Injili iliyopo kwa Samaki aina ya Eeli.

Injili iliyopo kwa Samaki aina ya Eeli.

Injili ya Yesu Kristo imejificha katika viumbe vya asili. Bwana mahali biblia inamfananisha Bwana Yesu na Mwanakondoo, sehemu nyingine kama Simba, sehemu nyingine Bwana Yesu anafanishwa na “Jiwe” , mahali pengine Roho Mtakatifu anafanishwa na Huwa (njiwa).

Lakini pia kuna mahali Bwana Yesu alituwaambia tuwatazame kunguru pamoja na Maua ya kondeni (Luka 12:24), na sehemu nyingine aliufananisha mbinguni na Wafanya biashara, na sehemu nyingine wakulima, na sehemu nyingine aliufananisha na wavuvi wanaokwenda kuvua..Na sehemu nyingine aliwafananisha watu kama samaki wanapaswa kuvuliwa.

Kwahiyo kwa ufupi ni kwamba Injili ya Bwana Yesu Kristo imejificha pia  katika viumbe vya asili. i.

Hivyo wakati mwingine hatuna budi kujifunza juu ya baadhi ya  viumbe, na kupata hekima..

Leo tutamtazama Samaki mmoja aitwaye Eeli.

Je unamjua Samaki aina ya Eeli? Je unayajua maajabu yake?, na Injili gani imejificha nyuma ya Maisha yake?

Eeli ni Samaki ambao ni familia moja na Kambale. Samaki hawa wanaishi katika maji mafupi, . Lakini Samaki hawa maajabu yake ni kwamba wanatengeneza umeme mkubwa sana katika miili yao, ambao umeme huo wanautumia kujilinda dhidi ya maadui na kujitafutia vitoweo.

Eeli  anapokumbana na hatari mbele yake, labda Samaki mwingine aliye mkubwa kuliko yeye, au kiumbe kingine chenye kutishia usalama wake,  basi huitoa shoti hiyo na kumpiga adui yake.

Na kiwango cha umeme Samaki Eeli mmoja anachoweza kuzalisha kwa pigo moja ni mpaka Volti 650, na wakati Volti za 150 tu zinatosha kumuua Mwanadamu, lakini yeye hutoa hadi volti hizo 650, ambazo kama zikimfikia mwanadamu, sio tu kumuua papo kwa hapo, bali pia zinaweza kumuunguza viungo vyake vya ndani.

Lakini Pamoja na kwamba Samaki huyu, anayo silaha hatari namna hiyo kuliko samaki wote,  ambayo inaweza kumuua mtu au kiumbe hai chochote ndani ya dakika moja, lakini bado ni Samaki mpole sana, bado hayupo katika orodha ya viumbe au viumbe hatari duniani. Hayupo hata 100 bora ya viumbe hatari, hata samaki sangara kamzidi kwa ukali!.

Ni samaki ambaye ni hatari sana lakini anayejihadhari sana na maadui zake, na asiyetumia uwezo wake wote kiasi kwamba hata ikitokea kakanyagwa na mtu ndani ya maji kwa bahati mbaya,  yeye hutoa  kiwango kidogo tu cha shoti, ambacho kitamshtua adui yake, amwache au akae mbali naye lakini si kumuua kabisa.

Tofauti na Samaki wengine kama samaki jiwe, au jelly au papa ambao hawana silaha kali kama hiyo,  lakini ni wakorofi mno, kiasi kwamba akipita adui mbele yao, au akihisi hatari basi ana uwezo wa kutumia uwezo wake wote, kudhuru.

Laiti Eeli angekuwa mwenye hasira kama za Papa, au samaki mwingine yeyote, leo hii engeshika nafasi ya kwanza kwa viumbe hatari ulimwenguni. Kwasababu hakuna kiumbe chochote chenye silaha kali kama hiyo, hata nyoka ijapokuwa sumu yake ni kali na inayoua kwa haraka, kama mtu hajapatiwa matibabu..

Eeli yeye silaha yake ya shoti, inaua papo kwa hapo endapo akitumia uwezo wake wote. Na kutokana na maisha yake hayo imemfanya kuwa moja ya samaki wanaoishi muda mrefu sana, mpaka kufikia miaka 85.

Ni nini tunajifunza kwa Eeli?

Na sisi kama watu wa Mungu, tunazungukwa na nguvu za Mungu,  kwa kiwango kikubwa sana… Lakini Nguvu hizi hatupaswi kuzitumia kuharibu wengine, nguvu hizi zimo ndani yetu, kutulinda tu na mishale ya yule adui, lakini si kutufanya tuonekane watofauti duniani.

Hebu tumtazame mmoja aliyekuwa kama huyu Samaki Eeli, ambaye alikuwa na nguvu nyingi kuliko wote, lakini hakuutumia uwezo wake wote..

Tusome,

Luka 9:51 “Ikawa, siku za kupaa kwake zilipokuwa karibu kutimia, yeye aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu;

52 akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.

53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu.

54 Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?

55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]

56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine”.

Hapo Bwana Yesu alikuwa ana uwezo wa kushusha moto, na ndani ya dakika moja wale wale wasamaria wangekufa wote, bila kubakia hata mmoja lakini, hakuutumia uwezo wake huo, bali aliwarehemu kwasababu alikuwa anajua hawajui watendalo. Soma tena kisa kama hicho hicho katika Mathayo 26:51-53.

Na sisi pia hatuna budi kuwa kama Bwana Yesu..Bwana Yesu alipigwa lakini hakurudishwa, ingawa alikuwa na uwezo wa kurudisha mapigo makali, alitukanwa lakini hakurudisha matusi, aliambishwa lakini hakuabisha, ingawa alikuwa na uwezo wa kuabisha..n.k.

Alikuwa mfano wa Eeli ambaye anao uwezo mwingi lakini ni pole..

Wafilipi 4:5 “Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu”.

Hatupaswi kuwalaani watu kwa jina la Bwana, hata kama wanatumia nguvu za giza, tunachopaswa kukilaani na kukiharibu ni zile kazi wanazozifanya, na tunazilaani kwa kuomba, kuhubiri, kusoma Neno na kuishi maisha matakatifu..

Tuwe kama Eeli.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

Je! Ni kweli kuna samaki mtu (Nguva) Baharini.

UVUVI BORA HAUCHAGUI, CHA KUVUA.

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
6 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
M
M
1 year ago

Be blessed

Ulimbaga Knowledge
Ulimbaga Knowledge
1 year ago

Bwana YESU awabariki, nashukuru nimejifunza tabia hii ya Mungu wetu mkuu Yesu kristo..

Peter
Peter
1 year ago

Asante sana mungu akubariki ndugu