Category Archive Uncategorized @sw-tz

NIFINYANGE BWANA

Jina la Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe sana, karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu lililo taa na mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).

Yeremia 18: 1 “Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, kusema,

2 Ondoka, ukashuke mpaka NYUMBA YA MFINYANZI, na huko nitakusikizisha maneno yangu.

3 Basi nikashuka mpaka nyumba ya mfinyanzi, na tazama, alikuwa akifanya kazi yake kwa magurudumu. 4 NA CHOMBO KILE, ALICHOKUWA AKIKIFINYANGA, KILIPOHARIBIKA MKONONI MWAKE YULE MFINYANZI, ALIKIFANYIZA TENA KUWA CHOMBO KINGINE, kama alivyoona vema yule mfinyanzi kukifanya”.

Katika mstari wa 4 tunasoma kuwa Mfinyazi alikifinyanga chombo kilichoharibika na kuwa chombo kingine, zingatia hilo neno “chombo kingine” maana yake sio tena chombo kile cha kwanza kilichoharibika.

Tuchukue mfano labda mfinyazi huyu alifinyanga kikombe cha maji hapo kwanza, na baadae akaone kimeharibika au kina kasoro, ndipo anapokivunja vunja kile kikombe cha udongo na kuutia tena maji na kuufinyanga tena kuwa sahani..

Sasa udongo ni ule ule umeweza kutoa chombo kingine kipya tofauti na kile cha kwanza, na MUNGU alimwambia hivo hivyo YEREMIA, lakini Yeremia hayupo sasa, ila sisi tupo, hivyo anatuambia sisi kuwa tujifunze kwa Mfinyanzi kwakuwe yeye (MUNGU) ndiye mfinyanzi mkuu wa maisha yetu.

Yeremia 18: 5 “Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,

6 Ee nyumba ya Israeli, je! Siwezi mimi kuwatendea ninyi vile vile kama mfinyanzi huyu alivyotenda? Asema Bwana. Angalieni, KAMA UDONGO ULIVYO KATIKA MKONO WA MFINYANZI, NDIVYO MLIVYO NINYI KATIKA MKONO WANGU, EE NYUMBA YA ISRAELI”.

Je wewe ni chombo cha aina gani?..

Kama maisha yako yametawaliwa na dhambi basi fahamu kuwa ni dhahiri kuwa wewe ni chombo kilichoharibika, kama maisha yako yametawaliwa na ugomvi, uasherati, wizi, masengenyo, kiburi na mambo mengine yote ambayo ni kinyume cha Neno la MUNGU (yaliyotajwa kwenye Wagalatia 5:19-20), huu ni wakati wa wewe kumkimbilia mfinyazi Mkuu YESU KRISTO, akufinyange kuwa chombo kingine cha heshima..

Warumi 9:21 “Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?”

Bwana YESU anaweza kukufanya kuwa mwingine kabisa, mtu wa maana kabisa, ambapo ile hali yako ya ulevi wa pombe au ulevi wa anasa inayokusumbua, kinachotakiwa tu ni kukiri kuwa wewe ni mkosaji mbele zake na unahitaji msaada wake,  na baada ya hapo kutubu dhambi zako mbele yake huku ukidhamiria kabisa kuacha mambo yote mabaya, na kumwambia naomba unifinyange tena, kupitia Roho wake mtakatifu atakayeingia ndani yako atakugeuza na kuwa mtu mwingine.

Kumbuka toba isiyo ya kumaanisha haileti matokeo yoyote kwa mtu anayetaka mabadiliko, hakikisha unapotubu dhamiria kujitakasa, kwa kujitenga na vichocheo vyote vya dhambi, kama ulikuwa ni mlevi acha kwenda Bar, kama ulikuwa unajiuza jizuie kwa bidii kwenda vituo vya ulivyokuwa unafanya biashara hiyo, ili uumpe nafasi Roho Mtakatifu ndani yako kukufinganya upya kuwa chombo kingine.

2Timotheo 2:21 “Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, kimetengenezwa kwa kila kazi iliyo njema”.

Bwana YESU akubariki sana.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ATAWAFANYIA WAMCHAO MATAKWA YAO.

Zaburi 145:19 “Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa”.

Pamoja na kwamba tumeagizwa kuomba “Mapenzi yake yatimie/yatimizwe (Mathayo 6:10”.

Lakini “Siri” moja kuu ni kwamba zaidi ya asilimia 90 ya Maombi ya wanaomcha MUNGU ni mapenzi ya MUNGU.Kwanini?..

Kwasababu maandiko yanatuambia hapo kuwa “Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa”.

Zingatia hilo neno “Atawafanyia wamchao matakwa yao”.

Kumbe Mungu anawapatia watu wake wanaomcha “Matakwa yao, yaani haja zao wanazozitaka”.

Kwa mtu anayemcha Mungu akiomba amani, ni asilimia kubwa ya hitaji lake hilo kuwa ni mapenzi ya MUNGU.

Mtu anayemcha MUNGU akiomba afya, ni asilimia zaidi ya nusu kuwa anaomba jambo ambalo ni mapenzi ya MUNGU.

Mtu anayemcha MUNGU akiomba akiomba mambo mengine yote ikiwemo mafanikio ya kiroho na kimwili ni mapenzi ya MUNGU, kwasababu MUNGU anawapa wamchao matakwa yao.

Je unataka kupewa matakwa yako na MUNGU?.Jibu ni rahisi “Mche Mungu tu”..Na Biblia inasema kumcha Mungu ndio hekima na kuepukana na uovu ndio ufahamu (Ayubu 28:28).

Sasa hatuwezi kumcha MUNGU kwa nguvu zetu, inahitajika kuwezeshwa na Roho Mtakatifu, kwasababu tabia ya kumcha MUNGU, ni zao la Roho Mtakatifu.Isaya 11:2 “Na roho ya BWANA atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, ROHO YA MAARIFA NA YA KUMCHA BWANA”.

Sasa kama kumcha Bwana ni zao la Roho Mtakatifu, je tunampataje Roho Mtakatifu..

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”

Kumbe kanuni ya kupokea Roho ni kutubu na kubatizwa kwa jina la YESU KRISTO!.

Basi maana yake tukitubu na kubatizwa tutapokea Roho Mtakatifu kama ilivyoandikwa, na matokeo ya kujaa Roho Mtakatifu, ni uwezo wa kumcha MUNGU kuingia ndani yako.Na matokeo ya kumcha MUNGU sana ni kusikiwa maombi yako na Bwana kukupa matakwa yako.

Je umeokoka?..Je unamcha Bwana?.

Zaburi 112:1 “Haleluya. Heri mtu yule amchaye BWANA, Apendezwaye sana na maagizo yake.

2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa”.

3 Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yakaa milele”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

AMBATANA NA WALIO HAI ROHONI.

Jina la Bwana YESU libarikiwe, karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu, lililo taa na Mwanga wa njia yetu.

Utatamani kutembea na wenye vyeo vikubwa vya ulimwengu, ambao wengi wa hao ni wafu kiroho,

Utatamani kuolewa na wenye mali nyingi, na uwezo mkubwa ambao wengi wa hao ni wafu rohoni.

Utawadharau wanaoonekana dhaifu na wanyonge ambao Biblia inawataja kama matajiri wa imani na walio hai kiroho..

Yakobo 2:5 “Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao?”

Dada ni heri uambatane na huyo mtu ambaye unamwona leo ni maskini lakini anaye YESU, kuliko uende kuolewa na  tajiri ambaye  hana YESU maishani ( ni mfu kiroho).

Heri uwe na marafiki maskini lakini wanaye YESU kuliko uwe na marafiki matajiri ambao ndani yao hawana uzima.

Huyo tajiri kwako ni “Simba” na huyo maskini kwako ni “Mbwa”…ambaye ni kama hana hadhi mbele ya macho yako lakini Biblia inatufundisha kinyume na hilo..

Mhubiri 9:4 “Kwa kuwa liko tumaini kwa yule aliyeambatana na wote walio hai; (maana ni afadhali mbwa aliye hai kuliko simba aliyekufa)”.

Ni afadhali mbwa, anayeishi, maana yake ni heri mtu maskini na mdhaifu mwenye uhai wa rohoni kuliko mtu aliye simba (yaani mwenye nguvu na mkali) lakini ni mfu rohoni.

Chagua  kwa makini nani wa kuambatana naye..

2 Wakorintho 6:14 “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?

15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari?Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?”

Bwana atusaidie..

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kuadibu ni nini kibiblia? (Zaburi 94:12)

Kitendo cha kumtia mtu adabu ndio kuadibu. Maana yake kuchukua hatua za makusudi kuadhibu, au kukaripia, au kuonyoosha mwenendo lakini kwa lengo la kujenga sio kulipiza kisasi.

Neno hilo utalipata kwenye vifungu hivi.

Zaburi 94:12

[12]Ee BWANA, heri mtu yule umwadibuye, Na kumfundisha kwa sheria yako; 

Zaburi 94:10

[10]Awaadibuye mataifa asikemee? Amfundishaye mwanadamu asijue? 

Mungu akiitwa Baba, basi tujue kuwa sisi ni watoto wake, na kama ni watoto wake basi atatuadabisha pale tunapokosea..

Kubali kuadibiwa na Bwana…

Shalom.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Beliari ni nini? (2Wakorintho 6:15)

‘laana ya torati’ maana yake ni nini?

Mapokeo ni nini?

WEKA MOYO WAKO UPANDE WAKO WA KUUME.

Jina la Mwokozi YESU libarikiwe, karibu tujifunze Biblia, Neno la MUNGU wetu lililo taa na Mwanga wa njia yetu (Zab. 119:105).

Sayansi ya mwili inatuonesha kuwa “moyo” wa mtu upo upande wake wa “kushoto”..jambo ambalo ni kweli kabisa, ukiweka mkono wako kufuani utaona moyo ni kama umelalia upande wa kushoto.

Lakini katika roho ni kinyume chake, Kwani Biblia inatufundisha kuwa Moyo wa mwenye hekima upo upande wake wa kulia(kuume), na kinyume chake moyo wa mpumbavu upo upande wake wa kushoto.

Mhubiri 10:2 “MOYO WAKE MWENYE HEKIMA UPO UPANDE WA KUUME; Bali moyo wake mpumbavu upo mkono wa kushoto”.

Sasa kwanini inasema moyo wa mwenye hekima upo upande wake wa kuume na wa mpumbavu upo upande wake kushoto?..

Je kuna ubaya gani moyo kuwepo upande wa kushoto kiroho?.

Jibu ni la! Lakini Kibiblia mkono wa Kuume unawakilisha “WINGI WA SIKU” na mkono wa kushoto unawakilisha “UTAJIRI NA HESHIMA”.

Mithali 3:16 “Ana wingi WA SIKU KATIKA MKONO WAKE WA KUUME, Utajiri na heshima katika mkono wake wa kushoto”.

Wingi wa siku unaozungumziwa hapo ni “Uzima wa milele”….kwahiyo mtu mwenye hekima moyo wake utaegemea zaidi kufikiri habari za “Wingi wa siku” yaani uzima wa milele siku zote.

Yaani akose kila kitu lakini si uzima Uzima wa milele/Wingi wa siku..

Lakini kinyume chake mtu mpumbavu moyo wake utakuwa unaegemea zaidi habari za “Utajiri na heshima”..na wala hawazi sana juu ya “Wingi wa siku/Uzima wa milele).

Hawazi baada ya miaka yake kuisha hapa duniani atakuwa wapi huko anakokwenda…

Je moyo wako upo upande gani? Wa “Uzima wa milele” au mali na fahari za dunia?…Upo upande wa kuume au wa kushoto?.

Sasa si vibaya kuwa tajiri na kupata heshima duniani, ni vizuri lakini iwe ni sehemu ya kushoto ya maisha yetu, na si upande wetu wa kuume.

Kwasababu Bwana YESU alisema..

Marko 8:36 “Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?

37 Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake?”

Kuna faida gani kupata utajiri wote na hauna uzima wa milele?..

Geuka leo hii na ufanye moyo wako ukae kuumeni mwako?..Fikiri zaidi kuhusu uzima wa milele, (wingi wa siku).

Kumbuka YESU anarudi, na uzima huu wa milele upo tu kwake na si kwa mwingine..

1 Yohana 5:11” Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe.

12 Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima”.

Zaburi 110:5 “Bwana yu mkono wako wa kuume; Ataseta wafalme, Siku ya ghadhabu yake”.

Bwana atusaidie.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MTOLEE BWANA KWA UFUNUO KAMA HANA

Jina la Bwana YESU libarikiwe, karibu tujifunze Biblia, Neno la MUNGU wetu lililo Taa na Mwanga wa njia zetu (Zab. 119:105).

Katika Biblia tunajifunza jambo kubwa sana kwa mwanamke “Hana” ambaye alikuwa tasa lakini baadae Bwana alimfungua tumbo lake na kuzaa watoto.

Katika usomaji wa kitabu cha 1Samweli mlango wa kwanza na wa pili, ni rahisi kufikiri kuwa Hana alimwekea MUNGU nadhiri ya kumtoa mtoto wake wa kwanza atumike kwenye nyumba ya MUNGU daima, bila kuwa na ufunuo au sababu yoyote (ni rahisi kufikiri hilo).

Lakini tukijifunza kwa undani, tunaona wazi kuwa sababu kuu ya Hana kumtoa mtoto wake wa kwanza (Samweli) atumike kwenye nyumba ya MUNGU daima, ni matatizo aliyoyaona  ndani ya nyumba ya MUNGU, kwa wakati ule.

Kwani walikuwepo wana wawili wa kuhani Eli, walioitwa Hofni na Finehasi, vijana hawa hawakuwa waaminifu katika nyumba ya MUNGU,

Kwani walikuwa wanatumia vibaya dhabihu na sadaka zilizokuwa zinaletwa nyumbani mwa Bwana, na zaidi sana walikuwa wakizini na wanawake waliokuwa wakihudumu ndani ya nyumba ya MUNGU, na sifa zao hizo mbaya zilijulikana na watu wote, na hata mwanamke “Hana” aliwajua kwa sifa hiyo.

1 Samweli 2:22 “Basi Eli alikuwa mzee sana; naye alisikia habari za mambo yote ambayo wanawe waliwatenda Waisraeli; na jinsi walivyolala na wanawake waliokuwa wakitumika mlangoni pa hema ya kukutania.

23 Akawaambia, Mbona mnatenda mambo kama hayo? Maana nasikia habari za matendo yenu mabaya kwa watu hawa wote.

24 Sivyo hivyo, wanangu, kwa maana habari hii ninayoisikia si habari njema; mnawakosesha watu wa BWANA.

25 Mtu mmoja akimkosa mwenzake, Mungu atamhukumu; lakini mtu akimkosa BWANA, ni nani atakayemtetea? Lakini hawakuisikia sauti ya baba yao, kwa sababu BWANA amekusudia kuwaua”.

Kwasababu hiyo basi Hana, aliona shukrani pekee ambayo anaweza kumpa MUNGU endapo Mungu atamfungua tumbo lake si kutoa pesa, kwasababu hata akizipeleka madhabahuni  nyumbani mwa MUNGU zitatumiwa vibaya na wale vijana wawili wa Eli (Hofni na Fineasi), wala si dhabihu kwasababu pia zinatumika vibaya.

Ndipo alipotafakari na kuona nadhiri bora na sadaka maalumu itakuwa ya kumtoa mwanae wa kwanza kwa Bwana akawe Mtumishi wa madhabahuni,

Hiyo aliona inaweza kuwa sadaka njema kwake kwa BWANA, Kwani mtoto yule atakuwa katika misingi sahihi ya kiMungu, na atasimama katika kazi ya nyumba ya Bwana kwa uaminifu na kuwa baraka kwa Israeli yote.

Ndivyo Hana alivyofanya, na kupitia sadaka yake hiyo ya kiufunuo, Mungu alisikia maombi yake na kumpa mtoto Samweli, ambaye ndiye aliyekuja kuwaa nabii mkuu Israeli kwa wakati ule.

Ni hivyo hivyo kwa MUNGU wetu, aliona baraka kubwa atakayoibarikia dunia si kuleta mvua nyingi yenye kustawisha nafaka ili matatizo ya njaa yaishe duniani, wala si kumfanya kila mtu kuwa milionea, bali ni kwa kumtoa mwanae pekee YESU KRISTO, Kama dhabihu iliyo hai na sadaka kuu, na kupitia sadaka hiyo leo hii tunabarikiwa kwa baraka zote.

Na sisi tunajifunza mambo hayo hayo, kutazama katika roho ni nini cha kumtolea BWANA, si kila wakati fedha au mali zitakuwa ni sadaka sahihi kwa MUNGU au kwa Nyumba yake au kazi ya MUNGU, wakati mwingine wewe mwenyewe unaweza kuwa sadaka bora kwa kujitoa mwili wako na muda wako kutumika.

Warumi 12:1 “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.

Au si wewe bali mwanao anaweza kuwa bora zaidi na akawa sadaka yenye kumpendeza Bwana. (Kwa wewe kumuandaa kuwa mtumishi, kwa kumfundisha, kumwombea na kumtolea sadaka kwa MUNGU).

Kuna wakati ardhi inaweza kuwa sadaka nzuri kwa Bwana zaidi ya fedha, kuna wakati, kununua kitu na kukipeleka nyumbani mwa Bwana inaweza kuwa bora zaidi kuliko kutoa tu fedha, na kuna wakati fedha ni muhimu zaidi kuliko kitu utakachopeleka, hivyo ni muhimu kuwa na jicho la kiroho na kujua ni kipi kinafaa kutoa kwa wakati huo.

Na kumbuka siku zote, ni heri kutoa kuliko kupokea (Matendo 2:35).

Bwana YESU atusaidie katika  kumtolea yeye matoleo yenye kumpendeza.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MUNGU AUMBAYE TENA.

Biblia inatuonyesha Mungu ndiye muumba wa vitu vyote 

Mwanzo 1:1 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.

Lakini hatujui ni nini kilitokea baadaye kikaifanya dunia kuwa ukiwa, mpaka akaanza kuirekebisha tena dunia aliyoiumba mwanzo.. 

Kwasababu mstari wa 2..unasema nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji, 

Mungu akaanza tena kuifanya ikaliwe na watu, akaleta tena nuru kutoka kwenye giza, akayatenga maji, na kuyaweka sehemu stahiki,  akalitokeza anga..akamuumba mwanadamu.

Dunia ikawa nzuri tena, lakini baadaye mwanadamu akaasi, akaiharibu duniani, mpaka ikaangamia kwa maji. 

Bado Mungu hakuikatia tamaa dunia yake, akawaongeza, Nuhu na wazao wake, baadaye akamchagua Ibrahimu ili kumwandaa mkombozi atakayeikomboa dunia kikamilifu, akaja Kristo ulimwenguni ndio mwokozi wetu.

Watu wakaokolewa, ijapokuwa waliendelea kuiharibu dunia, bado Mungu akawa kwenye mwendelezo wa uumbaji wake unaoharibiwa .

Na kama tunavyojua Kristo aliahidi kurudi tena duniani mara ya pili, kuwanyakua watu wake, kisha kuukarabati huu ulimwenguni na kuufanya kuwa mbingu mpya na nchi mpya.(Ufunuo 21)

Hivyo kama ukichunguza asili ya tabia ya Mungu, si kufanya kitu mara moja, kisha pale kinapoharibika anakikatia tamaa ..

Hapana utaona hukiumba tena na tena na tena…kwa miaka na miaka na miaka..tena huanzia mbali sana mpango wake wa ukarabati..

Na sisi ni lazima tujue tumeumbwa kwa mfano wake na sura yake..ikiwa unaona hakuna mwenye hekima duniani  kumzidi Mungu, na kila lifanyalo ni bora, na kamilifu basi jifunze kuiga tabia zake ufanikiwe…

Mungu wetu alikuwa na siku moja katika juma ya kupumzika, wewe si ‘busy’ zaidi ya Mungu mpaka siku zote saba katika juma, mwaka mzima unafanya kazi mpaka unakosa muda wa kumwabudu Mungu wako.

Vivyo hivyo ni lazima kutambua kuwa kazi zake zimepitia changamoto nyingi sana za kuharibiwa zaidi ya zako lakini amekuwa katika uumbaji wake kila siku..Na wewe pia kuharibiwa kwa maono yako, si sababu ya kukata tamaa na kusema sitaendelea mbele…inuka anza tena na tena..

Unamtumikia Mungu, ile huduma iliyokaa ndani yako, ni kama imekufa, mwanzoni uliona hatua lakini sasa huoni, pengine ni kutokana na kuwa umedhulumiwa, umeibiwa, umefukuzwa..inuka tena na tena, anza upya..

Kuacha kazi uliyokwisha itaabikia na kuitolea jasho jingi, ni ishara ya kuwa bado tabia ya Mungu haijaumbika ndani yako.

Kumbuka mpaka leo hii Mungu anaendelea kufanya uumbaji wake, ijapokuwa kazi hizo zingepeswa zikamilike tangu kule mwanzo…Wewe ni nani usifanye matengenezo yako yaliyokufa kila siku?

Anza sasa. Fanya kazi na Mungu.

Shalom.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MBONA MMESIMAMA HAPA MCHANA KUTWA BILA KAZI?

USIMPE MWANAO VITU SASA.

UPANGA USHIKAMANAO NA MKONO

2 Samweli 23:9-10

[9]Na baada yake kulikuwa na Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu waliokuwa pamoja na Daudi; walipowatukana Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko ili kupigana, na watu wa Israeli walikuwa wamekwenda zao; 

[10]huyo aliinuka, akawapiga Wafilisti hata mkono wake ukachoka, na mkono wake ukaambatana na upanga; naye BWANA akafanya wokovu mkuu siku ile; nao watu wakarudi nyuma yake ili kuteka nyara tu. 

Kibaolojia mwili wa mwanadamu unapokamata kitu, kwa muda mrefu sana, kwa nguvu, huwa unatabia ya kukakamaa katika hali hiyo hiyo hata kama mtu huyo hatakuwa na nia ya kuendelea kukishikilia kitu hicho.

Ndicho kilichomkuta huyu shujaa wa Daudi, alipokutana na jeshi la wafilisti angali yupo peke yake. Aligundua kitu pekee ambacho kingeweza kumtetea ni upanga wake. Hivyo aliukamata kwa nguvu sana bila kuuachia, akaanza kupambana na wafilisti wale kwa muda mrefu,  hakujua kuwa mkono wake utabakia katika hali ile ile…yeye aliendelea tu kupigana vita, mpaka  baadaye aliposhangaa  kuona hana jitihada yoyote tena ya kuushika upanga, ni kama vile ulikuwa ni sehemu ya kiungo chake…kazi yake ilikuwa ni kurusha tu mkono kuupeleka anapotaka, huku upanga ukiwa tu pale pale kiganjani hautoki…

Kikawaida hali ikishafikia hatua hiyo huwa inamgharimu mtu masaa mengi hata siku,  ili kung’atuka kutoka kwenye kitu kilichoshikamana naye..wakati mwingine ili kuharakisha uponyaji, wengine hutumia maji ya uvuguvugu na kuchua kiganja kwa muda baadaye kunyosha kidole kimoja baada ya kingine…

Sasa askari wa mwilini ni kivuli cha mtu wa rohoni. Yeye naye ana mikono na analazimika wakati wote kuwa na upanga…Lakini si upanga tu, wa kushika, bali ule Ugandao na mkono. 

Waefeso 6:11-14,17

[11]Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. 

[12]Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. 

[13]Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. 

[14]Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,..

[17]Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu; 

Kama maandiko yanavyotuonyesha hapo Mtu wa rohoni, hulazimika kubeba upanga wake, ambao ni Neno la Mungu.

Tunapoonyesha nia ya kuling’ang’ania Neno la Mungu, mwanzoni ni kama tutatumia jitihada zetu, lakini haitakuwa hivyo mbeleni …baadaye litashikamana na sisi..maana yake haitakuwa jitihada tena kuliishi.

Jambo lolote la kiroho, mfano maombi ya masafa marefu, mwanzoni ukianza utaona kama ni jitihada zinatumika lakini ukiendelea mara mbili, mara tatu utaona ni kawaida..

Mambo yote ya rohoni iwe ni upendo, unyenyekevu, utaanza kwa jitihada fulani lakini Kwasababu umekusudia tu kung’ang’nia kwa nguvu, utagandamana navyo.

Kumbuka hakuna wepesi wowote utakuja bila mtu kutia nia kwanza. Anza sasa kutendea kazi Neno la Mungu.

Bwana akubariki.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:


 

ZIDI KUTAFUTA UJAZO WA ROHO MTAKATIFU.

Luka 11:13 “Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni HATAZIDI SANA KUWAPA ROHO MTAKATIFU HAO WAMWOMBAO?”.

Kufuatana na maandiko haya, ni wazi kuwa Biblia inatufundisha  ujazo wa Roho Mtakatifu ni jambo endelevu siku zote za maisha ya mtu.

Ikiwa na maana kuwa ni lazima kila siku tujazwe Roho Mtakatifu kila siku kwa kipimo kipya, kwani maandiko yasema yeye hamtoi Roho kwa kipimo (Yohana 3:34) na tena yanasema Tujazwe Roho..

Waefeso 5:18 “Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; BALI MJAZWE ROHO”.

Sasa tunajazwaje Roho Mtakatifu?.

 Si kwa njia nyingine bali kwa kuomba.

Vifuatavyo ni vipengele muhimu katika maombi ya ujazo wa Roho Mtakatifu.

1.      OMBA KUFUNDISHWA NA ROHO MTAKATIFU.

Yohana 14:26 “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, ATAWAFUNDISHA YOTE…”

Unaposoma BIBLIA, Roho Mtakatifu akawe mwalimu wako katika kulielewa vizuri Neno, tenga muda wa kutosha kumwomba MUNGU akakujaze Roho wake wa ualimu.

Watu waliojaa Roho Mtakatifu kweli kweli, wanajifunza Biblia na kuielewa vizuri kwasababu ndani yao Roho Mtakatifu anawafundisha.

Pia wanakuwa ni watu wenye maisha yaliyostaarabika kwasababu ndani yao wanaye mwalimu anayewafundisha kanuni za maisha.

2.      OMBA KUKUMBUSHWA NA ROHO.

Yohana 14:26 “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na KUWAKUMBUSHA YOTE niliyowaambia”.

Kuna mambo uliyowahi pengine kufunuliwa na MUNGU zamani, kwa njia ya Neno au ndoto, na umesahau, unapojaa Roho Mtakatifu, basi atakukumbusha yote aliyekuambia au kukuonesha.

Na sio tu kukumbusha  maneno ya Mungu au maagizo yake bali hata mambo yako mengine ya kimaisha yaliyo ya muhimu, Roho Mtakatifu atakukumbusha na kukutahadharisha.

Hata katika elimu za Dunia, Wanafunzi waliojaa Roho Mtakatifu, ni ngumu kusahau kabisa waliyojifunza, kwani yupo msaidizi ndani yao anayewakumbusha waliyojifunza.

Hali kadhali watu wenye Roho Mtakatifu kweli kweli huwa hawasahau maelekezo au maneno ya Mungu kwani yupo Msaidizi, Roho Mtakatifu anayewakumbusha kila siku.

Kwahiyo tenga muda wa kutosha kuomba ujazo wa Roho Mtakatifu ndani yako.

3.      KUONGOZWA NA ROHO.

Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, ATAWAONGOZA awatie kwenye kweli yote….”.

Pia Roho Mtakatifu kazi yake nyingine ni kumwongoza Mtu, nini cha kusema, nini cha kufanya, au ni wakati gani wa kusema na wakati gani wa kunyamaza, ni wakati gani wa kutenda na wakati gani wa kutulia.

Zaidi sana Roho Mtakatifu pia anamwongoza mtu nini cha kusikiliza na nini ambacho hakifai kusikiliza au kufanya..

Na katika maombi pia, Roho Mtakatifu anamwongoza mtu nini cha kuomba na jinsi ya kuomba.

Warumi 8:26 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo…..”.

Kwahiyo tenga muda wa kutosha kuomba Ujazo wa Roho Mtakatifu, ili uweze kunufaika na tunda hili la kuongozwa na Roho.

4.      OMBA KUFUNULIWA NA ROHO MAMBO YAJAYO.

Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, NA MAMBO YAJAYO ATAWAPASHA HABARI YAKE”.

  Ni muhimu sana kuyajua mambo yajayo yahusuyo maisha yako, kanisa, familia…kwani uishivyo sasa ni kutokana na kile unachokiona mbele yako, na Roho Mtakatifu pekee ndiye awezaye kufunua mambo yajayo ya mtu au watu kwa usahihi.

Kwa mambo haya manne, tutaimarisha  ile safari yetu ya kuenenda kwa Roho.

Wagalatia 5:16 “Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili”.

Bwana atusaidie.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kauli ya Bwana ya “Heri kutoa kuliko kupokea” tunaisoma wapi?

Swali: Katika Matendo 20:15, tunasoma Mtume Paulo akirejea kauli ya Bwana kwamba akisema “Heri kutoa kuliko kupokea”.. Je ni wapi katika Injili nne, Bwana YESU alisema maneno hayo?

Jibu: Tuanzie kusoma ule mstari wa 33..

Matendo 20:33 “Sikutamani fedha wala dhahabu, wala mavazi ya mtu.

34 Ninyi wenyewe mnajua ya kuwa mikono yangu hii imetumika kwa mahitaji yangu na ya wale waliokuwa pamoja nami.

35 Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, NA KUYAKUMBUKA MANENO YA BWANA YESU, JINSI ALIVYOSEMA MWENYEWE, NI HERI KUTOA KULIKO KUPOKEA”.

Katika vitabu vyote vinne vya injili (yaani kitabu cha Mathayo, Marko, Luka na Yohana) hakuna mahali popote pameandikwa  maneno hayo ya Bwana kama yalivyo kwamba “heri kutoa kuliko kupokea”. Lakini ni wazi kuwa aliyasema mahali fulani ila hayakuandikwa katika vitabu vinne vya injili.

Tunalithibitisha vipi hilo?.. Turejee kitabu cha Yohana 21:24..

Yohana 21:24 “Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa”.

Hapa Mtume Yohana anasema, yapo mambo mengi aliyoyafanya Bwana YESU ambayo hayakuandikwa katika vitabu hivyo..maana yake yapo maneno mengi aliyoyafundisha na mifano mingi na ishara nyingi alizozifanya ambazo laiti kama zingeandikwa moja baada ya nyingine, dunia isingetoshea kwa vitabu..

Kwa mantiki hiyo basi tunaanza kuelewa kuwa maneno hayo ya “heri kutoa kuliko kupokea” ni kweli Bwana YESU aliwahi kuyasema mahali fulani, isipokuwa tu hayakunukuliwa na waandishi wa vitabu vinne vya injili.

Lakini pamoja na hayo, yapo maneno aliyoyasema yenye mlengo huo huo wa “uheri wa kutoa kuliko kupokea”

Luka 6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”.

Hii ni kauli ya Bwana YESU akitufundisha faida za kuwapa watu vitu, kwani tunapotoa ndivyo tutakavyopokea, na si tupokee kwanza na ndipo tutoe.. hiyo ikithibitisha kuwa ni kweli Bwana alifundisha uheri wa kutoa kuliko kupokea, na pia alituonya tujilinde na “uchoyo”.

Luka 12:15  “Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo”.

Je umempokea YESU?.. Je una uhakika akirudi leo utakwenda naye?

Kama bado tengeneza maisha yako kwani majira tunayoishi ni ya hatari na parapanda ya mwisho imekaribia sana kulia.

Bwana atusaidie.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine: