Title January 2023

Mungu anatufundisha kusamehe mara saba sabini, ila Kwanini yeye hakumsamehe Adamu alipoasi?.

Jibu:  Adhabu iliyompata Adamu na Hawa, haikutokana na hasira ya Mungu!.. bali ilikuwa ni matokeo ya walichokifanya.

Hebu tafakari mfano huu…. “unamwonya mtu asile kitu Fulani kwasababu unajua madhara ya hicho kitu kwamba endapo akikila basi kitamsababishia apofuke macho na hata kufa huko baadaye, kwasababu kina sumu mbaya ndani yake”.

Lakini huyo mtu ambaye ulimtahadharisha asifanye hivyo, hakukusikiliza wewe badala yake akaenda kula hicho kitu ambacho madhara yake ni kupofuka macho na hata kufa. Na siku alipokula wewe ukajua na kwa huzuni  ukaenda kumwuliza kwanini ulikula?..yeye akatoa sababu zake anazozijua yeye, kisha wewe ukamwambia kwamba.. “kwasababu umekula hicho kitu basi macho yako yatapofuka siku si nyingi  na pia utakufa!.

Sasa swali ni je!, kwa wewe kumwambia hivyo kwamba “atapofuka macho na kufa” je umemhukumu, au umemwambia tu mambo yatakayompata kutokana na kitu alichokifanya?.. Au je kwa wewe kumwambia hivyo, kuna uhusiano wowote wa wewe kumsamehe au kutomsamehe?.. Jibu ni la!, wewe umemwambia tu madhara ya alichokifanya na kuanzia pale utaanza kumhurumia na kumtafutia suluhisho ili ile sumu iliyoingia ndani yake iweze kutoka….

Ndicho kilichotokea pale Edeni, adhabu aliyoipata Adamu na Hawa ni kwasababu ya matokeo ya walichokifanya na si kwasababu ya hasira ya Mungu!!. Na Mungu kwa huruma zake, kuanzia pale ndio akaanza mpango wa kumponya mwanadamu kwa madhara aliyoyaingiza katika maisha yake.

Na ndipo akapata mpango bora, ambao huo utaondoa moja kwa moja madhara yaliyoingia ndani ya Mwanadamu, na mpango huo si mwingine zaidi ya ule wa kumtoa Mwanawe wa pekee YESU KRISTO, aje kufa kwa ajili ya dhambi zetu, na kutukomboa, kuanzia hapo Mungu akamtoa Adamu pale Edeni ili amweke katika mpango mpya na ulio kamili, utakaomkamilisha.

Yesu Kristo pekee ndiye tiba ya KIFO  ambacho kilikuwa kimeingia katika maisha yetu tangu siku ile wazazi wetu, Adamu na Hawa walipoasi.

Yohana 11:25  “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi”

Yesu Kristo ndiye tiba ya mambo yote, ndiye suluhisho la matatizo yote ya maisha, na pasipo yeye sisi hatuwezi kufanya lolote.

Yohana 15:5  “Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote”.

Na nje ya Yesu Kristo hapana wokovu..

Matendo 4:12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”

Je! Umempokea Yesu katika maisha yako?.. je umebatizwa katika ubatizo sahihi? Je umepokea Roho Mtakatifu wa kweli?. Kama bado unasubiri nini?

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JUMA LA SABINI (70) LA DANIELI

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

JINA LAKO NI LA NANI?

BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.

KWANINI TUNAPASWA KWENDA KUIHUBIRI INJILI KWA UJASIRI WOTE?

Rudi nyumbani

Print this post

AKAPITA KATIKA LILE SHAMBA AMBALO YAKOBO ALIMPA YUSUFU MWANAWE

Kuna wakati Bwana Yesu alianza safari ya kuchosha ya kutembea kutoka Yerusalemu kuelekea Galilaya..lakini maandiko yanatuonyesha katika safari yake yote hiyo hakuona mahali popote pa kupumzika, japo alikatiza katika vijiji na miji midogo midogo.

Lakini alipofika Samaria mahali ambapo hapakai wayahudi, aliingia katika eneo ambalo, huwenda alihisi amani  nyingi ya Mungu ikibubujika ndani yake, na hapo hapo akaona kisima cha maji akatulia apumzike kidogo.

Lakini maandiko yanatupa uelewa eneo hilo lilikuwa ni la namna gani mpaka likamfanya Yesu avutiwe nalo…yanasema..mahali pale palikuwa ni karibu na Shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe..

Yohana 4:3-8

[3]aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya.

[4]Naye alikuwa hana budi kupita katikati ya Samaria.

[5]Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe.

[6]Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.

[7]Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.

[8]Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula.

Yesu aliiona ardhi ile katika roho, aliona mbaraka ule wa Yakobo kwa mwanawe Yusufu unavyomkaribisha pale, hivyo hakuweza kupita hivi hivi bila kutenda jambo…aliiona haki ya Yusufu inamlilia shambani kwake.. Kumbuka Israeli yote ilikuwa ni Milki ya wana wote 12 wa Yakobo, lakini si kila shamba la mwana wa Yakobo Yesu alipumzika.

Hivyo kitendo cha Yesu tu kutulia pale, kama tunavyojua habari watu wengi wa Samaria wakapokea wokovu akawaokoa watu ambao hawakustahili wokovu kabisa (yaani wasamaria).

Unaweza kujiuliza ni wakati gani Yakobo alimpa Yusufu shamba hilo? Waweza kusoma habari hiyo katika..Mwanzo 48:21-22

Utaona akipewa sehemu mara dufu ya wenzake.. Na hiyo yote ni kwasababu Yakobo alimpenda Yusufu kwa tabia zake njema.

Ile Tabia ya Yusufu ya kumcha Bwana alipokea thawabu sio tu za wakati ule alipofanyika kuwa waziri mkuu wa Misri.. Lakini tunaona pia hadi kipindi cha Bwana Yesu baraka zake bado zilitembea.

Leo hii ukimcha Mungu wewe kama kijana, utawasababishia wengine kupokea neema ya wokovu  hata wakati ambapo haupo hapa duniani.. Kumcha Mungu ni uwekezaji mkubwa sana zaidi ya mali.

Bwana akikubariki uzao, basi huwenda vitukuu vyako vikawa majeshi hodari ya Kristo, kwasababu Yesu anapita kuangalia ni wapi mbaraka wa Yusufu upo  ili apumzike? akakuona wewe.

Akikubariki mashamba au mali, siku za mbeleni aidha uwapo hai au ufapo, Kristo atapita hapo na patakuwa kitovu cha madhabahu nyingi za Mungu.

Chochote kile ukiachacho duniani, kama sio mali, kama sio shamba, kama sio vitu..basi Mungu atatumia hata mifupa yako kuwaponya wengine.. Ndivyo Mungu alivyofanya kwa Elisha baada ya kufa na miaka mingi kupita ameshasahaulika, amebakia tu mifupa, kaburini, lakini maiti ilipoangukia mifupa yake, ile maiti ikafufuka.

Je ni tabia gani unaionyesha kwa Mungu sasa, hadi akupe shamba lake spesheli ambalo Kristo atakuja kupumzikia hapo siku za mbeleni? Watoto wako, vijukuu vyako, vitabarikiwaje kama wewe hutamcha Mungu sasa?

Tafakari maisha ya Yusufu, kisha fananisha na yako utapata majibu. Yatupasa tuichukie dhambi, tuchukie uasherati, tuchukie wizi, tuwe waaminifu, tuishi maisha yanayompendeza Mungu sikuzote. 

Na hatimaye na sisi tutakuwa wokovu kwa vizazi vyijavyo. 

Bwana atuponye..Bwana atusaidie.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

WALA HAKUSIMAMA MTU PAMOJA NAYE, YUSUFU ALIPOJITAMBULISHA KWA NDUGUZE

Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?

UVUMILIVU NA MIKAKATI YA ABSALOMU, INA FUNZO NYUMA YAKE.

Kuiaua Nchi ni kufanya nini? (Waamuzi 18:2).

Injili iliyopo kwa Samaki aina ya Eeli.

Rudi nyumbani

Print this post

HAKUONA MAHALI PA KUTUA KWA WAYO WA MGUU WAKE.

Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia, Neno La Mungu wetu.

Mwanzo 8:6 “Ikawa baada ya siku arobaini, Nuhu akalifungua dirisha la safina, alilolifanya; 

7 akatoa kunguru, naye akatoka akaenda huko na huko, hata maji yakakauka juu ya nchi.

 8 Kisha akatoa njiwa, aone kwamba maji yamepunguka usoni pa nchi; 

9 bali YULE NJIWA HAKUONA MAHALI PA KUTUA KWA WAYO WA MGUU WAKE, akamrudia Nuhu safinani, maana maji yalikuwa juu ya uso wa nchi yote; naye akanyosha mkono, akamtwaa, akamwingiza mle safinani”

Tunaona wakati wa Nuhu kutoka safinani… Aliwaachia ndege wawili ili kupima hali ya mazingira ya nje. Na ndege wa kwanza ambaye ni “KUNGURU” aliondoka lakini hakumrudia Nuhu.. lakini ndege wa pili ambaye ni “NJIWA” Alipoondoka na kukuta nje maji yamejaa kila mahali, alirudi safinani..

Sasa ni kwanini Njiwa arudi na kunguru asirudi?.

Siri ipo katika ile sura ya Saba, kuhusiana na wanyama Najisi na wasio Najisi.

Mwanzo 7:1 “Bwana akamwambia Nuhu, Ingia wewe na jamaa yako yote katika safina; kwa maana nimekuona wewe u mwenye haki mbele zangu katika kizazi hiki.

 2 Katika wanyama wote walio safi ujitwalie saba saba, mume na mke; na katika wanyama wasio safi wawili wawili, mume na mke. 

3 Tena katika ndege wa angani saba saba, mume na mke; ili kuhifadhi hai mbegu juu ya uso wa nchi yote”

Sasa Kunguru yupo katika kundi la Ndege Najisi,

Walawi 11:13 “Kisha katika ndege hawa watakuwa ni machukizo kwenu; hawataliwa, ndio machukizo; tai, na furukombe, na kipungu;

14 na mwewe, na kozi kwa aina zake,

15 na kila kunguru kwa aina zake”

Na njiwa yupo katika kundi la ndege Safi (yaani wasio najisi) ndio maana alikuwa anatumika katika matoleo.

Sasa tabia ya ndege/wanyama najisi ni za tofauti na zile za wasio najisi. Wanyama najisi wanakula chochote na wanaweza kuishi popote.. lakini Wanyama/ndege wasio najisi wanachagua vitu vya kula, vile vile wanachagua mazingira ya kuishi, si kila mahali wanaweza kuishi.

Ndio maana tunaona huyu kunguru alipoachiwa, alienda kuzunguka zunguka huko nje, lakini njiwa aliona mazingira ya nje si salama, bado wakati wake, na hatimaye akarudi safinani.

Sasa wanyama najisi kiroho wanafananishwa na watu wa ulimwengu huu, walio mbali na MUNGU, na wanyama Safi (yaani wasio najisi) wanafananishwa na watu wa Mungu, waliookolewa kwa damu ya thamani ya YESU KRISTO, ambao hawajitii unajisi na mambo ya dunia.

Kama vile njiwa alivyozunguka huko na huko na kuona safinani ni mahali salama katika dunia iliyoharibika.. vile vile watu wa Mungu, kamwe hawawezi kuona hii dunia ipo salama, au ni mahali pa kustarehe kuliko safinani. Na safina ni BWANA YESU!.

Ukiona unaifurahia dunia iliyochafuka, dunia iliyojaa anasa, dunia iliyojaa mabaya basi katika roho wewe ni najisi.. Ukiona unaufurahia uasherati, ulevi, wizi unaoendelea duniani, na hata wewe mwenyewe kuwa mshirika wa hayo, basi fahamu kuwa unafanana na Yule kunguru! Na hivyo ni najisi mbele za Mungu kulingana na biblia.

Mathayo 15:18 “….vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.

19  Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano;

20  hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi…”

Je! wewe ni miongoni mwa walio najisi au safi? Kama bado dhambi inatawala maisha yako basi upo hatarini hivyo suluhisho ni kumgeukia Yesu kwa kutubu na kumaanisha kuacha dhambi, na Yesu atakupokea na kukupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu, ambaye kupitia huyo atakutakasa kwa kukupa uwezo wa kufanya yale mema ambayo ulikuwa unashindwa kuyafanya kwa nguvu zako.

Kataa ukunguru!

Bwana akubariki

maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini Mungu aliwaita Adamu na Hawa jina moja?

JIHADHARI NA ROHO ZIDANGANYAZO.

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

HUJAPEWA MBAWA ZA KUKIMBIA MATATIZO

Rudi nyumbani

Print this post

Je Yesu ni Mungu au Nabii?

Maandiko yanaonyesha kuwa YESU ni Mungu na pia ni NABII.  Ni sawa na mkuu wa nchi anaweza kuwa RAISI kwa wananchi, lakini pia anaweza kuwa BABA au MAMA kwa watoto wake. Hivyo mtu mmoja anaweza kuwa na vyeo zaidi ya kimoja kufuatana na mazingira aliyopo. Raisi akiwa ofisini ataitwa Raisi, akiwa nyumbani kwake na watoto wake ataitwa Baba/mama.

Vile vile Kristo akiwa mbinguni ni Mungu, akiwa duniani ni Mwana wa Adamu na Nabii na Mwokozi, na akiwa ndani yetu ni Roho Mtakatifu.

Sasa ni wapi maandiko yanatuonyesha kuwa Yesu alikuwa ni Nabii?

Luka 24:19  “Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, ALIYEKUWA MTU NABII, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote”

Kumbukumbu 18:15 “Bwana, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye”.

Vile vile ni wapi maandiko yanatuonyesha kuwa Yesu alikuwa Mwana wa Mungu?

Mathayo 16:15  “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

16  Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

17  Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni”

Na ni wapi maandiko yanatuonyesha kuwa YESU alikuwa Mungu?

Tito 2:13  “tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu”

Soma pia 1Timotheo 3:16 na Yohana 1:1.

Kwahiyo Yesu ni yote katika vyote, na ndio Mwokozi wa Ulimwengu, na ndiye Njia ya kufika mbinguni. Hakuna mwanadamu yeyote atakayefika mbinguni isipokuwa kwa njia yake yeye.

Je umempokea Yesu?.. Kama bado unasubiri nini?

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

Je shetani anaweza kushusha moto kutoka mbinguni?

Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

AKAZIDI KUENDELEA KATIKA HEKIMA NA KIMO.

Rudi nyumbani

Print this post

Kalibu maana yake nini? (Mathayo 6:30).

Mathayo 6:30 “Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?”

Neno hili “kalibu” limerudiwa pia kutajwa katika Luka 12:28, na maana ya neno hili ni “TANURU LA MOTO”. Kwa kawaida baada ya kusafisha mazingira, kwa kuondoa Nyasi au takataka huwa zinatupwa katika tanuru la moto, sasa tanuru hilo ndilo linaloitwa “Kalibu”, Na Bwana Yesu alitoa mfano huo kuonyesha maisha yetu jinsi yalivyo na thamani mara nyingi zaidi kuliko maua ya kondeni.

Kwani kama Mungu anavyoyavika utukufu maua ya kondeni, kwa rangi rangi zake za kuvutia, basi sisi ni zaidi sana mbele zake kuliko hayo MAUA ya kondeni, ambayo leo yapo lakini kesho yanatupwa motoni.. Sisi tuna thamani mbele zake kuliko maua, maana yake sisi atatuvisha zaidi kuliko Maua, atatulisha zaidi kuliko ndege, atatubariki kuliko viumbe vyote vya asili. Huo ni upendeleo wa kipekee sana.

Tunachopaswa kufanya ni kuutafuta tu ufalme wake na haki yake, halafu hayo  mengine ya chakula, mavazi tumwachie yeye, kasema atatuzidishia, na yeye kamwe hawezi kusema uongo.

Luka 12:29 “Ninyi msitafute mtakavyokula wala mtakavyokunywa; wala msifanye wasiwasi,

30  kwa maana, hayo yote ndiyo watafutayo mataifa ya duniani, lakini Baba yenu anajua ya kuwa mna haja na hayo.

31  Bali utafuteni ufalme wa Mungu, na hayo mtaongezewa.

32  Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je suruali ni vazi la kiume tu?

Wakati wakina Shadraka wanatupwa katika tanuru la moto, Danieli alikuwa wapi?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

Nyinyoro ni nini?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Rudi nyumbani

Print this post

RUHUSU TOHARA IPITE JUU YA KARAMA YAKO.

Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo mwokozi wetu. Karibu tujifunze maneno yake ya uzima.

Ni wazi kuwa kila mmoja wetu anatamani kumzalia Mungu matunda mengi, anatamani kuona karama yake ikifanyika Baraka kwa watu wengi, anatamani kuona watu wakiokoka, watu wakijengeka, watu wakiinuliwa. Lakini anapoona haoni matokeo haya, katika hatua za awali za utumishi, anaishia kuvunjika moyo na kusema nachofanya ni kama sio huduma yangu.

Lakini hajui kanuni za Mungu anazozitumia ili kutufikisha katika viwango vya uzaaji wa matunda. Bwana Yesu alisema, tukikaa ndani yake, na yeye ndani yetu, tutazaa sana,(Yohana 15:1-8)  Lakini bado wengi tunadhani kukaa ndani ya Bwana, ni kusema nimeokoka..hilo tu!. Jambo ambalo si kweli, wapo waliokaa kwa muda mrefu lakini hawazai matunda yoyote. Kukaa ndani ya Kristo sio tu kuokoka bali  ni kujua kanuni za Kristo za uzaaji wa matunda.

Tusome, maandiko haya, yatusaidie kuona jambo hili kwa undani.  Haya ni maagizo ambayo Bwana aliwapa wana wa Israeli kuhusiana na miti yao ya matunda watakayoipanda wafikapo Kaanani.

Walawi 19:23 “Nanyi hapo mtakapoingia nchi ile, mkiwa mmepanda miti ya namna zote kwa ajili ya chakula, ndipo mtayahesabu matunda yake kama ni KUTOTAHIRIWA; muda wa miaka mitatu miti hiyo itakuwa kwenu kama kutotahiriwa; matunda yake hayataliwa. 

24 Lakini mwaka wa nne matunda yake yote yatakuwa ni MATAKATIFU, kwa ajili ya kumpa Bwana shukrani.

25 Na katika mwaka wa tano mtakula katika matunda yake, ili ipate kuwapa MAONGEO YAKE; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu”.

Mungu anawaonyesha kanuni ya uzaaji matunda, ambayo imegawanyika katika hatua kuu tatu.

Hatua ya kwanza, ni ile miaka mitatu ya kwanza(Kutokutahiriwa):

Katika hii miaka miti huwa inazaa matunda, lakini matunda yale, huhesabiwa kama ni najisi: Wakulima wanaelewa vema kuwa sikuzote matunda ya kwanza, huwa ni dhaifu, hayana ladha nzuri, hivyo  yameapo, hukatwa na kutupwa, ili kupisha ukuaji mwingine, na umeaji mzuri wa matunda mapya kwa msimu ujao.

Kufunua karama zetu, pindi uokokapo, huna budi kuzaa matunda haya ya awali. Ambayo ki-msingi huwa hayana matokeo yoyote makubwa,  unaweza ukafanya kazi  ya Mungu ambayo ni kama vile haina matunda yoyote, utajiona haustahili, au haujui, lakini ni sharti uendelee kuzaa, kwa kipindi ulichowekewa mbele yako. Ukishavuta hatua hii,ndipo unaingia ya pili. Huwezi pelekwa nyingine kama hii ya kwanza hujapitia.

Hatua ya pili: Kuyafanya  matakatifu kwa Bwana.

Wana wa Israeli, bado hawakuruhusiwa, kuyala matunda yao, hata katika mwaka wanne, japo  matunda yanakuwa yameshakomaa na kukidhi kuliwa kabisa, lakini hawakuruhusiwa kuyala, bali waliagizwa wayatoe wakfu kwa Bwana. Hii maana yake ni nini, karama au huduma uliyopewa, wapaswa uigharimie wewe, hapa ni kukubali kujitoa kikamilifu katika wito huo uliopewa na Mungu. Nguvu zako, akili zako zote, hata mali zako ziwekeze kwa Bwana. Watu wengi,wafikapo hatua hii,wanasema huku ni kugumu, uzalendo umenishinda, tena nimpe Mungu, badala yeye ndio anipe mimi. Ndivyo hata huyu mkulima anavyowaza, nimesubiria miaka yote hii mitatu ‘matunda yanakuja na kuanguka tu’, halafu mwaka huu wa nne, badala  nifaidi, nashangaa, kuambiwa nimtolee tena Bwana. Ndugu hiyo ndiyo kanuni ya Ki-Mungu. Kutoa! Hakuepukiki kwa Bwana.

Hatua ya tatu: Maongeo.

Maongeo ni maongezeko, yaani Baraka. Au kuzaa kupita kiasi.

Katika mwaka wa Tano, ndio mkulima anaanza kuona faida ya kazi yake yote. Miti ya waisraeli ilibarikiwa kipekee tofauti na ile ya mataifa mengine,kwasababu ilifuata  kanuni hii ya Mungu. Walikuwa wanavuna kupita kiasi, kila mwaka mizeituni, mizabibu, tini, ilitoa matunda mengi kupita miti yote ya matunda ulimwenguni.

Nasi pia, ili tufikie hatua ya kuona maongeo katika huduma zetu. Hatuna budi, kwanza kutumika kwa uaminifu na kwa uvumilivu kwa kipindi Fulani, bila kuona faida yoyote inayoeleweka katika huduma/karama zetu, hatuna budi kupitia kukosea sana, unamuhubiria mtu, unadhani atasimama, kesho anarudi nyuma, matunda yako ni kama kazi bure. Lakini hilo halina budi lifanyike, kamwe mambo hayaji ndani ya siku moja, fanyia kazi kwanza kile ulichopewa,bila kujali matokeo ya nje.

Vilevile Baada ya kipindi Fulani. Utagharimika, ujitoe, haswaa, katika huduma/karama  hiyo. Hapa usizuie chochote ulichonacho, unampa Mungu vyote, kama malimbuko kwake, hii ni kuonyesha upendo wako kwa hicho unachotaka umzalie Mungu matunda.

Na mwisho. Bwana anabariki.  Matunda yanakuja, katika utimilifu wote. Maono yako yanatimia, karama yako  inakuwa sababu ya wengi kumgeukia Mungu.

.Lakini kumbuka “Kamwe usikae tu na kusema siku moja nitafikia pale” bila kuonyesha bidii sasa. Utamaliza miaka 20 katika wokovu, hujamzalia Mungu tunda lolote. Bwana atusaidie kulitambua hili.

Njia mojawapo ya kutambua hicho ulichopewa ni karama yako, ni kusikia msukumo wa kukifanya kwa Mungu. Huo msukumo utendee kazi sana. Utakuwa msaada mkubwa sana mbeleni.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?.

ICHOCHEE KARAMA YAKO.

Maongeo ni nini?(Wakolosai 2:19)

NENO LA MUNGU NI UFUNUO MKAMILIFU.

NI KWA NAMNA GANI ROHO HUTUTAMANI KIASI CHA KUONA WIVU?

TWAENENDA KWA IMANI NA SI KWA KUONA.

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

Rudi nyumbani

Print this post

UFANYE WEMA WAKO KATIKA MAARIFA.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, Karibu tujifunze biblia..

2Petro 1:5 “Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, NA KATIKA WEMA WENU MAARIFA”

Wema usiokuwa na Maarifa bado haujakamilika.. Ni kweli unaweza kufanya Wema na nia yako ikawa ni njema, lakini wema huo usipoufanya katika maarifa, huenda ukakuletea madhara hata wewe mwenyewe uliofanya huo wema.

Hebu tuangalie mtu mmoja katika biblia ambaye aliufanya wema wake katika maarifa yote, na huyo si mwingine zaidi ya Yule Msamaria-mwema.

Hebu tusome habari yake na kisha tutafakari…

Luka 10: 30 “ Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.

31  Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.

32  Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.

33  Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,

34  akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.

35  Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa”

Tunaona Msamaria huyu alipopita njiani na kukuta mtu kalala kando, hakukurupuka  na kumpeleka nyumbani kwake, akalale na watoto wake au ndugu zake.. Badala yake alimchukua na kumpeleka katika nyumba ya kulala wageni (yaani Guest-house), na akiwa huko huenda aliendelea na hatua nyingine za kuripoti habari yake katika vyombo vilivyohusika, ili kama ikiwezekana apate msaada zaidi wa kuwapata watu wa nyumbani kwake.

Sasa kwanini hakumpeleka nyumbani kwake moja kwa moja?, si kwasababu hakuwa na huo uwezo, au labda ni mbali.. La! Bali ni kwasababu alitumia maarifa katika Wema wake, kwasababu Yule mtu alikuwa hamjui, hivyo kumchukua na kumpeleka nyumbani moja kwa moja, ingeweza kuwa hatari kwasababu huenda akafa, na matatizo yakawa kwa Yule aliyemsaidia, au huenda si mtu mzuri wakati wa kulala usiku akapata nafuu na kuamka na kumdhuru Yule aliyemsaidia.

Hivyo suluhisho la akili na hekima si kumpeleka nyumbani, bali katika nyumba ya kulala wageni.

Hali kadhalika na sisi tunapaswa tufanye wema wetu katika MAARIFA.. Si kila anayehitaji msaada basi ni wa kumpatia kile anachokihitaji yeye, bali tunapaswa tupime namna ya kumsaidia katika maarifa..

1 . Mtu  usiyemjua akikuomba fedha ya hitaji Fulani, ni vizuri usimpe hiyo fedha bali ukamnunulia hilo hitaji lake na kumpatia.

2. Ukimkuta mtu usiyemjua yupo katika hali ya kuhitaji msaada wa kimalazi.. usimchukue moja kwa moja na kumpeleka kwako, jitahidi umtafutie mahali pa kulala hususani kama gesti, angalau kwa siku moja, huku unaendelea kufuatilia taarifa zake na kuziripoti, na ukishajiridhisha vya kutosha ndipo umwamishie kwako.

3. Mtu usiyemjua akikuomba nguo, kama una uwezo basi mnunulie yake mpya, lakini usiitoe ile ya mwilini mwako na kumpatia, kwasababu shetani anaweza kuitumia hiyo kama mlango wa kukuletea matatizo maishani mwako. Lakini kama mtu unamjua au umejiridhisha kabisa kuwa ni mhitaji asiye na tashwishi basi waweza kumpa moja kwa moja nguo inayotoka moja kwa moja.

4. Mtu usiyemjua akikuomba Lift ya gari, au pikipiki, au baiskeli..kama una uwezo mlipie nauli apande katika chombo kingine, kwasababu humjui mtu huyo ni nani, na hivyo ni rahisi kutumiwa na adui kuleta dhara lolote lile.

5. Mtu usiyemjua akikuomba chakula kutoka katika sahani yako, usimpe kile chakula, badala yake mnunulie cha kwake binafsi, (sio uchoyo kufanya hivyo, bali ni hekima) kwasababu shetani anaweza kumtumia kama chombo cha kukuletea matatizo, kwasababu unaweza kumpa na kumbe kile chakula hakiendani na mwili wake, hivyo kikamletea madhara au hata kifo, jambo ambalo linaweza kutafsirika kwamba umemwekea sumu au dhara lolote, na kukuingiza wewe matatizoni pasipo sababu yoyote, hivyo ni lazima katika WEMA wako uweke na maarifa. (Kumbuka usiache kutenda wema, bali utende katika maarifa).

Na mambo mengine yote mema unayoyafanya kwa Mtu au watu, hakikisha unayafanya katika maarifa yote, ndivyo biblia inavyotufundisha.

2Petro 1:5 “Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, NA KATIKA WEMA WENU MAARIFA

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

AINA SABA (7) ZA UNAFIKI, AMBAZO UNAPASWA UJIEPUSHE NAZO.

Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?

Tofauti kati ya Hekima, ufahamu na maarifa, ni ipi?

Nuru yetu inapaswa iangaze au isiangaze kulingana na Mathayo 5:16 na Mathayo 6:1?

MAWE YALIYOKWISHA KUCHONGWA MACHIMBONI.

Rudi nyumbani

Print this post

Kuiaua Nchi ni kufanya nini? (Waamuzi 18:2).

Jibu: Tusome,

Waamuzi 18:2 “Basi wana wa Dani wakatuma watu wa jamaa zao, watu watano katika hesabu yao yote, watu mashujaa, kutoka Sora, na kutoka Eshtaoli, ili kuipeleleza hiyo nchi, KUIAUA; wakawaambia, Haya, endeni mkaikague nchi hii; basi wakaifikilia nchi ya vilima vilima ya Efraimu, hata nyumba ya huyo Mika, Wakalala huko”

Kuiaua nchi maana yake ni KUITEMBELEA NCHI au KUIZURU. Kwahiyo watu wanaozunguka zunguka ndani ya nchi kwa lengo la kuipeleleza au kwa lengo la utalii, maana yake ni WAMEIAUA HIYO NCHI.

Mungu wetu anaiaua dunia hii tunayoishi, kutafuta watu wanaomcha yeye, kuwatia nguvu na kuonyesha uweza wake juu yao.

2Nyakati 16:9 “Kwa maana macho ya Bwana hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake…”

Lakini pia adui yetu shetani ANAIAUA dunia nzima kutafuta mwenye haki mmoja amwangushe..

Ayubu 1:6 “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao. 

7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.

 8 Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu”

Hivyo hatuna budi kuutunza ukamilifu wetu ili tusije tukanaswa katika mitego ya shetani na hatimaye kuanguka kabisa.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

TABIA ZITAKAZOMTAMBULISHA MPINGA-KRISTO AJAYE.

Marago ni nini? ( Waamuzi 10:18)

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

MUNGU HANA MBARAKA MMOJA TU!..MWAMINI.

Rudi nyumbani

Print this post

Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; (Mithali 11:16)          

Huu ni mwendelezo wa Mafundisho maalumu yawahusuyo wanawake.

Mithali 11:16          

[16]Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; ..”

Ujumbe huu ni kwako wewe binti/Mama/ ambaye unapenda kuheshimiwa na Mungu pamoja na wanadamu.

Kumbuka  heshima inatafutwa na si wote wanayo, kwasababu inagharama yake kuipata…heshima sio uzuri, heshima sio elimu, sio u-kisasa, wala sio pesa..Ni thamani yako ya ndani, inayoonwa na wengine.

Dada Ukitaka kufahamu ni nini kitakupa heshima usiwafuate mabinti wenzako,la! Hata na  akili zako pia usizifuate, Bali mtafute aliyekuumba ili akupe siri ni nini kitakuthaminisha hapa duniani kwa wanadamu.

Inatia huruma kuona, mabinti wengi wanadhani wanaheshimiwa kwa urembo wao..hivyo hubuni kila namna ya kujipamba, na kujichubua ngozi zao, wanavaa mawigi na makucha ya bandia, kisha kwa ujasiri wanatembe mbele ya watu..wakidhani kuwa ndio wanaonekana watu wa maana sana kwenye jamii..Ukifanya hivyo Binti umepotea!

Wanadhani kuonyesha miili yao barabarani, na kujifanya wakisasa ni heshima, dada hapo huheshimiwi unasanifiwa tu. Unachofanya ni kujiongezea nafasi tu ya kuwa kiburudisho cha macho ya wahuni..na ndio maana watakupigia miluzi na kukutazama tazama.mara mbili ili kesho urudie kufanya hivyo tena, wajiburudishe macho yao, lakini zaidi ya hapo wewe ni FELIA…

Hivyo fahamu heshima yako inatoka wapi..

Biblia inaeleza heshima ya mwanamke inakuja katika mambo haya  saba

  1. Kumcha Bwana
  2. Adabu
  3. Upole
  4. Kiasi
  5. Utulivu
  6. Kujisitiri
  7. Utiifu

Yote haya utayasoma katika vifungu hivi:

Mithali 31:30

[30]Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili;  Bali mwanamke AMCHAYE BWANA, ndiye atakayesifiwa.

1 Timotheo 2:9-11

[9]Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa MAVAZI YA KUJISITIRI, pamoja na ADABU nzuri, na MOYO WA KIASI; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;

[10]bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.

[11]Mwanamke na ajifunze katika UTULIVU, AKITII kwa kila namna.

1 Petro 3:3-4

[3]Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

[4]bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya UPOLE NA UTULIVU, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

Ukiyazingatia haya binti/mwanamke, heshima itakufuata yenyewe…na lolote ulitamanilo kwa Mungu utalipata tu..Kama ni mume bora Mungu atakuletea, tena zaidi ya matarajio yako kama Ruthu alivyoletewa Boazi, 

Kama ni kibali, utakipata tena cheo kikubwa zaidi ya wengi, ikiwa ni utumishi, Bwana ataizidisha karama yako pakubwa sana..Na zaidi ya yote una uzima wa milele. Hata ukienda mbinguni unawekwa kundi moja na akina Sara na Ana na Debora, Mariamu, na wanawake wote mashujaa walioishindania imani ipasavyo.

Lakini kinyume chake ni kweli, usipoyashika hayo, utafanana tu na Yezebeli na ukienda kuzimu utawekwa kundi moja na yeye.

Usiiuze heshima yako.

Jithamini.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

USHAURI KWA MWANAMKE WA KIKRISTO.

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

Wanaowachukua wanawake wajinga mateka ni akina nani?

Kama Malkia Esta alijipamba je! Kuna ubaya gani wanawake wa wakikristo wa leo kujipamba?

Rudi nyumbani

Print this post

Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala Mwangalie sana

SWALI: Mstari huu unamaana gani?

Mithali 23:1-3

[1]Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala, Mwangalie sana yeye aliye mbele yako.

[2]Tena ujitie kisu kooni, Kama ukiwa mlafi.

[3]Usivitamani vyakula vyake vya anasa; Kwa maana ni vyakula vya hila.


JIBU: Sulemani akiwa kama mfalme alielewa sana tabia za wafalme zilivyo na hivyo kwa uzoefu wake hapa anatoa mapendekezo yake kwa mtu yeyote ambaye ataitwa na mfalme au mtu yeyote mkuu kula chakula pamoja nao.

Anasema chukua tahadhari “Mwangalie sana”..uwe na kiasi na hizo zawadi zake akupazo, hapo ametumia lugha ya vyakula, lakini yaweza kuwa uongozi, fursa, pesa, n.k..anasema uwe na kiasi, kwasababu nyingi za hizo huwa ni za hila.

Kwasababu mfalme hawezi kumwalika mtu, kama haoni kuna faida fulani anaweza kuipata kwake, ingekuwa ni hivyo angekuwa anamwalika kila mtu tu, ikulu na kushiriki naye.

Mfano wa wazi tunauona, kwa malkia Esta alipomwalika Hamani, kama Hamani angelielewa andiko hili, angetafakari mara mbili mbili ni kwanini apewe tu yeye kipaumbele cha juu zaidi ya wengine..Lakini alikuwa anacheka na kufurahia tu mialiko, na matokeo yake yakawa ni kujipeleka mwenyewe kitanzini.

Ni kawaida ya shetani akishaona una hatari ya kuupindua ufalme wake, haji kwa hasira au kiboko, atakuja kwa anasa, alifanya hivyo kwa Bwana Yesu, na kumwambia “hivi vyote nitakupa, endapo utaanguka na kunisujudia”..Bwana akamkemea, na kumfukuza, wakati mwingine mfalme Belshaza alimwita Danieli, amtabirie vizuri juu ya ufalme wake akamuahidi atakuwa mtu wa tatu kwenye ufalme wake, Danieli hakupumbazika na kukaa pamoja naye katika utawala wake wa dhambi, kinyume chake akakataa akatabiri na kuondoka zake..Lakini usiku huo huo kumbe ndio ulikuwa mwisho wa mfalme Belshaza, akavamiwa na wamedi, na kuuawa, sasa kama Danieli angekutwa pale anafanya anasa nao naye pia habari yake ingeishia pale.

Watumishi wengi wa Mungu wakubwa, wamepoozwa moto wao wa injili au utumishi wao kwa ujumla na watu wakuu au wa mamlaka, kwa kukosa kwao kiasi. 

Hivyo mstari huu unatupa tahadhari, katika ngazi yoyote ile,  iwe ni ngazi ya chini, katika kampuni,au shirika,  au katika serikali, tualikwapo, tuwe makini, kuchunguza ni mashauri gani yapo nyuma yake.

Bwana akubariki.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

Biblia inamaanisha nini iliposema “wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa;?

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU

NUHU WA SASA.

Rudi nyumbani

Print this post