Title October 2022

Je! Siku ilihesabiwaje kabla ya jua na mwezi kuumbwa?

Swali: Katika kitabu cha Mwanzo tunasoma jua na mwezi viliumbwa katika siku ya 4 , sasa napenda kujua kabla ya hapo siku zilihesabiwaje, maana jua ndilo linalotenga mchana na usiku…na maandiko yanatuonyesha kuwa lilikuja kuumbwa siku ya 4?

Jibu: Ni kweli jua na mwezi viliumbwa siku ya 4, tena baada ya miti na miche ya kondeni kuumbwa (Mwanzo 1:14).

Lakini ukisoma kuanzia mstari wa pili katika kitabu hiko cha Mwanzo, utaona Mungu tayari alikuwa ameshaumba mchana na usiku na ameshatenga giza na nuru.

Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.

2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.

4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; MUNGU AKATENGA NURU NA GIZA.

5 MUNGU AKAIITA NURU MCHANA, NA GIZA AKALIITA USIKU. IKAWA JIONI IKAWA ASUBUHI, SIKU MOJA”.

Umeona?..kumbe tayari Mungu alikuwa ameshaumba mchana na usiku kabla hata ya kuumba jua. Maana yake hata kama asingeumba jua bado majira na mchana na usiku yangekuwepo kwasababu yeye mwenyewe ndio Nuru ya ulimwengu (mwilini na rohoni).

Yohana 8:12 “Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima”.

Ndio maana katika ile mbingu mpya na nchi mpya hakutakuwepo  na jua na bado Nuru itakuwepo.

Ufunuo 21:23 “Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-Kondoo”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kuwa Mungu aliumba mchana na usiku, kabla ya kuliumba jua..na hiyo ni kuonyesha utukufu wake yeye, na pia kuonyesha kuwa yeye ndiye Nuru halisi Na ndio chanzo cha Nuru yote.

Je umempokea Bwana Yesu aliye Nuru ya kweli? Kama bado fahamu kuwa bado upo gizani ijapokuwa jua linakumulika…kwahiyo ni vyema ukafanya maamuzi thabiti leo ya kumpokea na kuokoka.

Yohana 12:46 “Mimi nimekuja ili niwe nuru ya ulimwengu, ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani”

Soma pia Yohana 9:5 na Yohana 11:9.

Bwana Yesu akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?

HAMA KUTOKA GIZANI

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Biblia inamaanisha nini iliposema “wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa;?

Je mke wa Musa alikuwa ni Mweusi?

Rudi nyumbani

Print this post

KWA WINGI WA WASHAURI HUJA WOKOVU.

Nakusalimu katika jina kuu lenye uweza la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya Mungu ambayo ndio uzima wetu.

Mungu ana njia nyingi za kuzungumza, anaweza kutumia ufunuo wa roho, anaweza kutumia Neno, anaweza kutumia maono anaweza kutumia mambo ya asili au matukio. Lakini si wakati wote Mungu ataleta majibu kwa kupitia njia hizo. Haijalishi utakuwa ni wa kiroho kiasi gani. Ipo njia nyingine ambayo Mungu huitumia na hiyo tusipoifahamu vema, tutapata hasara ya mambo mengi kama sio kupotea kabisa. Na njia yenyewe ni kupitia mashauri yetu sisi wenyewe tunapokuwa wengi pamoja..

Kwamfano embu tafakari hivi vifungu;

Mithali 11: 14 “Pasipo mashauri taifa huanguka; Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu”

Maana yake ni nini? Kwamba taifa linapokataa maoni, mapendekezo, mawazo mbalimbali, kutoka kwa wananchi wake, kamwe taifa hilo haliwezi kufanikiwa,

Maandiko bado yanasema..

Mithali 15: 22 “Pasipo mashauri makusudi hubatilika; Bali kwa wingi wa washauri huthibithika”.

Mithali 24:6 “Maana kwa mashauri ya akili utafanya vita; Na kwa wingi wa washauri huja wokovu”.

Maana yake ni nini? Kwamba palipo na vita, ni lazima yawepo maono ya askari wengi, ni jinsi gani watapambana na adui yao, huyu anasema hivi, Yule vile, na mwisho wa siku linatoka jawabu moja madhubuti ambalo litaleta mafanikio makubwa, lakini ikiwa pendekezo linatoka kwa mmoja tu yaani yule mkuu wa kikosi, ni dhahiri kuwa jeshi, litakuwa dhaifu, na matokeo yake ni kupigwa..

Amen.

Hili ni jambo la muhimu sana kwa sisi tulio wakristo. Bwana Yesu aliposema tuwe na umoja, tunie mamoja, alijua kabisa atatumia njia hiyo kuleta majibu ya mambo mengi pasipo hata kusubiria mafunuo au maono.

Utauliza jambo hili lilifanyika wapi katika kanisa kwenye agano jipya.

Utakumbuka, Paulo na Barnaba walipokwenda kuhubiri injili kwa watu wa mataifa, walitokea wayahudi kadha wa kadha, wakaanza kuwaambia mataifa kuwa msipotahiriwa ninyi hamwezi kuokoka()..Hivyo jambo hilo likaleta mkanganyiko mkubwa sana, ikawabidi hadi Paulo na Barnaba warudi Yerusalemu wakasikilize mitume na wazee wanasema nini juu ya hilo.

Hivyo walipofika Yerusalemu, akina Petro na wazee, waliitisha baraza, na kuanza kulitathimini jambo hilo. Je ni sawa watahiriwe na kuishika torati ya Musa au sio sawa.. Sasa maandiko yanatuambia walihojiana sana, huyu anasema hivi, yule vile (Lakini katika amani na upendo, na sio katika mashindano).. na matokeo yake Roho wa hekima akaingia ndani yao, likapatikana shauri moja thabiti. Na kwa kupitia hilo kanisa la mataifa likathibitika sana kwa waraka waliowaandikia, likaenenda katika furaha ya Roho Mtakatifu daima.

Embu tusome pale kidogo, litusaidie…

Matendo 15:7  “NA BAADA YA HOJA nyingi Petro akasimama, akawaambia, Ndugu zangu, ninyi mnajua ya kuwa tangu siku za kwanza Mungu alichagua miongoni mwenu ya kwamba Mataifa walisikie neno la Injili kwa kinywa changu, na kuliamini.

8  Na Mungu, ajuaye mioyo ya watu, akawashuhudia, akiwapa Roho Mtakatifu vile vile kama alivyotupa sisi;

9  wala hakufanya tofauti kati yetu sisi na wao, akiwasafisha mioyo yao kwa imani…..

13  Na hao walipokwisha kunyamaza Yakobo akajibu, akisema, Ndugu zangu, nisikilizeni.

14  Simeoni ametueleza jinsi Mungu hapo kwanza alivyowaangalia Mataifa ili achague watu katika hao kwa ajili ya jina lake.

15  Na maneno ya manabii yapatana na hayo, kama ilivyoandikwa, 16  Baada ya mambo haya nitarejea, Nami nitaijenga tena nyumba ya Daudi iliyoanguka. Nitajenga tena maanguko yake, Nami nitaisimamisha;”

Kwa muda wako isome habari yote katika kitabu hicho cha Matendo ya mitume sura ya kumi na tano (15),

NINI BWANA ANATAKA SISI TUJUE  KAMA KANISA?

Lazima  tujifunze wakati mwingine tuwe watu wa Hoja nyingi, mapendekezo mengi, (lakini katika upendo na amani), ili kanisa lijengwe, ili injili ihubiriwe katika ufasaha wote. Kama tulivyosoma hapo juu inavyosema.. “kwa mashauri ya akili utafanya vita; Na kwa wingi wa washauri huja wokovu.” Hatutaweza kushindana na shetani kama tutakuwa hatuna mikakati, na mipango ya mara kwa mara,.

Kila kiungo katika mwili wa Kristo, kina nafasi ya kuchagia mashauri mema. Hivyo tujifunze njia hii, ili Mungu azungumze na sisi. Lakini tukikosa mapatano, “Taifa huangamia”..Sisi hatutaangamia kwa kutii agizo hili.

Bwana alibariki kanisa lake.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

Ni kwa namna gani, upendo husitiri wingi wa dhambi? (1Petro 4:8)

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

MITHALI AU METHALI ZA BIBLIA

Rudi nyumbani

Print this post

NAYAJUA MATENDO YAKO.

Mara kadhaa, Bwana Yesu kabla hajasema Neno lolote alianza kwanza na kauli hii “Nayajua matendo yako” Kwamfano Soma vifungu hivi uone alivyosema, (Ufunuo 2:2, 2:19, 3:1, 3:8).

Nikwanini aanze kwa kusema hivyo? Ni kwasababu anataka hilo tuliweke akilini, tufahamu kuwa yupo karibu sana na hatua zetu kuliko tunavyoweza kudhani, hususani zile ambazo tunafikiri kuwa yeye hazijui, au hazioni.  Tutawaficha wanadamu lakini yeye kamwe hatuwezi kumficha chochote.

Wewe ni mchungaji, unazini na washirika, unazungumza lugha za mizaha na wake za watu, unadhani Kristo hajui nia yako, halafu unasimama madhabahuni unahubiri habari za wokovu..Bwana anakupa onyo, tena kali sana, anayajua matendo yako, na hasira yake ipo juu yako.

Wewe ni mkristo, unasema umeokoka, umebatizwa, unashiriki meza ya Bwana, lakini kwa siri unatazama picha za ngono, unafanya uasherati..Ukija kanisani unasema Bwana Asifiwe! Tena bila aibu unasimama na madhabahuni kuimba..utamficha mchungaji, utawaficha washirika wote, utamficha hata na shetani..Lakini Yesu anayajua matendo yako nje-ndani..Anajua mnapokutania, mnapotekelezea mipango yenu miovu, anajua ni nini unachofanya unapokuwa chumbani mwenyewe.

Wewe ni mwanandoa, unaigiza kwamba unampenda mwenzi wako, muwapo pamoja, lakini akisafiri kidogo tu, mkiwa mbali, unachepuka, mke umetoa mimba nyingi, na huko nje wewe mume umezaa watoto, hata mkeo haujui, unadhani unamficha  nani rafiki? .

Leo hii lipo kundi kubwa la washirikina  miongoni mwa watakatifu, tukiachilia mbali wachawi, lakini cha ajabu hujawahi kumsikia hata mmoja akijivunia kazi yake hiyo au akijitangaza? Wameficha hirizi chini ya biashara zao, wana mazindiko kwenye nyumba zao, wanajifanya wana maadili na hodari wa kusema AMEEN!!..Lakini hawajui kuwa Bwana anayajua matendo yao.

Ufunuo 3:1  “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na hizo Roho saba za Mungu, na zile nyota saba. NAYAJUA MATENDO YAKO, ya kuwa una jina la kuwa hai, nawe umekufa.

2  Uwe mwenye kukesha, ukayaimarishe mambo yaliyosalia, yanayotaka kufa. Maana sikuona matendo yako kuwa yametimilika mbele za Mungu wangu.

3  Basi kumbuka jinsi ulivyopokea, na jinsi ulivyosikia; yashike hayo na kutubu. Walakini usipokesha, nitakuja kama mwivi, wala hutaijua saa nitakayokuja kwako”

Ndugu ni heri ukatubu, uwe na amani na Kristo katika nyakazi hizi za hatari, kwasababu ukiendelea na hali hiyo hiyo utakufa na kwenda kuzimu, na adhabu yako itakuwa ni kubwa sana.

Bwana anasema…

“Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema”. (Mithali 28:13)

Leo hii ziungame dhambi zako, usiyafiche moyoni hayo unayoyafanya, wala usione aibu, wakati ndio sasa, hata kama umeshindwa kuacha, au hujui cha kufanya kwa uliyoyatenda, embu mfuate kiongozi wako wa kiroho mshirikishe akupe ushauri,.aombe pamoja na wewe,  Ili Bwana akusamehe makosa hayo uliyoyofanya.

Unachopaswa kufanya ni kutubu tu kwa kumaanisha..Ukiwa na nia kweli ya kuacha, ili Bwana atakusamehe na kukusaidia kuyashinda, lakini ukiwa upo vuguvugu, hueleweki, bado unayo hatia ya dhambi..kwasababu anayajua matendo yako.

Ufunuo 3:15  “NAYAJUA MATENDO YAKO, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16  Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa change”.

Jimimine kwelikweli kwa YESU akusaidie..Wakati wa Yesu kuyahukumu mambo yote ya sirini, umekaribia sana, Hukumu ipo karibu. Jiepushe nayo. (Warumi 2:16, 1Wakor 4:5). Ni wakati wa lala-salama.

Ikiwa utapenda kupata msaada huo wa kumkaribisha tena Kristo upya maishani mwako. Basi waweza wasiliana nasi kwa namba hizi kwa ajili ya mwongozo huo bure. +255693036618 / +255789001312.

Bwana akubariki.

Shalom. (Bwana Yesu anarudi).

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KUONGOZWA SALA YA TOBA

NINI MAANA YA KUTUBU

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

SEMA KWA LUGHA NYINGINE.

Kupiga ramli ni nini katika biblia?

Kumwambia mtu mwenye dhambi kuwa atakwenda kuzimu asipotubu Je! ni kuhukumu?

Rudi nyumbani

Print this post

NI UTUKUFU WA MUNGU KUFICHA JAMBO.

Jina la Mkuu wa Uzima, Simba wa kabila la Yuda na Mungu katika mwili, YESU KRISTO libarikiwe!.

Kuna mambo ambayo ni muhimu kuyajua sisi kama watu wa Mungu ili tuende sawa na Mungu na pia ili tuwe na amani kama maandiko ya avyotuelekeza katika Ayubu 22:21.

Ayubu 22:21 “Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia”

Ipo tabia moja ya Mungu ambayo ni muhimu kuijua ili tuishi kwa amani.

Na tabia yenyewe ni kuficha jambo/mambo. Biblia inasema hivyo katika…Mithali 25:2

Mithali 25:2 “Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo…”.

Mpaka mwenyewe anasema kuwa ni utukufu wake kuficha jambo…maana yake ni kuwa hiyo ni fahari yake yeye kufanya hivyo, hatuwezi kumbadilisha…

Kwahiyo ukiona ni kwanini kakuficha jambo fulani usilijue au usilipate kwa wakati fulani unaotoka wewe ni kwasababu ndivyo ilivyompendeza, anafanya hivyo kwa utukufu wake.. Na anafanya hivyo kwa watu wote wala hana upendeleo.. Wala usijione unayo mikosi unapojikuta hujui kitu au kinapokuwa ni kigumu kukipata.

Ukiona ni kwanini humwoni Mungu sasa kwa sura na mwonekano…ni kwasababu ni utukufu wake yeye kufanya hivyo..

Sasa ni nini anachotaka kwetu kutokana na hiyo tabia yake.

Anachotaka kutoka kwetu ni sisi TUTAFUTE KWA BIDII MPAKA TUPATE.

Luka 11:9 “Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa”

Ukitaka kumjua Mungu kwa viwango vya juu, haiwezi kuwa ni jambo la kulala na kuamka tu!..hapana! Inahitajika bidii sana katika kumtafuta..

Yeremia 29:12 “Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.

13 Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote”.

Vile vile ukitaka kuwa Mkamilifu si suala la kufumba na kufumbua tu, bali inahitajika bidii sana kuutafuta utakatifu na ukamilifu..kujazwa na Roho Mtakatifu ni hatua ya awali, baada ya hapo ni kuongeza juhudi kila siku, ndivyo maandiko yanavyosema katika Waebrania 12:14.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”

Na mambo mengine yote ya KiMungu yaliyo mazuri yamefichwa na Mungu mwenyewe Na hayapatikani kwa njia nyingine yoyote isipokuwa kwa kutafuta kwa bidii.

Na hatuwezi kumwuliza kwanini ayafiche hivyo!…ni fahari yake yeye na kwa utukufu wake

Tukitaka kuyavumbua basi ni sharti tuyatafute.

Dada/kaka anza leo kumtafuta Mungu kwa bidii sana, kwasababu anapatikana..adhimia kumtafuta kama Daudi…..

Zaburi 27:8 “Uliposema, Nitafuteni uso wangu, Moyo wangu umekuambia, BWANA, uso wako nitautafuta”

Tumia muda mwingi katika kutafuta kuliko kungoja, tumia muda mwingi katika kutafuta kuliko kunung’unika. Na Bwana atakufunulia.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TAFUTA KWA BIDII KUWA MTAKATIFU.

Kwanini Eliya alijulikana kama “Eliya Mtishbi”?

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake

Rudi nyumbani

Print this post

Paulo alikuwa na maana gani aliposema “nimeaminiwa uwakili”

SWALI: Mtume Paulo alikuwa na maana gani aliposema “nimeaminiwa uwakili”?

1Wakorintho 9:16  “Maana, ijapokuwa naihubiri Injili, sina la kujisifia; maana nimewekewa sharti; tena ole wangu nisipoihubiri Injili! 17  Maana nikiitenda kazi hii kwa hiari yangu nina thawabu; ila ikiwa si kwa hiari yangu, nimeaminiwa uwakili”.


JIBU: Mtume Paulo aliifanya kazi ya Mungu, kana kwamba ni muajiwa/kibarua aliyepewa dhamana ya kusimamia kazi zote alizowekewa chini yake kwa uangalifu, kana kwamba akipoteza chochote au akileta hasara ya jambo lolote atawajibishwa, na boss wake utakapofika muda wa mahesabu.

Tofauti na mtu aliyejitolea tu kazi, kama kusaidia, mtu wa namna hiyo hata akiacha wakati wowote, hawezi kuwajibishwa zaidi sana atapewa shukrani, kwa kutoa mchango wake katika shughuli hiyo, na kupewa viposho.

Ndio maana ya hiyo kauli, “nimeaminiwa uwakili”..kwa lugha nyepesi “nimeamiwa kazi ya mtu mwingine niisimamie kama kijakazi” Na hiyo ndiyo iliyompelekea Mtume Paulo, kusema mimi ni ‘mtumwa na mfungwa’ wa Yesu Kristo (Warumi 1:1,Waefeso 3:1).. Kwasababu hiyo akaitenda kazi ya Mungu kwa uaminifu wote, na kwa umakini wote, hata zaidi ya mitume wengine.

Ni funzo gani tunalipata.

Nasi pia tukiichukulia kazi ya Mungu kama sio jambo la hiari, au la kujitolea tu, bali kama ndio sehemu ya kazi yetu tuliyoajiriwa na Mungu hapa duniani, na kwamba tusipoifanya kwa uaminifu tukaleta hasara, tutatolea hesabu yake siku ya mwisho,..

Yaani tukimtumikia Mungu kama vile tuzitumikiavyo kazi zetu maofisi, bila kuwa na udhuru wowote.

basi tutajifunza kuitenda bila ulegevu Na mwisho wake utakuwa ni kupewa thawabu kubwa na kutukuzwa sana na Bwana Yesu  tutakapofika kule mbinguni.

Lakini kama tutajitoa kwa Mungu pale tunapojisikia tu, au tunapokuwa na nafasi, au tunapokumbushwa, au tunapofanikiwa sisi si watumwa au wafungwa wa Yesu Kristo, bali ni watumishi wake tu. Hatujafikia hatua hiyo ya kuitwa watumwa wake.

Bwana atujalie utumishi bora, kama huo, wa kuaminiwa uwakili

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JIFANYIE RAFIKI KWA MALI YA UDHALIMU.

Mungu alikuwa anaongea na nani aliposema na “Tumfanye mtu kwa mfano wetu”

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Pesa za bindoni ni nini?(Marko 6:8)

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

UTAMBUE UJUMBE WA SAA UNAYOISHI.

Rudi nyumbani

Print this post

KAMA MHUBIRI USIWE MFANO WA DIOTREFE.

Je! Unamjua Diotrefe katika biblia?

Diotrefe alikuwa ni kiongozi katika kanisa moja ambalo mtu wa Mungu ,Gayo alikuwa akishiriki. Kiongozi huyu alianza vizuri na Bwana lakini mwisho wake ulikuwa mbaya.. mpaka Mtume Yohana anamwandikia Gayo waraka juu yake,  ili asiziige tabia zake..

Hebu tumsome huyu Diotrefe jinsi alivyokuwa na tabia zake..

3Yohana 1:8 “Basi imetupasa sisi kuwakaribisha watu kama hao, ili tuwe watenda kazi pamoja na kweli.

9  Naliliandikia kanisa neno, lakini Diotrefe, apendaye kuwa wa kwanza kati yao, hatukubali.

10  Kwa hiyo, nikija, nitayakumbuka matendo yake atendayo, atoavyo upuzi juu yetu kwa maneno maovu; wala hatoshwi na hayo, ila yeye mwenyewe hawakaribishi hao ndugu, na wale watakao kuwakaribisha, huwazuia, na kuwatoa katika kanisa”.

Sasa hebu tuzitazame hizi tabia 4 Diotrefe alizokuwa nazo.

1: ANAPENDA KUWA WA KWANZA:

 Hii ni tabia ya kwanza Diotrefe aliyokuwa nayo;  Sasa Kupenda kuwa wa kwanza si jambo baya, lakini mtu anapotaka kuwa wa kwanza kwa lengo la kutukuzwa na watu, au kwa lengo la kuwatawala wa wengine, au kwa lengo la kutumikiwa.. hususani ndani ya kanisa, basi hiyo ni mbaya sana na ni kinyume na Neno la Mungu..

Kwasababu Bwana Yesu alisema..

Mathayo 20:25  “Lakini Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.

26  LAKINI HAITAKUWA HIVYO KWENU; BALI MTU YE YOTE ANAYETAKA KUWA MKUBWA KWENU, NA AWE MTUMISHI WENU;

27  NA MTU YE YOTE ANAYETAKA KUWA WA KWANZA KWENU NA AWE MTUMWA WENU;

28  kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi”.

Kwahiyo kama Mhubiri wa Injili: Katika nafasi yoyote uliyopo aidha ni Mchungaji, au Mwalimu, au Nabii, au Mtume au Mwimbaji kumbuka kuwa unapaswa uwe Mtumwa wa wote!, kama unataka kuwa wa Kwanza, lakini kamwe usijiinue wala usitafute utukufu wa wanadamu kama huyu Diotrefe. Ni hatari kubwa!

2. ANANENA MANENO YA UPUUZI  JUU YA MITUME

Hii ni tabia ya pili Diotrefe aliyokuwa nayo.. Alikuwa anawachafua Mitume wa Bwana Yesu (Ikiwemo Yohana, Mtume wa Yesu ambaye alipendwa sana na Bwana Yesu). Ijapokuwa aliwajua kuwa wamechaguliwa na Bwana lakini yeye aliwachafua kwa maneno mabaya na kuwafanya waonekane si kitu mbele ya kanisa la Mungu…Na hiyo yote ni kutokana na wivu.

Roho hii pia ipo kwa baadhi ya watu, ambao kutokana na Wivu, basi wapo radhi hata kuwachafua watumishi wa kweli wa Mungu, na huku mioyoni wakishuhudiwa kuwa wanawachafua ni watumishi wa kweli wa Mungu, lakini kutokana na wivu wanaendelea tu kuwachafua!,.. Hili ni jambo la kuzingatia sana  wewe kama Mwimbaji, au Mchungaji, au Mtume au Nabii au Mwinjilisti.

3. HAWAKARIBISHI NDUGU

Hii ni tabia ya tatu ambayo Diotrefe alikuwa anaionyesha katika kanisa… Yeye alikuwa ni kiongozi lakini kamwe hakutaka kupokea Watumishi wengine waliokuja kuhubiri katika mitaa yake, au mji wake, au waliokuwa wakipita njia yake kuelekea sehemu nyingine kuhubiri. Na sababu ya kufanya hivyo ni ile ile ya wivu na kutaka kuwa wa kwanza..

 Aliona kama mtu mwingine akija kuhubiri katika mji wake basi yeye hadhi yake, au heshima yake itashuka, na Yule alitakayekuja atatukuzwa zaidi..Hivyo hiyo roho ikampelekea mpaka kukataa kupokea wahubiri walio wageni.

Vile vile na sisi hatuna budi kuikataa hiyo roho kwasababu ni roho kutoka kwa Yule adui, siku zote hatuna budi kuwakubali na kuwakaribisha Watumishi wengine wanaotaka kuja kuhubiri maeneo tuliyopo, maadamu tumewahakiki kuwa kweli ni watumishi wa Mungu kwa Neno la Mungu, na wamekuja kwa nia ya kuhubiri injili.

4. ALIWAZUIA WATU WENGINE WASIWAKARIBISHE NDUGU

Hii ni tabia ya mwisho aliyoionyesha huyu Diotrefe.. Hakuridhika tu kuwakataa Mitume waliokuja kuhubiri pande zake, bali pia aliwakataza washirika wa kanisa lile wasimpokee mtumishi mwingine yoyote atakayekuja kuomba hifadhi kwao, kwaajili ya kuhubiri injili.. Na hakuishia hapo, bali aliendelea na kuwafukuza katika kanisa wale wote waliodhubutu kuwakaribisha Mitume. (Uone jinsi hii roho ilivyoenda mbali).

Lakini huyu Diotrefe hakuanza hivi.. Alianza vizuri tu!, ndio maana hata akafikia hatua ya kuwa kiongozi wa Makanisa (Huenda alikuwa Askofu).  Lakini roho nyingine ya kujiinua ilimwingia na ya kupenda kutukuzwa na watu na kuinuliwa, na akaipalilia mwishowe ikawa ni roho ya uadui mbaya sana na iliyoiharibu kanisa.

Na sisi hatuna budi kujifunza katika haya, ili tusijikute tunaangukia katika makosa hayo hayo ya Diotrefe (Ndio maana Mungu karuhusu kisa cha Diotrefe kiwepo katika biblia hata kama kwa ufupi sana). Ili tujifunze na tujihadhari na roho ya kujiinua, na kupenda utukufu wa wanadamu zaidi ya utukufu wa Mungu, na tama nyingine zote za kiulimwengu.

Bwana atusaidie tuwe kama Mzee Gayo aliyekubali kupokea mashauri hayo.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Ni sahihi kusema sikuitiwa kuhubiri ubatizo kama Paulo alivyosema (1Wakorintho 1:17)?.

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

Rudi nyumbani

Print this post

EPUSHA WIVU KATIKA NDOA:

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WANANDOA: Epusha Wivu katika ndoa:

Sehemu ya kwanza: Upande wa Mwanamke.

Huu ni mfululizo wa mafundisho maalumu yawahusuyo wanandoa: Ikiwa hukupata sehemu za nyuma, basi waweza kututumia ujumbe kwa namba zetu zilizo chini ya somo hili, tukutumie;

Leo tutaona  jinsi wivu unavyoweza kuathiri kwa sehemu kubwa mahusiano ya wanandoa.

Kibiblia wivu upo wa aina mbili:

1)  Wivu wa kipepo: Ni ule wa kumuonea mtu kijicho, yaani kutotaka, mwenzako kufanikiwa kwasababu wewe hukufanikiwa kama yeye alivyofanikiwa, kutaka kile ambacho mwenzako anacho uwe nacho wewe huku hutaki yeye awe nacho. Biblia imetuonya sana dhidi ya wivu huu, kwasababu ni zao la shetani. Ndio walikuwa nao masadukayo na makuhani kwa Bwana wetu Yesu na mitume wake, pale walipoona neema ya Mungu ipo juu yao kubwa lakini kwao haipo, (Matendo 5:17, Warumi 13:13)

2)  Wivu wa kimahusiano: Wanandoa, Huu ni wivu ambao ni wa asili, Mungu kauweka ndani ya mtu, huu upo katika mahusiano ya kindoa,au maagano Na ndio Wivu ambao Mungu amekiri pia mwenyewe anao.(Kutoka 20:5)..Huu ni wa kuulinda sana, hususani pale unapoingia kwenye ndoa, kwasababu madhara yake ni makubwa zaidi hata ya hasira, au ghadhabu. Biblia inasema hivyo katika..

Mithali 27:4 “Ghadhabu ni kali, na hasira ni gharika; Lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu”.

Huu ndio umesababisha watu, kugombana, kuchukiana, kusalitiana  na hata wakati mwingine kuuana, na kuwasababishia matatizo na wengine ambao hata hawahusiki.

Leo  tutatazama, ni kwa namna gani, kinywa cha mwanamke, kinaweza kuwasha wivu mbaya sana, kwa upande wa pili. Na somo linalofuata tutaona tabia ambazo mwanaume anapaswa ajiepushe nazo, kuepukana na madhara ya wivu kwenye ndoa yake.

 hii itakusaida, kuishi kwa amani na utulivu na kuinusuru ndoa yako, .

Sasa embu tusome kisa hichi tunachokiona katika 1Samweli 18:7. Si kisa cha kindoa lakini ni kisa kimuhusucho Daudi na Sauli, Wengi wetu tunajua sababu iliyomfanya Sauli amchukie Daudi, ambaye hapo mwanzo alimpenda ilikuwa ni Wivu. Lakini wachache sana, wanafahamu CHANZO cha wivu huo, kilikuwa ni nini?

Biblia inatupa majibu, kilikuwa ni wanawake, waliotoka na kutoa sifa zao, mahali pasipostahili kwa wakati ule. Embu Tusome.

1Samweli 18:5 “Basi Daudi akatoka kwenda kila mahali alikotumwa na Sauli, akatenda kwa akili; SAULI AKAMWEKA JUU YA WATU WA VITA; jambo hili likawa jema machoni pa watu wote, na machoni pa watumishi wa Sauli pia.

6 Hata ikawa, walipokuwa wakienda, hapo Daudi aliporudi baada ya kumwua yule Mfilisti, wanawake wakatoka katika miji yote ya Israeli, kwa kuimba na kucheza, ili kumlaki mfalme Sauli; wakatoka na matari, na shangwe, na vinanda.

7 NAO WALE WANAWAKE WAKAITIKIANA WAKICHEZA, WAKASEMA, SAULI AMEWAUA ELFU ZAKE, NA DAUDI MAKUMI ELFU YAKE.

8 Basi Sauli akaghadhibika sana, na maneno haya yakamchukiza; akasema, Wamempa Daudi makumi elfu, na mimi wamenipa elfu tu; kuna nini tena awezayo kupata, isipokuwa ni ufalme?

9 Sauli akamwonea Daudi wivu tangu siku ile”.

Hicho ndicho kilichokuwa chanzo, cha vita vya Daudi na anguko la Sauli,. Wanawake wale walikuwa wanasema kweli, kwa waliyoyaona, lakini hawakutumia busara kuimba mbele ya mfalme, kwa wakati ule.. Huwenda hata Daudi, alitamani wakae kimya, wasimsifie yeye zaidi ya mfalme wake, mbele ya umati.. Lakini wale wanawake hilo halikuwa akilini mwao. Hawakujua kuwa kumbe nyimbo zao, sifa zao, maneno yao, ni panga ndani ya mioyo ya wakuu wao.

Ndio ikawa sababu ya Sauli kughahiri, hata vyeo vyote alivyompa Daudi, akampokonya na kumfukuza na kutaka kumuua kabisa, kwa kosa tu la wale wanawake.  Lakini kama wale wanawake wangetumia busara, kumwimbia mfalme zaidi, basi Daudi angeendelea kustarehe na kudumishwa katika ufalme ule.

Maana yake ni nini?

Maneno yoyote ya sifa yanayotoka kinywani mwako wewe kama mwanamke, yana matokeo makubwa sana kwa upande wa pili. Sasa tukirudi katika upande wa ndoa, Wivu unatokea pale ambapo unathamini, au unasifia wanaume wengine zaidi ya mume wako. Ukiwa umeolewa tambua kuwa mume wako ndio,bora kuliko wanaume wote ulimwenguni, ndio mwenye sifa zote kuliko wanaume wote ulimwenguni.Hata kama wale wengine wamemzidi yeye kwa kiwango kikubwa kiasi gani, acha kuwazungumza zungumza mbele ya mume wako.

Hii ni kwa faida yako, na kwa wengine. Wanaume wengi wanagombana na marafiki zao vipenzi, kisa tu wake zao,wanapowasifia, wanakuwa mpaka maadui kwa sababu ndogo ndogo tu kama hizi,..Labda utasikia mmoja anasema, “mume wangu,rafiki yako huwa anapendezaga uvaaji wake, yaani navitiwa nao”..Kauli kama hizi ziepuke kinywani mwako, ili kunusuru, urafiki au ujirani wenu.

Kwa ufupi kauli zozote za sifa, zichungumze mara mbili mbili; Unaweza usione shida yoyote, au ukadhani ni jambo dogo tu, lakini upokee huu ushauri utakufaa kwa siku za mbeleni, , hilo jambo linamuathiri sana mwanaume. Usimzungumze zungumze mwanaume mwingine mbele ya mumeo, isipokuwa kwa kiasi, hata wale unaowaona kwenye tv, au unaowasiliana nao kwenye simu. Kumbuka wivu unawashwa na mambo madogo sana.

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Je! Unauhakika wa maisha yako ya milele baada ya kifo? Kumbuka Kristo yupo mlangoni kurudi, dalili zote zimeshatimia, Huu si wakati wa kumbelezewa tena wokovu, ni wakati wa kujitahidi kuingia ndani ya Safina(Yesu Kristo) kwa nguvu zote, maana muda umekwisha.. Tubu dhambi zako, ukabatizwe mgeukie Bwana akupe uzima wa milele.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)

WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

Ndoa ya serikali ni halali?

Rudi nyumbani

Print this post

Nchi ya Nodi ambayo Kaini alikimbilia ndio nchi gani kwasasa?(Mwanzo 4:16).

Jibu: Tusome,

Mwanzo 4:15 “BWANA akamwambia, Kwa sababu hiyo ye yote atakayemwua Kaini atalipizwa kisasi mara saba. BWANA akamtia Kaini alama, mtu amwonaye asije akampiga.

16 Kaini akatoka mbele za uso wa BWANA, akakaa katika nchi ya Nodi, mbele ya Edeni

17 Kaini akamjua mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Henoko; akajenga mji akauita Henoko, kwa jina la mwanawe ”.

“Nodi” sio jina la nchi kama vile Tanzania, Kenya au Uganda bali ni sifa ya nchi..Tafsiri ya neno Nodi ni “kutanga”. Hili ni neno la kiebrania lenye maana hiyo ya “kutanga”.

Kwahiyo biblia iliposema kuwa Kaini alienda nchi ya Nodi, haikumaanisha kuwa alienda kwenye Nchi inayoitwa “Nodi”.. La! bali ilimaanisha kuwa Kaini alienda katika Nchi ya “Kutangatanga”.  Hakuwa na kikao maalumu, wala nchi maalumu sawasawa na laana Bwana Mungu aliyomlaania.

Mwanzo 4:11 “Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;

 12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; UTAKUWA MTORO NA MTU ASIYE NA KIKAO DUNIANI”.

Vile vile dhambi inaweza kutufanya tusiwe watu wa vikao duniani, (tukawa watu wa kutanga tanga tu kutwa kuchwa). Tunazunguka huku na kule kutafuta unafuu wa maisha lakini hatuoni..Acha leo kutanga tanga, Suluhisho ni moja tu!, mkimbilie Bwana Yesu leo, mlilie akusamehe dhambi zako na akuokoe, kwasababu damu yake hata sasa bado inaondoa dhambi..

Na ukifanya hivyo kwa imani atakuokoa na laana ambayo imetajwa juu ya wote wamwachao Bwana..

Zaburi 107:4 “Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika; Hawakuona mji wa kukaa. 

5 Waliona njaa, waliona na kiu, Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao. 

6 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao. 

7 Akawaongoza kwa njia ya kunyoka, Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa”.

Bwana Yesu akubariki.

Ikiwa utatamani kujua zaidi Mke wa Kaini alitokea wapi basi fungua hapa >>>JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kaanani ni nchi gani kwasasa?

SISI NI WINDO BORA SANA, LA DHAMBI.

CHOCHOTE UMFANYIACHO KRISTO KINA THAMANI.

ANAKUJA KAMA “MWIVI” NA SI KAMA “ASKARI” FANYIKA CHOMBO CHA THAMANI.

LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.

Rudi nyumbani

Print this post

JE UMEZALIWA MARA YA PILI KWA NENO LA MUNGU?

Jina kuu la Bwana na Mwokozi wetu, Yesu Kristo, Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana lihimidiwe!. Karibu tujifunze biblia.

Je unajua maana ya kuzaliwa mara ya pili kwa Neno?.. Kupo kuzaliwa mara ya pili kwa maneno ya watu au ya mtu na pia kupo kuzaliwa mara ya pili kwa Neno la Mungu.

Neno la Mungu linasema hivi…

Yohana 3:3 “ Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.

4  Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?

5  Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, MTU ASIPOZALIWA KWA MAJI NA KWA ROHO, HAWEZI KUUINGIA UFALME WA MUNGU”.

Umeona tafsiri ya kuzaliwa mara ya Pili kwa Neno la Mungu ni ipi?…si nyingine zaidi ya KUZALIWA KWA MAJI NA KWA ROHO.

Sasa unaweza kujiuliza maana ya kuzaliwa kwa maji na kwa roho ni nini?

Kuzaliwa kwa maji ni “Ubatizo wa Maji mengi”, na kuzaliwa kwa roho ni “Ubatizo wa Roho Mtakatifu” Kwahiyo unapoamini na kubatizwa kwa Maji tele (Yohana 3:23).. Na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, basi hapo unakuwa umezaliwa mara ya Pili kwa NENO LA MUNGU…(Kwasababu Neno la Mungu ndio linaelekeza hivyo).

Sasa umuhimu wa kufanya hivyo ni nini?

Ukiamini na kubatizwa na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, faida yake ya kwanza ni kwamba WOKOVU WAKO UNAKUWA NI WA KUDUMU, unakuwa sio wa kuchafuka chafuka..bali unakuwa ni thabiti siku zote mpaka siku utakapomaliza maisha yako hapa duniani.. Kwasababu Neno la MUNGU ni mbegu isiyoharibika.. Hivyo ukizaliwa kwa Neno la Mungu hilo (yaani kwa kubatizwa kwa maji na kupokea Roho mtakatifu), basi wokovu wako unakuwa imara daima…Ndivyo Neno la Mungu linavyosema..

1Petro 1:23 “Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si KWA MBEGU IHARIBIKAYO, BALI KWA ILE ISIYOHARIBIKA; KWA NENO LA MUNGU LENYE UZIMA, lidumulo hata milele”

Ni kwanini leo wokovu wa watu wengi unakuwa ni wa kusuasua, unakuta mtu leo kamkiri Yesu, lakini baada ya siku kadhaa au wiki kadhaa karudi kule kule, ijapokuwa yupo kanisani na karibu na wapendwa?.. ni kwasababu huenda mtu huyo hajazaliwa mara ya pili kwa Neno la Mungu (yaani kwa kubatizwa sahihi na kupokea Roho Mtakatifu)

Huenda baada ya kumkiri Yesu akaambiwa hakuna haja ya ubatizo, au akakawishwa kubatizwa! Na kupokea Roho Mtakatifu… Hivyo kwa mbegu hiyo aliyopandikiziwa ndani yake, hawezi kusonga mbele kwasababu ni MBEGU INAYOHARIBIKA.. Lakini kama angezaliwa mara ya pili kwa Neno la Mungu, ambalo ndio mbegu isiyoweza kuharibika basi wokovu wake ungekuwa ni imara siku zote.

Ndugu unayesoma ujumbe huu, huenda wokovu wako ni wa nusu nusu, kiasi kwamba hata wewe mwenyewe hujielewi kama Kweli Kristo yupo ndani yako au la!.. katika hali hiyo uliyopo hebu jichunguze kama kweli umezaliwa katika Neno la Mungu.. Kwasababu Neno la Mungu linasema “Ni lazima kuzaliwa mara ya pili kwa maji na kwa Roho”.

Je! Wewe umebatizwa inavyopaswa?.. kumbuka ubatizo sahihi ni ule wa maji tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Bwana Yesu Kristo (Matendo 2:38)..Na ubatizo sahihi wa Roho Mtakatifu ni ule unaozaa matunda yale yaliyoorodheshwa kwenye Wagalatia 5:22. Kama vitu hivyo viwili umevikosa, basi ni vizuri ukatafuta ubatizo sahihi haraka iwezekanikavyo na vile vile ubatizo wa Roho Mtakatifu.

Ikiwa mahali ulipo unaweza kupata ubatizo sahihi basi anza kwenda kuutafuta kuanzia sasa, lakini ikiwa unapata ugumu katika kutafuta, basi unaweza kuwasiliana nasi kupitia namba zetu hapo chini, tutakusaidia kukuelekeza mahali karibu na ulipo, ambapo utaweza kupata ubatizo sahihi.

Bwana Yesu akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

UMUHIMU WA KUZALIWA MARA YA PILI.

Mkomamanga ni nini? Na katika biblia unawakilisha nini?

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Rudi nyumbani

Print this post

Yerusalemu ni nini?

Yerusalemu, ni Neno la kiyahudi linalomaanisha  “Mji wa amani” au “msingi wa amani” .

Kabla ya mji huu kupata sifa tunayoifahamu sasahivi, awali ulikuwa ni mji wa wakaanani, waliojulikana kama wayebusi, kipindi ambacho wayahudi bado hawajaimiliki nchi yao.

Hivyo baada ya wana wa Israeli kuiteka nchi ya kaanani, eneo ambalo lilikuwepo huu mji, liligawanya kwa kabila la Yuda. Lakini hawa wayebusi hawakuondolewa moja kwa moja katika mji huo wa Yerusalemu, bado ukaendelea kuwa chini ya milki yao.

Mpaka baadaye, Daudi alipouvamia na kuwaondoa wayebusi. Ndipo Mji huo ukaitwa “Mji wa Daudi”.(2Samweli 5:6-10) Baadaye akalihamishia Sanduku la Mungu la agano, mpaka mji huo,  hivyo kidogo kidogo ukaanza kupokea sifa ya kuwa kiini cha dini (2Samweli 6:1-19). Daudi akaazimia kumjengea Mungu hekalu ambalo, atamwekea Mungu agano lake huko. Lakini hakuruhusiwa kwasababu ya mauaji mengi aliyoyasababisha, Mpaka mtoto wake Sulemani, alipokuja kulijenga, Hapo ndipo wana wote wa Israeli wakapafanya Yerusalemu kuwa kitovu cha kumwabudia Mungu. Na Mungu pia akapabariki na kupachagua pawe mji wake mtakatifu, kati ya miji yote, ambapo ataliweka jina lake, lijulikane kwa mataifa yote ya ulimwengu..

Japokuwa eneo la mji huu, lilibomolewa na kujengwa mara kadhaa, lakini hapo ndipo mfalme  wetu Yesu Kristo atakapokuja kutawalia dunia yote katika ule utawala wa miaka 1000 kama mfalme wa wafalme na Bwana wa Mabwana, atakaporudi mara ya pili.

Lakini biblia inatuonyesha kuwa upo mji mwingine wa kimbinguni, ambao Mungu amewaandalia watu wake,..ujulikanao kama YERUSALEMU MPYA.

Umechukua jina la Yerusalemu hii ya duniani, ili kutupa picha tuelewe vizuri utakavyokuwa.  Mji huo utashuka kutoka mbinguni kwa Mungu mwenyewe na kuja hapa duniani. Ndani ya mji huo maandiko yanasema “hakitaingia chochote kilicho kinyonge”. Isipokuwa watu maalumu sana wajulikanao kama bibi-arusi wa Kristo.. Kumbuka si kila atakayepokea uzima wa milele, atakuwa na daraja sawa na mwenzake..Uaminifu wako, na utumishi wako sasa, vinaeneleza wewe utastahili kukaa wapi utakapofika kule ng’ambo. Wapo ambao watastahili kukaa ndani ya mji, na wapo ambao watakaa nje ya mji huo mtakatifu. Japo wote watakuwa ni watakatifu.

Ndani ya huo mji ndio yatakuwa makao mapya ya Mungu milele (Ufunuo 21:3), Mambo yaliyopo huko ni mazuri biblia inasema jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia(1Wakorintho 2:9). Kwa ufupi ni kwamba kila mmoja wetu atajuta, kwanini hakujibidiisha kwa Mungu sana kwa uzuri atakaokutana nao huko.

Huu ndio mji ambao Ibrahimu aliuona..ukamfanya aishi kama mpitaji tu hapa duniani, japokuwa alikuwa na mali nyingi na utajiri mwingi..

Waebrania 11:9 “Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.

10 Maana alikuwa AKIUTAZAMIA MJI WENYE MISINGI, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu”.

Tafakari maandiko haya;

Ufunuo 21:1 “Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.

2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.

3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.

4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.

5 Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.

6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.

7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.

8 Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.

Je! Na wewe utakuwa na sehemu ndani ya mji ule?

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

Israeli ipo bara gani?

JINSI MUNGU ANAVYOIPIGA NA KUIPONYA AFRIKA.

Mretemu ni mti gani?

Hisopu/ Hisopo ni nini katika biblia?(Zaburi 51:7)

Neno ‘Kima’ linamaanisha nini Katika biblia? (Mathayo 27:9 )

Uchaga ni nini? (Luka 12:24)

Rudi nyumbani

Print this post