Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

Wajibu wa wanandoa ni upi?

Mume: Kumpenda mke wake Kama mwili wake mwenyewe, ( Waefeso 5:25):  Ikiwemo kumuhudumia kiafya, kimavazi, kimalazi, na kiroho.

Mke: Kumtii Mume wake: Kumsikiliza, kumuheshimu, kukubali kuongozwa. (Waefeso 5:22).

Wote: Haki ya ndoa. (1Wakorintho 7:5)

Lakini ikitokea mmoja, ameshindwa kusimama katika nafasi yake, labda tuseme, mume hamjali mkewe, anampiga, anatoka nje ya ndoa, anamtukana, hamtimizii majukumu yake ya kimwili na watoto wake. Afanyaje?

Au mke hamweshimu mume wake, anamdharau, anafanya ukahaba, anamzungumzia vibaya kwa watu wa nje, anajiamulia mambo yake mwenyewe pasipo kumshirikisha mumewe..afanyaje?

Je! na yeye aache kutimiza wajibu wake?

Jibu ni hapana:  Embu wazia hili jambo; Ulishawahi kuishi katika nyumba ya kupanga, ambapo mnajikuta wapangaji mpo 10 mnashea umeme au maji, na kila mwisho wa mwezi bili inakuja, na mnapaswa muigawanye sawa sawa kwa kila mmoja wenu.  Kwa kawaida hapo panakuwa na ukinzani mkubwa, kwasababu wapo wengine watasema, mimi sina matumizi mengi kama ya Yule.. Na hiyo inapelekea mwingine kujiongezea  matumizi yake kwa makusudi ilimradi tu afanane na wale wengine, labda atufungulia bomba la maji ili yamwagike, ili mwisho wa mwezi utakapofika alipe sawasawa na matumizi ya wale wengine.

Lakini hajui kuwa anajiumiza yeye mwenyewe na wale wenzake, kwasababu anapoongeza matumizi ndipo gharama inapokuja juu zaidi, atalipa zaidi ya mwanzo. Ni heri angebakia vilevile akubali kuumia yeye, ili wote wapone.

Ndivyo ilivyo katika ndoa ikiwa mmoja hatimizi wajibu wake wa kindoa, suluhisho sio mwingine kujibu mapigo, bali ni kuendelea hivyo hivyo katika nafasi yake.  Ili kuinusuru ndoa. Kama mwanaume hakupendi, wewe mtii, mweshimu, msikilize, kama mwanamke hakutii, wewe mpende, mpe haki yake, ..

Na faida yake ni ipi?

  1. 1) Utamgeuza mwenzako:

Biblia inasema; .. 1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; 2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu”.

Inaendelea kusema;

1Wakorintho 7:16 “Kwa maana wajuaje, wewe mwanamke, kama utamwokoa mumeo? Au wajuaje, wewe mwanamume, kama utamwokoa mkeo?

 Haijalishi itachukua miaka mingapi. Kuwa mvumilivu, timizia wajibu kwao. Hayo mengine mwachie Mungu.

  • ) Utampalia makaa ya moto kichwani:

Mithali 25:21 “Adui yako akiwa ana njaa, mpe chakula; Tena akiwa ana kiu, mpe maji ya kunywa; 22 Maana utatia makaa ya moto kichwani pake; Na Bwana atakupa thawabu.

Hili andiko linaingia pia kwa wanandoa. Wakati unaona kama wewe unaonewa, hujui kuwa Yule mwingine anateswa rohoni  anapoona hurudishi mapigo, hilo jambo linakuwa ni moto mkubwa ndani yake, na sikumoja tu, atakuja kwa machozi, na kutubu mbele zako. Ni kitendo cha muda.

  • 3) Utampa Mungu nafasi ya kulipiza kisasi yeye mwenyewe:

Unapoumizwa, usidhani kuwa Mungu haoni, lakini unapomwachia Mungu yote, basi yeye peke yake ndiye atakayeshughulika kutafuta njia ya kutatua hilo tatizo. Kiboko cha Mungu kitapita, kitamnyoosha. Hivyo unapaswa uwe mtulivu, simama katika nafasi yako. Bwana atamtengeneza yeye mweyewe.. au atatengeneza njia kwa namna nyingine. Hivyo dumu katika utakatifu.

Warumi 12:17 “Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.

18 Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.

19 Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana”.

Zingatia hayo, usirejeshe ubaya kwa mwanandoa mwanzako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?

MJUE SANA YESU KRISTO.

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

NDOA NA HARUSI TAKATIFU.

VIJANA NA MAHUSIANO.

Kwanini Bwana Yesu alie machozi, na ilihali yeye ni Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments