Category Archive maswali na majibu

Makwazo ni nini kibiblia? Na madhara yake ni yapi?

Makwazo ni  mambo yanayozuia mwendelezo wa jambo Fulani lililokuwa limekwisha anza, au linalotaka kuanza. Kwamfano ulikuwa unasafiri lakini ghafla kwenye safari yako unakutana na mto mpana, unaokufanya ushindwe kuvuka, hicho kinaitwa kikwazo. Au ulikuwa unapika chakula chako, halafu ghafla gesi ikaishia katikati na chakula bado hakijaiva, hicho kinatiwa kikwazo.

Na rohoni pia vivyo hivyo yapo makwazo ambayo yanamzuia mtu asimalize mwendo wake wa imani, au asiendelee mbele tena katika kumtafuta Mungu. Na muhimu sana kuyajua na kujiepusha nayo.

Kibiblia makwazo yamegawanyika katika sehemu kuu tatu.

  1. Makwazo yanayowakumba watu wa Mungu kutoka kwa wapendwa wenzao
  2. Makwazo yanayowakumba watu wa Mungu kutoka kwa wapagani
  3. Makwazo yanayowakumba wapagani kutoka kwa watu wa Mungu.

1) Makwazo yanayowakumba watu wa Mungu kutoka kwa wapendwa wenzao

Tukianzana  na hilo kundi la kwanza, wapendwa tunaowazungumzia hapa ni wale ambao hawajasimama vema katika kweli. Ndio hawa ambayo Bwana Yesu anawazungumzia katika vifungu hivi;

Luka 17:1  Akawaambia wanafunzi wake, Makwazo hayana budi kuja, lakini ole wake mtu yule ambaye yaja kwa sababu yake! 2  Ingemfaa zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake, akatupwe baharini, kuliko kumkosesha mmojawapo wa wadogo hawa. 3  Jilindeni; kama ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe. 4  Na kama akikukosa mara saba katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe.

Kwa namna gani hawa wanaweza kumkosesha ndugu. Kwamfano ni pale, Mpendwa mwezako anaposikia umemsengenya, Sasa Kama ni mdhaifu kiimani Hili linaweza kuwa ni kwazo kubwa sana kwake ambalo likamfanya hata nguvu yake ya kuendelea kudumu katika kusanyiko ikapoa. Zipo shuhuda nyingi sana za wapendwa ambao wamerudi nyuma kiwokovu kwasababu ya maisha haya. Hivyo kama mwanaminio hakikisha, kinywa chako, unakichunga. Jifunze kuwa na kiasi na uvumilivu. Jifunze kujiepusha na mambo mabaya Kwa wapendwa wenzio.

Kwazo hili linaweza pia kuwa katika ufahamu wa kiroho .

Utakumbuka Ayubu, alipopitia majaribu yake mazito, hakuna mahali popote alinena maneno yasiyo faa, lakini wale marafiki zake watatu, yaani Sofari, Elifazi na Bildadi, (ambao wanawawakilisha watumishi wa Mungu), walipofika, walitumia ujuzi wao wa kibinadamu kumuhukumu Ayubu, kwamba ni kwasababu alitenda dhambi,  hiyo ikampelekea Ayubu kunena hata maneno yasiyofaa.

Kama mtumishi wa Mungu, epuka hukumu ya macho,ukiletewa tatizo la mtu/ watu, usiangalie kwa jicho la nje, mwingine ni Mungu mwenyewe anampitisha katika madarasa yake, ukajikuta badala ya kutatua tatizo ndio unaongeza tatizo juu yake. Usianze kuhukumu matukio, bali kuwa katika Roho, tegemea zaidi uongozo wa Roho Mtakatifu. Hekima itakusaidia.

Pia lipo katika ujuzi.

Ukisoma Warumi 14, maandiko yanaeleza kwa upana jinsi ujuzi wetu unaweza kuwa kwazo kwa wengine wadhaifu was imani, kwamfano wewe ukipewa chakula ambacho umesikia kimepitishwa kwenye matambiko, ukashukuru, ukakila, ukijua kabisa chakula hakiwezi kukuondoa kwenye mpango wa Mungu. Lakini kwa ujuzi huo mwingine mwenye imani haba akakuona, na yeye akaanza kula vyakula vya kimatambiko na mila, akajikuta anashirikiana na uganga na mizimu, utakuwa umemsababishia kwazo kubwa kwa Mungu.

Lolote tunalolifanya, lazima tuangalie wengine wanaiga nini kwetu sisi wenye ujuzi. Uvaaji wako, wewe kama mkristo, unaweza ukajiona hauna shida kwako, lakini wengine wakaona ni sawa, hata kuvaa mavazi hayo ambayo hayana utukufu mbele za Mungu, utakuwa umefanyika kwazo kwao

2) Makwazo yanayowakumba watu wa Mungu kutoka kwa wapagani

Wapagani wanaweza kuzuia injili, isihubiriwe mahali, wakawapiga au wakawafunga watu wa Mungu n.k. Utaona Herode alimpinga Yohana akamweka gerezani hakuweza tena kuhubiri injili, wapagani waliwapinga watakatifu wengi. Hata mitume katika ziara zao walikutana na vikwazo vingi kutoka kwa watu wa mataifa, mahali pengine hawakuweza kuhubiri kwa utulivu (1Wakorintho 15:32, 1Wathesalonike 2:2).

3) Makwazo yanayowakumba wapagani kutoka kwa watu wa Mungu.

Watu ambao hawajakamilika katika imani. Kwamfano ni mpendwa lakini mzinzi, sasa wale watu wa nje, ambao walikuwa wanakaribia kuvutwa katika imani, wanapoona matendo ya watu kama hawa, wanasema kama ukristo wenyewe ndio huu ni heri niendelee kuwa mpagani. Hayo ni makwazo. Au unakuta mwingine ni tapeli, mwingine ni mtukanaji, mambo kama haya hufanyika kwazo kubwa sana kwa wapagani kuihubiri injili.

2Wakorintho 6:3  Tusiwe kwazo la namna yo yote katika jambo lo lote, ili utumishi wetu usilaumiwe; 4  bali katika kila neno tujipatie sifa njema, kama watumishi wa Mungu; katika saburi nyingi, katika dhiki, katika misiba, katika shida;

Hitimisho:

 Hivyo wewe kama ni mkristo jitahidi sana kuyaepuka makwazo kwa waaminio wenzako au kwa wapagani. Lakini pia kama ulikwazwa na ndugu yako, basi,  suluhisho sio kuvunjika moyo au kuuacha wokovu, bali ni kunyanyuka tena na kuendelea mbele. Biblia inasema;

Mithali 24:16 Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.

Amka tena, mtumikie Bwana, kwasababu alishatujuza tangu mwanzo kwamba hayana budi kuja, hivyo hilo liwe ni jambo la kawaida kwako, jitie nguvu uendelee mbele.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mafundisho mengine:

Mpagani ni nani?

USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.

Kutoka 21:10 ina maana gani?

Biblia inasema tusiwe kwazo kwa yeyote, je! inawezekanikaje kwa dunia hii ya sasa?(2Wakorintho 6:3).

MIMI SIOMBI KWAMBA UWATOE KATIKA ULIMWENGU.

HISIA YA MUNGU ILIYO MBAYA KULIKO ZOTE.

KIKWAZO CHA EUODIA NA SINTIKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Nchi ya “Kabuli” ndio nchi gani kwasasa, na kwanini iliitwa hivyo? (1Wafalme 9:13).

Jibu: Tusome,

1 Wafalme 9:12 “Naye Hiramu akatoka Tiro kuitazama hiyo miji Sulemani aliyompa; wala haikumpendeza.

13 Akasema, Miji gani hii uliyonipa, ndugu yangu? Akaiita NCHI YA KABULI, hata leo”.

Nchi hiyo iliitwa “Nchi ya Kabuli” na sio “Nchi ya Kaburi”.Kuna tofauti ya “Kabuli” na “Kaburi”.

Maana ya “kaburi” ni shimo la kuzikia mtu aliyekufa, lakini “Kabuli” maana yake ni “isiyofaa kitu”. Kwahiyo hapo inaposema Nchi ya Kabuli, maana yake ni nchi isiyofaa kitu.

Sasa kwanini nchi hiyo iliitwa hivyo na huyu Hiramu?. Na ni funzo gani tunapata?.

Kipindi Sulemani anaijenga nyumba ya Mungu pamoja na nyumba yake mwenyewe, aliingia makubaliano na Mfalme wa Tiro kwamba Mfalme wa Tiro atampa Sulemani Malighafi za ujenzi (Miti ya Mierezi na mawe pamoja na malighafi nyingine baadhi, 1Wafalme 5:17-18), kwa makubaliano ya kwamba Mfalme Sulemani atampa Hirimu, mfalme wa Tiro ardhi kama malipo.

Sasa baada ya Sulemani kukamilisha ujenzi wa nyumba hizo mbili, ambapo alitumia miaka 20 (1Wafalme 9:10), aliazimu kumlipa Hirimu malipo yake.

Hivyo Sulemani akaamua kumpa Mfalme wa Tiro miji 20, (maana yake kila mji mmoja kwa mwaka mmoja aliotumikiwa). Zaidi ya hayo Sulemani alimpa Hiramu mwaka kwa mwaka kori nyingi za mafuta na ngano.

1Wafalme 5:10 “Basi Hiramu akampa Sulemani miti ya mierezi na miti ya miberoshi kadiri alivyotaka. 

11 Sulemani akampa Hiramu kori ishirini elfu za ngano, chakula cha watu wake, na kori ishirini za mafuta safi. Ndizo Sulemani alizompa Hiramu mwaka kwa mwaka”.

Lakini tunasoma Hiramu, Mfalme wa Tiro hakupendezwa na miji hiyo 20 iliyokuwa kaskazini mwa Israeli (Galilaya, mpakani na Tiro), na biblia haijataja sababu za yeye kutopendezwa na miji hiyo, huenda pengine aliona si mizuri na yeye alitegemea kupewa miji mingine mizuri yenye kupendeza, ambayo huenda ipo katikati ya Israeli.

Na kwasababu hakupendezwa nayo, aliipokea tu hivyo hivyo, na kuiita “miji isiyo na faida” yaani “Kabuli”

Lakini yote katika yote biblia haijaelezea kwa kina sababu ya Sulemani kufanya vile, au sababu ya Hiramu, Mfalme wa Tiro kutopendezwa nayo na hata kuiita nchi ya Kabuli (Maana yake isiyofaa kitu).

Ni nini tujajifunza kupitia habari hiyo na miji hiyo?.

Tunachoweza kujifunza ni kuwa tunapotenda wema “tusitegemee malipo kutoka kwa wanadamu, bali kutoka kwa Mungu”. Malipo ya wanadamu siku zote yana mapungufu mengi.

Mfalme huyu wa Tiro, alikuwa ni mtu mwema sana kuliko wafalme wote waliowahi kutokea Tiro, na zaidi sana alikuwa ni rafiki yake Mfalme Daudi, baba yake Sulemani, na hata alivyosikia kuwa Sulemani anataka kumjengea Mungu nyumba alifurahi sana na kumtukuza Mungu wa Israeli, (1Wafalme 5:7) hivyo akamtia nguvu Sulemani kwa sehemu kubwa sana, lakini pamoja na hayo alitazamia kupewa thawabu nyingi (malipo mengi) kutoka kwa Sulemani, kwasababu alijua Sulemani alikuwa Tajiri sana, Zaidi ya wafalme wote duniani, lakini kinyume chake akapewa vichache tofauti na alivyotegemea, hivyo moyo wake ukauma!, lakini Laiti kama angetegemea vichache ni wazi kuwa asingeumia kwa vile alivyopewa badala yake angeshukuru na thawabu yake ingezidi kuwa kubwa mbele za Mungu.

Hivyo na sisi hatupaswi kutegemea malipo kutoka kwa watu, pale tunapotenda wema bali tunapaswa tuwe na nia ya kiasi, ili wakati wa Bwana ukifika tupate thawabu kulingana na kile tulichokitenda.

Bwana atubariki.

Maran atha.

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mafundisho mengine:

Miji ya Tiro na Sidoni ni miji gani kwasasa?

Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)

Je! Sulemani alienda mbinguni?

Je Mungu anaketi katika giza? (1Wafalme 8:12)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 14 (Yoeli, na Obadia).

Rudi nyumbani

Print this post

Sakafu ya mawe/ Gabatha ni nini?

Neno hilo utalisoma katika andiko hili;

Yohana 19:13  Basi Pilato, aliposikia maneno hayo, akamleta Yesu nje, akaketi juu ya kiti cha hukumu, mahali paitwapo Sakafu ya Mawe, au kwa Kiebrania, Gabatha

Maana ya Gabatha ni “eneo lililoinuka”. Ni sehemu iliyojengwa mbele ya jumba la kifalme la Pilato ambapo hukumu zake alizitolea hapo. Kama biblia inavyosema paliitwa sakafu ya mawe. Maana yake palikuwa ni eneo la sakafu iliyojengwa kwa mawe.  (Tazama picha juu).

Hapo ndipo hukumu ya Bwana wetu Yesu Kristo ilipotolewa ya yeye kusulibiwa.

Lakini jambo ambalo unapaswa utafakari kuhusiana na tukio hilo, ni kuwa Mungu, ambaye ndiye muhukumu wa wanadamu wote, anasimama mbele ya kiti cha hukumu cha wanadamu kuhukumiwa. Mungu kukubali kuhukumiwa  Ni ishara ya unyenyekevu usiokuwa wa kawaida. Na hapo tunathibitisha kuwa hukumu za wanadamu hazitendi haki. Lakini utafika wakati na yeye mhukumu mkuu ataketi katika kiti chake cha enzi kuwahukumu wanadamu wote. Ambapo kwa haki kila mtu atalipwa sawasawa na matendo yake.

Jiulize wakati huo utakuwa upande upi?. Kwake hakuna upendeleo wa kibinadamu kama alivyofanya Pilato kwa wayahudi, kwake hakuna rushwa, kwake hakuna siri, yote yatamulikwa na kuwekwa wazi, na kama jina lako halipo katika kitabu cha uzima, utatupwa katika lile ziwa la moto, ambapo utateketea huko usiku na mchana.

Ufunuo 20:11  Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12  Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13  Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14  Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15  Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.

Je!  Umejiandaaje kukutana na mhukumu wa haki? Kumbuka huwezi kuokoka, ikiwa bado upo nje ya Kristo Yesu. Unachopaswa kufanya ni kutubu leo,  ili upate ondoleo la dhambi zako. Ndipo kuanzia huo wakati na kuendelea uwe na amani na Mungu wako,. Hakuna ukombozi kwa yoyote Yule zaidi ya Yesu Kristo.Huwezi kuokoka kwa nguvu zako mwenyewe. Yesu alikufa tayari kwa dhambi zako, ili aziondoe, akuhesabie sio mkosaji.

Ikiwa upo tayari leo kumkabidhi Bwana maisha yako ayaokoe na kuyaongoza, Basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mafundisho mengine:

Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)

Uga ni nini? Na kazi yake ni ipi kibiblia?

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

Wote wanaokumbwa na mauti sasa ni kutokana na dhambi zao?

Chetezo ni nini katika biblia? (Walawi 10:1)

“Shinikizo” ni nini kibiblia, Na maana yake rohoni ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inaposema Yesu ameketi mkono wa kuume inamaana gani?

Mungu mara nyingi huwa anatumia lugha ya picha au maumbo, ili kutupa sisi uelewa mzuri kuhusiana na mambo ya rohoni. Kama tunavyojua inapotokea mtawala, labda raisi amekualika uketi pamoja naye meza moja ule chakula, ni wazi kuwa kwa tendo hilo litakuwa limekupandisha hadhi sana.

Sasa zamani, za wafalme ilikuwa mtu aliyepewa heshima kubwa aliwekewa kiti chake kidogo pembeni mwa mfalme upande wake wa kuume. Na hiyo ilikuwa inamaana kubwa zaidi ya heshima peke yake, bali pia ilimaanisha kupewa mamlaka.

Hivyo katika biblia unapokutana na “mkono wa kuume” Mungu ametumia picha hiyo kumaanisha aidha mambo haya makuu matatu;

  1. Heshima
  2. Mamlaka
  3. Ulinzi

1. HESHIMA.

Maandiko kutuambia Kristo, ameketi mkono wa kuume wa Mungu, ni kutuonyesha, hadhi na ukuu alionao sasa. Mbinguni wapo malaika wengi wenye nguvu, wapo wenye uhai wanne, wapo maserafi na mamilioni ya malaika, lakini hakuna hata mmoja alipewa hadhi ya kuwa karibu/sawa na Mungu zaidi ya Kristo, Bwana wetu.

Waebrania 1:13  Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? 14  Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?

Kwahiyo, aliyepokea heshima, ya juu zaidi ya viumbe vyote ni Kristo Yesu Bwana wetu. Na ndio maana tunamwabudu na kumtukuza. Na heshima zote na shukrani zinamwelekea yeye tu peke yake. Ndiye Mfalme wa Wafalme, na Bwana wa Mabwana. Hafananishwi na mwanadamu yoyote duniani, au malaika yoyote mbinguni.

2. MAMLAKA.

Lakini pia mkono wa kuume sio tu heshima bali pia huwakilisha mamlaka, Kuketi kwake kule, ni kuonyesha mamlaka ya kumiliki na kutenda jambo lolote na kutiisha vitu vyote chini yake anayo.

Waefeso 1:20  aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; 21  juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; 22  akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo 23  ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote

> Vilevile anayo mamlaka ya kutuombea na kutuondolea dhambi, kama kuhani mkuu,

Warumi 8:34  Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.

>Mamlaka ya kutumwagia vipawa vya rohoni na nguvu ya kushuhudia habari njema.

Matendo 2:33  Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia,

Luka 16:19  Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kuume wa Mungu. 20  Nao wale wakatoka, wakahubiri kotekote, Bwana akitenda kazi pamoja nao, na kulithibitisha lile neno kwa ishara zilizofuatana nalo

3. ULINZI.

Uwapo karibu na mfalme, maana yake upo salama, chini ya mfumo wa ulinzi wake. Hivyo Mungu kumweka Kristo kuumeni mwake ni kutuonyesha sisi,ufalme wa Kristo hauhasiki. Na wanaompinga kazi yao ni bure. Na Mungu atawaweka maadui zake chini ya miguu yake.

Zaburi 110:1 Neno la Bwana kwa Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwafanyapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako.

Lakini jambo ambalo watu wengi hawajua ni kwamba Bwana anataka na sisi tumweke yeye mkono wetu wa kuume, maana yake tumpe heshima yake, katika mambo yetu, na yeye, atatuheshimisha, atatuinua, na atatulinda.

Matendo 2:25  Maana Daudi ataja habari zake, Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote, Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.

Usiweke Mali kuumeni kwako, usiweke elimu, au mwanadamu kuumeni kwako. Bali Kristo tu peke yake.

Unaweza pia kupitia vifungu hivi Kwa maarifa zaidi; Mathayo 22:44 , Matendo 7:55, Wakolosai 3:1, Waebrania 1:3,13, 10:12, 1Petro 3:22.

Bwana akubariki.

Je! Kristo yupo kuumeni kwako? Fahamu tu ili Kristo awe pembeni yako, na wewe pembeni yake wakati wote, ni sharti uwe umeokoka. Na wokovu unakuja kwanza kwa kutubu (, yaani kukubali kuacha njia mbaya), na hapo hapo unaupokea msamaha wa dhambi, kisha Kristo anaingia moyoni mwako. Na baada ya hapo unaitimiza haki yote kwa kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi, wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu, na Roho atakuwa tayari ameshakuja ndani yako kuanzia huo wakati na kuendelea. Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu leo akusamehe dhambi zako, basi fungua hapa kwa mwongozo mfupi wa sala ya toba>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Ubarikiwe.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume, maana yake nini?

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

Nini maana ya.. “Utoapo sadaka mkono wako wa kuume usijue ufanyalo mkono wako wa kushoto”

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

Je! waliokufa kabla ya Bwana Yesu wataokolewaje?

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

Rudi nyumbani

Print this post

Nuru ilitokea wapi wakati jua lilikuwa bado halijaumbwa?

SWALI: Siku ya kwanza Mungu aliumba Nuru, Je ilitokea wapi wakati Tunafahamu jua ambalo ndio lenye kutoa Nuru liliumbwa siku ya Nne?(Mwanzo 1:14-19)

Mwanzo 1:3-5

[3]Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru. [4]Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza. [5]Mungu akaiita nuru Mchana, na giza akaliita Usiku. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku moja.


JIBU: Mungu si kama sisi wanadamu ambao tukitaka kuunda jambo ni lazima tuwe na chanzo Fulani husika. Kwamfano hatuwezi kumleta mtu duniani Kwa kumchukua mwanamke na kumfungia ndani tu peke yake bila mwanaume tukitarajia baadaye ajifungue .

Lakini Mungu ni tofauti anaweza kumpa uzao pasipo kumkutanisha na mwanaume. Tunaona alifanya Kwa Mariamu. Lakini ameamua kuunda njia rasmi ya sisi kuzaliana, ambayo ndio hiyo ya watu wawili kukutana.

Vivyo hivyo na pale mwanzo Mungu kutanguliza Nuru, SI jambo la kushangaza kwake. Yeye ni mweza wa yote, Dunia hii ingeweza kumulika sikuzote Daima pasipo kutegemea jua Wala mwezi Wala nyote.

Lakini aliamua aviundie na chanzo chake, Kwa lengo la kutenganisha majira.

Lakini pia ni vema tukapata ufunuo, wa tukio lile, Nuru Ile ilimwakilisha nani. SI mwingine zaidi ya Yesu. Kumbuka Yesu katika agano la kale alijifunua katika maumbo. Lakini katika agano jipya waziwazi. Hivyo ilihitaji Nuru iwepo ili shughuli zote za uumbaji ziendelee.

Yohana 1:1-5

[1]Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.[2]Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. [3]Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. [4]Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. [5]Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza.

Je! Kristo Ameangaza ndani Yako? Tambua kuwa pasipo Kristo hakuna maisha, hakuna uhai, Tubu Leo mgeukie Kristo Akusamehe dhambi zako.Ili uumbwe upya na Mungu. Hivyo  Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa fungua hapa Kwa mwongozo wa Sala ya Toba>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Nini maana ya huu mstari Ayubu 23:10 ‘Lakini yeye aijua njia niendeayo; Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu’?

Je! Siku ilihesabiwaje kabla ya jua na mwezi kuumbwa?

JE UMEKUFA PAMOJA NA NANI?

JE! KUNA UMUHIMU WOWOTE WA KULIPA ZAKA?

Je ni sawa kuomba novena ya Mtakatifu Rita wa Kashia?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?

SWALI: Kikombe cha maji ya baridi ni  kipi Bwana alichokitaja katika;

Mathayo 10:42  Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia, haitampotea kamwe thawabu yake


JIBU: Ni kawaida mtu anayetoka kufanya kazi ngumu, labda ya shamba, au wanaoshiriki katika michezo labda riadha au mipira, utaona huduma ya kwanza wanayoihitaji, sio chakula, bali ni maji, kwasababu mwili huwa unapoteza maji mengi sana pale jasho linapotoka. Na gharama ya maji sikuzote ni ndogo kuliko chakula. Hivyo mtu yeyote huwa ni rahisi kupata huduma hiyo, kwani mtu anaweza kumtolea ndani mwake kwenye pipa lake la kutunzia maji masafi, au kuchota kisimani, na kumpa n.k. Na pale anapompa ya baridi kabisa basi humfanya mtu yule ayanywe yale maji sio tu kwa kukata kiu lakini pia kwa burudiko.

Vivyo hivyo na Bwana naye anawafananisha watu wake, na watenda kazi waliotoka kufanya kazi ya kuchosha, hivyo na wenyewe huwa wanakuwa na kiu chao, wanahitaji maji yao. Lakini zaidi sana maji baridi. Na mtu anayefanya hivyo Mungu amemuahidia kumpa thawabu yake.

Maji ya mwaminio ni yapi?

Yanaweza kuwa ni vyakula: Kwamfano umuonapo, mtumishi wa Mungu labda anahudumu au anahubiri pengine kwenye masoko, au mahali fulani kwa muda mrefu, na wewe ukathamini kumpatia chakula au hata chupa ya maji. Akanywa au akala ashiba akamshukuru Mungu. Hiyo ni thawabu kwako kwa Mungu.

Yaweza pia kuwa sadaka yako: Kile kidogo, kinachoweza kumtunza hata kwa siku hiyo, kwa ajili ya usafiri, au sabuni, au vocha kwa ajili ya mahitaji yake madogo madogo. Bwana amekuahidia pia thawabu yako hata kama utakiona ni kidogo, si zaidi  ukampa vya ziada? Kinabadilika kuwa kikombe cha maji ya baridi.

Yaweza kuwa pia ni “vitu”: Mfano mwingine hana fedha au chakula, lakini ana kitu Fulani cha kumpa, labda nguo, au kiatu, au simu, au huduma n.k. Hicho nacho Bwana anakihesabu kama kikombe cha maji ya baridi.

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa zipo thawabu mbalimbali ambazo Bwana anatoa, kwa kutenda mema, zipo thawabu za kuwasaidia maskini, zipo thawabu za kuwasaidia ndugu, lakini zaidi pia Bwana ameahidi thawabu kwa wale wote wanaowajali watumishi wake.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mafundisho mengine:

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA.

JE NI KIKOMBE KIPI UTAKINYWEA SIKU ILE?

YESU ANA KIU NA WEWE.

UWE KIKOMBE SAFI 

AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.

MAJI YA UZIMA.

Rudi nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Mhubiri 10:9 Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo;

SWALI: Nini maana ya Mhubiri 10:9 Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo; Naye apasuaye miti huona hatari katika hiyo.


JIBU: Mstari huu unatuonyesha hatari ya kazi yoyote inayotendwa na mtu. Hapo ametumia mfano wa wanaochonga mawe. Wajenzi wa zamani walikwenda kuchonga mawe miambani kwa ajili ya ujenzi wa majengo yao, lakini wakiwa kule walikutana na hatari nyingi, aidha kuangukiwa na mawe hayo, na kuwaponda viungo vyao, vifaa vyao  vya uchongaji kuwajeruhi.

Vilevile anatumia tena mfano wa wanaopasua miti, kwa ajili ya mbao za ujenzi, bado na wao pia wanakutana na hatari, aidha kuangukiwa na miti yenyewe, au shoka kuteleza na kumjeruhi mtu au yeye.

Kumbukumbu 19:5 kama aingiapo mtu na mwenziwe mwituni kwenda kukata kuni, akapeleka mkono wake na shoka ili kukata mti, likatoka shoka katika mpini, likampiga yule mwenziwe hata akafa; basi na akimbilie katika miji hii mmojawapo awe hai.

Ni sawa na mjenzi ambaye amezoea kupiga sana nyundo au kuwepo maeneo ya ujenzi muda wake mwingi, utaona upo wakati nyundo itateleza na kumponda kidole chake, au atakanyaga msumari n.k. Tofauti na kama angekuwa hajishughulishi na kazi hiyo yupo nyumbani tu.

Hii ni kufunua nini rohoni?

Kama wana wa Mungu tufahamu kuwa kazi yake ya kwenda kung’oa mapando ya mwovu, katika shamba la Bwana  tutarajie kukutana na madhara yake, si wakati wote utakuwa ni mwepesi tu (yaani kuvuna), zipo nyakati tutakutana na kupigwa, au kudhalilishwa, au kufungwa na wakati mwingine hata kuuawa. (Mathayo 10:17-19)

Mtume Paulo alipokuwa katika ziara zake za kupanda ukristo Asia na Ulaya, alikutana na hatari nyingi, ikiwemo kupigwa mawe na watu wabaya, kufungwa, na kurushiwa vitisho mbalimbali. Wamishionari kama dr David Livingstone walioleta injili Afrika zamani walikutana na hatari za magonjwa kama malaria, na wanyama wakali.

Lakini katika yote, Bwana ameahidi, mafanikio makubwa,  kuliko hatari zake. Hivyo hatupaswi kuogopa na kudhani kuwa kazi ya Mungu ni kazi ya kwenda kujichinja wakati wote. Hapana, zipo nyakati nyingi za raha, na mafanikio makubwa ya rohoni yasiyokuwa na ghasia yoyote, lakini Bwana hajatuficha pia hatari zake wakati mwingine. Ili tutakapokutana nazo tusihuzunike moyo na kukata tamaa, bali tuendelee na kazi.

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Je! Umesamehewa dhambi zako? Kama ni la, ni nini kinachokusubirisha? Ukifa leo utakwenda wapi, kumbuka lipo ziwa la moto, kumbuka ipo hukumu kwa waovu. Tubu leo mgeukie Kristo akusafishe dhambi zako,  Ukabatizwe katika jina la Yersu Kristo upokee ondoleo la dhambi. Hizi ni siku za mwisho, Kristo anakaribia kurudi.

Ikiwa upo tayari leo kufanya hivyo basi fungua hapa kwa mwongozo huo>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mafundisho mengine:

Yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.

Je! fedha ni jawabu la mambo yote? (Mhubiri 10:19).

TUUTAFUTE UMOJA WA ROHO.

Fahamu maana ya Mithali 28:20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana jijaribuni wenyewe na ‘isipokuwa mmekataliwa’?

SWALI: Biblia inamaana gani inaposema jithibitisheni wenyewe kama mmekuwa katika imani, na pale pia inaposema “isipokuwa mmekataliwa”? Maana yake ni nini?

2 Wakorintho 13:5

[5]Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa.

JIBU: Kama wakristo biblia inatuasa tuwe watu wa kufanyia mazoezi Imani yetu, ili tujithibitishe kama kweli tupo katika mstari sahihi wa Imani au la.

Ili kuelewa tuchukue mfano wa  kijana mdogo ambaye anajifunza kuendesha baiskeli. Kwa hatua za mwanzo ni dhahiri kuwa atatumia baiskeli yenye miguu mitatu, ili iweze kumsaidia kumpa uwiano asianguke, na hivyo akiwa katika baiskeli Ile anaweza kuiendesha Kwa jinsi awezavyo kwasababu akikosa ule uwiano( balance), basi Ile miguu ya pembeni itamsaidia..na hivyo ataendesha bila changamoto yoyote, kama tu yule mtu anayejua kuendesha.

Lakini ijapokuwa atakuwa  anaiendesha Kwa kasi au maringo kiasi gani bado hajaweza kuwa mwendeshaji kamili, Mpaka siku yatakapotolewa Yale matairi ya pembeni, na kumwacha aimudu  mwenyewe ile baiskeli kama waendeshaji wengine. Pale ndipo utakapojua kweli huyu alikuwa ameshaweza au la!. 

Hivyo tunaweza kusema, kama hajaweza kujisimamia mwenyewe tayari amekataliwa (yaani, hajakubalika kama mwendesha baiskeli kamili)

Ndivyo ilivyo katika ukristo. Kuna wakati utakuwa unashikwa mkono, lakini upo wakati utahitaji kusimama mwenyewe kujithibitisha, kwamfano labda ilikuwa ikifika muda wa maombi unapigiwa simu/ au unahimizwa na kiongozi wako kufanya hivyo, na kweli unaamka na unasali sana. Lakini huna budi kujijengea ufahamu huu ikiwa siku moja kiongozi wako hayupo, au amesahau kukupigia simu au amepoa  je utaamka mwenyewe uombe?. Ukiona Unaweza kufanya hivyo basi tayari wewe umethibitika katika Imani. Lakini ikiwa ni kinyume chake basi bado kiroho hujakubalika.

Jiulize unapokuwa Mazingira yasiyo ya kikanisa, mazungumzo unayozungumza ni ya namna gani. Ikiwa sio ya maana, hata kama utakuwa unahubiri na kuzungumza habari za Mungu, uwapo na wapendwa muda mrefu kiasi gani..bado kiroho hujakubalika (umekataliwa)..unapaswa ujitengeneze .

Hivyo yatupasa tujijaribu Kwa namna hiyo. Ukristo ni sisi kuwa Nuru katika Giza, sio Nuru katika Nuru tu. Hatuvai vizuri tunapokwenda kanisani tu, Bali hata tunapokuwa katika Mazingira yasiyo ya ibadani. Huko ndiko kujithibitisha. Mungu anavutiwa na mkristo anayethibitisha Imani yake miongoni mwa wenye dhambi zaidi ya yule anayefanya Kwa waaminio. Jitathimini unapokuwa mwenyewe, ni Nini unatazama mitandaoni, muda wako mwingi unautumiaje,ni nani unayechati naye?. Wajibu wako Kwa Bwana unautimizaje? Huko ndiko kujithibitisha.

Lakini ikiwa tuwapo nje tunashindwa kuwa kama tuwapo ndani basi hilo Neno “isipokuwa mmekataliwa”, ndio linakuja..maana yake bado hatujakidhi vigezo vya kiroho, Mungu anavyovitazamia kwetu. Ukiwa ni kundi la kusukumwa  kutenda jambo Fulani la kiroho lililo wajibu wako, bado hujakubalika.

ukiona hivyo basi yakupasa ufanye juhudi, kumaanisha wokovu wako Kwa Mungu. Kama mkristo usijisifu kwenye juhudi za kusimamiwa, jisifu kwenye juhudi za kujisimamia.

Hiyo ndio tafsiri yake, lakini Neno hilo halimaanishi kama watu wengine wanavyodhani kuwa wapo watu ambao “Mungu amewakataa” ambao hata iweje hawawezi kuupokea wokovu hapana, watu wote wanapokelewa na Mungu wanapotii sauti ya Mungu. Hakuna mtu ambaye akimfuata Mungu hata akionyesha juhudi kiasi gani  atakataliwa, hapana.

Bwana akubariki.

Je! Na wewe upo kundi gani? Una habari kuwa hizi ni nyakati za mwisho? Neema ya Kristo inakuita hata Leo, ujue kuwa haitafanya hivyo milele. Ni heri utubu dhambi zako ufanye badiliko, upate ondoleo la dhambi, Yesu Akupe uzima wa milele. 

Ikiwa upo tayari Kwa jambo hilo basi..fungua hapa Kwa mwongozo huo >>>  KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Mathayo 23:15 inaposema namfanya kuwa mwana wa jehanum mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe.

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

Nini maana ya “wanawake saba watamshika mtu mume mmoja”

NI NANI ATAKAYEWAPA ILIYO YENU WENYEWE?

Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?

UNAVYOZIDI KUWA MWENYE HAKI, NDIVYO KUJITAMBUA KWAKO KUNAVYOPUNGUA.

Rudi nyumbani

Print this post

Jina Lusifa (lucifer), tunalisoma wapi kwenye biblia? 

JIBU: Hakuna Mahali popote katika biblia ya Toleo letu la Swahili Union version (SUV) au matoleo mengine kadha wa kadha ya kiswahili, utapishana na hili Neno Lusifa. Lakini swali, kama ni hivyo Kwanini tunalitumia kumwakilisha shetani. Je! Limetokea wapi?

Neno hili ni la kilatini, ambalo linamaanisha NYOTA YA ALFAJIRI. Hivyo tukirudi katika maandiko upo unabii katika kitabu Cha Isaya unaomwelezea shetani, na unamtaja yeye kama ndio  Ile “Nyota ya alfajiri”

Isaya 14:12

[12]Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi!  Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa!

Hivyo watakatifu wa zamani, walipokuwa wanatafsiri biblia kutoka katika lugha ya kiyahudi kwenda kilatini (vulgate), kwenye Karne ya 4  Ndipo Neno hili nyota ya alfajiri ambalo linalosomeka kama “Helel” Kwa lugha ya kiebrania likaandikwa kama “lusifa” Kwa kilatini.

Na baadaye Neno hili lilikuja kupata umaarufu, zaidi katika biblia ya Toleo la kiingereza inayojulikana  kama King James version (KJV), kwani waliendelea kuliacha Neno hili la kilatini, Mahali palepale  panaposema nyota ya alfajiri. 

Hivyo umaarufu wa Neno hilo ukasambaa sio tu Kwa waongeaji wa lugha ya kilatini, Bali mpaka Kwa wale wa kiingereza. Na ndio maana mpaka sasa wewe unalifahamu.

Lakini matoleo mengine mengi, Ikiwemo letu hili la kiswahili (SUV), haikutoa katika hiyo lugha ya kilatino, Bali imeacha vilevile kama nyota ya alfajiri.

Hivyo Kwa kuhitimisha ni kuwa shetani ndio huyo huyo Lusifa. Ikiwa utapenda kufahamu majina yake mengine kama yanavyotajwa kwenye biblia basi fungua hapa >>> APOLIONI.

Je! Unahabari kuwa hizi ni siku za mwisho na Yesu anakaribia kurudi? Umejiandaaje? Kumbuka shetani anatambua kuwa muda wake umeisha(Ufunuo 12:12), iweje wewe usitambue. Ni nini unachokisubiria usimkaribishe Yesu katika maisha Yako?  Huu ulimwengu hauna muda mrefu unaisha, itakufaidia nini upate kila kitu, kisha upate hasara ya nafsi yako? Jifikirie  usisubiri kukumbushwa kumbushwa, ni wewe mwenyewe kuona hali halisi, kisha uchukue hatua

, ikiwa upo tayari Kumpa Bwana Yesu maisha yako, basi fungua hapa Kwa mwongozo wa Sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

 Ubarikiwe.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

NYOTA ZIPOTEAZO.

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

Shetani ni nani?

YUKO WAPI MFALME WA WAYAHUDI?

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 3)

Rudi nyumbani

Print this post

Washami ni watu gani katika biblia?

Jibu: Washami wametajwa mara nyingi katika biblia, baadhi ya mistari iliyowataja na kama ifuatayo.. 2Samweli 8:6, 1Wafalme 20:21, 2Wafalme 5:2, Yeremia 35:11, Amosi 9:7 na sehemu nyingine nyingi utaona jamii hii ya watu ikitajwa.

Tukio mojawapo maarufu lililozungumziwa katika biblia liwahusulo Washami, ni lile la Nabii Elisha kulipiga upofu Jeshi lao na kuliongoza mpaka katikati ya Samaria. (soma 2Wafalme 6:10-20).

Sasa swali hawa Washami walikuwa ni watu gani?

Washami walikuwa ni watu walioishi katika Nchi ijulikanayo kama Siria/Syria kwasasa,

Kiswahili cha Siria ni  “Shamu” hivyo wenyeji wa nchi ya Shamu ndio walioitwa Washami.

Jamii ya watu hawa Washami, kwasasa haipo!, wala haijulikani, kutokana na Falme nyingi kupita zilizotawala dunia na hivyo kuchanganya jamii za watu katika maeneo husika, hivyo hakuna jamii ya washami ijulikanayo leo duniani, lakini nchi hiyo bado ipo, na sasa wanaishi waarabu (Uzao wa Ishmaeli), ndio inayoitwa Siria, na makao makuu yake ni Dameski. (Kumbuka hawa waarabu sio washami  waliozungumziwa katika biblia, bali wapo tu kama wahamiaji waliohamia katika hiyo nchi)

Kiroho Washami wanawakilisha jeshi la Adui, kwani ukisoma katika biblia  utaona ni karibia mara zote jeshi hili lilikinzana na Israeli. Na utaona wakati ule Elisha alipokuwa na mtumish wake, walipoona jeshi la Washami limewazunguka, Elisha alimwambia mtumishi wake asiogope kwani walio upande wao ni wengi kuliko jeshi wanaloliona mbele yao.

2Wafalme 6:15 “Hata asubuhi na mapema mtumishi wake yule mtu wa Mungu alipoondoka, na kwenda nje, kumbe! Pana jeshi la watu, na farasi na magari, wameuzingira mji ule. Mtumishi wake akamwambia, Ole wetu! Bwana wangu, tufanyeje?

16 Akamjibu, USIOGOPE; MAANA WALIO PAMOJA NASI NI WENGI KULIKO WALE WALIO PAMOJA NAO.

17 Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote.”

Hali kadhalika na sisi ni lazima siku zote tuone, na kufahamu kuwa jeshi la Mungu linalotuzunguka ni kubwa kuliko lile la Adui, ikiwa tupo ndani ya Neema ya damu yake!, lakini kama tupo nje ya Neema ya damu yake (yaani wokovu), basi tufahamu kuwa adui atakuwa na nguvu juu yetu, na wala hakuna tutakachoweza kumfanya, Nguvu yetu na ujasiri wetu upo katika Yesu tu?

Je umeokoka? Kama bado ni afadhali ukaokoka leo, maana hujui kesho itakuwaje, na kama unahitaji msaada huo basi wasiliana nasi kwa namba zetu tajwa hapa chini.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Wasamaria walikuwa ni watu gani?

Kisiwa cha Patmo kipo nchi gani?.

KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.

BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.

Je Yuda alienda wapi, ni mbinguni au jehanamu?

Rudi nyumbani

Print this post