Title June 2018

Ni nani anayetawala dunia kati ya Mungu na shetani?

Swali linaendelea….Na kama ni Mungu anayetawala kwa nini kuna matukio ya kutisha kama ajali mbaya za magari,ndege,mafuriko kama ya Japan kama Mungu ndiye anayetawala kwanini hayazuii anaacha yanaua watu??? Na ukisoma Mathayo 4:1 na kuendelea, shetani anamwambia Yesu dunia ni Mali yake, nataka kufahamu pia je! Kuna tofauti gani kati ya dunia na ulimwengu nisaidie?
 
JIBU: Dunia yote ni ya Mungu ukisoma;
 
Zaburi 24:1 ” Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana, Dunia na wote wakaao ndani yake.
2 Maana ameiweka misingi yake juu ya bahari, Na juu ya mito ya maji aliithibitisha. “
 
Na pia Bwana Yesu Kristo baada ya kufufuka kwake aliwaambia wanafunzi wake maneno haya; 
 
Mathayo 28:18″Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. “
 
Kwahiyo kwa maandiko hayo tunaona kabisa kuwa dunia yote inamilikiwa na Mungu na wala sio shetani, lakini kumbuka pia”dunia sio ulimwengu”. Huu ulimwengu ndio mali ya shetani na ndio yeye anayeumiliki na kitakachokuja kuteketezwa sio dunia bali ni ulimwengu huu mbovu wa shetani ambao ni milki yake aliyojijengea..
 

Tofauti kati ya dunia na ulimwengu ni hii;

 
• Dunia ni vitu vyote vya asili na vya kijeografia unavyoviona kama vile mabara, bahari, miti, milima, hewa, ardhi, mito,mabonde, visiwa,anga, n.k.
 
• Na Ulimwengu ni ustaarabu uliobuniwa na aidha Mungu au shetani ili kuifanya dunia iwe na mantiki, paonekane kama ni mahali pa kuishi. mfano. elimu, burudani, miziki, utawala, uchumi, mahakama,Milki, fahari, uchukuzi, mawasiliano, n.k. Haya yote ni mambo yaliyobuniwa kuipa dunia muonekano unaoleta maana. Na ndio maana kwenye Mathayo 4 shetani alimwambia Bwana Yesu nitakupa ULIMWENGU na fahari yake ukianguka kunisujudia.
 
Kwahiyo dunia itadumu siku zote, lakini ustaarabu uliowekwa na shetani (yaani ulimwengu )utaangamizwa utabaki tu ule uliowekwa na Mungu, na hata hivyo 99% ya ustarabu uliopo duniani leo hii unakaliwa na shetani na ndio maana siku ya Bwana itaharibu ustaarabu wote wa shetani na kuleta ustaarabu mpya wa Kristo hapa duniani huo ndio utakaodumu milele na utakaokuwa ni ule utawala wa miaka 1000 Ufunuo 19 & 20.
 
Na sababu ya Mungu kuruhusu mambo mabaya kutokea kama ajali, vimbunga, mafuriko ni kwasababu ya mambo maovu ya huu ulimwengu yaliyopo kama umwagaji damu, rushwa, uasherati, ulevi, uaribifu wa mazingira, ushoga, vita, n.k. mambo kama haya ardhi haiwezi ikavumilia, yanaiharibu dunia na kupelekea gadhabu ya Mungu kumwaga juu ya nchi.
 
Tujitahidi tujiepushe na mambo ya ulimwengu huu yanayopita..Tuyatazame yaliyo juu.
Kumbuka hizi ni siku za mwisho na Kristo yupo mlangoni kurudi. Kizazi tunachoishi kina dalili za kushuhudia mwisho wa dunia.
Chunguza wokovu wako jiweke sawa.
 
Mungu akubariki.
 
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada zinazoendana:

Jehanamu ni nini?

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! ni sahihi kuning’iniza picha nyumbani mwako kama ya Yesu?

Swali linaendelea…maana imeandikwa kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. “

Sasa naomba kufahamu kufanya hivyo ni makosa?


JIBU: kwa kulijibu hili swali tumalizie kusoma mstari huo..

Kutoka 20:4-5″ Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,”…

Sasa tunaona katika huo mstari wa tano msisitizo umewekwa pale katika neno “USIVISUJUDIE WALA KUVITUMIKIA”, lakini sio kwamba ukiweka picha yoyote kama ya Yesu nyumbani mwako ni vibaya hapana! unaweza kuweka picha yoyote upendayo ilimradi iwe ni njema,

Maana tukisema tusiweke picha yoyote basi hata tunaponing’iniza picha zetu wenyewe ukutani majumbani mwetu tunafanya vibaya kwasababu maandiko yanasema usijifanyie mfano wa kitu chochote sio tu kilicho juu mbinguni bali hata kilichopo chini duniani.

Unaona hapo msisitizo ni kwamba unapoweka picha yoyote au sanamu yoyote hupaswi kuiabudu wala kuisujudia kwa kufanya hivyo ni machukizo makubwa mbele za Mungu. Lakini leo hii kuna baadhi ya watu,na dini na madhehebu yanaabudu sanamu za Yesu na bikira Mariamu au watakatifu waliokufa zamani za kale hao ni dhahiri kuwa wanamwabudu shetani aidha kwa kujua au kwa kutokujua.

Ikiwa wewe ni mkatoliki na unayo sanamu ya Yesu au sanamu ya bikira Maria nyumbani mwako, nashauri iondoe haraka sana, kwasababu dini hiyo inahusisha ibada zao na sanamu, vinginevyo utamtia Mungu wivu na kujikuta umeenda Jehanamu.

Lakini kama picha ipo kwa ajili ya urembo au kwa ajili ya kufikisha tu ujumbe fulani katika mazingira yanayokuzunguka au nyumbani kwako, wala husujudii wala kuabudu basi hakuna shida yoyote. Zingatia tu hilo neno ”USIVISUJUDIE WALA KUVITUMIKIA’ kwasababu yeye ni Mungu mwenye wivu.

Biblia inasema;

1 Wakorintho 10:14

[14]Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu.
[15]Nasema kama na watu wenye akili; lifikirini ninyi ninenalo.

Ubarikiwe sana.

 
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada nyinginezo

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

Hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge.(Ufu 21:27)

LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

 


Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini mtu afanye miujiza na bado asiende mbinguni?

SWALI: Naomba kuelewa kwanini mtu atoe pepo, aombee wagonjwa wapone, asikie sauti ya Mungu Ikimwambia hiki na kile kuhusu watu na yeye mwenyewe kufunua siri za mioyo yao, halafu bado asiende mbinguni au asinyakuliwe? Hili linawezekanikaje?


JIBU: Ni sababu ile ile ya Mungu kumpa mwovu afya, chakula, miaka mingi ya kuishi, mvua, uzao, ujuzi, akili, utashi,n.k. vipawa hivi vyote vinatolewa na Mungu, kwasababu yeye anawanyeshea mvua yake waovu na wema. sasa kwa kupewa baraka zote hizo haimpi uhakika mtu huyo kupata uthibitisho ya kuwa Mungu yupo na yeye,

Kwasababu hivi vitu vyote hata mchawi anapewa kitendo cha kuwa tu mwanadamu tayari vinaambatana na wewe, kuna vitu Mungu akikupa haviondoi hata uwe mbaya kiasi gani kama ilivyo kwa shetani Mungu hakumnyang’anya nguvu zake zote japokuwa ni muasi, lakini sababu ya Mungu kuruhusu hayo yote ni kuonyesha uwepo wake dhahiri ili mtu asiwe na udhuru katika siku ya hukumu kwamba hakuuona utukufu wake…

Siku zote Mungu anabaki katika NENO lake, mtu anayempendeza ni yule anayelishika NENO lake kwa kuishi maisha matakatifu yampendezayo, HILO TU! na ndio maana Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake katika Luka 10:20″

Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni. “

Unaona tunapaswa tufurahie pale majina yetu yanapoandikwa mbinguni na sio pale pepo wanapotutii kwasababu kuna watakao toa pepo, watakaoona maono, watakao ponya wagonjwa, watakaotabiri na bado watakuwepo kuzimu.

Soma mistari ifuatayo;

Kumbukumbu 13:1 Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu,

2 ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo;

3 wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda Bwana, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote.

4 Tembeeni kwa kumfuata Bwana, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye.

5 Na yule nabii, au yule mwotaji wa ndoto, na auawe, kwa kuwa amesema yaliyopotoka juu ya Bwana, Mungu wenu, aliyewatoa katika nchi ya Misri, akakukomboa katika nyumba ya utumwa, apate yule mtu kukupotoa katika njia aliyokuamuru Bwana, Mungu wako, uiendee. Ndivyo utakavyouondoa uovu utoke katikati yako.

Na ndio maana Bwana alimalizia na kusema….

Mathayo 7:21-27 ” Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

24 Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;

25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.

26 Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;

27 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.”

Hivyo usipumbazwe na karama yoyote ile uliyonayo au mtu aliyonayo, Dumu katika Neno la Mungu na utakatifu. Hilo tu.

‘bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni’.

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada zinazoendana:

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

Wale manabii 400 waliomtabiria mfalme Ahabu wakati wa Mikaya walikuwa ni manabii wa Mungu au?

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

JE! KARAMA NI UTHIBITISHO WA KUWA NA MUNGU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?

Swali linaendelea… kulingana na huu mstari   (1Wakoritho15:29) inaonekana kuwa wale wanaobatiza watu kwa ajili ya watu waliokufa zamani katika dhambi zao au kuwaombea, wapo sahihi na wanachofanya ni sawa kwasababu hata maandiko yanathibitisha hilo?.. Naomba kufahamu juu ya hilo.


 JIBU: Ili tuweze kuelewa vizuri Ni vema Tukiisoma hiyo habari tokea juu kuanzia ule mstari wa 12-14 ili tupate picha halisi kwanini alisema hivyo..Biblia inasema…

” 12 Basi, ikiwa Kristo anahubiriwa ya kwamba amefufuka katika wafu, mbona baadhi yenu husema kwamba hakuna kiyama ya wafu?

13 Lakini kama hakuna kiyama ya wafu, Kristo naye hakufufuka;

14 tena kama Kristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yenu ni bure.

15 Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi.

16 Maana kama wafu hawafufuliwi, Kristo naye hakufufuka.

AMEN!

Mpaka hapo Tunaona Paulo alipokuwa huko Koritho alikutana na kundi la watu waliokuwa wanajiita WAAMINI na bado hawaamini kama kweli kuna kiyama ya wafu( ufufuo wa wafu),

na wakati huo huo wapo wengine waliokuwa wanashikilia imani ya kubatiza watu kwa ajili ya wafu. Mambo hayo yalikuwa yanafanywa na hawa wakoritho kama ilivyoelezewa na mwandishi mmoja wa historia aitwaye st.John Chrysostom wa karne ya nne, Achbishop;alisema …Korintho kulikuwa na utaratibu wa mtu ambaye amekufa kabla ya kuamini na hajabatizwa ili kwamba mtu huyo aweze kwenda mbinguni ni lazima mtu mwingine aliye hai ajitokeze na kubatizwa kwa niaba yake, walikuwa wanafanya kumchukua mtu mzima na kumficha chini ya kitanda cha yule marehemu, kisha kuhani anakuja na kumwongelesha yule maiti na kumuuliza kama yupo tayari kubatizwa au la na kama maiti Yule asipojibu, basi yule mtu aliyelala chini yake atamjibu kuhani kwa niaba ya yule maiti kisha atakwenda kubatizwa, na kwa kufanya hivyo atakuwa amemkomboa yule mtu aliyekufa kutoka katika adhabu ya milele.

Sasa kwanini mtume Paulo alinukuu hilo?

Ukiendelea mpaka mstari wa 29” utakutana na jambo hili..”Au je! WENYE kubatizwa kwa ajili ya wafu watafanyaje? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, KWANINI KUBATIZWA KWA AJILI YAO? . “

Jambo hili mtume Paulo alilizungumzia kwa kutaka kuwakumbusha wale wasioamini kuwa kuna kiyama cha wafu kuwa kama hawaamini hivyo, kwanini basi wanabatiza mtu kwa ajili ya mfu?Kama wafu hawafufuliwi kamwe. maana kama hawaamini kiyama cha wafu ingewapasa wasifanye hivyo maana kwa kufanya kitendo hicho ni dhahiri kuwa wanaamini kwamba kuna maisha baada ya kufa. je! hawaoni kama wanajichanganya wao wenyewe? ..Hiyo ndiyo sababu ya mtume Paulo kuandika hivyo.

Lakini Mtume Paulo hakumaanisha kuwa yeye au wakristo wa kweli waliokuwa Korintho walikuwa wanafanya hicho kitendo cha kubatiza kwa niaba ya wafu bali ni wengine na ndio maana alitumia neno “WENYE”. wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu Ikiashiria kuwa ni kundi lingine,tofauti na watakatifu.

Na sio tu jambo hilo potofu peke yake la kubatizwa kwa ajili ya wafu lilikuwepo kwenye makanisa bali pia imani nyingine potofu kama ya kusema ” siku ya Bwana imeshakuja” N.K. zilikuwa zikihubiriwa katikati ya makanisa ya Mungu (soma 2Timotheo 2:18, 2Wathesalonike 2:2).

Leo hii imani kama hizi zimeasilishwa pia katika baadhi ya makanisa na madhehebu kama Kanisa Katoliki, likishikilia mistari hii kuthibitisha fundisho la (wakristo kwenda toharani purgatory “) ikiwa na maana kuwa mkristo aliyekufa katika dhambi na hajakamilishwa katika neema anakwenda mahali pa mateso ya muda kwa ajili ya utakaso wa dhambi zake kisha akishatakasika anaweza kwenda mbinguni, hivyo basi muda wa kuendelea kukaa katika hiyo sehemu ya mateso inaweza ikafupishwa kwa kutegemea maombi au sala za walio hai wakimwombea.

Hiyo ndio maana ya kwenda toharani, Jambo ambalo sio sahihi Biblia inasema mwanadamu ameandikiwa kufa mara moja na baada ya kufa ni hukumu (waebrania 9:27), kumuombea mtu aliyekufa, au kubatizwa kwa ajili yake ni moja ya mafundisho potofu ya kuwafanya watu waendelee kustarehe katika dhambi wakiamini kwamba hata wakifa katika dhambi watakuwa na nafasi ya pili ya kusafishwa, usidanganyike hizo ni elimu za shetani wakiyapindua maandiko kuthibitisha uongo wao, hakuna kitu kama hicho cha kwenda Toharani baada ya kufa biblia pia inasema

1 Timotheo 4:1 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, WAKISIKILIZA ROHO ZIDANGANYAZO, na mafundisho ya mashetani; kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;”.

Amen.

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Biblia inamaanisha nini kusema Yeye aliye na sikio, na asikie?

UFUNUO: Mlango wa 19

NILIMWONA SHETANI, AKIANGUKA KUTOKA MBINGUNI.

Rudi Nyumbani:

Print this post