Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

JIBU: Moja ya vitu vilivyokuwepo ndani ya hekalu la Mungu, ni kinara cha Taa, vingine vilivyokuwepo ni sanduku la agano, madhabahu ya dhahabu ya kuvukizia uvumba, na sanduku la agano.

Sasa kama tunavyojua nyumba ikijengwa na kisha haina chanzo cha Nuru ndani yake, nyumba hiyo bado haijakamilika…Hiyo ndio maana kila nyumba ikijengwa ni lazima iwekwe na mfumo wa taa ili kwamba wakati wa usiku ndani kusiwe giza shughuli zikakwama…

Na ndani ya Hema lililotengenezwa na Musa, Bwana aliagiza kuwepo na chanzo cha mwanga ndani ya lile hema, ili shughuli za kikuhani ziweze kufanyika, kama kuvukiza uvumba na kuhani mkuu kuweza kufanya upatanisho (Hivyo Bwana aliagiza pawepo kinara cha taa chenye matawi saba)….

Hali kadhalika mpaka wakati wa hekalu lilipokuja kujengwa na Sulemani jambo ni lile lile, nyumba ya Mungu haiwezi kuwa giza ndani ni lazima kuwepo na Nuru…na kwasababu nyumba ile Sulemani aliyoijenga ilikuwa ni kubwa kuliko hema la Musa, ilihitajika vinara vingi zaidi kule ndani ili pawe na mwanga wa kutosha…Hivyo vikaongezeka kutoka kinara kimoja na kuwa vinara 10…Na kila kinara kilikuwa na taa 7…Hivyo kwa ujumla ndani tu ya ile nyumba kulikuwa na taa 70..(Hivyo kulikuwa na mwanga wa kutosha).

Sasa biblia inasema sisi ni NURU ya Ulimwengu…Maana yake ni kwamba wakristo wa kweli au kanisa la Kristo linafananisha na Taa. Maana yake linamulika na kuangaza kote kote..

Mathayo 5: 14 “Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.

15 Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.

16 Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni”.

Hivyo basi kanisa la Kristo ndilo linalofananishwa na “kile kinara cha taa ndani ya Nyumba ya Mungu” Siri hiyo haikujulikana tangu zamani mpaka wakati Bwana Yesu alipokuja kuifichua siri hiyo tukisoma katika..

Ufunuo 1:20 “Siri ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume, na ya vile vinara saba vya dhahabu. Zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba; na vile VINARA SABA NI MAKANISA SABA”.

Unaona? Na kama ukifuatilia kwa makini maagizo Musa aliyopewa kuhusu kile kinara cha taa ni kwamba…kinapaswa kiwake daima!…(hakuna siku kinapaswa kiwe kimezima kwa kuishiwa mafuta), hivyo hilo lilikuwa ni agizo la Mungu kwahiyo wana wa Israeli walikuwa wanahakikisha kuwa hakizimi kwa gharama zozote zile…hivyo kwa mamia ya miaka viliendelea kuwaka tu hivyo hivyo…hakuna siku kilizima, wakati wa Mfalme Sulemani.

Na sisi hatupaswi Nuru yetu izime kama biblia inavyosema hapo katika Mathayo 5:16, Na nuru yetu ni matendo yetu..Yanapaswe yawe yanaangaza muda wote..Na tunapaswa tutoe mwanga mweupe na si mwekundu wala wa blue…tunapokuwa wauaji, wazinzi, watukanaji na bado tujajiita wakristo hapo ni tonatoa mianga ya rangi nyingine…

Bwana atubariki na atujalie Neema yake siku zote.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

UUMBAJI BORA WA MUNGU, UPO NDANI YA MWANADAMU.

IMANI NI KUWA NA UHAKIKA WA MAMBO YATARAJIWAYO.

Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?

MJUMBE WA AGANO.

WANA JUHUDI KWA AJILI YA MUNGU, LAKINI SI KATIKA MAARIFA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments