Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?

Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?

Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?


JIBU: Tukisoma kitabu cha Kumbukumbu 7:11 biblia inasema…

“Basi zishike AMRI, NA SHERIA, NA HUKUMU ninazokuamuru leo, uzitende.

12 Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiliza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimilizia agano na rehema aliyowaapia baba zako”

Ukisoma kwa makini utaona kweli kuna vitu vitatu hapo..Amri, Sheria na Hukumu..Hivi vi vitu vitatu tofauti lakini vinategemeana sana.

Tukianza na Amri:

Amri maana yake ni Agizo lililotolewa na mamlaka iliyo kuu ambalo linapaswa litekelezwe bila shuruti..Amri huwa haina uchaguzi kwamba mtu anapaswa aitekeleze au asiitekeleze..Amri ikitolewa ni sharti wote waitekeleze na asiyefanya hivyo atakuwa hatihani. Katika Agano la kale..Mungu alitoa Amri kuu kumi kama tunavyozisoma katika kitabu cha Kutoka Mlango wa 20, na Kumbukumbu 5:3-21. (Unaweza ukazisoma binafsi).

Sheria:

Lakini pamoja na hizo Amri 10 kuwepo…bado zilikuwa hazijakamilika…Kwamfano kuna Amri moja inayosema USIZINI…Hiyo ni amri kweli..Mtu hatazini na mke wa jirani yake…lakini je! Ikitokea kazini na mnyama itakuaje?..atachukuliwa hatua gani? Atahukumiwaje?, au ikatokea mtu kazini na mzazi wake je atahukumiwaje? Hukumu yake itakuwaje, ikitokea mtu hajazini na mke wa jirani yake lakini kalala na mtu wa jinsia moja na yeye itakuwaje? N.k…Sasa maswali kama hayo unaona kabisa amri peke yake haijajitosheleza inahitajika ziwepo sheria pamoja na hukumu juu ya hizo amri…

Ndio maana unaona kwenye biblia zimeongezeka sheria nyingi nyingi ambazo zote zinasapoti Amri ya USIZINI. Na baadhi ya sheria hizo ni kama zifuatazo.

Walawi 18: 23 “Wala usilale na mnyama ye yote, ili kujitia unajisi kwake; wala mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kulala naye; ni uchafuko”…Hii ni sheria inayosapoti amri ya USIZINI.

Nyingine ni hizi.

Walawi 18: 6 “Mtu ye yote aliye wa kwenu asimkaribie mwenziwe aliye wa jamaa yake ya karibu ili kumfunua utupu; mimi ndimi Bwana.

7 Utupu wa baba yako, wala utupu wa mama yako, usifunue, maana ndiye mama yako; usifunue utupu wake.

8 Utupu wa mke wa baba yako, usifunue; maana, ni utupu wa baba yako.

9 Utupu wa umbu lako, binti ya baba yako, au binti ya mama yako, kwamba alizaliwa nyumbani mwenu au kwamba alizaliwa kwengine, utupu wa hao usifunue.

10 Utupu wa binti ya mwanao mume, au wa binti ya binti yako, utupu wao hao usifunue; kwa kuwa ndio utupu wako mwenyewe.

11 Utupu wa binti ya mkewe baba yako, aliyezaliwa na baba yako, yeye ni umbu lako, usifunue utupu wake”. Kufunua Utupu wa mtu maana yake kulala na huyo mtu (hiyo ni lugha ya kibiblia).

Hukumu:

Sasa hizo ni sheria zinazogongelea msumari Amri ya USIZINI..Lakini pamoja na hizo sheria ikitokea mtu kazikiuka atahukumiwaje?..Ndio hapo zijahitajika pia HUKUMU juu ya sheria na Amri.

Mfano wa hukumu hizo ni kama ifuatavyo..

Kutoka 22: 19 “Mtu awaye yote alalaye na mnyama sharti atauawa”.

Walawi 20: 10 “Na mtu aziniye na mke wa mtu mwingine, naam, yeye aziniye na mke wa jirani yake, mtu mume aziniye, na mwanamke aziniye, hakika watauawa.

11 Na mtu mume atakayelala pamoja na mke wa baba yake amefunua utupu wa baba yake; wote wawili hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao.

12 Na mtu mume akilala na mkwewe mwanamke wote wawili hakika watauawa; wamefanya yaliyo uchafuko; damu yao itakuwa juu yao.

13 Tena mtu mume akilala pamoja na mtu mume, kama alalavyo na mtu mke, wote wawili wamefanya machukizo; hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao”.

Umeona na Amri nyingine zote 9 zilizosalia zina sheria zake na hukumu zake…Kwahiyo Amri hazijakamilika bila sheria na hukumu. Hiyo ndiyo tofauti ya Amri, sheria na Hukumu.

Hivyo Mungu alipowaambia wana wa Israeli wazishike hukumu zake, alikuwa anamaanisha pia wazitelekeze hukumu za amri zote bila kuacha hata moja, aliyestahili kutozwa kitu atozwe, aliyestahili kutengwa atengwe, aliyestahili kifo, afe n.k.

Je katika agano jipya, amri,sheria na hukumu zinatekelezwaje?

Lakini Katika Agano jipya tulilopo sasa Amri za Mungu zinaandikwa ndani ya mioyo yetu, na kadhalika sheria na hukumu (Soma Yeremia 31:31-34)...Roho Mtakatifu anapoingia ndani yetu, hatuhitaji sheria kuzishika amri za Mungu..Sisi hatuhitaji kuambiwa kuzini na mnyama ni dhambi..tayari Roho aliyeko ndani yetu anatushuhudia kwamba jambo hilo si sawa..

Sheria anakuwa zinakuwa zimeandikwa ndani kabisa ya mioyo yetu..hatuhitaji kuambiwa kulala na mtu wa jinsia moja nasi ni dhambi..tayari sheria hiyo imeandikwa ndani ya mioyo yetu ipo..Hatuhitaji kuambiwa kuvaa vimini au nguo za nusu uchi ni dhambi..tayari ndani ya moiyo yetu Roho Mtakatifu anashuhudia kuwa jambo hilo si sawa kabla hata ya kuambiwa…hatuhitaji kupewa sheria ya kwamba tuwaheshimu wazazi wetu..tayari sheria hiyo ipo ndani ya mioyo yetu tunaitimiza bila shuruti…Hiyo ndio maana biblia inasema hatuishi kwa sheria bali kwa Imani..

Watu wa agano la kale hawakuwa na upendeleo tuliopewa sisi wa kipawa cha Roho Mtakatifu ambaye angewasaidia kuziishi sheria pasipo nyaraka…lakini sisi tumepewa zawadi hiyo ya Roho..Ni Neema ya ajabu sana..Ndio maana kuna umuhimu sana wa kuwa na Roho Mtakatifu. Ukiwa na Roho Mtakatifu hutakuwa kuwa ngumu kwako kuyatekeleza maagizo yote yaliyopo katika maandiko.

Je umepokea Roho Mtakatifu?..

kumbuka biblia inasema wote wasiokuwa na Roho Mtakatifu hao sio wake (Soma Warumi 8:9). Hivyo kama unaona bado ni ngumu wewe kuishi maisha matakatifu basi hauna Roho Mtakatifu, unamhitaji..Na huyo ataingia ndani yako ikiwa utaamua kabisa kwa moyo wako kuukana ulimwengu na kumgeukia yeye..kwa kutubu dhambi zako leo, na kujinyenyekeza mbele zake..Na baada ya kutubu kwa dhati kabisa..bila kuchelewa nenda katafute ubatizo sahihi ukabatizwe kama hujabatizwa…Kumbuka ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi(Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu Kristo (Matendo 2:38)..Na kisha Roho Mtakatifu atakutia muhuri uwe wake milele. Hapo na kuendelea sheria za Mungu kwako hazitakuwa ni utumwa..bali zitabubujika zenyewe moyoni mwako pasipo hata kusukumwa sukumwa wala kuhubiriwa hubiriwa…

Bwana akubariki sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Tofuati kati ya Myahudi, Mwisraeli na Muebrania ni ipi?

TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!

Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?

ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!

 

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
7 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Joseph
Joseph
1 year ago

Watumishi baraka tele kutoka kwa MUNGU

Nuru mhondele
Nuru mhondele
2 years ago

Nimebarikiwa sana na naamini ntakua kiroho vizuri nikiendelea kusikiliza mafundisho yenu

Getrude Charles
Getrude Charles
2 years ago

Amina, Barikiwa Sana watumishi wa Mungu.

AGRIPINA LILI
AGRIPINA LILI
3 years ago

Nmefurahia napenda kujifunza maneno ya Mungu kwakupitia website yenu