Je! Israeli wote wataokolewa siku ya mwisho kulingana na Warumi 11:26?

Je! Israeli wote wataokolewa siku ya mwisho kulingana na Warumi 11:26?

Jibu: Tusome,

Warumi 11:25 “ Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake”

Ni kweli upo unabii wa Israeli wote kuokolewa katika siku za mwisho, kuna kipindi ambacho injili itahamia katika Taifa la Israeli baada ya unyakuo kupita!..wakati huo kanisa la mataifa litakuwa limeshanyakuliwa, Ndipo injili itaanza kuhubiriwa tena katika Taifa la Israeli na wale manabii wawili tunaowasoma katika kitabu cha Ufunuo 11, watahubiri kama nyakati za Yohana Mbatizaji isipokuwa zama hizo itakuwa ni kwa ishara nyingi na miujiza mfano wa ile ya Musa na Eliya.

Na kupitia injili ya hao manabii wawili, waisraeli wengi watamkubali Yesu kama Masihi, kumbuka kwasasa wayahudi wengi (yaani waisraeli wengi), hawaamini kuwa Yesu Yule aliyekuja na kufa na kufufuka kuwa ndiye Masihi aliyetabiriwa na manabii zamani, wanaamini kuwa Masihi bado hajaja, na Yesu sio Masihi, hivyo wanamsubiria mwingine!!..Biblia inasema macho yao yamefumbwa wasimtambue Yesu kuwa ndiye Masihi, ili sisi watu wa mataifa tupate neema. (Warumi 11:30-31).

Sasa swali la Msingi hapo, ni je Israeli wote wataokolewa?..hata kama ni watenda maovu?..na je kitendo tu cha kuzaliwa  Muisraeli tayari umeshapewa tiketi ya kuurithi uzima  wa milele?.

Jibu ni La!… Sio wote watakaookolewa, kwasababu wapo waisraeli wasioamini kabisa hata kama Mungu yupo, wapo wachawi na manabii wa uongo katikati ya jamii za Israeli mfano wa akina Bar-Yesu (Matendo 13:6), hao hawataokolewa na wataenda katika ziwa la moto, kama hawatatubu!..

Sasa kwanini hapo biblia iseme ni  “Israeli wote”, na si baadhi!.. kama watakuwepo baadhi ambao hawataokolewa?, kwanini iseme wote?.. Ili kuelewa vyema tusome mstari ufuatao.

Warumi 9:6  “Si kana kwamba neno la Mungu limetanguka. MAANA HAWAWI WOTE WAISRAELI WALIO WA UZAO WA ISRAELI.

7  Wala hawawi wote wana kwa kuwa wazao wa Ibrahimu, bali, Katika Isaka wazao wako wataitwa; ”

Unaona hapo?.. Sio Waisraeli wote ni waisraeli, ni sawa na kusema “Si wote wanaojiita au wanaojulikana kuwa ni wakristo ni wakristo”. Sasa hivi duniani kuna zaidi ya mabilioni ya wakristo. Lakini kiuhalisia “Wakristo wa kweli ni wachache”, ni wale wanaozishika amri za Mungu na kufanya mapenzi yake, hao wengine ni wakristo jina tu!. Kwahiyo kwenye biblia kungekuwa na mstari unaosema “wakristo wote wataokolewa” bila shaka, ingekuwa imemaanisha “wale wakristo wa kweli” na si wakristo jina!.. mtu anayejiita mkristo lakini mchawi, hawezi kuurithi uzima wa milele, mtu anayejiita mkristo lakini ni mzinzi vivyo hivyo!

Kadhalika biblia iliposema “Israeli wote wataokolewa” ilimaanisha wale “wale waisraeli kweli kweli” ambao wanakwenda katika sheria za Mungu bila kupinda panda. Hao ndio wote watakaookolewa. Mfano wa hao ni wakina Nathanieli katika Yohana 1:47 “Basi Yesu akamwona Nathanaeli anakuja kwake, akanena habari zake, Tazama, MWISRAELI KWELI KWELI, hamna hila ndani yake”

 Lakini wengine wasiompenda Mungu, maana yake ni waisraeli jina tu!, Lakini sio waisraeli hasa!!, hao hawataokolewa, Ndicho Mtume Paulo alichokuwa anakimaanisha hapo katika Warumi 9:6 kuwa “….HAWAWI WOTE WAISRAELI WALIO WA UZAO WA ISRAELI”.

Vivyo hivyo hawawi wote wakristo, walio wa uzao Kristo!!. Walio uzao wa Kristo ni wale waliozaliwa mara ya pili, hao ndio Wakristo, wengine ni wakristo jina tu!..

Je wewe ni Mkristo halisi au mkristo jina tu!.. Mkristo jina ni Yule anayekwenda kanisani lakini anafanya uzinzi kwa siri, ni yule mwenye jina la kikristo lakini ni mtu wa kidunia, mkristo jina ni Yule anayeupenda ulimwengu kuliko kumpenda Mungu, mkristo jina ni yule asiyechukua msalaba wake na kumfuata Yesu. Lakini mkristo kweli kweli ni Yule aliyeukataa ulimwengu, anayejitwika msalaba wake kila siku na kumfuata Yesu kwa gharama zozote.

Bwana atusaidie tuwe wakristo halisi!

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

AINA TATU ZA WAKRISTO.

AINA TATU ZA WAKRISTO.

Je Musa kumwoa Sipora, Mkushi alifanya dhambi?

LIPI TUNAJIFUNZA KWA WALIOMWONA YESU ALIYEFUFUKA?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments