SWALI: Tukisoma Kitabu cha Waebrania tunaona mwandishi akitaja vitu viwili vya Mungu visivyoweza Kubadilika ambavyo tumepewa viwe kama nanga ya Roho, je ni vipi hivyo? Au Maana yake ni nini?
Waebrania 6:17-19
[17]Katika neno hilo Mungu, akitaka kuwaonyesha zaidi sana warithio ile ahadi, jinsi mashauri yake yasivyoweza kubadilika, alitia kiapo katikati;
[18]ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo, tupate faraja iliyo imara, sisi tuliokimbilia kuyashika matumaini yale yawekwayo mbele yetu;
[19]tuliyo nayo kama nanga ya roho, yenye salama, yenye nguvu, yaingiayo hata mle mlimo ndani ya pazia,
JIBU: Ukisoma hiyo habari vifungu vya juu na vile vinavyoendelea mbele yake. Habari inayozungumziwa pale ni ya Ibrahimu na jinsi Mungu alivyompa ahadi ya mbaraka pamoja na uzao wake. Na jinsi alivyokuja kuitimiza
Lakini tunaonyeshwa ahadi ile pekee aliyopewa, haikutosha kumfanya Ibrahimu, aamini bali Mungu Ili kumthibitishia kuwa atavipokea kweli kweli basi aliongezea Na kiapo.
Mwanzo 22:15-17
[15]Malaika wa BWANA akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni
[16]akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema BWANA, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,
[17]katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;
Kwasababu kiapo ni kifungo cha mwisho ambacho Mtu humaliza shuku zote, mashaka yote mijadala yote..
Ilimbidi Mungu aweke kiapo ijapokuwa angetimiza Ahadi zake bila kiapo. Lakini ilimbidi afanye vile ili kumpa uthabiti Ibrahimu juu ya maadhimio yake.
Hivyo mambo hayo mawili yasiyoweza Kubadilika ya Mungu ni;
1)Neno lake(ambalo lilikuja kama ahadi),
2) lakini pia Kiapo, ambacho hukata maneno yote.
Na kweli tunakuja kuona yote Mungu aliyomuahidi Ibrahimu yalitokea kama yalivyo..
Lakini Ahadi hiyo haikuishia kwa Ibrahimu, bali ilitimilizwa yote na Bwana wetu Yesu Kristo.
Ambao sisi tuliomwamini, tunaingizwa Katika ahadi hizo..alizozithibitisha Kwa kiapo kupitia Bwana wetu Yesu Kristo. Ambaye Mungu alimthibitisha kama kuhani mkuu wa milele mfano wa Melkizedeki kuhani Wa Ibrahimu (rohoni)..
Waebrania 7:21-25
[21](maana wale walifanywa makuhani pasipo kiapo; bali yeye, pamoja na kiapo, kwa yeye aliyemwambia, Bwana ameapa wala hataghairi, Wewe u kuhani milele;)
[22]basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.
[23]Tena wale walifanywa makuhani wengi, kwa sababu wazuiliwa na mauti wasikae;
[24]bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.
[25]Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.
Hivyo sisi tuna Neno la ahadi..kwamba tunaomwamini tunapokea uzima wa milele kama yeye.. Lakini pia jambo Hilo amelikolezea Kwa kiapo kuwa hatalibatilisha..Ni hakikisho kubwa sana..Haleluya!
Hivyo ni wajibu wetu kuendelea mbele kwaujasiri na bidiii katika imani na kumtumikia yeye kwasababu yupo pamoja nasi, wala kamwe hawezi kutuacha hata Iweje.
Kwasababu Neno lake ni hakika, alilotuahikikishia Na kiapo juu.
Je umempokea Bwana Yesu kwenye Maisha yako?. Fahamu kuwa hakuna tumaini lolote nje ya Kristo. Okoka leo.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Katika agano la lake, iliruhusiwa Kufanya hivyo, ikiwa mtu amefiwa na ndugu yake na hana mtoto, aliruhusiwa kwenda kumwoa mke wa ndugu yake ili amwinulie uzao, lakini halikuwa kwa lengo la kimahisiano ya kindoa kana kwamba ni wapenzi. Bali kwa kusudi tu la kumwinulia uzao.
Kumbukumbu la Torati 25:5-10
[5]Watakapoketi pamoja mtu na nduguye, mmojawapo akafa, wala hana mwana wa kiume, mke wa yule aliyekufa asiolewe nje na mgeni; nduguye yule mumewe amwingilie amweke kwake awe mkewe, kumfanyia yampasayo nduguye mumewe.
[6]Na iwe, yule mzaliwa wa kwanza atakayemzaa, amfuate nduguye aliyekufa kwa jina lake, lisije likafutwa jina lake katika Israeli.
[7]Na yule mtu kwamba hapendi kumtwaa mke wa nduguye, aende huyo mke wa nduguye langoni kwa wazee, akawaambie, Nduguye mume wangu yuakataa kumsimamishia nduguye jina katika Israeli, hataki kunitimizia yampasayo nduguye mume wangu.
[8]Ndipo wamwite wazee wa mji wake waseme naye; naye akisimama na kusema, Sitaki mimi kumtwaa mwanamke huyu,
[9]ndipo mke wa nduguye amkaribie mbele ya hao wazee, amvue kiatu chake mguuni mwake, na kumtemea mate ya uso; kisha atajibu yule mwanamke, aseme, Mume akataaye kumjengea nduguye nyumba yake na afanywe hivi.
[10]Na jina lake katika Israeli liitwe, Nyumba ya mvuliwa kiatu.
Halikadhalika tunapokuja kwenye agano jipya hatuoni pia agizo lolote la moja kwa moja linalokatazama ndugu kuoa mke wa ndugu yake aliyekufa…
Zaidi inasema mwanamke Yeyote anapokuwa mjane yupo huru kuolewa na ‘Yeyote’ amtakaye katika Bwana..
1 Wakorintho 7:39
[39]Mwanamke hufungwa maadamu mumewe yu hai, lakini ikiwa mumewe amefariki, yu huru kuolewa na mtu ye yote amtakaye; katika Bwana tu.
Warumi 7:3
[3]Basi wakati awapo hai mumewe, kama akiwa na mume mwingine huitwa mzinzi. Ila mumewe akifa, amekuwa huru, hafungwi na sheria hiyo, hata yeye si mzinzi, ajapoolewa na mume mwingine.
Hiyo ikimaanisha kuwa anaweza akawa huru kuolewa hata na ndugu wa kaka yake (aliyefariki)…
Lakini lazima tufahamu kuwa si kila jambo linalohalalishwa kibiblia linaweza likafaa katika mazingira yote au majira yote, yapo mambo mengine ya kuzingatia, mfano utamaduni wa mahali fulani..
Kwasababu Biblia bado inatuambia…
1 Wakorintho 10:23
[23]Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo.
Kwa mfano kwa wayahudi ilikuwa ni tamaduni Watu kusalimiana kwa ‘busu’ la upendo. Lakini katika mazingira ya jamii zetu jambo kama hilo huleta ukakasi, au kutoa tafsiri nyingine hata kama nia sio mbaya..ndio maana tunaishia kipeana mikono, na ikizidi sana kukumbatiana kwa jinsia tu zinazofanana.
Vivyo hivyo katika jambo hili, kuoa mke wa ndugu yako aliyefariki, kijamii halina munyu ndani yake.
Hivyo twaweza sema kijamii halikubaliki, lakini kibiblia halijakatazwa..ukiniomba mimi ushauri nitakuambia usifanye hivyo..kaoe pengine..lakini ukimwoa mke wa ndugu yako aliyekufa pia hujafanya dhambi ikiwa tu, pana makubaliano kamili katika pande zote mbili, lakini pia wewe mwenye uwe haupo katika ndoa.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NDOA NA IHESHIMIWE NA WATU WOTE.
Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?
https://wingulamashahidi.org/2019/08/31/bwana-yesu-alikuwa-anamaanisha-nini-kusema-marko-219%e2%80%b3walioalikwa-harusini-wawezaje-kufunga-maada
SWALI: Yule tajiri alimaanisha nini kumwambia Lazaro, achovye ncha ya kidole chake majini uuburudishe ulimi wake?
Luka 16:24
[24]Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.
JIBU:
Habari hiyo la Tajiri na Lazaro, Bwana Yesu aliieleza kufunua uhalisia wa jehanamu jinsi ulivyo… Na mambo ambayo mtu aliyeukataa wokovu atakutana nayo baada ya kifo.
Anaeleza jinsi yule tajiri alivyokufa katika hali ya dhambi..na hatimaye akajikuta mahali pale pa mateso, ambapo hakutana hata ndugu zake wafike, tunaona hata alipoomba mtu atokaye kwa wafu aende kuwahubiria ndugu zake akaambiwa hawatashawishwa…Ni kuonyesha kuwa mahali pale palikuwa pa mateso Sana, kiasi cha kutaka mwingine yeyote kufika.
Lakini tukio lingine tunaonyeshwa akimwomba Ibrahimu Amruhusu Lazaro achovye ncha ya kidole Chake majini amburudishe ulimi wake, nalo pia akaambiwa haiwezekaia kwasababu kuna kizuizi kikubwa Sana katikati yao.
Sasa swali linakuja tukio lile linamaana gani Je kiu kile ni halisi au ni ufunuo?.
Bwana Yesu alipokuja duniani.. aliona Dunia nzima ina Kiu kikubwa sana.. na hivyo inahitaji maji ya kuweza iponya.
Sasa maji inayohitaji sio haya ya mtoni..bali maji ya rohoni ambayo ni ya uzima, na mtu pekee awezayo kutoa hayo ni yeye mwenyewe..hakuwahi kutokea mtu aliyeweza kuyatoa.
Kama tunavyojua mwili ukikosa maji, mwishowe utakufa..Ndivyo ilivyokuwa sisi sote, hapo mwanzo kabla ya Kristo, Wote tulikuwa wafu kiroho..
Utauliza vipi kwa watakatifu wa kale kama akina Musa na Eliya?…Wale walikuwa wanaishi kwa ahadi ya Kristo, Hivyo walitii madhihirisho yake aliyokuwa akijifunua kwao kwa namna mbalimbali huku wakiiongejea ahadi kamili ya ukombozi ambayo alikuja kuikamilisha yeye mwenyewe (Yesu Kristo) alipofufuka Katika wafu..(waebrania 11)
Yeye mwenyewe Alisema..
Yohana 7:37-39
[37]Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.
[38]Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.
[39]Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.
Sasa kiu hii ni ya nini?
Ya maisha….
Tangu zamani mwanadamu amekuwa akitafuta ‘maisha’ ambayo hata sasa hajayapata…ndio maana wengi wanakimbilia kutafuta elimu, fedha na utajiri wakidhani kuwa ndio wamepata maisha, lakini hivyo vipo mbali sana na maisha …vitakufanya ule vizuri tu, unywe vizuri, ulale vizuri kama maandalizi ya heri ya kifo chako baadaye..kwasababu Haviwezi kukudumishia maisha.. vinapooza tu kiu..lakini haviondoi kiu.
Yesu amekuja kuondoa kiu.
Sasa watu Ambao watapuuzia kuyapokea maji hayo ambayo Yesu anatupa…wakifa Katika hali hiyo hiyo huko waendapo ni majuto makubwa.
Kwasababu watataka hata tone dogo la maji hawatapata…yaani kiwango kidogo tu cha neema ya uzima hawatapata…
Leo Yesu hatupi maji tu, kwa kipimo fulani bali anapanda kabisa chemchemi za maji ndani yetu Ambazo zinabubujika uzima wa milele.
Yohana 4:14
[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
Madhara ya kukosa maji ya uzima si tu baada ya kufa…hata hapa Hapa duniani.. mtu ambaye hana Kristo rohoni anajulikana kama nchi kamena matokeo yake ni kuwa makao ya mapepo yanakuwa Ndani yake hata kama hujui..
Angalia Yesu alichokisema juu ya hilo.
Mathayo 12:43-45
[43]Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate.
[44]Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa.
[45]Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya.
Yanakwenda mahali pasipo na maji…yaani moyo ambao hauna Kristo ndani yake.
Ndugu…umeona hatari waliyonao wenye dhambi, hapa duniani na baada ya kifo?
Shetani asikupumbaze, tubu leo kwa kumpokea Bwana Yesu katika maisha yako ili upate ondoleo la dhambi zako haraka sana.
Hizi ni siku za mwisho, dunia hii inakwisha…vilevile hujui ni siku Gani utakufa…Acha kuchezea maisha yako, ukafanana na yule tajiri aliyekosa maji ya uzima angali akiwa hai.
Okoka leo..
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Bwana Yesu alitutahadharisha kuwa karibia na kurudi kwake, tabia za watu zitabadilika na kukaribia kufanana na zile za watu wa Nuhu na Lutu.
Luka 17:26 “Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu.
27 Walikuwa WAKILA NA KUNYWA, walikuwa WAKIOA NA KUOLEWA, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote.
28 Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa WAKILA NA KUNYWA, walikuwa WAKINUNUA NA KUUZA, wakipanda na kujenga;
29 lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote.
30 Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu”.
Sasa ishara hii ya watu kununua na kuuza, kuoa na kuolewa na kula na kunywa ilikuwa inalenga makundi mawili, kundi la kwanza ni WATU WASIOMJUA MUNGU, na kundi la pili ni WATU WANAOMJUA MUNGU, hetu tuanze tathmini ya kundi moja baada ya lingine.
1. WATU WASIOMJUA MUNGU.
Kipindi cha Nuhu na Sodoma na Gomora walikuwa wakila kwa anasa, na kunywa kwa kulewa, na wakamsahau Mungu, lakini pia walikuwa wakioa na kuolewa kwa ndoa haramu (maana yake za watu waliocha waume zao au wake zao, au wa jinsia moja) vile vile walikuwa wakinunua vitu haramu na kuuza vitu haramu kwa njia zisizo halali, ikiwemo dhuluma na rushwa, na utapeli na wakamsahau Mungu, hivyo gharika ikawachukua wote.
Ndicho kinachoendelea sasa kwa watu wengi walio nje ya wokovu, rushwa ni kitu cha kawaida kwao, kuoana kiholela ni kitu cha kawaida, (yaani mtu kuoa/kuolewa leo na kesho kuachana na kwenda kuoa/kuolewa na mwingine ni jambo la kawaida), hali kadhalika kuhudhuria kwenye karamu za ulafi na kula bila kiasi pamoja na kulewa ni mambo ya kawaida kila mahali, ndio maana utaona Bar ni nyingi kila kona.
Lakini hiyo ni ishara kwa watu wasiomjua Mungu, ambayo kiuhalisia pia inatangaza kwamba tunaishi katika siku za mwisho, lakini hebu tuangalie kwa upande mwingine kwa watu wa Mungu (kanisa.)
2. WATU WANAOMJUA MUNGU (Kanisa)
Utauliza je! Watu wanaomjua Mungu pia wanaangukia katika hili kundi la kula na kunywa, kuoa na kuolewa, kununua na kuuza?.. Jibu ni ndio!.. sasa labda utauliza ni kwa namna gani?.. hebu tusome maandiko yafuatayo..
Luka 14:16 “Akamwambia, Mtu mmoja alifanya karamu kubwa akaalika watu wengi,
17 akamtuma mtumwa wake saa ya chakula awaambie wale walioalikwa, Njoni, kwa kuwa vitu vyote vimekwisha kuwekwa tayari.
18 Wakaanza wote kutoa udhuru kwa nia moja. Wa kwanza alimwambia, NIMENUNUA SHAMBA, SHARTI NIENDE NIKALITAZAME; tafadhali unisamehe.
19 Mwingine akasema, Nimenunua ng’ombe jozi tano, ninakwenda kuwajaribu; tafadhali unisamehe.
20 Mwingine akasema, NIMEOA MKE, na kwa sababu hiyo siwezi kuja”
Nataka tuone huo udhuru hao watu walioutoa!.. Kumbuka hao ni waalikwa, maana yake watu wenye mahusiano na mwenye harusi, na huo ni mfano ambao Bwana aliutoa kuhusu karamu ya mwanakondoo itakayofanyika mbinguni baada ya unyakuo,
Kwamba sasa anawaaalika watu, lakini waalikwa (yaani watu wanaomjua Mungu) wanatoa udhuru!, kwamba Nimeoa Mke, wengine nimenunua shamba sharti nikalitazame!.. Je huoni haya ndio yale yale Bwana aliyoyasema kwamba siku za mwisho watu watakuwa wakioa na kuolewa, na kununua na kuuza?
Kumbe ishara hii pia inatimia kwa watu wa Mungu!.. watu wasiomjua Mungu wao wataoana ndoa haramu, watanunua vitu haramu na kuuza kwa njia haramu.. lakini watu wa Mungu wataoa kihalali, na kununua na kuuza kihalali lakini watavifanya hivyo kuwa udhuru utakaowazuia kumsogelea MUNGU zaidi.
Hii ni hali halisi kabisa ya kanisa la leo!.. Asilimia kubwa ya tunaojiita wakristo, shughuli zimetusonga kiasi cha kuupunja muda wa Mungu, hatuombi tena kwasababu ya wingi wa kazi, hatuifanyi tena kazi ya Mungu kwasababu ya majukumu ya kifamilia na ndoa!, hatukusanyiki tena pamoja na wengine kwasababu ya mialiko mingi tuliyonayo ya kula na kunywa!..
Je unajua matokeo yake ni nini?.. Hebu tuendelee na mistari ile..
“20 Mwingine akasema, NIMEOA MKE, na kwa sababu hiyo siwezi kuja,
21 Yule mtumwa akaenda, akampa bwana wake habari ya mambo hayo. Basi, yule mwenye nyumba akakasirika, akamwambia mtumwa wake, Toka upesi, uende katika njia kuu na vichochoro vya mji, ukawalete hapa maskini, na vilema, na vipofu, na viwete.
22 Mtumwa akasema, Bwana, hayo uliyoagiza yamekwisha tendeka, na hata sasa ingaliko nafasi.
23 Bwana akamwambia mtumwa, Toka nje uende barabarani na mipakani, ukawashurutishe kuingia ndani, nyumba yangu ipate kujaa.
24 Maana nawaambia ya kwamba katika wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu yangu”.
Matokeo yake ni kwamba Neema tuliyoipewa watapewa watu wengine , wote wenye kuwa na udhuru mwingi kwa Bwana wapo katika hatari ya kukosa kuingia mbinguni, wapo katika hatari ya kukumbana na gharika ya mwisho ya moto kulingana na Biblia.
Je wewe upo kundi gani?.. Unakula na kunywa kwa anasa au kihalali?, na kama kihalali je hiyo kwako ni udhuru wa kumtafuta Mungu?.. je wewe unanunua na kuuza kiharamu au kihalali?.. na kama ni kihalali je hiyo kwako ndio udhuru wa kutojitoa kwa Mungu?.. majibu yapo kwako na kwangu.
Bwana atusaidie tusiwe watu wa udhuru, bali tumtumikie Bwana kwa moyo wote, kwani hiyo ni amri tuliyopewa.
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je mtu anaweza kubatizwa mara mbili?
Je tumepewa kujua nyakati na majira ya kurudi kwa Bwana au la?.
KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.
SWALI: Bwana Yesu alikuwa na maana gani kusema ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’.
Luka 13:33
[33]Pamoja na hayo imenipasa kushika njia yangu leo na kesho na kesho kutwa; kwa kuwa haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu.
JIBU: Bwana Yesu alikuwa anaeleza asili ya mji wa Yerusalemu nyakati zote ulivyokuwa wa mauaji, mji ambao ungepaswa uwe wa kupokea manabii wa Mungu, lakini kinyume chake uligeuka mji wa kuwaua Manabii…
Sasa kusema maneno yale ni kutokana na taarifa aliyoletewa na wale mafarisayo kuwa Herode anataka kumwangamiza, hivyo aondoke pale aende mji mwingine…ndipo Bwana Yesu akawaambia ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’ yaani haipaswi nabii afe nje ya Yerusalemu…
Manabii wengi wa Mungu, waliuliwa pale pale Yerusalemu hivyo hata na yeye kuangamia hapo si jambo geni, …
Na ndivyo ilivyokuwa
Mfano wa hao katika maandiko alikuwa;
Zekaria mwana wa Yehoyada (2Nyakati 24:20-21). Ambaye aliuliwa hekaluni
Mwingine ni Uria nabii (Yeremia 26:20 – 24)
Na manabii wengine wengi ambao hawajatajwa, moja kwa moja katika maandiko waliuawa Yerusalemu…ndio sababu ya Yesu kusema maneno Haya;
Mathayo 23:37-39
[37]Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!
[38]Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa.
[39]Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana.
Jambo hili hujirudi sasa rohoni..
Watu wote ambao wanaipinga injili mioyoni mwao leo, hata kama hawajashiriki moja kwa moja kuwarushia mawe watu wa Mungu, ni shirika moja tu na wale waliokuwa wanawaua manabii wa Bwana zamani.
Ndivyo walivyodhani mafarisayo kwamba wenyewe hawahusiki na mauaji ya manabii wa Bwana, angali wanampinga yeye waziwazi, kwa unafiki wao aliwaambia maneno haya..
Mathayo 23:29-36
[29]Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki,
[30]na kusema, Kama sisi tungalikuwako zamani za baba zetu, hatungalishirikiana nao katika damu ya manabii.
[31]Hivi mwajishuhudia wenyewe, ya kwamba ninyi ni wana wao waliowaua manabii.
[32]Kijazeni basi kipimo cha baba zenu.
[33]Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum?
[34]Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji;
[35]hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu.
[36]Amin, nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki.
Hii ni hatari kubwa sana kwa walio nje ya Kristo.
Mwamini Yesu leo uoshwe dhambi zako. Upokee uzima wa milele. Kwingineko si salama.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote (Yohana 16:23)
MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.
SWALI: Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote ’
Kwanini ajiangue kwa namna hiyo angali yeye ndiye mwokozi wa kutegemewa kila kitu?
Yohana 16:23
[23]Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.
JIBU:
Kama tunavyojua hakukuwahi kutokea kiongozi aliyekuwa na matokeo makubwa duniani kama Yesu Kristo.
Namna ya uongozi wake, Kwa jinsi ulivyokuwa thabiti na bora Matokeo yake ndio tunayoana mpaka sasa duniani kwenye imani.
Hivyo maisha yake na huduma yake sio tu vinatufundisha njia ya wokovu lakini pia vinatufundisha namna kiongozi bora anavyopaswa Awe.
Matokeo Ya mitume wake kuwa nguzo kwa makanisa ya vizazi vyote ni matokeo ya namna ambavyo alivyowakuza anawakuza.
Bwana Yesu hakutengeneza Wafuasi, bali alitengeneza watu kama Yeye…Na hivyo katika kuwafundisha wanafunzi wake aliwakuza Ki vitendo zaidi kuliko maneno ya vitabu vingi vya kidini na mapokeo.
Kwamfano utaona kuna mahali anawatuma wawili waenda kuhubiri injili mahali ambapo angepaswa kwenda yeye mwenyewe, lakini aliwaacha waende.
Luka 10:1
Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.
Mahali pengine aliwaacha watoe pepo na waliposhindwa hakusema ‘wanangu nyie ni wachanga, basi nitakuwa nawasaidia tu’…hapana Kinyume chake aliwakemea Kwa upungufu wa imani zao.
Vivyo hivyo katika tukio hili, wanafunzi wake walitarajia kila siku watakaa naye wamuulize maswali yeye, kisha awajibie kutoka kwa Baba.. Ni sawa na mtoto mchanga ambaye kila siku anasubiria atafuniwe tu chakula apewe…unadhani hilo litaendelea sana?
Vivyo hivyo hilo halikuwa lengo la Bwana Yesu, bali alitaka kuwafundisha kanuni za wao wenyewe kumuuliza Mungu na kujibiwa moja kwa moja kama yeye alivyokuwa anajibiwa…
Na njia moja wapo ilikuwa ni yeye kuondoka, kisha kwa kile kitendo cha wao kumkosa Bwana wa kumuuliza, wajifunze kuomba kisha Roho ajae ndani yao, ndipo waanze sasa kupokea mafunuo ya kweli na ujasiri kutoka kwa Mungu..
Lakini pia waombe jambo lolote kwa jina la Yesu, wapokee mahitaji yao. Na Kweli mambo hayo yalianza Kutokea baadaya ya Pentekoste.. wote walikuwa ni kama ‘Yesu-dunia’ hakuna hata mmoja alifikiri au kuwaza kwamba kuna umuhimu tena wa Yesu kutembea nao, kimwili bali waliweza kuyafanya yote.
Hiyo ni tabia ya kiongozi bora…huwafanya wanafunzi wake kuwa kama yeye, na wakati mwingine kutenda hata zaidi ya yeye…Yesu aliwainua zaidi kwa kusema.
Yohana 14:12
[12]Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.
Hiyo ndio sababu kwanini aliwaambia hayo maneno.
Yohana 16:23-24
[23]Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.
Hata sasa Bwana anataka kuona ukomavu kama huu ndani ya maisha ya wakristo wengi.. Ikiwa kila siku utakuwa unategemea Mchungaji wako akuombee, ni lini utaweza wewe mwenyewe kuomba na kuwaombea wengine? Sababu ya watu wengi kutojibiwa maombi yao na Mungu ni hiyo.. Ameshakomaa kiroho, Mungu anaona anaouwezo wa kupambana na tatizo yeye mwenyewe, atataka kiongozi wake amsaidie..
Hicho kitendo kinapunguza utendaji Kazi wa nguvu za Mungu, kwasababu yeye hataki tumgeuze mwanadamu Mungu..Ukiokoka, fahamu kuwa Roho Mtakatifu yupo ndani yako, na kuanzia huo wakati na kuendelea unawajibu wa kuufanyia mazoezi wokovu wako, jifunze kuomba mwenyewe, jifunze kuombea watu, soma biblia mwenyewe Mungu akufundishe..
Hizo ndio hatua bora za ukuaji kiroho.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Jambo jingine Kuu la kujifunza kama mkristo ni Kumshukuru Mungu kila wakati na kwa kila jambo, kwamaana maandiko ndivyo yanavyotufundisha..
1Wathesalonike 5:18 “shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu”.
Kuna mambo yanafunguka tu yenyewe baada ya kumshukuru Mungu!..haihitaji nguvu nyingi.. Maombi ya shukrani ni maombi yanayougusa moyo wa Mungu zaidi hata ya kupeleka mahitaji!, kwani ni yanauelezea uthamani wa Mungu katika maisha ya mtu, ni maombi ya kushuka sana na ya kuithaminisha kazi ya Mungu katika maisha yako au ya wengine, na hivyo ni maombi yenye nguvu sana na kuugusa moyo wa Mungu kuliko tunavyofikiri.
Na kiuhalisia maombi ya kushukuru ndiyo yanayopaswa kuwa maombi ya kwanza kabisa kabla haya yale ya toba na mahitaji..kwasababu, uzima tu ulionao ni sababu ya kwanza kumshukuru Mungu, kwasababu usingekuwa nao huo hata maombi mengine usingeweza kuomba..
Leo tuangalie faida moja ya kumshukuru Mungu, kwa kujifunza kupitia Bwana wetu YESU KRISTO.
Kama wewe ni msomaji wa Biblia utagundua kuwa kila wakati ambapo Bwana YESU alitaka kufanya MUUJIZA usio wa kawaida, alianza kwanza kwa kushukuru..
Kwamfano kipindi anaigawa ile mikate kwa watu elfu nne alianza kwanza kwa kushukuru..
Mathayo 15:33 “Wanafunzi wake wakamwambia, Tupate wapi mikate mingi hapa nyikani, hata kushibisha mkutano mkuu namna hii?
34 Yesu akawaambia, Mnayo mikate mingapi? Wakasema, Saba, na visamaki vichache.
35 Akawaagiza mkutano waketi chini;
36 akaitwaa ile mikate saba na vile visamaki, AKASHUKURU AKAVIMEGA, akawapa wanafunzi wake, nao wanafunzi wakawapa makutano.
37 Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate makanda saba, yamejaa”.
Pengine unaweza usione uzito wa shukrani katika huo muujiza wa mikate… hebu tusome mahali pengine palipoonesha kuwa ni SHUKRANI ya Bwana ndio iliyovuta ule muujiza mkuu wa mikate.
Yohana 6:23 “(Walakini zikaja mashua nyingine kutoka Tiberia mpaka karibu na mahali pale walipokula mikate, WAKATI BWANA ALIPOSHUKURU)”..
Hapo anasema.. “wakati Bwana aliposhukuru”… Kumbe! Ile shukrani ilikuwa na maana kwa sana kwa muujiza ule kutendeka.. Na wala pale hapaonyeshi kwamba Bwana YESU alimwomba Baba augawe ule mkate!.. la! Bali alishukuru tu kisha akaumega!, muujiza ukatendeka.
Kuna mambo mengine unahitaji kushukuru tu na kuendelea mbele!, na mambo yatajiweka sawa yenyewe, kuna nyakati hutahitaji kuomba sana.. bali kushukuru tu, na kumwachia Bwana..na maajabu yatatendeka..
Pia utaona kipindi kile kabla ya Bwana kumfufua Lazaro alianza kwanza kwa KUMSHUKURU MUNGU..
Yohana 11:39 “Yesu akasema, Liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana, ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne.
40 Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?
41 Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, BABA, NAKUSHUKURU KWA KUWA UMENISIKIA.
42 Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia sikuzote; lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kwamba ndiwe uliyenituma.
43 Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje.
44 Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake”.
Umeona? Ni shukrani tu, ndio iliyomtoa Lazaro kaburini..
Je na wewe unayo desturi ya kumshukuru Mungu?.. Maombi ya shukrani yanapaswa yale maombi marefu sana, kwani tunazo sababu nyingi sana za kumshukuru Mungu, kama umeokoka, huo wokovu ulio nao ni sababu ya kumshukuru Mungu hata masaa sita mfululizo, kwasababu kama ungekufa kabla ya kuokoka leo ungekuwa wapi?.
Kama unapumua hiyo ni sababu ya kumshukuru Mungu, kwasababu wapo walioondoka na wengine ni wema kuliko hata mimi na wewe.
Na zaidi ya yote si tu kushukuru kwa mambo mema au mazuri Mungu anayokutendea, bali hata kwa yale ambayo yameenda kinyume na matarajio yako, ni lazima kushukuru, kwasababu hujui kwanini hiyo jambo limekuja kwa wakati huo, endapo Ayubu asingemshukuru Mungu kwa majaribu aliyokuwa anayapita zile Baraka zake mwishoni asingeziona.
Ni hivo hivyo mimi na wewe, hatuna budi kumshukuru Mungu kwa vyote, viwe vizuri au vibaya.. kwasababu tunajua mwisho wake utakuwa mzuri.
Yeremia 29:11 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho”.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
UNAZO KILA SABABU ZA KUMSHUKURU MUNGU
Kwanini BWANA awaagize wakoma wakajionyeshe kwa Makuhani?(Luka 17:14
KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU.
Maombi kama sehemu ya maisha ya mwamini mpya.
SWALI: Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, ni vita ya namna gani tunashindana nayo katika ulimwengu wa Roho?
JIBU: Katika biblia tunaposoma Neno “pepo”, ni vema tufahamu ufunuo wake upo katika namna mbili;
Yote mawili unapaswa kufahamu, Ili ujue ni nani unashughulika naye katika vita hivyo vya kiroho.
Kwamfano, ukisoma ile waefeso 6:12 inayosema kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama, bali juu ya falme na mamlaka na wakuu wa giza hili pamoja na majeshi ya mapepo wabaya.. Sasa hao wanaotajwa hasaa ni malaika waasi.
Lakini hawa malaika waasi, huwa na mapando yao, ambayo huyapanda ndani ya watu, mfano wa hayo ni magonjwa, ukichaa, ububu, udhaifu (Marko 9:25)uuaji, uchungu, majivuno, kiburi, masengenyo n.k.. na haya mapando wakati mwingine huitwa mapepo, kwasababu asili yao ni kutoka kwa hao malaika waasi.
Luka 13:11 Na tazama, palikuwa na mwanamke aliyekuwa na pepo wa udhaifu muda wa miaka kumi na minane, naye amepindana, hawezi kujinyosha kabisa.
Pepo linalozungumziwa hapo, hasaa sio yale mashetani, bali ni pando la udhaifu waliloliweka ndani ya huo mwanamke.
Hizi zote ni kazi za shetani na malaika zake duniani. Sasa mapando haya ndio tunaweza kuyaua (kwa kuyang’oa), lakini sio wale malaika waasi. Ndio maana Bwana Yesu alisema..
Mathayo 15:13 Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang’olewa
Wale malaika waasi (yaani wakuu wa giza, wafalme, majeshi ya mapepo yote)hatuwezi kuwaua, kwa maombi au kwa namna yoyote, isipokuwa tayari wameshawekewa hukumu yao, siku ile ya mwisho ambapo watatupwa wote kwenye lile ziwa la moto.
Na mapando haya, Bwana Yesu alitoa maelezo yake vema, wakati ambapo adui hupandwa ndani ya mtu..
alisema.
Mathayo 13:24 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.
27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?
28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?
29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.
30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.
Kumbe wakati ambapo watu wamelala, ndipo hupanda mbegu zake. Yaani wakati ambapo watu wamekuwa walegevu kiroho ndipo shetani hupata nguvu ya kuja kupachika, mbegu zake za uharibifu, zitakazokuja kusumbua baadaye. Ndio maana ni lazima ujue kanuni mbalimbali za kumpinga shetani.
Na haya mapando, yanaweza kuwekwa kwa mtu yeyote, hata mtu aliyeokoka, anaweza kuwa nayo. Ndio maana utaona wapo watu wengine wameokoka, lakini wanasumbuliwa na mapepo, kiuhalisia, hawana malaika wale waasi ndani yao, wanayo mapando yao.
Ni sawa, na mtu ambaye anamilika chombo kama komputa, akiwa anaitumia kwa matumizi yake tu ya sikuzote, tu ambayo ni lazima, si rahisi computa hiyo kuvamiwa na virusi, lakini akianza kutembea mitandaoni, kisha kubofya, au kupakua kila kitu anachokiona ni wazi kuwa chombo hicho kipo hatarini kuvamiwa na virusi, na matokeo yake ni kuwa mfumo wote wa kumpyuta unaliwa, au kuharibifu chombo kabisa, ndio maana wanaweka ulinzi (anti-virus) sikuzote,
Vivyo hivyo na maisha ya mwanadamu yakiwa ovyo ovyo, hawezi kukwepa mapando ya mashetani ambayo yamezaa kila mahali. Mtu yeyote ambaye hajaokoka tayari kuna pepo fulani ndani yake.
Kwamfano, mwingine, labda mkristo ameokoka, halafu akiwa kanisani, anaanza kuruhusu masengenyo kinyume na mchungaji wake, au mama-mchungaji, sasa mtu kama huyo akiwa anaendelea na tabia hiyo..matokeo yake ni kwamba pepo la uchungu litamvaa, ataanza kuwachukia viongozi wake hata bila sababu, na kuzusha vita, na uharibifu hata wengine. Yeye atadhani ni tabia yake kumbe sio, bali pepo limeshamvaa la uchungu.
Nikupe huu ushuhuda, Kulikuwa na mama mmoja kanisa, kipindi chote ulikuwa ukikutana naye, anamzungumzia vibaya mama mchungaji wa kanisa alilokuwa mwanzo, hapo mwanzo alikuwa vizuri tu kiroho, lakini kwa jinsi siku zilivyozidi kwenda, akiendeleza chuki zake, , hali yake ilikuja kubadilika ghafla, akaomba tumwombee, tulipomwombea alilipuka mapepo, lile pepo likawa linasema “mama mchungaji” yaani asili yangu ni chuki kwa mama mchungaji, tulipolikemea likamwacha akarudia hali yake ya kawaida, akawa mtu mzuri tu.
Samsoni, alipokwenda kuwashindana na wafilisti, hakushughulika kwanza na wafilisti, bali mashamba yao ya ngano. (mapando yao). Kwa kuyachoma moto. Vivyo hivyo na sisi ili tuyamalize nguvu haya mashetani, tuangushe ngome zao. Ni lazima fikra zetu hasaa zielekee mapando yao.
Injili:
Kwamfano kuwaangusha wakuu wa giza sio kuwatumia makombora ya moto hapo angani. Hapana, bali ni kwenda kuhubiri injili ili watu wamsikie Kristo waokoke,
Ndio maana Yesu alipowatuma wanafunzi wake wawili wawili kuhubiri waliporudi Yesu aliwaambia ‘nalimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme’.
Kumbe anguko lake lilikuwa katika kuhubiri na si kumtumia makombora.
Maombi:
Hii ni silaha kubwa, ya kumpinga shetani. Maombi huruhusu, utendaji kazi wa Mungu ndani ya maisha ya mwamini, usipokuwa mwombaji tarajia shetani kuyapangalia maisha yao. Yesu alituagiza tukeshe kuomba tusije ingia majaribuni.
Upendo:
Upendo hupinga, wivu, chuki, uchungu, mashindano, uzinzi, n.k. ambayo haya yote huzaliwa mahali ambapo hapana upendo. Ni lazima kila siku wewe kama mwamini kila siku ujifunze kutendea kazi upendo….ili uondoe mazingira ya mashetani kuangua mayao yao hapo.
Neno:
Ukiwa na Neno la Mungu la kutosha ndani yako, adui hawezi kukushinda. Utakumbuka kule jangwani, shetani alipojaribu kumpandia Kristo maneno ya uongo kwa kupitia biblia, yeye mwenyewe alilitumia Neno la Kweli, kumpinga. Watu wengi wanavamiwa na maroho ya upotevu, kwasababu hawana Neno la Mungu mioyoni mwao. Jifunze kusoma biblia. Ni silaha inayoitwa Upanga.
Imani:
Imani huzaa ujasiri, na ujasiri hutoa mamlaka ndani yako. Biblia huiita imani “Ngao” Shetani anapenda kutumia silaha ya woga, ili kuzimisha utendaji kazi wa Mungu mioyoni mwetu. Hatuna budi kusimama kwa utimilifu wa imani kumtumikia Mungu.
Kukemea:
Fahamu adui ni mpingamizi sikuzote, hapembelezwi, bali analazimishwa kutoka, Yesu alimkemea shetani alipotaka kumjaribu kwa kinywa cha Petro, aliyakemewa mapepo yote sugu, yaliyokuwa ndani ya watu yawatoke. Hivyo na wewe pia ukutanapo na kazi hizi za mwovu, jifunze kutumia kinywa chako, kwa mamlaka uliyopewa na Kristo kukemea haraka sana, kila pepo, au kimelea chochote cha uovu kinachozaliwa na adui.
Hivyo kwa hitimisho ni kuwa, mashetani hawafi, lakini kazi zao zinakufa.. Hatuwaui hao, bali tunaziua kazi zao. Usipoteze muda mwingi kumrushia shetani mabovu hawezi kufa, bali tuma nguvu zako nyingi kurushia mabovu mapanda yake, kwa kanuni hizo tulizojifunza. Utawashinda kabisa kabisa.
Bwana akubariki
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?
MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.
SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.
Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?
Mithali 4:23 “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako CHEMCHEMI ZA UZIMA”.
Chemchemi kazi yake ni kutoa “maji ya kunywa” lakini pia ya maji ya “kustawisha mimea”.
Kama chemchemi ikitoa maji ya chumvi au ya magadi, ni wazi kuwa maji yake hayatafaa kwa matumizi yoyote yale, hivyo mahali hapo hapana uhai, watu hawawezi kuishi wala wanyama wala mimea..
Lakini kama chemchemi ikitoa maji safi yasiyo na magadi wala chumvi, na tena masafi, basi mahali pale kila kitu kitasitawi ikiwemo watu, wanyama na mimea, na hata shughuli zote nyingine za kiuchumi.
Mfano wa maji machungu na yasiyofaa ni yale wana wa Israeli waliyokutana nayo kule ‘Mara’
Kutoka 15:22 “Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji.
23 Walipofika mahali palipoitwa Mara hawakupata kuyanywa yale maji ya Mara, kwa kuwa yalikuwa machungu; kwa ajili ya hayo jina lake likaitwa Mara.
24 Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema, Tunywe nini?
25 Naye akamlilia Bwana; Bwana akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na hukumu huko, akawaonja huko”.
Sasa Biblia inafananisha “Mioyo yetu na chemchemi zinazotoa maji”… Maana yake yanayotoka mioyoni mwetu yanaweza kukuza, kustawisha au kudhoofisha afya zetu, wanyama wetu, mimea yetu…kwaufupi kila kitu kinachotuzunguka ikiwemo kazi zetu, elimu zetu, nafasi zetu, kibali chetu na mambo mengine yote yanategemea sana yanayotoka mioyoni mwetu.
Sasa najua utauliza haya maji machungu au matamu ni nini?.. Turejee maneno ya Bwana Yesu.
Mathayo 12:34 “Enyi wazao wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake.
35 Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya”.
Tusome tena Mathayo 15:18-20…
Mathayo 15:18 “Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.
19 kwa maana MOYONI hutoka MAWAZO MABAYA, UUAJI, UZINZI, UASHERATI; WIVI, USHUHUDA WA UONGO, NA MATUKANO
20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi…….”.
Umeona hapo?.. kumbe moyoni ndiko kunakotoka matukano, uzinzi, wizi, uongo n.k mambo ambayo ndiyo yanayomtia mtu unajisi, na bila shaka hayo ndiyo Maji machungu yatokayo moyoni kupita kinywani, ambayo hayafai kwa kustawisha chochote…
Wengi wamepoteza na kuharibu maisha yao kwasababu ya uzinzi, na wengine kwasababu ya wizi, na wengine kwasababu ya mauaji, wapo waliopoteza kibali kwa Mungu na kwa watu kwasababu ya wizi, au uzinzi, au mauaji..wapo walipoteza kazi zao za mikono na huduma zao zilizokuwa zenye utukufu kwasababu ya uzinzi, au wizi au matukano..
Wapo walioharibu ndoa zao zilizokuwa za heshima na mfano kwasababu ya uzinzi, uongo, na mauaji (utoaji mimba) Kwanini?.. kwasababu chemchemi zao zinatoa maji machungu yanayoua ndoa, kazi, huduma, kibali, heshima na nguvu.
Yakobo 3:8 “Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.
9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu.
10 Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo.
11 Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu?
12 Ndugu zangu, Je! Mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Kadhalika chemchemi haiwezi kutoa maji ya chumvi na maji matamu”.
Lakini kama moyoni kukutoka mambo masafi, ambayo ni upendo, ukweli, utu wema, uvumilivu (kwa ujumla utakatifu)… hakika hiyo ni chemchemi bora inayostawisha kila kitu, maji yake yatastawisha wokovu, kazi ya Mungu, kazi ya mikono, elimu, heshima, ndoa, nafasi na mambo mengine yote mazuri.
Je wewe chemchemi ya moyo wako inatoa maji ya aina gani?.. machungu au matamu?.. Kama inatoa machungu ipo dawa leo?.. dawa hiyo ni Roho Mtakatifu… Mwamini YESU leo kisha ukabatizwe na Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukutakasa moyo wako Bureeeee kabisa!
Baada ya hapo ndoa yako iliyokufa itafufua upya, huduma yako, kazi yako, elimu yako au kitu kingine cha thamani ulichopewa na Bwana, kitafufuka kwani tayari maji yatokayo ndani yako ni masafi..
Lakini labda tayari chemchemi yako ni safi, nayo inatoa maji masafi.. bado kuna jambo lingine la ziada la kufanya nalo ni KUILINDA chemchemi yako..
Mithali 4:23 “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako CHEMCHEMI ZA UZIMA”.
Utaulinda moyo wako kwa MAOMBI, kusoma NENO, kujihadhari na ulimwengu na kushiriki ibada pamoja na watu wenye imani moja na wewe kila mara.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nini maana ya Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu?
Fahamu Maana ya Mithali 15:24 Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;
JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.
SWALI: Nini maana ya Yeremia 31:30 “Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi”.
JIBU: Zamani za agano la kale katika taifa la Israeli, kulikuwa na usemi maarufu, unaosema “Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi”.
Kikawaida zabibu au matunda mengine yenye asidi nyingi mtu alapo , huwa meno yanatia ganzi, lakini kamwe haiwezekani mtu mwingine akatiwa ganzi kwa ulaji wa mwingine.
Hapa Waisraeli wakiwa wanamaanisha kuwa adhabu za Mungu huwa zinatembea hata kwa kizazi cha watu, Lakini Mungu kwa kinywa cha Yeremia anawasahihisha kuwa hilo si jambo lake..Anawaambia kila mtu ataadhibiwa sawasawa na uovu wake, wala watoto hawatauchukua uovu wa wazazi wao..Jambo ambalo alilirudia pia kwa kinywa cha Nabii Ezekieli (Ezekieli 18:20).
Lakini pia ukisoma muktadha wa vifungu hivyo, utaona anatoa unabii wa agano jipya ambalo atalifanya na watu wake kupitia Yesu Kristo, akimaanisha kuwa wokovu wake pia , utakuwa ni wa mtu binafsi, mmoja mmoja. Tusome habari yote tokea juu.
Yeremia 31: 27 Tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapoipanda nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda, mbegu ya mwanadamu na mbegu ya mnyama.
28 Tena itakuwa, kwa kadiri nilivyowaangalia, ili kung’oa, na kubomoa, na kuangusha, na kuangamiza, na kutesa; kwa kadiri iyo hiyo nitawaangalia, ili kujenga, na kupanda, asema Bwana.
29 Siku zile, hawatasema tena, Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi.
30 Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi.
31 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.
32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.
33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
Hivyo vifungu hivi, vinatupa kutambua kuwa wajibu wa kulitunza agano la Mungu ni la mtu binafsi, sawasawa na alivyokuja kulifunua katika agano jipya kupitia Yesu Kristo, kwamba ijapokuwa wokovu umeachiliwa kwa wote, lakini haupokelewi kijumuiya, kifamilia, au kikabila, bali kibinafsi.
Kila mtu atalibeba furushi lake mwenyewe. (Wagalatia 6:5)
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Tafsiri ya Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.
Yeremia alikuwa na umri gani alipoitwa?
Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?