Title December 2022

MIEZI 13 YA KIYAHUDI.

Tofauti na Kalenda ya Kirumi ambayo ndiyo tunayoitumia sasa yenye miezi 12, Kalenda ya kiyahudi yenyewe inakuwa na miezi 13 kwa mara saba kila baada ya miaka 19. (Yaani katika kipindi cha miaka 19, miaka 7 inakuwa na miezi 13, na miaka 12 iliyosalia inakuwa na miezi 12 kama kawaida), Na miaka yenye miezi 13 ni inakuwa ni mwaka wa 3, 6,8,11,14, 17 na 19 na mzunguko wa miaka 19, unapoisha na unapoanza mzunguko mwingine, basi mgawanyo wa miezi unakuwa ni huo huo, wa baadhi ya miaka kuwa na miezi 13 na mingine 12.

Sasa mwezi wa 13, unaoongezeka juu ya miezi 12 ya kiyahudi ni mwezi ujulikanao kama Adari II, Sasa kabla ya kwenda kuutazama huu mwezi wa 13 wa Adari, hebu tuitazame miezi 12, na rejea zao katika biblia.

Mwezi wa 1: Abibu au Nisani.

Mwezi wa Abibu au Nisani ni mwezi wa kwanza katika kalenda ya kiyahudi, mwezi huu unaanza katika mwezi Machi katikati na kuisha mwezi Aprili katikati katika kalenda yetu ya kirumi tunayoitumia..

Mwezi wa Abibu ndio mwezi ambao wana wa Israeli walitoka Misri..

kutoka 13:3 Musa akawaambia hao watu, Kumbukeni siku hii, mliyotoka nchi ya Misri, kutoka nyumba ya utumwa; kwa kuwa Bwana aliwatoa mahali hapa kwa nguvu za mkono wake; na usiliwe mkate uliochachwa.

 4 Ninyi mwatoka leo katika MWEZI WA ABIBU.

Na wakati ambapo Hamani ananyanyuka kutaka kuwaangamiza Israeli yote katika ufalme wote wa Ahasuero, tunasoma wazo hili lilimjia katika Mwezi wa Nisani/ Abibu..

Esta 3:7 “Basi mwezi wa kwanza, ndio MWEZI WA NISANI, mwaka wa kumi na mbili wa mfalme Ahasuero, wakapiga Puri, yaani kura, mbele yake Hamani; siku kwa siku, na mwezi kwa mwezi, hata mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari”.

Na pia tunausoma huu mwezi ukitajwa wakati Nehemia alipoingiwa na wazo la kwenda kuujenga Yerusalemu..

Nehemia 2:1 “Ikawa katika MWEZI WA NISANI, mwaka wa ishirini wa mfalme Artashasta, na divai imewekwa mbele yake, nikaishika ile divai, nikampa mfalme. Nami mpaka sasa sikuwa na huzuni mbele ya mfalme wakati wo wote.”.

 Mwezi wa 2: Zivu au Ayari

Mwezi huu unaangukia kati ya mwezi Aprili na mwezi May kwa kalenda yetu tunayoitumia, na ni mwezi wa pili katika kalenda ya kiyahudi.

Mwezi huu ndio mwezi ambao Mfalme Sulemani alianza kulijenga Hekalu la Mungu katika Yerusalemu..

1Wafalme 6:1 “Ikawa katika mwaka wa mia nne na themanini baada ya kutoka wana wa Israeli katika nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa kutawala kwake Sulemani juu ya Israeli, katika MWEZI WA ZIVU, ndio mwezi wa pili, akaanza kuijenga nyumba ya Bwana.

 2 Nayo nyumba hiyo mfalme Sulemani aliyomjengea Bwana, urefu wake ulikuwa mikono sitini, na upana wake ishirini, na kwenda juu kwake mikono thelathini”.

Mwezi wa 3: Siwani

Huu ni mwezi wa tatu kwa kalenda ya kiyahudi, lakini kwa kalenda yetu ni mwezi unaoangukia kati ya mwezi Mei na mwezi Juni.

Katika mwezi huu ndio mwezi ambao Mfalme Ahasuero, enzi za malkia Esta alitoa ruksa kwa wayahudi kujilipizia kisasi juu ya adui zao.

Esta 8:9 “Basi, waandishi wa mfalme wakaitwa pale pale, siku ya ishirini na tatu ya mwezi wa tatu, ndio MWEZI WA SIWANI; na kama vile Mordekai alivyoamuru, Wayahudi wakaandikiwa, pamoja na maakida na maliwali, na wakuu wa majimbo toka Bara Hindi mpaka Kushi, majimbo mia na ishirini na saba, kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake; na Wayahudi kwa mwandiko wao na kwa lugha yao”.

Mwezi wa 4: Tamuzi

Huu ni mwezi wa Nne katika kalenda ya kiyahudi, lakini kwetu sisi unaanguka katika ya mwezi Juni na mwezi Juni na mwezi Julai.

Mwezi huu katika bibli unaonekana kutajwa mara moja tu katika kitabu cha Ezekieli.

Ezekieli 8:14 “Ndipo akanileta mpaka mlango wa kuingilia katika nyumba ya Bwana, ulioelekea upande wa kaskazini, na tazama, wanawake wameketi wakimlilia TAMUZI”.

Mwezi huu wa nne umetajwa sehemu nyingine kama kwa namba na si kwa jina (Soma Yeremia 39:1-2, na Yeremia 52:6-7).

Mwezi wa 5: Avu

Huu ni mwezi wa tano kwa wayahudi na kwetu sisi unaangukia kati ya mwezi wa Julai na Mwezi Agosti.. Mwezi huu katika biblia haijatajwa kwa jina bali kwa namba..

Kwamfano tunasoma Ezra aliwasili Yerusalemu katika mwezi wa 5

Ezra 7:8 “Naye Ezra akafika Yerusalemu mwezi wa tano katika mwaka wa saba wa huyo mfalme”

Na pia katika (2 Wafalme 25:8-10, Yeremia 1:3 na Yeremia 52:12-30)

Mwezi wa 6: Eluli

Huu ni mwezi wa 6 kwa kalenda ya kiyahudi na unaangukia kati ya mwezi wa Agosti na Septemba katika kalenda yetu.

Katika biblia mwezi huu ndio mwezi ambao Nehemia alimaliza kati ya kuukarabati ukuta Yerusalemu..

Nehemia 6:15 “Basi huo ukuta ukamalizika siku ya ishirini na tano ya mwezi wa ELULI, katika muda wa siku hamsini na mbili”

Mwezi huu pia umetajwa kwa namba katika kitabu cha Hegai 1:14-15.

Mwezi wa 7: Ethanimu

Huu ni mwezi wa 7 kwa kalenda ya kiyahudi na kwa kalenda yetu unaangukia katika ya mwezi wa Septemba na Oktoba.

Hekalu la Sulemani liliwekwa wakfu katika mwezi huu wa Ethanimu

1Wafalme 8:1 “Ndipo Sulemani alipowakusanya wazee wa Israeli, na wakuu wote wa kabila, wakuu wa mbari za mababa wa wana wa Israeli, wamwendee mfalme Sulemani huko Yerusalemu, ili walipandishe sanduku la agano la Bwana kutoka mji wa Daudi, yaani, Sayuni. 

2 Wakakutana mbele ya mfalme Sulemani watu wote wa Israeli wakati wa sikukuu, katika MWEZI WA ETHANIMU, ndio mwezi wa saba.  3 Wazee wote wa Israeli wakaja, nao makuhani wakajitwika sanduku”

Unaweza kuusoma pia mwezi huu katika..(1Wafalme 8:2, Walawi 23:24, Nehemia 8:13-15).

Mwezi wa 8: Buli.

Mwezi huu ni mwezi wa 8 kwa kalenda ya kiyahudi na unaangukia kati ya mwezi Octoba na mwezi mwezi Novemba katika kalenda yetu ya kirumi.

Katika mwezi huu ndio mwezi ambao Sulemani alimaliza kuijenga nyumba ya Mungu (Hekalu).

1Wafalme 6:38 “Hata katika mwaka wa kumi na mmoja, katika MWEZI WA BULI, ndio mwezi wa nane, nyumba ikaisha, mambo yake yote, na sharti zake zote. Basi muda wa miaka saba alikuwa katika kuijenga.

Unaweza kusoma pia habari za mwezi huu katika  (1Wafalme 12:32-33, 1Nyakati 27:11).

Mwezi wa 9: Kisleu

Huu ni mwezi wa 9 kwa kalenda ya kiyahudi na unaangukia kati ya mwezi wa Novemba na Disemba katika kalenda yetu ya sasa ya kirumi.

Katika mwezi huu Nabii Zekaria alioneshwa maono juu ya Yuda na Israeli.

Zekaria 7:1 “Ikawa katika mwaka wa nne wa mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria, siku ya nne ya mwezi wa kenda, yaani, KISLEU”

Mwezi wa 10: Tebethi

Huu ni mwezi wa 10 kwa Wayahudi na kwa kalenda ya kirumi unaangukia kati ya mwezi Disemba na January.

Katika biblia mwezi huu ndio mwezi ambao Esta aliingizwa katika nyumba ya kifalme..

Esta 2:16 “Basi Esta alipelekwa kwa mfalme Ahasuero, katika nyumba ya kifalme, mwezi wa kumi, ndio mwezi wa Tebethi, mwaka wa saba wa kumiliki kwake. 

17 Mfalme akampenda Esta kuliko wanawake wote, naye akapata neema na kibali machoni pake kuliko mabikira wote; basi akamtia taji ya kifalme kichwani pake, akamfanya awe malkia badala ya Vashti”.

Na ndio mwezi ambao Nebukadreza aliuhusuru Yerusalemu (2Wafalme 25:1, Yeremia 52:4).

Mwezi wa 11: Shebati

Mwezi huu unaangukia kati ya mwezi Januari na mwezi Februari kwa kalenda ya kirumi na katika kalenda ya kiyahudi ni mwezi wa 11.

Katika mwezi huu ndio mwezi ambao Zekaria aliona maono tena juu ya Yerusalemu..

Zekaria 1:7 “Siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani, mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria, mwana wa Berekia, mwana wa Ido, nabii, kusema,

 8 Naliona wakati wa usiku, na tazama, mtu amepanda farasi mwekundu, akasimama kati ya mihadasi iliyokuwa mahali penye uvuli; na nyuma yake walikuwapo farasi wengine wekundu, na wa rangi ya kijivujivu, na weupe”.

Mwezi wa 12: Adari I.

Huu ni mwezi wa 12 na wa mwisho kwa kalenda za kiyahudi, ambapo kwa kalenda ya kirumi unaangukia kati ya Mwezi Februari na mwezi Machi.

Esta 3:7 “Basi mwezi wa kwanza, ndio mwezi wa Nisani, mwaka wa kumi na mbili wa mfalme Ahasuero, wakapiga Puri, yaani kura, mbele yake Hamani; siku kwa siku, na mwezi kwa mwezi, hata mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari”.

Kutokana na kuwepo na miaka mirefu na mifupi, Marabi wa kiyahudi katika karne ya 4, wakiongozwa na Rabbi Hillel II, waliongeza mwezi mmoja wa 13, katika kalenda ya kiyahudi ambao waliuita mwezi ADARI II (Adari wa pili).

Lengo la kuongeza mwezi huu ni ili kuziweka sikukuu za kiyahudi katika majira halisia, vinginevyo sikukuu za kiyahudi zingeangukia misimu ambayo sio, kwamfano sikukuu ya pasaka ambayo kwa wayahudi inaseherekewa katika mwezi wa March au April kwa kalenda yetu, kama kusingekuwepo huu mwezi wa 13, basi huenda miaka mingine sikukuu hii ingeangukia mwezi wa 8 kwa kalenda yetu, jambo ambalo lingekuwa halina uhalisia hata kidogo.

Lakini swali ni je!, sisi wakristo tunapaswa kuifuata kalenda ipi?, ya kiyahudi au hii inayotumika sasa ya kirumi?

Jibu ni kuwa Kalenda hazitusogezi karibu na Mungu wala hazipeleki mbali na Mungu,  tukitumia kalenda ya kiyahudi, au ya kirumi au ya kichina au hata ya kichaga haituongezei chochote, kilicho cha muhimu ni kuishi kwa kuukomboa wakati kama biblia inavyosema katika..

Waefeso 5:15 “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;

16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu”

Na tunaukomboa wakati kwa kufanya yale yanayotupasa kufanya, ikiwemo Kujitakasa, kufanya ibada, kuomba, kusoma Neno, kuifanya kazi ya Mungu kupitia karama iliyo ndani yako kabla ya ule mwisho kufika na mambo mengine yote yanayohusiana na hayo.

Bwana akubariki.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mwandamo wa mwezi/Mwezi mpya Ni nini kibiblia?

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

Je! kuna sikukuu za pasaka mbili? (Hesabu 9:11)

Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?

Nini maana ya wokovu watoka kwa Wayahudi? (Yohana 4:22)

Rudi nyumbani

Print this post

AKAKIVUNJA KIBWETA AKAIMIMINA KICHWANI PAKE.

Yesu alipokuwa nyumbani kwa Yule Simoni mkoma, alitokea mwanamke mmoja na kufanya jambo ambalo lilizua malalamika mengi sana kwa wale waliokuwa pale, kama tunavyoifahamu habari, mwanamke Yule alikuwa na kibweta (kijagi), kilichojaa marhamu(pafyumu), na thamani yake ilikuwa ni kubwa sana, ni sawa na pesa za kitanzania, milioni 6, Mshahara wa mwaka wa mtu anayelipwa vizuri.

Lakini maandiko yanatuambia, mwanamke Yule hakufungua tu kile kifuniko cha kibweta ili aimimine pafyumu  kichwani pa Yesu hapana, bali “ alikivunja kabisa”, kwa namna nyingine aliharibifu kijagi hicho, kuonyesha kuwa hii pafyumu haitatumiwa tena sehemu nyingine yoyote, itaishia yote hapa, na hilo ndio lililowafanya wale watu waliokuwa pale walalamike, na kusema upotevu wote huu wa nini?..

Anaimwaga pafyumu yote kama maji, lakini Yule mwanamke hakujali, aliimaliza yote, mpaka nyumba yote ikiwa inanuka pafyumu.

Tusome kidogo..

Marko 14:3  “Naye alipokuwapo Bethania, nyumbani mwa Simoni mkoma, ameketi chakulani, alikuja mwanamke mwenye kibweta cha marhamu ya nardo safi ya thamani nyingi; akakivunja kibweta akaimimina kichwani pake.

4  Palikuwa na watu waliochukizwa katika nafsi zao wakisema, Kwani kupoteza marhamu namna hii? 5  Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa dinari mia tatu na kuzidi, wakapewa maskini. Wakamnung’unikia sana yule mwanamke.

6  Yesu akasema, Mwacheni; mbona mnamtaabisha? Amenitendea kazi njema;7  maana sikuzote mnao maskini pamoja nanyi, na kila mpendapo mwaweza kuwatendea mema; lakini mimi hamnami sikuzote.

8  Ametenda alivyoweza; ametangulia kuupaka mwili wangu marhamu kwa ajili ya maziko. 9  Amin, nawaambia, Kila ihubiriwapo Injili katika ulimwengu wote, na hili alilotenda huyu litatajwa kwa kumbukumbu lake”

Nachotaka tuone juu ya habari hii, ni kwamba tunaweza kudhani kuwa ni huyu mwanamke tu, ndiye aliyekuwa na kibweta kile cha thamani,..Ukweli ni kwamba wale wote walikuwa na vibweta vyao, isipokuwa tu katika maumbile tofuati.. kuna mahali walivivunja au watavivunja, na kutumia kwa ajili ya vitu watakavyoviona vya thamani..

Hata sasa, kila mmoja wetu anachokibweta chake, ni suala tu la muda.. Utajiuliza, unamtazama msanii Fulani kwenye tv, anamwaga pesa, na kuwapa makahaba, au ananunua gari la kifahari, halafu wewe unaanza kulalamika na kusema upotevu wote huo wa nini, si ni heri angewasaidia maskini, kuliko kutumia kwa anasa.. Usimlaumu kibweta chake ndio amekivunjia hapo.

Leo hii, utaona, mtu kumtolea Mungu, au kusapoti huduma ambazo zinamsaidia kiroho ni ngumu, hata halifikirii.. Lakini mwanawe akitaka kwenda shule, atahangaika kila mahali kumtafutia ada, au akiumwa, anahitaji kwenda kutibiwa India, atauza, gari mpaka shamba, kusudi kwamba aokoe maisha ya mwanawe..Hicho ni kibweta chake amekivunja.

Kuonyesha kuwa kumbe anaweza kupoteza chochote cha thamani kwa ajili ya kitu cha muhimu. Tujiulize, Utasema mimi sina kibweta cha thamani..Ukweli ni kwamba unacho, bado hujaona mahali pa muhimu pa kukimwaga. Wakati utafika tu,.

Tujiulize, vipi kuhusu Mungu wetu..Yesu wetu aliyetuokoa, twaweza kudhubutu kuwa kama huyu mwanamke? Ambaye alikivunjia kwa Bwana?..Hakujua kwa kufanya vile, injili yake itahubiriwa kizazi baada ya kizazi.. Na Yesu ni yeye Yule jana na leo na hata milele.. Kama alimfanyia huyu, anaweza pia akakufanyia na wewe, kwa namna yako..Lakini ni lazima ukivunje kibweta chako kwake..Kumbuka Bwana anasema maskini manao siku zote,..Unafurahi vipi, Bwana akuhudumie, halafu wewe umuhudumii?

Tafakari.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

USICHELEWE KUMPAKA BWANA MARHAMU!

YESU HAYUPO KATIKA MAZINGIRA YALEYALE TU SIKUZOTE, USIJISAHAU.

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Rudi nyumbani

Print this post

MIGAWANYO MINNE (4), YA HUDUMA YA YESU.

1.) DUNIANI (miaka 33 na nusu)

2) KUZIMU (Siku tatu)

3) MBINGUNI (Miaka elfu mbili na …)

4) DUNIANI TENA (Miaka 1000)

Ni vema tukaifahamu hii migawanyo kwa kina ili tujue huduma ya Bwana wetu Yesu sasa ni ipi kwa watu wake.

1.DUNIANI (miaka 33 na nusu):

 Bwana aliposhuka duniani, aliishi miaka thelathini na tatu na nusu, ndani ya miaka hii alikuwa na lengo la kuwafundisha na  kuwakomboa wanadamu wote kutoka katika laana ya dhambi na mauti. Na siku ile alipokwenda msalabani, ndipo akakamilisha kusudi hili. Ndio pale aliposema IMEKWISHA. Akiwa na maana  kuwa kuanzia huo wakati na kuendekea kila mwanadamu atakayemwamini yeye ni lazima aokolewe.

Kusudi lake la kwanza likawa limekwisha.

2) KUZIMU (Siku tatu):

Kusudi la pili lilikuwa ni kuzimu.  

Pindi tu alipokufa hakwenda mbinguni moja kwa moja bali alishuka kuzimu. Kuzimu ni mahali pa wafu. Hivyo zamani wafu wote waliokuwa wema na waovu, wote walikuwa wapo makaburini, isipokuwa waovu walitengwa mahali pao mbali na wema. Waovu walikuwa katika vifungo vya hukumu. Lakini wema walikuwa sehema salama. 

Sasa Bwana Yesu aliposhuka kuzimu, alifanya huduma kwa makundi yote mawili. Kwamfano lile Kundi la waovu alikwenda kulihubiria makosa yao, ni kwanini wamestahili hukumu, Soma..

1Petro 3:19 “ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri;

20 watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji”.

Maana yake ni kuwa hata sasa, ikiwa utakufa katika dhambi, ni moja kwa moja utakwenda huku wafu hawa walipo ambapo hapana raha, ndio Jehanamu yenyewe iliyopo chini ya dunia.

 Lakini  walio wema Bwana Yesu aliwachukua na kuwafungua kutoka katika vifungo vya kaburi, na kuwahamishia mahali pazuri sana  pajulikanapo kama peponi.

Mathayo 27:50 “Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.

51 Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;

52 makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala;”

Hivyo ikiwa wewe ni mtakatifu ukifa sasa, hutajiona ukishuka makaburini, bali utajiona ukichukuliwa juu, mbinguni. Lakini sio kule Kristo alipokwenda,(huko tutafika baadaye) bali katika mbingu ya katikati, ambayo hiyo utakaa huku ukisubiria ule ukombozi wa miili yetu, Siku ile ya Unyakuo. Ambapo kwa pamoja utaungana na watakatifu walio hai, na moja kwa moja kwenda mbinguni kule Kristo alipo kwenye karama ya mwana-kondoo. Hivyo hudumu hii ya Yesu iliishia pale siku ile alipofufuka.(1Wakorintho 15:51-55)

  1. 3) MBINGUNI (Miaka elfu mbili na …)

Hii ndio huduma ambayo mpaka sasa inaendelea ya mwokozi wetu. Alisema mwenyewe maneno haya..

Yohana 14:1 “Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.

2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.

3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo”.

Mpaka anasema ninakwenda kuwaandalia makao, maana yake ni kuwa hapo kabla sisi hatukuwa na makao yoyote mbinguni. Hivyo makao haya ndio ile Yerusalemu mpya, ambayo itashuka kutoka kwa Mungu mbinguni, baada ya utawala wa miaka 1000 kuisha.

Haya ni makao ya milele, hivyo hatushangai ni kwanini hadi sasa Bwana anatuandalia. Bwana atusaidie tusiikose ile mbingu mpya na nchi mpya ambayo Yerusalemu mpya ipo ndani yake. Ni makao ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia. Huko tutamashangaa Mungu sana, kwa kipindi kisichokuwa na mwisho.

  • 4) DUNIANI tena (Miaka 1000):

Huu ndio wakati wa ule utawala wa miaka elfu moja, ambao Kristo atakuja kutawala na watakatifu wake, hapa duniani, ndio kule kurudi kwa pili kwa Yesu Duniani, akiwa kama Mfalme wa wafalme, na Bwana wa Mabwana.  Ni wakati wa sabato ya watakatifu wote. Utajiuliza kulikuwa na umuhimu gani Mungu kuipitisha kwanza hii miaka 1000, na sio tuingie moja kwa moja kwenye Yerusalemu yake iliyo ndani ya mbingu mpya na nchi mpya?

Ni kwasababu Bwana anataka kuwahakikishia watu wake kuwa hakuna chochote walichokipoteza pindi walipokuwa wanataabika kwa ajili yake hapa duniani, pindi walipojikana, kwa kuacha kila kitu, na kudharauliwa,.hivyo ili kuwaonyesha hakuna walichokipoteza, atawarudishia hiyo miaka ya raha, na wenyewe watakuwa wafalme na Mabwana duniani. Wakati huo dunia haitakuwa kama hii tena, bali itarejezwa hata zaidi ya Edeni, na amani itakuwepo duniani.(Soma Ufunuo 20:1-4). Watatawala pamojanna Kristo kwa amani na furaha isiyoelezeka.

Ndugu, tukiyaona haya, tunatambua sasa wakati tuliobakiwa nao ni mchache sana. Siku yoyote unyakuo utapitia, mlango wa neema utafungwa, dalili zote zimeshatimia Jiulize Je, umejiandaaje? Au umejiwekaje tayari kumpokea Bwana Yesu. Na hata kama hatarudi wakati wako. Ukifa leo hii, huko uendako utakuwa ni mgeni wa nani?

Yesu yupo mlangoni kurudi, tubu dhambi zako ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, upate ondoleo la dhambi zako. Hizi ni siku za mwisho. Tunachokisubiri sasa ni unyakuo tu, dalili zote zimeshatimia.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 3)

Je mbinguni itakuwa ni kuimba tu wakati wote?.

KWANINI KUWE NA UTAWALA WA MIAKA 1000

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Kukaramkia ni kufanya nini? (2Wakorintho 7:2)

Swali: Kukaramkia ni nini?

Jibu: Tusome,

2Wakorintho 7:2  “Tupeni nafasi mioyoni mwenu. Hatukumdhulumu mtu ye yote, wala kumharibu mtu, wala kumkaramkia mtu.

3  Sisemi neno hilo ili niwahukumu ninyi kuwa na hatia; kwa maana nimetangulia kusema, ya kwamba ninyi mmo mioyoni mwetu hata kwa kufa pamoja, na kuishi pamoja”

“Kukaramkia” ni Kiswahili kingine cha neno “Utapeli” (ambao unahusisha kuchukua fedha kutoka kwa mtu kwa njia ya ulaghai wa maneno). Mfano wa watu wanaokaramkia watu ni manabii wa uongo, na makristo wa uongo!, ambao wanaweza kutumia chochote kile kudanganya nacho watu, ili lengo lao wapate fedha kutoka kwao. ( Na fedha hizo ndizo zijulikanazo Kama mapato ya aibu, ambayo yanatajwa katika kitabu Cha Tito 1:7)

Katika siku hizi za mwisho manabii wa uongo wanatumia maji, mafuta, udongo na vyote vijulikanavyo kama visaidizi vya upako kulaghai watu, hivyo wanawakaramkia watu na kuchukua fedha zao na mali zao, huku wakiwaaminisha kuwa matatizo yao yameondoka.

Watumishi hawa wa uongo, maandiko yanasema kuwa mungu wao ni tumbo!!..

Wafilipi 3:17 “Ndugu zangu, mnifuate mimi, mkawatazame wao waendao kwa kuufuata mfano tuliowapa ninyi.

18  Maana wengi huenenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, kuwa ni adui za msalaba wa Kristo;

19  mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.

20  Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo”

Mitume wa kanisa la kwanza hawakumkaramkia mtu yeyote, ili kupata faida.. Zaidi walihubiri injili kamili yenye kumgeuza mtu kutoka katika dhambi kuingia katika haki kupitia Yesu Kristo.

Na sisi hatuna budi kuwa kama hao, tuifanye kazi ya Mungu bila kumkaramkia mtu yeyote.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya ELOHIMU?

Kwa namna gani mauti hufanya kazi ndani yetu na uzima kwa wengine? (2Wakorintho 4:12).

Je jina Eva na Hawa ni sawa?

USHIRIKA WA ROHO MTAKATIFU UKAE NANYI NYOTE.

JIHADHARI NA DHAMBI YA WIVU/HUSUDA.

Rudi nyumbani

Print this post

NAFASI YAKO WEWE MAMA KWA MTOTO NA WAJUKUU WAKO NI IPI?.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu, lihimidiwe.. karibu tujifunze biblia..

Neno la Mungu linasema..

Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”

Faida ya kumlea mtoto wako katika njia inayompasa ni kwamba atakapokuwa mzee hataiacha, na maana yake zaidi ni kwamba hawezi kufikia uzee kabla na yeye kuwa na watoto wake.. hivyo na wajukuu wako pia watanufaika kwa malezi yako wewe kwa mwanao, kwasababu kile mwanao alichokipokea kutoka kwako, na yeye atawafundisha watoto wake, hivyo kizazi chako chote hata cha tatu na cha nne au zaidi ya hapo kitakuwa kitakatifu na cha baraka.

Ukiona kuna shida kwa mjukuu, basi ujue kuwa shida ilianzia kwa bibi au babu, ikaingia kwa mtoto na kisha ikamalizikia kwa mjukuu.. Lakini kama babu au bibi alimlea mwanae katika njia inayompasa, ya kumcha Mungu na kumpenda Mungu, huyo mtoto naye pia ni lazima atawafundisha watoto wake njia hiyo hiyo, na hivyo wajukuu watakaozaliwa basi watakuwa wenye mwenendo mwema wa kumpendeza Mungu.

Tuangalie mfano mmoja wa kwenye biblia wa mtu aliyemlea vyema mtoto wake, na hata mjukuu aliyezaliwa akawa na mwenendo mzuri.

Mtu huyo si mwingine zaidi ya BIBI LOISI, ambaye alikuwa na binti yake aliyeitwa EUNIKE, ambaye ndiye aliyemzaa Askofu Timotheo, mtumwa wa Bwana..

2Timotheo 1:4  “Nami natamani sana kukuona, nikiyakumbuka machozi yako, ili nijae furaha;

5  nikiikumbuka imani uliyo nayo isiyo na unafiki, ambayo ilikaa kwanza katika bibi yako Loisi, na katika mama yako Eunike, nami nasadiki wewe nawe unayo”.

Hapa tunaona Paulo anamwandikia waraka Timotheo, na kukiri chanzo cha imani yake Timotheo, kwamba ilianzia kwa bibi yake Loisi, na hatimaye kwa mama yake aliyeitwa Eunike, na ndipo ikaja kwake, ikimaanisha kuwa msingi wa Timotheo kumpenda Mungu haukuanzia kwake, bali ulianzia kwa bibi yake huko.. Ndio maana ikawa hata vyepesi Timotheo kuiamini injili ya Bwana Yesu na hata kuja kuwa Askofu wa makanisa mengi,  na ndiye aliyekuwa pamoja na Paulo mpaka hatua ya mwisho.

Timotheo hakuwa Mwisraeli moja kwa moja, bali mama yake ndiye aliyekuwa mwisraeli, lakini baba yake alikuwa myunani… pamoja na mchanganyiko huo lakini malezi ya bibi yake na mama yake yalimfanya awe mwenye mwenendo bora kuliko vijana wengi.

Matendo 16:1  “Basi akafika Derbe na Listra, na hapo palikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, mwana wa mwanamke Myahudi aliyeamini; lakini babaye alikuwa Myunani.

2  Mtu huyo alishuhudiwa vema na ndugu waliokaa Listra na Ikonio.

3  Paulo akamtaka huyo afuatane naye, akamtwaa akamtahiri kwa ajili ya Wayahudi waliokuwako pande zile; kwa maana wote walijua ya kuwa babaye ni Myunani”.

Je na wewe kama mzazi un akitu gani cha kuwarithisha watoto wako na wajukuu wako?… je ni elimu tu ndio unayoona ni ya muhimu kwao???….

Nataka nikuambie kama watakuwa na elimu ya kidunia halafu hawana Mungu, basi jua kuwa umewapoteza wanao, haijalishi watakuwa mamilionea huko mbeleni!!.. Bibi Loisi, aliona utukufu wa mjukuu wake mbeleni, na kwamba atakuja kuwa mtumishi wa MUNGU hodari katika kuwavuta watu kwa Mungu, hivyo akaanza kuweka msingi bora kwa binti yake Eunike, na Eunike akamfundisha mwanae Timotheo malezi bora.

Walikuwepo vijana wengi wenye elimu nyakati za akina Timotheo, lakini wapo wapi leo??..walikuwepo vijana mamilionea kipindi cha akina Timotheo, lakini hakuna hata mmoja habari yake tunaisoma leo, lakini Timotheo habari zake tunazisoma na zinawaponya mamilioni ya watu duniani hata leo. Bwana amempa Timotheo kumbukumbu lisilofutika..

Walikuwepo wamama wengi na wabibi wengi nyakati za akina Timotheo, lakini hakuna hata mmoja tunayezisoma habari zake, ila hawa wawili Loisi pamoja na mwanae Eunike, habari zao tunazosoma hadi leo..

Na Mungu ni yeye Yule, hajabadilika..ikiwa na sisi tutatembea katika kanuni zake atatupa kumbukumbu ambalo halitafutika. Ikiwa na sisi tutawalea watoto wetu katika njia zitupasazo basi kumbukumbu letu pamoja na watoto wetu, na wajukuu wetu, na vitukuu vyetu, na vilembewe na vilembwekeze litadumu milele na milele.

Anza kuwafunza watoto wako biblia, wafundishe wamjue Yesu zaidi ya Hisabati, wafundishe wazijue amri za Mungu, na kuwa waombaji na watu wa ibada zaidi hata ya shule za ulimwengu. Ukimfanya Mungu wa kwanza katika maisha yao, na Mungu atawafanya wa kwanza katika mambo yao.

Bwana atubariki sote.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

“Si watu wa kutumia mvinyo sana”, je tunaruhusiwa kutumia mvingo kidogo?(1Timotheo 3:8).

KWANINI UNAPASWA UWE BIBI ARUSI NYAKATI HIZI ZA MAJERUHI?

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

Je! Mfalme Abiya na Mfalme Asa walikuwa ni ndugu?

Rudi nyumbani

Print this post

ICHOCHEE KARAMA YAKO.

2Timotheo 1:6 “Kwa sababu hiyo nakukumbusha, uichochee karama ya Mungu, iliyo ndani yako kwa kuwekewa mikono yangu”.

Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo.

Neno la Mungu linatufundisha kuzichochea KARAMA tulizopewa,.. Ikiwa na maana kuwa “Kuwa na karamaa pekee haitoshi kuifanya kazi ya Mungu vizuri”..bali inahitajika Karama iliyochochewa. Na anayeichochoea si Mungu, bali ni sisi ndio tunaoichochea.

Mtu anapomgeukia Kristo na kuokoka, tayari Mungu anakuwa ameiweka karama ndani yake, kama mbegu ndogo sana.. Lakini karama ile isipochochewa inaweza kufa ndani ya mtu, na hatimaye mtu yule akabaki  kama mtu asiye na karama kabisa.

Hata wanaoshiriki michezo ya kidunia, ijapokuwa wanavyo vipaji vya michezo hiyo, lakini wasipovifanya mazoezi ya kutosha, haijalishi wana vipaji vikubwa kiasi gani, bado vipaji vyao hivyo vitakuwa si kitu. Na vipaji vina muda wake, mwanamichezo akifikia umri Fulani kama hajakitumia vizuri kipaji chake, basi kinapungua nguvu chenyewe, kwasababu tayari umri umeshaenda!.

Na karama za rohoni au vipaji vya rohoni ni ivyo hivyo.. visipochochewa vinakufa na visipotumika katika muda fulani, vinaisha thamani nguvu ndani yake..Ndio maana maandiko yanasema..

Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo. 

2 Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua”

Na pia inasema..

1Yohana 2:14  “…..Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu”

Sasa maandiko yanasema Bwana alitoa wengine kuwa mitume, wengine manabii, wachungaji, waalimu, wainjilisti, karama za kuponya, matendo ya miujiza, karama za lugha, karama za masaidiano, imani, hekima, maarifa  n.k (kasome Waefeso 4:11-12, 1Wakorintho 12). Lakini wengi hawajijui kama wanazo hizo karama.. kwasababu wanadhani zinaanza katika ukubwa wanaotugemea wao.

Wengi sana leo hii ni wainjilisti tangu siku ile wanapookoka, lakini kwasababu hawajijui kama wao ni wainjlisti, pale wanapojiona kuwa hawafanani na mwinjilisti mmoja maarufu, basi moto unazima ndani yao, pasipo kujua kama wanamzimisha roho, wengi ni waalimu tangu siku ile wanapookoka, lakini kwasababu hawajui namna ya kuzitumia karama zao na wanapoona wao si kama waalimu Fulani maarufu wanaowajua basi moto unazima ndani yao, wanabaki kusubiria muujiza siku moja wajikute wamekuwa wahubiri wenye uwezo wa kuhubiri kama watu Fulani maarufu.

Wengi wamepewa karama za kumwimbia Mungu, tangu siku walipookoka lakini kwasababu wanajiona kama sauti zao bado zinakwaruza, kwa kujilinganisha na wengine ambao tayari wanamwimbia Mungu kwa muda mrefu, basi wanatulia huku wakisubiri muujiza mwingine uwashukie utakaowafanya wawe kama hao wengine.

Kungoja huko ndiko kunakuua karama za watu wengi ndani yao.

Leo tutatazama njia 3, za namna ya kuzichochea karama zetu ili zifanye kazi katika viwango ambavyo Mungu amevikusudia.

1.KUJIFUNZA NENO.

Msingi wa karama zote ni Neno la Mungu, mtu aliyepungukiwa Neno la Mungu ndani yake, tayari karama yake inazima yenyewe tu ndani yake.. Kwanini Neno la Mungu??… kwasababu Neno la Mungu linatia hamasa, linatia moyo, linatupa sababu ya kuzitumia karama zetu, linafundisha jinsi ya kuzitumia kupitia mifano mbali mbali ya watumishi wa Mungu ndani ya biblia, na pia linatuonya madhara ya kutozitumia karama zetu. Hivyo Mtu mwenye Neno la Mungu la kutosha ni lazima tu karama yake itanyanyuka.

2. MAOMBI.

Hii ni njia ya pili ya kuchochoe karama zetu, Maandiko yanasesema tuombe bila kukoma  (1Wathesalonike 5:17), Na kuomba kunajumuisha pia na kufunga, vitu hivi viwili vinaenda pamoja..tunapoomba Bwana anatuongezea uwezo na upako katika karama zetu.

Mathayo 17:21 “Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.”

3. MAZOEZI.

Hii ni njia ya tatu na ya muhimu sana, chochote kisichofanyiwa mazoezi hakiwezi kuwa bora.. hata karama isipofanyiwa mazoezi haiwezi kuwa bora, maana yake ni kwamba kama wewe una karama ya kuimba, kamwe usitegemee utakuwa bora, bila kuifanyia mazoezi karama hiyo, ni lazima uwe na vipindi vya kuinoa sauti yako, kutafuta na kujifunza jinsi ya kuzipangilia sauti kupitia waliokutangulia au waalimu, huku wewe mwenyewe ukifanya mazoezi ya kurudia rudia mara kadhaa… hivyo ndivyo karama yako itakavyoongezeka nguvu, lakini ukiiacha tu na kujiona tayari unajua kila kitu, basi hutaweza kupiga hatua..

Vile vile kama umepewa karama ya kiualimu, au kiinjiilisti..kama utaketi tu kusubiri kufundishwa, basi kamwe hutaweza kufundisha wengine..unapaswa utenge muda wa wewe kwenda kufundisha wengine, hata kama bado hujui vitu vingi,.. wewe kafundishe hivyo hivyo, Bwana atakufundisha huko mbele ya safari, makosa utakayoyafanya ndiyo yatakuwa darasa lako la kufanya vizuri katika matukio ya mbele..hivyo usiogope, nenda kahubiri..

Vile vile kama umepewa karama ya matendo ya imani, au karama za kuponya, usingoje ngoje.. nenda mahospitalini, nenda sehemu mbali mbali kafanye maombezi huku ukiwahubiria habari za njema za wokovu, usiogope wala kuvunjika moyo, unapoona umeombea watu 10, na hakuna aliyepona hata mmoja.. wewe endelea mbele, hizo ni hatua za awali, katika matukio yanayokuja Bwana atakutumia kwa maajabu mengi.

Na karama nyingine zote ni hivyo hivyo, ni lazima UZICHOCHEE!!..kama vile moto unavyochochewa.

Na ulingo mzuri wa kuiona karama yako ikifanya kazi ni ndani ya KANISA, yaani unapokuwa katika kusanyiko la Kristo ni kipindi kizuri cha kuiona karama yako kuliko unapokuwa nje ya kusanyiko, kwasababu Biblia inasema karama hizi lengo lake la kwanza ni kuujenga mwili wa Kristo, maana yake kulijenga kanisa (Waefeso 4:11).

Ichochee karama yako!

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini tofauti kati ya Kipawa na Karama?

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

USINIE MAKUU.

Uzima wa milele ni nini?

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

Rudi nyumbani

Print this post

WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU

Mungu kamwe hajatuweka hapa duniani tutafute “dunia njema”, Dunia ambayo tutaishi mbali na hatari, mbali na majanga, mbali ni watu wabaya au waovu, hapana, hili ni jambo ambalo kila mtu aliyempokea Kristo au aliyeokoka anapaswa alijue, hata tujitahidi vipi kutafuta mahali ambapo patakuwa pazuri kwetu bado hatutapaona…

Kwasababu duniani hii ilishaharibika tangu Adamu alipoasi, na iliendelea kuwa hivyo hivyo, na hata sasa itakuwa hivyo hivyo ya hatari hadi mwisho wake, hakuna  mahali utaenda au utakaa na kusema hapa hakuna ukinzani, hakuna masumbufu.., ni kitendo cha muda tu, ukiyashazoelea hayo mazingira mapya utavumbua shida nyingine nyingi na hatari zilizopo hapo,ambazo kule hukuziona, nenda kote ulimwenguni ndio uhalisia ulivyo..

Kitu Mungu anachokifanya ni kutufanya tuwe salama katika mazingira haya mabaya, lakini sio kubadili mazingira yawe mbingu kwetu. Anachofanya ni kutuandalia meza, tule tunywe, katikati ya watu waovu, katikati ya wachawi, katikati ya waganga, katikati ya wauaji, katikati ya wapagani.. Lakini tusidhuriwe na wao..Na anafanya hivyo ili tumaini letu liwe kwake tu.

Daudi alilijua hilo akasema maneno haya katika Zaburi..

ZABURI 23

1 Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.

2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji

5 WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.

Umeona, anasema waandaa meza mbele yangu machoni pa watesi wangu.. Machoni pa wafanyakazi wenzangu wanaonionea wivu, machoni pa wafanya-biashara wenzangu wanaoniendea kwa waganga, machoni pa majirani zangu wanaoniundia visa kila kukicha..Hapo ndipo Mungu anapokuletea chakula chako, anapokuchunga, anapokupa faraja..Kamwe usitazamie atakupeleka mbinguni, kukupa rizki, au Baraka zako.

Usihangaike kumwomba Mungu akubadilishie mazingira akupe mengine, au akubadilishie watu akupe wengine, au akubadilishie majirani, au wafanyakazi, au akuhamishe mahali ulipo akusogeze kwingine kwasababu hapo ulipo ni pabaya sana.. Mungu atakusogeza wakati wake ukifika, lakini fahamu kuwa hata huko uendako, hata hao watu wengine uwakutao, matatizo yanaweza kuzuka hata makubwa kuliko ya kwanza.. Lakini mwombe Bwana katika mazingira yoyote akusaidie,, Hilo linatosha yeye awe mchungaji wako, awe mwamba wako, awe jemedari wako wa vita, ndio maombi anayotaka kuyasikia, na huwa anayajibu upesi, maombi ya namna hii. Mwombe akufanikishe hapo hapo ulipo, akupe amani na faraja hapo hapo ulipo..

Bwana Yesu alimwomba Mungu maneno haya..

Yohana 17:15 “Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu”.

Si mapenzi ya Bwana, wewe ukae mbali na walimwengu, bali katikati yao, mpaka wakati wa Bwana utakapofika ndio akuondoe na kukupeleka pengine.  Wakristo wengi wameathiriwa na mazingira yanayowazunguka, wanapoona hatari nyingi mbele yao au  nyuma yao. Badala waweke tegemeo lao kwa Bwana awasaidie watimize mapenzi ya Mungu, wanabakia kuyalaumu mazingira, wakisema, ni kwasababu ya hiki, ni kwasababu ya kile..Yule ananipiga vita ndio maana sina muda na Mungu..Laiti ningeondoka hapa na kwenda kule ningetumika vizuri zaidi  n.k…

Ndugu, Dunia hii iliyoanguka haina mahali utakuta pana unafuu, zaidi ya pengine, hapatakuwa na wachawi lakini patakuwa na magonjwa, hapatakuwa na magonjwa lakini patakuwa na uzito kiroho, au mwitikio wa watu kwa Mungu ni mdogo, hapatakuwa na maskini lakini patakuwa na majanga,..Hivyo hatari zipo na zitaendelea kuwepo kwasababu mkuu wa ulimwengu huu yupo kote.

Lakini tukiegemea kwa Bwana, na kumlilia yeye atembee nasi, atulinde, atuokoe, atupe amani, atupe faraja,atupiganie, na sio kuyalaumu mazingira, tutakuwa salama.

Wakati Fulani Mungu alinionyesha usiku katika ndoto, nilijikuta nimeingia katika jumba Fulani, lakini sikufahamu kama ni milki ya adui..Hivyo nikiwa kule nikawa kuzungumza na mama mmoja ambayr alikuwa kama kafungwa, lakini ghafla, mahali pale palibadilika,nikaanza kuwaona watu wanaotumiwa na ibilisi ndani ya mazingira yale, nikagundua uwepo wa pale sio wa ki-Mungu, bali ni milki ya ibilisi, basi nikawa natafuta mlango wa kutoka niondoke, lakini milango yote ilikuwa imepotea, basi nikawa nazunguka zunguka kwenye lile jumba lenye mazingira ya kutisha, kutafuta mlango wa kutokea sioni, kila nikiingia kwenye mlango mmoja, nakutana na chumba kingine, nikifungua kile huku nikitazamia ndio mlango wa kutoka nje, ndio kwanza nazama katika vyumba vya ndani zaidi..

Lakini nikiwa huko ndotoni, nikajikuta Napata hisia nyingine, nikasema Bwana ndiye ngome yangu ninahofu ya nini..Nikasema sitahangaika tena kutafuta mlango wa kutokea, nitatulia tuli, niendelee kumwangalia Bwana wangu, nikasema hapa nitatoka tu nisiwe na hofu..Na muda huo huo ghafla , nikawaona wenzangu wakiwa katika chumba kimoja wapo ndani ya hilo jumba, tukakutana wote tukiwa na amani sana kana kwamba pale sio ndani ya jumba la shetani, tukawa tunakula na kunywa, halafu tukaanza kuimba nyimbo nzuri za kumsifu Mungu, nakumbuka mahali pale niliona uwepo mzuri wa Bwana kana kwamba tulikuwa kanisani,

Na ghafla nikashutuka, ndipo Mungu akanifundisha neno hili..

Zaburi 23:5 Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.

6 Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.

Hivyo tuondoe hofu ya watu, tumtazame Bwana. Na yeye atatuokoa.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP

Mada Nyinginezo:

Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)

Je ni lazima kushiriki Meza ya Bwana?

YESU ANAKWENDA KUIBADILISHA OFISI YAKE.

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU.

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

Ni miaka mingapi ya njaa Daudi aliyoambiwa achague? Ni miaka 7 au miaka 3?

Rudi nyumbani

Print this post

Karismatiki ni nini?

karismatiki maana yake nini?

Karismatiki ni neno la kiyunani lenye maana ya “Zawadi za neema”.. Au kwa lugha nyepesi zaidi, tunaweza kusema, “vipawa vya neema”. Ambavyo hivyo hutolewa na Roho Mtakatifu mwenyewe na sio mwanadamu. Neno hili utalisikia sana vinywani vya madhahebu mbalimbali ya kikristo.

Ni mkondo ambao ulianza, mwanzoni mwa karne ya ishirini, (1906), kule Azusa Marekani, wakati ambapo dhehebu la Pentekoste lilipoanza. Lililoamini kuwa uthibitisho wa Mungu kuwepo katikati ya watu basi ni kuonekana kwa zile karama za Roho Mtakatifu, ambazo zinazungumziwa katika kitabu cha 1Wakorintho 12.

Kwamba kanisa ili liwe hai, ni sharti vipawa vya Roho kama vile Kunena kwa lugha, kutoa unabii, uponyaji na miujiza, vidhihirike ndani yake. Ikumbukwe kuwa tangu kanisa la kwanza la mitume kupita, vipawa hivi vilionekana kama vimekufa, havipo tena, lakini, viliibuliwa tena na Roho Mtakatifu mwanzoni mwa hiyo karne ya ishirini, ambapo baadhi ya wakristo walikaa chini na kufunga na kumwomba Mungu ajifunue kwa namna hiyo kama ilivyokuwa katika kanisa la kwanza la mitume. Na kweli wakiwa katika maombi hayo, Roho Mtakatifu alishuka, watu wengi wakaanza kunena kwa lugha, na karama mbalimbali kuonekana.

Ni jambo ambalo lilikuwa  gheni, kwa madhehebu mengi makongwe, ambayo yalikuwa tayari yameshajikita katika mifumo ya kidini kwa muda mrefu. Kama vile Katoliki, Lutheran, Angalican, Moravian n.k.

Hivyo basi mvuto  wa vipawa hivi, ulivyoendelea kuwa mkubwa, mpaka kufikia miaka ya 1980, madhehebu mengine mengi yakaanza kurithi mfumo huu wa karismatiki, ikiwemo dhehebu kama Katoliki, ( wakaitwa Karismatiki Katoliki), mengine ni Lutheran, na Anglikana, n.k. ijapokuwa yamekuwa na upishano kati ya wao kwa wao katika mifumo ya imani hii .

Hivyo kwa ufupi tunaweza kusema kanisa lolote linalosisitiza udhihirisho wa vipawa/karama za Roho, kama vile uponyaji, unabii, kunena kwa lugha, huitwa Kanisa la Karismatiki.

Ni nini tunapaswa tufahamu kuhusu vipawa vya Roho(Karismatiki).

Ni kweli kanisa linalokosa vipawa hivi, ni kanisa lililo nusu-mfu, au mfu kabisa. Kwasababu Mungu sio sanamu, ambaye anapokea tu ibada, lakini hatoi vipawa/zawadi kwa watu wake. Hayupo hivyo. Lakini pia ukengeufu mkubwa umeingia na kuvichafua vipawa vya Mungu, ikiwa na maana, kuwa mkristo usipokuwa makini utajikuta unapokea Roho nyingine na sio Yule wa Mungu.

Ni kuwa makini katika siku hizi za mwisho, wimbi kubwa la manabii wa uongo, linazukia huku, mafunuo yasiyo ya ki-Mungu yanaibuka na kuwapoteza watu kutoka huku, matumizi ya visaidizi kama maji, na chumvi za upako, vimewapoteza wengi,..Hivyo kumetokea mvurugano mkubwa sana. Mtu atanena kwa lugha leo, kesho atakwenda kuzini, jiulize ni roho gani ameipokea huyo?

Ni nini tunapaswa tufanye?

Nyakati hizi za mwisho, Tujitahidi sana kuitegemea  BIBLIA kwa kila kitu tunachokitenda, au tunachoongozwa kukifanya, Ikiwa ni karama hakikisha haikinzani na kanuni za msingi za Neno la Mungu, hiyo ndio njia pekee ya kuthibitisha kuwa kipawa hicho ni cha ki-Mungu. Lakini nje ya hapo utapotea. Ikiwa utapokea ufunuo, au unabii, usiupokee tu, ilimradi ni fulani kasema, kisa kaona maono, hakikisha kwanza katika biblia, Je! Ndivyo ilivyo? Au La!. Kwasababu  shetani ameingilia sana mikusanyiko mingi, ajaribu kuiangusha kwa namna hii.

Haiwezekani,  useme mimi nimepokea Roho Mtakatifu, ninanena kwa lugha, ninaimba kwa Roho,  Halafu  anakuacha uendelee kuabudu sanamu la mtakatifu Fulani,sanamu la Mariamu au uombe sala za wafu. Huyu sio Roho Mtakatifu, haijalishi atajiita ni Karismatiki namna gani.

Hivyo ni kuwa makini, tusije pokea roho nyingine isiyokuwa ya Mungu. Hizi ni zama za uovu.

1Yohana 4:1  “Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani”

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP

Mada Nyinginezo:

Nini tofauti kati ya Kipawa na Karama?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

HATA ILIPOTIMIA SIKU YA PENTEKOSTE.

SEMA KWA LUGHA NYINGINE.

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.

Rudi nyumbani

Print this post

UKITAKA KUFANIKIWA, FANANA NA MWANAMKE WA SAREPTA

Jina kuu la Bwana na Mwokozi wetu Yesu KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze biblia.

Sarepta ulikuwa ni mji mdogo uliokuwepo nje kidogo mwa nchi ya Israeli, katika Taifa la Lebanoni.

Katika biblia tunasoma kipindi Nabii Eliya amefunga Mbingu miaka mitatu na nusu kwa Neno la Bwana,  aliongozwa aende mpaka mji huu wa Sarepta ambapo kulikuwepo na Mwanamke ambaye Bwana alikuwa amemwandaa ili amlishe.

Mungu angeweza kumshushia Nabii Eliya mana kutoka mbinguni na akala akashiba, lakini hakufanya hivyo, bali alitumia watu na viumbe kumlisha wakati dunia nzima inapitia njaa. Mara ya kwanza alitumia kunguru (1Wafalme 17:4), na mara ya pili akatumia Mtu (ambaye ndiye huyu mwanamke wa Sarepta).

Sasa huyu mwanamke wa Sarepta alikuwa na tabia ya kipekee ambayo kupitia hiyo tunaweza kuvuna hekima ya mafanikio ya kimwili na kiroho.

Inawezekana mambo yako hayaendi sawa, inawezekana unapitia kipindi kigumu sana cha mbingu kufungwa juu yako, kila mahali unapogusa hapaendi, kila unalojaribu halifanikiwi, kila mahali ni ukame!!

Kama unapitia hii hali, basi usiende kutafuta kuombewa! Bali fanya kama alivyofanya huyu mwanamke wa Sarepta.

Ukifanya kama alivyofanya huyu mwanamke wa Sarepta, basi kipindi ambacho wengine watakuwa wanalia matatizo na dhiki, wewe hutakuwa katika hayo matatizo wala hizo dhiki..

Sasa ni kitu gani alichokifanya huyu mwanamke mpaka kufikia hatua ya yeye kuishi vizuri katikati ya vipindi vya shida na njaa na mauti?

Hebu tusome habari yake kwa ufupi kisha tujifunze tabia aliyokuwa nayo.

1Wafalme 17:7 “Ikawa, baada ya siku kupita, kile kijito kikakatika, kwa sababu mvua haikunyesha katika nchi. 

8 Neno la Bwana likamjia, kusema,

9 Ondoka, uende Sarepta, ulio mji wa Sidoni, ukae huko. Tazama, nimemwagiza mwanamke mjane wa huko akulishe

10 Basi, akaondoka, akaenda Sarepta; hata alipofika langoni pa mji, kumbe! Mwanamke mjane alikuwako akiokota kuni; akamwita, akamwambia, Niletee, nakuomba, maji kidogo chomboni nipate kunywa.

11 Alipokuwa akienda kuleta, akamwita akasema, Niletee, nakuomba, kipande cha mkate mkononi mwako.

12 Naye akasema, Kama Bwana, Mungu wako, aishivyo, sina mkate, ila konzi ya unga katika pipa, na mafuta kidogo katika chupa; nami ninaokota kuni mbili ili niingie nijipikie nafsi yangu na mwanangu, tuule tukafe.

13 Eliya akamwambia, Usiogope; enenda ukafanye kama ulivyosema; lakini unifanyie kwanza mkate mdogo ukaniletee; kisha ujifanyie nafsi yako na mwanao. 

14 Kwa kuwa Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Lile pipa la unga halitapunguka, wala ile chupa ya mafuta haitaisha, hata siku ile Bwana atakapoleta mvua juu ya nchi.

15 Basi akaenda, akafanya kama alivyosema Eliya; na yeye mwenyewe, na Eliya, na nyumba yake, wakala siku nyingi. 

16 Lile pipa la unga halikupunguka, wala ile chupa ya mafuta haikuisha, sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa kinywa cha Eliya”.

Umeona tabia ya huyu mwanamke?.. alikubali kutoa chakula chake kipindi ambacho amebakiwa nacho kidogo!!.. kipindi ambacho hajui kesho itakuwaje.. Alikubali kuweka sababu zake kando ilimradi tu aone Neno la Mungu linazidi kusambaa kupitia mtumishi wake,  aliona mtu wa Mungu,au kazi ya Mungu ina thamani mara nyingi zaidi ya kazi zake yeye au uwepo wake yeye na mwanae.  

Hivyo akajitoa sadaka maisha yake.. akijua kuwa hata kama atakufa na njaa yeye na mwanae lakini atakuwa na thawabu kubwa mbinguni, atakuwa hajaifanya kazi ya Mungu isimame… Hicho ndicho kilichomfanya Mungu ayaangalie matatizo yake, na kumfungulia Mbingu wakati wengine bado mbingu zimefungwa.

Na Mungu ni yeye Yule jana, leo na hata milele hajabadilika (Waebrania 13:8)..  Ukitaka Bwana ayaangalie mambo yako, basi wewe weka kando mambo yako na shida zako, na anza kujishughulisha na mambo yake..

Hii ndio shida kubwa inayowakabili wakristo wengi, huwa wanatanguliza matatizo yao mbele za Mungu na huku hawataki kumjali Mungu katika maisha yao.. wanatafuta kuombewa mambo yao yakae sawa, lakini kutafuta kuyaweka sawa mambo ya Mungu hawataki..

Watamwambia Mungu, tazama mwanangu hajala, mwanangu hana ada ya shule, mwanangu yuko hivi yuko vile, mimi sina chakula, mimi sina kazi, mimi sina hiki au kile..(wanakuwa ni watu wa kujijali wao) na hawana habari na mambo ya Mungu au kazi ya Mungu, wakidhani kuwa kwasababu Mungu ni muweza wa mambo yote, hivyo hahitaji kupewa chochote au kufanyiwa chochote.

Ni kweli yeye ni mweza wa yote, na hahitaji kufanyiwa chochote, lakini wakati mwingine anafanya hivyo kutujaribu upendo wetu kwake,.. angeweza kumshushia Eliya Mana kama alivyowashushiwa wana wa Israeli jangwani lakini hakufanya hivyo kwa Eliya, bali alimpeleka Eliya kwa huyu mwanamke, ili aujaribu upendo wake kwake.

Wengi wetu hatujui kuwa Mungu anafurahiwa sana na matoleo yetu kipindi ambacho hatuna kitu zaidi ya kipindi ambacho tuna kila kitu. Utasema hilo tunalithibitisha vipi kimaandiko?… Rejea ile habari ya Yule mwanamke mjane aliyetoa riziki yake yote katika sanduku la hazina…Utaona baada ya kutoa Bwana Yesu anamsifia, na tena anasema katoa zaidi ya wote, kwasababu hao wengine walitoa katika sehemu zilizowazidi…

Marko 12:41  “Naye akaketi kulielekea sanduku la hazina, akatazama jinsi mkutano watiavyo mapesa katika sanduku. Matajiri wengi wakatia mengi.

42  Akaja mwanamke mmoja, mjane, maskini, akatia senti mbili, kiasi cha nusu pesa.

43  Akawaita wanafunzi wake, akawaambia, Amin, nawaambia, Huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote wanaotia katika sanduku la hazina;

44  maana hao wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi; bali huyu katika umaskini wake ametia vyote alivyokuwa navyo, ndiyo riziki yake yote pia”

Kwaufupi huyu mjane, hakubakiwa na kitu, huenda alijua baada ya kutoa vile atakaa siku kadhaa na njaa… lakini akiwa katika hiyo hali, Bwana Yesu alimsifia.. huenda baada ya pale, alishangaa kwa milango ya Baraka iliyofululiza mbele yake.

Na wewe ukitaka Mbingu zifunguke juu yako, usianze kutoa visababu katika kumtolea Mungu, usianze kusema sijalipa kodi, usianze kusema sina chakula, sijalipa ada, sijafanya hiki, sijafanya kile, ngoja nikusanye kidogo nitakapopata nitatoa.. Ni kweli siku ukipata na kutoa basi Bwana atakubariki, hataacha kukubariki!!!… lakini  hujui tarehe wala siku mambo yako yatakapokuwa sawa..

Walikuwepo wanawake wengi sana kipindi cha Eliya wenye matatizo ya chakula kama huyu wa Sarepta, ambao na wenyewe pengine walikuwa wanafunga na kuomba Mungu awape riziki kwasababu ya ukame…lakini Eliya hakutumwa kwao kwasababu hizo hizo, huenda angeenda kwao na kuwaambia wampe yeye kwanza mkate, wangemfukuza kwa mawe, tena wangemtukana…

Wangesema hatuwezi kuona watoto wetu wanakufa njaa halafu tukupe wewe mzee chakula chao, wangetumia hata na maandiko kuthibitisha hilo.. Kwaufupi kila mmoja angeeleza shida zake na sababu zake kwanini asingempa Eliya mkate.. Ndicho Bwana Yesu alichokisema katika Luka 4:25.

Luka 4:25 “Lakini, kwa hakika nawaambia, Palikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli zamani za Eliya, wakati mbingu zilipofungwa miaka mitatu na miezi sita, njaa kuu ikaingia nchi nzima;

26  wala Eliya hakutumwa kwa mmojawapo, ila kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni”.

Na sisi pia tukitaka mbingu zifunguke juu yetu kabla ya wakati wake, hatuna budi kumjali Mungu zaidi ya kujijali sisi, hatuna budi kuyatazama mambo ya Mungu zaidi kuliko mambo yetu. Hii ni moja ya kanuni za Mafanikio.

Bwana Yesu atubariki.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?

Kwanini wajane vijana hawakupaswa kuandikwa?

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

MWANAMKE, BINTI, MAMA. (Sehemu ya 3)

Nini maana ya kumpenda Bwana kwa moyo,roho, akili na nguvu zetu zote?

Rudi nyumbani

Print this post

Makanda ni nini?

Makanda ni neno lingine la KAPU.

Ambalo hutumika kuhifadhi au kubebea vitu mbalimbali hususani vyakula au nafaka.

Katika biblia Neno hilo utakutana nalo katika vifungu kadha wa kadha, mfano wapo ni hivyo ni hivi; 

Mathayo 15:37

[37]Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate makanda saba, yamejaa.

Marko 8:8

[8]Wakala, wakashiba, wakakusanya mabaki ya vipande vya mikate makanda saba.

Luka 16:6-7

[6]Akasema, Vipimo mia vya mafuta. Akamwambia, Twaa hati yako, keti upesi, andika hamsini.

[7]Kisha akamwambia mwingine, Na wewe wawiwani? Akasema, Makanda mia ya ngano. Akamwambia, Twaa hati yako, andika themanini.

Luka 16:5-7

[5]Akawaita wadeni wa bwana wake, kila mmoja; akamwambia wa kwanza, Wawiwani na bwana wangu?

[6]Akasema, Vipimo mia vya mafuta. Akamwambia, Twaa hati yako, keti upesi, andika hamsini.

[7]Kisha akamwambia mwingine, Na wewe wawiwani? Akasema, Makanda mia ya ngano. Akamwambia, Twaa hati yako, andika themanini.

Ni nini twapaswa kujua nyuma ya makanda ya mikate waliyoyakusanya wanafunzi wa Yesu ambayo baadaye waliyasahau mpaka wakaanza kulalamikiana na kulaumiana..Hadi Yesu akawakemea..(Marko 8:14-21)

Ni kwamba waliweka mioyo yao katika makapu yao, katika hazina zao, hata waliposahau wakapaniki.

Ni hali iliyopo sasa miongoni mwetu sisi, tuliookolewa. Tunafikiri sana makapu yetu yana nini, kwa miezi 10 mbele, kwa miaka 3 ijayo..na pale tunapopungukiwa hata uhusiano wetu na Mungu unakufa..Lakini Bwana Yesu anatuambia tusiwe wasiwasi, wala tusiyasumbukie hayo..bali tuutafuta kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine atatuzidishia..kwasababu maisha ni zaidi ya chakula.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Ila atapewa mara mia sasa,Ndugu wake(Marko 10:30)

JE! UNAMPENDA BWANA?

Mtu akizaa watoto mia, lakini nafsi yake haikushiba mema;

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA- Sehemu ya 2.

WAKINYAMAZA HAWA, MAWE YATAPIGA KELELE.

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

Rudi nyumbani

Print this post