Category Archive maswali na majibu

Kigutu ni nani? (Marko 9:43)

Swali: “Kigutu” ni mtu wa namna gani kama tunavyosoma katika Marko 9:43?


Jibu: Turejee,

Marko 9:43  “Na mkono wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima U KIGUTU, kuliko kuwa na mikono miwili, na kwenda zako jehanum, kwenye moto usiozimika;

44  ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]”

“Kigutu” ni mtu aliyekatwa mkono au aliyekatika mkono, tazama picha juu.

Biblia inatufundisha kuwa kiungo chetu kimoja kikitukosesha tukiondoa ili kisitupeleke katika jehanamu ya moto.

Sasa ni kweli kiungo kinaweza kuwa tabia, au marafiki, au vitu vya kimwili ambavyo vimejiungamanisha na mtu kiasi kwamba vinamkosesha katika Imani. Lakini pia biblia iliposema kiungo, imemaanisha pia kiungo kama kiungo, ikiwa na maana kwamba kama ni mkono ndio unakukosesha basi uondoe!, kama mkono wako umezoea kuiba, baada ya kutubu!, basi uondoe! Na hautaiba tena.

Kama ni jicho pia liondoe, na viungo vingine vyote… Na sababu ya Bwana kusema hivyo ni ili mtu aokoke na ziwa la moto, ambao kule kuna funza wasiokufa!, na moto wa kule hauzimiki, na wote wanaoshuka huko moshi wa maumivu yao unapanda juu milele na milele.

Ufunuo 14:10 “yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; NAYE ATATESWA KWA MOTO NA KIBERITI MBELE YA MALAIKA WATAKATIFU, NA MBELE ZA MWANA-KONDOO

11 Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku, hao wamsujuduo huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina lake”.

Kwa upana juu ya viungo vinavyokosesha fungua hapa >>YESU alimaanisha nini aliposema “mkono wako ukikukosesha ukate?

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Nini tofauti kati ya moyo na roho?

Bwana alimaanisha nini kusema “kila mtu atatiwa chumvi kwa moto”

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

Kulingana na 1Wakorintho 3:10-15, kama inavyosema..ni kwa namna gani kazi ya mtu itateketea, na kupimwa kwa moto?”

IFAHAMU FAIDA YA KUMKIRI KRISTO UKIWA HAPA DUNIANI.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini tarehe ya pasaka inabadilika kila mwaka?

(Maswali yahusuyo pasaka)

Swali: Je kwanini tarehe ya pasaka inabadilika kila mwaka, kwamfano mwaka 2023 pasaka ilikuwa ni Aprili 13, lakini mwaka huu 2024 ni Marchi 31, na inategemewa kubadilika tena katika mwaka ujao na miaka yote inayokuja, kwanini iwe hivyo, wakati Krismasi ni tarehe ile ile 25 miaka yote?


Jibu: Awali ya yote ni muhimu kujua kuwa pasaka ni moja ya sikukuu 7 za wayahudi, na inasheherekewa na wayahudi katika kila terehe 14 ya mwezi wao wa Kwanza, ambapo mwezi wao wa kwanza unaangukia katikati ya mwezi Machi na Aprili kwa kalenda tunayoitumia sisi.

Lakini kuhusiana na kwanini tarehe za pasaka zinabadilika kila mwaka kwa upande wa wakristo, ni kutokana na MWONEKANO WA MWEZI.

Mwezi unapozuka mzima (yaani angavu/full moon) basi jumapili inayofuata ndiyo inayosherekewa na wakristo wengi kama jumapili ya pasaka.

Kuna miaka ambapo “mwezi mwangavu” unawahi kuchomoza na kuna miaka unachelewa. Ikiwa na maana kuwa kama mwezi mwangavu  utaonekana jumatano basi jumapili inayofuata itakuwa jumapili ya pasaka, ambayo itakuwa ni baada ya siku nne,  Kwamfano kwa mwaka 2023 mwezi mwangavu ulionekana jumatano ya Tarehe 5 Aprili, hivyo jumapili iliyofuata ya tarehe 9 ndio ikawa jumapili ya pasaka.

Lakini kwa mwaka 2024, Mwezi mwangavu umewahi kuonekana, kwani umeonekana Jumatatu ya tarehe 25 Machi, hivyo jumapili inayofuata ya tarehe 31 Machi, ndio itakayokuwa jumapili ya pasaka.

Lakini pia kwa mwaka 2025, Mwezi mwangavu unatarajiwa kuonekana jumapili ya tarehe 13 Aprili, hivyo jumapili itakayofuata ya tarehe 20 Aprili ndio itakayokuwa jumapili ya pasaka.

Kwahiyo hiyo ndio sababu kwanini tarehe hizo zinabadilika badilika kila mwaka, (ni kutokana na mwonekano wa mwezi).

Sasa kujua pasaka ni nini na kama wakristo ni halali kuiadhimisha fungua hapa >>PASAKA NI NINI? NA JE TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA?

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Je! kuna sikukuu za pasaka mbili? (Hesabu 9:11)

KWARESMA IPO KIMAANDIKO?

Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana?

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

KRISIMASI (CHRISTMAS) NI NINI? JE IPO KATIKA BIBLIA?

Rudi nyumbani

Print this post

Yesu kuvishwa taji la miiba kichwani, kulifunua nini?

SWALI: Yesu kuvishwa taji la miiba kichwani alipokuwa anasulubiwa kulikuwa kuna funua nini rohoni?


JIBU: Kila tendo alilotendewa Yesu katika kipindi cha mateso yake lilikuwa lina ufunuo wake rohoni. Tunajua wale askari waliposikia kuwa yeye ni mfalme, muda ule ule walimvisha vazi la kifalme, kisha wakampa fimbo, na baada ya hapo wakasokota taji la miiba, wakamvisha kichwani, kisha wakaanza kumdhihaki, huku wakimpiga wakisema..  Salamu! Mfalme wa Wayahudi!

Yohana 19:2  “Nao askari wakasokota taji ya miiba, wakamtia kichwani, wakamvika vazi la zambarau. 3  Wakawa wakimwendea, wakisema, Salamu! Mfalme wa Wayahudi! Wakampiga makofi”

Tunajua lengo la wale maaskari kumvisha miiba ni kumfanya aumie zaidi, lakini upo ufunuo mkubwa rohoni, pengine kwanini asingevishwa la matambara mabovu, au taji la udongo, au la vyuma vyenye ncha kali, badala yake wakaona miiba.

Kibiblia, miiba, huwakilisha “mahali palipolaaniwa”.

Adamu alipoasi, Mungu alimwambia ardhi imelaaniwa kwa ajili yako, hivyo itatoa miiba na michongoma. Na matokeo yake ni kwamba italimwa kwa shida

Mwanzo 3:17 Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako;  18 michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni;

Ndio maana shamba ambalo  halipaliliwi  au halitunzwi, matokeo yake ni kuwa linatoa miiba.

Mithali 24:30 Nalipita karibu na shamba la mvivu, Na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili.  31 Kumbe! Lote pia limemea miiba; Uso wake ulifunikwa kwa viwawi; Na ukuta wake wa mawe umebomoka.  32 Ndipo nilipoangalia na kufikiri sana; Naliona, nikapata mafundisho.  33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, Bado kukunja mikono upate usingizi! 34 Hivyo, umaskini wako huja kama mnyang’anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha

Na vivyo hivyo rohoni, mioyo yetu inafananishwa na mashamba. 

Ukisoma ule mfano wa mpanzi, utaona mbegu(Neno la Mungu), lilipopandwa, zipo ambazo ziliangukia kwenye miiba (yaani mahali ambapo hapajafyekwa na kupapaliwa), ndipo pale kwenye miiba, na mwishowe zikakua na kumea. Lakini zikasongwa na ile miiba hazikashindwa kuzaa.

Yesu akatoa tafsiri yake, akasema, miiba ile ni “anasa, udanganyifu wa mali, na shughuli za ulimwengu huu”.

Luka 8:14  “Na zilizoanguka penye miiba ni wale waliosikia, na katika kuenenda kwao husongwa na shughuli na mali, na anasa za maisha haya, wasiivishe lo lote”.

Sasa Yesu alipokuja kufa msalaba, alishughulika na jambo hilo kubwa, kubeba laana hiyo kubwa kwenye kichwa chake.

Akimaanisha kuwa ile nchi iliyolaaniwa (yaani mioyo wa mtu), kuanzia sasa ni mwisho. Imekwisha.

Miiba iliyokuwa inatoka mimi nimeichukua kichwani mwangu.

Moyo wa mtu kuanzia sasa, utaanza kuzaa matunda, na wala hautasongwa na anasa, wala udanganyifu wa mali, wala shughuli za ulimwengu huu, usiivishe chochote.

Hii ikiwa ni kweli kabisa.

Sisi tunaomwamini Yesu, moja kwa moja tunapewa UWEZO wa kufanyika watoto wa Mungu (Yohana 1:12), na matokeo ya uwezo huo ni kuwa,  nguvu ya kusongwa na ulimwengu inakuwa ndogo, kwasababu Roho Mtakatifu aliyemwagwa ndani yetu anatusaidia, Kuukataa ulimwengu, na kuishi maisha ya utauwa. Utakuwa ulimwenguni lakini, hutasongwa na mambo yake. Kwasababu utafundishwa pia “kiasi” na Roho Mtakatifu.

Hivyo uwezo huu utakuja ndani yako, pindi tu unapomgeukia Kristo kwa kumaanisha kabisa, ambapo panaanza na kwa KUTUBU kwanza dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kugeuka,na kumfuata Kristo tangu huo wakati, na kisha kubatizwa, na kupokea Roho wake. Lakini nje ya hapo, huwezi kwenda popote.

Je! Umempokea Yesu?

Pasipo yeye huwezi ndugu kuushinda ulimwengu kwa nguvu zako, haiwezekani hata kidogo, hata ufanyeje haiwezekani,miiba itakusonga tu, dunia itakulemea tu, Unahitaji nguvu zake, kwa Roho wake Mtakatifu. Ili kuzipata maanisha tu kumgeukia,  na kusudia kutembea naye moyoni mwako.

Utaushinda huu ulimwengu. Wala hakuna mwiba wowote utakaomea kwenye moyo wako. Kwasababu Kristo alishayakomesha yote. Je! upo tayari kuokoka leo? Basi fungua hapa kwa mwongozo wa kimaombi>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

SHAMBA HUWA HALIMTAMBUI WALA KUMSUBIRIA MKULIMA.

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

Je vazi alilovikwa Bwana Yesu lilikuwa la Zambarau au Jekundu?

Mbaruti ni mmea gani? (Mathayo 7:16)

Rudi nyumbani

Print this post

Ipi tofuati ya “Kutakabari” na “kutakabali”?

Swali: Kuna tofauti gani ya “kutakabari” na “kutakabali”, sawasawa Warumi 1:30 na Mwanzo 4:4-5?


Jibu: Tuanze na 1) kutakabari..

Warumi 1:30  “wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao”.

“Kutakabari” maana yake ni “kuwa na kiburi” kinachokuja kutokana na kuwa na kitu Fulani, au kujiamini sana..

Matokeo ya kutakabari ni kuanguka..

Mithali 16:18 “Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.

19 Afadhali kuwa na roho ya unyenyekevu pamoja na maskini, Kuliko kugawanya nyara pamoja na wenye kiburi”.

Mfano wa mtu kwenye biblia aliyetakabari na akaanguka ni Mfalme wa Ashuru aliyeitwa Senakeribu.. Huyu alijiinua mbele za Mungu kwa kiburi kikuu na anguko lake likawa kubwa. (Soma 2Wafalme 19:28-37).

Unaweza kujifunza Zaidi juu ya kutakabari kwa kufungua hapa >>Kutakabari ni nini katika biblia?.

Mistari mingine inayozungumzia juu ya kutakabari ni pamoja na 1Samweli 2:3, Nehemia 9:10,  Isaya 13:3, na 1Wakorintho 13:4.

     2. KUTAKABALI.

“KUTAKABALI” ni tofauti na “kutakabari”…. Kutakabali ni “kukubali kitu”.. Utaona sadaka ya Habili Mungu aliitakabali (maana yake aliikubali na kuiheshimu zaidi ya ile ya Kaini).

Mwanzo 4:4 “Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. Bwana AKAMTAKABALI Habili na sadaka yake;

5 bali Kaini HAKUMTAKABALI, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana”

Na sisi tunapomtolea Mungu sawasawa na Neno lake, Sadaka zetu atazitakabali, lakini tukitoa nje na neno lake hatazitakabali kama vile sadaka ya Kaini alivyoikataa..

Yeremia 14:12 “Wafungapo, mimi sitasikia kilio chao; na watoapo sadaka za kuteketezwa na sadaka ya unga, sitazitakabali; bali nitawaangamiza kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni”

Vile vile tukimwomba Mungu sawasawa Neno lake basi Maombi yetu atayatakabali na kutujibu, lakini tusipoomba kulingana na Neno basi hata maombi yetu hayatajibiwa..

Zaburi 6:9 “Bwana ameisikia dua yangu; Bwana atayatakabali maombi yangu”.

Kujua kuomba kulingana na Neno la Mungu fungua hapa >>>>KWANINI MUNGU HAJIBU MAOMBI?

Mistari mingine inayohusu KUTAKABALI ni pamoja na Zaburi 20:3, Mhubiri 5:20, Ezekieli 20:41, Hosea 14:2 na Malaki 2:13.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

Kiburi cha Uzima ni nini? (1Yohana 2:16)

UDHAIFU WA SADAKA!

Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

MUNGU HUWAPINGA WENYE KIBURI.

Rudi nyumbani

Print this post

Anaposema zijapokuwa nyekundu kama bendera, ana maana gani?

SWALI: Mungu anaposema dhambi zetu zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu. Ana maana gani, kwenye hilo neno bendera?

Isaya 1:18 Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.  19 Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi;


JIBU: Hapa ni Mungu anaeleza mambo mawili hayuhuso dhambi walizotenda watu wake.

  • Jambo la kwanza ni ukubwa/wingi wa dhambi walizonazo. Ndio hapo anafananisha rangi nyekundu sana, ukilinganisha na kitu kilicho cheupe sana mfano wa theluji.

Tunajua theluji inang’aa sana mfano wa jua, Kuonyesha ni jinsi gani hawa watu walivyokuwa mbali sana na ukamilifu, yaani jinsi gani walivyokuwa hawakaribii hata kidogo kuwa wema mbele za Mungu, walau wangeonekana wa rangu ya kijani, basi wangekuwa na afadhali, lakini ni mbali sana, wana rangi ya damu. Ndivyo ilivyokuwa Israeli yake.

  • Jambo la pili ni usugu wa dhambi uliokuwa ndani yao.Ndio hapo anafananisha na Bendera, ukilinganisha ni sufu nyeupe.

Zamani bendera nyingi zilichovywa katika rangi nzito nyekundu, inayodumu sana, kwasababu ni kitu cha kudumu muda mrefu, hivyo haikuhitajika rangi inayofubaa haraka. Sio tu bendera, lakini mpaka mavazi ya kifalme, au nguo za thamani za sufu.

Hivyo unaposoma habari za bendera hapo, si bendera ya kila rangi, mfano wa bendera tulizonazo sikuhizi zina rangi mbalimbali, zamani nyingi zilichovya kwa rangi  nyekundu. Hivyo Mungu anawaambia ijapokuwa ni nyekundu kama bendera, basi zitageuzwa na kuwa nyeupe kama Sufu, (akiwa na maana ambayo haijachovywa), Yaani Mungu anaweza kuiondoa hiyo rangi sugu, kwenye hicho kitambaa kana kwamba hakijachovywa kabisa.

Kufunua nini,

Yesu Kristo mwokozi wetu ndiye aliyetimiza huo unabii. Kuonyesha kuwa dhambi zote tulizotenda haijalisha ni nyingi kiasi gani, haijalishi ni mbaya namna gani yeye kwa damu yake anaweza kuzifuta kabisa kabisa. Dhambi tulizotenda haijalishi hazisameheki namna gani, hazineneki, ni sugu namna gani, yeye anao uwezo wa kuziondoa, kwa neema yake.

Swali ni je! Umesamehewa dhambi zako? Kama ni la! Unangoja nini kuipokea neema hii, ya WOKOVU mkuu namna hii? Pokea sasa msamaha wa dhambi kwa kutubu dhambi zako, na kumaanisha kuishi maisha mapya ya wokovu. Kisha moja kwa moja atakupokea na kukupa ondoleo la dhambi zako. Na baada ya hapo unahesabiwa kuwa huna dhambi yoyote, umestahili uzima wa milele, bure.

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo basi, fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa maombi mafupi, na kwa kupitia sala hiyo kwa imani utakuwa umeshampokea Yesu Kristo, na amekusamehe dhambi zako zote.>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?

ALAMA ZA BENDERA YA ISRAELI ZINAWAKILISHA NINI?

MAANA YA RANGI KIBIBLIA.

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Rudi nyumbani

Print this post

Chrislam ni nini?

Ni muungamaniko wa maneno makuu mawili. (Yaani Christian na Islamic). Likachukuliwa Neno la kwanza Chris katika Christian, likaunganishwa na Neno la katikati “slam” kutoka katika Islamic. Kuunda Christlam

Hii ni imani iliyozuka, katika taifa la Nigeria miaka ya 1970.  Kufuatana ni migongano ya kiimani baina ya makundi haya mawili ya dini, ikizingatiwa kuwa Taifa La Nigeria ndio lenye watu wengi barani Africa, na takribani Nusu kwa Nusu, dini hizi mbili ndio zimechukua jamii kubwa ya watu.

Hivyo waasisi ya umoja huu walikuwa na madhumuni ya kuondoa tofauti za kidini, husani zilizo katika mataifa ya magharibu na ya mashariki ya kati, Lakini pia kwasababu hizi ndio dini kubwa duniani, basi pia zikiungana zinaweza kusaidia kuushinda upagani kwa sehemu kubwa.Na ukweli ni kwamba imani hii imepata umaarufu mkubwa duniani, hususani kwa kipindi cha sasa.

Waanzilishi walisukumwa kuunda umoja huu, wakiamini kuwa, sehemu kubwa ya dini ya kikristo inatajwa katika Quran, wakimrejea Yesu mwenyewe pamoja na manabii wa kale, kama Ibrahimu na wengineo. Lakini pia uislamu unamwingiliano mkubwa wa kitamaduni ambao hata katika ukristo upo. Hivyo kwa mujibu wa hoja zao hakuna sababu ya kuwa na utofauti wowote katika mashindano ya kidini.

Lakini je! Umoja huu, mbele za Bwana unakubalika?

Imani ya Kikristo pamoja dini ya kiislamu haviwezi kuchangamana, ni sawa na chuma na udongo. Kwasababu kiini cha imani ya ukristo ni KRISTO mwenyewe, na kwamba mtu hawezi kwenda mbinguni pasipo kumwamini YESU kama mwokozi PEKEE anayewaokoa wanadamu. Jambo ambalo linakinzana na dini ya Kiislam, katika imani ya kufika mbinguni, ambapo kwao Kristo ni kama mmojawapo wa manabii tu wengine. Na hivyo mbingu si kupitia Kristo, bali kupitia matendo mazuri kama vile kukaa mbali na uovu n.k.

Uislamu haumtambua Kristo kama Mungu, huamini kuwa yoyote anayemfanya Yesu Mungu, ni makufuru, kwasababu Mungu hajazaa, wala hana mshirika. Hivyo aaminiye uungu wa Yesu, pepo haimuhusu.

Kwa vigezo hivyo, uislamu na ukristo ni imani mbili tofauti kabisa, ijapokuwa zitaonekana kushea baadhi ya desturi, lakini bado haziwezi kuletwa pamoja kuwa kitu kimoja.

Je! Hatupaswi kuwa waamini wa Chrislam

Ndio wewe kama Mkristo,, imani yako haipaswi kuchanganywa na nyingine yoyote, ukifanya hivyo ni Kosa kiimani. Sisi tunaamini, wokovu ni kwa kupitia Yesu Kristo anaotupa BURE kwa neema katika kumwamini Yeye, kwa kifo chake pale msalabani.

Tunamtegemea Kristo kutuokoa, kutupa nguvu ya kuishi maisha makamilifu, kutuongoza, kwa asili mia. Hivyo hatuna msingi au tegemeo lingine nje yake yeye. Na hata hivyo kibiblia, yoyote asiyekubaliana na Kristo Yesu, kama ndiye mwokozi pekee. Huyo ni mpinga-Kristo.

Hivyo kw hitimisho ni kuwa wewe kama mwana wa Mungu, usijihusishe ni imani yoyote nje ya Kristo Yesu mwokozi wako.

Matendo 4:12  Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Dini ni nini, na Imani ya kweli ni ipi?

Praitorio ni nini? Na Kwanini ilikuwa ni najisi kwa wayahudi kuingia humo? (Yohana 18:28)

Uadilifu ni nini kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Merikebu ya Iskanderia kwanini itajwe jina lake ‘Ndugu Pacha’?

SWALI: Je kulikuwa na umuhimu wowote wa ile merikebu ya Iskanderia  walioipanda Paulo na wafungwa wengine kutajwa jina lake ‘ndugu Pacha’,?

Matendo 28:11  Baada ya miezi mitatu tukasafiri katika merikebu ya Iskanderia iliyokuwa imekaa pale kisiwani wakati wa baridi; na alama yake ni Ndugu Pacha. 12  Tukafika Sirakusa, tukakaa siku tatu. 13  Kutoka huko tukazunguka tukafikia Regio; baada ya siku moja upepo wa kusi ukavuma, na siku ya pili tukawasili Puteoli. 14  Huko tukakuta ndugu, wakatusihi tukae nao siku saba; na hivi tukafika Rumi.


JIBU: Safari ya mtume Paulo kama mfungwa, kutoka Kaisaria kwenda Rumi kuhukumiwa, haikuwa rahisi, iligubikwa na misuko suko mikubwa ambayo ilihatarisha maisha yao ukisoma Matendo 27, utaona mtume Paulo alionywa na Roho Mtakatifu kuhusu hatari hiyo lakini alipomwambia akida na manahodha, walipuuzia agizo lake, kwasababu watu wale hawakuamini habari za “miungu kabisa”. Maandiko yanasema walipoona upepo wa kusi umevuma kidogo tu, unaoruhusu kusafiri, wakadhani itakuwa hivyo mbeleni.

Lakini tunaona walipofika katikati, ghafla ile bahari iliwachafukia sana, upepo wa nguvu ukavuma merikebu yao ikawa karibu na kuzama, baadaye ilivunjika kabisa, na wakaokoka kwa shida kwasababu Mungu alimuhakikishia Mtume Paulo kuwa hakuna hata mmoja wao atakayeangamia.

Walipookoka na kufika kisiwa kile kilichoitwa Melita, walikaa miezi mitatu pale, kuruhusu hali ya hewa kutulia, kabla ya kuondoka. Lakini tunaona walipotaka kuondoka, safari hii wale mabaharia pamoja na maakida, hawakuichukulia safari yao kirahisi rahisi, yaani hivi hivi tu bila uongozo wowote. Ndipo walipojifunza kuchagua merikebu yenye “ulinzi wa kiroho”. Wakaipata hiyo ya Iskanderia iliyokuwa na nembo ya “Ndugu Pacha” kwa mbele.

Ndugu Pacha ni miungu ya kipagani ya kiyunani, ukisoma tafsiri nyingine za biblia imewataja moja kwa moja miungu hiyo kama Castor na Pollux. Ni miungu ambayo waliamini inahusika na ulinzi wa  safari za majini. Hivyo kwa imani yao ya kipagani, wakachukua nembo yao kuonyesha tunaiabudu na kuiheshimu hii miungu, na kutaka iwaongoze  salama katika safari yao, hawategemei tena elimu zao na nadharia zao.

Sasa tukirudi kwenye swali, linalouliza, kulikuwa ni umuhimu gani, hiyo merikebu ya Iskanderia kutajwa hadi nembo yake ya ndugu Pacha. Sababu ndio hiyo, Sio kwamba biblia inatufundisha, na sisi tukaweke miungu ya kipagani, kwenye vyombo vyetu vya usafiri kutuhakikishia ulinzi, hapana!

Bali inatufundisha Safari ya maisha hapa duniani. Kila mwanadamu anasafiri, lakini Je! Katika safari yako ni kitu gani kinakuongoza na kukulinda ili kukufikia ng’ambo yako salama?

Hakuna mwanadamu ambaye anaweza kujiongoza mwenyewe. Na ndio maana utaona hawa kwasababu hawakumjua Mungu wa kweli iliwabidi wakatafuta vinyago visivyoweza kuwasaidia kitu viwaongoze, na kama sio mtume Paulo kuwepo ndani ya Merikebu ile, safari yao ndio ingekuwa mbaya mara mbili zaidi. Hawakujua tu waliongozwa na Kristo Yesu pasipo wao kujua kwa neema tu!. Kwasababu watumishi wa Mungu walikuwa ndani.

Na sisi, hapa tulipo, fahamu kuwa maisha yako, bila KRISTO ni mauti mbele. Shetani hakuwazii mema, wala akili zako mwenyewe hazikusaidii ndugu, hiyo elimu ni kazi bure, huo uzoefu na ujuzi ulionao ni bure rafiki. Unamuhitaji Kristo, yeye ndio awe nembo  ya maisha yako. Mwamini leo akupe msamaha wa dhambi, mwamini leo akuokoe, safari yako iwe salama hapa duniani. Ukifa leo katika hali hiyo, fahamu ni jehanamu moja kwa moja. Umesikia injili ikihubiriwa mara ngapi, kwamba Yesu ni mwokozi lakini unapuuzia? Walio kuzimu wanatamani hata dakika moja, watubu hawawezi kwasababu kule hakuna maisha ya kuishi. Lakini wewe unaishi.

Usikiapo maneno haya, ugeuze moyo wako, umruhusu Kristo leo akuokoe, ikiwa upo tayari kumgeukia Bwana Yesu , na unatamani upate mwongozo wa kimaombi kwa ajili ya wokovu wako. Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii, bure.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NA UPEPO WA KUSI ULIPOANZA KUVUMA KIDOGO,

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

Kalafati ni nini? (Ezekieli 27:9)

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Mvinyo hudhihaki na kileo huleta ugomvi? (Mithali 20:1)

Jibu: Turejee.

Mithali 20:1 “Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi; Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima”.

Hili ni andiko linaloelezea mambo makuu mawili yanayowakosesha watu waliopungukiwa na Hekima.. na Mambo hayo ni “Mvinyo” pamoja na “Kileo”. Na vitu vyote hivi viwili vina madhara kwa mtu anayevitumia..

Sasa ni ipi tofauti kati ya Mvinyo na Kileo? Na madhara yake ni yapi kwa mtumiaji?.

“Mvinyo” (kwa lugha ya kiingereza ni “wine”) ni kilevi kinachotengenezwa kwa “Matunda yaliyosagwa” kama Zabibu, mananasi, maembe n.k Mfano wa mvinyo unaotengenezwa kwa zabibu ni “Divai”.

Wakati “Kileo” (Kwa lugha ya kiingereza Beer/Bia) ni kilevi kinachotengenezwa kwa nafaka kama Ngano, mahindi, ulezi, mtama, mchele n.k

Kikawaida Mvinyo ndio wenye kilevi kingi kuliko Kileo. Na matokeo ya mtu anayetumia mvinyo au kileo yanakaribiana. Hebu tuangalia madhara ya kimoja baada ya kingine kibiblia.

   1. MVINYO

Biblia anasema “Mvinyo hudhihaki”.. maana yake ni kuwa mtu anayetumia mvivyo anakuwa ni mtu wa kudhihaki na kudhihakiwa!.. kwasababu ya wingi wa maneno yao yasiyo na maana yatokayo midomoni mwao.

Ndio maana utaona kile kipindi cha Pentekoste, walipowasikia wanafunzi wa Bwana YESU wakinena kwa lugha, walidhani wamelewa kwa mvinyo mpya na hivyo wakaanza kuwadhihaki..

Matendo 2:12 “Wakashangaa wote wakaingiwa na shaka, wakiambiana, Maana yake nini mambo haya? 13  WENGINE WALIDHIHAKI, WAKISEMA, WAMELEWA KWA MVINYO MPYA.

14  Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.

15  Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;

16  lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli”.

Umeona hapo?.. walianza kuwadhihaki wakidhani wamelewa kwa MVINYO MPYA, ikimaanisha kuwa Mvinyo huleta dhihaka kwa anayekunywa. Na mtu anayelewa kwa mvinyo atapokea dhihaka nyingi katika maisha yake..

    2. KILEO

Biblia inaendelea kusema kileo huleta “UGOMVI”. Asilimia kubwa ya watu wanaogombana mpaka kufikia hatua ya kudhuriana ni walevi wa pombe, mafarakano mengi yanatoka kwa watu waliolewa..

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba, Ulevi wa aina yoyote ile uwe wa “Mvinyo” au wa “Kileo” matokeo yake ni mabaya katika maisha ya ulimwengu huu na ule ujao…. Kulingana na biblia walevi wote hawataurithi uzima wa milele (soma 1Wakorintho 6:9-10 na Wagalatia 5:19-20)..

Warumi 13:13 “Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ULAFI NA ULEVI, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu.

14  Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, wala msiuangalie mwili, hata kuwasha tamaa zake”.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

UPEPO WA KUSI HULETA MVUA;

“Si watu wa kutumia mvinyo sana”, je tunaruhusiwa kutumia mvingo kidogo?(1Timotheo 3:8).

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?

JE! ULEVI NI DHAMBI?.

Rudi nyumbani

Print this post

Je shauri la kuipepeleza Kanaani lilitoka kwa wana wa Israeli au kwa BWANA?

Swali: Je lile shauri la kupeleka wapelelezi Kanaani lilitoka kwa nani?..Maana sehemu moja katika biblia inasema lilitoka kwa Bwana (Hesabu 13:1-3) na sehemu nyingine inasema lilitoka kwa wana wa Israeli (Kumbukumbu 1:22-23). Je! lipi ni sahihi, na je biblia inajichanganya?.


Jibu: Turejee mistari hiyo, mmoja baada ya mwingine.

Hesabu 13:1 “Kisha Bwana akanena na Musa, akamwambia,

2 Tuma watu, ili waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani, niwapayo wana wa Israeli; katika kabila ya baba zao mtamtuma mtu mmoja, kila mtu na awe mkuu kati yao.

3 Basi Musa akawatuma kutoka nyika ya Parani kama alivyoagizwa na Bwana; wote walikuwa ni watu walio vichwa vya wana wa Israeli”.

Hapa tunaona ni MUNGU ndiye anamwamuru Musa apeleke wapelelezi.

Kumbukumbu 1:22 “Nanyi mkanikaribia kila mmoja wenu, mkasema, Na tupeleke watu mbele yetu, ili watupelelezee nchi na kutuletea habari za njia itupasayo kuipandia, na za miji tutakayoifikia.

23 Neno hili likanipendeza sana; nikatwaa watu kumi na wawili, mtu mmoja wa kila kabila”

Na hapa tunasoma kuwa ni “Wana wa Israeli” ndio waliopendekeza kupeleka wapelelezi Kanaani. Sasa swali ni je!..biblia inajichanganga?.

Jibu ni La!.. Biblia haijichanganyi mahali popote, isipokuwa fahamu/pambanuzi zetu ndizo zinachojichanganya au kuchanganyikiwa.

Sasa ni kwanini hapo sehemu moja iseme ni Mungu na sehemu nyingine iseme wana wa Israeli? Ukweli ni upi?

Ukweli ni kwamba wazo la kupeleka wapelelezi wakaiepeleze Kanaani ni Wana wa Israeli ndio waliolitoa, kamwe Mungu asingeweza kuwaambia wana wa Israeli wapeleke wapelelezi kwasababu yeye ana nguvu nyingi na wala hahitaji utafiti wa wanadamu katika kuokoa au kuharibu!…Kama ndivyo angefanya kwanza kwa Farao, lakini tunasoma Farao alikuwa kama mnyoo tu mbele za Bwana, na Taifa la Misri kwa wakati huo lilikuwa na nguvu Zaidi hata ya Kanaani.

Hivyo kilichowasukuma wana wa Israeli kupeleka wapelelezi ni hali ya ugumu wa mioyo yao, ambayo baada ya kutoka Misri walianza kuusahau uweza wa Mungu na kumdharau Mungu, kiasi kwamba hawakuamini kwamba angeweza kuwashindania kama alivyowashindania walipotoka Misri, lakini kinyume chake wakaukataa uweza wa Mungu, mioyo yao ikawa migumu, wakajitwika silaha, na wakapanga mipango yao.

Hesabu 14:11 “Bwana akamwuliza Musa, Je! Watu hawa watanidharau hata lini? Wasiniamini hata lini? Nijapokuwa nimefanya ishara hizo zote kati yao”.

Sasa kwakuwa wana wa Israeli tayari walikuwa wameshamdharau Mungu na uweza wake, hivyo Mungu aliruhusu baadhi ya Mambo wayafanye, katika kiwango cha uweza walichompimia. Na mojawapo ya jambo ambalo aliliruhusu ni hilo la kwenda kupeleleza.

Hivyo Musa aliposikia mpango wa wana wa Israeli kwenda kuipeleleza, alienda kuuliza kwa Bwana, na Bwana akawapa ruhusa sawasawa na hiyo Hesabu 13:1-6. Na sio jambo hilo tu ambalo Mungu alitoa ruhusa bali yapo na mengine mengi ambayo wana wa Israeli walijiamulia na Mungu akaruhusu yaendelee katikati yao, lakini hayakuwa mapenzi makamilifu ya Mungu, baadhi ya mambo hayo ni yale ya wana wa Israeli kujitakia mfalme katika (1Samweli 8:5) na yale ya talaka ambayo Bwana YESU aliyasema katika Mathayo 19:3-8.

Mathayo 19:3 “Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa kila sababu?

4  Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,

5  akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?

6  Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.

7  Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?

8  Akawaambia, MUSA, KWA SABABU YA UGUMU WA MIOYO YENU, ALIWAPA RUHUSA KUWAACHA WAKE ZENU; LAKINI TANGU MWANZO HAIKUWA HIVI.

9  Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini”

Hii ikitufundisha kuwa, kuna mambo ambayo Mungu anaweza kuyaruhusu katika maisha yetu yatokee lakini yakawa si mapenzi makamilifu ya Mungu. Hivyo ni muhimu sana kutafuta kuyajua na kuyafanya mapenzi makamilifu ya MUNGU, na ndivyo tutakavyompendeza Mungu, na kuishi kama atakavyo yeye.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Kanaani ililaaniwa (Mwanzo 9:20-25,) kwanini Mungu awapeleke wana wa Israeli katika nchi iliyolaaniwa?

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

EPUKA KUPELELEZA KILA KITU MUNGU ANACHOKUAHIDIA.

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

Nini maana ya Mithali 19:21Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.

Rudi nyumbani

Print this post

Roho ya kukata tamaa ni nini na inatendaje kazi?

Swali: Roho ya kukata tamaa ipoje na inatendaje kazi na inawezaje kumtoka mtu?


“Roho ya kukata tamaa” ni roho inayomwingia mtu na kumfanya asiweze kuendelea mbele Zaidi. Roho hii inapomwingia mtu inamfanya asiwe na nguvu ya kufanya au kutafuta jambo lolote lile lililo zuri. Ndio hapo utaona mtu anakata tamaa ya kuendelea kusubiri jambo Fulani au kuendelea kuomba au kuendelea kutafuta.

Roho hii inasababishwa na “shetani” kwasababu kamwe MUNGU hawezi kumkatisha mtu tamaa kwa jambo lolote jema mtu apangalo kulifanya au kulitafuta. Yeye (Mungu) anasema maneno yafuatayo..

Luka 18:1  “Akawaambia mfano, ya kwamba IMEWAPASA KUMWOMBA MUNGU SIKUZOTE, WALA WASIKATE TAMAA”.

Mathayo 7:7 “Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;

8  kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa”

Lakini adui kazi yake ni kukatishata tamaa, aidha kwa njia ya mawazo, ndoto au maneno ya watu.

Zifuatazo ni njia za kushughulika na roho ya kukata tamaa.

   1. MPOKEE YESU

Kama bado hujaokoka, fahamu kuwa wewe ni windo tosha la adui, na moyo wako ni malango ya maskani za roho zote chafu zikiwemo za kukatisha tamaa, hivyo maisha yako yatatawaliwa na kuvunjika moyo na kutokusonga mbele.

     2. SOMA NENO.

Soma sana Neno la MUNGU (Biblia) kwasababu ndani yake limejaa maneno ya Faraja, ambayo yanaweza kukufaa na kukutia nguvu katika nyakati zote utakayopitia za kukatisha tamaa, Kama magonjwa ndiyo yaliyokukatisha tamaa ndani ya biblia ipo mistari mingi ya kutia moyo wa kuendelea mbele.

Kama ni Ndoa ndio iliyokukatisha tamaa, yapo maneno ya faraha na kutia nguvu yahusuyo ndoa ndani ya biblia, kama ni anguko Fulani limetokea na likakukatisha tamaa, ndani ya biblia ipo mistari ya kutia nguvu ya kukunyanyua tena katika hali unayopitia. N.k

    3. MAOMBI

Fanya maombi kila siku, hii utakusaidia kukuweka katika lile joto la kiroho, na hivyo kufunga milango yote ya roho za adui za vitisho na kukatisha tamaa. Ukiwa mwombaji utakuwa katika usalama wa Roho daima.

Kwa njia hizo tatu basi waweza kujifungua na kila kifungo cha kukata tamaa, au kukatishwa tamaa.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NI JAMBO GANI LINALOMTAMANISHA SANA BWANA TUMWOMBE BILA KUKATA TAMAA?

KWANINI UKATE TAMAA?

Nini maana ya kupiga Kite! Katika biblia.

Maana yake nini, Mwe na hofu wala msitende dhambi? (Zaburi 4:4)

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

Rudi nyumbani

Print this post