Title July 2024

Orodha ya Miji ilivyojulikana Agano Jipya na inavyojulikana sasa

Ifuatayo ni orodha ya baadhi ya  Miji ya biblia katika AGANO JIPYA, jinsi ilivyojulikana na inavyojulikana sasa. 

(Ili kulisoma “Jedwali” lote, slide kuelekea kushoto)

Jina la Mji (Nyakati za biblia)Marejeo (Katika biblia)Jina la Mji sasa (Nyakati hizi)Nchi uliopo sasa
1. AdramitioMatendo 27:2BurhaniyeUturuki
2.Antiokia Matendo 11:26AntakyaUturuki
3.AntipatriMatendo 23:31Rosh HaAyin[Israreli (ya kati)
4.AsoMatendo 20:13BehramkaleUturuki
5.AtaliaMatendo 14:25AntalyaUturuki
6.Beroya Matendo 17:10VeriaUgiriki
7.KaisariaMatendo 23:23CaesareaIsraeli
8.KaudaMatendo 17:26GavdosUgiriki
9.KenkreaWarumi 16:1KechriesUgiriki
10.KorinthoMatendo 18:1KechriesUgiriki
11.KireneMatendo 11:20ShahhatLibya (Afrika)
12.GerasiMarko 5:1KursiIsraeli
13.IkonioMatendo 14:1KonyaUturuki
14.Laodikia Ufunuo 3:14EskihisarUturuki
15.LidaMatendo 9:32LodIsrareli (ya kati)
16.ListraMatendo 14:8KlistraUturuki
17.MitileneMatendo 20"14MytileneUgiriki
18.MiraMatendo 27:5DemreUturuki
19.NeapoliMatendo 16:11KavalaUgiriki
20.NikopoliTito 3:12PrevezaUgiriki
21.Pergamo Ufunuo 2:12BergamaUturuki
22.Filadelfia Ufunuo 3:7 AlaşehirUturuki
23.FilipiMatendo 16:12FilippoiUgiriki
24.TolemaiMatendo 21:7AcreIsraeli (Kaskazini)
25.PuteoliMatendo 28:13PozzuoliItalia (Rumi)
26.RegioMatendo 28:13Reggio CalabriaItalia (Rumi)
27.EfesoMatendo 19:35SelçukUturuki (Magharibi)
28.SardiUfunuo 3:1SartmustafaUturuki (Magharibi)
29.SmirnaUfunuo 2:8İzmirUturuki (Magharibi)
30.ThiatiraMatendo 16:14AkhisarUturuki (Magharibi)
31.ThesalonikeMatendo 17:1ThessalonikiUgiriki

Fuatilia tena hapa hapa, Orodha ya Miji ilivyojulikana AGANO LA KALE Hapa >>> Orodha ya majina ya Miji ya Biblia (Agano la kale) na Sasa

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ORODHA YA MITUME.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

MAJINA YA MANABII WANAWAKE

MANABII WA BIBLIA (Wanaume)

MAJINA YA MITUME WA BWANA YESU

Rudi Nyumbani

Print this post

MAOMBI YANGU YAFIKE KWAKO.

Mistari ya kujihamasisha kuzidi kuomba na kumsihi Bwana!

Zaburi 88:1 “Ee Bwana, Mungu wa wokovu wangu Mchana na usiku nimelia mbele zako.

2 MAOMBI YANGU YAFIKE MBELE ZAKO, Uutegee ukelele wangu sikio lako.

Zaburi 39:12 “Ee Bwana, usikie maombi yangu, Utege sikio lako niliapo, Usiyanyamalie machozi yangu. Kwa maana mimi ni mgeni wako, Msafiri kama baba zangu wote”.

Zaburi 54:2 “Ee Mungu, uyasikie maombi yangu, Uyasikilize maneno ya kinywa changu.

Zaburi 61:1 “Ee Mungu, ukisikie kilio changu, Uyasikilize maombi yangu”.

Zaburi 66:19 “Hakika Mungu amesikia; Ameisikiliza sauti ya maombi yangu

20 Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu, Wala kuniondolea fadhili zake.”

Zaburi 84: 8 “Bwana, Mungu wa majeshi, uyasikie maombi yangu, Ee Mungu wa Yakobo, usikilize”

Zaburi 86:6 “Ee Bwana, uyasikie maombi yangu; Uisikilize sauti ya dua zangu”.

Zaburi 88:13 “Lakini mimi nimekulilia Wewe, Bwana, Na asubuhi maombi yangu yatakuwasilia”.

Yona 2:7 “Roho yangu ilipozimia ndani yangu, Nalimkumbuka Bwana; Maombi yangu yakakuwasilia, Katika hekalu lako takatifu”.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618.

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?

KWANINI MUNGU HAJIBU MAOMBI?

FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU

Amka, Ee upanga, juu ya mchungaji wangu (Zekaria 13:7-9)

Je! Israeli wote wataokolewa siku ya mwisho kulingana na Warumi 11:26?

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! Uvimbe unatibika?

Jibu ni ndio.

Lakini sio njia zote zinaweza kutibu ugonjwa huo. Ni kweli madaktari hufanya kwa sehemu yao. Lakini Mungu hufanya zaidi, kwake yote hutibika.

Uvimbe wa aina yoyote ile, uwe ule wa kwenye mfuko wa uzazi, au kibofu, au  kwenye koo, au kichwa, au tumboni. Popote pale, maadamu ni uvimbe, haijalishi ukubwa wake, unaponyeka huo.

Na anayeweza kufanya hivyo ni YESU TU.

Tafsiri ya jina lake ni MWOKOZI. Ndiye aliyetumwa na Mungu mahususi kuwaokoa wanadamu na dhambi zao, pamoja na shida zao na magonjwa yao, alizaliwa kwa kusudi hilo tu moja. Hivyo maadamu yeye yupo huna haja ya kuwa na hofu.

Isaya 53:4 Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.  5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona

Huo ugonjwa alishauchukua zamani sana, kabla ya wewe kuzaliwa.  Alimponya Lazaro aliyekufa na ugonjwa, na kuzikwa na kuoza. Atakuponya na wewe, ambaye hata bado hujafa kwa ugonjwa huo. Ni kumwamini tu, basi,

Lakini hatua ya kwanza ni wewe kumpokea maishani mwako. Kukubali neema yake, kwa kutubu dhambi zako, kwa kumaanisha kabisa kuziacha, kisha yeye mwenyewe atakupa ondoleo la dhambi hizo, na utakuwa umeupokea uzima wa milele, Wala hatazikumbuka tena kuanzia siku hii ya leo na kuendelea.

Ikiwa upo tayari kupokea wokovu huu bure basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Ikiwa sasa tayari umeokoka. Basi unahitaji msaada ya kimaombi.

Piga namba uzionazo chini ya chapisho hili nasi tutakuombea (bure) na kwa imani utapokea uponyaji wako.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KANSA/SARATANI INATIBIKA.

SALA YA UPONYAJI/MAOMBI YA UPONYAJI.

UPONYAJI WA YESU.

JE! UKIMWI UNATIBIKA?

Rudi Nyumbani

Print this post

Kuhisi vitu vinatembea mwilini.

Yapo matatizo ya kimwili ambayo kwa tiba hutatulika, Ukiona unahisi vitu vinatembea mwilini kama vile wadudu, na kukusababishia madhara fulani mwilini lada kuchoka, mwili kuuma, ni vema ukaenda kwanza kuangalia afya yako kwa daktari, utashuariwa na kupewa tiba, Ukiona limetatulika basi ilikuwa ni shida ya kimwili.

Lakini ukiona tiba, haitatui haeleti majibu yoyote. Unahitaji msaada wa kiroho. Mara nyingi wanaokumbana na hali hii ya kuhisi vitu vinatembea mwilini, au sindano zipita zinachoma-choma, au kuhisi kitu kinatembea tumboni, au mgongoni, mikononi na miguuni, huwa ni dalili za mapepo kuwapo ndani yao.

Angalia, je, hali hiyo inapokutokea unakuwa katika mazingira gani? Je, kwenye maombi ndio huzidi? Je! Unapojaribu kusikiliza, au kusoma biblia? Ukiona hiyo hali inakujia halafu inaambatana na mambo kama kupoteza kumbukumbu, au unakuwa na hasira, au hofu, au ufanisi wako unapungua. Hizo ni dalili za mapepo. Hivyo hayana budi kuondolewa ndani yako.

Kumbuka mtu anafunguliwa kwanza kuwa kumkumbali Yule ambaye atamwokoa yaani YESU KRISTO. Hivyo jambo la kwanza ni wewe kumpokea moyoni mwako. Kwa msaada huo waweza fungua hapa, upata wokovu >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Lakini kwa msaada wa ki-maombi (bure), wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini mwa makala hii, na Bwana atakufanya huru kwelikweli.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

DALILI TISA (9) ZA PEPO KUWEPO NDANI YA MTU.

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Tafsiri ya Wakolosai 2:18 Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu,

SWALI: Nini maana ya vifungu tunavyovisoma katika Wakolosai 2:18,

 ‘Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili;


JIBU: Tukianzia mistari ya juu anasema..

16  Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;

17  mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo. 18 Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili;

Katika vifungu hivyo, Mtume Paulo anaanza kwa kuwaambia ‘mtu asiwanyang’anye thawabu yenu’. Akiwafananisha na wana-michezo ambao wanashiriki katika mashindano Fulani, ambao hujitahidi kwa kila namna kujizuia, na kujichunga ili wafanye vema katika mashindano hayo wachukue tuzo.

Sasa Paulo, anatoa angalizo, akirejea mfano wa washindani hao, yawezekana mwingine akamfanyia hila mwenzake, ili asiwe na ufanisi, kwenye michezo hiyo akashindwa kushiriki vema na kuchukua tuzo, kwamfano anaweza kumpa kinywaji Fulani ambacho kitadhoofisha uchezaji wake, au atamdanganya afanya zoezi Fulani,  ambalo anajua kabisa halina manufaa kwake, kwamfano labda mchezaji ni mwana-riadha, utaona Yule mwingine anamwambia akanyanyue vyuma vizito atakuwa mwepesi kukimbia. Kumbe kukimbia hakuhusiani na misuli mikubwa bali pumzi.

Vivyo hivyo Paulo aliona kuwa kuna waalimu wa uongo, viongozi wa uongo,watakaozuka, kuwadanganya watu waiache njia sahihi, ya kukubaliwa na Mungu. Na ndio hapo anataja  mambo matatu ambayo watakuwa nayo;

Jambo la kwanza,

Watachukua thawabu yao kwa kunyenyekea kwa mapenzi yao wenyewe tu,

Kunyenyekea sio kubaya, ni tunda la Roho Mtakatifu ndani ya mtu, na wakristo wote, tunasukumwa katika unyenyekevu. Lakini angalia hapo anasema kunyenyekea KWA MAPENZI YAKE MWENYEWE. Maana yake, ni kuwa hanyenyekei kwa mapenzi ya Mungu, bali yake. Na hiyo ni mbaya, kwasababu watu wa kidini leo hii ndio kanuni yao, hubuni njia zao za kumwabudu Mungu, na hiyo huwavutia watu wengi, waone kama ni Mungu kweli anaabudiwa, kwa unyenyekevu na heshima, nao wanaingia kwenye mkondo huo. Wanasahau kuwa ibada lazima ifanyike kwanza katika Roho na Kweli.

Mambo kama kusujudia, kuvaa mavazi Fulani meupe, kutawadha mwili, kuvua viatu katika nyumba za ibada, kuomba kwa sauti ya kuvuta sana, ya upole, huku umeinamisha kichwa chini, unaibusu biblia. Hudhanikuwa kuwa ndio hicho Mungu anakitaka,  Lakini ndani, kinywa chake kina matusi, akitoka hapo anakwenda kuishi maisha kishirikina, na ulevi.  Huo ni udanganyifu mkubwa sana.

Ndicho Paulo alichokiona kwa kanisa la Kolosai, kulitokea watu wanawaambia usile kambale ni chukizo kwa Mungu, shika siku  ya sabato, inatosha.. Yote hayo yakifanyika kimwili. Lakini wasifundishe kwamba unyenyekevu wa ki-Mungu hutoka rohoni, ukisukumwa na neema katika  Roho Mtakatifu, Ambapo mtu kupaswa kukubali wokovu kwanza, na kutii kwa kumfuata Kristo anayeweza kumfanya mtu kiumbe kipya, na sio jambo la kufanya kimwili tu, akidhani atampendeza Mungu.

Jambo la pili

 wanaweza kuwanyang’anya thawabu yao kwa mafundisho ya kuabudu malaika.

Tangu zamani, kulikuwa na watu waliowaweka malaika katika nafasi ya Mungu. Na kuvuka ile mipaka ya kutuhudumia tu sisi  (Waebrania 1:14). Hivyo ikiwa mtu alikuwa na karama Fulani ya maono, ambapo mengine huletwa kwa mikono ya malaika, tunaliona hilo mara nyingi tangu Musa, na wana wa Israeli jangwani, pamoja na mitume mpaka Yohana kule Patmo. Mungu aliwatumia malaika kwa sehemu kubwa kutufikishia sisi jumbe zake, kwasababu waliwekwa kutuhudumia sisi.

Lakini dini na imani zikazuka kuanzia hapo, kwa baadhi ya watu wakaanza kuwafanyia ibada, jambo ambalo ni chukizo kwa Bwana. Hata leo utaona zipo sala za malaika na watakatifu kuwataka wawaombee. Au wawasaidie vitani. Ikiwa wewe ni mtoto wa Mungu umeokoka, kuwa makini na ibada hizo, taabu yako kwa Mungu yaweza kuwa bure, kwasababu unamudhi Mungu. Ibada za namna hiyo hazina tofauti na ibada za majini. Usiabudu mwanadamu, wala kiumbe chochote kilicho mbinguni wala duniani.

Jambo la tatu

Na mwisho anasema wakijivuna bure kwa akili zao za mwili.

Kujivuna, maana yake kusifia vitu vya mwilini mfano vipaji vyao, wengine ujuzi wa kuongea vizuri, na kupangalia maneno, werevu, elimu za falsafa, mambo ambayo Paulo aliyaona, yakiwavuta wengi, na kuacha njia kamilifu ya Kristo iliyo katika neema, upendo,  Imani na nguvu za Mungu. (2Wakorintho 11:18-20).

Injili inabadilishwa inakuwa vichekesho, na kanuni za ki-ujasiriamali,

Hata leo mimi na wewe ni kuwa makini, bidii yako katika Kristo isichukuliwe na udini, bali Neno, isichukuliwe na maono na karama, na ibada za malaika bali Mungu, isichukuliwe na falsafa za kibinadamu, na mwonekano, bali, Roho Mtakatifu na kweli, katika neema.

mtu asichukue taji lako

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 2)

Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?

Rudi Nyumbani

Print this post

Malimbuko ya Akaya maana yake nini? (1Wakorintho 16:15).

Swali: Haya malimbuko ya Akaya tunayoyasoma katika 1Wakorintho 16:15 yalikuwaje?

Jibu: Turejee..

1Wakorintho 16:15 “Tena ndugu, nawasihi; (mnawajua watu wa nyumbani mwa STEFANA kwamba ni MALIMBUKO YA AKAYA, nao wamejitia katika kazi ya kuwahudumu watakatifu)”.

“Akaya” inayotajwa hapo si mtu, bali ni eneo/mji uliopo maeneno ya Ugiriki kwa sasa. Mji huu umetajwa pia katika Matendo 18:12, Matendo 19:21, 2Wakorintho 1:1, 1Wathesalonike 1:7-8 na Yuda 1:6.

Mji huu wa Akaya, ulikuwa ni moja ya miji ambayo Mtume Paulo alipita kuhubiri injili ya BWANA YESU. Na mmoja wa watu wa kwanza kabisa kumpokea Bwana YESU na kuokoka katika Mji huo ni huyu mtu aliyeitwa STEFANA pamoja na nyumba yake yote.

Hawa ndio walikuwa watu wa kwanza kabisa kuipokea injili katika mji huo, na baadaye wakaongezeka wengine wengi. Hiyo ndio maana ya Malimbuko iliyotajwa hapo… Sio malimbuko ya mazao ile inayotajwa katika Kutoka 22:29, bali inayomaanisha “wa kwanza kupokea injili”.. kwamaana maana tu ya malimbuko ni “kuzaliwa kwa kwanza”, hivyo hawa watu walikuwa ni wa kwanza kuzaliwa katika injili katika mji huo wa Akaya.

Lakini sifa nyingine ya kipekee aliyokuwa nayo huyu Stefana pamoja na nyumba yake yote ni roho ya UKARIMU, ambayo waliionyesha sana kwa Paulo na watumishi wengine waliokwenda kuhubiri injili katika miji hiyo, walikuwa tayari kutoa vya kwao ili kuwatunza watumishi wa Mungu.

Na kwa tabia hiyo, ndiyo Mtume Paulo kwa kuongozwa na roho anawaagiza watu wa Korintho pamoja na sisi kwa ujumla tuige tabia kama hiyo na pia tuwatii sana watu wanaojitoa kwaajili ya kuishika mkono kazi ya Mungu, na pia tuwe tayari kushirikiana nao..

1Wakorintho 16:14 “Mambo yenu yote na yatendeke katika upendo.

15  Tena ndugu, nawasihi; (mnawajua watu wa nyumbani mwa Stefana kwamba ni MALIMBUKO YA AKAYA, nao wamejitia katika kazi ya kuwahudumu watakatifu);

16  WATIINI WATU KAMA HAWA, NA KILA MTU AFANYAYE KAZI PAMOJA NAO, NA KUJITAABISHA.

17  Nami nafurahi kwa sababu ya kuja kwao Stefana na Fortunato na Akaiko; maana hawa wamenikirimia kwa wingi yale niliyopungukiwa kwenu”

Bwana atubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

SADAKA YA MALIMBUKO.

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

Yerusalemu ni nini?

HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.

IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.

Rudi Nyumbani

Print this post

UFUATILIAJI NI SEHEMU YA HUDUMA MUHIMU KWENYE UINJILISTI

Matendo  11:25

Kisha akatoka akaenda Tarso kumtafuta Sauli;

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, napenda leo tujifunza jambo moja ambalo huwenda linasahaulika miongoni mwetu kama watendakazi shambani mwa Bwana.

Hatuna budi kufahamu ,ufuatiliaji huenda sambamba na uinjilisti. Twaweza hubiria watu wakaokoka, wakamjua Kristo, wakati mwingine wakaweza hata kujisimamia wenyewe, lakini tusipojijengea tabia ya kuwafuatilia na kukaa nao, kuwaimarisha, basi kazi yetu yaweza kuwa bure, au isiwe na matunda mazuri kama ipasavyo.

tunajifunza kwa mtu mmoja aliyeitwa Barnaba, aliyejulikana pia kama mwana wa faraja. Huyu aliithamini huduma hii. Baada ya kusikia kuwa Paulo, amegeuka na kuwa mkristo, lakini akaenda mahali panaitwa Tarso, mbali kidogo na kanisa, Barnaba aliona si vema amwache huko. Ikabidi afunge safari yeye mwenyewe kutoka Antiokia aende kumtafuta.

Hatujui safari yake ilichukua siku ngapi, wiki ngapi, miezi mingapi. Lakini hatimaye akampata ..Alipomwona huwenda hakuridhishwa na mazingira ya kihuduma aliyokuwa nayo, hakuridhishwa na hali ya kiroho aliyokuwa nayo. Kwasababu hata mtume Paulo kuondoka Yerusalemu ilikuwa si kupenda kwake ni kutokana pia na kukataliwa na kanisa, na hatari ya kuuliwa na wayahudi.

Lakini Barnaba alipomuona. Akamchukua amlete mahali bora zaidi, ambapo kanisa lipo hai. Akafika akaendelea na huduma, akaanza kuwa moto tena na kutokea hapo ndipo Mungu alipomfanya mhubiri wa kimataifa.

Leo hii tunasoma ushujaa wa Paulo, lakini kusimama kwake kulichangiwa na nguvu ya kufuatiliwa kwa waliomtangulia kiroho.

Je na sisi tumejiwekea desturi hii? kuwafuatilia mara kwa mara tunaowashuhudia injili?

Kamwe usimdharau mwongofu mpya, hata kama atakuwa anasua-sua, au mdhaifu sasa. Fahamu kuwa huyo ndio Paulo wa baadaye. Usihubiri tu ukaacha, ukadhani atajikuza mwenyewe.  Shughulika naye, omba naye, mfuate alipo, mfundishe, ikiwezekana mwamishe eneo alilopo ikiwa linamfanya asisimame kiroho. Na kazi yako itazaa matunda, usichoke.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

MAMBO NANE (8), AMBAYO WEWE KAMA KIONGOZI UTAIGWA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Ijapokuwa amekufa, angali akinena(Waebrania 11:4)

SWALI: Maandiko yanaposema Habili ijapokuwa amekufa angali akinena, je! Ananenaje, wakati yeye ni marehemu. Je! Hiyo inamaana wazee wetu wa zamani wanaweza kunena na sisi?

Waebrani 11:4  Kwa imani Habili alimtolea Mungu dhabihu iliyo bora kuliko Kaini; kwa hiyo alishuhudiwa kuwa ana haki; Mungu akazishuhudia sadaka zake, na kwa hiyo, ijapokuwa amekufa, angali akinena


JIBU: Kibiblia ni kweli kabisa watakatifu waliokufa kale hunena nasi. Lakini kunena kwao ni tofauti na huku kunakodhaniwa, kwamba mzimu unakutokea kwenye ndoto, au unasikia sauti ya petro makaburini ikizungumza na wewe,  Hapana, ukiona hivyo ujue huzungumzi na huyo mtu, bali ni pepo.

Sasa watakatifu waliokufa wanazungumzaje na sisi?

Ni kwa ushuhuda waliouacha. Maisha yao na maagizo yao, ndio huzungumza nasi, sikuzote, kana kwamba tupo nao sasa, kwa mafundisho yao yaliyopo  mpaka sasa kana kwamba tunawaona wenyewe kumbe wamekufa.

Ndio maana ile habari ya Yule tajiri wa Lazaro, tunaambiwa alipofika kule kuzimu akaomba mtu atolewe kwa wafu awahubirie injili, akakataliwa, kuonyesha kuwa hakuna mtu aliyekufa mwenye uwezo wa  kuja tena kuzungumza na sisi, nafasi hiyo haipo kwao. Lakini waliambiwa WANAO MUSA NA MANABII, WAWASIKILIZE.

Luka 16:29  Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.

Maana yake ni kuwa sio kwamba Musa kweli alikuwepo duniani, au manabii wa kale kama Isaya walikuwa duniani kwa wakati huo, anaambiwa hayo maneno. Lakini shuhuda zao na mahubiri yao, huwawakilisha wao. Tunaweza kusema “ijapokuwa wamekufa wangali wakinena”

Ndivyo ilivyo kwa Habili, ijapokuwa aliuliwa na ndugu yake, lakini IMANI yake inasema nasi mpaka leo. Mitume wa Kristo ijapokuwa hawapo duniani lakini sauti zao tunazisikia hadi sasa.

Lakini pia kuna mahali pengine biblia inasema damu ya Yesu hunena mema kuliko ya Habili (Waebrania 12:24). Kufahamu kwa kina damu ya mtakatifu  hunenaje? Pitia somo hili. >>> DAMU YA ZAKARI BIN BARAKIA.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.

ALIPOKUWA ANGALI MBALI, BABA YAKE ALIMWONA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Yakobo alimaanisha nini kusema ‘ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu’ Mwanzo 28:21

Mwanzo 28:21

[21]nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu, ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu.


JIBU:

Sura hiyo inaeleza ugumu wa safari ya Yakobo alipokuwa anamkimbia ndugu Yake Esau kuelekea nchi ya ugenini ya baba zake. 

Hivyo akiwa huko jangwani peke yake, haoni mbele wala nyuma, haoni msaada kwa mtu wala kitu, ndipo akamwekea Mungu nadhiri, na kumwambia maneno hayo. 

‘nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu, ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu’. 

Lakini swali linakuja je hakumwamini Mungu, au kumfanya Mungu wake mpaka hapo ambapo angetimiziwa nadhiri zake? Kwamaana baada ya miaka 20, ndio tunaona yakitimia hayo yote? je hiyo miaka yote ya hapo katikati YEHOVA hakuwa Mungu wake, mpaka wakati ambapo angetimiziwa nadhiri yake?

Jibu: mstari huo haumaanishi kwamba Yakobo alikuwa anamweka kwanza Mungu kwenye majaribio halafu akishamfanikisha ndipo amfanye rasmi kuwa Mungu wake.

Hapana, ingekuwa hivyo tusingeona  katika kipindi hicho chote Yakobo akimtumainia Mungu wa baba zake, angeendelea tu na mambo yake mpaka huo wakati ufike.Lakini tunaona Yakobo hakucha kumwamini Mungu mahali popote.

Katika kauli hiyo hapo Yakobo alikuwa anaongezea tu, kujitoa kwakwe zaidi kwa Mungu, endapo  atarudishwa salama, na ndio maana maana ukiendelea vifungu vinavyofuata..

anasema atamtolea Mungu wake Fungu la kumi kwa kila atakachokipata..

jambo ambalo hapo mwanzo asingeweza kwasababu alikuwa hana chochote.

Mwanzo 28:21-22

[21]nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu, ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu.

[22]Na jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu; na katika kila utakalonipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi. 

Kwa namna nyingine..anamwambia Mungu nitafanya vizuri zaidi kwako, endapo nitarudi salama, kutoka katika nchi ya ugenini.

Au ni sawa na leo mtu aseme Bwana nitakutumikia endapo utaniondolea huu ugonjwa wangu wa kupooza. 

Hiyo haimaanishi kuwa amemwekea Mungu masharti, kwamba sasahivi hataki mtumikia mpaka aponywe hapana, lakini anaeleza kikwazo chake. Na kwamba kikiondolewa ataweza timiza vizuri matakwa yake ya kiutumishi. Ndicho alichokimaanisha Yakobo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

USIMPE NGUVU SHETANI.

Kutoka 21:10 ina maana gani?.

Print this post

TABIA SITA (6) ZA WANAFUNZI WA YESU.

Zifuatazo ni baadhi ya tabia za kuigwa walizokuwa nazo wanafunzi wa Bwana YESU ambazo nasi tunapaswa tuzionyeshe.

1. WALIJIKANA NAFSI ZAO.

Hii ni sifa ya kwanza waliyokuwa nayo wanafunzi wa YESU, Kwani mtu aliyekosa hii sifa hakuweza kuwa mwanafunzi wake.

Luka 14:27 “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.

Halikadhalika na sisi kama wanafunzi wa Bwana ni sharti tujikane nafsi kila siku, na kubeba msalaba. (Zingatia hilo neno, “Kila siku”), na si siku moja tu..

Luka 9:23 “Akawaambia wote, Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate”.

2. WALIKAA KUFUNDISHWA NA BWANA.

Maana ya kuwa mwanafunzi ni kuketi na kufundishwa mpaka kuhitimu. Na wanafunzi wa Bwana YESU walilijua hilo, hivyo walikuwa walijiunga na chuo hicho cha Bwana ili kupokea mafunzo.

Na leo ni hivyo hivyo, Mwalimu wetu ni ROHO MTAKATIFU na chuo chetu ni Biblia. Na kila mtu ni lazima apite chini ya chuo hicho, ili aweze kuwa mwanafunzi wa Bwana.

3. WALIMFUATA BWANA KILA ALIKOKWENDA.

Maisha ya Bwana YESU hayakuhusisha kukaa mahali pamoja, bali kuzunguka huku na kule, katika miji na vijiji kuhubiri injili.

Mathayo 9:35 “Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina”.

Hata wanafunzi wasomao chuo, upo wakati wanaenda katika mafunzo kwa njia ya vitendo kabla ya kuhitimu (maarufu kama mafunzo ya field).

Na vivyo hivyo na sisi kama wanafunzi  ni lazima tuifanye kazi ya Bwana kwa yale tuliyoyapokea hata kama hatubobea katika hayo..

Lakini utaona leo, mtu hataki kuwahubiria wengine kwa hofu ya kwamba yeye hajui….Ni kweli usifundishe usichokijua lakini kile kidogo ambacho umeshakijua, usikifukie chini bali kawape wengine wasiokijua kabisa.

4. WALIMTII BWANA.

Tabia nyingine ya mwanafunzi Halisi ni UTII na NIDHAMU.

Wanafunzi wa Bwana YESU wale 11 walimtii Bwana kwakila jambo, kuanzia maagizo ya ubatizo, kuhubiri, meza ya Bwana na mengineyo.

Na wote walimwogopa Bwana (hakuna aliyedhubutu kuhojiana naye wala kushindana naye) Luka 9:45.

5. WALIMWAMINI BWANA.

Wanafunzi halisi wa Bwana YESU hawakuwa na mashaka mashaka na Bwana YESU…walimwamini moja kwa moja…

Yohana 2:11 “Mwanzo huo wa ishara Yesu aliufanya huko Kana ya Galilaya, akaudhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini”

6. WALIMVUMILIA BWANA

Hata kama yalikuwepo mambo ambayo yalikuwa ni magumu kueleweka kwa katika hali yao.ya uchanga…lakini walivumilia wakiamini siku moja watakuja kuelewa vizuri..

Yohana 6:67 “Basi Yesu akawaambia wale Thenashara, Je! Ninyi nanyi mwataka kuondoka?

68 Basi Simoni Petro akamjibu, Bwana! Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.”

Na sisi kama wanafunzi wa YESU hatupaswi kurudi nyuma,  tunapokutana na mambo tusiyoyaelewa katika imani au maandiko..badala yake tunapaswa kuwa wavumilivu kwa matumaini mazuri yajayo.

Na kumbuka maana ya kuwa MRISTO ni kuwa MWANAFUNZI…Huwezi kusema ni mkristo na sio mwanafunzi.

Matendo ya Mitume 11:26 “hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi waliitwa Wakristo kwanza hapo ANTIOKIA”.

BWANA ATUSAIDIE.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU.

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

Rudi Nyumbani

Print this post