Title October 2020

Masheki ni nini?(Zaburi 105:22, Ayubu 29:10)

Masheki ni watu wenye hadhi ya juu sana, wenye jina kubwa na heshima katika jamii au taifa,

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi katika biblia;

Ayubu 29:9 “Wakuu wakanyamaa wasinene, Na kuweka mikono yao vinywani mwao;

10 Sauti yao masheki ilinyamaa, Na ndimi zao zilishikamana na makaakaa yao”.

Zaburi 68:31 “Masheki watakuja kutoka Misri, Kushi itamnyoshea Mungu mikono yake mara”.

Zaburi 83:11 “Uwafanye wakuu wao kama Orebu na Zeebu, Na masheki yao wote kama Zeba na Zalmuna”.

Zaburi 105:22 “Awafunge masheki wake kama apendavyo, Na kuwafundisha wazee wake hekima”.

Hata Kristo atakaporudi mara ya pili hapa duniani na kutawala kama BWANA WA MABWANA na MFALME WA WAFALME, Atakuwa na masheki wake chini yake. Watu ambao atawapa heshima kubwa kuwa makuhani wake na wafalme katika enzi yake yote duniani kote.

Na watu hao watakuwa si wengine zaidi ya watakatifu walioshinda zamani, na watakaoshinda sasa ulimwengu huu mbovu.

Hizi ni baadhi ya ahadi alizowaahidia watakaoshinda.

Ufunuo 2:26 “Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,

27 naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu”.

Ufunuo 3:12 “Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya”.

Ufunuo 3:21 “Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.

22 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”.

Je! Mimi na wewe tupo miongoni mwa watakaoshinda? Kama bado, Je! Upo tayari kumpa Yesu maisha yako leo? Ikiwa jibu ni ndio basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>> SALA YA TOBA

Bwana atutie nguvu.

Maran Atha.

Tazama maana ya maneno mengine ya biblia chini.

Na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Kicho ni nini? (Waefeso 5:21, 2Samweli 23:3)

MARINDA KATIKA BIBLIA NI KITU GANI?

Nini maana ya “chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu”?

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.

Mhubiri 7:20 “Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, ambaye afanya mema, asifanye dhambi.

21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana.

22 Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine”.

Kitabu cha Mithali na Mhubiri ni vitabu vilivyojaa mafunzo mengi ya maisha ya kawaida, tukiachilia mbali yale ya rohoni.  Vitabu hivi vimeandikwa na mtu mmoja ambaye ni Sulemani. Hivyo leo tutaangalia jambo moja la kujifunza kwenye maisha yetu ya kawaida sisi kama wakristo.

Kama tunavyosoma hapo katika mstari wa 21 na 22 inasema “usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa”… Sasa ni jambo la kawaida kwa kadiri tunavyoishi hapa duniani, kupitia katika hali tofauti tofauti, kuna wakati utapitia hali ya kuzungumziwa vibaya, kusengenywa, haijalishi utakuwa ni mwema, au umefanya mazuri kiasi gani, hilo haliepukiki, hata kama wewe ni mtakatifu vipi?.

Sasa biblia inatuambia, tunapokuwa katika mazingira kama hayo, tusitie moyoni kila kitu tunachokisikia, au kwa namna nyingine tuvipuuzie, haijalishi tulichoambiwa kinachoma  kiasi gani, hiyo ni kwa faida yetu wenyewe..

Lakini tatizo linakuja kwetu pale ambapo tunakisikia kidogo tu tumezungumziwa vibaya, na sisi hapo hapo tunaanza kutafuta, ni nani huyo kasema, ni nani kamwambia, na kama hiyo haitoshi tunaendelea kutafiti na yule aliyemwambia ni nani kamweleza, na yule aliyeelezwa katolea wapi taarifa hizo, na kwanini wamefanya hivyo, hivyo tunaendelea, mpaka unazalika mlolongo mrefu ambao hauna mwisho.

Sasa ukisoma mstari wa 22 utaona unatupa madhara ya kufanya hivyo na kutuambia ikiwa mtu ataendelea kutafuta tafuta hivyo, kuchunguza chunguza hivyo.., kutafuta mchawi ni nani,.mwisho wa siku atashangaa kusikia mambo ambayo asingetazamia kusikia kutoka kwa watu wake ambao hawategemei kabisa.. Ukisoma hapo anatumia mfano wa “mtumwa”, mtu ambaye ni mjakazi wake anayekuheshimu atasikia  anamtukana..

“21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana”.

Hivyo kabla hujaanza kuyafikiria mambo ya wanadamu, utakapoona habari fulani inakujia ya kusemwa vibaya, ikwepe, au ipuuzie kabisa kwa usalama wa moyo wako, kisha endelea na shughuli zako za kawaida, Watu wengi (hususani wakristo) wanaohangaika huku na huko kutafuta ni nani aliyewasengenya au Yule anazungumzia nini kuhusu mimi, mwisho wa siku wanakuwa na vinyongo na watu wote, wanakuwa na chuki zisizokuwa na sababu, wanapoteza hata imani na Mungu na kuanza kuishi maisha ya visasi, maisha ya kutokusamehe, na Maisha ya uchungu, hata maombi yao yanakuwa ni ya kuwalenga tu maadui zao,  mawazo yao ni kukomoa tu, nipate hiki nimfundishe yule adabu n.k. kisa tu alimsikia Fulani akimcheka.. Na pia kamwe hawawezi kuwa na maombi ya unyenyekevu mbele za Mungu, bali ya kunung’unika tu na kulalamika.

Na kumbe hajui yule mtu aliyemsengenya pengine hata hakuwa na chuki na yeye kwa kiwango hicho anachokifikiri yeye, alizungumza tu kama mwanadamu ambaye hawezi kuuzuia ulimi wake, na pengine alishatubu na akawa anamuombea, lakini yeye kwa kuwa alishasikia fulani alimzungumzia vibaya, hilo jambo ataendelea nalo moyoni mwake kwa miaka na miaka..Atasema kwanza yule nilishawahi kumsikia akinisema hivi au vile.

Hivyo kabla hatujamkasirikia fulani kwasababu ya kutuzungumzia vibaya, tunapaswa tujiulize je na sisi hapo nyuma hatujawahi kumsengenya mtu yeyote katika maisha yetu?. Kwasababu Ule mstari wa 22 unasema;

“21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana.

22 Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine”.

Unaona? Imetumia neno “mara nyingi”. Pengine hata wewe ulishawahi kuzungumza maneno ambayo usingeweza kuyasema mbele ya huyo jirani yako, Lakini akija mbele yako humwekei vinyongo.

Hivyo na sisi pia tunapaswa tuachilie, tusiwe wapelelezi sana kwa yale tunayoyasikia kuhusu sisi, ukisikia mtu anakuambia fulani kakuzunguzia hivi au vile, usitake kujua zaidi ya hapo.. Kwasababu utajikuta una chuki na kila mtu, pengine hata mke wako, au dada yako, au mwanao, kwa sababu hiyo tu ya udadisi.

Tunapaswa tufahamu tu, kuzungumziwa vibaya au kusengenywa ni sehemu ya maisha yetu maadamu tupo hapa duniani. Hivyo hakuna haja ya kufuatilia fuatilia. Hiyo kazi tumwachie shetani, Sisi tutafute mambo msingi ya imani yetu. Na kamwe hutapata mtu mkamilifu asilimia mia moja hapa duniani, kama unayemtaka wewe, tukilielewa hilo tutaishi Maisha ya upendo na furaha sana.

Bwana atusaidie katika hilo kwenye safari yetu ya wokovu.

Je! Umeokoka? Je! Unajua kuwa hizi ni nyakati za mwisho? Na kwamba hatutakuwa na muda mrefu sana Unyakuo utapita, na mwisho wa dunia utafika? umejiandaaje? Je! Bado upo vuguvugu? Ikiwa hujamkabidhi Yesu maisha yako ni heri ufanye hivyo sasa. Na wokovu unakuja kwa kutubu dhambi zako na kwa kubatizwa ipasavyo hivyo, zingatia hayo na uyakamilishe. Kwani hizi ni dakika za majeruhi. Bwana yupo mlangoni kurudi.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kicho ni nini? (Waefeso 5:21, 2Samweli 23:3)

Kicho ni hali ya hofu. Kwamfano pale biblia inaposema kicho cha Bwana, inamaanisha  hofu ya Bwana.

Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyolitaja neno hilo katika biblia;

Matendo 9:31 “Basi kanisa likapata raha katika Uyahudi wote na Galilaya na Samaria, likajengwa, likiendelea na kuongezeka katika kicho cha Bwana, na faraja ya Roho Mtakatifu”.

Waefeso 5:20 “na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;

21 hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo”.

Waebrania 12:28 “Basi kwa kuwa tunapokea ufalme usioweza kutetemeshwa, na mwe na neema, ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza, pamoja na unyenyekevu na kicho”;

Kumbukumbu 7:21 “Usiingiwe na kicho kwa sababu yao; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu katikati yako, Mungu mkuu, mwenye utisho”.

Kumbukumbu 28:67, 2Samweli 23:3, Ayubu 15:4

Hivyo nasi pia tunapaswa tuwe na kicho cha Mungu ndani yetu, hicho ndicho kitakachotufanya tuishi maisha yampendazayo yeye hapa duniani, tukikosa hofu ya Mungu, hatutaona hata shida kuua, au kuiba, au kuzini, kwasababu hatumwogopi Mungu. Lakini ikiwa kicho chake kinakaa ndani yetu,tutaogopa kufanya mambo yasiyompendeza kwasababu tunajua Mungu wetu ni mkuu sana, anaweza kutenda lolote juu ya maisha yetu.

Yeremia 5:22 “Je! Hamniogopi mimi? Asema Bwana; hamtatetemeka mbele za uso wangu; mimi niliyeweka mchanga kuwa mpaka wa bahari, kwa amri ya daima, isiweze kuupita? Mawimbi yake yajapoumuka-umuka, hayawezi kushinda nguvu; yajapovuma sana, hayawezi kuupita.

23 Lakini watu hawa wana moyo wa kuasi na ukaidi; wameasi, wamekwenda zao.

24 Wala hawasemi mioyoni mwao, Basi, na tumche Bwana, Mungu wetu, aletaye mvua, mvua ya mwaka, na mvua ya vuli, kwa wakati wake; na kutuwekea juma za mavuno zilizoamriwa”.

Bwana atusaidie kicho chake kiumbike ndani yetu.

Shalom.

Angalia maana ya maneno mengine ya biblia chini.

Na ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MARINDA KATIKA BIBLIA NI KITU GANI?

Nyuni ni nini?(Mathayo 13:32, Sefania 2:14)

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

Baghala ni nini katika maandiko?(2Wafalme 5:16).

Njuga ni nini (Isaya 3:16, Zekaria 14:20)?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MARINDA KATIKA BIBLIA NI KITU GANI?

SWALI: Marinda yanayozungumziwa kwenye Yeremia 13:26 ni kitu gani?

Jibu: Tuanze kusoma kuanzia juu kidogo..

Yeremia 13: 24 “Kwa sababu hiyo nitawatawanya, kama makapi yapitayo, kwa upepo wa jangwani.

 25 Hiyo ndiyo kura yako, fungu lako ulilopimiwa na mimi, asema Bwana; KWA KUWA UMENİSAHAU, NA KUUTUMAİNİA UONGO.

26 Kwa ajili ya hayo, MİMİ NAMİ NİTAYAFUNUA MARİNDA YAKO MBELE YA USO WAKO, na aibu yako itaonekana.

27 Nimeona machukizo yako, naam, uzinifu wako, na ubembe wako, na uasherati wa ukahaba wako, juu ya milima katika mashamba. Ole wako, Ee Yerusalemu! Hutaki kutakaswa; mambo hayo yataendelea hata lini”.

Habari hiyo sio maonyo kwa wanawake, au wanaume wazinifu waliomwacha Mungu..La! Bali ni maonyo ya Taifa zima la Israeli lililomwacha Mungu..

Kama wewe ni mwanafunzi wa biblia itajua kuwa karibia mara zote, Mungu wa mbingu na nchi analifananisha kanisa lake na mwanamke, kadhalika alilifananisha Taifa lake la Israeli na mwanamke, Ndio maana utaona sehemu kadhaa anazungumza habari za binti Sayuni,..sasa binti Sayuni anayezungumziwa katika biblia sio binti fulani ambaye anaitwa Sayuni, au anayeishi mji unaoitwa Sayuni.. La!..bali binti Sayuni anayezungumziwa ni Taifa zima la Israeli. Yeremia 13:8-10. Kwa urefu kuhusu Binti Sayuni unaweza kufungua hapa >> SAYUNI

Sasa basi kama jamii ya watu wa Mungu, kwa ujumla inafananishwa na mwanamke, kibiblia jamii hiyo ikimwacha Mungu na kwenda kuifuata miungu mingine ya kigeni, mbele za Mungu jamii hiyo ya watu inaonekana kama inafanya ukahaba/inazini. Mbele za Mungu ni kama mwanamke anayezini..

Vifuatavyo ni baadhi ya vifungu vya biblia vinavyozungumzia habari ya Taifa la Israeli jinsi linavyofananishwa na Mwanamke, na jinsi linavyoonekana kama linazini pale linapomwacha Mungu…vifungu hivi unaweza kuvisoma binafsi.. (Kumbukumbu 31:16, Waamuzi 8:27, Isaya 23:17, Yeremia 3:1-7, 1Nyakati 5:24-26).

Kwahiyo tukirudi kwenye huo mstari unaozungumzia MARINDA.. Sasa marinda yanayozungumziwa hapo sio kitu kingine kinachoweza kudhaniwa, bali ni SKETI ZENYE MARINDA. Sketi za wanawake zamani na hata siku hizi zipo zinazotengenezewa na marinda.. Nguo za mabinti zote nyakati za zamani ni lazima zitengenezwe na marinda. Hivyo biblia inaposema hapo “ MIMI NAMI NITAYAFUNUA MARINDA YAKO MBELE YA USO WAKO”.. maana yake ni kwamba “Taifa hilo limemwacha Mungu na kwenda kuvua sketi zao na kufanya uasherati, kwa siri”… Basi Mungu atalifanya jambo hilo kwa wazi, atalivua nguo taifa hilo na aibu yake (au uchi wake) utaonekana.

Na kweli tunaona jambo hilo lilikuja kutimia kama lilivyo, pale wana wa Israeli walipomwacha Mungu na kukataa kutubu, na badala yake ikaenda kuabudu miungu migeni (yaani kufanya ukahaba)..Na baada ya kuonywa muda mrefu bila matunda yoyote, Mungu alilivua nguo taifa hilo kwa kulipeleka Babeli kwa aibu kubwa. (huko ndio kufunuliwa marinda).

Maombolezo 1:8 “Yerusalemu amefanya dhambi sana; Kwa hiyo amekuwa kama kitu kichafu; Wote waliomheshimu wanamdharau, Kwa sababu wameuona uchi wake; Naam, yeye anaugua, Na kujigeuza aende nyuma.

9 Uchafu wake ulikuwa katika MARINDA YAKE; Hakukumbuka mwisho wake; Kwa hiyo ameshuka kwa ajabu; Yeye hana mtu wa kumfariji; Tazama, Bwana, teso langu; Maana huyo adui amejitukuza.

10 Huyo mtesi amenyosha mkono wake Juu ya matamaniko yake yote; Maana ameona ya kuwa makafiri wameingia Ndani ya patakatifu pake; Ambao kwa habari zao wewe uliamuru Wasiingie katika kusanyiko lako.

Sio hilo tu, yapo pia baadhi ya Miji kama Ninawi, nayo pia Mungu aliyaonya na kuyapa ujumbe kama huo huo wa wana wa Israeli, kwamba yatubie uchafu wao,  lakini hayakufanya hivyo, na siku ilipofika marinda yao, yalifunuliwa kwa aibu na Mungu mwenyewe kama Israeli walivyofunuliwa.

Nahumu 3: 4 “Kwa sababu ya wingi wa ukahaba wa yule kahaba mzuri, yule bibi wa mambo ya uchawi, auzaye mataifa kwa ukahaba wake, na jamaa za watu kwa uchawi wake.

 5 Tazama, mimi ni juu yako, asema Bwana wa majeshi; NAMİ NİTAFUNUA MARİNDA YAKO MBELE YA USO WAKO; nami nitawaonyesha mataifa uchi wako, na falme aibu yako.

  6 Nami nitatupa uchafu uchukizao juu yako, kukufanya uwe mchafu, nami nitakufanya kuwa kitu cha kutazamwa kwa dharau.

7 Hata itakuwa, wote wakutazamao watakukimbia, wakisema, Ninawi umeharibika; ni nani atakayeuhurumia? Nikutafutie wapi wafariji?”

Mungu hajabadilika ni yule yule jana, leo na hata milele..alilowatendea wana wa Israeli, na Ninawi, kwa kumwacha yeye ndicho anachokifanya kwa wale wote wanaomwacha yeye na kufuata miungu yao wanayoijua..

Biblia inasema Roho Mtakatifu anatutamani kiasi cha kutuonea wivu. Wivu anaotuonea ni wivu kama ule wa mtu na mke wake..Unaweza kujua ni wivu mbaya kiasi gani, maana yake ni kwamba tunapomkataa Roho Mtakatifu tunamtia Mungu wivu sana na hivyo tunajitafutia kupata aibu kubwa kama hiyo waliyoipata wana wa Israeli na Ninawi na kufunuliwa marinda yao..

1Wakorintho 10:21  “Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani.

22  AU TWAMTIA BWANA WIVU? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye?”

Kama hujampa Kristo maisha yako, fahamu kuwa unamtia Bwana wivu..ni wakati wako sasa wa kutubu na kusalimisha maisha yako kwake.. Kama upo tayari kutubu leo basi fuatisha sala hii kwa kufungua hapa >> SALA YA TOBA.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?

NI KWA NAMNA GANI ROHO HUTUTAMANI KIASI CHA KUONA WIVU?

WAFIRAJI KWENYE BIBLIA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! ile habari ya watu wawili wenye pepo inajichanganya?

SWALI: Biblia inajichanganya yenyewe katika Marko 5:1-6 na Mathayo 8:28-31?..Kwa maana tunaona ni habari moja lakini kila moja imezungumzwa tofauti na nyingine.


JIBU: Tusome

Marko 5:1  “Wakafika ng’ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi.

2  Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu;

3  makao yake yalikuwa pale makaburini; wala hakuna mtu ye yote aliyeweza kumfunga tena, hata kwa minyororo;

4  kwa sababu alikuwa amefungwa mara nyingi kwa pingu na minyororo, akaikata ile minyororo, na kuzivunja-vunja zile pingu; wala hakuna mtu aliyekuwa na nguvu za kumshinda.

5  Na sikuzote, usiku na mchana, alikuwako makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikata-kata kwa mawe.

6  Na alipomwona Yesu kwa mbali, alipiga mbio, akamsujudia;

7  akapiga kelele kwa sauti kuu, akasema, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakuapisha kwa Mungu usinitese”

Lakini habari hiyo hiyo tunaisoma pia katika Mathayo inasema..

Mathayo 8:28  “Naye alipofika ng’ambo, katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile.

29  Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?

30  Basi, kulikuwako mbali nao kundi la nguruwe wengi wakilisha.

31  Wale pepo wakamsihi, wakisema, Ukitutoa, tuache twende, tukaingie katika lile kundi la nguruwe”.

Sasa swali la msingi la kujiuliza, ni kwanini habari zinatofautiana hapo?.

Ili kupata jibu la hili swali vizuri , hebu tutafakari mfano ufuatao.

Upo wewe na rafiki yako, mmeenda mahali labda kwenye interview ya kazi, mlipofika sehemu ya kazi, mkasimamishwa getini na mlinzi, ili mkaguliwe kabla ya kuingia ndani, na kwenye hiyo ofisi ndogo ya mlinzi ndani kulikuwa na mlinzi mwingine wa pili, alikuwa kasimama pembeni akitazama, ambaye ni kama msaidizi, hivyo baada ya kukaguliwa na huyu mlinzi wa kwanza hapo nje, mkaandikishwa majina yenu,  kisha mkaruhusiwa muingie ndani. Na mlipomaliza interview mlitoka getini mkasaini kisha mkaondoka.

Mlipofika majumbani kwenu mkaulizwa kila  mmoja mambo yaliendaje  huko?..Na ushuhuda wa kila mmoja ulikuwa kama ifuatavyo.

WEWE: Wewe ulianza kusimulia, kwamba baada ya kutoka nyumbani mlifikia salama hadi sehemu ya interview lakini mlipofika getini mlisimamaishwa mkakaguliwa na MLINZI, kisha mkaruhusiwa kuingia ndani, na kufanya interview salama na kutoka. (sasa zingatia hilo neno MLINZI {maana yake ni mmoja}).

RAFIKI YAKO: Ushuhuda wa rafiki yako, naye akasimulia akasema… “Tulipotoka hapa tulifika kweli eneo la kazi, lakini tulipofika pale hatukuingia moja kwa moja, kulikuwa na WALINZI, pale getini wakatukagua, kisha wakaturuhusu kuingia ndani, tukaenda kufanya interview salama na tukaondoka. (Zingatia hilo neno WALINZI, maana yake ni zaidi ya mmoja)”.

Sasa hao ni mashuhuda wawili wanaelezea tukio moja!..Je kwa shuhuda zao hizo walizotoa, ni kwamba wametoa ushuhuda wa uongo au wa kujichanganya?.. Maana wa kwanza kasema kakaguliwa na MLİNZİ MMOJA, wa pili kasema KAKAGULİWA NA WALİNZİ maana yake ni zaidi ya mmoja… Sasa yupi tumwamini hapo, na yupi tusimwamini?.

Umeona?..ukitafakari kwa makini utagundua kuwa sio kwamba wote ni waongo, isipokuwa kila mmoja kaelezea kile alichokiona chenye umuhimu zaidi kwake..Ndio maana huyu wa kwanza kaeleza kakaguliwa na mlinzi mmoja..jambo ambalo ni kweli kabisa!..Aliyemkagua ni mlinzi mmoja tu na sio wawili, yule wa pili alikuwa ndani pembeni akitazama.

Na rafiki yako naye alikuwa yupo sahihi kusema “tulikaguliwa na walinzi” kwasababu ni kweli pale kulikuwa na walinzi wawili, ambao kazi yao wote ni moja, na wote wanashirikiana. Hivyo naye pia hajatoa ushuhuda wa uongo, kazungumza ukweli.

Sasa kwa mfano huu, tutakuwa tumeanza kupata picha ni nini kilichokuwa kinaendelea hapo kwenye Mathayo na Marko.

Ni kwamba Ushuhuda wa Mathayo hauwezi kufanana na ushuhuda wa Marko wala hauwezi kufanana na ushuhuda wa Luka asilimia mia moja. Lazima kutakuwa na tofauti kidogo, vinginevyo kama utakuwa umefanana asilimia mia basi ni uthibitisho kuwa sio ushuhuda wa ukweli lazima kutakuwa na (ku-copy na ku-paste). Na pia kulikuwa hakuna haja ya kuwepo injili tofauti tofauti kwasababu zote zingekuwa zinaeleza kitu kimoja.

Hiyo ndio sababu utaona Marko anatoa ushuhuda wa mtu mmoja aliyetoka makaburini, na Luka anatoa ushuhuda wa watu wawili. Lakini kiuhalisia walikuwepo pale watu wawili waliotoka makaburini, isipokuwa ndiye aliyekuwa amepagawa zaidi na ndiye aliyekuja kumsujudia Yesu na kumsihi asimtese.

Na sio tukio hilo tu katika biblia, ambapo habari mbili zinaonekana zikishuhudiwa tofauti. Lipo tukio lingine wakati Petro anamsaliti Bwana, sehemu moja inasema “kabla jogoo hajawika mara mbili utanikana mara tatu” na katika kitabu kingine inasema tu “kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu”. Sababu ni hizo hizo tulizozitaja hapo juu.

Bwana akubariki

Tunaomba usibadilishe chochote katika ujumbe huu na mwingine wowote, na pia jihadhari na watumishi wa shetani ambao wanatumia masomo haya, kwa kusema kuwa wao ni waalimu wa huduma hii, na mwisho  wanaomba hela!, wanaochangia huduma hii ni wale wanaoguswa wenyewe kwa moyo wao kuchangia lakini sio kwa kuombwa fedha. Wingu la Mashahidi haijawahi kumpigia mtu simu na kumwomba hela. Ukiona mtu yeyote kashare au kushiriki masomo haya na mwisho akaweka namba zake za simu tofauti na hizi zetu +255789001312. Tunaomba umwonye aache kufanya hivyo au utujulishe kwa namba yetu hii hii +255789001312

Maran atha

Na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?

Jehanamu ni nini?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nyuni ni nini?(Mathayo 13:32, Sefania 2:14)

Nyuni ni neno linalomaanisha ndege.

Hivi ni baadhi ya vifungu katika biblia vinavyolitaja neno hilo;

Mathayo 13:31 “Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake;

32 nayo ni ndogo kuliko mbegu zote; lakini ikiisha kumea, huwa kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti, hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi yake”.

Zaburi 102:5 “Kwa ajili ya sauti ya kuugua kwangu Mifupa yangu imegandamana na nyama yangu.

6 Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani, Na kufanana na bundi wa mahameni”.

Sefania 2:14 “Na makundi ya wanyama watalala kati yake, wanyama wote wa mataifa; mwari-nyuni na nungu watakaa juu ya vichwa vya nguzo zake; sauti yao itasikiwa madirishani; vizingitini mwake mtakuwa ukiwa; kwa maana ameifunua kazi ya mierezi”.

Soma pia Kumb 14:11,Ayubu 12:7

Kibiblia watu wa mataifa(wasiomjua Mungu) wanafananishwa na nyuni wa angani, na ndio maana utaona Bwana Yesu anaufananisha ufalme wa mbinguni na chembe ya haradali na kusema japo ni ndoto kuliko mbegu zote..Lakini inapokuwa ndani ya mtu inageuka na kuwa kubwa sana, kiasi cha kutoa matawi makubwa na watu kukaa chini yake kupumzika(yaani kujifunza Neno la Mungu, na kupokea baraka zote)

Hivyo na sisi pia tunapewa hamasa, tupende kuutafuta ufalme wake, kwani leo hii unaweza kuonekana ni kitu kisichokuwa na maana, lakini kama tukiendelea kumtafuta Mungu na kutaka kujua mapenzi yake ni nini maishani mwetu, Basi kesho tutakuwa ni msaada mkubwa kwa maelfu ya watu(Nyuni) kumjua yeye.

Bwana akubariki.

Tazama tafsiri ya maneno mengine ya biblia chini.

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Arabuni maana yake ni nini?

Kutabana ni nini? (Mika 5:12)

Fumbi ni nini?(Ayubu 6:15)

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kutabana ni nini? (Mika 5:12)

Kutabana ni kitendo kinachofanywa na wachawi cha kutabiri mambo yajayo kwa kutazama vitu fulani. Kwamfano wasomaji nyota, wasomaji viganja, watazamaji wa nyakati mbaya n.k. wote wanatabana

Utalisoma neno hilo kwenye kifungu hiki;

Mika 5:12 “nami nitakatilia mbali uchawi, usiwe mkononi mwako; wala hutakuwa tena na watu wenye kutabana;

13 nami nitakatilia mbali sanamu zako na nguzo zako, zitoke kati yako; wala hutaiabudu tena kazi ya mikono yako”.

Ukweli ni kwamba hakuna kiumbe chochote duniani, mbinguni au kuzimu chenye uwezo wa kutabiri au kujua mambo yajayo isipokuwa Mungu tu peke yake. Alishaliweka hilo wazi kuwa hakuna kitu chochote kinachoweza kujua hatma ya mtu isipokuwa yeye peke yake. Anasema;

Isaya 41:21 “Haya, leteni maneno yenu, asema Bwana; toeni hoja zenu zenye nguvu, asema mfalme wa Yakobo.

22 Wayatangaze na kutujulisha yatakayokuwa; watuonyeshe mambo ya zamani, ni mambo gani, tukapate kuyatia moyoni, tukajue mwisho wake; au wamdhihirishie yatakayotokea baadaye.

23 Tujulisheni yatakayokuwa baadaye, nasi tutakiri ya kuwa ninyi ni miungu; naam, tendeni mema au tendeni mabaya, ili tujipime, tukaone pamoja.

24 Tazameni, ninyi si kitu, tena kazi yenu si kitu; awachaguaye ninyi ni chukizo”.

Hivyo hatupaswi kufiriki kutabana kunaleta matokeo yoyote, zaidi ni kudanganywa  kama sio kurushiwa mapepo. Shetani sikuzote ni mwongo.

Isaya 46:9 “kumbukeni mambo ya zamani za kale; maana mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi;

10 nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote”.

Kama ukiwa ndani ya Kristo, yeye mwenyewe atakufunulia hatma njema ya maisha yako ya sasa na ya baadaye. Lakini ikiwa utatafuta ujuzi au maarifa yoyote ya mambo yajayo kutoka kwa wasoma nyota ujue unapotezwa.

Hivyo kama hujaokoka,  na upo tayari kutubu na kumkabidhi Kristo maisha yako, akufanye kiumbe kipya ni uhakika kuwa mbele yako ipo salama. Je! Upo tayari kufanya hivyo leo? Kama jibu ni ndio basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba na kupata maelekezo mengine ya kiroho  >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tazama maana za maneno mengine ya biblia chini;

Na kama  utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Fumbi ni nini?(Ayubu 6:15)

Chamchela ni nini kwenye biblia?(Zaburi 58:9, Amosi 1:14)

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

Hori ni nini kibiblia (Waamuzi 5:17, Luka 2:7)?

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya “chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu”?

SWALI: Biblia ina maana gani inaposema “chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu”?

Jibu: Tusome..

1Wakorintho 8:8 “Lakini chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu; maana, tusipokula hatupunguziwi kitu, wala tukila, hatuongezewi kitu.

9  Lakini angalieni huu uwezo wenu usije ukawakwaza wale walio dhaifu”.

“Kuhudhurisha” maana yake ni “kutusogeza karibu na kitu”.. Hivyo biblia inaposema chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu, maana yake ni kwamba “chakula hakitusogezi sisi kuwa karibu na Mungu”.

Huwezi kula mboga nyingi au nyama, au aina fulani ya chakula kikamfanya Mungu awe karibu na wewe zaidi, au huwezi kula chakula fulani kikakufanya Mungu asikukaribia..Kitu pekee ambacho kitatufanya sisi tumkaribie Mungu au Mungu ajitenge na sisi ni dhambi!..basi hicho tu!, wala hakuna kingine..

Isaya 59:1 “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;

2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusiki”

Kwahiyo tukila chakula chochote iwe nyama ya nguruwe, ya ng’ombe au chochote kile, hata tukila mboga, au aina yoyote ya chakula, hiyo haitusogezi wala kutuweka mbali na Mungu. Ndio maana ukiendelea kusoma mbele..Mtume Paulo anaendelea kusema maneno haya..“maana, tusipokula hatupunguziwi kitu, wala tukila, hatuongezewi kitu.”

Sasa unaweza kuuliza, Vipi kuhusu pombe?, na majani ya bangi je? Ni sahihi kuyatumia kama mboga?. vipi kuhusu sumu? Tunywe sumu na kusema haituhudhurishi mbele za Mungu?.

Pombe yoyote ile ina kilevi, ambacho kwa jinsi mtu anavyozidi kuinywa,inambadilisha mtu huyo akili (inamtoa katika hali ya asili, na kumpeleka katika hali nyingine isiyo ya asili ya kiakili, ambapo matokeo ya hiyo hali ni kuzaliwa kwa mambo maovu..mfano wa mambo hayo  ni ugomvi, uasherati, mizaha, matusi, hasira, mafarakano, kutokujali na mambo mengine mengi ambayo ndiyo yanayomchukiza Mungu).

Kwahiyo pombe sio sawa kuinywa, vile vile na bangi sio sawa kuivuta wala kutumia majani yake kama mboga, kwasababu zina vilevi ambavyo vinamuharibu akili na kumfanya atoe mambo maovu moyoni, na kumfanya awe najisi kama Bwana Yesu alivyosema katika… Mathayo 15:19 “ Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano; 20  hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi”

Kimiminika chenye kilevi kama Spirit, kinaweza kutumika kwa matumizi mengine ya nje kama ya kusafishia vidonda, au kuoshea vifaa lakini si kwa kuinywa, kwasababu hizo tulizojifunza hapo juu…lakini nyama ya nguruwe au ya ng’ombe haina kilevi chochote, ambacho mtu akitoka hapo, ataharibika akili na kuwa mtukanaji, au kuropoka, au kuwa na mizaha, au hasira, au itamfanya atafute kufanya uasherati wala uzinzi.

Waefeso 5:17  “Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.

18  Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho”

Ufisadi unaozungumziwa hapo sio ule wa “kuiba pesa” bali ni “tabia ya uasherati uliopindukia, ambyo imechanganyikana na mizaha, na kutokujali”

Kwahiyo chakula chochote kile ambacho hakitufanyi tutoe mambo machafu mioyoni mwetu,  hicho sio dhambi kukila, kwasababu hakituongezei chochote mbele za Mungu wala hakitupunguzii chochote kama biblia ilivyosema hapo.

Sasa swali la mwisho ambalo utauliza ni je! Kama chakula hakitusogezi mbele za Mungu, vipi kuhusu Meza ya Bwana?..je kile si chakula?, na mbona maandiko yanasema tunapoinywa damu yake tunatangaza mauti yake hata ajapo?.

Agizo la kushiriki meza ya Bwana ni agizo la kiibada, kadhalika na agizo la ubatizo..Hatuwezi kusema mkate ule ni chakula kitakatifu kwamba kila tunapokula hata tukiwa nyumbani au tukiwa kwenye sherehe ni kitu kitakatifu, hapana!… wapo wanaoitengeneza mikate ile kwa mfumo ule ule na kuitumia nyumbani mwao kama chakula cha siku zote, na isihesabike kama wameshiriki, kwasababu zile ni kama chapati tu! İsipokuwa zenyewe ni ngumu kidogo..Kwahiyo hata mtu asiyeamini anaweza kutengeneza nyumbani kwake akala kama chakula kingine tu, na isihesabike chochote kwake.

Umeona?..lakini Mkate ule unapotumika kwenye ibada ya meza ya Bwana (Pale waumini wanapokutana na kusema huu ni ishara ya mwili wa Kristo), tayari unabadilika maana, kulingana na tukio hilo, kadhalika maji yanapotumika katika ibada ya ubatizo, tayari yanabadilika maana kulingana na tukio hilo. Lakini baada ya tukio la ibada, yale maji ni kama maji mengine yoyote yanaweza kutumika kuogea au kunyeshea au yakamwagwa… Kadhalika mikate ile inayotumika katika meza ya Bwana au ngano ile baada ya ibada, inakuwa ni ngano kama ngano nyingine tu…haitusogezi mbele za Mungu.

Je umempokea Yesu?..au bado unatanga tanga na mambo ya duniani tu!..Biblia inasema katika Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”.

Umeona?..usipotaka kumgeukia muumba wako leo..Ipo miaka inakuja huko mbeleni, ambayo nafasi unayoichezea leo, hutaipata tena..Miaka hiyo utakosa furaha na kutakuwa hakuna msaada..Hivyo kama hujampokea Yesu, nafasi ni sasa..Unachopaswa kufanya ni kutubu kwa kumaanisha kuziacha dhambi zako zote. Kisha kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele na kwa Jina la Yesu, na kisha kupokea Roho Mtakatifu na kudumu katika Imani. Ukikubali kufanya hivyo Bwana atakupokea na kukutengeneza

Marana atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

JE! SISI KAMA WAKRISTO NI DHAMBI KUSHEHEREKEA KRISMASI?.

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Fumbi ni nini?(Ayubu 6:15)

Fumbi ni ni neno linalomaanisha kijito,

Utalisoma katika mstari huu;

Ayubu 6:15 “Ndugu zangu wametenda udanganyifu kama kijito cha maji. Mfano wa fumbi la vijito vipitavyo.

16 Vilivyokuwa vyeusi kwa sababu ya barafu, Ambamo theluji hujificha”.

Angalia tafsiri maneno mengine ya biblia chini.

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Chamchela ni nini kwenye biblia?(Zaburi 58:9, Amosi 1:14)

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

Shokoa ni nini katika biblia?

Hori ni nini kibiblia (Waamuzi 5:17, Luka 2:7)?

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Chamchela ni nini kwenye biblia?(Zaburi 58:9, Amosi 1:14)

Chamchela ni neno linalomaanisha  ‘kisulisuli’,

Utalisoma neno hilo kwenye vifungu hivi katika biblia;

Zaburi 58:9 “Kabla ya masufuria yenu kupata moto wa miiba, Ataipeperusha kama chamchela, Iliyo mibichi na iliyo moto. ”

Isaya 29:5 “Lakini wingi wa adui zako utakuwa kama mavumbi membamba, na wingi wao watishao utakuwa kama makapi yapitayo; naam, itakuwa mara na kwa ghafula.

6 Naye atajiliwa na Bwana wa majeshi kwa ngurumo, na tetemeko la nchi, na sauti kuu, na chamchela, na tufani, na mwali wa moto uteketezao”.

Amosi 1:14 “lakini nitawasha moto katika ukuta wa Raba, nao utayateketeza majumba yake; pamoja na kupiga kelele siku ya vita, pamoja na tufani katika siku ya chamchela”;

Hivyo,Chamchela au kisulisuli ni moja ya njia ambayo Mungu aliitumia kuonyesha mambo mawili makuu. Jambo la kwanza ni ili kudhihirisha ukuu wake kwa wanadamu, na jambo la pili ni kuonyesha ghadhabu yake kwa waovu.

Kwamfano utaona alijifunua kwa Ayubu kwa njia hii pale alipotaka kumuonyesha ukuu wake na uweza wake.

Ayubu 38:1 “Ndipo Bwana akamjibu Ayubu katika upepo wa kisulisuli, na kusema,

2 Ni nani huyu atiaye mashauri giza Kwa maneno yasiyo na maarifa”?

Soma pia Ayubu 40:6

Vilevile utaona pia anajidhihirisha kwa njia hii, kuonyesha ukali wa hasira yake jinsi anavyoweza kuwapeperusha waovu wasionekane kabisa kwa mfano wa kisulisuli.

Isaya 41:16 “Utawapepeta, na upepo utawapeperusha; upepo wa kisulisuli utawatawanya; nawe utamfurahia Bwana, utajitukuza katika Mtakatifu wa Israeli”.

Yeremia  23:19 “Tazama, tufani ya Bwana, yaani, ghadhabu yake, imetokea; ni dhoruba ya kisulisuli; itapasuka, na kuwaangukia waovu vichwani. 20 Hasira ya Bwana haitarudi, hata atakapokwisha kuyatimiza makusudi ya moyo wake; katika siku za mwisho mtalifahamu neno hili kabisa”.

Nasi pia tunapaswa tuishi maisha yampendezayo Mungu angali tukiwa hapa duniani, ili Bwana atakapojifunua kwetu, ajifunue kwa sauti ya upole na utulivu, kama alivyofanya kwa Eliya na sio kwa Chamchela.

Shalom.

Tazama maana ya maneno mengine ya kwenye biblia chini.

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

Kongwa ni nini kwenye biblia?(Wagalatia 5:1)

Hori ni nini kibiblia (Waamuzi 5:17, Luka 2:7)?

Neno Bildi linamaanisha nini kwenye biblia(Matendo 27:28) ?

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post