JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Fahamu jinsi ya kusoma biblia.


Awali ya yote ninakupongeza kwa nia yako kutamani kujua jinsi ya kusoma biblia. Hapo mwanzoni kabla sijamjua vizuri Mungu, kati ya  vitabu ambavyo nilikuwa ninaona ni vigumu kuvielewa, basi kimojawapo kilikuwa ni BIBLIA.

Lakini siku, na miaka ilivyozidi kwenda niligundua kuwa sio, nataka nikuambie hakuna kitabu kilicho kirahisi kama Biblia. Kwanini ninakuambia hivyo?.. Kwasababu ni kitabu kinachoweza kusomwa na watu wa makundi yote.  Mzee anaweza kukisoma, kijana anaweza kukisoma, asiye na elimu anaweza kukisoma mwenye PH.D anaweza kukisoma..Na wote wakafaidika na kilichoandikwa mule. Vilevile hakina ngazi yoyote ya awali kukipitia ndio uelewe kama vilivyo vitabu vingine. Leo hii ukihitaji kusoma kitabu cha Fizikia, itakugharimu kwanza upitie elimu za chini uwe na msingi, vinginevyo hutaweza kukielewa..Lakini biblia haina misingi hiyo.

Tena na cha kushangaza Zaidi ni kwamba, biblia imetoa nafasi ya kueleweka na watu wasio na elimu kuliko wenye hekima na ujuzi..(Luka 10:21)

Jinsi ya kusoma biblia.

Mambo ya kuzingatia kabla hujaanza kusoma biblia.

  • Kwanza: Omba Kabla hujaanza kusoma Habari yoyote, hata kama unaifahamu, mshirikishe kwanza Roho Mtakatifu, na mwombe msaada akusaidie kuyaelewa maandiko. Siri moja ya maandiko ni kuwa Habari ile ile inaweza ikawa na mafunuo mengi sana..Hivyo usipokuwa mnyenyekevu na kujiona kwamba Habari Fulani unaijua, nakuambia utabakia kuwa hivyo hivyo. Lakini ukimwomba kwanza Roho Mtakatifu akufunulie, maandiko basi utashangaa mambo mengi sana ambayo hukuwahi hata kuyafikiria.
  • Pili: Hakikisha upo katika utulivu wa kutosha. Mahali palipo na machafuko siku zote hata akili haiwezi kukaa katika utulivu wa kuzingatia kile kinachosomwa, na hivyo Roho Mtakatifu anakosa wigo wa kukufunulia, yale anayotaka kukufunulia. Hivyo kama upo kwenye makelele basi, subiri uwe katika utulivu, tenga muda wako, hususani usiku ni muda mzuri Zaidi.
  • Tatu: Tafakari Neno, Kumbuka Neno la Mungu halisomwi kama gazeti tu, Chukua muda mrefu kuyatafari maandiko Zaidi ya kuyasoma, ikiwa na maana mtu yule anayeitafakari sura moja vizuri, ni Zaidi na mtu yule atakayesoma kitabu kizima bila kutafakari chochote kilichoandikwa. Roho Mtakatifu anazungumza kwa kasi sana, pale mtu anapojibiisha kuitafakari Habari husika.
  • Nne: Endelea kutumia muda mwingi, katika kutafakari hilo Neno, kwa jinsi unavyokaa sana katika uwepo huo ndivyo unavyompa Roho Mtakatifu wigo wa kukufunulia maandiko katika uelewa mzuri zaidi. Mpaka dakika ya mwisho unamaliza, unatoka kitu ambacho hapo kabla hukuwahi kukijua, tena moyo wako ukiwa na amani ya kutosha.
  • Tano: Kuwa na daftari na kalamu. Hiyo itakusaidia kuandika kile Mungu anachokufundisha, kwa kumbukumbu la baada usije ukasahau, Kumbuka mwanafunzi mzuri ni yule anaandika chini kile mwalimu wake anachomfundisha, kila anapomfundisha. Hivyo na wewe hakikisha unakuwa na daftari lako.

Hivyo ukizingatia hizo hatua, utakuwa umeshajua jinsi ya kusoma biblia. Pia kumbuka, kwenye suala la kitabu kipi uanzane nacho, au kipi usianzane nacho, hilo halina umuhimu sana, unaweza kuanza na kitabu chochote kile na  huko huko Roho Mtakatifu mwenyewe atakufunulia mambo ya ajabu, Na kukufikisha pale anapotaka ufike kwa siku hiyo, kwasababu hiyo ndio kazi yake aliikusudia juu yetu.

Yohana 16:13  “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake”.

Jinsi ya kusoma biblia.

Pia Kujifunza biblia ni Pamoja na kusikiliza na mafundisho mengine ya Neno la Mungu yanayohubiriwa.. Yale yanakuwa kama TUTION kwako. Hivyo hapa pia yapo mafundisho mengi ya kukusaidia kuielewa biblia, kwenye website hii yapo mafundisho Zaidi ya 1000 ya mada mbalimbali, na Maswali na Majibu mengi sana, ambayo ukiyasoma naamini utapiga hatua kubwa sana katika kuielewa biblia..Hivyo kama upo tayari bofya hapa uende moja kwa moja katika orodha hiyo….>> MAFUNDISHO

                                                                                >> MASWALI NA MAJIBU

Bwana akubariki sana.

Jinsi ya kusoma biblia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au tutumie ujumbe kwa namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mihimili mikuu (4) ya mkristo katika safari yake ya wokovu.

USIPOLITENDEA KAZI NENO LA MUNGU.

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

KABLA YA MAANGAMIZI, KRISTO HUWA ANAONYESHA KWANZA NJIA YA KUTOROKEA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
9 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Thomas
Thomas
1 year ago

Naupenda sanaa ukurasa huu kuhusu kusoma bibilia

Thomas
Thomas
1 year ago

Asanteni sanaa kwa kunijuza habari ya kusoma bibilia, Mungu awabariki

Erastus nanjala
Erastus nanjala
2 years ago

Ningependa unitumie kwa fb

Anod msalege
Anod msalege
2 years ago

Asante xanaaaa ningependa huendeleee kunifundisha

Anod msalege
Anod msalege
2 years ago
Reply to  Admin

Asante xema nilikuwa nauliza jins ya kuwa na kufanya maomb au kuwa na nguvu ya kumuombea mtu

Neema
Neema
2 years ago
Reply to  Admin

0684603985 join me whsap group