Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

SWALI: Shalom wana wa Mungu Naomba msaada kuelewa andiko hili;

Mhubiri 9:11 “Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote”.


JIBU: Ukisoma utaona Sulemani anasema, nikarudi na kuona chini ya jua, ikiwa na maana kuwa ni jambo ambalo amekuwa akiliona likitokea mara kwa mara duniani, hivyo akaona aandike, pengine na sisi tukilichunguza tunaweza kuliona, au pengine tulishawahi kuliona sehemu fulani.

Kwamba si wote wenye mbio, au ujuzi, au maarifa, au nguvu, ustadi au hekima mara zote zinawasaidia kupata mafanikio makubwa kuliko wale wengine wasiokuwa navyo. Na ndio maana hapo mwishoni mhubiri anamalizia kusema “lakini wakati na bahati huwapata wote”..Ikiwa na maana  majira hubadilika, leo elimu yako inaweza ikawa na faida ikakuletea mfanikio mengin lakini kesho, isiwe na maana sana, lakini yule mwingine ambaye hakuwa na elimu mambo yakambadilikia pengine kwa ujuzi wake tu wa kuzaliwa aliokuwa nao ukamfanya apate fursa nyingi kuliko wewe, na matokeo yake akawa juu yako.

Na ndio maana tunapaswa tujue majira hayo yanayobadilika yapo mikononi mwa Mungu, Bahati hizo anazitoa Mungu mwenyewe na sio mwanadamu.. Paulo alisema..

Warumi 9:16 “Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu”.

Vivyo hivyo na sisi, kwa kuwa hatujui ni majira gani yapo mbele yetu, basi tujifunze kuwa  wanyenyekevu chini ya Mungu atoaye mema yote, bila kuwadharau wengine, haijalishi tutakuwa na maarifa mengi kiasi gani kuwazidi wao, au elimu kubwa kiasi gani, au nguvu hatupaswi kujiona tumefika, vinginevyo, neno hili linaweza kutimia mbele ya macho yetu kwa wale tunaowadharau.

1Petro 5:6 “Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake”;

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments