AKAZIDI KUENDELEA KATIKA HEKIMA NA KIMO.

AKAZIDI KUENDELEA KATIKA HEKIMA NA KIMO.

Shalom, karibu tujifunze maneno ya uzima.

Wengi wetu tunadhani Bwana Yesu alizaliwa akiwa na ufahamu kamili wa kila kitu, au ujuzi wa mambo yote, Hapana alizaliwa akiwa kama sisi kabisa, hajui kitu chochote, japo alikuwa ni Mungu kweli katika mwili.

Ilipasa iwe hivyo, ili kutimiza kusudi la Mungu, la kumfananisha na sisi  katika mambo yote ili  awe kielelezo cha sisi kuifuata njia yake. Hivyo kwa kuyatazama tu Maisha ya Bwana Yesu tunaweza kujifunza mambo ambayo hata sisi wenyewe tunaweza kuyafanya.

Mpaka Bwana kufikia hatua ya kufahamu siri nyingi sana za Mungu, halikuwa ni jambo alilozaliwa nalo, hapana, biblia inasema..

“Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu”.

Kuendelea katika hekima na Kimo, maana yake ni kukua kila siku katika hekima ya kumjua Mungu, yaani kutoka kiwango kimoja hadi kingine, hatua moja hadi nyingi.. Na hilo halikuja tu hivi hivi, Bali alikuwa na bidii tangu akiwa mtoto, ya kujifunza maneno ya Mungu, kwa kuwatafuta waalimu ili wamsaidie, Na alipokutana nao alikuwa akiwauliza maswali pale ambapo alikuwa haelewi na kutoa maoni yake pale ambapo alikuwa anapaelewa zaidi,..Jambo hilo unaweza  kulisoma katika…

Luka 3:46 “Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.

47 Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake.

48 Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.

49 Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?

50 Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia.

51 Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.

52 Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu”.

Jaribu kutafakari, kijana wa miaka 12 anatumia siku tatu usiku na mchana, kakaa tu kanisani, akijifunza Biblia, na hiyo ni desturi yake ya mara kwa mara.. Unategemea vipi kijana kama huyo akiwa mtu mzima, atakuwa sawa na watu wengine?

Ni lazima tu, atakuwa katika maarifa ya kumjua Mungu kwa kasi, na ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana, mambo yote hayakumjia tu ghafla ndani yake, labda kazaliwa nacho, hivyo hakuwa na haja ya kuongeza maarifa au kujifunza hapana.

Leo hii, utaona mkristo, hana habari ya kujifunza Biblia, hata akienda kujifunza haulizi maswali, wachungaji wake, au manabii wake, au waalimu wake,  yeye ni kusikiliza tu na kuondoka, akiambiwa jambo Fulani hata kama ni gheni kwake, atalipokea tu na kusema AMEN! Baba..Basi..

Kwa mtu ambaye ni msomaji wa biblia, ni lazima tu atakutana na mambo mengi sana yasiyoeleweka, Na Mungu ameyaficha hivyo makusudi, ili atujengee tabia ya kupenda kutafuta, na mwisho wa siku ampe majibu.. Lakini kama utasoma tu biblia kwa kujiburudisha, au kutimiza ratiba, ufahamu kuwa huo sio mpango wa Mungu.

Mungu anataka tujifunze biblia sio, tuisome kama gazeti, Biblia ni kitabu cha mafumbo, hakuna namna mkristo akose maswali ya kumuuliza Mungu..hilo haliwezekani..Embu kaa chini usome kitabu chochote kwa kumaanisha halafu uniambie kama ni mambo yote yaliyopo kule umeyaelewa..Hilo halipo..

Lakini Yesu hakuona aibu ya kutaka kujifunza pale ambapo alikuwa haelewi, na alitumia fursa hiyo vizuri kuwafuata waalimu wake wa torati…Vivyo hivyo na wewe kama unataka kukua katika hekima na Kimo katika kumjua Mungu, wafuate wale waliokutangulia katika Imani, yaani wachungaji wako, manabii wako, mitume wako, waalimu wako, waulize maswali kwa yale uliyojifunza katika biblia..ukiona majibu yao hayajakuridhisha..tafuta tena wachungaji wengine, kawaulize, maswali, hivyo hivyo mpaka Roho Mtakatifu atakufunulia jibu sahihi..

Japo Bwana Yesu alikaa chini ya waalimu, lakini mwisho wa siku yeye ndiye aliyekuwa MWALIMU WA WAALIMU… Alikuwa ni RABI, Alijua siri nyingi za ufalme wa mbinguni, kuliko watu wote waliokuwa duniani, sio tu wale walioishi naye, mpaka pia wale waliomtangulia.

Hata wewe ukiwa ni mtu wa kutoridhika na hali ya ufahamu wako kuhusu Mungu, ukaanza kujifunza, uwe na uhakika kuwa upo wakati, utakuwa ni mtu wa viwango vya mbali sana, na Mungu atajifunua kwako kwa namna ambazo wewe mwenyewe utashangaa.

Anza sasa, kumtafuta Mungu wako, kwa bidii kama za Bwana wetu YESU KRISTO.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

KWANINI MIMI?

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

MIUJIZA YA KRISTO, HAITEGEMEI KANUNI ZA KIBINADAMU.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments