Ni mtu yupi aliyeishi miaka mingi kwenye biblia?

Ni mtu yupi aliyeishi miaka mingi kwenye biblia?

Swali: Je mtu aliyeishi miaka mingi kwenye biblia alikuwa nani?..na Mtu aliyeishi miaka mingi duniani ni nani?.


Jibu: Katika biblia mtu aliyeishi miaka mingi kuliko wote, ni METHUSELA, mwana wa Henoko aliyetwaliwa na Mungu..Biblia inasema huyu Methusela aliishi miaka 969, na hakuna mwingine aliyerekodiwa kuishi miaka mingi kuliko yeye.

Mwanzo 5:25 “Methusela akaishi miaka mia na themanini na saba, akamzaa Lameki.

26 Methusela akaishi baada ya kumzaa Lameki miaka mia saba na themanini na miwili, akazaa wana, waume na wake.

27 Siku zote za Methusela ni miaka MIA KENDA NA SITINI NA KENDA, AKAFA”.

Wengine walioishi miaka mingi katika biblia ni pamoja na;

  1. Yaredi, aliishi miaka 962, (Soma Mwanzo 5:20).
  2. Nuhu, Miaka 950 (Soma Mwanzo 9:29)
  3. Adamu, Miaka 930 (Soma Mwanzo 5:5)
  4. Sethi, Miaka 912 (Soma Mwanzo 5:8)
  5. Kenani, Miaka 910 (Soma Mwanzo 5:14)
  6. Enoshi, Miaka 905 (Soma Mwanzo 5:11)
  7. Mahalaleli, Miaka 895 (Soma Mwanzo 5:17)
  8. Lameki, Miaka 777 (Soma Mwanzo 5:31)
  9. Henoko, Miaka 365 (Soma Mwanzo 5:18-24)

Baada ya “Gharika ya Nuhu” miaka ya wanadamu ilishushwa mpaka kufikia miaka 120.. Ambapo ni wachache sana walivuka miaka hiyo, wengi waliishi chini ya hiyo..

Mwanzo 6:3 “Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini”.

Lakini kwajinsi siku zinavyozidi kwenda Miaka ya mwanadamu kuishi duniani ilizidi kushuka.. kutoka 120 mpaka 80

Zaburi 90:9 “Maana siku zetu zote zimepita katika hasira yako, Tumetowesha miaka yetu kama kite.

10 Siku za miaka yetu ni MIAKA SABINI, NA IKIWA TUNA NGUVU MIAKA THEMANINI; Na kiburi chake ni taabu na ubatili, Maana chapita upesi tukatokomea mara”.

Lakini swali kuu ni hili; kwanini miaka ya wanadamu inazidi kupungua siku baada ya siku? Je ni kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa au mabadiliko ya vyakula?

Jibu rahisi ni kwasababu ya “kuongezeka kwa Maasi”. Wala si mabadiliko ya hali ya hewa! Bali ni DHAMBI!.. Kitu cha kwanza kilichopunguza miaka ya Adamu na Hawa kutoka kuishi MILELE mpaka kufikia kuishi miaka 930 si kingine Zaidi ya DHAMBI!.. wala si kwasababu walikuwa hawazingatii mazoezi au milo kamili!..La!! bali ni dhambi!..

Na kanuni hiyo hiyo ndiyo inayopunguza maisha ya mwanadamu inaendelea mpaka sasa… Na wakati huo huo upande wa pili shetani anajaribu kuwaaminisha watu kuwa ni “Milo wanayokula ndiyo inayopunguza miaka” kwamba wapunguze ulaji wa nyama, na mafuta, na wazingatie mazoezi wataishi miaka mingi.

Mambo hayo ni mazuri, na yanafaa..lakini hayafai katika kuongeza UREFU WA MAISHA YA MTU, Kwani kuna wengi ambao wamezingatia hayo yote lakini wamewahi kuondoka duniani!.. na kuna ambao hawajazingatia hayo yote lakini wanayo miaka mingi duniani.

Kanuni ya kuishi miaka mingi na ya heri NI KUMCHA MUNGU NA KUEPUKANA NA UOVU, hiyo tu… Zishike Amri, fanya mapenzi ya Mungu, maisha yako yatakuwa marefu, hapa na katika ulimwengu ujao.

Kutoka 20: 12 “Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.

NIFANYE NINI ILI NISILALE NINAPOSOMA BIBLIA.

MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments