TOFAUTISHA KATI YA MAFUNDISHO YA YESU, NA YA WAANDISHI.

TOFAUTISHA KATI YA MAFUNDISHO YA YESU, NA YA WAANDISHI.

Nakusalimu katika jina kuu lipitalo majina yote la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tuyatafakari maneno yake pamoja, Tukisoma kitabu cha Mathayo ile sura ya saba inatuambia..

Mathayo 7:28 “Ikawa, Yesu alipoyamaliza maneno hayo, makutano walishangaa mno kwa mafundisho yake;

29 kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye amri, wala si kama waandishi wao”.

Maandiko hayo yanatuonyesha, mafundisho ya Yesu yalikuwa ni ya tofauti sana na jinsi yalivyotegemewa na watu wengi wakati ule, na hata yanavyochukuliwa na watu wengi leo hii, hapo anasema alipoanza kufundisha makutano walishangaa “MNO”.. Ikiwa na maana maneno yake yalikuwa ni tofauti sana na walichokuwa wanakitarajia kwake, na sababu ya kushangaa kwao ni kwasababu alikuwa akifundisha kama mtu mwenye AMRI, na sio kama waandishi wao.

Mtu mwenye amri sikuzote huwa ni mtu mwenye mamlaka, na mtu wa namna hiyo maneno yake huwa sio ya kupinda pinda, au ya kupamba pamba, bali maneno yake yananyooka, na ya wazi sana, kwamfano  raisi akisimama mbele ya watumishi wake, huwa hawambelezi bembelezi, bali anapotoa maagizo, labda akisema, nataka huu mradi uishe ndani ya wiki mbili, hapo ni hakuna cha majadiliano, yule mtumishi ni lazima afanye ili uishe, asipofanya hivyo ni kazi hana, kamwe haji kumwambia naomba unisaidie kama ikikupendeza huu mradi uishe ndani ya wiki  2, Huwezi kusikia mwenye mamlaka yoyote kuzungumza maneno ya kusihi sihi namna hiyo.

Ndivyo Bwana Yesu alivyokuja kuhubiri ulimwenguni, ukisoma mistari iliyotangulia ya juu na mengine iliyofuata utaona maneno yake yalikuwa yamenyooka sana, bila maficho ficho tofauti na ya waandishi, ambao wenyewe walikuwa ni kufundisha desturi za kiyahudi tu kwa watu, na kuwapembeleza, hawawaambii watu wajibu wao kwa Mungu, au madhara yatokanayo na dhambi, au kumpenda Mungu kwa mioyo yao yote.

Lakini Bwana Yesu aliwaambia, mmesikia imenenewa, ‘Lakini mimi nawaambia hivi’ kuonyesha kuwa anayo mamlaka “YEYE”..Unaona,  kuna mahali akasema kiungo chako kimoja kikikukosea king’oe ukitupe mbali na wewe, kuliko mwili wako wote kutupwa jehanum, mahali ambapo funza wa kule hawafi wala moto wake hauzimiki..Maneno ambayo usingekaa uyasikie yakitoka kwenye vinywa vya waandishi hata siku moja, kumwambia mtu apoteze kiungo chake kimoja kwa ajili ya kunusuru maisha yake ya milele, hakuna jambo kama hilo. Kuipoteza biashara yakoe haramu, au kuwapoteza marafiki zake waovu, au kupoteza hata kiungo cha mwili wake mwenyewe kinachomkosesha, huwezi sikia wakifundisha  hivyo.

Aliwaambia, mtu asiyeuchukua msalaba wake, na kumfuata hawezi kuwa mwanafunzi wake, ampendaye Baba au mama kuliko yeye hamstahili, aipataye nafsi yake ataipoteza, na aipotezaye kwa ajili yake ataipata…

Wengi watakuja wakati ule wakisema, Bwana hatukutoa pepo, na kufanya miujiza mingi kwa jina lako? Lakini mimi nitawaambia Dhahiri, siwajui ninyi ondokeni kwangu mtendao maovu.

Jitahidini kuingia kupitia mlango uliomwembamba, kwasababu njia ni pana iendayo upotevuni. .

Unaona maneno hayo ni maneno yaliyonyooka, yanakueleza madhara ya kitu Fulani,kama usipochukua tahadhari.

Hata sasa kinywa cha Bwana ni kilekile, kwasababu anasema yeye ni yule yule jana na leo na hata milele. Bado anazungumza kama mtu mwenye amri, lakini watu wa leo, wanayatafsiri maneno ya namna hiyo kama KUHUKUMU au KUTISHA WATU. Watu wanataka kusikia maneno  kama  ya waandishi. ‘Yesu anakupenda’, wewe kuwa tu mtu mwema inatosha, utabarikiwa, utafanikiwa, waandishi hawataki kukueleza uvuuaji wako mbovu, kuwa hautakupeleka mbinguni, hawawezi kukueleza hivyo, kwasababu wanaogopa wasimpoteze mshirika wao.

Waandishi hawawezi kukueleza habari za siku za mwisho, wanahisi watakuogopesha, na hivyo utawakimbia.

Ndugu Ukiona upo mahali unahubiriwa maneno laini laini tu, wakati wote ujue kuwa Yesu hayupo hapo, bali ni waandishi ndio wanaokufundisha. Yesu sikuzote anazungumza kwa amri, ndivyo alivyo anasema..

Ufunuo 3:19 “Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu”.

Usidanganywe na mtu anayesema kufundishwa maneno laini ndio ishara ya upendo. Bwana Yesu hakufanya hivyo, lakini ni mtu aliyetupenda kuliko mtu yeyote aliyewahi kuishi hapa duniani.

Hii ni moja ya njia ambayo utayatambua mafundisho ya kweli ya Bwana..

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Amri zilizo ndogo alizozizungumzia Yesu ni zipi?

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

TUMEPEWA AMRI YA KUKANYAGA NGE NA NYOKA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments