaita, wakawaamuru wasiseme kabisa wala kufundisha kwa jina la Yesu.

19  Petro na Yohana wakawajibu wakawaambia, Kwamba ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe;

20  maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia.

Ukisoma pia 1Yohana 1:1-3  Mtume Yohana anasema..

1Yohana 1:1  Lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima;

2  (na uzima huo ulidhihirika, nasi tumeona, tena twashuhudia, na kuwahubiri ninyi ule uzima wa milele, uliokuwa kwa Baba, ukadhihirika kwetu);

3  HILO TULILOLIONA NA KULISIKIA, TWAWAHUBIRI NA NINYI; ili nanyi pia mpate kushirikiana nasi: na ushirika wetu ni pamoja na Baba, na pamoja na Mwana wake Yesu Kristo.

Hii ikiwa na maana, kuwa kila mkristo aliyekombolewa, anaoushuhuda wa mambo makuu aliyotendewa na Yesu tangu siku alipookoka, Tofauti kubwa aliyoipata katika maisha yake mpya ukilinganisha na yale ya zamani, jinsi mizigo yake ilivyotuliwa, hofu kuondolewa, magonjwa yake kuponywa, kufunguliwa, kupokea furaha ya wokovu isiyo na kiasi, amani, utulivu. N.k.

Yote haya kwa mkristo anayethamini wema wa Mungu hataona aibu kutamani na wengine wauonje uzuri huo ulio katika Kristo Yesu. Na hivyo atatoka nje! na kwenda kuwahubiria wengine Injili ya Yesu Kristo,kama mitume walivyofanya.

3) Kwasababu watu wanaouhitaji wa kusikia habari za Injili.

Hili lilimkuta mtume Paulo, Hapo mwanzoni alidhani yeye ndio anayekwenda kuwashawishi watu kuhusu Yesu, lakini siku moja aliona maono, watu wa mbali Makedonia wakiwa na uhitaji mkubwa sana wa kumjua Mungu. Hivyo akalitii ono lile akaenda.

Matendo 16:9  Paulo akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, akimsihi, na kumwambia, Vuka, uje Makedonia utusaidie.

10  Basi alipokwisha kuyaona yale maono, mara tukataka kutoka kwenda Makedonia, kwa kuwa tuliona hakika ya kwamba Mungu ametuita tuwahubiri Habari Njema.

Hata sasa, wapo watu wengi wana kiu ya kuijua njia ya kweli, mioyoni mwao wakiwa na shauku ya kuifahamu hiyo NJIA. Lakini sisi tukikaa na kusema hakuna mwenye haja, twajidanganya. Hatupaswi kuona watu kwa nje wanatuchekea, wanafurahi, wana raha, tukadhani hali zao rohoni ndio hivyo zilivyo, tukapuuzia kuwahubiria injili. Wengi wapo kwenye vifungo na wanatamani wapate msaada wa kutoka huko, hawasemi tu. Na anayeweza kuwatoa hapo ni Kristo tu peke yake. Siku ukizungumza nao ndio utajua kweli walikuwa na haja na Kristo. Hivyo usichague wa kumshuhudia. Fahamu tu watu wana haja na kuujua ukweli. Hubiri injili ya Kristo.

4) Kwasababu roho za watu zinakwenda kuzimu.

Tunajua mtu akifa nje ya Kristo, hakuta tumaini, ni moja kwa moja jehanamu. Tengeneza picha ndugu zako uwapendao, rafiki zako, wazazi wako, na wanadamu wenzako wanakwenda kwenye moto wa milele. Wewe una raha gani leo hii usiwashuhudie habari za Yesu Kristo?.Embu tengeneza picha habari ya Yule tajiri na Lazaro, (Luka 16:19-30) alitamani, mtu atoke kuzimu akawahubirie watu injili ili wasifike mahali pale pa mateso, lakini akaambiwa wapo Musa na manabii huko duniani (ambao ndio sisi), tuwahubirie.

Hivyo kwa sababu hizo kuu nne (4), wewe kama mwaminio uliyeokoka, huna budi kuwashuhudia wengine habari za Kristo. Utasema mimi sina uzoefu, Kumbuka Yesu haitaji uzoefu wako, kuwaokoa watu, kwasababu hata wewe hukuupokea kwa uzoefu wowote, anahitaji kuwaambia Yesu anasemehe dhambi, anaokoa wanadamu, anatoa uzima wa milele bure, anatuepusha na hukumu ya milele, anatua mizigo ya watu, anafariji, anaponya roho, anatupa nguvu ya kuushinda ulimwengu na dhambi. Njoo kwake, akufanye kiumbe kipya upokee uzima wa milele. Hivyo tu. Na hayo mengine mwachie yeye, usifikiri fikiri atakuongoza kwa jinsi utakavyokuwa unasema.

Mathayo 10:20 “ Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu”.

Anza sasa.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NI INJILI GANI UNAHUBIRI?

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Mungu alituumba?

Swali: Kwanini Mungu ametuumba? Na Sababu ya sisi kuwepo ni ipi?.. Na kwanini mmoja aumbwe hivi mwingine vile? kwa ujumla kwanini Mungu aliiumba dunia?


Jibu: Mungu katuumba sisi kwa “Kupenda kwake yeye (Mapenzi yake)”… Ili yeye afurahi kuwa pamoja nasi na sisi tufurahi kuwa pamoja naye!.

Ufunuo 4:11 “Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na KWA SABABU YA MAPENZI YAKO VILIKUWAKO, navyo vikaumbwa”.

Kwetu kuumbwa ni “faida kubwa”…kwasababu hakuna faida yoyote ya “kutokuwepo”.. tengeneza picha haupo au hatupo!..je ni faida gani unapata au tunapata?..Lakini kama tukiwepo na tukaishi maisha ya milele na furaha basi ni heri sana!.

Na Mungu mwenyewe ametuahidia uzima wa milele kupitia mwanae YESU KRISTO.

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”

Lakini kama mtu hatapenda kuishi, na wala hataki maisha basi njia ya kupoteza maisha ni kumkataa YESU.

1Yohana 5:12  “Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima”

swali la pili; kwanini mmoja aumbwe hivi mwingine vile?

Jibu rahisi ni kwasababu ndivyo ilivyompendeza yeye ili kututofautisha sisi kwa sisi (hajapenda wote tufanane kama sisimizi)…na hatuwezi kuhoji Zaidi!.

Warumi 9:20  “La! Sivyo, Ee binadamu; wewe u nani umjibuye Mungu? Je! Kitu kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, Kwani kuniumba hivi?

21  Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?”

Lakini kwa vyovyote vile tulivyoumbwa tunapaswa tuutafute uzima wa milele na pia ni muhimu kufahamu kuwa kwa Mungu hakuna upendeleo wa mmoja Zaidi ya mwingine, wote tupo sawa mbele zake, pasipo kuangalia mwonekano, wala kimo, wala umri, wala jinsia.. Wote tunapendwa sawa, na tunapimwa sawa mbele zake .

Je unao uzima wa milele ndani yako?..Kumbuka uzima wa Milele upo kwa mmoja tu! YESU KRISTO!, Ikiwa bado hujampokea na unahitaji msaada katika kumpokea basi  waweza wasiliana nasi kwa namba zetu..

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

NUNUA MAJI YA UZIMA.

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

FAHAMU VIASHIRIA VYA MTU ALIYESAMEHEWA DHAMBI ZAKE.

Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Kuota unakabwa, mara kwa mara ni ishara ya nini?

SWALI: Mimi kila nikilala, huwa kuna kitu kinanikaba koo, nakosa pumzi, kinanikandamiza naona kama nakwenda kufa au wakati mwingine ninaganda muda mrefu siwezi kusogea. Hata nikijaribu kukemea, natumia kushindana sana, baadaye kinaniachia, Je hili ni jinamizi?. Jambo hili limekuwa likijirudia mara kwa mara. Nimejaribu kufunga na kuomba zinaweza pita tu  siku kadhaa halafu kikajirudia tena. Naomba msaada nifanye nini?


JIBU: Hayo ni mashambulizi ya adui ndotoni. Tufahamu kuwa adui hashambulii tu katika mwili, lakini wakati mwingine pia katika ndoto. Wapo watu wanaosumbuliwa na shetani husasani katika maeneo ya ndoto.

Utakuta kila anapolala, ni mfululizo tu wa ndoto za kipepo, labda anafukuzwa-fukuzwa, au anazini-zini na mapepo hayo, au yupo makaburini, anafanya mambo ya kichawi, zaidi wengine zinakuwa ni mwendelezo, yaani pale alipoishia jana, leo anaendelea nazo sehemu ya pili, kila anapolala hana raha, kwasababu anajua vitisho ni vilevile anakwenda kukutana navyo. Wengine mpaka inazidi wanasikia sauti kabisa za mapepo, zikiwasemesha, au wanaona vitu vya ajabu vikipita mbele yao, na hiyo yote hutokea pindi tu wanapopitiwa na usingizi kidogo, haijalishi mchana au usiku. Kundi lingine ndio hili ambalo wanaona kama wananaswa, na kitu Fulani pumzi haitoki, wanaishia kutaabika. N.k.

Sasa, unapokutana na mojawapo ya shida, hizo au mashambulizi hayo ndotoni. Jambo la kwanza ‘hupaswi kuogopa’ Fahamu suluhisho ni moja tu nalo ni YESU KRISTO. Lakini wengi hawajui ni kwa namna gani.

Mambo haya matatu (3), yaelewe yatakusaidia..

1) Tumia jina la Yesu.

Unapojikuta kwenye mashambulizi hayo, usiwe tu bubu. Hakikisha unalitumia jina la YESU kukemea. Kuyadhibiti hayo mapepo na kazi zao. Kwasababu mamlaka hiyo umepewa.

Mathayo 10:19  Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Lakini ukiona unasumbuliwa na hizo ndoto, halafu unapambana mwenyewe mwenyewe, huna silaha yoyote mkononi mwako, jiandae kukugeuza wewe  kuwa ndio kijiwe chao. Vaa silaha za vita. Jina la Yesu ndio silaha yetu kuu, kutiisha nguvu zote za Yule mwovu.

2) Jiweke vema nafsini, kabla hujalala.

Penda kuwa mwombaji kabla hujalala, usilale tu bila kumkabidhi Bwana usiku wako. Lakini pia hakikisha moyoni mwako, huna makunyanzi ambayo shetani atapata sababu ya kukushitaki. Unajua ni kwanini biblia inasema maneno haya?

Waefeso 4:26  Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; 27  wala msimpe Ibilisi nafasi

Ni kwasababu shetani hupenda mipenyo kama hiyo, kwamfano moyoni mwako una vinyongo na wenzako, una hasira na jirani zao, mambo kama hayo, husababisha adui kukushambulia kwa njia yoyote nyakati za usiku. Hivyo ukabidhi moyo wako kwa Bwana.

3) Zidisha Imani.

Ikiwa mambo hayo mawili unayafanya, lakini bado unaona mashambulizi, yanaendelea. Basi tatizo kubwa kwako lipo kwenye IMANI.  Imani yako ni chache. Upo wakati mitume walipambana na mapepo wakashindwa kuyatoa. Baadaye wakamuuliza Bwana mbona sisi tulishindwa? Yesu akawaambia ni kwasababu ya upungufu wa imani yenu. Hata leo hii ukiona mkristo unasumbuliwa sana na vibwengo, na vipepo. Ujue pia imani yake bado haijawa imara.

Kwa namna gani?

Bado hujaamini vya kutosha nguvu iliyopo ndani ya JINA LA YESU. Na ushindi ulipoupata kupitia Kristo Yesu moyoni mwako. Unachopaswa kufanya ni kumwamini Yesu asilimia mia alimaliza yote msalabani, uwe jasiri, ondoa hofu, vipepo ni vinyago tu, havina chochote cha kukubabaisha wewe. Ukiona hiyo hali inakuja wewe kuwa  ujasiri na Imani yote, usiope kitu. Kemea. “Sema wewe pepo, mimi nimekombolewa na Yesu, huna uwezo wa kushindana na Roho Mtakatifu aliye ndani. Na sasa nisikilize, kuanzia sasa hili sio hekalu lako. Kwa mamlaka ya kifalme iliyo ndani ya jina la Yesu Kristo mwokozi wangu, nakuamuru toka na kwamwe usirudi hapa tena”.

Ukiwa na ujasiri unaotokana na imani ya Bwana unayemtumikia. Nakuambia pepo hilo litabadili uelekeo mara moja, hata likija kujaribu mara nyingine likakukuta na msimamo wako huo huo, hakuna hofu ndani yako. Ndio bye! bye! Halitakaa lirudi tena itakuwa ni historia.

Kumbuka Samsoni alipokutana na Yule Simba, yeye alimwona kama ni “mzinga” tu uliomletea asali. Hivyo akalirarua, na ndio maana baadaye akaja akakuta asali ndani yake akala akaondoka. Kwasababu alijua nguvu zilizo ndani yake, zinatuliza pepo na bahari, na milima  simbuse hichi kisimba-mbarara kinachonguruma hapa mbele yangu.

Na wewe vivyo hivyo, usiishi kinyonge-nyonge tu, unakubali kunyanyaswa nyanyaswa na hivyo vipepo ambavyo havina kitu kwako kama vile huna mtetezi hapa duniani.. KEMEA! KWA IMANI, na Ujasiri. KAZI ITAKUWA IMEISHA!. Wala usitafute maombezi.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine

IMANI “MAMA” NI IPI?

MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.

KUOTA UPO MAKABURINI.

Rudi nyumbani

Print this post

KWANINI MUNGU HAJIBU MAOMBI?

Kawaida MUNGU huwa anajibu maombi, isipokuwa Majira yake mara nyingi ni tofauti na Majira yetu.. Sisi uwa tunapenda tujibiwe maombi muda ule ule tunapoomba!.. Hiyo inaweza kutokea ikiwa ombi uliloomba linastahili kujibiwa wakati huohuo..

Lakini ikiwa si mapenzi ya Mungu upate hiko ulichokiomba kwa wakati huo, basi itakupasa usubiri mpaka wakati wa Bwana, na hiyo haimaanishi kuwa Mungu hajakujibu!.. Ameshakujibu isipokuwa jibu lako hajaliweka leo, bali kaliweka kesho, au mwezi ujao au mwaka ujao, au miaka kadhaa ijayo..Kwasababu majibu mengine yanahitaji kwanza mtu aandaliwe ndipo apokee alichokiomba.

Haiwezekanani mtoto ambaye hajaanza hata shule amwombe baba yake amnunulie gari ili aendeshe kwasababu tu baba yake ana uwezo, halafu yule mzazi amjibu kwa kumnunulia hilo gari na kumpa aendeshe siku ile ile alipoomba..Ni kitu ambacho hakiwezekani! Kwa mzazi mwenye akili timamu.

Badala yake mzazi atalichukua lile ombi la mwanae na kuliweka akiba, mpaka atakapokuwa mtu mzima, amekomaa kiakili na kielimu ndipo ampe zawadi ile ya gari, ambayo aliomba miaka kadhaa nyuma…kwasababu wakati huo atakuwa anajua jinsi ya kuliendesha na amekomaa kiakili. Lakini mtoto huyo huyo akiomba peremende kutoka kwa baba yake ni rahisi kupewa wakati ule ule alioomba, kwasababu ombi lake ni dogo, na halihitaji maandalizi yoyote.

Vile vile na kwa upande wa Mungu wetu (ambaye tunamwita BABA)..yapo maombi ambayo anayajibu papo kwa hapo na mengine yatachukua muda, mpaka mtu ajibiwe…

Ndio maana baada ya kuomba ni vizuri kuruhusu mapenzi ya MUNGU yatimie kama Daudi alivyosema katika..

Zaburi 69:13 “Nami maombi yangu nakuomba Wewe, Bwana, Wakati ukupendezao; Ee Mungu, Kwa wingi wa fadhili zako unijibu, Katika kweli ya wokovu wako.

14 Uniponye kwa kunitoa matopeni, Wala usiniache nikazama. Na niponywe nao wanaonichukia, Na katika vilindi vya maji”.

LAKINI PAMOJA NA HAYO YAPO MAOMBI AMBAYO MUNGU HAJIBU KABISA!!. NA MAOMBI HAYO NI KAMA YAFUATAYO.

   1. MAOMBI YA TAMAA.

Mfano wa maombi ya tamaa ni yale mtu anaomba kitu si kwasababu ana haja na hiko kitu, bali kwasababu anataka kukitumia kwa anasa, au kwa mashindano, au kwa maonesho.

Mfano mtu ataomba Mungu ampe pesa, si kwasababu anataka atokane na changamoto Fulani za msingi, bali lengo lake ni ili awe nazo ili awaoneshe watu, au ajivune mbele za watu, au azitumie kwa anasa.. Mtu huyu anaweza asiseme kwa kinywa lakini moyo wake ndivyo vitu unavyovitamani.. Sasa maombi ya mtu wa namna hiyo biblia imesema huwa hayajibiwi.

Yakobo 4:3 “Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”.

Kwahiyo ni muhimu sana, kuzichunguza NIA zetu, (kwamba kwanini tunaomba)..tuhakikishe nia zetu ni safi, na kweli tuna haja na hiko kitu tukiombacho kwa NIA njema.

    2. MAOMBI YA MTU MWOVU.

Mtu ambaye hamtaki Mungu moyoni mwake, lakini anataka vya Mungu (anataka kupokea kutoka kwa Mungu), maombi yake mtu huyo hayajibiwi!.

Ni muuaji na hataki wala hana mpango wa kuacha uuaji wake, ni mwizi wala hana mpango wa kuacha wizi wake, ni mzinzi na mwasherati wala hana mpango wa kuacha uasherati wake ijapokuwa anasikia mahubiri yahusuyo hayo kila siku, maombi yake mtu huyu hayajibiwi kulingana na biblia.

Isaya 1:15 “Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu.

16 Jiosheni, jitakaseni; ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu; acheni kutenda mabaya;

17 jifunzeni kutenda mema; takeni hukumu na haki; wasaidieni walioonewa; mpatieni yatima haki yake; mteteeni mjane”.

    3. MAOMBI YA MANUNG’UNIKO NA MALALAMIKO.

Maombi ya Manung’uniko na malalamiko ni yale mtu anaomba kwa kulaumu, na kunung’unika kana kwamba kaonewa au kadhulumiwa, maombi kama haya majibu yake mara nyingi ni kinyume.. badala ya mtu kupokea anachokinung’unikia kinyume chake anaweza kupoteza hata kile kidogo alicho nacho.

1Wakorintho 10:10 “Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu.

11  Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani”.

Epuka manung’uniko wakati wa maombi.. badala yake kuwa mtu wa shukrani, na mtu wa kumsihi Mungu kwa unyenyekevu na heshima.

    4. MAOMBI YA KUMJARIBU MUNGU.

Mfano wa maombi haya ni yale, shetani aliyompelekea Bwana YESU kule jangwani.

Luka 4:9  “Akamwongoza mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini;

10  kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake wakulinde;

11  na ya kwamba,mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

12  Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako”.

Usiombe maombi ya kumwangalia BWANA atafanya nini… maombi ya nama hiyo hayana majibu, na zaidi wakati mwingine yanaishi kupokea adhabu badala ya Baraka.

1Wakorintho 10:9 “Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka”

Jihadhari na aina hizo nne (4) za Maombi ili upokee majibu ya Maombi yako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

FAIDA ZA MAOMBI.

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?

NDUGU,TUOMBEENI.

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Rudi nyumbani

Print this post

FAHAMU VIASHIRIA VYA MTU ALIYESAMEHEWA DHAMBI ZAKE.

Si kila mtu anayesema “amemwamini” Yesu ni kweli, ameokoka, au amepokea msamaha wa dhambi zake. Ukweli ni kwamba kuupokea msamaha wa dhambi kwa kuiamini kazi aliyoimaliza Yesu Kristo pale msalabani ya ukombozi wa wanadamu si kugumu, Lakini haiji kwa kusema “naamini tu” halafu basi ndio uwe tayari umetiwa muhuri na Mungu kwamba ni wake milele.

Imani ya namna hiyo inatiwa imani ya” bure” (1Wakorintho 15:2).

Na sehemu nyingine inajulikana kama  “imani ya wote” ambayo hata mashetani wanayo. Wanamwamini Yesu kuwa ni mwokozi, lakini pia wanaiamini vizuri sana kazi ya msalaba (Yakobo 2:19). Lakini je! Wamesamehewa dhambi zao?

Zipo injili zinazowafundisha watu, “kuamini tu” au “kukubali tu msamaha” inatosha. Hakuna la ziada baada ya hapo. Ndugu hizo sio sifa za mwaminio yoyote.

Neno “kuamini” kwa kigiriki ni PISTIS, lenye maana ya sio tu kuwa na ujasiri na Mungu wako kwa kile anachokupa au kukuelekeza,lakini pia kuwa ‘mwaminifu”.

Maana yake ni kuwa ili tuseme tumeamini ni lazima pia tuwe waaminifu kwa Yule tuliyemwamini.

Sasa mtu yeyote aliyemwamini Kristo. viashiria hivi vitatu(3) utaviona ndani yake

  1. Atakuwa ni kondoo

Yohana 10:2  Aingiaye mlangoni ni mchungaji wa kondoo. 3  Bawabu humfungulia huyo, na kondoo humsikia sauti yake; naye huwaita kondoo wake kwa majina yao, na kuwapeleka nje. 4  Naye awatoapo nje kondoo wake wote, huwatangulia; na wale kondoo humfuata, kwa maana waijua sauti yake. 5  Mgeni hawatamfuata kabisa, bali watamkimbia; kwa maana hawazijui sauti za wageni…

27  Kondoo wangu waisikia sauti yangu; nami nawajua, nao wanifuata. 28  Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu. 29  Baba yangu aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote; wala hakuna mtu awezaye kuwapokonya katika mkono wa Baba yangu.

Umeona, ni kondoo tu, ndio hawawezi kupokonywa katika mikono ya mchungaji wake. Lakini mbuzi wanaweza, kwasababu hawategemei sana sauti ya mchungaji, wanaweza kujichunga wenyewe. Ukiona mtu anasema ameokoka, halafu, maisha yake ni kama ya mbuzi, ujue huyo si wa Kristo. Haisikii sauti ya Kristo ikimwelekeza aache maisha ya kiulimwengu, ajitofautishe na watu wa kidunia, . Ujue huyo bado hajapokea kweli msamaha wa dhambi, kwasababu hajaamini. Anapaswa ashuhudiwe mpaka aamini. Na aseme kuanzia leo, Kristo ndio kiongozi wa maisha yangu na sio dunia tena. Akubali TOBA ya kweli.

2. Atakuwa Ni kiumbe kipya.

Yesu alisema..

Yohana 1:12  Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.

13  waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu

Wenye sifa ya kwamba wamemwamini Yesu ni lazima pia wawe wamegeuzwa kuwa watoto wa Mungu, yaani wamezaliwa mara ya pili kwa mbegu isiyo ya kibinadamu, bali ya Mungu mwenyewe.

Na kama tunavyofahamu mtoto hubeba tabia za Baba. Vivyo hivyo mwaminio ni lazima moyoni mwake kuwake, tamaa za Baba yake. Maandiko yanasema Baba ni Mtakatifu, vivyo hivyo tamaa ya mwaminio huyo mpya itakuwa ni kupenda utakatifu, na kuutafuta huo kwa bidii.

Haiwezekani mtu aliyemwamini Yesu, awe na raha tena katika maisha ya kidunia ya dhambi. Au asipige hatua yoyote ya kuutafuta ukamilifu. Halafu tuseme ni mwaminio si kweli.

1Yohana 3:9  Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu

3) Atakuwa ni mwanafunzi

Mwaminio mpya amefananishwa na mwanafunzi, na mwanafunzi sikuzote huwa yupo tayari kujifunza, na kukua kiufahamu.

Matendo 2:41  Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42  Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.

Hivyo mtu yoyote anayesema amemwamini Yesu, na hapendi fundisho, hapendi kuchungwa, hapendi kufuatiliwa maendeleo yake ya kiroho, anapinga ubatizo, na wakati mwingine kufanya ushirika, huyo mtu bado hajaamini.

Lakini akiwa na sifa zote hizo tatu, ni uthibitisho kuwa amemwamini Yesu, na hivyo kaupokea pia msamaha wa dhambi. Mtu wa namna hiyo wokovu kwake ni uhakika. Kwasababu Yesu ameumbika ndani yake. Kazi ya Mungu kamilifu imetimilika ndani ya mwanadamu.

Je! Na wewe Umepokea ondoleo la dhambi zako? Je! Ni mwanafunzi, ni kondoo, ni mwana wa Mungu?. Kama bado basi fahamu unamwihitaji Kristo, fungua moyo wako mkaribishe ndani yako akuokoe. Sasa, Maanisha tu tangu sasa kuwa na badiliko na yeye mwenyewe atakuokoa.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

JE! UNAMPENDA BWANA?

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini tunafunga na kuomba?

Kanuni ya kufunga na kuomba inafananishwa na kanuni ya Kuku kuyaatamia mayai yake mpaka kufikia hatua ya kutotoa vifaranga.

Ili mayai yaweze kuanguliwa na vifaranga kutokea ni lazima Kuku ayaatamie mayai kwa siku 21, na ili aweze kuyaatamia kwa mafanikio, basi hana budi kujizuia kula kwa kipindi kirefu ili asipoteze joto la mayai yale. Ndio hapo utaona itampasa atoke mara chache chache kwenda kutafuta chakula kisha kuyarudia mayai yake, na atafanya hivyo kwa siku zote 21.

Maana yake kama kuku hatajiingiza katika hiyo adhabu ya kuutesa mwili wake na kujizuia na milo kwa siku 21, hawezi kupata vifaranga!.

Vile vile kuna mambo ambayo yanahitaji “Joto la kiroho” kwa siku kadhaa za MIFUNGO na MAOMBI na KUJITESA. Ili tuweze kuyapata…Vinginevyo hayatatokea kabisa haijalishi tutayatamani kiasi gani!.

Bwana YESU alisema mambo mengine hayatoki pasipo Maombi na Mifungo..

Mathayo 17:21  “[Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]”

> Ukiona umejaribu kutafuta kitu na hujakipata, ingia kwenye mfungo!

> Ikiwa umeomba na bado hujapata, ongezea na mfungo juu yake!.

> Ikiwa umetafuta na hujapata ongezea na mfungo wa maombi juu yake!.

> Ikiwa unataka Amani, Furaha, au Nguvu za kuendelea mbele, usikwepe mfungo! N.k

Ukiwa ni mtu wa kuomba pamoja na kufunga, utakuwa ni mtu wa mafanikio kiroho na kimwili. Utaangua vingi kwa wakati.. Lakini ukiwa ni mtu wa kukwepa mifungo basi utatumia nguvu nyingi sana kupata baadhi ya mambo.

Danieli 9:2 “katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.

3 Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka KWA MAOMBI, na dua, PAMOJA NA KUFUNGA, na kuvaa nguo za magunia na majivu.……………………….

21 naam, nilipokuwa nikinena katika kuomba, mtu yule, Gabrieli, niliyemwona katika njozi hapo kwanza, akirushwa upesi, alinigusa panapo wakati wa dhabihu ya jioni.

22 Akaniagiza, akaongea nami, akasema, Ee Danielii, nimetokea sasa, ili nikupe akili upate kufahamu.

23 Mwanzo wa maombi yako ilitolewa amri, nami nimekuja kukupasha habari; maana wewe unapendwa sana; basi itafakari habari hii, na kuyafahamu maono haya”.

Na kuna Toba nyingine zinahitaji Mfungo kabisa ili mtu aweze kufunguliwa.

Yoeli 2:12 “Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea;

13 rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie Bwana, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya”.

Usikwepe mifungo!

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

IJUE FAIDA YA KUFUNGA PAMOJA NA WANYAMA WAKO.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni mtu yupi aliyeishi miaka mingi kwenye biblia?

Swali: Je mtu aliyeishi miaka mingi kwenye biblia alikuwa nani?..na Mtu aliyeishi miaka mingi duniani ni nani?.


Jibu: Katika biblia mtu aliyeishi miaka mingi kuliko wote, ni METHUSELA, mwana wa Henoko aliyetwaliwa na Mungu..Biblia inasema huyu Methusela aliishi miaka 969, na hakuna mwingine aliyerekodiwa kuishi miaka mingi kuliko yeye.

Mwanzo 5:25 “Methusela akaishi miaka mia na themanini na saba, akamzaa Lameki.

26 Methusela akaishi baada ya kumzaa Lameki miaka mia saba na themanini na miwili, akazaa wana, waume na wake.

27 Siku zote za Methusela ni miaka MIA KENDA NA SITINI NA KENDA, AKAFA”.

Wengine walioishi miaka mingi katika biblia ni pamoja na;

  1. Yaredi, aliishi miaka 962, (Soma Mwanzo 5:20).
  2. Nuhu, Miaka 950 (Soma Mwanzo 9:29)
  3. Adamu, Miaka 930 (Soma Mwanzo 5:5)
  4. Sethi, Miaka 912 (Soma Mwanzo 5:8)
  5. Kenani, Miaka 910 (Soma Mwanzo 5:14)
  6. Enoshi, Miaka 905 (Soma Mwanzo 5:11)
  7. Mahalaleli, Miaka 895 (Soma Mwanzo 5:17)
  8. Lameki, Miaka 777 (Soma Mwanzo 5:31)
  9. Henoko, Miaka 365 (Soma Mwanzo 5:18-24)

Baada ya “Gharika ya Nuhu” miaka ya wanadamu ilishushwa mpaka kufikia miaka 120.. Ambapo ni wachache sana walivuka miaka hiyo, wengi waliishi chini ya hiyo..

Mwanzo 6:3 “Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini”.

Lakini kwajinsi siku zinavyozidi kwenda Miaka ya mwanadamu kuishi duniani ilizidi kushuka.. kutoka 120 mpaka 80

Zaburi 90:9 “Maana siku zetu zote zimepita katika hasira yako, Tumetowesha miaka yetu kama kite.

10 Siku za miaka yetu ni MIAKA SABINI, NA IKIWA TUNA NGUVU MIAKA THEMANINI; Na kiburi chake ni taabu na ubatili, Maana chapita upesi tukatokomea mara”.

Lakini swali kuu ni hili; kwanini miaka ya wanadamu inazidi kupungua siku baada ya siku? Je ni kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa au mabadiliko ya vyakula?

Jibu rahisi ni kwasababu ya “kuongezeka kwa Maasi”. Wala si mabadiliko ya hali ya hewa! Bali ni DHAMBI!.. Kitu cha kwanza kilichopunguza miaka ya Adamu na Hawa kutoka kuishi MILELE mpaka kufikia kuishi miaka 930 si kingine Zaidi ya DHAMBI!.. wala si kwasababu walikuwa hawazingatii mazoezi au milo kamili!..La!! bali ni dhambi!..

Na kanuni hiyo hiyo ndiyo inayopunguza maisha ya mwanadamu inaendelea mpaka sasa… Na wakati huo huo upande wa pili shetani anajaribu kuwaaminisha watu kuwa ni “Milo wanayokula ndiyo inayopunguza miaka” kwamba wapunguze ulaji wa nyama, na mafuta, na wazingatie mazoezi wataishi miaka mingi.

Mambo hayo ni mazuri, na yanafaa..lakini hayafai katika kuongeza UREFU WA MAISHA YA MTU, Kwani kuna wengi ambao wamezingatia hayo yote lakini wamewahi kuondoka duniani!.. na kuna ambao hawajazingatia hayo yote lakini wanayo miaka mingi duniani.

Kanuni ya kuishi miaka mingi na ya heri NI KUMCHA MUNGU NA KUEPUKANA NA UOVU, hiyo tu… Zishike Amri, fanya mapenzi ya Mungu, maisha yako yatakuwa marefu, hapa na katika ulimwengu ujao.

Kutoka 20: 12 “Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.

NIFANYE NINI ILI NISILALE NINAPOSOMA BIBLIA.

MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

KUUMBWA TU, HAITOSHI YAPO MAMBO MENGINE MAWILI

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya Mungu ya uzima.

Kama kichwa cha somo kinavyosema. “Kuumbwa tu haitoshi”. Ikiwa na maana yapo mengine yanapaswa yafanyike ili uumbaji huo ukamilike.

Ukisoma kitabu cha Mwanzo mstari wa kwanza kabisa wa kitabu kile unasema.

Mwanzo 1:1Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. 

Lakini cha ajabu ni kuwa uumbaji ule haukuukamlisha ulimwengu wetu, ndio maana ukisoma vifungu vinavyofuata anasema..

Mwanzo 1:2a “ Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji;…”

Dunia Ilikuwa ni Utupu, na ukiwa.  Na yenye giza, kitu cha kutisha. Ndio hapo Mungu anachukua hatua nyingine kuu MBILI (2), ili kuikamilisha. Ya kwanza ni “ROHO WA MUNGU” kutua juu yake, na ya pili kutamka “NENO” lake.

Baada ya hapo ulimwengu ukaanza kuumbika vizuri, na kuwa makao ya mwanadamu, pamoja na kila kiumbe kilichohai kilichoumbwa na mwenyezi Mungu, kama alivyokusudia yeye.

Mwanzo 1:2b…Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.  3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.  4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza

Kwamba kiumbe chochote kilichoumbwa, Kikikosa Roho wa Mungu, na Neno la Mungu. Kiumbe hicho ni Ukiwa na utupu haijalishi kitakuwa hodari, kikubwa, kina utashi  kiasi gani.

Ni kufunua nini?

Mimi na wewe tumeumbwa na Mungu tukaitwa wanadamu, ni vizuri. Lakini hiyo haitoshi. Bado hatujakamilika kama Neno La Mungu halijafunuliwa ndani yetu. Na Neno hilo si mwingine zaidi ya YESU. Yeye ndio ile sauti ya Mungu tangu pale mwanzo, iliyosema na iwe NURU. Ambayo baadaye ikaja  kufanyika mwili, likakaa na sisi;

Yohana 1:1  “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.

2  Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.

3  Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.

4  Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, NAO ULE UZIMA ULIKUWA NURU YA WATU. 5  NAYO NURU YANG’AA GIZANI, WALA GIZA HALIKUIWEZA”

Maana yake ni kuwa kama huna KRISTO YESU maishani mwako. Wewe ni bure.

Vilevile na Roho wake MTAKATIFU kuwa juu yako.

Warumi 8:9  Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote ASIPOKUWA NA ROHO WA KRISTO, HUYO SI WAKE.

Ndio maana kwanini upo umuhimu wa mtu kuzaliwa mara ya pili. Kwa kumpokea Kristo kama Bwana na mwokozi wa maisha yake, ili apate msamaha wa dhambi. Lakini pia kupokea Roho wake Mtakatifu.

Ukikamilisha hayo mawili wewe hapo unakuwa mtu KAMILI na HALISI, aliyeumbwa na Mungu. Unayeweza kumzalia Mungu matunda yote anayotaka.

Okoka ndugu, Fahamu kuwa hakuna maisha nje ya Kristo,  hizi ni siku za mwisho. Kristo anakaribia kurudi, ulimwengu upo ukingoni. Umejiandaaje na karamu ya mwanakondoo mbinguni? Ukamilifu wako upo wapi?

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NJIA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

Nitajuaje kuwa nimesamehewa dhambi zangu?

AGIZO LA TOBA LINAENDANA NA UBATIZO!.

Rudi nyumbani

Print this post

Mtande ni nini? Ni funzo gani lipo nyuma yake?

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi.

Waamuzi 16:13 Delila akamwambia Samsoni, Hata sasa umenidhihaki, umeniambia maneno ya uongo; niambie sasa, waweza kufungwa kwa kitu gani? Akamwambia, Ukivifuma hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo. 

14 Basi akazifunga kwa msumari, akamwambia Samsoni, Wafilisti wanakujia. Naye akaamka usingizini, akaung’oa ule msumari, na ule mtande. 

15 Mwanamke akamwambia, Wawezaje kusema, Nakupenda; na moyo wako haupo pamoja nami? Umenidhihaki mara hizi tatu, wala hukuniambia asili ya nguvu zako nyingi.

Mtande ni kifaa maalumu kinachotumika kufumia nyuzi za nguo, kwa kuzisokota pamoja ili kuunda nguo. Tazama mfano wa picha.

Hivyo nyuzi za nguo zilipitishwa katikati ya kamba hizo ngumu za mtande, kisha kuvutwa na kukazwa na mfumaji.

Katika habari hiyo tunaona Delila kazi yake huwenda ilikuwa ni ya ufumaji. Kwasababu ya uwepo wa kifaa hicho katika nyumba yake. Lakini katika harakati zake za kutaka kujua asili ya nguvu za Samsoni, biblia inatuambia, Samsoni alimdanganya kwa kumwambia ikiwa atavifuma vishungi vyake saba vya nywele katika mtande ule, basi, hatakuwa na nguvu za kujinasua, mahali pale.

Delila kusikia vile akaamini ni kweli, kwasababu kwa kawaida mtu ukishikwa tu nywele zako, si rahisi kuleta vurugu kwasababu utakuwa unajiumiza mwenyewe. Delila akizingatia kuwa alijua pia namna ya kufuma nyuzi vizuri. Hivyo alijihakikishia kuwa hilo linawezekana. Na cha kuongezea akapigilia na msumari kabisa, ili atakapojaribu kuzivuta nyewe zake, kutoka pale ashindwe. Kisha wafilisti waje kumchukua.

Lakini bado tunaona hilo halikuwezekana. Samsoni aling’oa misumari ile na kuuvunja mtande ule, Delila alipomwamsha.

Ni nini Tunajifunza katika habari hiyo kama waaminio?

KATIKA USINGIZI MUNGU ANAUMBA, NA SHETANI NAYE ANANASA.

Jiulize kwanini majaribio hayo yote Delila aliyafanya wakati ambao Samsoni amelala?. Alijua kabisa wakati akiwa macho Samsoni hawezi kukubali. Lakini pia swali lingine watu wanalojiuliza, iweje Samsoni, asisikie lolote wakati anatendewa vitendo vile. Kwamfano mpaka Delila anachukua nywele zake na kuziingiza kwenye mtande na kuzibana na kuzipigia misumari, asisikie chochote, ni usingizi wa namna gani?

Ndugu Mitego ya shetani, si rahisi kuigundua, kwasababu anaoutashi wa kuiweka kiasi cha kukufanya wewe usiwe mwepesi kuitambua, au kuisikia. Utashutukia tu umeshanaswa. Hivyo kama mwaminio ni kukimbia usingizi wowote wa kiroho kwa hali zote. Kwa kumtazama na kumfuata Yesu wakati wote. Unapomtazama Yesu, na kumtii kwa kuyakimbia machafu ya dunia. Hapo hujalala kiroho.

Lakini Pia katika usingizi Mungu pia hufanya jambo, na hilo si lingine zaidi ya kuumba. Utalithibitisha hilo kipindi kile alipomuumba Adamu, Mungu anasema.

Mwanzo 2:21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, 

22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. 

23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.

Umeona? Ukitulia kwa Bwana, akapumzika kwa Bwana, ukalala kwake. Jiandae kuumbiwa jambo lako bora kuliko yote katika maisha yako. Kama vile Mungu alivyomuumbia Adamu, msaidizi bora kuliko wote.

Kulala kwa Bwana ni kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yako, akupe ondoleo la dhambi. Kisha kuamua kuacha mambo yote ya kidunia na kumfuata yeye kwa uaminifu kwa kulitii Neno lake baada ya hapo. Na hapo ndipo unakuwa umelala kwake.

Hivyo chagua leo “Kuumbwa” badala ya “Kunaswa”. Mpokee Yesu sasa, ikiwa upo tayari kufanya hivyo. Basi fungua hapa kwa mwongozo huo wa sala ya Toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KITENDAWILI CHA SAMSONI

JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?

Je Bwana Yesu alikuwa na nywele ndefu?

Rubani ni nani katika biblia? (Ezekieli 27:8)

Rudi nyumbani

Print this post