Tofauti kati ya ufunuo, unabii na maono ni ipi?

Tofauti kati ya ufunuo, unabii na maono ni ipi?

  1. UFUNUO

Ufunuo ni jambo ambalo hapo kabla lilikuwa limesitirika au limefungwa lakini sasa limefunuliwa. Kwa mfano katika biblia, utaona, Watu wengi walishindwa kumtambua Yesu ni nani, wengine walidhani ni Yeremia, wengine, mmojawapo wa manabii wa kale, wengine ni Yohana mbatizaji, Lakini Yesu alipowauliza mitume wake, Petro akasema, wewe ndiye Kristo mwana wa Mungu aliye hai. Yesu kusikia vile tunaona akamwambia maneno haya;

Mathayo 16:17 “Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu HAVIKUKUFUNULIA HILI, bali Baba yangu aliye mbinguni.

18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda”.

Unaona, Petro alifunuliwa, siri ambayo ilikuwa haijulikani na watu hapo kabla.

Vivyo hivyo na sisi tunahitaji ufunuo wa Roho Mtakatifu kuyaelewa  maandiko vinginevyo tutakuwa tunakisia tu au hatuyaelewi pale tunapoyasoma.

2) MAONO.

Ni taarifa ya rohoni ambayo mtu anapokea kutoka kwa Mungu,aidha anapokuwa usingizini, au akiwa macho. Anajikuta anaona vitu ambavyo hakupanga kuviona, na taarifa hizo zinaweza kuwa kwa mafumbo, au kwa uwazi, na zinaweza kueleza matukio yaliyopita au ya hapo hapo, au yale yatakayokuja baadaye.

Katika biblia tunaona watu wengi sana wakionyeshwa Maono..

Matendo 10:1 “Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia,

2 mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima.

3 Akaona katika maono waziwazi, kama saa tisa ya mchana, malaika wa Mungu, akimjia na kumwambia, Kornelio!

4 Akamtazama sana, akaogopa akasema, Kuna nini, Bwana? Akamwambia, Sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu.

5 Sasa basi, peleka watu Yafa, ukamwite Simoni, aitwaye Petro”.

3) UNABII

Ni taarifa ya wakati ujao, (utabiri wa rohoni), ambayo Mungu anautoa moja kwa moja, hiyo inaweza kuwa katika maneno ya mtu anayozungumza bila yeye kujua, mfano utasoma mstari huu kuhani mkuu alitoa unabii pasipokujua kama yeye aliutoa.

Yohana 11:51 “Na neno hilo yeye hakulisema kwa nafsi yake; bali kwa kuwa alikuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, alitabiri ya kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa hilo”.

au kwa njia ya kuambiwa au kuhubiriwa,

Ufunuo 11:3 “Nami nitawaruhusu mashahidi wangu wawili, nao watatoa unabii siku elfu na mia mbili na sitini, hali wamevikwa magunia”.

Hii ikiwa na maana kuwa katikati ya mafundisho, au mahubiri, Mungu huwa anatoa unabii wa mambo yajayo ndani yake.

1Timotheo 1:18 “Mwanangu Timotheo, nakukabidhi agizo hilo liwe akiba, kwa ajili ya maneno ya unabii yaliyotangulia juu yako, ili katika hayo uvipige vile vita vizuri”;

Kwa njia ya kuonyeshwa au kwa maono.

Yuda 1:14 “Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu”,

Pia  kitabu chote cha Ufunuo ni kitabu kitabu cha unabii, ambacho Yohana alionyeshwa kwa njia ya maono.

Ufunuo 22:6 “Kisha akaniambia, Maneno haya ni amini na kweli. Naye Bwana, Mungu wa roho za manabii, alimtuma malaika wake kuwaonyesha watumwa wake mambo ambayo hayana budi kuwako upesi.

7 Na tazama, naja upesi; heri yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki”.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Mafundisho

UFUNUO: Mlango wa 1

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

THAWABU YA UAMINIFU.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments