Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?

Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?

SWALI: Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda na sio kwenye koo nyingine kama vile  Yusufu?


JIBU: Hatma ya yale makabila 12, na tabia zao tunaona kwa mara ya kwanza zikifunuliwa na Yakobo Baba yao siku ile alipokuwa anakaribia kufa, alipowaita na kuwabariki. ukisoma pale utaona kila mtoto alinenewa habari zake. Kwasasa hatuwezi kuziandika zote hapa lakini kwa muda wako soma Mwanzo 49:1-28. Utaona.

Sasa,  kulingana na tabiri zile ni kabila moja  la Yuda, ndio lilibeba, vimelea vikuu sana, vimstahili Kristo.

Kwamfano pale makabila hayo yalipofananishwa na Wanyama, utaona Ni Yuda peke yake ndiye aliyefananishwa na SIMBA. Wakati wengine kama vile Naflati lilifananishwa na Ayala, Isakari  kama na Punda, Dani kama na nyoka aumaye, Benyamini kama mbwa-mwitu mkali. Yusufu kama mti mchanga uzaao. Lakini Yuda ni kama SIMBA .

Na sikuzote simba anajulikana kama ni mfalme wa pori, tena jasiri.

Mwanzo 49:8 “Yuda, ndugu zako watakusifu, Mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako. Wana wa baba yako watakuinamia.

9 Yuda ni mwana-simba, Kutoka katika mawindo, mwanangu, umepanda; Aliinama akajilaza kama simba, Na kama simba mke; ni nani atakaye mwamsha?

10 Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda, Wala mfanya sheria kati ya miguu yake, Hata atakapokuja Yeye, mwenye milki, Ambaye mataifa watamtii.

11 Atafunga punda wake katika mzabibu, Na mwana-punda wake katika mzabibu mzuri. Amefua nguo zake kwa mvinyo, Na mavazi yake kwa damu ya zabibu.

12 Macho yake yatakuwa mekundu kwa mvinyo, Na meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa”.

Vilevile kama tunavyosoma utabiri wake, utaona anaambiwa, FIMBO YA ENZI, haitaondoka kwake, ikimaanisha  kuwa fimbo ya kifalme, itakuwa katika uzao wake daima. Yaani kabila hili la Yuda litakuwa ni kabila la kifalme.

Mambo ambayo yanabeba kabisa tabia zote za masihi atakayekuja. Kwamba ni lazima AWE simba, jasiri, mwenye nguvu, na hodari.. Na ndio maana hatushangai kwanini  Bwana Yesu alijiita Simba wa Yuda (Ufunuo 5:5).

Vilevile ni lazima awe Mfalme mkuu sana mwenye nguvu sawasawa na unabii wa (Isaya 9:6). Hivyo kabila lenye enzi za kifalme lilikuwa ni hili na tunathibitisha hilo tangu enzi wa Daudi.

Hivyo hiyo ndio sababu kwanini Bwana Yesu hakutokea kabila lingine lolote Zaidi ya kabila la Yuda, Kwasababu, ilimpasa awe juu ya yote..Lakini kama angetokea kabila ya Yusufu ambalo limetajwa kama kabila lenye mafanikio makubwa, ni wazi kuwa kusingekuwa na vimelea vyovyote vya kifalme kwake.. Jambo ambalo haliwezekani kwa Kristo. Yeye ni lazima awe juu, atawale kama Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana. Hivyo ni lazima tabia hizo zianze kuonekana tokea mbali sana, kwenye vizazi vya vya nyuma, hadi kumfikia yeye.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Makanwa ni nini katika biblia? (Danieli 6:22)

FUNGUO WALIZOKUWA NAZO MABINTI WATANO WA SELOFEHADI!

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments