Amri zilizo ndogo alizozizungumzia Yesu ni zipi?

Amri zilizo ndogo alizozizungumzia Yesu ni zipi?

SWALI: Tukisoma  Mathayo 5:19 Inasema..

“Basi mtu ye yote atakayevunja AMRI MOJA katika hizi ZILIZO NDOGO, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu ATAKAYEZITENDA na KUZIFUNDISHA, huyo ataitwa MKUBWA katika ufalme wa mbinguni”.

Swali langu 👆Amri ndogo zinazozungumziwa hapo ni zipi? Ningependa kuzijua!

Kama kuna Amri ndogo ,bila shaka na Amri kubwa au kuu zitakuwepo pia ningependa kufahamu hilo.

Asante na Mungu awabariki kwa majibu yenu.


JIBU: Ukisoma maneno ya juu yake yaliyotangulia utaona anasema.. sikuja kuitangua torati bali kuitimiliza, Hii ikiwa na maana kuwa vipo vipengele vya torati ambavyo havikukamilika, au havikueleweka kwa wengi ndio sasa yeye akaja kuviweka sawa, na kuvimalizia..

Sasa kwa wayahudi (Yaani mafarisayo  na waandishi) waliona kama ni sheria mpya Yesu anawaletea watu, sheria ambazo Musa hakuziandika, visheria vidogo vidogo ambavyo si lazima mtu kuvishika, japo vinaelezea uhalisia.

Kwa mfano Musa aliwaagiza wasizini, lakini jambo lingine lolote linalohusiana na uzinzi, kama vile kutazama pornography, au kufanya masturbation ni sawa, lakini Yesu alipokuja na sheria mpya kwamba kila amtazamaye mwanamke kwa kumtamani ameshakwisha kuzini naye.. Waliona kama ni jambo la ziada  (kama sheria ndogo tu), lakini hawajui kuwa mtu ambaye atazishika hizo ndizo zitakazomfanya awe mkubwa sana katika ufalme wa mbinguni.

Vilevile Musa alisema usiue, lakini Bwana Yesu akasema mtu atakayemwonea ndugu yake hasira tayari ni muuaji. Hivyo hatupaswi kuwekeana  vinyongo sisi kama ndugu, haijalishi tumeudhiana sana kiasi gani. Sasa ikitokea unapuuzia maneno haya, ujue kuwa katika ufalme wa mbinguni unaonekana ni mdogo sana, haijalishi kuwa hujawahi kufikiria hata kuua.

Musa alisema Jicho kwa jicho, na jino kwa jino, lakini Yesu alisema, tusishindane na watu waovu, mtu akupigaye shavu la kuume mgeuzie na la kushoto.

Musa alisema, usiape uongo, lakini Yesu alisema usiape kabisa kwa kiapo chochote.

Alisema tena mpende jirani yako, mchukie adui yako, lakini Yesu alisema wapendeni adui zenu waombeeni wanaowaudhi..n.k n.k.

Sasa amri kama hizo za Yesu  zilionekana ni ndogo hivyo zikadharauliwa, wengi wakawa hawazishiki, ni sawa na leo hii tu, mtu akuambie umuombee adui yako, ni jambo ambalo unaweza ukalidharau, na ndio maana huwezi kulisikia kwenye vinywa vya watumishi, vilevile ni ngumu kuviona watu wakiviishi, zinapuuziwa lakini ndizo zinazotupa ukubwa mbinguni.

Ndio maana Yesu alisema pale juu.. “Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni”(Mathayo 5:20).

Akiwa na maana tukiyatenda tu yale ambayo watu wa dini wanayatenda kwa desturi na mazoea, hatuna cha ziada ndani yetu, tujue kuwa mbinguni hatutaingia.

Nasi tunafundishwa, tuyashike kwa kuyaishi na kuyafundisha, sana hayo maagizo ya Yesu, ambayo ndio yanayokamilisha torati nzima. Soma  kitabu Mathayo sura ya 5 mpaka ya 7 utapata maagizo hayo yote kwa urefu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
1 year ago

Amen nimepata kitu hapo