Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

Zaburi maana yake ni “nyimbo takatifu”. Hivyo kitabu cha Zaburi katika biblia, ni kitabu cha Nyimbo takatifu. Zimeitwa nyimbo takatifu kwasababu zimetungwa kwa lengo la kumrudisha mtu kwa muumba wake, kwa njia hiyo ya kusifu na kumwimbia. Pia Pamoja na kwamba zilikuwa ni nyimbo, lakini ndani yake pia zilikuwa zimejaa unabii wa mambo yanayokuja.

Katika agano la kale nyimbo hizo ziliimbwa na wayahudi (yaani waisraeli) wakati wa kuabudu katika masinagogi yao, na hata leo wakristo tunatumia baadhi ya mashairi hayo kutengeneza nyimbo nzuri za kumwimbia Mungu wetu na kumshukuru na kumsifu.

Kitabu  cha Zaburi katika biblia kimeandikwa sehemu kubwa na Mfalme Daudi, wapo wengine wachache walioshiriki kuandika kitabu hicho kizima, lakini sehemu kubwa imeandika na Daudi. Na Daudi alianza kumwimbia Mungu tangu udogoni, biblia inasema hivyo.

Pia wapo wengine walioandika Zaburi (Nyimbo) katika biblia, ambazo mashairi yao hayawekwa katika kitabu cha Zaburi. Mfano wa watu hao ni Musa na Sulemani.  Kwamfano Zaburi za Musa unaweza kuzisoma katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 32.

Jambo dogo tunaloweza kujifunza ni kwamba..Zaburi hizi zilizoandikwa na Daudi, zimewezwa kutukuzwa na Mungu mwenyewe mpaka leo, kwasababu zimejaa maneno ya sifa kwa Mungu, na ya kumtukuza sana. Kwamfano hebu tafakari maneno ya mistari hii..

Zaburi 145:1 “Ee Mungu wangu, Mfalme, nitakutukuza, Nitalihimidi jina lako milele na milele.

 2 Kila siku nitakuhimidi, Nitalisifu jina lako milele na milele.

 3 Bwana ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana, Wala ukuu wake hautambulikani.

 4 Kizazi kwa kizazi kitayasifu matendo yako, Kitayatangaza matendo yako makuu.

 5 Nitaifikiri fahari ya utukufu wa adhama yako, Na matendo yako yote ya ajabu.

 6 Watu watayataja matendo yako ya kutisha, Nami nitausimulia ukuu wako.

 7 Watalihubiri kumbukumbu la wema wako mkuu. Wataiimba haki yako.

8 Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma, Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema,

9 Bwana ni mwema kwa watu wote, Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote”.

Hivyo na sisi pia inapendeza kama tukimwimbia Mungu wetu, wimbo wa sifa za kweli za kumtukuza yeye na kumpa yeye utukufu, kwasababu Mungu anaketi katika sifa, na ni vizuri kabisa tukamwimbia kwa vinanda vya zote,

Zaburi 147:1 “Haleluya. Msifuni Bwana; Maana ni vema kumwimbia Mungu wetu, Maana kwapendeza, kusifu ni kuzuri”

 Zaburi 149:1 “Haleluya. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Sifa zake katika kusanyiko la watauwa”

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

TENZI ZA ROHONI

SIKU YA HUKUMU ITAKUWAJE?

JE KUHUDUMU KWA NYIMBO ZA INJILI KUKOJE?

YOTE NAMTOLEA YESU_Tenzi za Rohoni.

MWAMBA WENYE IMARA

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
James Mwansyemela
James Mwansyemela
1 year ago

Ahsante kwa ujumbe mwema.