KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)

Nakusalimu katika jina kuu, la Bwana wetu Yesu Kristo karibu katika sehemu ya pili ya Makala hii inayohusu migogoro katika ndoa. Sehemu ya kwanza tuliona Upande wa mwanaume, Leo tutaangazia upande wa mwanamke. Kwa kurejea mgogoro uliozuka katika ndoa ya kwanza ya Adamu. Kama hukupata sehemu ya kwanza tutumie msg inbox tukutumie uchambuzi wake.

Wewe kama mke.

Unapaswa utambue kuwa mume ndio kichwa cha Familia, Ndoa ya kwanza ulitikiswa na mwanamke, kuonyesha kuwa vyanzo vya migororo ya ndoa nyingi hadi sasa ni WANAWAKE.

Na hiyo yote ni kwasababu wepesi kufungua milango kwa shetani kuwadanganya kirahisi. Kwamba wao pia wajione wanauwezo wa kujiamulia tu mambo yao bila hata ya waume zao au kumshirikisha Mungu ? Hiyo ni hatari kubwa sana.

Usijaribu kufanya hivyo mwanamke, utaiharibu ndoa yako kwa mikono yako mwenyewe. Kinyume chake, anza kuwa MTIIFU kwa mume wako kama biblia inavyosema katika..

Waefeso 5:22 “ENYI WAKE, WATIINI WAUME ZENU KAMA KUMTII BWANA WETU.

23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.

24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo”.

Kuwa mtiifu, mume wako anapokutakana uwahi kurudi nyumbani, TII, anapokuambia nipikie chakula, Tii, anapokuambia nifulie nguo, usimwambie housegirl si yupo, anapokuambia fanya hivi, au fanya vile wewe tenda, anapokushauri usifanye shughuli Fulani, sio nzuri, tii pia, kwasababu yule ndio kichwa chao. Ondoa kiburi ndani yako, wewe sio kichwa, ukijaribu kufanya hivyo, ndipo hapo shetani atakupa mbinu mbadala, utafute marafiki/wanaume wengine nje ya ndoa yako wenye pesa, ili kumkomoa mume wako, kumbe hujui kuwa ndio unajiangamiza wewe mwenyewe. Ndicho alichokiwaza Hawa alipokwenda kutafuta mashauri kwa nyoka.

Kwahiyo, simama katika nafasi yako, ya utiifu. Mbinu aliyotumia shetani kumwangamiza Hawa, ndio hiyo hiyo ataitumia na kwako, isiposimama katika nafasi yako kama mwanandoa. Na majuto utayaona baadaye sio sasa wakati una kiburi.

Kumbuka, mwanamke hutakaa ufanikiwe kwa kujitenga na mume wako? Kamwe halitawezekana.  Mwanaume anaweza kujaribu kuishi,  japo itakuwa kwa shida sana, lakini wewe sahau kuishi kwasababu Ubavu hauna ubongo,wala mikono, wala miguu, wala pua, wala macho,. Ni kipande cha nyama tu. Ndivyo ilivyo kwako wewe, ujue kuwa huna Maisha nje ya mume wako wa ndoa. Ukimwacha leo, haijalishi, una kipato kikubwa kuliko yeye, au ni mjanja kuliko yeye, nataka nikuambie hauna Maisha wewe duniani.

Na mwisho kabisa, hayo yote unaweza kuyafikia, ikiwa tu upo ndani ya Kristo, Haiwezekani kuwa mtiifu, au mwombaji, au mtakatifu, au mtu wa kusamehe, kama hutakuwa  ndani ya Kristo. Kwahiyo hatua ya kwanza ni kumpa Kristo Maisha yako.

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo. Basi unaweza kufuatisha sala hii kwa Imani. Ukiifuatisha kwa kumaanisha kabisa ujue kabisa Bwana Yesu atakusamehe leo na kuja ndani yako….Tafuta sehemu ya utulivu kisha piga magoti, na useme sala hii kwa sauti.

“EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU, (KWA KUIJERUHI NDOA YANGU). LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.”

Ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani, ujue kuwa Kristo ameshakusamehe na kuanzia sasa anza kuwajibika kwa ajili ya ndoa yako. Na kama hujabatizwa, na unahitaji kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi, na kwa jina la Yesu Kristo, basi wasiliana na sisi kwa namba hizi, +255693036618 au +255789001312 Tukusaidie.

Mungu akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)

Nini maana ya..“wakiwazuia watu wasioe” (1Timotheo 4:1)

Kwanini wajane vijana hawakupaswa kuandikwa?

NDOA NA TALAKA:

NINI TUNAJIFUNZA KWA THEOFILO MTUKUFU?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments