Je Yesu ni Mungu au Nabii?

Je Yesu ni Mungu au Nabii?

Maandiko yanaonyesha kuwa YESU ni Mungu na pia ni NABII.  Ni sawa na mkuu wa nchi anaweza kuwa RAISI kwa wananchi, lakini pia anaweza kuwa BABA au MAMA kwa watoto wake. Hivyo mtu mmoja anaweza kuwa na vyeo zaidi ya kimoja kufuatana na mazingira aliyopo. Raisi akiwa ofisini ataitwa Raisi, akiwa nyumbani kwake na watoto wake ataitwa Baba/mama.

Vile vile Kristo akiwa mbinguni ni Mungu, akiwa duniani ni Mwana wa Adamu na Nabii na Mwokozi, na akiwa ndani yetu ni Roho Mtakatifu.

Sasa ni wapi maandiko yanatuonyesha kuwa Yesu alikuwa ni Nabii?

Luka 24:19  “Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, ALIYEKUWA MTU NABII, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote”

Kumbukumbu 18:15 “Bwana, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye”.

Vile vile ni wapi maandiko yanatuonyesha kuwa Yesu alikuwa Mwana wa Mungu?

Mathayo 16:15  “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

16  Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

17  Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni”

Na ni wapi maandiko yanatuonyesha kuwa YESU alikuwa Mungu?

Tito 2:13  “tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu”

Soma pia 1Timotheo 3:16 na Yohana 1:1.

Kwahiyo Yesu ni yote katika vyote, na ndio Mwokozi wa Ulimwengu, na ndiye Njia ya kufika mbinguni. Hakuna mwanadamu yeyote atakayefika mbinguni isipokuwa kwa njia yake yeye.

Je umempokea Yesu?.. Kama bado unasubiri nini?

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

Je shetani anaweza kushusha moto kutoka mbinguni?

Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

AKAZIDI KUENDELEA KATIKA HEKIMA NA KIMO.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments