Kwanini samaki wasio na mapezi na magamba hawakuruhusiwa kuliwa?

Kwanini samaki wasio na mapezi na magamba hawakuruhusiwa kuliwa?

Mambo ya Walawi 11:9-12

[9]Katika hao wote walio ndani ya maji mtakula hawa; kila aliye na mapezi na magamba, ndani ya hayo maji, na ndani ya bahari, na ndani ya mito, mtakula hao.

[10]Na hao wote wasio na mapezi na magamba, ndani ya bahari, na ndani ya mito, katika hao waendao majini, na katika wote wenye uhai, waliomo majini, hao ni machukizo kwenu,

[11]watakuwa machukizo kwenu; msiile nyama yao, na mizoga yao itakuwa machukizo kwenu.

[12]Kila asiye na mapezi wala magamba aliye ndani ya maji ni machukizo kwenu.

Mapezi ya samaki, ni vile vitu kama mbawa ngumu zenye mfano wa miiba  zinazokaa Kwa juu, au pembeni au nyuma mwa mwili wa samaki.Ukitazama samaki kama perege, sato au sangara utaona mapezi Yao.Na faida za mapezi hayo ni kuwa yanasaidia kuogelea, kuelea vema kwenye maji, kukunja Kona, kuongeza kasi na kusimama au kugeuka Kwa haraka.

Halikadhalika samaki waliokuwa na magamba ndio tu walioruhusiwa kuliwa. Na magamba yaliwasaidia kujilinda na maadui au wadudu wavamiaji kwenye mwili. Kwani ngozi ya samaki ni laini hivyo isipofunikwa na magamba magumu kama yale, meno makali ya maadui yanapopita ni rahisi kujeruhiwa, Yanakaa kama dirii kifuani mwa askari.

Lakini si samaki wote walikuwa na haya mapezi na magamba, Bali wengine hawakuwa nayo mfano wa Hawa ni kama kambale, papa, pomboo, pwezi.

Sasa Kwanini viumbe hivyo vikatazwe kuliwa na ufunuo wake ni upi Rohoni?

Kama tunavyofahamu agano la kale ni kivuli Cha agano jipya, sio kwamba viumbe hivyo vikiliwa vitamkosesha mtu mbingu, au vitamnajisi roho , hapana. Bali vilifanywa vile kwa makusudi ili kutupitishia sisi ujumbe wa Rohoni katika agano letu jipya. Kwamba na sisi kama tutafanana na mojawapo wa viumbe hivyo Rohoni basi tunakuwa najisi mbele za Mungu.

Samaki mwenye magamba ni mwenye ulinzi wa kutosha dhidi ya mashambulizi ya maadui. Na sisi tunapokosa ulinzi wa Rohoni mfano wa yule askari anayezungumziwa katika Waefeso 6, mwenye dirii ya haki kifuani, ngao ya Imani mkononi na chepeo ya wokovu kichwani. Tunakuwa ni wadhaifu, kiasi Cha kutoweza simama mbele ya adui yetu shetani. Hivyo ni kuhakikisha kuwa umesimama imara katika wokovu wako, lakini pia utambue haki uliyopewa katika  msalaba wa Yesu Kristo na Imani Yako timilifu ndani ya wokovu wako. Hapo utakuwa umejidhatiti vya kutosha mfano wa samaki mwenye gamba gumu, au mamba aliyefunikiwa na ngozi yenye gamba.

Ayubu 41:13 “Ni nani awezaye kumbambua magamba yake? Ni nani atakayepenya dirii yake maradufu?  14 Ni nani awezaye kuifungua milango ya uso wake? Meno yake yatisha kandokando yake.  15 Magamba yake yenye nguvu ndiyo fahari yake, Yamefungamana pamoja kama kwa kufungwa kwa muhuri.  16 Jinsi yalivyoshikamana Hata upepo hauwezi kupita kati.  17 Yamefungamana pamoja; Yameshikamana, hata hayawezekani kutengwa”

Vilevile samaki aliyekuwa na mapezi alikuwa ni mwepesi kukatiza katika maji. Ni sawa na mabawa Kwa ndege, au miguu na kwa mtu. Hivyo na sisi katika ulimwengu huu wa dhambi ili tusionekane kuwa najisi tuvae mapezi yetu ambayo maandiko yanasema .Ndio ule utayari wa kuihubiri injili.

Waefeso 6:15

[15]na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;

Tusienende Kama watu wasio na kusudi maalumu la kufanya duniani, tuvae utayari, ndio mapezi yetu tutembee ulimwengu kote kiuhubiri/ kushuhudia habari njema.Kwasababu tukikosa haya, siku ile ya mwisho, tutatengwa samaki wema na waovu..Kisha wale waovu watatupwa nje.

Mathayo 13:47  ‘Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna;

48  hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa. 49  Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki’

Tusiwe samaki najisi.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Injili iliyopo kwa Samaki aina ya Eeli.

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

Mjombakaka ni nani kwenye maandiko? (Walawi 11:29)

Lumbwi ni nini katika biblia?

Je! Ni kweli kuna samaki mtu (Nguva) Baharini.

Je! Ni dhambi kumpiga au kumuua mnyama bila sababu yoyote?

Manyoyota ni nini (Ayubu 37:6)

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
5 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
1 year ago

Amen

Anonymous
Anonymous
1 year ago

Barikiwa sana mwalimu

Michael Paul
Michael Paul
1 year ago

Amina,nimebarikiwa na somo zuri.Tutende matendo mema yatakayotuweka mbali na unajisi(Ugomvi,Uasherati,Ulevi,Matukano,Chuki n.k)