Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?

Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?

SWALI: Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “je! Wana wenu huwatoa pepo kwa uweza wa nani?” pale Mafarisayo walipomwambia kuwa yeye anatoa pepo kwa Beelzebuli mkuu wa pepo?


JIBU: Tusome kuanzia juu kidogo habari yenyewe,

Mathayo 12:24 “Lakini Mafarisayo waliposikia, walisema, Huyu hatoi pepo, ila kwa Beelzebuli mkuu wa pepo.

25 Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama.

26 Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika juu ya nafsi yake; basi ufalme wake utasimamaje?

27 Na mimi nikitoa pepo kwa Beelzebuli, JE! WANA WENU HUWATOA KWA NANI? KWA SABABU HIYO HAO NDIO WATAKAOWAHUKUMU.

28 Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia”.

Tukumbuke kuwa neema ya Mungu ya uponyaji ilikuwepo tangu zamani za agano la lake, isipokuwa tu haikuwa imefunuliwa katika utimilifu wote kama ilivyokuwa kwetu sisi wa agano jipya kwa kupitia Yesu Kristo mwokozi wetu. Utaona kuna wakati Mungu alikuwa anawaponya wayahudi pale walipokuwa wanamwomba, japo halikuwa jambo la papo kwa papo kama alivyokuja kufanywa na Bwana Yesu mwenyewe, mti wa uzima.

Kwa mfano ukisoma Yohana 5, utaona kulikuwa na birika moja mashuhuri lililoitwa Bethzatha huko Yerusalemu, ambapo kuna wakati Mungu analikuwa anamtuma malaika wake, kuyatibua maji kisha yule mtu wa kwanza kutumbukia alikuwa anaponywa ugonjwa wake saa ile ile .Haijalishi alikuwa anasumbuliwa na vifungo vya magonjwa au mapepo ya udhaifu mengi kiasi gani,  ilikuwa akiingia tu mule ni lazima atoke mzima, na ndio maana utaona yule mtu ambaye alikuwa anasumbuliwa na ule ugonjwa wa udhaifu kwa muda wa miaka 38, (na bila shaka lilikuwa ni pepo la udhaifu)? Bwana Yesu alimfungua badala yake, Utauliza tumejuaje alikuwa na pepo la udhaifu? Ni kwasababu mwishoni kabisa Bwana Yesu alimwambia asifanye dhambi tena yasiye yakamkuta yaliyo mabaya zaidi ya yale aliyokuwa nayo..Kumbuka hilo ndio lile Yesu alilolisema katika Luka 11:24 kwa habari ya mapepo, ambayo hayo yana tabia ya kufanya hali ya mtu kuwa mbaya zaidi pale yanaporudi na kukuta nyumba yao imefagaliwa.

Kwahiyo ni wazi kuwa mtu Yule alikuwa na mapepo ya udhaifu, na kwamba kama angeingia tu kwenye yale maji, basi mapepo hayo yangemwondoka. Hivyo huo ni mfano tu mmojawapo wa Mungu alioutumia kuwafungua wayahudi, zipo njia nyingine pia walizomwombea Mungu, na Mungu akawasikia na kuponywa hata na mapepo. Hivyo jambo la kutoa pepo lilikuwa linafanywa na wayahudi hata kabla ya kuja kwa Bwana Yesu, utalithibitisha hilo kwa wale wayahudi wapunga pepo, (Matendo 19:13), ambao walikurupuka tu na wao wakajaribu kulitaja jina la Yesu, bila kujua linahitaji mamlaka ili kulitaja. Lakini wao wakajaribu kufanya kwa njia zao, na huku matendo yao maovu, yakawakuta yaliyowakuta.

Lakini sasa tukirudi kwenye ile habari, tunaona walipokuja kwa Yesu na kuona mambo mapya yanafanyika, yaani kitendo cha Neno moja tu, mapepo yanatoka, magonjwa yanatoweka, wafu wanafufuliwa, tofauti na wao walivyokuwa wanaomba, au wanafanya, wakahitimisha kuwa huyu atakuwa anatumia nguvu za giza. Na ndio hapo Yesu akawauliza swali tu la kufikirikika, ikiwa mnasema mimi ninatoa pepo kwa beelzebuli, Je! Hao wana wenu (wanafunzi wenu), huwatoa kwa nani?, wanapoingia katika lile birika la Bethzatha na kufunguliwa ni kwa uweza wa pepo gani? Wanapomwomba Mungu wakati mwingine juu ya mapepo na mapepo yanawatoka, je! Ni kwa uwezo wa pepo wa namna gani?  Lakini Kama mnaamini ni kwa msaada wa Mungu wa Ibrahimu wanafanya hivyo na sio mapepo, kwanini mnahitimisha kuwa na mimi ninatoa pepo kwa uwezo wa mashetani?. Kumbukeni hao ndio watakaowahukumu.

Unaona? Nasi tunapaswa tuwe makini, palipo na nguvu za Mungu za kweli zinawaponya watu, hatupaswi kuhitimishi na kusema ule ni uchawi, hiyo ni dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu, ambayo haiwezekaniki kusameheka, sio kila mtumishi unayemwona ni mchawi, hivyo tuchunge vinywa vyetu. Tuzungumze tu pale ambapo tumethibitisha kuwa hizi ni nguvu za giza, lakini sio kuhitimisha kila mahali unapoona nguvu za Mungu zinadhihirika kuwa ni nguvu za giza. Hapo tutakuwa tumejiweka vitanzini wenyewe.

Bwana atusaidie.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KUNA UMUHIMU WA KUWA MTU WA KURIDHIKA.

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

UTENDAJI KAZI WA MPINGA-KRISTO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments