Title December 2022

Biblia inasemaje kuhusu Nywele?

Biblia imetoa maelekezo kuhusu Nywele kwa jinsia zote mbili (Ya kike na Kiume).

JINSIA YA KIUME:

Biblia inasema Mwanaume hapaswi kuwa na Nywele ndefu.. kwasababu kichwa chake yeye ni Utukufu wa Mungu..

1Wakorintho 11:3 “Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu

Hivyo kwa Mwanaume kuziweka Nywele zake kuwa ndefu ni aibu kwake na ni kukiaibisha Kichwa chake hicho ambacho ni  Kristo.

Tusome..

1Wakorintho 11:14  “Je! Hayo maumbile yenyewe hayawafundishi ya kwamba mwanamume akiwa na nywele ndefu ni aibu kwake?”

Na sio tu hatakiwi kuwa na Nywele ndefu, bali hata “Kufunika kichwa” awapo ibadani, maana yake ni kwamba  mwanaume anapokuwa ibadani hapaswi kuvaa kofia, au kuweka kitu chochote kichwani kinachoashiria kufunikwa kwa kichwa chake (maana yake kichwa chake siku zote kinapaswa kiwe wazi).

Na vile vile Mwanaume hapaswi kusuka Nywele, wala kuweka mitindo mitindo kichwani kwasababu kichwa chake ni utukufu wa Mungu.

JINSIA YA KIKE:

Katika jinsia ya Kiume tumesoma kuwa ni aibu kwa mwanaume kufunika kichwa, lakini tukirudi katika jinsia ya kike ni kinyume chake. Kwamba ni Aibu mwanamke kuwa na Nywele fupi na ni FAHARI MWANAMKE KUWA NA NYWELE NDEFU.

1Wakorintho 11:15 “Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni fahari kwake. Kwa sababu amepewa zile nywele ndefu ili ziwe badala ya mavazi”.

Wanawake wote ni sharti waache nywele zao ziwe ndefu kulingana na biblia, kuzikata Nywele au kuzifanya fupi, pasipo sababu yoyote ya msingi kama vile magonjwa, au udhaifu wa mwili, ni kwenda kinyume na maagizo ya Mungu.

Ndio maana Upara (Ulaza) huwa hauwapati wanawake, bali wanaume tu!!..Hiyo ni kuonyesha kuwa wanawake wamekusudiwa kuwa na Nywele vichwani mwao wakati wote wa maisha yao, na wanaume ni kinyume chake.

Na zaidi sana biblia inazidi kuelekeza kuwa hata kama Mwanamke atakata nywele zake kutokana na matatizo Fulani Fulani, labda magonjwa au kutokana udhaifu wa nywele kukatika zenyewe basi hapaswi kutembea nje akiwa na nywele zake hizo fupi, bali anapaswa afunike kichwa chake kwa kitambaa au kwa kitu chochote kile.

1Wakorintho 11:6  “Maana mwanamke asipofunikwa na akatwe nywele. Au ikiwa ni aibu mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa, na afunikwe.

7  Kwa maana kweli haimpasi mwanamume kufunikwa kichwa, kwa sababu yeye ni mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume”.

Na mwanamke anapokuwa ibadani awe na nywele ndefu au fupi, ni Agizo la Bwana kwamba afunike kichwa chake, kwasababu kuu 2

Sababu ya Kwanza ni ili asikiabishe kichwa chake ambacho ni MWANAUME. Na sababu ya pili ni kwaajili ya MALAIKA. Tunapokuwa ibadani Malaika wa Bwana wanahudumu pamoja na watakatifu. Malaika hawa Bwana aliowaweka kwaajili yetu wana uhusiano mkubwa sana sisi katika kutuhudumia Soma Mathayo 18:10.

Kwahiyo tunapokuwepo katika ibada na ndani yake kukawa kunafanyika mambo ambayo ni kinyume na Neno la Mungu, malaika hawa wanaondoka, na hivyo kufanya ibada kupoa na utukufu wa Mungu kupungua.

Na pia Wanawake hawapaswi kusuka nywele zao, au kuvaa wigi, au kuzibadilisha maumbile nywele zao aidha kwa kuziweka kemikali, au dawa za kuzifanya zilale, Biblia haijawapa maagizo ya kuzifanya nywele zilale au zing’ae au ziwe kama za jamii ya watu Fulani, Hapana!.. imesema “ZIWE NDEFU!!” Basii!!..

1Timotheo 2:9  “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;

10  bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.

11  Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)

Je kuchonga Nywele na Ndevu ni dhambi?

MSHAHARA WA DHAMBI:

FUVU LA KICHWA.

NGUVU YA MNADHIRI WA BWANA.

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inasemaje kuhusu Kazi?

Jibu: Biblia imetuelekeza kufanya kazi za Mikono, ambayo kupitia hiyo Mungu atatupa riziki zetu za kila siku.

1Wathesalonike 4:11  “Tena mjitahidi kutulia, na kutenda shughuli zenu, na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe, kama tulivyowaagiza;

12  ili mwenende kwa adabu mbele yao walio nje, wala msiwe na haja ya kitu cho chote”

Hivyo ni wajibu wa kila mmoja mwenye uwezo wa kufanya kazi, afanye kazi, aidha za Mikono au za kiutumishi.

Kazi za mikono ni zile zote zinazohusisha kuajiriwa au kujiajiri, na kazi za kiutumishi ni zile zote za Madhabahuni au za kiinjilisti. Mkristo yoyote ni lazima awepo katika kundi mojawapo ya hayo mawili, akikosekana katika yote (na ilihali ni mzima, au hana tatizo lolote lile) basi mtu huyo yupo kinyume na Neno la Mungu, aidha kwa kujua au kutokujua.

Mtume Paulo alisema kwa uongozo wa Roho, kuwa mtu yeyote asiye na shughuli yoyote katika Mwili wa Kristo, yaani asiyefanya kazi yoyote ya Madhabahuni  kama Uchungaji, Uinjilisti, au Shemasi, au Mzee wa kanisa au ya Uinjilisti, au mfanya kazi wa kanisani (inayomfanya muda wake mwingi atumie kuhubiri) mtu huyo basi asipewe fungu lolote kutoka kanisani..

1Wathesalonike 3:10 “ Kwa kuwa hata wakati ule tulipokuwapo kwenu tuliwaagiza neno hili, kwamba ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula.

11  Maana twasikia kwamba wako watu kwenu waendao bila utaratibu, hawana shughuli zao wenyewe, lakini wanajishughulisha na mambo ya wengine.

12  Basi twawaagiza hao, na kuwaonya katika Bwana Yesu Kristo, watende kazi kwa utulivu na kula chakula chao wenyewe”

Kumbuka pia unapoamua kufanya kazi za Mikono, basi huwezi kuwa Mchungaji kwa wakati huo huo, kwasababu huwezi kushikilia mambo mawili kwa wakati mmoja.. Ni aidha ushikilia moja uache lingine! Huwezi kuwa mchungaji na huku ni Mbunge, huwezi kuwa Mchungaji na huku ni Mfanya biashara mashuhuri.. jambo hilo haliwezekani!, haijalishi mtu atalilazimisha kiasi gani?.

Mathayo 6:24  “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali”

Tofauti na inavyodhaniwa na wengi kwamba Mtume Paulo alikuwa anafanya kazi muda wote!, kwamba alikuwa anashona Mahema kila wakati ili kujipatia riziki, nataka nikuambie kuwa haikuwa hivyo, ni sehemu chache sana ndizo alizokuwa anashona mahema, lakini sehemu kubwa ya maisha ya Paulo ilikuwa ni kuhubiri injili, na Mungu alikuwa anamfungulia milango ya riziki kupitia injili hiyo, na alikuwa haombi kwa watu fedha wala mali, (ili awe kielelezo) bali watu walikuwa wanampa kwa kadiri wanavyoguswa.

Tunalithibitisha hilo katika kitabu cha Wafilipi, 4:1-19, (Zingatia Mistari iliyoainishwa kwa herufi kubwa)

Wafilipi 4:14  “Lakini mlifanya vema, mliposhiriki nami katika dhiki yangu.

15  Nanyi pia, ninyi wenyewe mnajua, enyi Wafilipi, ya kuwa katika mwanzo wa Injili, nilipotoka Makedonia, hakuna kanisa lingine lililoshirikiana nami katika HABARI HII YA KUTOA NA KUPOKEA, ila ninyi peke yenu.

16  KWA KUWA HATA HUKO THESALONIKE MLINILETEA MSAADA KWA MAHITAJI YANGU, WALA SI MARA MOJA.

17  Si kwamba nakitamani kile kipawa, bali nayatamani mazao yanayozidi kuwa mengi, katika hesabu yenu.

18  Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; NIMEPOKEA KWA MKONO WA EPAFRODITO VITU VILE VILIVYOTOKA KWENU, HARUFU YA MANUKATO, SADAKA YENYE KIBALI, IMPENDEZAYO MUNGU.

19  Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu”

Umeona hapo ? Sio wakati wote Paulo alikuwa anafanya kazi ya kushona, Soma pia 2Wakorintho 8:1-5..

Lakini biblia inatufundisha nini katika hali tulizopo (yaani ya kufanya kazi ya Mikono au ya Madhabahuni)?

Biblia imetufundisha kutumika kwa uaminifu popote pale tunapopatumikia, maana yake kama ni Mtumwa basi tumika ipasavyo kwa Bwana wako (maana yake Boss wako, au Mkubwa wako) kana kwamba unamtumikia Kristo.

Waefeso 6:5  “Enyi watumwa, watiini wao walio bwana zenu kwa jinsi ya mwili, kwa hofu na kutetemeka, kwa unyofu wa moyo, kana kwamba ni kumtii Kristo;

6  wala si kwa utumwa wa macho tu kama wajipendekazao kwa wanadamu bali kama watumwa wa Kristo, mkitenda yampendezayo Mungu kwa moyo;

7  kwa nia njema kama kumtumikia Bwana wala si mwanadamu;

8  mkijua ya kuwa kila neno jema alitendalo mtu atapewa lilo hilo na Bwana kwamba ni mtumwa au kwamba ni huru”.

Vile vile kama tunatumika katika utumishi wowote ule.. Maandiko yanatufundisha  KURIDHIKA, Maana yake TUSIJISIKIE VIBAYA kutumika pale tulipopachagua sisi, kwasababu ni mapenzi ya Mungu. Kama ni Mfanyakazi wa kuajiriwa maana yake wewe ni Huru kwa kazi ya Bwana ya madhabahuni, hivyo usijisikie vibaya kuifanya kazi hiyo, kilicho kikubwa na cha muhimu ni wewe kuwa Mwaminifu katika kazi unayoifanya na pia katika kumtolea Bwana, na mwisho wa siku utapokea thawabu kutoka kwa Mungu, vile vile kama wewe ni mtumishi wa Madhabahuni au wa Injili, maana yake wewe ni Huru katika utumishi wa kazi za kidunia, hivyo basi usijisikie vibaya kutumika hivyo, maana ni Mungu kakuita katika hali hiyo, wala usiitamani kazi nyingine zaidi ya hiyo uliyopewa!.  

1Wakorintho 7:21  “Je! Uliitwa u mtumwa? Usione ni vibaya lakini kama ukiweza kuwa na uhuru, afadhali kuutumia.

22  Kwa maana yeye aliyeitwa katika Bwana hali ya utumwa, ni huru wa Bwana. Vivyo hivyo yeye naye aliyeitwa hali ya uhuru, ni mtumwa wa Kristo.

23  Mlinunuliwa kwa thamani; msiwe watumwa wa wanadamu”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

MAOMBI YA KUFUNGULIWA KIUCHUMI.

Orodha ya mistari ya biblia kuhusu watoto.

Kwanini iwe ni nchi ibubujikayo maziwa na asali?

Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?

Rudi nyumbani

Print this post