Title January 2021

kwanini Yakobo amefananishwa na mdudu?(Isa 42:14)

SWALI: Mtumishi wa Bwana napenda kufahamu Neno hili kwenye Isaya 41:14 kwanini Yakobo amefananishwa na mdudu?


JIBU: Tuanzie kusoma juu kidogo mstari wa 8 na kuendelea ili tupate picha nzuri Zaidi..

Isaya 41:8 “Nawe, Israeli, mtumishi wangu; Yakobo, niliyekuchagua; mzao wa Ibrahimu, rafiki yangu;

9 wewe niliyekushika toka miisho ya dunia, na kukuita toka pembe zake, nikikuambia, Wewe u mtumishi wangu; nimekuchagua wala sikukutupa;

10 usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.

11 Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia.

12 Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako.

13 Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia.

14 USIOGOPE, YAKOBO ULIYE MDUDU, NANYI WATU WA ISRAELI; mimi nitakusaidia, asema Bwana, na mkombozi wako ni Mtakatifu wa Israeli.

15 Tazama, nitakufanya kuwa chombo kikali kipya cha kupuria, chenye meno; utaifikicha milima, na kuisaga; nawe utafanya vilima kuwa kama makapi.

16 Utawapepeta, na upepo utawapeperusha; upepo wa kisulisuli utawatawanya; nawe utamfurahia Bwana, utajitukuza katika Mtakatifu wa Israeli”.

Kama tunavyoweza kuona hapo Mungu anawafananisha Israeli watu wake na  wadudu, viumbe wanyonge wasio na uwezo wala nguvu yoyote ya kushindana, au kujitetea, tena mdudu anayezungumziwa hapo ni yule mnyoo, ambaye hawezi kutembea umbali mrefu, ni rahisi kukanyagwa, na kupotea,..

Hiyo ni kuonyesha kuwa watu waliochaguliwa na Mungu ni kama wadudu tu, masalia ya dunia, mabaki, watu wasiokuwa na kitu chochote cha kujivunia, , wasioweza kufanya lolote,

Kumbuka wakati  Mungu anayazungumza hayo maneno  taifa la Israeli wakati huo halikuwa taifa hodari sana kama mataifa mengine duniani, ulinganisha na   Babeli au Misri, au Ashuru, au Tiro, au Sidoni, bali lilikuwa ni taifa la kawaida tu linyonge.

Lakini kwasababu lilimfanya Mungu kuwa tegemeo lao, ndio maana likaonekana kuwa ni tishio ulimwenguni kote,.Na mataifa yakawa yanaliogopa taifa hilo kwa jambo hilo tu moja la Mungu wao Yehova.

Sasa kulingana na vifungu hivyo tunaona Mungu akilifariji dhidi ya maadui zao ambao watakuja kukusanyika  kupigana nao, na ndio hapo utaona akiwaambia japo wao ni kama wadudu tu, lakini atawafanya kuwa kama chombo kikali cha kupuria, chenye meno, ya kuisambaratisha milima mikubwa na kuisagasaga..(Mstari wa 15-16). Na sote tunajua jinsi Mungu alivyokuwa akilipigania taifa hili katika vita vigumu vilivyoshindakana

Na sisi pia, tukimfanya Mungu kuwa tegemeo letu, haijalishi tutakuwa ni dhaifu kiasi gani mbele za watu, tutakuwa ni wadudu wadogo kiasi gani, lakini tutaiangusha milima mikubwa, na mambo mengine yote ambayo hayawezekaniki. Lakini hiyo yote. Ni mpaka tumfanye Mungu kuwa kila kitu kwetu. Kama ilivyokuwa kwa Israeli.

Isaya 41:8 “Nawe, Israeli, mtumishi wangu; Yakobo, niliyekuchagua; mzao wa Ibrahimu, rafiki yangu;”

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Ni kwanini mifugo ya Yakobo iliongezeka kwa wingi kiasi kile?

Mataifa ni nini katika Biblia?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 7 (Yeremia na Maombolezo)

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.

Rudi nyumbani

Print this post

Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji zilikuwaje?

Jibu: Katika agano la kale zilitolewa sadaka mbali mbali, na sadaka zote zilizotolewa zilikuwa ni lazima zifike madhabahuni pa Mungu, ili sadaka iitwe sadaka ni lazima ihusishe madhabahu. Isipohusisha madhabahu hiyo haiitwi tena sadaka bali mchango, au zawadi, au msaada. Lakini chochote kinachotolewa na kupelekwa kwenye madhabahu ya Mungu, hicho kinaitwa sadaka.

Sasa katika agano la kale, wana wa Israeli Bwana aliwaagiza wamtolee sadaka, kila mtu kwa hiari yake, na si kwa kulazimishwa..

Kutoka 35: 4 “Kisha Musa akanena na mkutano wote wa wana wa Israeli, akawaambia, Neno hili ndilo aliloliamuru Bwana, akisema,

5 Katwaeni kati yenu matoleo kwa Bwana; MTU AWAYE YOTE ALIYE NA MOYO WA KUPENDA, ayalete matoleo; dhahabu na fedha na shaba”

Hapo anasema Bwana anasema..“kila mwenye moyo wa kupenda” na sio kulazimishwa.. Maana yake kama mtu hajisikii kumtolea Mungu, basi halazimishwi, lakini atajipunguzia Baraka zake kutoka kwa Mungu.

Sasa katika agano la kale yalikuwepo makundi kadhaa ya sadaka, (yaani aina za sadaka watu walizokuwa wanamtolea Mungu). Zilikuwepo sadaka za Wanyama, kama vile Ng’ombe, Mbuzi, kondoo, na Njiwa, Hawa walikuwa wanaletwa Nyumbani kwa Mungu, na kuchinjwa, na kisha damu yao kutumika kufanya upatanisho, na baadhi ya viungo vya miili yao kuteketezwa juu ya madhabahu, na sehemu ya nyama iliyobakia isiyoteketezwa juu ya madhabahu, walikuwa wanapewa makuhani, pamoja na watoto wao..

Pamoja na hayo pia zilikuwepo sadaka za vyakula.. Ambapo watu walikuwa wanaleta nafaka zao kama sadaka kwa Mungu, Ndio hapo zinazaliwa sadaka za Unga na sadaka za vinywaji. Na katika makundi yote hayo ya sadaka, yote yalitolewa fungu la kumi, na malimbuko.

Sasa sadaka za unga, zilikuwa zilihusisha unga (wa ngano au shayiri) uliosagwa vizuri, na kisha kupelekwa kwenye madhabahu, huo unaweza kuwa kilo kadhaa, au au pungufu kidogo, na mtu akishaupeleka, Kuhani anachukua kiwango kidogo cha huo unga, na kuuchanganya na ubani, na kisha kuuchoma huo unga pamoja na ubani ule..Na kiwango kingine cha unga kilichobakia kisichochomwa (ambacho kinakuwa ni kingi) wanapewa makuhani, kama riziki yao.

Walawi 2:1 “Na mtu atakapomtolea Bwana matoleo ya sadaka ya unga, matoleo yake yatakuwa ya unga mwembamba; naye ataumiminia mafuta, na kutia na ubani juu yake;

2 kisha atauleta kwa wana wa Haruni, hao makuhani; naye atatwaa konzi moja katika huo unga mwembamba, na katika mafuta yake, na huo ubani wote; kisha kuhani atauteketeza kuwa ndio ukumbusho wake juu ya madhabahu, ni kafara ya kusongezwa kwa njia ya moto, ya harufu ya kupendeza kwa Bwana;

3 na huo uliosalia wa ile sadaka ya unga utakuwa ni wa Haruni na wanawe; ni kitu kitakatifu sana katika sadaka zilizosongezwa kwa Bwana kwa njia ya moto”.

Na kama mtu atapenda asilete unga, bali alete unga uliokadwa tayari na kuokwa (Yaani mkate kamili), basi yalikuwepo maagizo ya jinsi ya kuuandaa huo unga (mkate), na kuuleta madhabahuni.. kwamba huo unga uliokandwa na kuokwa haupaswi kuwekwa hamira wala asali. (Walawi 2:4-11).

Mistari mingine inayozungumzia sadaka hiyo ya unga ni pamoja na Kutoka 29:40-41, Kutoka 30:9, Kutoka 40:29, Walawi 5:13, Walawi 6:15, Walawi 9:17, Walawi 14:10.

Na pamoja na kuwepo sadaka hiyo ya unga, ilikuwepo pia sadaka ya kinywaji ambayo ilikuwa inaambatana na hii ya unga, Isipokuwa katika sadaka ya kinywaji kilichokuwa kinatolewa ni Divai, (Kwasababu ndio kinywaji kilichokuwa cha gharama na heshima, kwa enzi hizo, na kwa tamaduni za kiyahudi), Na Divai haikutumika kwa matumizi ya ulevi, wala anasa,bali kwa matumizi matakatifu. (Kutoka 29:41)

Sasa sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji (Divai) zinafananishwa na mwili na damu ya Yesu. Kristo aliutoa mwili wake na damu yake kama sadaka, kwa ajili yetu..Na Mungu aliruhusu watu wamtolee sadaka hiyo ya unga na ya kinywaji katika agano la kale, kufunua mwili wa Yesu na damu yake katika agano jipya. Na pia aliruhusu makuhani wa agano la kale washiriki sehemu ya sadaka hiyo, kufunua “ushirika wa meza ya Bwana” kwa makuhani wa agano jipya.

Mathayo 26:26 “Nao walipokuwa wakila Yesu alitwaa mkate, akabariki, akaumega, akawapa wanafunzi wake, akasema, Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu

27  Akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, Nyweni nyote katika hiki;

28  kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi”.

Kwahiyo kama vile makuhani walivyoshiriki sehemu ya unga(mkate) na sehemu ya divai iliyokuwa inaletwa madhabahuni, vivyo hivyo na sisi pia tunashiriki mwili na damu ya Yesu, ili tuwe na sehemu katika madhabahu ya Bwana. Kwasababu wote tuliompokea Yesu, tunafananishwa na makuhani wa Bwana.

Ufunuo 1:5  “tena zitokazo kwa Yesu Kristo, shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake,

6  NA KUTUFANYA KUWA UFALME, NA MAKUHANI KWA MUNGU, naye ni Baba yake; utukufu na ukuu una Yeye hata milele na milele. Amina”.

Hivyo kuna umuhimu mkubwa sana wa kuishiriki meza ya Bwana, kwa kila aliyemwamini Yesu, na kuishi katika Neno lake.

Yohana 6:53  “Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.

54  Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.

55  Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli”.

Kama hujajua namna ya kushiriki meza ya Bwana, na ungetamani kujua basi unaweza kutujuza kwenye box la maoni, chini kabisa mwa somo hili, ili tukutumie somo juu ya hilo kwa urefu.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU.

Je tunapaswa tushiriki Meza ya Bwana mara ngapi?

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

JE! KUNA UMUHIMU WOWOTE WA KULIPA ZAKA?

ALIYOKUTANA NAYO YESU, YERIKO.

Rudi nyumbani

Print this post

ITAMBUE NAFASI YA WITO WAKO.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima, karibu tujifunze maneno ya uzima, Leo tutaangazia juu wito, na jinsi unavyoweza kutofautiana kati ya mtu na mtu.

Tusome vifungu hivi,.

Mathayo 11:18 “Maana Yohana alikuja, hali wala hanywi, wakasema, Yuna pepo.

19 Mwana wa Adamu alikuja, akila na kunywa, wakasema, Mlafi huyu, na mlevi, rafiki yao watoza ushuru na wenye dhambi! Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa kazi zake”.

Kama tunavyojua Yohana mbatizaji, aliitwa kwa namna ya kitofauti sana, aliishi maisha ya kuwa mbali na watu kwa muda mrefu jangwani, na kama tunavyojua huko jangwani hakuna vyakula vizuri, au mavazi mazuri, biblia inasema chakula chake kilikuwa ni nzige, na asali  basi!, hakujua juisi ya zabibu, wala supu ya makongoro, wala kuku, wala mayai, wala yogati, wala pizza, wala pilau, bali aliishi maisha ya kawaida kabisa, ya kula vyakula vya jangwani siku zote za maisha yake, na alikuwa na Amani katika maisha yale, wala hakuwa anaona kuna ugumu wowote au uzito wowote kuishi vile.

Vivyo hivyo na mavazi yake yalikuwa ya ngozi, magumu yasiyo na mvuto ..ndio maana Bwana aliwauliza wale watu..

Luka 7:24 “… Mlitoka kwenda nyikani kutazama nini? Unyasi ukitikiswa na upepo?

25 Lakini mlitoka kwenda kuona nini? Mtu aliyevikwa mavazi mororo? Jueni, watu wenye mavazi ya utukufu, wanaokula raha, wamo katika majumba ya kifalme”.

Unaona? Lakini maisha hayo ya kuishi majangwani na ya kula mapanzi hayakuwa kanuni kwamba kila mtu ayaishi, na sio kwamba ukiyaishi wewe ndio yatakufanya uwe wa rohoni zaidi ya wengine hapana.. Tunamwona Bwana Yesu yeye alipokuja, biblia inasema alikuwa anakula na kunywa..

Yeye hakuishi jangwani kama Yohana mbatizaji, bali aliishi katikati ya watu, na alikuwa anahudhuria karamu nyingi , na sherehe mbalimbali alizoalikwa na watu wa kawaida pamoja na watu wakubwa kama vile mafarisayo na waandishi, na watoza ushuru. Kwa ufupi hakujizuia kula chochote kizuri alichokaribishwa..mpaka ikafikia hatua watu wengine wakamwona huyu mbona kama ni mlafi, na mlevi? Unaona..

Lakini alikuwa anaufahamu wito wake, na kusudi lake aliloitiwa hapa duniani, Na sote tunajua hakuna mwanadamu aliyewahi kuishi maisha makamilifu yasiyokuwa na dhambi kama Bwana Yesu.

Hata na sisi pia, wito wa Mungu unatofautiana kati ya mtu na mtu.. Lipo jambo Mungu anaweza akawa ameliweka ndani yako, na unaona kabisa ukilifanya katika hali hiyo, ndio litakupa Amani kuliko kufanya katika mazingira kama ya mtu mwingine, ukishaona hivyo wewe fanya bila kuwaangalia watu.

Kuna watu wameitwa katika hali ya uhuru, na kuna watu vilevile wameitwa katika hali ya utumwa biblia inasema hivyo..Ikiwa uliitwa kutumika ukiwa chini ya mamlaka fulani usione vibaya kuwa hivyo, mtumikie Mungu kwenye nafasi yako, kwa uaminifu, na ukalitimiza kusudi la Mungu vema tu, kama alivyofanya  Nehemia, yeye alikuwa ni mnyweshaji wa mfalme, lakini kwasababu alijua nafasi yake na cheo chake alichopewa, alikuwa chachu kubwa ya kuikarabati upya Yerusalemu.

Lakini pia kama uliitwa katika hali ya uhuru, (sio chini ya mamlaka Fulani,) na unaona vema kutumika katika hali hiyo, basi mtumikie Mungu kwa bidii katika nafasi hiyo.

1Wakorintho 7:20 “Kila mtu na akae katika hali ile ile ambayo alikuwa nayo alipoitwa.

21 Je! Uliitwa u mtumwa? USIONE NI VIBAYA lakini kama ukiweza kuwa na uhuru, afadhali kuutumia.

22 Kwa maana yeye aliyeitwa katika Bwana hali ya utumwa, ni huru wa Bwana. Vivyo hivyo yeye naye aliyeitwa hali ya uhuru, ni mtumwa wa Kristo”.

Vivyo hivyo kuna walioitwa kuoa/kuolewa, na wengine kutokuoa, au kutokuolewa.. Ikiwa wewe huoni shida yoyote kuishi maisha ya kuwa na mke au mume, endelea na wito wako huo huo, mtumikie Mungu, sio lazima uishi kama yule au wale.. Lakini pia ikiwa umeitwa  katika kuoa, au kuoelewa, vilevile umtumikie Mungu kwa uaminifu katika nafasi hiyo.. usione ni vibaya.

1Wakorintho 7:27 “Je! Umefungwa kwa mke? Usitake kufunguliwa. Umefunguliwa? Usitafute mke.

28 Lakini, kama ukioa, huna hatia; wala mwanamwali akiolewa, hana hatia; lakini watu kama hao watakuwa na dhiki katika mwili nami nataka kuwazuilia hayo.

Mathayo 19:11 “Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa.

12 Maana wako matowashi waliozaliwa hali hiyo toka matumboni mwa mama zao; tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi; tena wako matowashi waliojifanya kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na alipokee”.

Hivyo wito unatofautiana kati yetu sisi kwa sisi, usijilaumu sana kwanini haupo kama yule, au kama Fulani, au kwanini haufanani na Yohana mbatizaji, Zaidi tumia muda wako kutafuta mapenzi ya Mungu Katika nafasi uliyopo kama alivyofanya Nehemia, kisha uujenge ufalme wa Mungu. Kuna wengine wamebarikiwa ujuzi, kuna wengine mali, kuna wengine ulezi, kuna wengine karama n.k. Hakuna kiungo cha Kristo kinachoweza kukosa kabisa nafasi yake katika kanisa, ikiwa kitamaanisha kweli kumtumikia Mungu.

Hivyo tuanze sasa kujua nafasi za wito wetu, na tuzitumie, kuujenga ufalme wa mbinguni.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KUNA MAJIRA MUNGU ATAIVURUGA MIPANGO YETU.

KUNA UMUHIMU WA KUWA MTU WA KURIDHIKA.

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

KWANINI MIMI?

UNYAKUO.

Rudi nyumbani

Print this post

WAOMBEENI WANAOWAUDHI.

Bwana Yesu alisema..

Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;

44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki…..

48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.

Kumuombea anayekuudhi sio kitu kirahisi hata kidogo, huo ndio ukweli..afadhali ungeambiwa achana naye tu yapite, lakini unaagizwa  umuombee, si jambo jepesi, Lakini hivyo ndivyo vipimo vya ukamilifu wa mtu kwa Mungu. Hakuna njia ya mkato.

Pale unapoona jirani yako anakuzungumzia vibaya, mpaka anakuharibia  pengine siku yako, badala umchukie na kumwekea vinyongo, au umzungumze na wewe vibaya , unaambiwa na Yesu umuombee.. Ukishindwa kufanya hivyo, basi wewe bado hujawa na tabia kama za Mungu ndani yako, bado hujawa mkamilifu kulingana na maandiko.

Bwana Yesu alitoa, mfano hai akasema, hata Mungu mwenyewe, huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua yake waovu na wema..Kiasi kwamba mchawi anatoka kuwaloga watu usiku, na kuwasababishia matatizo, lakini asubuhi anaamka na mvua kwenye shamba lake, na linastawi vizuri yake , mpaka anavuna, na kuuza, na kupata chakula kwa ajili yake na watoto wake na cha akiba.

Jambazi, anatoka kuiba usiku na kuharibu, na akiamka asubuhi anakutana na jua kama wewe unavyoliona, sio kwamba Mungu anapendezwa na tabia zake, la, lakini anaonyesha rehema zake kwao pengine siku moja watatubu, na kuacha njia zao.

Na sisi pia kuna wakati tulishawahi kuwa waovu mbele za Mungu, kiasi kwamba ilikuwa ni haki ya Mungu atulipizie kisasi tuondoke chini ya jua, lakini mara nyingi tumeona hakufanya chochote, mpaka sasa tumetubu tumeokolewa, na tunamtumikia. Laiti kama asingekuwa mvumilivu kwetu, leo hii tungekuwa kwenye moto wa jehanumu.

Huo ndio ukamilifu wa Mungu, na yeye pia akatupa agizo hilo hilo kwamba tuwaombee wale wanaotuudhi, wale ambao tunawaona ni maadui zetu haswa haswa, tuwaombee, tusijifanye sisi ni washupavu sana, tunajua kupambana, tunajua kusimamia haki zetu, tukadhani kuwa mawazo ya Mungu ni kama ya kwetu, badala ya kuwaombea mema, tukaanza kuwaombea vifo, kuwaombea njaa, kuwaombea wasifanikiwe..n.k.

Mungu atahuzunishwa na sisi, na kutuona kama ni wachanga ya njia zake.

Kumbuka hatujaitwa kuwaiga wanadamu, bali tumeitwa kumuiga Mungu. Kama vile Yesu alivyosema,…

Yohana 5:19 “Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda; kwa maana yote ayatendayo yeye, ndiyo ayatendayo Mwana vile vile”.

Haijalishi wanadamu wote watasema, wapige maadui zako. Lakini maneno ya Yesu ni tuwaombee. Hata kama yataonekana ni maombi magumu kwetu, lakini kwa Mungu ni manukato. Tujizoeshe kuwa watu na namna hiyo kila siku. Ndipo tutakapoona Mungu akituzidishia na sisi rehema zake kila siku.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Rudi nyumbani

Print this post

“Kinga kilichotolewa motoni “Kinafunua nini kibiblia?

SWALI: Kwanini Yoshua aliambiwa yeye ni kinga kilichotolewa motoni? Hichi kinga kilichotolewa motoni kina maana gani kibiblia?


JIBU: Kinga ni kama kijiti, hivyo inaposema kinga cha moto inamaanisha kijiti cha moto. Neno hilo utaliona sehemu kadha wa kadha katika biblia, na hususani wakati ule, Yoshua kuhani mkuu alipokuwa amesimama mbele za Mungu, na shetani naye amesimama pembeni yake kumshitaki, Lakini yule malaika aliyekuwa amesimama pembeni yake, aliyazungumza maneno haya;

Zekaria 3:1 “Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye.
2 Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; JE! HIKI SI KINGA KILICHOTOLEWA MOTONI?
3 Basi, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu sana, naye alikuwa akisimama mbele ya malaika.
4 Naye huyo akajibu, akawaambia wale waliosimama mbele yake, akisema, Mvueni nguo hizi zenye uchafu. Kisha akamwambia yeye, Tazama, nimekuondolea uovu wako, nami nitakuvika mavazi ya thamani nyingi”.

Sasa ukisoma kwa ukaribu maneno hayo, utaona sio Yoshua anaambiwa yeye ni kinga kilichotolewa motoni, bali ni Yerusalemu ndio inayofananishwa na kinga kilichotolewa motoni.

Kama tunavyojua kipande chochote cha mbao kikiingia kwenye moto, huwa hakina namna ni lazima kiteketee tu, tofauti na vitu vingine kama chuma. Sasa kama kimetolewa motoni, inamaanisha kimenyakuliwa kutoka katika uharibifu uliokuwa unakila.

Hivyo Malaika wa Mungu alikuwa anamwambia shetani, kuwa Yerusalemu, ambayo Mungu alikuwa ameiteketeza ili ipotee kabisa milele, sasa ameihurumia na kuiokoa tena imsimamishie nyumba, na Yoshua huyu aliyesimama hapa ndiye atakuwa kuhani mkuu katika nyumba itakayojengwa Yerusalemu.

Israeli tangu ilipoasi Mungu  aliiweka katika  moto wa mfalme wa Babeli Nebukadreza, ili aingamize kabisa, Na ndio maana ukisoma Yeremia 29: 22 Utaona Mungu anatoa unabii kwa wale manabii wa uongo waliokuwa wanaitabiria Israeli habari za amani wakati hakuna amani, na kuwaambia kwamba huyu mfalme wa Babeli ndio atakuwa wa kwanza kuwaoka, hawa manabii katika moto.

Yeremia 29:22 “Tena katika habari zao laana itatumiwa na wafungwa wote wa Yuda, walioko Babeli, kusema, Bwana akufanye uwe kama Sedekia, na kama Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwaoka motoni”

Neno hilo utaliona tena, sehemu nyingine  kwenye biblia ambapo Mungu aliiadhibu Israeli kwa mapigo ya kila namna, mfano wa Sodoma na Gomora, aliitia katika moto wa uharibifu, lakini baadhi yao aliowapa neema ya kuokoka hawakutambua kuwa wamenyakuliwa katika moto, kama vinga vilivyokuwa vinateketea, bali waliendelea kutenda maovu..

Amosi 4:7 “Tena nimeizuia mvua msiipate, ilipobaki miezi mitatu kabla ya mavuno; nami nimenyesha mvua juu ya mji mmoja, nikaizuia mvua isinyeshe juu ya mji mwingine; sehemu moja ilipata mvua, na sehemu isiyopata mvua ilikatika.
8 Basi kutoka miji miwili mitatu walitanga-tanga kuendea mji mwingine wapate kunywa maji, wasipate ya kuwatosha; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
9 Nami nimewapiga kwa ukavu na koga; wingi wa bustani zenu na mashamba yenu ya mizabibu, na mitini yenu na mizeituni yenu imeliwa na tunutu; Lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
10 Nimewapelekea tauni, kama tauni ya Misri; vijana wenu nimewaua kwa upanga, na farasi wenu nimewachukulia mbali; nami nimeupandisha uvundo wa matuo yenu na kuuingiza katika mianzi ya pua zenu; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.

11 Baadhi yenu nimewaangamiza, kama hapo MUNGU ALIPOIANGAMIZA SODOMA NA GOMORA, NANYI MKAWA KAMA KINGA KILICHONYAKULIWA MOTONI; LAKINI HAMKUNIRUDIA MIMI, ASEMA BWANA.

Soma pia Isaya 7:4

Hata sasa, dunia inapopitia katika majanga mengi ya maafa, lakini tukijiangalia sisi bado tupo hai, tujue kuwa ni Mungu anatutaka sisi tutubu, kama sio kwenda kumtumikia kama iliyokuwa kwa Yoshua.

Tunapoepushwa na matetemeko ya ardhi, vimbunga, magonjwa makali ya kuua kama hili la CORONA, tujue kuwa ni vinga vilivyo nyakuliwa motoni, tunapaswa tujue huu ni wakati wa kutubu na kumrudia Mungu wetu kwasababu ulimwengu upo motoni.

Lakini tukipuuzia tukajiona kama sisi ni wa kipekee sana, tujue kuwa tutakutana na adhabu kali Zaidi ya hizi tulizonazo sasa hivi. Mungu ni moto ulao.

Tuyatambue makosa yetu tumrudie Mungu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

Nini maana ya uvuvio?.

Kuwatema farasi, maana yake ni nini?

KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Tumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii”?

Jibu: Tusome..

Waefeso 2: 20 “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni”.

Katika mstari huo yapo mambo makuu mawili ya kuzingatia kwa makini.

1) Msingi na 2) Mitume na manabii

Tukianza na Msingi.

Hapo anasema mmejengwa juu ya “Msingi” na si “misingi”. Maana yake ni msingi mmoja tu, na si mingi.. Na anaendelea kwa kusema..”mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii”..na sio “mmejengwa juu ya mitume na manabii”.. Maana yake ni kwamba msingi waliokuwa nao mitume na manabii ndio sisi pia tunajengwa juu ya huo.. Mtu akisema “natembea juu ya misingi na kanuni za Baba yangu au babu yangu, hajamaanisha anatembea juu ya baba yake”..Bali juu ya kanuni na taratibu alizorithishwa na Baba yake, ambazo hata baba yake alikuwa anazifuata na kuziishi….Kadhalika na hapo, Neno la Mungu linasema, mmejengwa juu ya msingi wa Mitume na manabii, maana ya kuna msingi ambao Mitume na manabii walikuwa wanaiishi na kuifuata, na hatimaye wakairithisha kwa kizazi kinachofuata. Kwa misingi hiyo ndio sisi tunajengwa.

Sasa kabla ya kujua vizuri huo msingi ni nini, hebu tujue kwanza hawa Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapo ni wakina nani?..

Tofauti na inavyodhaniwa kwamba Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapo, ni kundi la manabii na Mitume wanaozuka leo… unakuta inatokea mtu fulani mahali fulani anayejiita Mtume au Nabii, anaanza kujigamba kwamba karama yake ndio karama kuu yakulijenga kanisa. Na kwamba yeye ndio msingi na kanisa, limejengwa juu yake. Jambo ambalo ni uongo, tena kwa asilimia zote.

 Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapo ni Manabii wote wa agano la kale, na Mitume wa kanisa la kwanza wa agano jipya.  Hao Msingi waliouweka na kuufuata ndio msingi sisi tunaojengwa juu ya huo na huo si mwingine zaidi ya  biblia takatifu, ambapo ndio tunanukuu maneno kutoka huko.  Ndio maana leo hii, msingi ni biblia takatifu, Maneno yaliyoandikwa na Mitume kama Paulo, Petro, Yohana, Yakobo n.k hayo ndio msingi wetu leo hii, ndio maana leo hatunukuu Neno la Nabii yeyote aliyepo leo, wala Mtume  yeyote aliyepo leo na kulihubiri hilo, kana kama ni Neno la Mungu, badala yake tunanukuu maneno yaliyoandikwa na Mtume Paulo, au Nabii Isaya, au Nabii Yoeli n.k..Hao ndio mitume na manabii ambao tumejengwa juu ya msingi wao.

Kwahiyo mtu yeyote anayejiita mtume au nabii au mwalimu au muinjilisti, na anasema na kujivuna kwamba kanisa limejengwa juu yake, na kujivuna kwamba yeye ndio nguzo kuu, au karama yake ndio karama kuu…kwa kufuatia huo mstari, mtu huyo anadanganya aidha kwa kujua au kwa kutokujua.

Msingi wetu sisi ni biblia takatifu, ambayo imeandikwa na mitume wa Yesu na manabii wa agano la kale, hao ndio Mababa. Na kiini cha biblia takatifu ni YESU KRISTO. Vitabu vyote katika biblia vimebeba habari au unabii wa Yesu Kristo, hakuna kitabu hata kimoja kisichobeba ufunuo wa Yesu Kristo ndani ya biblia. Kwasababu yeye ndio Mungu mwenyewe katika Mwili. (1Timotheo 3:16).

1Wakoritho 3:11 “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo”.

Je umemwamini Yesu?, umepokea Roho Mtakatifu?..Kama bado mwamini leo na kumkabidhi maisha yako, naye atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu (Matendo 2:38)

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Je! Imani ya mitume ipo katika maandiko?

Mtume Paulo alikuwa na maana gani kusema katika 1Wakorintho 15:31″…NIKAKUFA KILA SIKU?

TUSIWE WATU WA KUPUNGUKIWA AKILI.

JINSI PAULO ALIVYOPAMBANA NA UJINGA WA ROHONI.

POPOBAWA NI KWELI YUPO?

Rudi nyumbani

Print this post

MZUNGUKO WAKO NI UPI?

Ukichunguza utaona Mungu kaweka vitu vingi vya asili katika mzunguko wake. Na kulikuwa na sababu maalumu wa yeye kufanya hivyo..

Mhubiri 1:6 “Upepo huvuma kusi, hugeuka kuwa kaskazi; hugeuka daima katika mwendo wake, na upepo huyarudia mazunguko yake.

7 Mito yote huingia baharini, walakini bahari haijai; HUKO IENDAKO MITO, NDIKO IRUDIKO TENA”.

Hakushindwa kuufanya upepo upotelee tu huko hewani, au maji yapotelee tu ardhini, lakini ameamua kuyaweka katika mzunguko, kiasi kwamba hayo maji unayoyamwaga sasa hivi kwenye sinki, kuna wakati Fulani yatakurudia wewe wewe na utayatumia tena.

Hiyo ni kufunua kuwa kuna mambo mengi ya rohoni yapo kwenye mzunguko wake, na tusipoitambua mizunguko hiyo, yatatupita mengi kama sio kupata hasara nyingi sana.

Lolote unalolifanya sasa hivi, liwe ni jema au baya, moja kwa moja linaingizwa katika mzunguko huu wa rohoni usioonekana. Kama ni baya litaondoka lakini siku moja litakurudia tu.. haijalishi litachukua umbile gani.

Kama ni jema vilevile litakurudia tu, haijalishi litachukua umbile gani baadaye.. Hivyo ni vizuri ukajua wewe upo katika mzunguko upi, Na ndio maana Bwana Yesu alisisitiza sana maneno haya.

Mathayo 7:12 “Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; …”.

Luka 6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”.

Ufunuo 13: 10 “Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga…”

Hizi ndio kanuni za asili ambazo mtu yeyote akizitumia hata kama sio mkristo, zitamletea majibu tu. Na ndio maana watu wengi wanashangaa kwanini mataifa yaliyoendelea yanazidi kutajirika, japokuwa hayamchi Mungu.

Ukiangalia utagundua kuwa  yanatoa misaada mingi  kila mwaka kwa mataifa maskini, na ndio maana yanazidishiwa.

Vilevile ukimpa Mungu, Ni kama vile umeingizwa kwenye mfumo wa mzunguko wa Baraka zake rohoni, pengine utaona kama umepoteza, lakini siku isiyokuwa na jina kitakurudia tu, kikiwa kimeshindiliwa na kusukwa sukwa, na kumwagika, kinaweza kisirudi kwa namna ile ile, lakini kitarudi kwa thamani ile ile tena mara dufu.

Mithali 11:25 “Nafsi ya mtu mkarimu itawandishwa; Anyweshaye atanyweshwa mwenyewe”.

Lakini ukiwa mwovu, unaiba, unawarusha watu, unadhulumu haki za wengine,  mchoyo, mbinafsi, unawachonganisha wengine, unaua, moja kwa moja unaingia katika mzunguko huo wa laana za waovu, na mwisho wa siku malipo yake yatakurudia kichwani pako ukiwa hapa hapa duniani, tena kwa kusukwa-sukwa na kuzidishiwa na kumwagika.

Mithali 11:31 “Tazama, mwenye haki atalipwa duniani; Basi mwovu na mkosaji si mara nyingi Zaidi”?

Kwa maneno hayo machache Mungu atufumbue macho yetu tuelewe tupo katika mzunguko upi. Ili tuishi maisha ya mafanikio hapa duniani.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

HALI ZETU JINSI ZINAVYOWEZA KUATHIRI UTOAJI WETU.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Neno Bildi linamaanisha nini kwenye biblia(Matendo 27:28) ?

Je tunapaswa tushiriki Meza ya Bwana mara ngapi?

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

JE UPENDO WAKO UMEPOA?

Rudi nyumbani

Print this post

NI NINI KITAKACHOTUFANYA TUPIGE MBIO BILA KUPUNGUZA MWENDO?

Paulo akijua kuwa anakaribia ukingoni kabisa mwa safari yake, hakujali taarifa yoyote mbaya iliyoletwa mbele yake, utaona yeye mwenyewe anasema, mji kwa mji Roho Mtakatifu alimshuhudia kuwa vifungo na dhiki nyingi vinamngojea kule Yerusalemu alipokusudia kwenda, lakini bado alisema, siachi kupiga mbio nimalize mwendo wangu.

Matendo20:23 “isipokuwa Roho Mtakatifu mji kwa mji hunishuhudia akisema, ya kwamba vifungo na dhiki vyaningoja.

24 Lakini siyahesabu maisha yangu kuwa kitu cha thamani kwangu kama kuumaliza mwendo wangu na huduma ile niliyopokea kwa Bwana Yesu, kuishuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu”.

Kama hilo halitoshi alipofika Kaisaria, karibu kidogo na Yerusalemu, Nabii mmoja aliyeitwa Agabo, alitokea na kumtolea unabii kwa uweza wa Roho Mtakatifu akisema, Paulo atakwenda kufungwa, na kupata dhiki, hivyo asiende, Yerusalemu.

Lakini hilo nalo halikumfanya Paulo, aache kwenda Yerusalemu, badala yake aliwaambia;

Matendo 21:13 “Ndipo Paulo alipojibu, Mnafanya nini, kulia na kunivunja moyo? Kwa maana mimi, licha ya kufungwa, ni tayari hata kuuawa katika Yerusalemu kwa ajili ya jina lake Bwana Yesu”.

Unaona, alifikia hatua, mawazo yake yote yalikuwa  ni kuimalizia kazi yake kwa kishindo, kiasi cha kutojali dhiki zozote atakazokumbana nazo mbele yake

Sasa usifikirie ni jambo rahisi kuchukua maamuzi hayo kama asingekuwa ni mtu anayefahamu ni nini anakitafuta.. Paulo alikuwa ni mtu mwenye malengo, ni mtu aliyekuwa anatazama vya mbali sana, alijua kupiga mbio huko kuna tuzo Fulani kubwa mbeleni, hivyo ni sharti aishindanie kwa nguvu ili asiikose.

1Wakorintho 9:24 “Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.
25 Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika.
26 Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;
27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”

Unaona alijua sikuzote mkimbiaji ambaye anajua lengo la kukimbia kwake ni nini huwa hakimbii kwa kuubembeleza mwili, bali anakimbia huku mawazo yake yakuwa kweney tuzo iliyowekwa mbele yake, hilo ndilo linalomfanya asitembee tembee njiani, asikubali kuusikiliza mwili, kwamba umechoka, hivyo apunguze mwendo.

Hali kadhalika mkimbiaji mzuri kwa namna ya kawaida, anapokaribia mzunguko wake wa mwisho ndio huwa anaongeza mwendo Zaidi, na ndicho alichokifanya Paulo.

Embu tumtazame mtu mwingine wa mwisho ambaye safari yake sikuzote ilikuwa ni ya mwendo tu, mtu ambaye yeye hakujali kikwazo chochote alipokuwa anamalizia mwendo wake hapa duniani. Na huyo si mwingine Zaidi ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Biblia inatuambia wakati wa kupaa kwake ulipokaribia, “ALIUKAZA” uso wake kwenda Yerusalemu.

Luka 9:51 “Ikawa, siku za kupaa kwake zilipokuwa karibu kutimia, yeye aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu;
52 akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.
53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu”.

Kuukaza uso maana yake, ni kutokuwa tayari kuambiwa chochote, au kushauriwa chochote au kukwamishwa na chochote mpaka utimize malengo yako uliyoyakusudia mbele yako. Ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu, wakati ambapo anajua amebakiwa na kipindi kifupi sana, amalize mwendo wake pale Yerusalemu, huku akijua moyoni mwake kuwa Mateso makali anakwenda kukumbana nayo, kusulibiwa, yeye hakujali chochote, Zaidi ndio alilazimisha kwenda huko huko.

Yohana 10:7 Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, Twendeni Uyahudi tena.
8 Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, juzijuzi tu Wayahudi walikuwa wakitafuta kukupiga kwa mawe, nawe unakwenda huko tena?

Je na sisi kipindi hichi cha kufunga majira, bado tunapiga mbio au tumepunguza mwendo wetu wa Imani ? Pengine tumeacha kukimbia kwasababu hatujajua malengo yetu ni nini? tunakumbana na milima mrefu, tunakata tamaa, lakini pia tunapaswa tujue jambo moja ili uitwe mlima ni lazima utakuwa na upande wa pili wa mteremko pia.

Ni heri maisha mafupi ya hapo duniani, tuyaishie kupanda mlima, lakini tutakapofika kule ng’ambo kwenye umilele tuyaishie kwenye mteremko,..

Hizi ndizo nyakati za kuzidisha mwendo, kutojali vitisho vyovyote vya kiimani, vitisho  vya ndugu, au rafiki, au majirani, kwasababu kama unyakuo hautatukuta, basi pia siku zetu za kuishi duniani zinapungua siku baada ya siku.

Hivyo tupige mbio tukijua kuwa zipo tuzo mbele yetu zinatungojea, lakini tukiwa walegevu hatutazipata.

2Timotheo 2:5 “Hata mtu akishindana katika machezo hapewi taji, asiposhindana kwa halali”.

Shalom

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

DAMU YA ZAKARI BIN BARAKIA.

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

NITAFANYA YERUSALEMU KUWA JIWE LA KUWALEMEA .

JINSI PAULO ALIVYOPAMBANA NA UJINGA WA ROHONI.

Nini maana ya neno ‘Kuabiri’ kama linavyotumika katika  biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

ELIMA MCHAWI, ANAFANYA KAZI HADI SASA.

Sikuzote roho haiji hivi hivi tu, bila kuwa na chanzo Fulani, na chanzo hicho kinaweza kuwa mtu, au kitu au sehemu, Sasa pale yule mtu anapoondoka, huwa anaacha tabia yake Fulani inayoendelea na tabia hiyo ikishakita mizizi vizuri ndio inaitwa roho,..

Kwamfano kwenye biblia utamwona mwanamke anaitwa Yezebeli, huyu mwanamke alikuwa ni mchawi, na mzinzi, na tabia zake tunazijua vizuri kwenye biblia, jinsi alivyoiharibu Israeli na kuigeuzwa kuwa nchi ya kichawi. Lakini tunasoma mara baada ya kufa kwake, roho yake iliendelea kutembea duniani, na ndio maana miaka mingi baadaye utaona Bwana Yesu anamzungumzia tena habari zake kana kwamba bado yupo duniani, katika kitabu cha Ufunuo,

Ufunuo 2:19 “Nayajua matendo yako na upendo na imani na huduma na subira yako; tena kwamba matendo yako ya mwisho yamezidi yale ya kwanza.
20 Lakini nina neno juu yako, ya kwamba wamridhia yule mwanamke Yezebeli, yeye ajiitaye nabii na kuwafundisha watumishi wangu na kuwapoteza, ili wazini na kula vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu”

Utamwona pia Eliya, pindi alipoondoka roho yake ilianza kutembea tena wakati baada ya wakati, Kumbuka hawi Eliya mwenyewe kama Eliya, Au Yezebeli kama Yezebeli, bali ile tabia  ya rohoni iliyokuwa juu ya Eliya, ndiyo inayotembea juu ya watu kadha wa kadha, Roho hiyo ilikuja juu ya Elisha, baadaye Yohana Mbatizaji n.k. na itaendelea kutembea hadi wakati wa nyakati za mwisho kabisa.(Malaki 4:5)

Halikadhali Na Bwana wetu Yesu Kristo, yeye alitembea hapa duniani, kwa miaka 33 na nusu, lakini alipoondoka, hakuondoka hivi hii ilikuwa ni sharti aichalie Roho yake katikati yetu, na ndio Roho Mtakatifu tuliye naye sasa. Kiasi kwamba mtu akiyaamini maneno yote ya Bwana Yesu moja kwa moja anampokea Roho wake ambaye atamsaidia aisha maisha kama ya Yesu.

Sasa tukishaweka msingi kama huo, tuende moja kwa moja katika somo letu la leo ambalo linamzungumzia yule Elima mchawi aliyekutana na Paulo na Barnaba  pindi walipokuwa wanahubiri injili huko Pafo, tusome.

Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake Bar-Yesu;
7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali Sergio Paulo, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu.
8 Lakini Elima, yule mchawi (maana ndiyo tafsiri ya jina lake), akashindana nao, akitaka kumtia yule liwali moyo wa kuiacha ile imani.
9 Lakini Sauli, ambaye ndiye Paulo, akijaa Roho Mtakatifu, akamkazia macho,
10 akasema, Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, adui wa haki yote, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka?
11 Basi, angalia, mkono wa Bwana u juu yako, nawe utakuwa kipofu, usilione jua kwa muda. Mara kiwi kikamwangukia na giza, akazunguka-zunguka na kumtafuta mtu wa kumshika mkono na kumwongoza.
12 Ndipo yule liwali, alipoyaona yaliyotendeka, akaamini, akiyastaajabia mafundisho ya Bwana”`.

Huyu mtu alikuwa ni mchawi, na wakati huo huo ni nabii wa Uongo. Kazi yake na lengo lake, lilikuwa ni kuwafanya watu wasiiamini njia ya wokovu, pale tu wanapokutana na injili ya kweli ya msalaba. Ni mchawi aliyebobea kwenye kitendo cha kupinga tu, na kushawishi watu kuiacha imani, na ndio maana mtume Paulo alimwambia “Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka?”

Kwa kazi yake hii, mpaka akawa ameshawafikia kabisa na watu wakubwa na wenye akili kama huyu Sergio Paulo, ikiwa na maana kuwa  huku chini tayari alishaburuza.

Kama tunavyoona hapo, Paulo alipoanza kumuhubiria huyu liwali, yeye bila kupoteza muda alianza kuwabishia wakina Paulo, na kutoa hoja zake za uongo, na pengine kumwambia yule liwali hawa watu ni waongo, wapiga dili, hakuna kitu kuokoka hapa duniani, huyo Yesu aliibiwa hajafufuka, hawa ni wapotoshaji n.k.

Lakini Paulo kulijua hilo, akamkemea saa ile ile akawa kipofu kwa muda.

Sasa huyu mtu alishakufa lakini aliiacha roho yake hapa duniani, na roho hiyo inatembea kwa kasi sana, sasa hivi duniani imewavaa watu wengi, na wenyewe hawajijui kuwa wanafanyika kuwa wachawi, pasipo wao kujijua.

Kuna watu kazi yao ni kupinga tu kila habari ya Kristo, wakiona kila mtumishi wa Mungu anahubiri, au kushuhudia, wanasema ni nabii wa uongo, wanasema ni wazinzi, wakisikia injili ya kweli inahubiriwa wanasema anapotosha,

Sasa kibiblia watu kama hao ni wachawi, hawajijui tu kama wameshafikia hiyo hatua

Katika nyakati hizi za kumalizia ni kujiangalia sana, si kila wazo la kila mtu la kulisikiliza, au kulipokea haijalishi atakuwa ni ndugu yako, au rafiki yako, au mfanyakazi mwenzako. 

Bwana Yesu alisema, angalieni jinsi msikiavyo (Luka 8:18)

Kaa mbali nao, ikiwa unaona kila wakati tu wanakosoa habari za Mungu au watumishi wa Mungu, hakuna kipengele hata kimoja watakisifia, kaa mbali nao, wanakuwekea tu moyo mgumu wa kutokuamini.

Ukikutana na watu kama hao ujue unaongea na wachawi, jiupushe nao. Leo hii duniani utakutana nao wengi sana akina Elimu, Bar Yesu. Wewe jikite katika kumtafuta Muumba wako kwa bidii, mpende Mungu wako, sikiliza na soma Neno la Mungu, achana na hao wanaoipuuzia, au kukejeli kila kitu cha ki Mungu kinachokatiza mbele yao.

Jiepushe nao.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI PAULO ALIVYOPAMBANA NA UJINGA WA ROHONI.

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Nini maana ya neno ‘Kuabiri’ kama linavyotumika katika  biblia?

ILI NIWE KIELELEZO KWA WALE WATAKAOMWAMINI BAADAYE.

KUMTUMIKIA MUNGU, KUNAWEZA KUWE KINYUME NA MATARIJIO YAKO.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni nani aliyesema “Nitume mimi”? katika (Isaya 6:8)

SWALI: Mtumishi wa Mungu! Bwana asifiwe, naomba ufafanuzi kidogo juu ya andiko hili katika Isaya 6:1-10 Ni Nani aliyesema “Nitume Mimi”?je Ni isaya au!? Na kwanini Isaya pia alitakaswa kwa kaa la moto?


JIBU:  Tusome baadhi ya vifungu hivyo;

Isaya 6: 5 “Ndipo niliposema, Ole wangu! Kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana wa majeshi.
6 Kisha mmoja wa maserafi wale akaruka akanikaribia; naye alikuwa na kaa la moto mkononi mwake, ambalo alikuwa amelitwaa kwa makoleo toka juu ya madhabahu;
7 akanigusa kinywa changu kwa kaa hilo, akaniambia, Tazama, hili limekugusa midomo yako, na uovu wako umeondolewa, na dhambi yako imefunikwa.
8 Kisha nikaisikia SAUTI YA BWANA, AKISEMA, NIMTUME NANI, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, MIMI HAPA, NITUME MIMI.
9 Naye akaniambia, Enenda, ukawaambie watu hawa, Fulizeni kusikia, lakini msifahamu; fulizeni kutazama, lakini msione.
10 Uunoneshe moyo wa watu hawa, ukayatie uzito masikio yao, ukayafumbe macho yao; wasije wakaona kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kufahamu kwa mioyo yao, na kurejea na kuponywa”.

Shalom, Unabii huo ulikuwa unamuhusu Nabii Isaya mwenyewe aliyekiandika kitabu hicho, tofauti na watu wengi wanavyodhani kuwa huyo ni Yesu ndiye aliyesema maneno hayo, nitume mimi.?

Hiyo yote ni baada ya Isaya kuijiona amesimama mbele ya kiti cha enzi cha Mungu mbinguni, na kwamba muda mfupi baadaye atahitajika kufanya mahojiano na Mungu. Hivyo kwa kulijua hilo kabla hata hajasema chochote, alijitambua hali yake ilivyo kuwa yeye ni mtu mwenye midomo michafu, akiwa na maana mwongo, msengenyaji, mtukanaji n.k. Jambo ambalo halikuwa kuwa midomoni mwa Yesu, tangu anazaliwa.

Hivyoo akaomba kwanza tiba, asafishwe kinywa chake, kabla ya kuzungumza na Mungu,  ndipo hapo utaona huyo kerubi akichukua kaa la moto kutoka katika madhabahu ya Mungu kwa koleo.. Sasa zingatia hilo neno madhabahu, kaa lile halikutolewa sehemu nyingine yoyote Zaidi ya madhabahuni pa Mungu. Na pia hakupewa kipelekewa kitu kizuri mdomoni labda tuseme embe au ndizi, au tango kimponye badala yake alipelekewa kaa la moto.

Na kama tunavyofahamu moto kazi yake ni kuunguza, tena, mbaya Zaidi pale unapokutana na mdomo, jaribu kutengeza picha kaa jekundu linakuja kugusana na midomo yako, mshituko na maumivu utakayosikia hapo yatakuwa ya namna gani, ni heri ungelikanyaga kwasababu mguu kidogo ni mgumu, kuliko kukutana na ulimi.

Lakini ndiyo njia ambayo Mungu aliichagua kumponya Isaya na midomo yake michafu.

Hata leo hii, ili Mungu aweze kutuponya na midomo ya usengenyaji, uongo, fitina, kiburi, ya faraka, n.k. Ni lazima tukubali kaa la Mungu lipitishwe vinywani mwetu.

Na kaa hilo halitoki sehemu nyingine isipokuwa madhabahuni pa pake, ikiwa hatutaki kukemewa dhambi zetu, hatutaki kukaripiwa, hatutaki kuonywa kwa mafundisho sahihi ya Neno la Mungu, hatutaki kuhubiriwa maneno magumu yanayochomo mioyo yetu, ili tubadilike, kamwe, tusitegemee kama usengenyaji utaondoka vinywani mwetu.

Kama tutapenda wakati wote injili ya kupiga adui zetu, na injili za mafanikio, hatutaki kukemewa dhambi zetu, na kuelezwa uhalisia wa ziwa la moto  kamwe vinywa vyetu haziwezi kuponywa.

Hivyo tukubali kukaripiwa na Mungu, tukubali kukemewa na yeye, kwasababu kwa njia hiyo ndio kaichagua ili kutuponya sisi, hakuna short-cut, Mungu anatujua vizuri sisi wanadamu, wakati mwingine tutahitaji moto ili tuponywe.

Ufunuo 3:19 “Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu”

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?

KWANINI MIMI?

Nini maana ya uvuvio?.

UFUNUO: Mlango wa 15

Rudi nyumbani

Print this post