SWALI: Naomba kufahamu Warumi 7:25 ina maana gani?
Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi, kama ni hivyo, mimi mwenyewe kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.
JIBU: Katika sura yote ya saba, mtume Paulo, anaeleza kwa kina mapambano yaliyo ndani ya mwamini. Kwamba nia yake kutoka ndani ni kuitii sheria ya Mungu, lakini mwili wake kwa nje ni kikwazo kikubwa kiasi cha kumfanya ashindwe kabisa kutimiza maadhimio yake.
Warumi 7:19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. 20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu
Na ni kweli huo ndio uhalisia wa kila mtu. Na ndio maana mwishoni mwa sura hiyo anahitimisha kwa kueleza hali hiyo, Lakini katika vifungu hivyo, wengi wanatafsiri vibaya wakidhani Paulo anatetea udhaifu wa mwili hapana.. Kinyume chake alianza kwanza kueleza uhalisia wa kibinadamu, ili atoe suluhisho halisi la namna ya kushinda, ambalo ndio tunalisoma katika sura inayofuata ya nane (8)
Ambapo sasa kwenye sura ya nane(8) inayofuata, anaeleza namna ambayo Kristo anatusaidia kuishinda hiyo hali, kwa sheria nyingine mpya ya Roho ambayo anaiweka ndani yetu.
Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.
2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti. Maana yake ni kuwa, Roho Mtakatifu, anatuweka huru katika huo utumwa wa mwili unaotupelekesha.
Inahitaji tu kutii, kwa kumfuata Roho Mtakatifu, kisha yeye mwenyewe atatupa nguvu ya kushinda mambo yote ya mwilini. Lakini sio kwa kutegemea nguvu zetu tu wenyewe.
Warumi 8: 5 Kwa maana wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili; bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho.6 Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani.
7 Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii. 8 Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
9 Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.
10 Na Kristo akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki.
Hivyo ukiishi kwa kumtii Roho Mtakatifu, basi huwezi tumikishwa tena na mwili,
Wagalatia 5:16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. 18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.
Warumi 7:25, Paulo analenga hasaa sababu ya sisi kushindwa kutimiza sheria ya Mungu, Ni kwasababu ipo sheria nyingine (ya dhambi iliyojificha ndani yetu) ambayo ni ngumu kutoka kwa namna ya kibinadamu, hivyo anataka hilo tulijue ili tufahamu kuwa kwa nguvu zetu wenyewe hatuwezi kuishinda, Lakini kwa Yesu Kristo atupaye Roho wake ndani yetu, tukienenda kwa kumtii huyo, basi sheria hiyo ya dhambi tutaishinda kabisa kabisa.
Ni wito wa kila mwamini kujifunza kutembea katika Roho.
Je! Unafahamu namna ya kutembea katika Roho kama sio. Basi tutumie ujumbe kwa namba uzionazo chini ya somo hili tukutumie.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Nyaraka za Paulo tunaona ni barua kwenda kwa makanisa yaliyokuwepo wakati huo, kama Korintho, Efeso, Kolosai na Galatia na nyingine kwenda kwa watu waliokuwepo wakati huo, kama Timotheo, Tito na Filemoni sasa iweje nyaraka hizo zituhusu na sisi na hata ziwe ni neno la MUNGU?, na kuzitumia hizo kufundishia sasa?
Jibu: Swali zuri lakini ili tuweze kupata majibu yaliyojitosheleza, hetu tutafakari mifano ya kawaida iliyopo,
Alikuwepo mwanasayansi mmoja wa kijerumani maarufu ambaye sasa ni marehemu ajulikanaye kama Albert Einstein (Mgunduzi wa kanuni ya kutengeneza bomu la Nyuklia), huyu wakati wa vita vya pili vya dunia alimwandikia waraka Raisi wa Marekani aitwaye Roosevelt, kwamba atengeneze silaha ya Nyuklia, kabla Adolf Hitler hajaitengeneza, na katika waraka huo alimpa pia hiyo fomula/kanuni ya kutengeneza silaha hiyo. (Waraka huo uliandikwa mwaka Agosti 2,1939).
Na matokeo ya waraka huo ni Raisi Roosevelt kuunda bomu la Nyuklia, na kwenda kulifanyia majaribio katika miji miwili ya nchi ya Japani (Mji wa Heroshima na Nagasaki).
Lakini ajabu ni kwamba baada ya wakati huo, sehemu za waraka huo zilizobeba kanuni za utengenezaji wa nyuklia zilivuja na kufikia mataifa mengine, na mataifa hayo kama Urusi hayakulaza damu bali nayo pia yakaunda mabomu ya nyuklia yenye kanuni ile ile, zilizokuwepo ndani ya ule waraka.
Na cha ajabu zaidi ni kwamba miaka mingine mingi mbele mataifa mengine kama Ufaransa, Pakistani,India, na mengine machache yakaichukua kanuni hiyo hiyo ya kuunda bomu la Nyuklia na kutengeneza mabomu yao,
Na cha kushangaza zaidi na zaidi ni kwamba mataifa mengine mengi leo yanafanya jitihada kuunda mabomu yao kupita kanuni ile ile ya mwanasayansi huyo Albert Einstein aliyetokea miaka mingi huko nyuma kupitia waraka wake aliomwandikia Raisi wa Marekani.
Sasa swali la kujiuliza, ni hili; kulikuwa kuna haja gani ya Mataifa kama Urusi, Ufaransa, na mengineyo kufuatilia waraka Einstein aliomwandikia Raisi Roosevelt na hata kuzitumia kanuni/fomula alizoziandika ndani yake kutengeneza mabomu yao??..
Tulitegemea waraka wa Einstein kwenda kwa Raisi huyo, uishe matumizi baada ya kusomwa na kutumika na Raisi huyo wa Marekani, lakini ajabu ni kwamba mpaka sasa una matokeo katika ulimwengu wetu, ingawa uliandikwa miaka mingi iliyopita.
Kwahiyo Utaona kwamba sababu pekee ya mataifa mpaka leo hii kuitumia kanuni ya mwanasayansi huyo aliyetokea miaka mingi huko nyuma ni kwasababu alichokigundua Albert Einstein ni kitu cha Kweli chenye manufaa na tija si tu kwa wakati wake tu, au Taifa lake tu bali hata kwa mataifa mengine na kwa vizazi vingi vijavyo.
Na ni hivyo hivyo Nyaraka za Mtume Paulo na za Mitume wengine… kwa jicho la nje zitaonekana kama zimeandikwa kwaajili ya makanisa yale ya wakati ule, au kwaajili ya watu wa wakati ule, lakini kwa jicho la rohoni ni ujumbe kwetu zaidi hata ya watu wa wakati ule.
Kwasababu yaliyoandikwa katika nyaraka za Mitume wa kwenye Biblia ni maneno ya kweli yanayoishi katika vizazi vyote, na tena kwa jinsi muda unavyozidi kwenda ndivyo yanavyohitajika zaidi kwasababu yaliyokuwa yanatendeka zamani, sasa hivi yamezidi mara nyingi sana.
Vita vya kiroho walivyokuwa wanapigana watu wa kanisa la Korintho, Galatia, na mengineyo nyakati hizo ndizo tunazopambana sasa, tena wakati huu zimezidi zaidi, kwahiyo tunahitaji fomula na kanuni za wanasayansi wetu wa kiroho (Mitume na manabii wa kwenye Biblia) kutengeneza silaha zetu za kiroho sasa, na kupambana hivi vita mpaka tushinde.
Lakini tukibaki na kusema zile nyaraka zilikuwa ni za wakorintho tu peke yao na wagalatia tu peke yao, na kwamba sisi hazituhusu tutamalizwa vizuri na shetani, ni sawa na Taifa la Urusi liseme ule waraka wa Einstein aliomwandikia Raisi wa Marekani, kuhusu utengenezaji wa Nyuklia uliwahusu Wamarekani peke yao, wangekuwa na akili hiyo, leo wangeisha, au wangetawaliwa!.
Na sisi ni lazima tuiamini Biblia, kuwa ni Neno la MUNGU linaloishi kwa nyakati zote na vizazi vyote, hakuna wakati litaisha matumizi, au litapitwa na wakati, Mafunuo yaliyokuwemo ndani ya Biblia yana nguvu na Uwezo, kwani waliofunuliwa wamefunuliwa kwa uweza wa Roho Mtakatifu na si kwa akili zao.
Mwisho; Je umempokea YESU kwelikweli au kidini?.. kama maisha unayoishi ni ya uvuguvugu bado hunaye YESU, unamhitaji YESU aingie maishani mwako, unahitaji kujikana nafsi na kubeba msalaba na kumfuata YESU, Fanya mageuzi na acha kuishi maisha ya uvuguvugu, kwani tunaishi nyakati za hatari na muda umeenda sana, na parapanda inalia muda wowote, na mambo yote yatapita.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Timotheo alikuwa wapi wakati anaandikiwa nyaraka zake na mtume Paulo?
Je ni nyaraka zipi mtume Paulo aliziandikia gerezani?
NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)
Sadaka inayotolewa kwa mwongozo wa Neno la MUNGU ina matokeo makubwa sana kwa anayeitoa. Yapo madhara yanayoondoka kwa maombi tu peke yake, lakini yapo mengine yanahitaji sadaka pamoja na maombi.
Hebu turejee Biblia kidogo tujifunze jambo..
Wakati ambapo Nabii Samweli anataka kwenda kumpaka mafuta Daudi ili awe mfalme mahali pa Sauli..biblia inatuambia kuwa alipofikiri kwenda tu hofu ilimwingia..
Na hofu hiyo ni kwamba alimwogopa Mfalme Sauli, kwani alijua kabisa endapo Sauli akisikia mtu mwingine anaenda kupakwa mafuta ya kifalme kuchukua sehemu yake, wivu utamwingia na atataka kumwua nabii Samweli na yule atakayeenda kupakwa mafuta.
Sasa ili zoezi la Daudi kupakwa mafuta likamilike bila kuleta madhara yoyote kwa Nabii Samweli na Daudi anayeenda kupakwa mafuta ya kifalme, SADAKA ILIHUSIKA!.
Utauliza ilihusika vipi?…turejee maandiko…
1 Samweli 16:1 “BWANA akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe.
2 Samweli akasema, Nawezaje kwenda? Sauli akipata habari, ataniua. Basi BWANA akasema, Chukua ndama pamoja nawe, ukaseme, Nimekuja ili kumtolea BWANA dhabihu.
3 Ukamwite Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonyesha utakayotenda; nawe utamtia mafuta yule nitakayemtaja kwako”
Je umeiona nafasi ya sadaka katika kuyaokoa maisha ya Samweli na Daudi?.
Hapo MUNGU hakushindwa kumwambia nabii Samweli aende hivyo hivyo na kwamba atamlinda!…La! Hakufanya bali alimwambia aende na dhabihu..
Jambo hilo Bwana MUNGU wetu aliliruhusu pia ili tuelewe umuhimu dhabihu/sadaka.
Unapomtoleo MUNGU kwa ufunuo wa Neno, bila kushurutishwa na mtu wala uchungu, kuna mambo mengi katika ulimwengu wa roho yanafanyika, kama ni nira za mauti zinalegea na kama kuna vifungo vya dhambi pia vinaondoka.
Na kumbuka sadaka kwa BWANA inapelekwa kwa BWANA, maana yake mahali ambapo BWANA anatumikiwa (mfano kanisani au mahali panapofanyika kazi ya MUNGU ikiwemo mikitano ya injili)..hapo ndipo penye neema.
Usipeleke sadaka yako maalumu mahali pengine kama kwa marafiki, au watu au maskini wa barabarani…ni vizuri kufanya hivyo na kuna baraka zake lakini vya Bwana vinapaswa vipelekwe kwa Bwana ndivyo maandiko yanavyofundisha..
Tenga kiasi chako kungine peleka kwa maskini na wenye uhitaji, lakini hakikisha una sadaka yako maalumu kwa BWANA utakayopeleka aidha kanisani au mahali popote kazi ya MUNGU inapofanyika kwa usahihi.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, Hutoa sauti yake katika viwanja; 21 Hulia penye mikutano mikubwa ya watu, Mahali pa kuyaingilia malango, Ndani ya mji hutamka maneno yake.
Kibiblia, hekima, ni uwezo wa kupambanua , kuhukumu na kufanya maamuzi yenye matokeo makamilifu ya Ki-Mungu duniani.
Kwamfano, biblia inatuambia kwa hekima Mungu aliziumba mbingu na nchi (Mithali 8:22-31)
Sulemani alimwomba Mungu hekima ya kuchunga na kufanya hukumu kwa watu wake Israeli, na Mungu akampa, Danieli alipewa hekima ya upambanuzi wa ndoto na maono yote ya siri,
Kwa ufupi hekima ya ki-Mungu ni zaidi ya maarifa, elimu, au akili, ni uwezo wa juu sana ambao unazidi upeo wa ki-binadamu.
Kumbuka Biblia inaitaja hekima pia kuwa ni mtu. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.
1Wakorintho 1:24 bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu.
Na kama Ndio hekima mwenyewe..Basi ndani yake matunda yote ya hekima yapo.
Wakolosaia 2:3 ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.
Hivyo ili mtu kuiona hekima tafsiri yake ni kuwa anapaswa amwone YESU. Na kumwona Yesu ni kumpokea kama Bwana na mwokozi wa maisha yako (Warumi 10:9), pamoja na kumtii kutembea katika njia zake.
Katika mahubiri, Mahubiri yanapatikana wapi? Kila mahali, kwenye njia kuu, viwanja, kwenye mikutaniko ya watu, mastendi, masokoni, mitandaoni n.k.
Anapazaje sauti?
Anapaza sauti kupitia watumishi wake mbalimbali Aliowatuma kumuhubiri.
Hivyo, hilo andiko linalosema,
Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, Hutoa sauti yake katika viwanja; 21 Hulia penye mikutano mikubwa ya watu, Mahali pa kuyaingilia malango, Ndani ya mji hutamka maneno yake.
Unaweza kuelewa sasa analenga injili, inayohubiriwa kila mahali duniani kote. Ukweli ni kwamba hakuna mtu anayeweza kusema hajawahi kuisikia injili, kwasababu kila mahali inahubiriwa kwa nguvu. Kuonyesha kuwa hekima haijajificha ipo sikuzote, bali ni watu ndio wanaikwepa.
Mtu yeyote anayemwamini Kristo basi tayari amefungua mlango wa ufahamu mkubwa sana unaoweza kufungua mambo yote katika hii dunia.
Bwana akubariki.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JIBU: Haya ni maneno ya kiyunani, yanayoeleza namna tofauti ya kutafsiri maandishi.
Ni namna ya kutafsiri maandiko kwa kuzingatia mtazamo wa awali uliokusudiwa na mwandishi, kwa kuzingatia muktadha, hali ya kihistoria, matamshi na matumizi ya lugha.
Ni namna ya kutafsiri Maandiko kwa namna ya mtazamo wa mtu mwenyewe, kwa kulileta andiko liendane Na wazo lake binafsi,. Namna hii haitilii maanani sana kusudio La kwanza la mwandishi, bali lile aliaminilio kuwa ni sahihi Kwake. (Mfano wa hii ni ile namna ya kusema nimefunuliwa)
Kwa ufupi eksejesisi ni Kuliruhusu andiko lijitafsiri lenyewe huku Eisojesisi ni lilete andiko litafsiri ninachokitaka au kiamini.
Ijapokuwa Eksejesisi,(tafsiri ya awali) ndio msingi hasaa wa kusimamia katika kuyaelewa maandiko lakini eisojesisi pia Mungu huitumia kusema na sisi katika nyakati Fulani.
La kuzingatia ni kwamba kabla hujaipokea namna nyingine.. Ifahamu kwanza asili ya kwanza ya andiko hilo, ilikuwa ni nini.
Kwamfano Bwana Yesu aliposema.
Mathayo 11:28
[28]Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
Katika Eksejesisi hiyo mizigo inayozungumziwa hapo na Bwana Yesu sio umaskini, Mateso, madeni, familia, majukumu,n.k. hapana, bali mizigo ya dhambi. Ndicho Bwana Yesu alichomaanisha na kusudi la kwanza lililomfanya kuja duniani lilikuwa ni hilo kumkomboa mwanadamu kutoka katika dhambi zake.
Lakini pia Bwana anaweza tumia andiko hilo kulenga na mizigo mingine, kwasababu ni ukweli usiopingika alisema pia tumtwike yeye fadhaa zetu zote.
1 Petro 5:7
[7]huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.
Hivyo namna zote Mungu anaweza kutumia kutujenga. Kwasababu Neno lake ni pana na njia zake hazichunguziki, katika kuwajenga, kuwafariji na kuwaponya watu. Isipokuwa hatari inakuja mtu kukosa kulipambanua vizuri Neno na matokeo yake kutegemea zaidi mtazamo (alioupokea), na kuacha biblia yenyewe kujieleza.
Hii ndio Imekuwa chumbuko la mafundisho mengi ya uongo, na potofu, kwamfano mtu atasema chapa ya mnyama (ufunuo 13) Ni ugonjwa wa Korona (covid-19). Wakati si kweli.
Au mtu atasema Yesu alitengeneza matope kwa mate yake akampaka mtu machoni akaona,(Yohana 9:6-7) hivyo na sisi kufanya kwa namna hiyo si kosa. Kumbe lile lilikuwa ni “ingilio la Mungu” la wakati husika lakini sio agizo la kudumu. Kwani agizo la daima ni kutumia jina la Yesu kutenda/kuamuru jambo lolote.(Kol 3:17)
Hivyo ili kubaki katika upande sahihi ni vema ukajifunza eksejesisi, (kufahamu muktadha wa kimaandiko), na ndio pale esiojesisi inapokuja Basi unaeweza Kuligawanya vema Neno la Mungu. Bila kuleta uharibifu/ madhara yoyote, katika imani au kwa kile unachowafundisha wengine.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Jina la Mwokozi YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze Biblia Neno la MUNGU wetu, lilio taa na mwanga wa njia yetu.
Unapofika wakati MUNGU wetu wa UPENDO, anapotaka kututoa sehemu moja kwenda sehemu nyingine kwa kuondoa matatizo makuu yanayotishia maisha yetu, basi huo haondoi tu chanzo cha tatizo bali pia na mkondo wake wote anauondoa.
Ili tuende pamoja, hebu turejee wakati Bwana YESU anazaliwa, maandiko yanasema Herode alitafuta kumwua mtoto YESU, lakini Yusufu na Mariamu kupitia onyo la Malaika wa Bwana waliambiwa wakimbilie Misri ili Herode asimwue mtoto.
Lakini jambo la ajabu ni kwamba baada ya Herode kufa, biblia inatuambia hakufa peke yake bali na wengine waliokuwa na nia kama ya kwake ya kumwangamiza mtoto, ambao biblia haijawataja majina yao.
Mathayo 2:19 “Hata alipofariki Herode, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto huko Misri,
20 akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mamaye, ushike njia kwenda nchi ya Israeli; kwa maana WAMEKUFA WALIOITAFUTA ROHO YA MTOTO”.
Hapo anasema “WAMEKUFA”..na si “AMEKUFA” Maana yake hakuwa mmoja bali wengi, maana yake si Herode peke yake, walikuwepo na wengine waliokuwa na nia kama ya Herode…huenda wakuu wa majimbo waliofanya kazi na Herode, au makuhani au raia wa kawaida.
Kwahiyo waliokuwa wanaitafuta roho ya mtoto, hawakuwa wachache, bali wengi (ulikuwa ni mkondo) na wote walikufa..Herode alikuwa tu ni kichwa cha pweza, lakini mikia ilikuwa mingi!.
Endapo Yusufu na mtoto wangeendelea kubaki Bethlehemu walikuwepo wapelelezi wengi hivyo taarifa kuhusu mtoto zingemfikia Herode haraka, hata baada ya yale maangamizi kupita bado hatari ilikuwepo, kwahiyo suluhisho ni wote wafe kwanza ndipo usalama uwepo wa Bwana YESU kurudi Israeli.
Sio hilo tu, utakumbuka pia ile habari ya Malkia Esta, wakati Hamani, adui wa wayahudi alipoandika waraka wa wayahudi wote kuuawa, katika siku moja!.. kama ni mwanafunzi wa Biblia utagundua kuwa si Hamani peke yake aliyekuwa adui wa waisraeli kwa wakati ule!, bali walikuwepo wengine wengi katika kila jimbo la mfalme Ahasuero, Hamani yeye alikuwa ni kichwa tu cha pweza kama alivyokuwa Herode!.
Ndio maana mambo yalivyoharibika kwa Hamani, hakufa peke yake bali na maadui wote wa wayahudi katika ufalme wote.
Esta 9:1 “Hata ulipofika mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari, siku yake ya kumi na tatu, amri ya mfalme na mbiu yake ilipowadia kutekelezwa; ambayo siku ile ADUI ZA WAYAHUDI walitumaini kuwatawala, bali kumebadilika kinyume, hata Wayahudi waliwatawala wale waliowachukia;
2 siku ile ile Wayahudi wakakusanyika mijini mwao katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero ili kuwatia mikono wale watu waliowatakia hasara; wala asiweze mtu kuwazuia, kwa kuwa hofu yao imewaangukia watu wote. …….
5 Basi Wayahudi wakawapiga adui zao wote mapigo ya upanga, na machinjo, na maangamizo, wakawatenda kama wapendavyo wale waliowachukia.
6 Hata huko Shushani ngomeni Wayahudi wakawaua watu mia tano, na kuwaangamiza…………
16 Nao Wayahudi wengine waliokaa katika majimbo ya mfalme walikusanyika, wakazishindania maisha zao, wakajipatia raha mbele ya adui zao, wakawaua waliowachukia, WATU SABINI NA TANO ELFU; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono”.
Watu zaidi ya Elfu 75 walikufa pamoja na HAMANI, ingawa kwa haraka tunaweza kuona kama aliyekuwa adui wa wayahudi alikuwa ni Hamani peke yake, kumbe hakuwa peke yake bali ulikuwa ni mkondo mkubwa ibilisi alioutengeneza kwa muda mrefu!.
Hivyo ukiona mtu mmoja mashuhuri anafanya vita na wewe katika vitu vilivyo sahihi unavyovifanya basi fahamu kuwa hayupo peke yake bali upo mkondo wa ibilisi nyuma yake!, na wakati wa MUNGU ukifika huwa anakiondoa chanzo na mkondo wake, ili amani irejee..
Na MUNGU anapokiondoa chanzo na mkondo wake si lazima awaue maadui zako kama inavyodhaniwa na wengi, La! Kifo chaweza kuwa njia ya mwisho kwa MUNGU wetu dhidi ya tunaowaona kama maadui zetu,
Lakini badala yake MUNGU anaweza kuwahamisha na kuwapeleka mbali au kukuhamisha wewe ukae mbali nao sehemu salama, au anaweza kuwabadilisha na kuwafanya watu wazuri (wakamrudia MUNGU)..na lile tatizo likawa limeondoka, na hambadilishi yule chanzo tu peke yake, bali na mkondo mzima, Ndio hapo unashangaa watu waliokuwa wanakuchukia na kukupiga vita sasa wanakupenda, waliokuwa maadui zako sasa mnaishi kwa amani n.k
Swali: Niombe maombi gani ili Mungu aondoe chanzo cha matatizo na mkondo wake?
Badala ya kufikiri namna ya kuomba, fikiri kuzitengeneza njia zako mbele za MUNGU, njia zako zinaponyooka mbele za MUNGU (kwa kuishi maisha ya kumpendeza MUNGU), basi MUNGU anashughulika na vyanzo vyote na mikondo yake, kwa kukurejeshea amani..
Mithali 16:7 “Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye”.
Lakini usiponyoosha njia zako kwa MUNGU, na ukategemea maombi tu peke yake, bado safari itakuwa ndefu, Maisha yetu yanajalisha sana katika kuelezea vyanzo vya matatizo tuliyonayo, yakizidi kuwa safi mbele za MUNGU ndivyo matatizo yatakavyozidi kuwekwa mbali.
Je umempokea YESU?.
Unao uhakika Bwana YESU akirudi leo unakwenda naye?
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Ni kwa namna gani Bwana YESU alikula Siagi na Maziwa? (Isaya 7:15)
Kuonja ni kufanya nini? (Kutoka 15:25).
NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?
Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?
Shalom,
Je unajua Pepeto ni nini na kazi yake ni ipi?
Turejee Mathayo 3:11-12.
Mathayo 3:11 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
12 Ambaye PEPETO LAKE li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake; na kuikusanya NGANO yake ghalani, bali MAKAPI atayateketeza kwa moto usiozimika”.
Pepeto ni kifaa maalumu chenye umbile kama la “UMA” ambacho wakulima wa nafaka kama ngano, wanakitumia kupuria/kupepetea ngano.. sasa jamii zetu zinatumia NYUNGO kupepetea nafaka kama mchele na ngano, ambapo ungo ule unazurusha juu nafaka kisha upepo unatenga ile nafaka na makapi.
Lakini zamani wakulima wa ngano hawakutumia nyungo, kwani kulikuwa na matita mengi ya ngano, hivyo UNGO usingetosha kuimaliza kazi yote, hivyo walitumia kifaa hiko kinachoitwa Pepeto, ambacho kinafanana sana na UMA. (Tazama picha chini).
Sasa kiroho Ngano ni “NENO LA MUNGU”, na makapi ni “NDOTO NA MAONO YA UONGO” katika siku za mwisho Bwana atatenga Neno lake na maono ya uongo, na watu wanaolifuata Neno lake na wanaofuata manabii wa uongo.
Yeremia 23:25 “Nimesikia waliyoyasema manabii wanaotabiri uongo kwa jina langu, wakisema, Nimeota ndoto; nimeota ndoto.
26 Je! Mambo hayo yatakuwa katika mioyo ya manabii wanaotabiri uongo hata lini, manabii hao wenye udanganyifu katika mioyo yao wenyewe?
27 Wanaodhania ya kuwa watawasahaulisha watu wangu jina langu kwa ndoto zao, wanazomhadithia kila mtu jirani yake, kama vile baba zao walivyolisahau jina langu, kwa ajili ya Baali.
28 Nabii aliye na ndoto, na aseme ndoto yake; na yeye ALIYE NA NENO LANGU, na aseme neno langu kwa uaminifu. MAKAPI NI KITU GANI KULIKO NGANO? Asema Bwana”.
Mstari wa mwisho hapo anasema, “Makapi ni kitu gani kuliko Ngano” ikimaanisha kuwa makapi ni unabii/ndoto za uongo zinazotolewa na manabii wa uongo si kitu mbele ya Neno la MUNGU linalofananishwa na Ngano.
Kwahiyo katika siku za mwisho, YESU KRISTO ambaye ndiye pepeto lenyewe, atatenga makapi na ngano, na wanaotumainia makapi na wale wanalotumainia Neno lake.
Hizi si siku za kupelekwa huku na kule na manabii wa uongo, wanaoshinda kutwa kuchwa kutabiri maono ya uongo, wakiwaaminisha na kuwatumainisha watu katika vitu vya ulimwengu huu, kwamba kuwa na hivyo ndio kielelezo cha kwanza cha kukubaliwa na MUNGU.
Bwana YESU alisema, itamfaidia nini mtu apate ulimwengu mzima na kisha apate hasara ya nafsi yake (Marko 8:36)?..maana yake utabiriwe na nabii au mchungaji au mtume kwamba utapata hiki na kile cha ulimwengu huu, na wakati huo huo haioni dhambi maishani mwako, je hayo aliyokutabiria yatakufaidia nini ikiwa utapoteza uzima wa milele?
Hizi ni siku za mwisho na pepeto hili limeshaanza kupita, na Roho Mtakatifu anawatenga walio wa kwake, hatua hizo zikimalizika kinachofuata ni unyakuo wa kanisa, ambapo walioishi na kulifuata Neno la MUNGU watakusanywa ghalani (mbinguni).. lakini waliofuata makapi watatupwa katika lile ziwa la moto, ndivyo maandiko yanavyosema..
Mathayo 13:29 “Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.
30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu…
40 Basi, kama vile magugu yakusanywavyo na kuchomwa motoni; ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia.
41 Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi,
42 na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MAMBO SITA, AMBAYO MUNGU HUTUMIA KUONDOA UOVU NDANI YA MTU.
Ipi tofauti kati ya Uhai na Uzima kibiblia?
KIMBIA MACHAFU YA DUNIA. (2Petro 2:20)
Je kibiblia ni sahihi kuadhimisha jumapili ya mitende?
“Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia;Achukiaye mambo ya dhamana yu salama
Jina la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe daima.
Je unajua matendo ya Imani, yanaweza kuleta utambulisho mwingine kwako tofauti na ule wa kwanza, na kibali kipya.
Turejee Biblia, kisa cha Daudi kumwua Goliati, biblia inaonyesha kuwa kabla ya Daudi kumwua Goliati, alikuwa anaishi nyumbani kwa Mfalme Sauli katika jumba la kifalme, na kazi yake pale ilikuwa ni kupiga kinubi, wakati roho mbaya ilipomjia Sauli.
1Samweli 16:21 “Basi Daudi akamwendea Sauli, akasimama mbele yake, naye akampenda sana; naye akapata kuwa mtu wa kumchukulia silaha zake.
22 Kisha Sauli akapeleka watu kwa Yese, akasema, Tafadhali, MWACHE DAUDI ASIMAME MBELE YANGU; MAANA AMEONA KIBALI MACHONI PANGU.
23 Ikawa, ile roho mbaya kutoka kwa Mungu ilipomjilia Sauli, ndipo Daudi akakishika kinubi, akakipiga kwa mkono wake, naye Sauli akaburudishwa, na ile roho mbaya ikamwacha”.
Hapa tunaona tayari Mfalme Sauli amemjua Daudi na tena amemfanya kuwa mchukua silaha wake, sasa ni ngumu kumfanya mtu kuwa mchukua silaha, kama bado hujamjua wala kumkubali.
Lakini tukiendelea kusoma habari hii mbele kidogo baada ya Daudi kumwua Goliati tunaona jambo lingine la kushangaza.. kwamba Sauli anamwuliza tena Daudi yeye ni mwana wa nani, kana kwamba alikuwa hamjui hapo kwanza..
1Samweli 17:54 “Naye Daudi akakitwaa kichwa chake yule Mfilisti na kukileta Yerusalemu; lakini silaha zake akaziweka hemani mwake.
55 Basi Sauli, hapo alipomwona Daudi akitoka ili kumwendea yule Mfilisti, alimwambia Abneri, jemadari wa jeshi, Je! Abneri, kijana huyu ni mwana wa nani? Abneri akamjibu, Ee mfalme, kama iishivyo roho yako, mimi siwezi kusema.
56 Basi mfalme akasema, Uliza wewe, KIJANA HUYU NI MWANA WA NANI.
57 Hata na Daudi alipokuwa yuarudi kutoka katika kumwua yule Mfilisti, Abneri alimtwaa, akamleta mbele ya Sauli, naye anacho kichwa chake yule Mfilisti mkononi mwake
58 Basi Sauli akamwuliza, Wewe, kijana, u mwana wa nani? Naye Daudi akamjibu, Mimi ni mwana wa mtumishi wako, Yese, mtu wa Bethlehemu.”
Kama Daudi asingefanya tendo lile la imani na kishujaa, la kumwua Goliati, Mfalme asingemjua Daudi, ingawa tayari alishajitambulisha kwake na hata kuishi naye… Baada ya tukio hilo tunazidi kuona kibali cha Daudi kuongezeka kwa kiwango kingine.
1Samweli 18:1 “Ikawa Daudi alipokwisha kusema na Sauli, roho ya Yonathani, ikaambatana na roho ya Daudi, Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe”.
Hapo kabla Yonathani huwenda alikuwa anamwona Daudi kama mwimba ngojera tu! kwenye nyumba ya mfalme.
Kama Goliati akiendelea kusimama katika maisha yako usipomwangusha kwa imani unaweza kuendelea kubaki pale pale, lakini kama ukichukua mawe matano kama Daudi na kumwangusha chini, basi hapo umefungua kibali kipya!.. Jina lako linakuwa sio lile lile tena, nafasi yako sio ile ile tena, kujulikana kwako kunakuwa sio kule kule tena.
Goliati ni roho yoyote inayojiinua ya vitisho, na Goliati wa kwanza katika maisha yetu ni Dhambi!.. Huyu ndiye anayesumbua!, ndiye anayeficha kibali chetu, ndiye anayeficha nafasi zetu na kutuzuilia kusonga mbele, tukiweza kumwangusha huyu na jeshi lote la wafilisti (magonjwa, shida, na mambo mengine yatesayo) yanakimbia, na tunabaki washindi na wenye kibali kingine.
Je umetubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha?..kama bado ni nini unasubiri?.. kumbuka kuomba msamaha sio kutubu, bali toba halisi inakamilishwa kwa kuacha matendo yote mabaya ya giza, maana yake baada ya kuomba msamaha wa dhambi kutoka kwa MUNGU, kinachofuata ni kuacha zile njia mbaya, ikiwemo kujitenga na makundi ya watu yanayopalilia dhambi iliyokuwa inakusumbua.
Vile vile kuacha kufanya vitu, au kuangalia vitu vilivyokuwa vinakukosesha, na pia kuacha kuvaa mavazi yaliyokuwa yanakaribisha dhambi maishani mwako. Kwa kufanya hivyo utakuwa umemwangusha Goliati na kubali chako kitaongezeka kama ilivyokuwa kwa Daudi.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini MUNGU alimzuia Daudi asimjengee HEKALU? (1Nyakati 17:12)
Daudi alikuwa na wake wangapi, na je ni halali kuwa na wake wengi?
Waanaki ni watu gani katika biblia?
JE! UNAWEZA KUWA NA GEUKO KAMA LA DAUDI?
Swali: Katika kitabu cha Mathayo 17:4 Mtume Petro na wenzie waliwezaje kufahamu kuwa wale ni Musa na Eliya?
Jibu: Turejee habari hiyo kuanzia ule mstari wa kwanza..
Mathayo 17:1 “Na baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani;
2 akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang’aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru.
3 Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye.
4 Petro akajibu akamwambia Yesu, Bwana, ni vizuri sisi kuwapo hapa; ukitaka, nitafanya hapa vibanda vitatu, kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya”.
Biblia haijaeleza kama Musa na Eliya walijitambulisha katika maono yale, ikiwa na maana kuwa kuna njia nyingine iliyowafanya Petro na wenzie kujua kuwa wale ni manabii Musa na Eliya na si wengine.
Sasa njia Pekee iliyomfanya Petro na wenzie kufahamu kuwa wale walikuwa ni Musa na Eliya na si wengine, ni UFUNUO WA ROHO MTAKATIFU.
Kama vile ufunuo wa Roho Mtakatifu ulivyomjia Petro kumhusu YESU.
Mathayo 16.15 “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?
16 Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni”.
Umeona hapo?, aliyemwambia Petro kuwa YESU ni KRISTO tena ni MWANA WA MUNGU aliye juu sio YESU mwenyewe!, bali ni ufunuo wa alioupokea kutoka kwa Baba.
Na hiyo sio ajabu kwani walikuwa wameenda mlimani kuomba.. ni kawaida kwa watumishi wa MUNGU kupokea mafunuo ya mambo yaliyopo, au yajayo wanapokuwa katika maombi, hususani kama hayo ya mlimani.
Kwahiyo Mtume Petro na wenzie walipata ufunuo wa ujio au uwepo wa manabii hao wawili wakiwa katika maombi, utaona jambo kama hilo lilishatokea tena kwa Petro wakati yupo kwa Yule Simoni mtengenezaji wa ngozi wa kule Yafa, wakati ambapo Roho Mtakatifu alimfunulia alipokuwa katika maombi kuwa kuna watu watatu wanamwulizia, hivyo aende nao asiogope!, na kweli ikawa hivyo..
Matendo 10:17 “Hata Petro alipokuwa akiona shaka ndani ya nafsi yake, maana yake ni nini maono hayo aliyoyaona, wale watu waliotumwa na Kornelio, wakiisha kuiulizia nyumba ya Simoni, wakasimama mbele ya mlango,
18 wakaita; wakauliza kwamba Simoni aitwaye Petro anakaa humo.
19 Na Petro alikuwa akiyafikiri yale maono. Roho akamwambia, Wako watu watatu wanakutafuta.
20 Basi ondoka ushuke ufuatane nao, usione tashwishi, kwa maana ni mimi niliyewatuma.
21 Petro akawashukia wale watu, akanena, Mimi ndiye mnayemtafuta. Mmekuja kwa sababu gani?”
Kwa namna hiyo hiyo, huenda Petro na wenzake walipokea ufunuo kuwa wale ni Musa na Eliya, labda walipokea ufunuo huo muda mchache kabla hawajawatokea, au wakati ule ule walipotokea.
Kikubwa tunachoweza kujifunza ni kuwa tuwapo katika uwepo wa MUNGU kama katika maombi, ni rahisi kupokea ufunuo wa Roho Mtakatifu kwani tunakuwa tupo katika roho, na mtu anapokuwa katika roho anayatambua mambo yote ya rohoni pasipo kuambiwa!
Hivyo ni muhimu sana kuwa waombaji, na wasomaji wa Neno la MUNGU, endapo akina Petro wangekuwa si watu wa kusoma maandiko, ni dhahiri kuwa wasingemjua Musa wala Eliya na hiyo ingezuia Roho kuwafunulia watu hao, kwani Roho Mtakatifu anamfunulia mtu kitu ambacho kinahusiana na Neno la MUNGU.
Je na wewe ni mtu wa kudumu uweponi mwa MUNGU? Je KRISTO YESU?..Je unao uhakika kwamba akirudi unaenda naye?
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini Eliya afunge Mbingu miaka mitatu na nusu? (1Wafalme 17:1)
TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?
Je! Tutatambuana tukifika mbinguni?
Je Mariamu alikuwa na umri gani alipochukua mimba ya Bwana YESU?
Je unaujua ufunguo wa wewe kumpenda Bwana zaidi?.. kuna jambo ukilifanya basi upendo wako kwa MUNGU utaongezeka kwa kiwango kikubwa sana.. Utajikuta unampenda MUNGU zaidi, unamheshimu zaidi na unamtumikia zaidi.
Na ufunguo huo si mwingine zaidi ya kuutafakari MSAMAHA WAKE KWAKO KWA MAPANA!.. Unaweza kuona jambo la msahama kwako ni dogo tu!.. Lakini nataka nikuambie Msamaha wa MUNGU kwako una uhusiano mkubwa sana na UPENDO WAKO KWAKE!.
Maandiko yanasema “aliyesamehewa sana hupenda sana, na aliyesamehewa kidogo hupenda kidogo”
Luka 7:47 “Kwa ajili ya hayo nakuambia, Amesamehewa dhambi zake ambazo ni nyingi kwa kuwa amependa sana; lakini asamehewaye kidogo, huyo hupenda kidogo”.
Hebu tafakari huu mfano: Mtu mmoja alikuwa anadaiwa shilingi 500 na mwenzake na akasamehewa na mwingine aliukwa anadaiwa shilingi laki 5 na mtu huyo huyo mmoja, naye pia akasamehewa kiasi chote cha pesa (shilingi laki 5)..
Je yupi kati ya hao wadaiwa wawili waliosamehewa, atampenda zaidi Yule aliyewasamehe?.. Bila shaka Yule aliyesamehewa deni kubwa ndiye atakayempenda zaidi aliyemsamehe, na hata kumheshimu sana..
Lakini Yule aliyesamehewa deni dogo, anaweza kuwa mtu wa shukrani lakini si katika kiwango kikubwa, na wala hawezi kutoa heshima ya kiwango kikubwa kwa yule aliyemsamehe.
Ni hivyo hivyo katika upande wa Imani, watu waliojiona ni wenye dhambi nyingi na kubwa kubwa!, na kujiona kama hawajastahili msahama kwa makosa yao, wanapoungama na kupokea msamaha, huwa wanampenda sana Bwana YESU na kumheshimu.
Lakini watu wanaojiona ni wasafi au watakatifu sana, kwamba hawamkosei sana MUNGU huwa hata upendo na MUNGU hawana, au upo kwa kiwango kidogo.
Sasa kiuhalisia wote tumemkosea MUNGU pakubwa sana!.. ukijiona huna dhambi nyingi, basi fahamu kuwa kuna shida kwako ya kutafakari, ambayo hiyo sasa ndio unapaswa ushughulike nayo.
Unapaswa ushughulike na hiyo hali mpaka ifikie hatua ujijue kuwa hukustahili, na wewe ulikuwa ni mbaya mno, na mbovu, na makosa yako yalikuwa makubwa sana!.. ukiweza kufikia hiyo tafakari, basi jua matunda yako ni wewe kumpenda BWANA na kumheshimu sana.
Unawezekana wewe sio mwizi, au muuaji au mzinzi lakini hebu tafakari vipindi ulivyomsema ndugu yako, na MUNGU alikufumbia macho, ingawa ulistahili adhabu ya mauti papo kwa hapo.
Hebu tafakari vipindi ulivyotamani vitu visivyofaa moyoni mwako, na MUNGU alikufumbia macho ingawa ulistahili kufa papo kwa hapo.
Hebu tafakari vipindi ulivyokasirika bila sababu, tafakari vipindi uliyokuwa unawaza mawazo mabaya, tafakari vipindi ulivyodanganya na kusema uongo, tafakari vipindi miguu yako ilipokuwa inaelekea kufanya maovu, tufakari vipindi ulivyotukana mdomoni na moyoni mwako, tafakari mambo ya upumbavu uliyoyafanya mitandaoni, hayo yote si kwamba MUNGU alikuwa haoni, au hata sasa hayaoni, anayaona yote!.
Inawezekana hujawahi kuua, lakini tafakari vipindi ulivyokuwa mbinafsi, tafakari visasi na vinyongo ulivyokuwa navyo, na huenda unavyo hata sasa, tafakari udunia wote ulioufanya, rudi nyuma kumbuka tukio moja baada ya lingine katika maisha yako, yatakafari sana halafu fikiri YESU AMEJITWIKA makosa yako yote hayo, ambayo kama si rehema zake huenda ungekuwa umeshakufa na upo KUZIMU sasa!.
Lakini alikizuia kifo kisikupate!, umempa nini?, au una umaalumu gani hata akusamehe hayo yote?, kwani waliokufa bila kupata huu msamaha wana kasoro gani zaidi yako?.
Je huoni kama aliyekupa huu msahama ni wa thamani kubwa? Huoni kama amekusamehe makubwa sana.. bado humpendi tu!.. ungepaswa uwe kuzimu muda huu, lakini bado unaishi! Bado kwako unamwona vile vile?
Ndugu tenga muda sana utafakari msamaha wa YESU, kwani ndio uliobeba funguo za kumpenda YESU zaidi, Ukiutafakari msamaha wa YESU utaishia kumpenda, lakini pia kumwogopa (kutokutenda dhambi tena)
Zaburi 130:4 “Bwana, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama?
4 Lakini kwako kuna msamaha, Ili Wewe uogopwe”.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NI KWA NAMNA GANI KRISTO ALIZIBEBA DHAMBI ZETU?
JE UMEUPOKEA UWEZA WOTE WA UUNGU NDANI YAKO?