Title March 2022

WALA TUSIACHE KUKUSANYIKA PAMOJA

Waebrania 10:25 “WALA TUSIACHE KUKUSANYIKA PAMOJA, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia”.

Kukusanyika kunakozungumziwa hapo, ni kukusanyika na wapendwa wengine kanisani.

Mbinu ya kwanza shetani anayoitumia kuwaangusha watu, ni kuwatoa katika kundi!..(kuwatenga na kundi), atanyanyua kisa tu , ambacho kitamfanya huyo mtu akereke na aache kwenda kanisani. Na yule mtu kwa kudhani kuwa “kujitenga na wenzake, ndio atakuwa salama, kumbe ndio kajimaliza”.

Vifuatavyo ni visa vichache ambavyo shetani anawahubiria watu, lengo ni kuwatoa ndani ya kundi.

 1. IBADA INACHUKUA MUDA MREFU.

Ukishaanza kuona au kusikia hii sauti ndani yako inayokuambia kuwa “ibada ndefu sana”..basi jua ni shetani anakuhubiria kutaka kukutoa katika kundi, kwasababu anaona kuna hasara unataka kumletea katika ufalme wake.

Siku zote fahamu kuwa siku ya Bwana, ni amri kuwa yote iwe takatifu.. Ni heri ukose ibada za katikati ya wiki, lakini ya Siku ya Jumapili, siku hiyo ifanye takatifu yote kwa Bwana!..ukijiwekea hilo akilini, hutababaishwa na masauti ya shetani yanayokuambia ibada ni ndefu sana.

 2. KUSIKIA HABARI ZA WATU WENGINE.

Wengi shetani anawatoa katika makusanyiko, kuwasikilizisha kwanza habari mbaya za watu wengine wanaoshiriki nao katika kusanyiko hilo, au viongozi wa kanisa hilo. Mara watasikia mshirika Fulani kagombana na mwingine, au Mchungaji haelewani na mtu Fulani, au kafanya hiki au kile..

Na kwasababu hiyo basi wanaamua kuacha kwenda kanisani, kukusanyika kama ilivyokuwa kawaida yao, na kuishia kukaa tu nyumbani…wakidhani kuwa nyumbani ndio wapo salama, pasipo kujua kuwa ni shetani ndio kawatoa kule.

Siku zote fahamu kuwa hakuna mahali patakosa kasoro…kasoro kila mahali zipo, na zitaendelea kuwepo, hivyo kazi mojawapo ya wewe kukuweka pale ni ili uwe sababu ya kuziondoa hizo, kwa kuomba na kuonya, na sio kwa kukimbia na kuacha…

 3. KUKWAZWA NA MTU/BAADHI YA WATU KATIKA KANISA.

Hii ni sababu nyingine shetani anayoitumia kuwatenga watu wengi na kundi!.. utaona mtu kaaambiwa au kafanyiwa jambo moja tu, ambalo ameliona kuwa sio zuri! Lakini utaona hilo hilo analitumia kama sababu ya kutokanyaga tena kanisani.. Lakini akila wali na kukuta kipande kidogo cha jiwe, hamwagi chakula chote!. Lakini kwa Mungu anakuwa ni mtu wa kususa vitu vidogo..

Kumbuka ijapokuwa tunaitwa wakristo, bado hatutakosa kasoro kabisa, mchungaji hawezi kuwa mkamilifu saa zote, muumini mwanzako hawezi kuwa Malaika.. hivyo viwango unavyovitaka uvione hutaviona katika kanisa lolote lile duniani, unachopaswa kufanya ni kuwa mvumilivu, na kuendelea kudumu pale ukiomba na kupambana kurekebisha hizo kasoro..ili hatimaye zipotee kabisa ndani ya kanisa na si kuondoka..

Ukiondoka na kuamua kubaki nyumbani tu!, jua ni shetani ndio kakutoa katika kundi, kwasababu ameona utakuja kumsumbua huko mbeleni.

 4. HOFU YA MATOLEO.

Ni kweli kuwa katika siku hizi za mwisho, watatokea watu wa kupenda fedha hata katika madhabahu za Bwana, lakini usiitumie hiyo kama sababu ya wewe kuacha kwenda kanisani..

Kwasababu hata kama ukihimizwa kutoa, kama kweli na wewe unampenda Bwana huwezi kuchukia.. kwasababu unajua kabisa kwamba unamtolea Mungu, na si mwanadamu.. na hivyo thawabu zako zinazidi kuongezeka tu mbinguni.

Ukisikiliza hubiri la shetani linalokuambia usiende kanisani kwasababu utaambiwa utoe hela, afadhali ukae nyumbani tu!, jua kuwa upo katika hatari kubwa sana..

Kuna faida nyingi za kukusanyika Pamoja, lakini leo tutazitama faida 2 tu!

 1. UNAKUWA IMARA KATIKA IMANI.

Unaweza kusema nikiwa peke yangu, ninaweza kusimama… lakini nataka nikuambia..mtu anayelala hajui dakika aliyoingia usingizini, vile vile mtu aliye pekee yake siku za kwanza atajiona nafuu lakini ndivyo anavyozidi kupoa kidogo kidogo na mwisho kupotea kabisa..

Hebu soma maneno haya…

Mhubiri 4:9 “Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.

10 KWA MAANA WAKIANGUKA, MMOJA WAO ATAMWINUA MWENZAKE; LAKINI OLE WAKE ALIYE PEKE YAKE AANGUKAPO, WALA HANA MWINGINE WA KUMWINUA!

11Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona moto?

12 Hata ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi”.

Hivyo usiache kamwe kukusanyika Pamoja na wengine, kwasababu kuna vitu ambavyo ukiwa peke yako inakuwa ni ngumu kuvipata, mfano wa vitu hivyo ni Faraja, ari, motisha, hamasa,.. Na vile vile kuna vitu ambavyo ukiwa peke yako ni ngumu kuvifanya kikamilifu.. Mfano wa vitu hivyo ni maombi!.. ukiwa mwenyewe nyumbani ni ngumu kukesha kuomba.. lakini ukiwa kwenye mkesha mahali ambapo watu wote wanaomba.. ukitazama kushoto Jirani anaomba, ukitazama kulia mwingine anaomba ni lazima na wewe utapata nguvu ya kuomba.. lakini nyumbani peke yako ni ngumu.

Hiyo ni hekima ya kiMungu, hivyo usijione unayo hekima kuliko Mungu..

Ndio maana utaona ni kwanini Bwana Yesu alikuwa anawatuma wanafunzi wake kwenda kuhubiri, wawili wawili.. na si mmoja mmoja, ni kwasababu alikuwa anajua madhara ya mtu kwenda peke yake.

Marko 6:7 “Akawaita wale Thenashara, akaanza kuwatuma wawili wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu”

 2. UNAPATA BARAKA.

Kuna baraka mara dufu, ukiwa katika kanisa kuliko ukiwa nyumbani

Zipo baraka ambazo Mungu anaziachia kwa Watoto wake kwa umoja.. na hizo zinaachiliwa kanisani…Na baraka hizo ni za kiroho na kimwili..

Mathayo 18:18 “Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.

19 Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.

20 Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao”.

Hapo Bwana Yesu hajasema.. “akikusanyika mmoja nyumbani kwake, atakuwa katikati yake”..sasa sio kwamba “kila unapokuwa peke yako Bwana anakuwa hayupo nawe” ..yupo na wewe lakini, si kama utakavyokuwa na wengine. Kwasababu Bwana siku zote anahubiri umoja na anapendezwa na umoja.. Lakini ukijitenga Bwana hawezi kupendezwa na wewe.

Mithal 18:1 “Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe; Hushindana na kila shauri jema”.

Hivyo mkatae leo shetani, na anza kwenda kukusanyika na wengine, hiyo ni kwa faida yako wewe, kumbuka siku zote kuwa shetani anafananisha na simba atafutaye mawindo..na anawawinda watu walioanza safari ya wokovu watu kwa njia nyingi, na ya kwanza ndio hiyo.. ya kuwatenda na kundi.

1 Petro 5:8 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

UTAWALA WA MIAKA 1000.

KUOTA NYOKA.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

NI KIPI KINAMZUIA MUNGU KUZUNGUMZA NA SISI?

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

SWALI 1: Je! Shetani anaweza kuumba, kama Mungu? Kama sio Mbona kipindi cha Farao, tunaona wale waganga waliweza kuleta vyura na nyoka, kama alivyofanya Musa. Je wale vyura aliwaumbaje, uhai alitolea wapi kama sio Mungu?


JIBU:  Bwana Yesu anasema; Shetani ni mwongo, na sio tu mwongo, bali ni Baba wa huo;

Yohana 8:44 “..wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo”.

Maana yake ni kwamba ufalme wake ameujenga juu ya misingi ya uongo. Alitumia uongo kumnyang’anya Adamu nafasi yake ya umiliki. Vivyo hivyo hadi sasa anatumia uongo kuwadanganya watu wasiutambue ukweli  wote kuhusu yeye.

Anataka kuwadanganya watu, wadhani kuwa yeye ana nguvu za kuweza kukaribiana hata na Mungu au anao uwezo wa kuumba kama Mungu. Lakini ukweli ni kwamba, shetani au kiumbe chochote kile hakiwezi kuumba hata sisimizi. Uwezo huo anao Mungu tu, peke yake.

Kama ni hivyo, ni nini alikifanya kipindi cha Farao?

Alichokifanya kipindi cha Farao, si kingine zaidi ya uongo. Kutokana na maarifa aliyokuwa nayo kipindi kile ambayo anayo hadi sasa, shetani anaweza kubaliki kitu fulani kionekane ni kitu kingine mbele tu ya macho ya watu, au hata kujibadilisha yeye, aonekane ni malaika wa kweli, kumbe ndani ni yeye Yule yule shetani..Biblia inatuambia uwezo huo anao..

2Wakorintho 11:14 “Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru”.

Hivyo tabia hiyo anayo.. kipindi kile hakuumba nyoka wenye pumzi ya uhai, kama nyoka wengine, au vyura wapya..bali alifanya kazi yake hiyo ya kubadilisha maumbile ya vitu mbele ya macho ya watu.. Kwa lugha ya sasa wanaita “kiini-macho” au “mazingaumbwe”, na ndio maana nyoka wa Musa, hakuwaona wale kama ni nyoka wenzake, wanaohitaji mapambano, bali aliona kama ni chakula tu, akala.

Ni sawa na mwanadamu ambaye amefikia maarifa ya kutoa ‘photocopy’ kitu orijino, Shetani naye hapo amepafikia.Lakini hana uwezo wa kutengeneza orijino.

Kama shetani angekuwa na uwezo wa kuumba chura, hata mbwa angeweza, hata ng’ombe pia angeweza, na  sokwe nao. Na matokeo yake dunia, ingejawa na vitu vilivyoumbwa na Mungu, na vilivyoumbwa na shetani, leo hii tungesikia wale nguruwe si wa Mungu bali ni wa shetani, usiwaguse. Lakini hadi sasa hakuna rekodi ya kitu chochote kilichoumbwa na shetani, zaidi sana rekodi aliyonayo ni kuumba uovu na uasi duniani.

Pia tazama..

1 Jehanamu ni wapi?
2 Nini kinatokea baada ya kifo?
3 Freemason ni nini?
4 Siku ya unyakuo itakuwaje?
5 Upendo ni nini, je kuna aina ngapi za upendo?
6 Je! umepokea Kweli Roho Mtakatifu?
7 Mauti ya pili ni nini?
8 Faida za maombi
9 Jinsi ya kusoma biblia.
10 Je! kuna aina ngapi za malaika?

SWALI 2 : Je! Jini au pepo ni roho tu au pia wana miili inayoonekana, kiasi kwamba tunaweza kuwashika? Kama ndivyo Mbona Bwana Yesu alisema.

Luka 24:39 “Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo”.

JIBU: Ni kweli sawasawa na maneno ya Bwana Yesu, hakuna jini au pepo, au kiumbe chochote cha rohoni, chenye mwili, na kikaweza kuishi hapa duniani kama sisi.. Hakuna.

Kumbuka, Bwana Yesu alisema..

Mathayo 12:43 “Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate.

44 Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa.

45 Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya”.

SWALI 2 : Je! Jini au pepo ni roho tu au pia wana miili inayoonekana, kiasi kwamba tunaweza kuwashika? Kama ndivyo Mbona Bwana Yesu alisema.

Maandiko hayo ni kutuonyesha kuwa, mapepo, hayana miili yao wenyewe ya kuishia hapa duniani, yanategemea watu,au wanyama,ili kutembea duniani, kama wakati ule yalivyomwomba Bwana yawaingie wale nguruwe. Lakini yenyewe kama yenyewe, hayawezi kusimama na kuwa kama wanadamu kutembea duniani.

Lakini Je! Wale wanaoshuhudia kwamba mapepo yanawatokewa, na pengine kuzuni nao, ni nini vile?

Mapepo yanaouwezo wa kujidhihirisha mbele ya mtu kwa taswira ya kitu fulani, aidha ya mtu, au kitu, kukutisha au kukufanya uogope,  (Mathayo 14:26), au kukutokea katika ndoto,au maono.. lakini zaidi ya hapo yasiweza,  kuendelea na kuchukua maumbile na kuwa kama mwanadamu mwingine na kuishi hapa duniani, kama vile kula, kunywa, kufanyabiashara, kuoa, au kuolewa n.k. huo uwezo hawana kwasababu hawana miili. Pepo haliwezi kuzaa na wewe.

Vinginevyo, shetani angeshajidhihirisha siku nyingi na kuwa mfalme wa dunia. Lakini mpaka sasa ni roho tu, na atabakia kuwa roho, mpaka atakapotupwa kwenye ziwa la moto na mapepo yake.

Lakini kumbuka ukiwa ni mtu wa kujishughulisha na mambo ya ushirikina, aidha wewe ni mganga, au mchawi, au ulishawahi kwenda huko, ukafanyiwa matambiko, au kufanyiwa mazindiko ya kipepo, au ukala vitu vyao, Huo nao ni mlango unaoongeza wigo mkubwa sana, wa shetani au mapepo yake, kujidhihirisha kwako, kwasababu umeingizwa katika mtandao wao wa kiroho, hivyo inakuwa rahisi sana kwao kujidhihirisha kwako, na pengine kuchukua umbile ya kitu chochote kukuletea madhara mwilini. Tofauti na mtu ambaye  yupo mbali na mambo hayo.

Hivyo dawa pekee, ya kumfukuza shetani na majini yake, yasikutokee tokee au yasikufuate fuate ni kumkabidhi Yesu maisha yako. Kwa kumaanisha kabisa kuacha maisha ya dhambi, na baada ya hapo, ukazingatia kusoma NENO..

Kwasababu kuokoka ni sehemu ya kwanza, ya kuwekwa huru.. Ili kuukamilisha uhuru wako ni lazima Neno la Mungu likae ndani yako kwa wingi ili uweze kumshinda kabisa kabisa shetani.

 Biblia inasema.

Yohana 8:32 “tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru”.

Bwana Yesu, alikuwa ni mtakatifu wa Mungu, ambaye hakutenda dhambi, lakini hilo halikumzuia shetani asimjie, na kuzungumza naye. Lakini utaona alimshinda kwa Neno la Mungu lililokuwa ndani yake, na si kitu kingine.

Vivyo hivyo na wewe, ikiwa tayari umeshaokoka, Jifunze sana Neno, ujue mamlaka, na haki uliyonayo katika Msalaba wa YESU KRISTO. Hiyo itakufanya usiishi maisha ya woga,wala wasiwasi wa nguvu zozote za giza, kwasababu utakuwa tayari umeshajua uwezo uliopewa jinsi ulivyo mkubwa kuliko wa ibilisi

Lakini ukiwa ni mkristo, mvivu, Neno husomi ujue kabisa shetani ataendelea kukusumbua tu, haijalishi utakuwa ni mwombaji kiasi gani.

Hivyo zingatia hayo mambo mawili.

  1. Wokovu
  2. Neno

Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari leo, kumpa Yesu maisha yako, ili akusamehe na kukupa wokovu, na kuyafukuza maroho yote machafu yaliyokuvamia. Basi uamuzi huo ni wa busara sana kwako, ambao hautakaa uujutie milele.

Hivyo fungua hapa, kwa mwongozo wa sala hiyo>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

Mjoli ni nani katika biblia?

Gombo ni nini?

WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.

Rudi nyumbani

Print this post

IJUE SIRI YA UTAUWA.

Maandiko yanasema..

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka SIRI YA UTAUWA NI KUU…”.

Utauwa, maana yake ni UUNGU!.. Hivyo maandiko yanaposema.. “Siri ya Utauwa ni kuu”..maana yake ni kwamba “Siri ya Uungu ni kuu (yaani ni pana sana na ya kipekee)”.

Na Uungu (Utauwa)..unaozungumziwa hapo ni “Uungu wa Mungu”. Maana yake yeye ni nani, yupoje, anaonekanaje, anatendaje kazi, n.k

Sasa Mtume Paulo, kwa neema za Mungu, alipewa kuijua sehemu ndogo ya Uungu wa Mungu..na pasipo mashaka yoyote ya ufunuo huo alioupokea, akaiandika hivi..

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka SIRI YA UTAUWA NI KUU. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.

Hebu tuviangalie kwa ufupi, hivyo vipengele 6 vya siri hiyo ya Uungu wa Mungu, ambavyo Mtume Paulo alifunuliwa kwa uweza wa Roho.

 1. MUNGU ALIDHIHIRISHWA KATIKA MWILI.

Sasa ni wakati gani Mungu alidhihirishwa katika Mwili?..bila shaka yoyote, ni kupitia Bwana Yesu Kristo.. kwahiyo kumbe Bwana Yesu alikuwa ni Mungu katika mwili?.. Hakika hiyo ilikuwa ni siri ya kipekee.. Kumbe yule aliyekuwa anazungumza na akina Petro, alikuwa ni Mungu mwenyewe, kumbe yule aliyekuwa anaongea na mafarisayo alikuwa ni Mungu mwenyewe, kumbe yule aliyepandishwa msalabani alikuwa ni Mungu mwenyewe!.. Hiyo ilikuwa ni Siri kubwa sana.

Mtume Yohana naye aliiona siri hiyo kwa sehemu na kusema..

Yohana 1:1 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu…..

14 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.”

Umeona?, Tito naye aliiona hiyo siri kwa sehemu katika ..Tito 2:13 “tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu” ..Na baadhi ya Mitume wa Bwana Yesu kama Tomaso, na  Manabii kama Isaya, walionyeshwa siri hiyo kwa sehemu. (Soma Yohana 20:28 na Isaya 9:6). Na zaidi sana Bwana mwenyewe, aliigusia siri hiyo katika Yohana 14:8-11.

 2. AKAJULIKANA KUWA NA HAKI KATIKA ROHO

Bila shaka hakuna mwingine aliyepata kibali, cha mambo ya rohoni kuliko Bwana Yesu, hakuna mtu aliyewahi kufanya miujiza mikubwa kuliko Bwana Yesu. Kwa mara ya kwanza pepo wameanza kutolewa kwa kukemewa na Bwana Yesu Kristo, Kwa mara ya kwanza wafu wanafufuliwa kwa kutamkiwa neno tu!, na idadi kubwa ya watu likuwa inaponywa kupitia jina lake..Hivyo katika roho hakuna mwingine aliyejulikana kuwa na Haki (yaani kupata kibali), kuliko Yesu.

 3. AKAONEKANA NA MALAIKA.

Ni wazi kuwa Malaika wanawaona watu wote, lakini hawawajui watu wote, Malaika wala shetani hawajui kilichopo ndani ya moyo wa wanadamu, siri hiyo ipo kwa Mungu tu!, na kwa mtu mwenyewe.

Vile vile Malaika hawajui sura ya mtu atakayezaliwa mwaka ujao..anayejua ni Mungu tu!.. Hivyo Malaika walikuwa hawamjua Masihi (ambaye ni Mungu katika mwili) atakuwaje kuwaje, na Zaidi sana walizijua sifa chache tu, lakini si zote..

Lakini siku ilipofika ya kuzaliwa kwake walimwona..na alipoishi na kuifanya kazi ya Mungu ndipo walimwelewa Zaidi.. Ndio likatimia hilo neno.. “akaonekana na Malaika”. Malaika wakamwona Mungu katika mwili.

 4. AKAHUBIRIWA KATIKA MATAIFA.

Ni nani mwingine aliyehubiriwa katika mataifa na anayehubiriwa sasa?.. bila shaka si mwingine Zaidi ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Marko 16:15 “Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe”.

 5. AKAAMINIWA KATIKA ULIMWENGU.

Yesu Kristo ndiye peke yake ndiye anayeongoza kwa kuaminiwa na watu wengi duniani kuliko mtu mwingine yoyote, dini karibia zote (za uongo na za ukweli) pamoja na shetani mwenyewe na mapepo yake wanaamini kuwa Yesu katumwa kutoka mbinguni. Dini hizo zinaweza zisimkiri wazi, lakini zinaamini kuwa Bwana Yesu katoka mbinguni.

Yohana 12:42 “Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi”.

Na zaidi sana siku ya Mwisho, kila goti litapigwa na kila ulimi utakiri, kuwa Yesu Kristo ni Bwana.

Wafilipi 2:10 “ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;

11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba”.

 6. AKACHUKULIWA JUU KATIKA UTUKUFU.

Yohana 3:13 “Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu”.

Kwa hoja hizi sita ni wazi kuwa Bwana Yesu ndiye siri ya Mungu, na ndiye Mungu mwenyewe aliyejidhihirisha katika mwili.

Sasa unaweza kuuliza kwanni Mtume Paulo auandike ufunuo huu kwetu, kwa uongozo wa Roho?.

Ni ili sisi tuzidi kuwa na Imani na Bwana Yesu, ili sisi tuzidi kumwamini, na kumtumainia?.. Je!, kwa kusikia kuwa Yesu ndiye Mungu, huoni inatuongezea Faraja sisi?, inatuongezea ujasiri na kuamini kuwa hakuna chochote kitakachoharibika, maadamu tunaye Mungu?..Hivyo Siri hiyo ni kwa faida yetu.

Lakini jukumu tulilonayo sisi, sio kusoma Habari hizi kama gazeti, bali kama Neno hai lenye kuleta mabadiliko ndani yetu.. Huu ni wakati wa kumwamini Bwana Yesu, na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu, na vile vile kujitenga na dunia, na kukusanyika Pamoja na watakatifu wengine, huku tukiingoja ile ahadi tuliyoahidiwa ya mbingu mpya na nchi mpya.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group


Mada Nyinginezo:

Ni SIRI gani Paulo aliyokuwa anaimaanisha katika Waefeso 5:32?

MPINGA-KRISTO

AKETIYE MAHALI PA SIRI PAKE ALIYE JUU.

Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri.

NG’OMBE MWEKUNDU ALIYEZALIWA ISRAELI, ANAFUNUA NINI?

Rudi nyumbani

Print this post

Kisiwa cha Patmo kipo nchi gani?.

Kisiwa cha Patmo kipo nchi ya Ugiriki kwa sasa…Kisiwa hicho kipo mashariki mwa Taifa la Ugiriki na magharibi mwa nchi ya Uturuki, kama vile Zanzibar ilivyo mshahariki mwa nchi ya Tanzania ndivyo kilivyo hichi kisiwa cha Patmo kwa Ugiriki.

Kisiwa hicho ndicho Mtume Yohana, ambaye alikuwa mwanafunzi wa Bwana Yesu, alifungwa.

Warumi walimkamata Yohana na kumtupa katika kisiwa hicho, kwa lengo la kumtesa kwa kosa la kumhubiri Yesu. (Kwa maelezo kwa njia ya sauti, fungua hapa chini)

[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=EhBLp-8-vPw[/embedyt]

Lengo la kumtupa Yohana katika kisiwa hicho cha Patmo, sio tu afe, bali afe kwa mateso. Kwani kisiwa hicho hakikukaliwa na mtu yeyote wakati huo, kwasababu kilikuwa ni kisiwa ambacho hakistawi nafaka, wala miti na zaidi sana, kilisifika kuwa na nyoka wengi.

Kwahiyo yoyote aliyetupwa katika kisiwa hicho, ilikuwa ni lazima afe kama hatakuja kuokolewa huko.

Lakini tunasoma, Yohana alipelekwa kule, kwaajili ya ushuhuda wa Neno la Mungu, wakati Jeshi la Warumi linaona limempeleka kwaajili ya mateso, yeye Yohana alijiona amepelekwa kwaajili ya ushuhuda…Kwamba akashuhudie mambo atakayokwenda kufunuliwa au kuambiwa na Mungu huko.

Ufunuo 1:9 “Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na subira ya Yesu Kristo, nalikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu”

Hii ikifunua kuwa sio kila jaribu baya, lengo lake ni baya!. Yohana asingepelekwa Patmo, tusingekuwa na kitabu cha ufunuo, hali kadhalika Bwana Yesu asingepelekwa msalabani, tusingepata wokovu.

Kisiwa cha Patmo, sasahivi kinakaliwa na watu, kutokana na kuongeza kwa idada kubwa ya watu ulimwengu na yenye kuhitaji makazi..vile vile, kuongezeka kwa teknolojia ya mawasiliano, na usafiriwa wa haraka, umekifanya kisiwa hicho kiweze kukalika na watu leo.

Kisiwa cha Patmo, jina lake mpaka leo halijabadilika, kinaitwa hivyo hivyo Patmo, kama vile Yerusalemu jina lake lisivyobadilika siku zote.

Wakazi wa kisiwa cha Patmo kwasasa hawazidi 4,000 kulingana na sensa za Ugiriki.

Na kisiwa hicho, hakina miujiza yoyote ya kiroho, kwamba yeyote afikaye kule basi atapata ufunuo kama aliopata Yohana.

Bwana akubariki.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Kutakabari ni nini katika biblia?.

Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?

Kwanini Yakobo na Yohana waliitwa “Wana wa Ngurumo”?

KWANINI KRISTO AFE?

Rudi nyumbani

Print this post

ALITOKA HUKO, AKAENDA MAHALI KARIBU NA JANGWA.

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, utukufu na heshima vina yeye milele na milele, amina. Karibu tuyatafakari maneno yake, maadamu siku zenyewe zimekaribia kuisha.

Ukisoma vitabu vya injili utaona jambo la kushangaza sana kuhusu Bwana Yesu. Utaona kuna wakati alikuwa anatembea kwa wazi kabisa katikati ya wayahudi, utalithibitisha hilo katika maneno yake mwenyewe aliyomwambia kuhani mkuu  katika Yohana 18:20, kupindi kifupi kabla ya kusulubiwa, Lakini kuna wakati hakutembea kwa wazi hata kidogo, bali alikwenda mbali na makazi ya watu, karibu na jangwa, akakaa huko yeye peke yake Pamoja na wanafunzi wake tu.

Yohana 11:53 “Basi tangu siku ile walifanya shauri la kumwua.

54 Kwa hiyo Yesu hakutembea tena kwa wazi katikati ya Wayahudi; bali alitoka huko, akaenda mahali karibu na jangwa, mpaka mji uitwao Efraimu; akakaa huko pamoja na wanafunzi wake”.

Unaweza ukajiuliza kwanini Bwana Yesu aonyeshe tabia kama hii? Ili hali alikuwa na uwezo wa kuishi analivyopenda Bila wasiwasi wowote, kwasababu Baba yake alikuwa Pamoja naye kumpigania na kumshindania asiuliwe kabla ya wakati?

Hiyo ni kutuonyesha kuwa, Kristo, hana utawala wa mabavu, ukimkataa, atakwenda mbali na wewe, na hutamwona haijalishi utamtafuta vipi. Ni jambo ambalo linaendelea sasa hivi katika roho ulimwenguni. Bwana Yesu anaulilia ulimwengu, lakini ulimwengu ndio kwanza unaipinga injili yake, unataka kuiua kabisa isiwaokoe watu.

Tukiona hivi tujue kabisa  Bwana ameshakwenda mbali na watu wa ulimwengu huu, kujificha. Siku hizi kupokea wokovu wa kweli ni ngumu kuliko ilivyokuwa zamani, kwasababu Kristo hapatikani tena kwa uwazi. Na ndio maana, utaona watu wengi wanasema wameokoka, lakini huoni nguvu za wokovu ndani yao..Si jambo la kawaida!!

Bwana huwa anajificha..

Yohana 12:36 “Maadamu mnayo nuru, iaminini nuru hiyo, ili mpate kuwa wana wa nuru. Hayo aliyasema Yesu, akaenda zake, akajificha wasimwone“.

Ukirudi katika maandiko, utaona tena, alipokuwa Galiliya, alipita katikati yao lakini hakutana mtu yeyote ajue kuwa yupo mjini, bali alipita kimya kimya, akawa anawafundisha wanafunzi wake tu.

Marko 9:30 “Wakatoka huko, wakapita katikati ya Galilaya; naye hakutaka mtu kujua.

31 Kwa sababu alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake, akawaambia, …”.

Hata sasa, Yesu anachofanya ni kujidhihirisha kwa watu ambao ni wanafunzi wake tu, usipofanyika mwanafunzi wa Yesu siku hizi za mwisho ni ngumu kuushinda ulimwengu. Mwanafunzi kulingana na (Luka 14:33), ni mtu ambaye amejikana nafsi na kudhamiria kweli kweli kumfuata Yesu.

Ukiwa tutakuwa na wokovu wa midomoni tu, na kusema tumeokoka, Na huku Maisha yetu yapo mbali na Kristo, tusijidanganye, bado hatujakutana na Bwana Yesu. Bali tumemsikia tu kwamba yupo.

Ndugu yangu hizi ni siku za mwisho, Bwana yupo kweli duniani anaokoa watu..Lakini si wote, anawatembelea watu, bali walio wanafunzi kwelikweli. Kuiona miujiza ya Yesu, kusikia injili, kwenda kanisani hakukufanyi uwe umeshamwona Yesu..Hivyo tuitambue tabii hii pia ya Bwana Yesu ili tuepukane na kujificha kwake, kwasababu anafanya hivyo sasa katika roho.

Kama hujaokoka, au ulikuwa unaishi Maisha ya uvuguvugu, yaani Maisha nusu nusu kwa Mungu basi fanya uamuzi wa kumgeukia sasa kwa  moyo wako wote, huku umejikana nafsi yako. Na Bwana Yesu atajidhihirisha kwako. Na atakusaidia kuushinda ulimwengu na kuishi Maisha ya utakatifu.

Ubarikiwe.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

FANYA KAMA UONAVYO VEMA.

KUNA WAKATI YESU ATAPITA NA WATU HAWATAJUA.

UVUVI BORA HAUCHAGUI, CHA KUVUA.

Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?

Kigao ni nini? Na Je kinafunua nini kwa agano jipya?

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Je mwanamke Fibi, alikuwa ni askofu wa makanisa, kama mitume?

SWALI: Je mwanamke Fibi, alikuwa ni askofu wa makanisa, kama mitume? Kulingana na (Warumi 16:1)

Warumi 16:1

16:1 “Namkabidhi kwenu Fibi, ndugu yetu, aliye mhudumu wa kanisa lililoko Kenkrea;

2 kwamba mmpokee katika Bwana, kama iwapasavyo watakatifu; mkamsaidie katika neno lo lote atakalohitaji kwenu; kwa sababu yeye naye amekuwa msaidizi wa watu wengi, akanisaidia mimi pia”.


JIBU: Fibi hakuwa askofu wa makanisa, wala maandiko hayasemi hivyo, bali alikuwa ni “Mhudumu”..Yaani alikuwa akilihudumia kanisa la Kristo lililokuwa Kenkrea. Ni mwanamke aliyekuwa akilijali sana kanisa kwa kuwasaidia watu wengi, ikiwemo na mtume Paulo pia. Pengine kwa mali zake, kama walivyofanya wakina Yoana na Susana, waliomuhudumia Bwana kwa mali zako (Luka 8:3), au alivyokuwa Martha na Miriamu jinsi walivyompenda Bwana na kujitaabisha kwa ajili yake..

Au kama alivyokuwa Dorkasi, ambaye, kanisa zima lililokuwa Yafa lilimshuhudia, jinsi alivyotoa sadaka nyingi na kuwashonea watakatifu mavazi. Ndivyo ilivyokuwa pia kwa huyu mwanamke ambaye aliitwa Fibi. Pengine alikuwa anawakaribisha watakatifu na kuwapa makao nyumbani kwake, au alikuwa anachapisha injili za mitume na kuyasambazia makanisa yaliyokuwa Kenkrea.

Kwa ufupi ni kwamba Fibi likuwa ni muhudumu kweli kweli kwa Bwana, kiasi cha kuwafanya mitume wampe heshima ya kipekee katika kanisa.

Lakini hiyo haimaanishi kuwa yeye naye alikuwa ni Askofu (Mwangalizi), wa makanisa kama mitume. Hapana andiko limeweka wazi kabisa kuwa mwanamke hana uongozi wowote katika kanisa. Ni kinyume na utaratibu wa Mungu.

1Timotheo 2:11 “Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.

12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu.

13 Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye.

14 Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa”.

Lakini tunajifunza nini kwa Fibi?

Hii ni kuonesha jinsi gani mwanamke anaweza kumtumikia Bwana katika nafasi yake, na akawa na heshima kubwa katika kanisa la Kristo, mfano wa Fibi. Ni vizuri wewe kama mwanamke uifahamu nafasi yako, katika mwili wa Kristo, kisha simama katika hiyo, watazame kwanza wanawake wenzako katika biblia jinsi walivyoenenda, na jinsi walivyokuwa wanamtumikia Mungu na wewe waige, kabla hujakwenda kuwatazama kwanza mitume wanaume.

Hiyo ni muhimu sana kufahamu hilo, usije ukawa unapiga mbio bure, halafu baadaye unapokea thawabu isiyolingana na juhudi yako.

Ikiwa wewe ni mwanamke na utapenda kupata mafundisho ya namna hiyo yanayohusiana na huduma za wanawake katika kanisa, basi nitafute inbox kwa namba hizi +255693036618, nikutumie mafundisho hayo, au fungua link hii utakutana nayo, moja kwa moja >>>  https://wingulamashahidi.org/2021/07/21/masomo-maalumu-kwa-wanawake/

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

NI KITU GANI TUNAJIFUNZA KWA RISPA, BINTI AYA?

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

MAMA UNALILIA NINI?

Unyenyekevu ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

KABILA LA BENYAMINI.

Jina la Bwana na mwokozi wetu Yesu, Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia..

Katika wana wa Yakobo, aliyekuwa mdogo kiumri kuliko wote alikuwa ni Benyamini, ambaye alikuwa ni mdogo wake Yusufu. Huyu Benyamini ndiye mtoto pekee wa Yakobo ambaye hakupata kumfaidi mama yake mzazi, hata kunyonya kutoka kwa mama yake, hakunyonya kabisa..kwani siku ile anazaliwa tu!, ndipo na mama yake anakata roho.

Na siku anazaliwa mama yake alimwite “Benoni” maana yake “mwana wa uchungu wangu”..lakini baba yake alimbadilisha hilo jina na kumwita “Benyamini” maana yake “mwana wa mkono wangu wa kuume” (Kutoka 35:16-20).

Kabila la Benyamini, wakati linaingia katika nchi ya ahadi, ndilo lililokuwa kabila lenye watu wachache kuliko yote.

Na Zaidi ya yote, baada ya kuingia katika nchi ya ahadi, maandiko yanaonesha kuwa kuna kipindi wabenyamini wengi waliuawa..wakabaki watu mia sita tu! (600). Na waliuawa kutokana na kosa la kumtendea ukatili yule Suri wa Mlawi, wa Bethlehemu-Yuda.

Kosa lile liligharimu Maisha ya wabenyamini wengi sana wakike na wakiume na watoto..na kama sio hekima ya Mungu kuingilia kati, basi kabila hili lingetoweka kabisa..Kwani waliosalia walikuwa ni wanaume 600 tu, katika kabila lote..na wengine wote walikufa..

Wakati makabila mengine kama Yuda yalikuwa na watu Zaidi ya milioni moja..kabila la Benyamini lilibakiwa na watu 600 tu!..(tena ni wanaume tu!, wanawake wote walikufa) na Zaidi ya yote bado ndio kabila dogo kuliko yote, kwani baba yao Benyamini ndiye aliyekuwa mdogo kuliko wote katika wa nawa Yakobo.

Waamuzi 21:17 “Wakasema, Lazima kuwa urithi kwa hao wa Benyamini waliopona, isiwe kabila kufutika katika Israeli”.

Hivyo lilikuwa ni kabila la kudharaulika kuliko yote!.. siku zote Wabenyamini hawakuwa watu wa heshima sana, ukilinganisha na makabila mengine kama Lawi, au Yuda au Efrahimu.

Lakini ijapokuwa ndio lilikuwa kabila dogo kuliko yote, na lenye watu wachache kuliko yote, na lililodharaulika kuliko yote, machoni pa watu.. lakini jicho la Mungu ni tofauti na la wanadamu, kwasababu Mungu haangalii kama wanadamu.

Ilipofika kipindi ambacho Israeli wanataka Mfalme wa kuwatawala mfano wa mataifa mengine yote, walikutana na jambo kinyume na mategemeo yao.

Wakati wanadhani kuwa pengine Mungu angemchagua mtu Fulani mashuhuri kutoka katika kabila mojawapo kubwa kubwa, tena lenye heshima.. kinyume chake, alimchagua mtu kutoka katika lile kabila dogo kuliko yote, tena katika ile familia ndogo kabisa.. Kinyume na matarajio yao. Na mtu huyo hakuwa mwingine Zaidi ya Mfalme Sauli.

1Samweli 9:21 “Basi Sauli akajibu, akasema, JE! MIMI SI MBENYAMINI, MTU WA KABILA ILIYO NDOGO KULIKO KABILA ZOTE ZA ISRAELI? NA JAMAA YANGU NAYO SI NDOGO KULIKO JAMAA ZOTE ZA KABILA YA BENYAMINI? kwa nini basi, kuniambia hivyo?”.

Sauli aliwatawala Israeli kwa muda miaka 40, sawasawa kabisa na alivyotawala Daudi na Sulemani.. Ijapokuwa Sauli alikuwa na kasoro kasoro nyingi, lakini Bwana alimchagua kuliongoza taifa lake takatifu kwa wakati huo.

Ni nini tunajifunza kwa kabila hili?

Tunachoweza kujifunza ni kuwa jicho la Mungu si la mwanadamu.. Yule ambaye anaonekana si kitu mbele za watu leo, yule anayeonekana kuwa hafai.. Mungu anaweza kumnyanyua kutoka mavumbini na kumpandisha juu.. Hivyo kwa vyovyote hatupaswi kujidharau, wala kuwadharau wengine.. wala tusiziogope dharau kwasababu jicho la Mungu ni tofauti na la wanadamu.

1Wakorintho 1:26 “Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa;

27 bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;

28 tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko;

29 mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu”.

Bwana alilinyanyua kabila la Benyamini, anaweza kufanya kwako au kwa mwingine yeyote.. Mwamini Mungu, wala usijidharau.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Bwana Yesu alikuwa kabila gani?

Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?

Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?

Amri zilizo ndogo alizozizungumzia Yesu ni zipi?

NA ABARIKIWE KILA AKUBARIKIYE, NA ALAANIWE KILA AKULAANIYE.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana Yesu alivikwa taji ya miiba?

Taji ya miiba juu ya kichwa cha Bwana Yesu, iliashiria nini kiroho?..

Tusome,

Mathayo 27:27 “Ndipo askari wa liwali wakamchukua Yesu ndani ya Praitorio, wakamkusanyikia kikosi kizima.

28 WAKAMVUA NGUO, WAKAMVIKA VAZI JEKUNDU.

29 WAKASOKOTA TAJI YA MIIBA, WAKAIWEKA JUU YA KICHWA CHAKE, NA MWANZI KATIKA MKONO WAKE WA KUUME; WAKAPIGA MAGOTI MBELE YAKE, WAKAMDHIHAKI, WAKISEMA, SALAMU, MFALME WA WAYAHUDI!

30 Kisha wakamtemea mate, wakautwaa ule mwanzi, wakampiga-piga kichwani.

31 Walipokwisha kumdhihaki, wakalivua lile vazi, wakamvika mavazi yake, wakamchukua kumsulibisha”.

Kumbuka Pilato alipomuuliza Bwana Yesu kama yeye ni mfalme wa Wayahudi, Bwana hakukanusha… alimwambia “wewe wasema” maana yake “mimi ndiye”.

Hivyo wale Askari waliposikia Bwana Yesu kakiri kuwa ndiye  mfalme wa wayahudi, walicheka sana.. na kwasababu askari wa kirumi walikuwa wanawadharau wayahudi.. Hivyo ili kuwadhalilisha wayahudi.. ndio wakamvua zile nguo za thamani Bwana Yesu na kumvika vazi la jekundu, na kisha kumpa mwanzi (yaani fimbo)..na kumvika taji ya miiba…na mwisho kuinama kama vile wanamsujudia..

Lengo la kufanya vile ni kumweka katika mazingira kama ya kifalme… kwasababu kikawaida Mfalme anakuwa anavaa mavazi mekundu, pia anakuwa ameshika/anatembea na mwanzi wa thamani, na vile vile kichwani anakuwa na taji la thamani sana.. Lakini kwasababu hawa askari lengo lao lilikuwa ni kufanya dhihaka kwa wayahudi…ndio wakafanya hayo kwa Bwana Yesu, ili aonekane kama mfalme lakini asiye na utukufu, ambaye asiyejielewa.

Lakini walifanya vile kwa lengo la kufanya dhihaka tu!, (na kuwadhalilisha wayahudi) na si vinginevyo!…Na walifanya hivyo kwasababu hawakumjua yeye ni nani?.. kwasababu laiti kama wangemjua kuwa huyo wanayemfanyia dhihaka ndiye Mfalme wa kweli wa mbinguni na duniani, na pia ni Mungu mwenyewe katika mwili, wasingelimsulubisha zaidi ya yote wangemwabudu.

1Wakorintho 2:7 “bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu;

8 ambayo wenye kuitawala dunia hii HAWAIJUI HATA MMOJA; MAANA KAMA WANGALIIJUA, WASINGALIMSULIBISHA BWANA WA UTUKUFU”.

Sasa swali ni kwanini Bwana Yesu asingezuia hayo yatokee na ilihali alikuwa na uwezo huo?

Sababu zipo kuu (2).

 1. ILI SISI TUPATE WOKOVU.

Bwana Yesu asingelisulubiwa maana yake sisi tusingelipata wokovu…

 2. ILI AINULIWE JUU.

Bwana Yesu mwenyewe alisema… ajikwezaye atashushwa, naye ajishushaye atakwezwa.. Maana yake siri ya kuinuliwa juu, wakati mwingine ni kujishusha…Ili uwe mkubwa kuliko wote sharti uwe mdogo kuliko wote, ili upate heshima kuliko wote, sharti ukubali kukosa heshima kuliko wote, hiyo  ni kanuni kubwa sana, ambayo Bwana Yesu aliijua..

Alifahamu kuwa ili anyanyuliwe juu kuliko vitu vyote, hana budi kukubali kuonekana si kitu sasa.

Wafilipi 2:5 “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;

6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba”.

3. KUTUPA SISI KIELELEZO.

Sababu ya mwisho ni ili kutufundisha sisi kuwa wema, kama yeye!… kama yeye mwenyewe alivyosema.. “mtu akupigaye shavu hili mgeuzie na la pili” au mtu akulazimishaye mwendo wa maili moja, nenda naye mbili..Kwasababu kwa kufanya hivyo, ataiona haki yako na mwisho atavutiwa na imani yako, na hata kumbadilisha kabisa… (Umeona askari hao hao waliomfanyia dhihaka, masaa machache tu mbele walikiri kuwa yeye kweli alikuwa Mwana wa Mungu, Marko 15:39).

Na sisi hatuna budi kuwa kama Bwana Yesu, tunapotukanwa tunapaswa tustahimili, tunapoudhiwa na kudhalilishwa tunapaswa tustahimili kama Bwana Yesu, kwasababu mwisho wake ni mzuri..

1Petro 2:19 “Maana huu ndio wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo isivyo haki.

20 Kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu.

21 Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.

22 Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake.

23 Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakuogofya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki.

24 Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa.

25 Kwa maana mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu”.

Waebrania 12:3 “Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu.

4 Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

MJUE SANA YESU KRISTO.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

Kwanini hatuirithi neema kama tunavyoirithi dhambi?

Rudi nyumbani

Print this post

UNAVYOZIDI KUWA MWENYE HAKI, NDIVYO KUJITAMBUA KWAKO KUNAVYOPUNGUA.

Tofauti na tunavyoweza kudhani, kwamba pale unapoongezeka viwango vya kiroho, Au pale unapopiga hatua moja kwenda nyingine kwa Mungu  basi utajitambua, au utapata hisia Fulani ya kitofauti kwamba amehama ulimwengu mmoja na kwenda mwingine, au utahisi nguvu Fulani zimeongezeka ndani yako, Lakini sivyo. Ni ngumu sana kujitambua wewe mwenyewe..Bali mwingine ndiye atakayekutambua.

Tunamwaona Musa aliposhuka kutoka mlimani kuzungumza na Mungu kwa muda wa siku 40, usiku na mchana, hakujua kama lipo badiliko lolote, limetokea katika uso wake.

Lakini aliposhuka tu, mlimani wana wa Israeli ndio waliokuwa wa kwanza kumtambua na kumfunulia siri ambayo hakuijua kwa muda siku zote arobaini alizokuwa anamkaribia Bwana..

Kutoka 34:29 “Hata ikawa, Musa aliposhuka katika mlima Sinai, na zile mbao mbili za ushuhuda zilikuwa mkononi mwa Musa, hapo aliposhuka katika mlima, Musa hakujua ya kuwa ngozi ya uso wake iling’aa kwa sababu amesema naye.

30 Basi Haruni na wana wote wa Israeli walipomwona Musa, tazama, ngozi ya uso wake iling’aa; nao wakaogopa kumkaribia.

31 Musa akawaita; Haruni na wakuu wote wa kusanyiko wakarudi kwake; Musa akasema nao.

32 Baadaye wana wa Israeli wote wakakaribia; akawausia maneno yote ambayo Bwana amemwambia katika mlima Sinai”.

Hii ni kutukumbusha, Mtu uliyeokoka, ukiongeza ukaribu wako kwa Mungu, kwa hatua nyingine, ni ngumu sana kuona kama utukufu wako umeongezeka  ndani yako kwa hatua moja zaidi..Mfano unapoongeza kiwango chako cha maombi, utajiona wewe ni yule yule tu, kama ulivyokuwa juzi..Lakini tayari utukufu wako umeongezeka kwa ngazi moja juu Zaidi, isiyoijua au kuihisi wewe.

Unaposema, embu ngoja nianze kujizoesha kwenda mikesha kanisani kila ijumaa, unaweza kujiona upo vilevile tu, lakini ipo hatua kubwa sana umepiga.. Ukitaka kufahamu kuwa umepiga hatua, embu sema sikumoja niache kwenda mikesha, halafu uone, huo ukame utakaouhisi ndani ya nafsi yako, utakavyokuwa.

Unapojilinda kila siku na dhambi, ya uasherati, matusi, wizi, n.k. ni rahisi kutohisi ongezeko lolote, ndani yako, lakini fahamu kuwa utukufu wako umeongezeka sana, wale wa nje ndio watakaokuja kushuhudia, Pamoja na Mungu mwenyewe. Watu wengi wanaishiwa na nguvu njiani, kwasababu wanaona kama bidii wanayoizidisha kwa Mungu, haiwarejeshei, badiliko kubwa ndani yao, kama wanavyotarajia.

Kumbuka huwezi kuuona uso wako..Ndivyo ilivyo nasi katika roho, hatuwezi kujiona wenyewe ndani yetu jinsi tunavyokuwa kiroho..Lakini walio nje ndio watakaotuona, hata kama hawatosema.

Ufalme wa Mungu ni kama mbegu, inayotupwa katika Shamba, ambayo biblia inasema, inakua kwa jinsi asivyojua mtu, Lakini mwisho wa siku ghafla tu, inatoa yenyewe matunda

Marko 4:26 “Akasema, Ufalme wa Mungu, mfano wake ni kama mtu aliyemwaga mbegu juu ya nchi;

27 akawa akilala na kuondoka, usiku na mchana, nayo mbegu ikamea na kukua, asivyojua yeye.

28 Maana nchi huzaa yenyewe; kwanza jani, tena suke, kisha ngano pevu katika suke.

29 Hata matunda yakiiva, mara atapeleka mundu, kwa kuwa mavuno yamefika”.

Hivyo, usihangaike sana, kujichunguza chunguza, kwasababu hutaona lolote. Lakini fahamu kuwa kila hatua unayoiongeza kwa Mungu, ina utukufu mkubwa sana kwako. Ndugu Usipunguze maombi, hata kama huoni chochote, usipunguze kushuhudia wengine Habari njema, usipunguze kumtolea Mungu kwa mali zako, hata kama huoni marejesho yoyote kutoka kwake, usipunguze kwenda ibadani na kuhudhuria mikesha. Kinyume chake ndio uzidishe, kuyatenda hayo.

Mwisho wa siku utukufu wako utaangaza sana kama ilivyokuwa kwa mtumishi wa Mungu Musa, hadi wengine watakuogopa kwa jinsi ulivyomkaribia Mungu sana.

Ubarikiwe na Bwana.

Tafadhali shea na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi// Ushauri/ Maswali/Whatsapp.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.

TUTAWEZAJE KUMZALIA MUNGU MATUNDA?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Tarshishi ni mji gani kwasasa?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana Yesu alisema “Msimwamkie mtu njiani”?

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema, msimwamkie mtu njiani? (Luka 10:4).. Na wakati huo huo alisema katika Mathayo 5:47, kuwa “tukiwaamkia ndugu zetu tu!, tunatenda tendo gani la ziada”.

Jibu: Labda tuanzie kusoma kuanzia mstari wa kwanza…

Luka 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.

2 Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake.

3 Enendeni, angalieni, nawatuma kama wana kondoo kati ya mbwa-mwitu.

4 Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; WALA MSIMWAMKIE MTU NJIANI”.

Mwalimu anapotoa tangazo kwa wanafunzi wake na kuwaambia… “si ruhusa kuzungumza na mtu yeyote ndani ya chumba cha mtihani”.. Kwa kusema hivyo hajamaanisha kuwa “si ruhusa kuzungumza na mtu kila mahali” Hapana!.. bali ni katika chumba cha mtihani tu!..wakiwa mahali pengine wanaweza kuzungumza..

Na kadhalika Bwana hakuwakataza wanafunzi wake “kuwaamkia/kuwasalimia watu kabisa”..hapana!..bali wanapokuwepo katika “Safari ya uinjilisti” hapo ndipo “Alipowazuia wasiamkie amkie watu njiani”.

Sasa kwanini awazuie kufanya hivyo, wakiwa katika safari ya kwenda kuhubiri?

Ni kwasababu salamu zinacheleweza lile kusudi, na ni rahisi kumhamisha mtu kifikra kutoka katika mawazo ya kwenda kuhubiri mpaka kuanza kufikiri mambo mengine tofauti na yanayohusu injili anayokwenda kuhubiri..

Hebu tengeneza picha Mwanafunzi mmojawapo wa Bwana Yesu, anakwenda kuhubiri, halafu njiani anapita karibu na nyumba ya Mjomba wake..halafu anaingia kumsalimia, na katika mazungumzo anapewa taarifa mbalimbali aidha za misiba, au za watu wengine au nyingine zozote..

Au anapewa jukumu lingine la kufanya huko anakokwenda, labda anaambiwa ukifika mahali fulani naomba uninunulie kitu fulani, ukirudi nipitishie hapa, au ukifika mahali fulani nisiaidie kuulizia hili au lile, au ukifika sehemu Fulani kumbuka kumsalimia mtu Fulani, au huko unakokwenda kuwa makini nako kuna hatari n.k..

Ni wazi kuwa kuanzia huo wakati na kuendelea mawazo ya yule mwanafunzi yatakuwa yametawaliwa na yale aliyoyasikia kutoka kwa ndugu yake huyo, na yale ya injili yatakuwa yamemezwa…

Kwahiyo ili kulizuilia hilo.. ndipo Bwana akasema… “Msiwaamkie watu njiani”.. ili mawazo yao na akili zao ziwe katika Injili wanayokwenda kuihubiri..

Lakini watakapomaliza safari yao hiyo ya injili wapo huru kuwaamkia watu wowote pasipo kupendelea sawasawa na Neno hilo la Bwana katika Mathayo 5:47

Kadhalika na sisi, tunapokuwa katika uinjilisti, hatupaswi kuuchanganya na mambo mengine, tunapokuwa katika kuifanya kazi ya Mungu, hatuna budi akili zetu, mawazo yetu, kuyafunga yasiingiliwe na mawazo mengine.. (kadhalika tunapokuwa katika ibada ni sharti kuzima simu, ili kuongeza umakini katika kuomba, kusifu na kusikiliza Neno).

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

BADO TUTAHITAJI TU KUSAIDIANA.

UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

Rudi nyumbani

Print this post