MITHALI AU METHALI ZA BIBLIA

MITHALI AU METHALI ZA BIBLIA

“Mithali” na “Methali” ni neno lenye maana moja.. ambalo maana yake ni kipande cha sentensi chenye kubeba ujumbe halisi wa kimaisha…Methali/Mithali zinaweza kuwa ni sentensi zenye ujumbe wa wazi au zenye ujumbe wa fumbo.

Kwa mfano methali inayosema “akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli” hii ni methali iliyo wazi kabisa yenye ujumbe wa kwamba…mtu Yule ambaye wakati wa dhiki yupo na wewe huyo ndiye rafiki wa kweli tofauti na Yule ambaye wakati wa dhiki anakukimbia lakini wakati wa raha ndio anakukaribia.

Lakini pia kuna mithali kama “mtaka cha uvunguni sharti ainame” methali hii inahitaji kutafakari sana ndipo upate ujumbe… “Kwamba ili upate jambo Fulani huna budi kuingia gharama” Na nyingine zote ni hivyo hivyo.

Sasa katika biblia pia zipo methali/Mithali…Mithali hizi Roho Mtakatifu karuhusu ziandikwe na wenye hekima ili ziwape hekima watoto wa Mungu.

Katika biblia tunamsoma mtu mmoja anayeitwa Sulemani, ambaye alimwomba Mungu Hekima badala ya Mali, na hivyo Mungu alimpa hekima nyingi sana, mpaka wafalme na mamalkia wa dunia wakawa wanamwendea kusikiliza hekima zake. Na nyingi ya hekima alizojaliwa aliziandika kwa mfumo huo wa Methali na nyimbo.

1Wafalme4: 29 “Mungu akampa Sulemani hekima, na akili nyingi sana, na moyo mkuu, kama mchanga ulioko pwani.

30 Hekima ya Sulemani ikapita hekima ya wana wote wa mashariki, na hekima zote za Misri.

31 Kwa kuwa alikuwa na hekima kuliko watu wote; kuliko Ethani Mwezrahi, na Hemani, na Kalkoli, na Darda, wana wa Maholi; zikaenea sifa zake kati ya mataifa yote yaliyozunguka.

32 NAYE AKANENA MIFANO ELFU TATU, NA NYIMBO ZAKE ZILIKUWA ELFU MOJA NA TANO.

33 Akanena habari za miti tangu mwerezi ulioko Lebanoni hata hisopo umeao ukutani; pia akanena habari za wanyama, na za ndege, na vitambaavyo, na samaki.

34 Wakaja wa mataifa yote ili waisikie hekima ya Sulemani, toka wafalme wote wa ulimwengu, waliokuwa wamepata habari za hekima yake”.

Kwahiyo biblia ni kitabu kilichojitosheleza..asilimia 100, kina faraja, kina wasaa, kina elimu, kina Mithali, na hekima na maarifa. Kama mtu mmoja alivyowahi kusema “kama nikipatiwa biblia na mshumaa katika chumba chenye giza, basi nitaweza kukuelezea kila kitu kinachoendelea katika dunia”. Na hiyo ni kweli kabisa..

Sasa hebu tusikilize baadhi ya Mithali za biblia, kama methali  tu methali ya kidunia inayosema “akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli” inaweza kutusaidia kutambua marafiki wa kweli, basi biblia ni dhahiri kuwa ina mithali nyingi zinazofanana na hizo ambazo zimejaa hekima kuliko mithali hizi zetu za kidunia..

Mithali juu ya wanaokuchukia/kukuwazia mabaya:

Mithali 24: 17 “Usifurahi, adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;

18 Bwana asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake.

19 Usikasirike kwa sababu ya watenda mabaya; Wala usiwahusudu wabaya;

20 Kwa maana mtu mbaya hapati thawabu; Taa ya mtu mbaya itazimika”.

Hiyo ni Methali ya maisha, kamwe usifurahi…adui yako anapopatwa na mabaya!..bali uhuzunike!, na kumhurumia na Bwana atakuongezea amani na furaha, na kukupenda!…

Na mithali nyingine ni hii..

Mithali 25: 21 “Adui yako akiwa ana njaa, mpe chakula; Tena akiwa ana kiu, mpe maji ya kunywa;

22 Maana utatia makaa ya moto kichwani pake; Na Bwana atakupa thawabu”.

Mithali ya Njia unayoiendea:

Mithali 14: 12 “Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti”.

mithali

Maana yake ni kwamba kuwa makini na ile njia ambayo unaweza kuiona ni sawa machoni pako…. “chunguza sana njia zako, hususani zile unazoziona zipo sawa, nyingi zinaishia upotevuni”. Njia zinazofuatwa na watu wengi zinaishia upotevuni.

Zipo methali nyingi sana katika kitabu cha Mithali, Mhubiri, Zaburi na Ayubu, hatuwezi kuziandika zote hapa, lakini hizi chache ni ili kukukumbusha wewe ndugu kwamba Biblia ni neno la Mungu lililojitosheleza… anza kutenga muda kusoma biblia, kuna mambo mengi ambayo ulikuwa huyajui utayajua, kuna hekima nyingi ambazo zitakufumbua macho katika hali unayopitia sasa…Mambo ambayo ulikuwa huna majibu nayo, basi utayapata ndani ya biblia.

Anza leo kusoma vitabu hivyo vya mithali na vingine vyote, na Bwana atakuwa na wewe, zipo ambazo zina ujumbe wa wazi na zipo zenye ujumbe wa mafumbo, zenye ujumbe wa kimafumbo, yupo Roho Mtakatifu kutusaidia kuyafumbua mafumbo hayo.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

RAFIKI WA KWELI NI YUPI?

https://wingulamashahidi.org/2020/07/03/kutomzuia-kutombana-mtoto-wako-ni-dhambi/

IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!

Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments