JE! HAMPOTEI KWA SABABU HII?

JE! HAMPOTEI KWA SABABU HII?

Jina la Bwana wetu Yesu libarikiwe daima. Karibu tuyatafakari maandiko pamoja ndugu yangu.

Wakati ule masadukayo walimfuata Bwana Yesu, na kumuuliza maswali ambayo, ndio yaliyowafanya waamue kuwa  masadukayo kama walivyo wasioamini  kuwa kuna kitu kinachoitwa ufufuo wa wafu. Na swali lenyewe lilikuwa ni kuhusu ndoa baada ya kifo..Walikuwa na sababu nzuri kabisa za kufikirika kwa akili za kibinadamu, kwamba kama kiyama ipo basi Musa asingeruhusu mtu kuoa mke wa mtu baada ya kufa, ili huko ng’ambo kusiwe na migongano ya kindoa,.Lakini kama aliruhusu kuoa mke wa marehemu, ni wazi kuwa mambo yote ni ya hapa hapa duniani, hakuna kufufuliwa wafu.

Embu Tusome kwa ufupi habari yenyewe na pale mwishoni lipo jambo ambalo Bwana atatufundisha siku ya leo..

Anasema..

Marko 12:18 “Kisha Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza na kusema,

19 Mwalimu, Musa alituandikia ya kwamba ndugu ya mtu akifa, akamwacha mkewe wala hana mtoto, ndugu yake amtwae yule mkewe akampatie ndugu yake mzao.

20 Basi kulikuwa na ndugu saba, wa kwanza akatwaa mke, akafa, asiache mzao.

21 Wa pili naye akamtwaa akafa, wala yeye hakuacha mzao. Na wa tatu kadhalika;

22 hata na wote saba, wasiache mzao. Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.

23 Basi, katika kiyama atakuwa mke wa yupi katika hao? Maana wote saba walikuwa naye.

24 Yesu akajibu, akawaambia, JE! HAMPOTEI KWA SABABU HII, KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO WALA UWEZA WA MUNGU?

Kama tunavyosoma hapo kulingana na maneno ya Bwana Yesu, aliona watu hao wamepotea, na kupotea kwako kulichangiwa na sababu mbili kubwa, ya kwanza 1) Walikuwa hawayajui maandiko 2) Walikuwa hawaujui uweza wa Mungu.

Hizi ni sababu kuu ambazo zinaweza kumfanya mtu apotee hata leo hii, aidha katika Dini za uongo kama hawa Au arudi nyuma katika ulimwengu kabisa aseme, haya mambo hayawezekani.

  1. Tukianzana na kutokuujua uweza wa Mungu

Hawa mafarisayo, waliishi kwa fikra za kibinadamu na sio kwa fikra za Ki-Mungu, hawakukaa kujiuliza hao malaika wanaishije ishije huko mbinguni, bila kuoana au kuzaliana lakini bado wanaishi kwa furaha mbele za Mungu. Hata leo hii, Hawakujua kuwa Mungu pia anao uwezo wa kuwafanya kama Malaika. Akaondoa katika miili yao tamaa za mwili, wakawa ni miili ya utukufu isiyokuwa na mapungufu, isiyosinzia, isiyoumwa, isiyochoka kama wao..Hilo hawakuliwaza, kwasababu hawakuujua uweza wa Mungu kuwa unaweza kufanya na hilo pia.

Imani kama hizo hata leo zipo katika baadhi ya dini, wakidhani kuwa mtu akifa atakwenda kupewa wake 70 huko mbinguni. Hiyo yote ni kwasababu hatuujui uweza wa Mungu.

Kukosa kuujua uweza wa Mungu hata sasa, kunawafanya watu wengi, wapotee sana, wakidhani pia Mungu hawezi kuwaokoa wanadamu wakiwa hapa duniani..kwa kuwafanya wawe watakatifu..Na hiyo inawapelekea wajidanganye hivyo hivyo kwamba hakuna mtu anayeweza kushinda dhambi akiwa duniani, na matokeo yake wanakufa katika dhambi zao, na mwisho wa siku wanajikuta wapo kuzimu.

Kumbe hawajua uweza huo wa kufanywa wakamilifu hautoki kwa mwanadamu bali kwa Mungu pale mtu anapomwamini na kumpokea. Alisema..

Yohana 1:12 “Bali wote waliompokea ALIWAPA UWEZO wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;”

Mtu akimwamini Kristo, na kumtii yeye, kitu kinachotokea kwake ni kupokea uwezo mpya, wa kufanyika mwana wake wa kushinda dhambi. Ukishindwa kuyajua hayo, basi ni rahisi sana kupotea..

2) Sababu ya pili ni: Ni kutojua Maandiko.

Tukirudi kwenye lile swali lao walilomuuliza tunaona mbele kidogo Bwana akiwauliza, HAMJASOMA?. Akitazamia kuwa kama wangekuwa wamesoma vema wasingekuwa na swali kama hilo..

Marko 12:26 “Na kwa habari ya wafu ya kwamba wafufuliwa, hamjasoma katika kitabu cha Musa, Sura ya Kijiti, jinsi Mungu alivyomwambia, akisema, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo?

27 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. HIVYO MWAPOTEA SANA”.

Unaona? Dini ambayo ilikuwa imeshakita mizizi yenye wafuasi wengi, kama baadhi ya dini nyingi leo hii duniani lakini kumbe ilikuwa imeshapotea kwa kutoyajua tu maandiko.

Leo hii watu wengi wamepotoshwa kwa kutoyafahamu maandiko, ukiona unaabudu sanamu, Ukiona unashikilia sabato na kusema huo ndio muhuri wa Mungu, wakati biblia inasema muhuri wa Mungu ni Roho Mtakatifu (Waefeso 4:30) ujue umepotoshwa na dini, ukiona unaabudu sanamu na kudhani kuwa zile ni viunganishi au vipatanishi na Mungu basi ujue umepotoshwa.

Hivyo sote kwa pamoja ni sharti tuufahamu uweza wa Mungu, kwamba hapa duniani wokovu upo, na watakatifu pia wapo, na kwamba pasipo utakatifu hakuna mtu atakayemwona Mungu asipokuwa nao sawasawa na (Waebrania 12:14) vilevile tuyasome maandiko, tuyatafakari sana, kila siku ili tusije tukazama katika madanganyo ya dini au madhehebu, au upotofu wa kidunia uliopo leo hii duniani.

Tukizingatia hayo mawili kama Bwana Yesu alivyosema, tusahau kupotea.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya ufunuo, unabii na maono ni ipi?

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

Neema ni nini?

Je! Ni dhambi kumpiga au kumuua mnyama bila sababu yoyote?

CHANGIA SASA.

MAPEPO YANATAFUTA HIFADHI NDANI YAKO KWA BIDII SANA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
2 years ago

Mbarikiw