TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi

TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi

Mafundisho maalumu Kwa ajili ya watumishi wa Mungu.

Huu ni mwendelezo wa mafundisho maalumu Kwa ajili watumishi wa Mungu, ikiwa wewe ni Mchungaji, mwalimu, mtume, askofu,Nabii, au mtu yoyote unayemtumikia Mungu katika nafasi yoyote kanisani au kwenye huduma basi mafundisho haya yatakufaa sana.

Wakati ule Yakobo alipodhamiria kwenda kukutana na ndugu yake Esau baada ya kutengana naye Kwa muda mrefu..maandiko yanasema walifurahi sana walipoonana kule nyikani. Na baada ya mazungumzo Yale kuisha,  sasa ikiwa ni wakati wao wa kuondoka pale nyikani walipokutana waelekee Kaanani.

Na kama tunavyosoma habari tunaona ndugu yake Esau alimshurutisha wasafiri pamoja naye. Ndipo Yakobo akamwambia Esau kuwa jambo hilo ni gumu kwake..kwasababu ya Hali ya makundi mbalimbali na watu na mifugo aliyokuwa nayo..Tusome..

Mwanzo 33:12-17

[12]Kisha Esau akamwambia, Twende zetu, tusafiri, nami nitakutangulia.

[13]Akamjibu, Bwana wangu anajua ya kuwa watoto ni wachanga, tena kondoo na ng’ombe nilio nao wanyonyesha. Hao wanyama wakiharakishwa siku moja, watakufa wote.

[14]Tafadhali bwana wangu na apite mbele ya mtumwa wake; nami nitawaongoza polepole kwa kadiri ya mwendo wa wanyama walio mbele yangu, na kwa kadiri ya mwendo wa watoto, hata nitakapofika kwa bwana wangu huko Seiri.

[15]Esau akasema, Nikuachie, basi, baadhi ya watu walio pamoja nami. Akasema, Pana haja gani? Na nione kibali tu machoni pa bwana wangu.

[16]Basi Esau akarudi siku ile ile akishika njia yake mpaka Seiri.

[17]Yakobo akaendelea mpaka Sukothi. Akajijengea nyumba, akawafanyia makundi yake vibanda. Kwa hiyo jina la mahali pale pakaitwa Sukothi.

Ni nini cha kujifunza hapo?

Yakobo alilitambua kundi analolichunga, alijua kuwa wapo watoto wachanga ndani yake, na mifugo pia michanga, Ambayo haijazoezwa kupelekwa mkiki mkiki, kwani ikilazimishwa kufanywa hivyo itakufa yote njiani. Hivyo akaomba muda wa kusafiri wake uongezwe, kusudi kwamba ayakokote taratibu taratibu mpaka yatakapofika kule Shekemu alipokuwa anapakusudia. Pengine mwendo wa siku moja tu ikamgharimu mwezi.

Tofauti na Esau yeye alikuwa na watu wa vita tu,watu walio hodari, Lakini Yakobo alikuwa na makundi yote. Na hivyo kwenda nayo taratibu taratibu ilimgharimu .

Hii ni kutufundisha asili ya msimamizi wa kweli, kwanza hulijali kundi lake, pia anakuwa tayari kuchukuliana na vile vyombo dhaifu. Kwasababu sio wote katika kanisa watakuwa na mwendo kama wa kwao, SI wote watakuwa wepesi kustahimili vishindo kama baadhi yao. Hivyo wewe kama kiongozi ni lazima ujifunze kuendana na makundi yote kama Musa kule jangwani, ili kisipotee chochote. Maana yake ni kuwa usiwe na haraka ya kufikisha kundi Mahali Fulani Kwa jinsi utakavyo, vinginevyo utawaua wengine.

Yakobo alipaita mahali pale Sukothi, kwasababu ndipo alipowajengea makundi yake vibanda. Na wewe pia jenga Sukothi yako.

Bwana akubariki.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

TOFAUTI YA MITUME, MANABII, WAINJILISTI, WACHUNGAJI NA WAALIMU NI IPI?

Mtu asiye na akili ni nani kibiblia?

MAFUNDISHO YA NDOA.

MIGAWANYO MINNE (4), YA HUDUMA YA YESU.

Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments