Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Mtu ni kiumbe cha kwanza kilichoumbwa na Mungu duniani, chenye mfano wake na sura yake, kilichoumbiwa utashi na ujuzi ndani yake, kilichotofautishwa  na wanyama wote na viumbe vyote vilivyoumbwa na  Mungu duniani Ndicho kinachoitwa mtu.

Tunasoma hilo katika,

Mwanzo 1:26

[26]Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

Lakini jina Binadamu/mwanadamu, ni neno lililozuka kufuatana na jina la mtu wa kwanza aliyeitwa Adamu.

Jina hilo alipewa na Mungu..Hivyo watu wote waliozaliwa na yeye waliita “wana wa Adamu”kwa kifupi “wanadamu” ambapo jina hilo kwa kiharabu linatamkwa “bin-Adam” ambapo sisi tunatamka “Binadamu”

Lakini ni mtu yule yule..isipokuwa asingeweza kuitwa binadamu siku ile ya kwanza alipoumbwa kwasababu alikuwa bado hajapewa jina, na pia halikuwa hana baba wa mwilini.

Ni sawa na Neno mwebrania na mwisraeli… kabla ya Yakobo kubadilishwa jina lake wana wote wa Ibrahimu hata Ibrahimu mwenyewe aliitwa Mwebrania..(Mwanzo 14:13)

Lakini Yakobo alipobadilishwa jina na kuitwa Israeli, utaona uzao wake wote baada ya pale ulizoeleka na kuitwa waisraeli mpaka leo. Lakini bado mahali pengine waliendelea pia kuitwa waebrania kwa asili yao.

Ndivyo ilivyo kwa mtu na mwanadamu. Ni yule yule kulingana na majira.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?

Uru wa Ukaldayo ni nini?

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

Utasi ni ugonjwa gani? (Marko 7:32).

Mjoli ni nini/ ni nani katika biblia?

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Peter Mgaza
Peter Mgaza
1 year ago

Amen mtumishi wa Mungu, ubarikiwe

Lucas mhula
Lucas mhula
2 years ago

Amen mtumishi 🙏🙏🙏

Anonymous
Anonymous
2 years ago

AMINAA UBARIKIWE SANA MTUMISHI

peter msonge
peter msonge
2 years ago

AMINA