Guruguru na Goromoe ni wanyama gani? (Walawi 11:30)

Guruguru na Goromoe ni wanyama gani? (Walawi 11:30)

Jibu: Turejee.

Walawi 11:29 “Tena katika vitu vile vitambaavyo, vitambaavyo juu ya nchi, hivi ni najisi kwenu; kicheche, na panya, na mjombakaka, kwa aina zake, 

30 na GURUGURU na kenge, na mjusi na GOROMOE, na lumbwi. 

31 Wanyama hao ndio walio najisi kwenu katika hao watambaao; awaye yote atakayewagusa, wakiisha kufa, atakuwa ni najisi hata jioni”

Guruguru ni jamii ya mijusi wanaishi katika miti, tazama picha juu, na Goromoe ni mijusi wanaishi katika miamba au mchanga, tazama picha chini.

Kumjua Lumbwi ni mnyama gani fungua hapa >> Lumbwi ni nini katika biblia?

Viumbe hawa, Bwana Mungu aliagizwa wasiliwe katika Agano la kale, si kwasababu vilikuwa na sumu au madhara katika mwili, bali vilikuwa vimebeba tabia zinazowakilisha tabia za  jamii/ aina Fulani ambayo haikuwa inampendeza Bwana Mungu.

Na tulipoingia katika Agano jipya hakuna sheria tena ya kula au kutokula wanyama hao, maadamu hawana sumu kwenye mwili.

Kwahiyo Guruguru na Goromoe ni halali kuliwa kibiblia , ingawa si chakula kifaacho sana kwa jamii zote, ikiwa na maana kuwa kama ukiona havikufai vitu hivyo pia si dhambi kutovila, ingawa ni halali kuliwa.

1Wakorintho 10:23  “Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo”

Maran atha

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Lumbwi ni nini katika biblia?

Kwanini samaki wasio na mapezi na magamba hawakuruhusiwa kuliwa?

Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?

Mjombakaka ni nani kwenye maandiko? (Walawi 11:29)

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments