Title August 2023

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu lililo hai (Zab.119:105)

Je unaijua nguvu ya kinywa chako? Biblia inasema kuwa MAUTI na UZIMA huwa katika uwezo wa ULIMI. Na mtu awezaye kuutumia vizuri ulimi wake atakula matunda yake.

Mithali 18:21 “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake”.

Sasa ULIMI una matunda mawili tu!, ambayo ni “Uzima na Mauti”. Maana yake mtu anaweza kuutumia ulimi wake ukamletea UZIMA, lakini pia anaweza kuutumia na ukamletea MAUTI.

Yule kijana aliyempelekea Daudi habari za kifo cha Sauli, kinywa chake mwenyewe kilimletea “Mauti” (2Samweli 1:16) hali kadhalika Mfalme Yehoshafati alipokuwa katika hatari ya kufa, kwa kinywa chake mwenyewe alijiokoa. (2Nyakati 18:31).

Lakini leo nataka tuangalie faida za kutumia ULIMI katika eneo la  MAOMBI.

Wengi tumezoea kuomba kimoyomoyo, jambo ambalo ni zuri lakini si wakati wote linafaa!!.. kuna mazingira ni lazima utumie kinywa chako kutoa maneno dhahiri yanayosikika!..Kuna ngome zinahitaji kusikia sauti ndipo zitii!, Kuna ngome zinahitaji kuamrishwa na kukemewa ndipo zitii (Kuta za Yeriko zilihitaji kelele nyingi ili zianguke)….Hali kadhalika katika imani inahitajika sauti ya kinywa ili kuthibitisha wokovu mtu alioupata…

Warumi 10:9  “Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.

10  Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu”.

Kwa hiyo si kila wakati maombi ya ukimya yanafaa… Ni lazima ujifunze kubadili gear unapoingia katika maombi ya vita, hata motokaa haisaifiri kwa gear moja tu, ikienda hivyo itakwamaa mahali Fulani.

Sasa biblia inatufundisha kuwa “Mauti na Uzima” huwa katika uwezo wa kinywa. Maana yake ni kwamba tukitumia vizuri ndimi zetu wakati wa kuomba tunauwezo wa kuvihuisha vitu vingi vilivyokufa, na pia kuviua baadhi ya vitu visivyofaa maishani mwetu.

Tunaviuaje vitu visivyofaa?.. Tunaviua kwa “kuvitamkia kifo” kwa mfano ule ule wa Bwana Yesu alivyoutamkia ule Mtini, na ukafa wakati ule ule.

Mathayo 21:18  “Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa.

19  Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; AKAUAMBIA, YASIPATIKANE MATUNDA KWAKO TANGU LEO HATA MILELE. MTINI UKANYAUKA MARA.

20  Wanafunzi walipoona, walistaajabu, wakisema, Jinsi gani mtini umenyauka mara?

21  Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng’oka, ukatupwe baharini, litatendeka.

22  Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea”.

Mstari wa 19 unasema “..akauambia, yasipatikane matunda kwako tangu leo hata milele, mtini ukanyauka mara.” Hapo Bwana Yesu aliuua huo mtini kwa kutumia kinywa chake. (Aliutumia ulimi wake na akala matunda yake), na anatuambia tukiwa na Imani tunaweza kufanya kama hayo na hata Zaidi ya hayo.

Hivyo na sisi ni lazima tujifunze kutumia Ndimi zetu kuua baadhi ya vitu ambavyo shetani kavipanda katika maisha yetu.

Unapoamka kusali Ua kazi za giza katika siku yako, unapotembea zihukumu kazi za giza kwa kutumia kinywa chako.. kwasababu unapotamka na kuamini moyoni mwako basi fahamu kuwa ni lazima yatokee hayo uliyoyasema.

Zitamkie mauti kazi za shetani katika utumishi wako, katika familia yako, katika watoto wako, katika shughuli zako, katika vitu vyako unavyomiliki, Usiishie tu kuomba kimya kimya pasipo kutoa maneno yoyote.. Paza sauti kwasababu kuna nguvu Mungu kaiweka katika ulimi wa mwanadamu.

Wachawi na mawakala wote washetani wanajua nguvu iliyopo katika ulimi, ndio maana wanautumia kuleta madhara makubwa katika maisha ya watu.. sasa na watu waliookoka ni lazima kutumia ulimi kutangua maneno yote yaliyonenwa au yanayonenwa kinyume na maisha yetu ya kiroho na kimwili.

Vile vile ni lazima tutumie Ndimi zetu kutamka UZIMA wa vitu vilivyokufa katika maisha yetu. Nabii Ezekieli aliambiwa aitabirie mifupa mikavu ili iweze kuwa na uhai tena, na katika maono yale aliitabiria mifupa ile kwa kinywa chake na ikarudia uzima na likaamka jeshi kubwa sana (soma Ezekieli 37:1-8).

Sehemu zote Bwana Yesu alipoenda kuponya wagonjwa alitumia kinywa chake kutamka, na sisi ni lazima tutumie vinywa vyetu kutamka uzima juu ya vitu viliyokufa ndani yetu. Ikiwa ni huduma, ikiwa ni karama, ikiwa ni shughuli unayoifanya, ikiwa ni watoto, au kitu kingine chochote kilicho chema ni sharti kipate uzima kupitia kinywa chako!. Fanya hivyo daima, usiache hata siku moja hata kama unaona kwa nje ni pakavu, endelea kwasababu vita vya kiroho si vita vya kimwili, na ukiwa na bidii kufanya hivyo mwisho utakula matunda ya ulimi wako.

Mithali 18:21 “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?

HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

Rudi nyumbani

Print this post

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu lililo taa ya miguu yetu na Mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).

Ni muhimu kujua kanuni kadhaa za kuomba ili maombi yetu yawe na majibu.

Tumewahi kujifunza kanuni kadhaa huko nyuma na leo imempendeza Bwana tujifunze kanuni nyingine.

Neno la Mungu linasema yafuatayo katika kitabu cha Yakobo 4:2-3.

Yakobo 4:2 “ Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi!

3  Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”.

Kumbe sababu ya kutopata yale tunayoyaomba ni jinsi tunavyoomba!.. (kwamba tunaomba vibaya!).

Na kuomba vibaya kunakozungumziwa hapo si kukosea kupangilia maneno wakati wa kuomba, bali ni kuomba kusikompendeza Bwana, ambako ni nje na mapenzi ya Mungu, mfano wa maombi hayo ni yale mtu anaomba Bwana ampatie fedha ili awe nazo awakomeshe wanaomdharau. (Maombi ya namna hii ni maombi mabaya, na mara nyingi hayana majibu)

Hivyo unapoomba zingatia mambo yafuatayo.

1.Kuwa na Nia Njema:

Nia njema, maana yake ni kusudi jema… Kama unahitaji Bwana akupe mafanikio Fulani ya kiroho au ya kimwili, hakikisha Nia yako ni njema, kwamba utokane tu na ugumu unaoupitia, na pia upate kitu cha kuwasaidia wengine, na si kwa lengo la kuwakomesha wanaokudharau. Ukiwa na Nia ya kupata vitu ili wengine waone, maombi hayo yanaweza yasijibiwe kabisa.

2. Mwombe Mungu mahitaji na si Fedha.

Wengi wetu tunapenda kupeleka maombi ya kupata fedha kutoka kwa Mungu.. Lakini kiuhalisia hayo si maombi bora. Tunasahau kuwa tunachokihitaji sana ni mahitaji yetu kama chakula, mavazi, makazi, afya na mengineyo, ambayo hayo Mungu anaweza kukutimizia pasipo fedha.

Ukiwa na haja ya chakula, mwambie Bwana naomba chakula na yeye anajua namna ya kukupatia hicho chakula kama kwa njia ya kukupatia fedha ukanunue, au kwa kukuletea mtu atakayekupa hicho chakula, (usikimbilie moja kwa moja kumwambia Bwana akupe fedha ya chakula), kwani yeye anazo njia nyingi za kukulisha wewe, si lazima kwa kutumia fedha.

Vile vile ukitaka mavazi, makazi, biashara, afya n.k  Mwambie Bwana akupe vitu hivyo, na wala usiombe fedha za kupata mavazi, au za kupata makazi, au za kufanya biashara.. wewe mwambie naomba mavazi, yeye anajua jinsi ya kukupatia kama kupitia mlango huo wa fedha au kupitia watu yeye anajua, vile vile usiombe mtaji kwa Mungu, badala yake iombe ile kazi kwasababu wakati wewe unawaza kupata mtaji kwanza kumbe pengine Mungu amekuandalia mahali utakapoanza kufanya kazi pasipo mtaji.

Ukihataji Bwana akupe kifaa cha kazi au chombo za kukurahisishia usafiri, usimwambie Bwana akupe Pesa za kununua chombo hicho, badala yake mwombe Bwana akupe hicho chombo, kwa njia anayoijua yeye.

Ukitaka kusafiri usimwombe Bwana fedha za kusafiri, wewe mwombe akusafirishe, yeye atajua njia atakayotumia kukufikisha kule unakotaka kwenda, kama amtanyanyua mtu na kukusafirisha kwa gharama zake au bure, au atafungua mlango wa wewe kupata fedha hizo, ila usijifunge kwa kanuni ya fedha.

Vile vile unapoumwa usimwombe Mungu pesa za matibabu, mwombe afya, yeye anajua njia atakayotumia kukupa hiyo afya, na mambo mengine yote, epuka Kutaja “Pesa” mbele za Mungu!!.. bali taja lile hitaji!.

Kwanini maombi mengi ya kuomba Pesa hayajibiwi?

Kwasababu kuna roho nyuma ya pesa, inayowasukuma watu katika tamaa mbaya za kidunia, na kuwatoa wengi kwenye Imani, ndivyo maandiko yanavyosema.

1Timotheo 6:10  “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi”

Ndio maana utaona asilimia kubwa ya watu waliopata pesa wanakuwa na kiburi!. Lakini waliopewa na Bwana ni wanyenyekevu. Mtu aliyezawadiwa baiskeli na yule aliyenunua baiskeli kwa fedha, utaona yule aliyenunua anakuwa na kiburi Zaidi ya yule aliyepewa. Ingawa wote wana baiskeli!.

Yule aliyezawadiwa nyumba na yule aliyejenga kwa fedha yake, utaona yule aliyejenga anakuwa na kiburi Zaidi ya yule aliyezawadiwa. Na mapenzi ya Mungu ni sisi tuwe wanyenyekevu na si watu wenye viburi, hivyo kamwe hawezi kukupa kitu ambacho baadaye kitakuja kukupa kiburi.

Ni wachache sana ambao Mungu anawabariki kwa fedha, kwasababu anajua tayari ameshawatengeneza mioyo yao, hawawezi kuwa na kiburi hata wawe na kiasi gani cha fedha, na hiyo naweza kusema ni asilimia 1% lakini wengi Mungu hawapi hizo fedha wanazozihitaji kwasababu anajua tamaa tulizo nazo. Na ukiona mtu ana fedha nyingi na ana kiburi (hizo fedha hajapewa na Mungu!!).

Kama mkristo biblia inatufundisha tusiwe watu wa kupenda fedha, wala kuzisifia wala kuzitukuza, badala yake tumtukuze Mungu na tumfanye Mungu siku zote kuwa MPAJI WETU (YEHOVA YIRE)!!. Kwamba fedha ziwepo au zisiwepo bado tutaishi, bado tutavaa, bado tutakula, bado tutamiliki vitu.. Tuliookoka tuna uwezo wa kuishi bila fedha wala vitu vilivyotukuzwa na wanadamu na bado tukawa na maisha bora kuliko watu wenye mambo hayo.

Mhubiri 5:10 “Apendaye fedha hatashiba fedha, Wala apendaye wingi hatashiba maongeo. Hayo pia ni ubatili”.

Bwana atusaidie.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE UMEJIANDAA KUTIMIZA UNABII UPI?

Ni kwa namna gani haki huinua taifa? (Mithali 14:34)

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.

JE UNA MATUMAINI YA KUPATA TENA KILE ULICHOPOTEZA?

Rudi nyumbani

Print this post

Alani ni nini?(1Samweli 17:51)

Alani ni kifuko cha kuhifadhia upanga ambacho huvaliwa kiunoni na askari hususani wakati wa vita. Tazama picha juu.

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;

1Samweli 17: 51 “Ndipo Daudi akapiga mbio, akasimama juu ya Mfilisti, akautwaa upanga wake, akaufuta alani mwake, akamwua, akamkata kichwa kwa upanga huo. Nao Wafilisti walipoona ya kuwa shujaa wao amekufa, wakakimbia”

1Nyakati 21:27 “Bwana naye akamwamuru malaika; naye akaurudisha upanga wake alani mwake tena”.

Yohana 18:11  “Basi Yesu akamwambia Petro, Rudisha upanga alani mwake; je! Kikombe alichonipa Baba, mimi nisikinywee?”

Soma pia,  Ezekieli 21:3, 5

Je! Chombo hichi kinafunua nini rohoni?

Kama tujuavyo upanga na alani, ni kama pochi na pesa, havitengani. Na upanga, kibiblia ni Neno la Mungu (Waefeso 6:17, Waebrania 4:12). Hivyo Neno la Mungu halihifadhiwi penginepo zaidi ya kwenye moyo. Pale linapohitajika kutumika hutolewa moyoni na sio penginepo. Kwahiyo chombo hichi kijulikanacho kama Alani, kinauwakilisha moyo wa Mtu.

Na kama tunavyojua upanga hutumiwa na mtu yoyote, unaweza hata kumwangamiza  mwenye nao, ukitumiwa na adui. Ndivyo alivyojaribu kufanya shetani alipomjaribu Bwana na kumwambia ‘imeandikwa’, Lakini kwasababu Yesu alikuwa amejaa ‘Kweli yote’. Aliweza kumpokonya upanga huo huo na kummaliza nao.

Hivyo ni muhimu pia kujaa ‘Kweli yote’ sio Neno tu peke yake, yaani kuufahamu ukweli wa Neno la Mungu. Kwasababu ibilisi anaweza kulitumia kukuangusha ikiwa hutakamilishwa katika hilo, kwamfano anaweza kuja kukwambia kuoa wake wengi si dhambi, kwani Yakobo, alioa wake wengi, Daudi alioa wake wengi, Sulemani alioa wake wengi, na wote hawa walikubaliwa vizuri na Mungu, vivyo hivyo na wewe ukifanya hivyo utakubaliwa tu, hamna shida,. Lakini je! Hiyo ni kweli yote? Kweli yote inasema Mungu alimuumba mtu mke na mume, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.(Mathayo 19:4-9), hakuumba Adamu mmoja, Hawa wengi. Hivyo usipojua kuligawanya vema Neno la Mungu kwa msaada wa Roho ni rahisi shetani kukupiga.

Na ndio maana maandiko yanatusihi tuivae ‘kweli’ kiunoni.

Waefeso 6:13  “Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. 14  Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?

Silaha za Mkono wa kuume na za mkono wa kushoto ni zipi

Kwanini Bwana Yesu aliwaagiza wanafunzi wake wakanunue upanga?

Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?

Kwanini Mungu aseme “Alaaniwe azuiaye upanga wake usimwage damu” (Yeremia 48:10).

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

Rudi nyumbani

Print this post

Kutoka 21:10 ina maana gani?.

Jibu: Tuanze kusoma  kuanzia mstari wa 7..

Kutoka 21:7 “Mtu akimwuza binti yake awe kijakazi, hatatoka yeye kama watumwa wa kiume watokavyo. 

8 Kwamba bwana wake hakupendezewa naye, akiwa amemposa, ndipo atakubali akombolewe; hana amri yeye kumwuza aende kwa watu wageni maana amemtenda kwa udanganyifu. 

9 Kwamba amposa mwanawe, atamtendea kama desturi zipasazo binti zake. 

10 Kwamba ajitwalia mke mwingine, chakula chake huyo, na nguo zake, na ngono yake, hatampunguzia.  11 Kwamba hamfanyii mambo haya matatu, ndipo atatoka aende bure, pasipo kutolewa mali”.

Jibu: Kwa desturi za kiyahudi mtumwa wa kiume au wa kike anapaswa amtumikie bwana wake kwa muda miaka 6 tu, ukifuka mwaka wa 7 anakuwa yupo huru kuondoka.,

Kumbukumbu 15:12 “Ikiwa nduguyo, mume wa Kiebrania, au mwanamke wa Kiebrania, akiuzwa kwako, naye amekutumikia miaka sita; basi mwaka wa saba mwache huru aondoke kwako.

 13 Nawe utakapomwacha huru aondoke kwako, usimwache aende zake mikono mitupu”

Ikiwa mtumwa wa kiume aliingia na mke wake basi utakapofika mwaka wa 7 ataondoka na mke wake huyo, (Kutoka 21:1-3) lakini kama aliingia bila mke ana akaozwa mke kutoka katika familia ya bwana wake, basi utakapofika mwaka wa 7 atatoka yeye kama yeye, lakini mke na watoto watabaki kwa baba wa mke wake, hana amri ya kuondoka nao, lakini kama hataki kumwacha mke wake na watoto wake basi atamtumikie bwana wake huyo daima kwa agano la kutobolewa sikio kwa uma.

Kutoka 21:5 “Lakini huyo mtumwa akisema waziwazi, Mimi nampenda bwana wangu, na mke wangu na watoto wangu; sitaki mimi kutoka niwe huru; 

6 ndipo hapo huyo bwana wake atamleta mbele ya Mungu na kumleta mlangoni, au penye mwimo wa mlango; na bwana wake ATALITOBOA SIKIO LAKE KWA UMA; ndipo atamtumikia sikuzote”.

Hivyo ishara ya kutobolewa sikio ilikuwa ni ishara ya mtuwa wa kukataa uhuru wake.

Lakini kwa upande wa mtumwa wa kike (yaani kijakazi) ilikuwa ni tofauti kidogo. Kama kijakazi aliingia bila kuolewa na baadaye kijana wa bwana wake akampenda na kumwoa, kama mke wa kwanza basi famila ya kijana inapaswa kumfanya kama binti yao.

Lakini kama ameolewa kama mke wa pili, na bado ni kijakazi, na bwana wake hamtaki tena awe mke wake au suria wake, basi utakapofika mwaka wa 7, wakati wa maachilio, yeye hatamwachilia kama mabinti wengine wajakazi wanaoachiwa huru, bali kinyume chake ataachiliwa kwa gharama (maana yake atakombolewa).

Hivyo yule baba wa mtoto wa kiume aliyemwoa huyo binti, atamwuza kwa mojawapo wa ndugu aliye karibu, na si kwa mgeni (yaani mtu kutoka taifa lingine tofauti na Israeli), na asipopatikana wa kumnunua ndipo yule kijana ataendelea kuishi naye huku akimtimizia haki yote ya ndoa, ikiwemo CHAKULA, MAVAZI NA HAKI YA NDOA (Ngono).

Vitu hivyo vitatu ni sheria avitimize, si kwasababu hamtaki tena na kakosa mtu wa kumnunua basi aanze kumnyanyasa kwa kumnyima chakula chake na mavazi pamoja na haki ya ndoa ambayo imenenenwa na mtume Paulo kwa uongozo wa Roho katika 1Wakorintho 7:5. Na ikitokea kashindwa kumtimizia hayo mambo matatu basi atamwacha aende zake huru, bila gharama zozote za kumkomboa.

Kutoka 21: 10 “Kwamba ajitwalia mke mwingine, chakula chake huyo, na nguo zake, na ngono yake, hatampunguzia. 

11 Kwamba hamfanyii mambo haya matatu, ndipo atatoka aende bure, pasipo kutolewa mali”.

Mambo gani tunajifunza?

1.Kutoboa masikio si ishara nzuri.

Asili ya kutoboa sikio na kuweka hereni haikuwa nzuri, watu waliotobolewa masikio enzi za zamani ni watu waliokataa uhuru wao, hali kadhalika roho hiyo hiyo inatembea mpaka leo, kibiblia mwanamke au mwanamke hapaswi kutoboa masiko yake. Huenda ulitobolewa enzi hujaokoka, sasa umeshaokoka usiweke hereni baki katika uhalisia wako.

Wengi wanaosumbuliwa na nguvu za giza ni kutokana na vitu wanavyoviweka katika miili yao, na hawajui kuwa hivyo ndio vyanzo vya roho zinazowasumbua.

2. Ni lazima kutimiza haki ya Ndoa

Mtu aliyeoa au aliyeolewa ni sharti amtimizie mwenzie haki zote za ndoa ikiwemo upendo, na ukaribu wakati wowote unapohitajika. Maandiko yanasema mume hana amri juu ya mwili wake kadhalika mke.

1Wakorintho 7:2  “Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe.

3  Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.

4  Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.

5  Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

EPUKA MUHURI WA SHETANI

USIMPE NGUVU SHETANI.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

Tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Bwana Yesu alikuwa na nywele ndefu?

JIBU: Picha nyingi zinazochorwa kumweleza Yesu, takribani nyingi ya hizo  zinamwonyesha ni mtu mwenye nywele ndefu. Lakini Je uhalisia wake ni upi, ni kweli alikuwa na nywele ndefu au fupi?

Maandiko yanaeleza utamaduni wa wayahudi, kwa wanaume ilikuwa kuacha nywele zirefuke kama zile za mwanamke ni aibu kwa mtu huyo. Anajivunjia heshima kubwa.

1Wakorintho 11:14  “Je! Hayo maumbile yenyewe hayawafundishi ya kwamba mwanamume akiwa na nywele ndefu ni aibu kwake? 15  Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni fahari kwake. Kwa sababu amepewa zile nywele ndefu ili ziwe badala ya mavazi”

Hivyo hakukuwa na mtu aliyekuwa na nywele ndefu isipokuwa tu mtu aliyeitwa mnadhiri wa Mungu.

Lakini Je! Yesu alikuwa ni Mnadhiri ?

Kabla ya kufahamu kama Yesu alikuwa mnadhiri au la! Tufahamu kwanza mnadhiri alikuwa ni nani, na sheria ya mnadhiri ilikuwaje

Mnadhiri ni mtu aliyetengwa au aliyejitenga mwenyewe/ aliyejitoa wakfu kwa Mungu, kufuata na sababu binafsi, aidha kwa sababu ya shukrani yake ya kutendewa jambo Fulani kama vile kuponywa ugonjwa, au  kupatiwa mtoto, au kupata kitu Fulani kwa Mungu alichokuwa anamwomba. Hivyo katika agano la kale, kulikuwa na sheria ya mnadhiri. Na mnadhiri alikuwa yoyote Yule aidha mwanamke au mwanaume.

Sheria za mnadhiri ni zipi?

Kulingana na Hesabu 6:1-8

  1. Hakuruhusiwa kunywa divai, wala zabibu, wala juisi ya zabibu,  wala mbegu zake. Yaani kwa ufupi kitu chochote kilichomzao wa zabibu hakuruhusiwa kunywa
  2. Hakuruhusiwa kukata nywele zake, tangu siku hiyo aliyomwekea Mungu nadhiri mpaka atakapoitoa
  3. Hakuruhusiwa kugusa maiti. Hata kama ni ndugu yake wa karibu amekufa, baba yake au dada yake. Hakuruhisiwa  kufanya hivyo
  4. Ni lazima awe mtakatifu kwa Bwana; Maana yake ajitenge na mambo yote yaliyo najisi kipindi chote awapo katika kiapo chake.

Katika biblia, kulikuwa na makundi mawili ya wanadhiri

  1. Wanadhiri wa daima: Hawa ni waliotengwa tangu tumboni mwa mama zao: Mfano wao alikuwa  ni Samsoni, Samweli, Yohana Mbatizaji.. Hawakukatwa nywele zao, lakini pia hawakunywa divai maisha yao yote.
  2. Wanadhiri wa muda: Hawa ni aidha waliamua wenyewe katika kipindi Fulani katika maisha yao waingie kwenye viapo hivyo kwa Mungu, yaani wamtumikie yeye daima mpaka kufa kwao, au waliokuwa na nadhiri za muda, ambapo pengine baada ya miezi miwili, au mwaka mmoja wanaiondoa na kwenda kunyoa nywele zao, na kuendelea kutumia mizabibu nk. Mfano wa Hawa alikuwa ni mtume Paulo, ambaye kipindi Fulani anashuhudia naye alikuwa na nadhiri hiyo.

Matendo 18:18  “Baada ya hayo Paulo akazidi kukaa huko siku nyingi, kisha akaagana na ndugu akaabiri kwenda Shamu; na Prisila na Akila wakaenda pamoja naye, alipokwisha kunyoa kichwa chake huko Kenkrea; maana alikuwa ana nadhiri”

Sasa tukirudi kwa Bwana Yesu.

Je! Na Yeye alikuwa ni mnadhiri?

Jibu ni hapana, kwasababu Bwana alikunywa mzao wa mzabibu.

Mathayo 26:29  Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.

Kuonyesha kuwa hapo kabla alikuwa anakunywa.

Soma pia  Mathayo 11:19, Na Yohana 2:1-12, inatupa picha alitumia mzao wa mzabibu. Halikadhalika aligusa maiti, (Marko 5:41), na zaidi ya yote Bwana hakufungwa na sheria za torati.

Hivyo kwa kifupisho ni kwamba Bwana Yesu hakuwa na nywele ndefu, yawezekana alikuwa na nywele nyingi lakini hazikuwa ndefu kama za mwanamke, mfano wa aonekanavyo kwenye baadhi picha zinazochorwa.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)

NGUVU YA MNADHIRI WA BWANA.

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

Nini maana ya Kucheka kwenu na kugeuzwe kuwa kuomboleza (Yakobo 4:9)

Fahamu maana ya Mithali 29:4 “Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni nyaraka zipi mtume Paulo aliziandikia gerezani?

Kati ya nyaraka kumi na tatu (13) alizoziandika mtume Paulo, Nne (4) kati ya hizo, aliziandika akiwa gerezani. Alipokuwa Rumi, ambapo maandiko yanatuonyesha  alipelekwa na kuwekwa chini ya kifungo maalumu ambacho aliruhusiwa watu kumtembelea lakini pia kuwahubiria injili akiwa katika kifungo hicho cha nyumba.

Matendo 28:16  “Tulipoingia Rumi Paulo alipewa ruhusa kukaa kwake mwenyewe pamoja na askari aliyemlinda…. 30  Akakaa muda wa miaka miwili mizima katika nyumba yake aliyokuwa ameipanga, akawakaribisha watu wote waliokuwa wakimwendea, 28.31  akihubiri habari za ufalme wa Mungu, na kuyafundisha mambo ya Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri mwingi, asikatazwe na mtu”.

Hivyo huko ndipo panaaminika aliandika nyaraka hizi nne. Ambazo ni

  1. Waefeso,
  2. Wafilipi,
  3. Wakolosai,
  4. Filemoni.

Sasa ni kwanini Nyaraka hizi na si nyingine?

Ni kwasababu ya habari za kufungwa kwake, alizozitaja katika nyaraka hizo; Ambazo zinaonyesha mazingira hayo alikuwa kifungoni.

Kwamfano ukisoma vifungu hivi, utaona,

Waefeso 3:1,4:1, Wafilipi 1:13, Wakolosai 4:3, Filemoni 1:10.

Je Ni nini cha kujifunza, katika vifungo vya mtume Paulo?

Yamkini Paulo alitamani awe huru kwa wakati ule ili aendelee kuihubiri injili kwa mataifa yote. Lakini hakujua mpango wa Mungu kwa nyaraka zake. Hakujua kuwa  Mungu atazihifadhi kwa mamia ya miaka, ili ziwe injili kwa vizazi vijavyo. Na matokeo yake ni kuwa nyaraka hizo zimehubiri injili kuliko hata wakati alipokuwa anazunguka mwenyewe kwenye mataifa akiwa huru.

Kwamfano mafunzo yaliyo katika kitabu cha Waefeso, yanatoa mwongozo mzuri kuanzia Viongozi wa kanisa, watakatifu hadi ngazi za kifamilia. Na jinsi gani mtakatifu anavyopaswa avae silaha za haki ili aweze kumpinga adui yake shetani (Waefeso 6:11-18)

Hii ni kuthibitisha maneno yale ya maandiko yanayosema kwamba injili  haifunguki.

2Timotheo 2:9  “Nami katika hiyo nimeteswa hata kufungwa kama mtenda mabaya; lakini neno la Mungu halifungwi

Na wewe pia ujionapo upo katika mazingira yanayokubana kuitangaza injili ya Bwana, usiwe na mawazo ya kukata tamaa, hapo hapo tazama upenyo wowote uutumie, kwasababu wewe umefungwa lakini sauti ya Mungu iliyo ndani yako, inauwezo wa kufika duniani kote, kwa vizazi vyote, hata kama umefungiwa kwenye chumba cha giza, namna gani, injili ya Kristo, inaangusha ngome popote.

Nyanyuka sasa, fanya jambo kwa Bwana, iamini nguvu ya msalaba.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Mtume Paulo alikuwa ni Mrumi, Myahudi au raia wa Tarso?

Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).

Tarishi au Matarishi ni akina nani  kwenye biblia?

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

SIRI YA KUFANIKIWA KWA MTUME PAULO.

Paulo alikuwa na maana gani aliposema “nimeaminiwa uwakili”

Rudi nyumbani

Print this post

Je Paulo na Petro walishindania nini? (Wagalatia 2:11).

Swali: Kwanini Petro na Paulo walishindana na pia tunajifunza nini katika kushindana kwao?.

Jibu: Tusome,

Wagalatia 2:11 “Lakini Kefa alipokuja Antiokia, nalishindana naye uso kwa uso, kwa sababu alistahili hukumu”

Kushindana kunakozungumziwa hapo si kushindana kwa maneno ya dini kule kunakozungumziwa katika 1Timotheo 6:4, 2Timitheo 2:14 na Wafilipi 2:14, kwamba tutende mambo yote pasipo mashindano wala manung’uniko.

Wala si mashindano ya Imani, yale yanayozungumziwa katika Wafilipi 1:30 na Waebrania 12:1 ambayo tunapaswa tuwe nayo, (yaani kushindana dhidi ya nguvu za giza na kuishikilia imani).

Bali neno “mashindano” kama lilivyotumiwa hapo na Paulo lilimaanisha “kukabiliana”. Maana yake Paulo alipofika Antiokia na kukutana na Petro alikabiliana naye uso kwa uso na kumwonya kuhusiana na tabia aliyoonesha ya uvuguvugu juu ya desturi za wayahudi katika kula.

Maana yake Petro alipokuwa ameketi na wayahudi aliungana nao kwa kutokula vyakula vilivyo najisi kwa hofu ya wayahudi…lakini mahali alipoketi katika chakula pamoja na watu wa mataifa, alishirikiana nao katika vyakula hivyo vilivyo najisi kwa wayahudi.

Sasa tabia hiyo haikuwa sawa, ndipo Paulo alipoona na kumkabili na kumwambia dhahiri kuwa anachokifanya sio sawa.

Wagalatia 2:11 “Lakini Kefa alipokuja Antiokia, nalishindana naye uso kwa uso, kwa sababu alistahili hukumu

12 Kwa maana kabla hawajaja watu kadha wa kadha waliotoka kwa Yakobo, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa; lakini walipokuja wao, akarudi nyuma akajitenga, huku akiwaogopa waliotahiriwa.

13 Na hao Wayahudi wengine wakajigeuza pamoja naye, hata na Barnaba pia akachukuliwa na unafiki wao.

14 Walakini, nilipoona ya kuwa njia yao haiendi sawasawa na ile kweli ya Injili, nalimwambia Kefa mbele ya wote, Ikiwa wewe uliye Myahudi wafuata desturi za Mataifa, wala si za Wayahudi, kwa nini unawashurutisha Mataifa kufuata desturi za Wayahudi?”.

Tunachoweza kujifunza kwa Paulo ni ujasiri wa kusimama kuitangaza kweli pasipo kujali cheo cha mtu wala heshima ya mtu, ikiwa na maana kwamba ikiwa yeyote ananyanyuka na kwenda kinyume na kweli basi anapaswa akabiliwe na kuonywa pasipo kujali cheo chake wala umaarufu wake lakini kwa nia ya upendo.

Vile vile tunachojifunza kwa Mtume Petro ni unyenyekevu, kwani baada ya kuonywa na Paulo alitubu na huoni popote akimkasirikia Paulo zaidi sana utaona anakuja kuwaelekeza watu kwenye nyaraka za Paulo kwamba wazisome..

2 Petro 3:15 “Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa

16 vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe”.

Na sisi hatuna budi kuiga ujasiri wa Paulo na unyenyekevu wa Petro, huo ndio ukristo!!!..Lakini si kuona dhambi na kuzifumbia macho au kuambiwa ukweli na kukasirika badala ya kujifunza na kubadilika.

Bwana atusaidie katika hayo yote.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Yesu aliwezaje kuchukuliwa na shetani juu ya kinara cha hekalu kujaribiwa?

SWALI: Wakati shetani anamjaribu Yesu, biblia inasema alimchukua na kumpandisha kwenye kinara cha hekalu, swali ni je! Alikuwa anachukuliwaje mahali pale ni njia gani ilikuwa inatumika?


JIBU: Awali ya yote ni lazima tufahamu kuwa Bwana Yesu hakupelekwa sehemu nyingine yoyote ili kujaribiwa zaidi ya pale jangwani. Hii ikiwa na maana majaribu yake yote yalimtokea akiwa palepale jangwani.

Mathayo 4:1  “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi,2  Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa”

Sasa kama ni hivyo iweje, shetani amtoe pale na kumpeleka kwenye kinara cha Hekalu na wakati huo huo amwonyeshe milki zote za ulimwenguni? Je! Aliondokaje pale? Au alichukuliwa kimazingara?

Mathayo 4:5  “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu 6  akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 7  Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako. 8  Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, 9  akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia. 10  Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. 11  Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia”

Jibu ni kwamba majaribu yale yalikuwa katika roho, na sio katika mwili, Kwa ufupi yalikuwa ni mfano wa maono. Na kikawaida maono yanapokuja ikiwa ni ya kukuonyesha tukio husika utashangaa waweza kujiona kama upo pale pale eneo lenyewe, lakini sio. Kama tu vile ndoto. Unaota upo kijijini kwenu, anashughulika, unaongea na ndugu, lakini kiuhalisia kumbe umelala palepale kitandani.

Ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu, alikuwa palepale jangwani, wala hakutoka, isipokuwa alikuwa katika roho, akayaona hayo yote, aliyoonyeshwa na shetani.

Bwana akubariki.

Lakini pia ni vizuri, kutambua maana ya majaribu yale, Kwasababu hayo pia ndio shetani anayotumia kumjaribu kila mtakatifu aliyepo duniani. Kwa upana wa habari hiyo waweza fungua link hii >>> MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

DAKIKA MOJA TU, INAKUFANYA UMWAMINI SHETANI?

Tofauti kati ya ufunuo, unabii na maono ni ipi?

NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

UFUNUO: Mlango wa 11

DALILI TISA (9) ZA PEPO KUWEPO NDANI YA MTU.

KWA WINGI WA WASHAURI HUJA WOKOVU.

Rudi nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 9:17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza”

SWALI: Je! mstari huu unaelewekaje? Mithali 9:17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza”


JIBU: Mstari huo unamfunua mtu mwenye asili ya dhambi, jinsi vitu vilivyo kinyume na mapenzi ya Mungu vinavyoweza kupendeza mbele yake zaidi ya vile ambavyo ni sahihi kwake kuvifanya.

Kwamfano katika habari hiyo ukianzia vifungu vya juu utaona vinamweleza mwanamke kahaba, anavyowateka watu kuzini naye. Na mtu mjinga ataona ni sahihi kwenda kwake, lakini mwisho wake ni mbaya. Watu wengi wanaacha ndoa zao nakwenda kuzini nje! Kwasababu wanaona kile wanachokipata huko nje, kina uzuri kuliko kile walichokizoea ndani, wengine wanafanya uasherati, kwasababu wanaona wakingojea mpaka wakati wa ndoa, watakosa mambo mengi. Hao ndio wanaotembea katika usemi huo  “Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza”

Wengine wanaona wakitumia njia ya udanganyifu, ndio zitawafikisha katika malengo yao kwa haraka, kuliko njia za halali, hivyo hujiingiza katika wizi, na magendo.

Lakini ukizidi kusoma mstari unaofuata anasema..

.  Lakini huyo hajui ya kuwa wafu wamo humo; Ya kuwa wageni wake wamo chini kuzimuni.

Maana yake ni kuwa wote wafanyao mambo kama hayo, mwisho wao unakuwa ni kifo, na kuishia kuzimu kabisa. Dumu katika ndoa yako, kataa vya wengine, epuka mambo ya sirini. Yusufu hakukubali kuzini na mke wa boss wake. Lakini Daudi alidanganyika akazini na mke wa kijakazi wake, matokeo yake yakawa na yeye kunajisiwa wake zake vilevile, mtoto wake kufa, na ufalme wake kutikiswa na mwana wake mwenyewe aliyeitwa Absalomu, lakini zaidi sana kupoteza furaha ya wokovu kwa miaka mingi sana. Daudi alijutia makosa yake kwa muda mrefu sana.

Hivyo usipumbazwe na vivutio vyovyote vya dhambi vitakugharimu sana.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Mithali 27:21  inaposema “mtu hujaribiwa kwa sifa zake?”

Fahamu maana ya Mithali 29:4 “Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

Jicho ni  nini (Yakobo 3:11)

NI NINI BWANA ANATAZAMIA KILA TUNAPOSHIRIKI MEZA YAKE.

KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni lazima nibadili jina baada ya kuokoka?

SWALI: Je ni lazima nibadili jina baada ya kuokoka, na kama ni hivyo ni mazingira gani yaliyo sahihi kufanya hivyo?


JIBU: Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu Kristo.

Unapookoka, ni vema kufahamu Kristo akishakukomboa amekombolewa kwelikweli, Huwezi kukosa mbingu kwasababu ya jina lako, hata kama linamaana mbaya, kwasababu wapo watu waliokuwa na majina mabaya, mmojawapo ni Yabesi ambaye jina lake lilimaanisha “huzuni”, kwasababu alizaliwa katika kipindi cha huzuni, na wazazi wake wakamwita hivyo lakini alimlingana na Mungu na Mungu akambariki na kumtukuza sana (1Nyakati 4:9-10).Lakini walikuwepo pia watu wenye majina mazuri mmojawapo Yuda, lakini tabia zake hazikuendana na jina lake.

Hivyo ikiwa jina lako si zuri sana, na huoni shida kuendelea nalo, huwezi kumkosa Mungu kwasababu ya hilo. Lakini pia, yapo mazingira ambayo, inampasa mkristo abadili jina endapo kuna ulazima wa kufanya hivyo. Na mazingira yenyewe ni kama haya;

  1. Umefunuliwa na Mungu mwenyewe: Wakati mwingine Mungu anaamua kumwambia mtu abadili jina, sio kwasababu jina lile ni baya, hapana, bali kwasababu ya kusudi alilowekewa mbele yake kulifanya. Kwamfano Mungu alimbadili jina Abramu, akamwita Ibrahimu, na tafsiri yake ni ‘Baba wa mataifa mengi’, hivyo huduma yake ya kuwa baba wa wengi, ilimpasa iendane na jina lake. Na ndivyo  ilivyokuwa kwa Sara na baadhi ya mitume.
  2. Jina lenye tafsiri ya imani nyingine/ au miungu: Yapo majina ambayo, ukiitwa mtu atatambua wewe ni wa dini nyingine, sasa hapa ni amani tu ya Kristo itawale ndani yako, ukiona ni vema ubadili, ni sawa, ili injili au ushuhuda wako usiwe na kikwazo kwa wengine mbeleni. Lakini bado hilo halikufanyi Mungu asikutumie, utatumiwa tu. Katika biblia tunaona Danieli, aliitwa jina la kipagani na Nebukadreza, Belteshaza (Danieli 1:7), Lakini hakuling’ang’ania hili jina, badala yake aliendelea kujiita Danieli, na mbingu pia ilimtambua hivyo. Japokuwa mfalme alimuita Belteshaza kufuatana na jina la miungu yake. Kwahiyo ikiwa jina lako halikaribiani na imani, ukiona vema kubadilisha hutendi dhambi.
  3. Maisha mapya:  Wakati mwingine historia yako ya nyuma, inaacha sifa mbaya katika jina lako. Kwamfano, ulikuwa ni mtu jambazi na mwizi, na unajulikana kwenye jamii kama ‘Yule Fulani kibaka’. Sasa wengi wanapookoka, wanasukumwa kabisa kubadilisha na majina yao, wawe wapya kote kote. Mfano mmojawapo wa hawa ni mtume Paulo, alikuwa mwuaji, na alikuwa anaitwa Sauli. Lakini alipomgeukia Mungu na jina lake pia akalibadili.
  4. Jina lisilo na tafsiri nzuri: Kumbuka pia wapo wengine wanakwazwa na tafsiri za majina yao. Labda anaitwa majuto, au shida, au msiba, au masumbuko. Hivyo anapookoka anapendelea ajiite majina ya ushindi au yenye Baraka. Hivyo anayechagua hili ni vizuri zaidi.

Kwahiyo hivyo ndio vigezo vya mtu kusukumwa abadili jina. Lakini usibadili kwasababu ya shinikizo la mtu, ikiwa huoni kikwacho chochote kuitwa jina hilo lako. Kwasababu wokovu wako, hauwezi kuzuiwa na jina. Hilo ulifahamu.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINA LAKO NI LA NANI?

MAANA YA MAJINA NA TAFSIRI ZAKE.

Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)

Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

KWA WINGI WA WASHAURI HUJA WOKOVU.

UPEPO WA KUSI HULETA MVUA;

Rudi nyumbani

Print this post