Kongwa ni nini kwenye biblia?(Wagalatia 5:1)

Kongwa ni nini kwenye biblia?(Wagalatia 5:1)

Kongwa ni kifungo cha shingoni. Kwa jina lingine ni nira. Tazama picha.

Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyolitaja neno hilo;

Kumb 28:48 “kwa hiyo utawatumikia adui zako atakaowaleta Bwana juu yako, kwa njaa, na kwa kiu, na kwa uchi, na kwa uhitaji wa vitu vyote; naye atakuvika kongwa la chuma shingoni mwako, hata atakapokwisha kukuangamiza”.

Matendo 15:10 “Basi sasa mbona mnamjaribu Mungu na kuweka kongwa juu ya shingo za wanafunzi, ambalo baba zetu wala sisi hatukuweza kulichukua”.

Wagalatia 5:1 “Katika ungwana huo Kristo alituandika huru; kwa hiyo simameni, wala msinaswe tena chini ya kongwa la utumwa”.

1 Timotheo 6:1 “Wo wote walio chini ya kongwa, hali ya utumwa, na wawahesabie bwana zao kuwa wamestahili heshima yote, jina la Mungu lisitukanwe wala mafundisho yetu.

Walawi 26:13 “Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, niliyewaleta mtoke katika nchi ya Misri, ili msiwe watumwa wao; nami nimeivunja miti ya kongwa lenu, nikawaendesha mwende sawasawa”.

1Wafalme12:4 “Baba yako alilifanya zito kongwa letu; basi sasa utupunguzie utumwa mzito tuliotumikishwa na baba yako, na lile kongwa zito alilotutwika, nasi tutakutumikia”.

Swali ni je! sisi tupo chini ya kongwa la nani? La Mungu au la shetani?. Mtu yeyote ambaye hajaokoka, haijalishi atakuwa na mafanikio makubwa kiasi gani, tayari yupo chini ya kongwa la shetani, na anaongozwa kuelekea kuzimu. Lakini aliyemwamini Yesu na kuoshwa dhambi zake, yupo chini ya kongwa/Nira ya Kristo, akiongozwa kuelekea uzimani (Mathayo 28:11).

Hivyo tujitathimini sisi tupo upande gani, na kama hatujaokoka, basi tumpe Bwana leo maisha yetu ayaokoe, kwasababu hizi ni nyakati za mwisho.

Shalom

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Hori ni nini kibiblia (Waamuzi 5:17, Luka 2:7)?

Nyungu ni nini kibiblia?(Ayubu 41:20,31, Waamuzi 6:19)

Areopago ni nini? Kwanini mtume Paulo walimpeleka huko?

Arabuni maana yake ni nini?

Nyama zilizosongolewa ni zipi?Je kunywa damu ni dhambi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Jacob ayubu
Jacob ayubu
2 years ago

Amen