Category Archive Mafundisho ya msingi

JE! NI CHEMCHEMI IPI INATOKA NDANI YAKO, YA MITO AU YA KISIMA?

Mtu yeyote aliyeokoka, ndani ya moyo wake kunatokea chemchemi ya maji  yaliyo hai (Mithali 4:23). Na maji hayo huwa hayakauki, kwasababu yanatoka kwenye chanzo chenyewe  halisi ambacho ni Yesu Kristo,

Na Kama vile tunavyojua maji hufanya kazi zisizopungua nne.

  1. kukata kiu,
  2. kumeesha,
  3. kusafisha,
  4. na kugharikisha pale yanapozidi,

Ndivyo ilivyo kazi ya maji haya  katika moyo wa mtu, hukata kiu ya mambo maovu(Ufunuo 21:6, Yohana 4:14), humeesha mambo mema ya Mungu , husafisha moyo wa mtu, lakini pia  hugharikisha kazi za Yule  mwovu.

Ndio maana maandiko yanasema pepo limtokapo mtu hupitia mahali pasipo na maji, ni kwanini? Ni kwasababu eneo lenye maji  rohoni, haliwezi pepo hawezi kukaa anaona gharika, na mafuriko makubwa hawezi kusogelea hapo. Na eneo lenye maji ni moyo wa mtu aliyeokoka.

Luka 11:24  Pepo mchafu amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika; asipoona, husema,

25  Nitairudia nyumba yangu niliyotoka

26  Hata afikapo, akaiona imefagiwa na kupambwa, ndipo huenda akachukua pepo wengine saba, walio waovu kuliko yeye mwenyewe, wakaingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza

Sasa wengi wetu hatujui kuwa hayo maji, yanakuwa kama maji ya “KISIMA” tu, ambayo hutulia pale pale, ni neema ya bure ambayo kila mwamini amepewa. Lakini ili ayafanye maji hayo kuwa “MITO” yaani yatiririke mbali. Si jambo la kusema tu nimeokoka. Bali kitu cha ziada lazima kifanyike kwenye maisha ya mtu.

Kama tunavyojua mito, huenda mbali kuwasaidia, hata watu wasiojua chanzo chake kilianzia wapi, Kwamfano mamilioni ya  wakazi wa mji wa Kilimanjaro, kutegemea maji yanayotiririka kutoka katika mlima wa Kilimanjaro, Na ni wazi wengi wao hawajui chanzo ni mwamba gani. Lakini wananufaika. Hata Pale Edeni Mungu alitoa mto katikati ya bustani, lakini haukuishia pale bali ulitoka mpaka nje ya bustani, kuyanufaisha mataifa. (Mwanzo 2: 10-14)

Vivyo hivyo ili na wewe yale maji uliyoyapokea siku ulipookoka, kama chemchemi ya kisima, unataka yatoke nje, huna budi kufanya jambo lingine la ziada.

Ndio maana mitume walishindwa kulitoa lile pepo sugu, wakijiuliza kwanini, ndipo   Bwana Yesu alisema maneno haya

Mathayo 17:21  [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]

Ni nini hiyo haitoki?

Ni maji yaliyo ndani yako. Kubadilika na kuwa mito, ni lazima uingie gharama za kuwa mwombaji. Si kuomba tu bali Kuomba bila kukoma. Mwombaji yoyote huuvutia uwepo wa Mungu maishani mwake. Maombi ni ‘pump ‘ya Mungu inayoyavuta yale maji nje! Yakawasaidie wengine. Huwezi kuwa mtu wa mafunuo kama huna desturi ya kuomba, huwezi kuwasaidia wengine rohoni, hata kuwaombea wasaidike, kama wewe si mtu wa kuomba. Unatazamia mumeo aache pombe, halafu sio mwombaji, utapona tu wewe peke yako, lakini hutaweza kumponya mwingine. Unatazamia familia yako iokoke, halafu wewe mwenyewe huingii gharama za mifungo na maombi, yasiyo koma, mara kwa mara, zitakuwa ni ndoto tu, labda Mungu awaguse kwa njia zake mwenyewe, lakini sio kwa matamanio yako.

Na si tu katika eneo la kuwasaidia wengine, bali hata katika maeneo ya maisha yako ambayo unataka uone maingilio Fulani ya Mungu makubwa. Huna budi kuyatoa hayo maji yaende kuponya hayo maeneo.

Maandiko yanasema imetupasa kumwomba Mungu sikuzote bila kukata tamaa (Luka 18). Hiyo ndio njia pekee itakayoleta majibu.

Yohana 7:38  Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.

Na Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI WAPI UTAKUTANA NA MALAIKA WA BWANA?

Mruba ni mdudu gani kwenye biblia?(Mithali 30:15)

Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini Musa amtake Hobabu na tayari kulikuwa na Wingu linalowaongoza?

Swali: Kwanini Nabii Musa amtake Hobabu (shemeji yake) kama dira yake ya kuelekea Kaanani na tayari Mungu alishawafunulia juu yao nguzo ya wingu wakati wa mchana na Nguzo ya moto wakati wa usiku kama dira yao na kama kitu cha kuwaongozea?


Jibu: Lipo jambo kubwa sana hapa la kujifunza..

Awali ya yote kama bado hujamfahamu Hobabu ni nani na inakuwaje awe shemeji yake Musa fungua hapa >>>Huyu Mkeni shemeji yake Musa alikuwa ni mtu wa namna gani? (Waamuzi 1:16)

Sasa kwa muhtasari ni kwamba kipindi wana wana wa Israeli wanatoka Misri kuelekea Kaanani, ni kweli Bwana aliwapa wingu na nguzo ya moto iwaongoze mchana na usiku.

Lakini Zaidi ya hayo Musa alitafuta tena mtu ambaye atamwongoza njia yao kuelekea nchi ya ahadi.. sasa swali ni alifanya makosa?… na tena akataka kumfanya kama “Macho” katika safari hiyo..

Waamuzi 10:28 “Ndivyo zilivyokuwa safari zao wana wa Israeli kwa majeshi: yao; nao wakasafiri kwenda mbele.

29 Kisha Musa akamwambia Hobabu, mwana wa Reueli Mmidiani, mkwewe Musa, Sisi twasafiri kwenenda mahali ambapo Bwana amenena habari zake hivi, Nitawapa ninyi mahali hapo; uje pamoja nasi, nasi tutakufanyia mema; kwa kuwa Bwana ametamka mema juu ya Israeli.

30 Naye akamwambia, Siendi mimi; ila nitairudia nchi yangu mwenyewe, na kwa jamaa zangu mwenyewe.

31 NAYE AKAMWAMBIA, USITUACHE, TAFADHALI; KWA KUWA WEWE WAJUA JINSI TUTAKAVYOPANGA NYIKANI, NAWE UTAKUWA KWETU BADALA YA MACHO.

32 Itakuwa, ukienda pamoja nasi, naam, itakuwa mema yo yote Bwana atakayotutendea sisi, tutakutendea wewe vivyo

34 NA WINGU LA BWANA LILIKUWA JUU YAO MCHANA HAPO WALIPOSAFIRI KWENDA MBELE KUTOKA KAMBINI.

35 Ilikuwa, hapo sanduku liliposafiri kwenda mbele, ndipo Musa akasema, Inuka, Ee Bwana, adui zako na watawanyike; na wakimbie mbele zako hao wakuchukiao”.

Jibu ni La!.. Musa hakuwa Mjinga, wala hakuwa mtu wa kumtegemea Mwanadamu.. Daima alijua Mungu ndiye Ngao yake na watu wake, na wala hakuna mtu yeyote awezaye kumsaidia kazi.  Lakini Nabii Musa alifikiri Zaidi, Alijua watu aliona ni  watu wenye mioyo migumu, na shingo ngumu.

Alijua Imani yao kwa Mungu ilikuwa ni ndogo, na wengi wao ni watu wa mwilini, na alijua wasipopata mtu wa kuwapanga vyema kule nyikani, aliyemzoefu wa jangwa na njia, zitanyanyuka shida nyingi na hatimaye watamkufuru Mungu na kuadhibiwa wote.

Hivyo kwa faida ya watu wasiangamia aliwatafutia mwalimu wa mwilini ili awaongoze, na kuwafundisha jinsi ya kukaa jangwani, na hiyo ikawa dawa kwa sehemu kubwa sana.

Na utaona hii familia ya Yethro (babamkwe wake Musa na mashemeji zake), ilikuwa msaada mkubwa sana kiushauri katika safari ya wana wa Israeli jangwani na kwa Musa kwa ujumla. Kwani kipindi ambacho Musa alikuwa anawaamua watu wote peke yake kuanzia asubuhi mpaka jioni, alipokuja huyu babamkwe wake alimpa ushauri bora sana wa kuweka wakuu wa maelfu, wakuu wa mahamsini na wakuu wa mamia na wakuu wa makumi (Soma Kutoka 18:12-27).

NINI TUNAJIFUNZA KWA MUSA:

Musa alikuwa na “Macho juu” ambaye ni Roho Mtakatifu juu (kama wingu likimwongoza na watu wake) lakini pia alikuwa na “macho chini” (Hobabu, shemeji yake) kwaajili ya watu wake. Mambo haya yanaenda pamoja..

Wewe kwama Mzazi, unaye Roho Mtakatifu anayekuongoza wewe na familia yako kama Macho ya Juu, lakini hayo hayatoshi pekee, ni lazima watoto wako uwapatie waalimu watakaowafundisha njia za Roho Mtakatifu katika mashule yao waliopo, katika makanisa yao, katika shughuli zao n.k

Ukisema utawaacha na kuongozwa na Roho Mtakatifu kama wewe uongozwavyo, utawapoteza…wawekee waalimu.

Vilevile Mtumishi wa Mungu weka waalimu kwa watoto wako wa kiroho, weka wachungaji watakaowaangalia, itakuwa afya na heri kwao.

Bwana atusaidie

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

KAZI ZA ROHO MTAKATIFU

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

Je Musa kumwoa Sipora, Mkushi alifanya dhambi?

Kiti cha Musa ni kipi? (Mathayo 23:2)

Rudi Nyumbani

Print this post

JITAHIDI KUJA KABLA YA WAKATI WA BARIDI.

2Timotheo 4:21  “Jitahidi kuja kabla ya wakati wa baridi. Eubulo akusalimu, na Pude, na Lino, na Klaudia, na ndugu wote pia”

Mtume Paulo ni mtu aliyetambua kuwa kustawi kwa huduma yake kunategemea sana sapoti ya watendazi wenzake wengine wenye ni moja na yeye. Hivyo tunasoma wakati akiwa Rumi kama mfungwa, alimwandikia waraka mwanawe Timotheo, aiharakishe huduma yake, ili amfuate kule Rumi wasaidiane katika huduma kabla ya wakati wa bariki kuanza.

“Jitahidi kuja kabla ya wakati wa baridi”.

Paulo alijua mazingira yanaweza kukawiisha kusudi la Mungu. Hivyo alitambua kuwa mtu akiongeza jitihada anaweza kukamilisha mambo yake mapema kabla mazingira Fulani hayajamuathiri kutenda kusudi lingine la Mungu.

Kwa ukanda waliokuwa, ilikuwa ni ngumu sana, meli kusafiri nyakati za baridi kwasababu ya barafu baharini, hivyo safari zote za majini zilisitishwa kwa miezi kadhaa mpaka baridi itakapoisha ndipo safari zianze tena, Paulo aliliona hilo akatambua ni jambo la asili haliwezi kuepukika kwa kufunga na kuomba, isipokuwa kwa kupangilia tu ratiba vizuri.

Hii ni kutufundisha sisi, tufahamu kuwa mazingira Fulani, au nyakati Fulani zisizo rafiki sana huwa zinapita, au zitakuja mbele yetu ambazo zinaweza zikawa ni kikwazo cha utumishi kwa sehemu Fulani.

Kwamfano wakati wa baridi kwako, unaweza kuwa ni wakati wa ndoa. Kama wewe ni kijana hujaoa/ hujaolewa, unanafasi sasa ya kumtumikia Mungu kwa uhuru wote. Titahidi sana kufanya hivyo sasa, kwasababu nafasi hiyo inaweza ikapungua kwa sehemu uingiapo katika majukumu ya kindoa. Usipojitahidi sasa kujiwekea msingi mzuri kwa Mungu wako, utataabika sana kuujenga huo uwapo kwenye ndoa.

Wakati wa baridi unaweza ukawa ni kipindi cha kazini au masomoni. Ikiwa bado hujapata kazi, au upo likizo kazini au shuleni, embu tumia vema wakati wako, kuongeza kitu kikubwa katika ufalme wa Mungu, kwasababu shughuli zitakapokulemea, kuujenga tena huo msingi itakuwia ngumu sana, na kama ikiwezekana yaweza kukuchukua wakati mrefu. Uwapo ‘free’ usilale, bali tumia sasa kuongeza mikesha, maombi ya masafa marefu, kusoma biblia yote.

Wakati wa baridi waweza kuwa uzee. Kwa jinsi umri unavyokwenda ndivyo uwezo wa mwili wako unavyopungua, Hivyo utengenezapo mambo yako mapema na Bwana, basi wakati huo ukikukuta hautakuathiri sana, kwasababu tayari yale ya msingi uliyopaswa uyafanye umeshayafanya mapema, uzeeni ni kumalizia tu.

Zipo nyakati nyingi za baridi. Chunguza tu maisha yako ujue wakati wako wa baridi unafika lini na ni upi, kisha jitahidi sana, kuwekeza kwa Mungu sasa, kimaombi, kiusomaji Neno, na kiuinjilisti.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MCHE MWORORO.(Opens in a new browser tab)

Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?

Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?

(Opens in a new browser tab)Fahamu maana ya Mithali 25:13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno;(Opens in a new browser tab)

(Opens in a new browser tab)Rudi Nyumbani

Print this post

Ipi tofuati kati ya UTAKATIFU na UKAMILIFU?

Swali: Ipi tofuati kati ya kuwa MTAKATIFU (1Petro 1:15-16) na kuwa MKAMILIFU (Mathayo 5:48)?

Jibu: MTAKATIFU ni Mtu aliyetakaswa, aliye safi, asiye na mawaa na anayefanya matendo mema.. Na biblia inatufundisha tuwe watakatifu kama Baba wa mbinguni alivyo mtakatifu…

1Petro 1:15  “bali kama yeye aliyewaita ALIVYO MTAKATIFU, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;

16  kwa maana imeandikwa, MTAKUWA WATAKATIFU KWA KUWA MIMI NI MTAKATIFU”.

Na tena Mambo ya Walawi 19:2  inarudia jambo hilo hilo..

Walawi 19:2 “Nena na mkutano wote wa wana wa Israeli, uwaambie, Mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana, Mungu wenu, ni mtakatifu”.

Lakini MKAMILIFU ni Mtakatifu aliye kamilika….. Wapo Watakatifu waliokamilika na ambao hawajakamilika.

Mtakatifu aliye kamilika ni yule ni anayefanya JAMBO LA ZIADA katika UTAKATIFU WAKE linalomtofautisha na wengine na kufanya afanane na MUNGU … Mfano wa mambo hayo ni kama yale yote Bwana YESU aliyoyataja katika Mathayo 5.

Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;

44  lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

45  ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.

46  Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

47  Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, MNATENDA TENDO GANI LA ZIADA? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?

48  Basi ninyi MTAKUWA WAKAMILIFU, KAMA BABA YENU WA MBINGUNI ALIVYO MKAMILIFU

Kwahiyo na sisi ni Lazima tuutafute UKAMILIFU na si UTAKATIFU TU!.

> “Mtakatifu” anafunga na kuomba kwaajili yake peke yake, lakini “Mkamilifu” anafunga na kuomba kwaajili yake na kwaajili ya wengine,

> “Mtakatifu”  anasoma neno na kuomba basi!…Lakini “Mkamilifu”  anasoma Neno na kuomba na kuwafundisha wengine mambo aliyojifunza, ili nao wabarikiwe kama yeye.

> “Mtakatifu”  anafanya kazi ya Mungu kwa moyo ili akapate thawabu mbinguni, lakini “Mkamilifu”  pamoja na kufikiri thawabu mbinguni lililo kubwa zaidi analolifikiri ni ndugu zake wasiangamie katika moto wa milele (moyo wake unaugua juu ya roho za wengine kupotea).

> “Mtakatifu”  atampa Mungu siku moja katika wiki ya kukusanyika nyumbani kwa Mungu, lakini “Mkamilifu”  atafikiri Zaidi ya siku moja.

> Mtakatifu” atazishika AMRI ZOTE ZA MUNGU, lakini Moyo wake utakuwa pia katika mali…. Lakini “Mkamilifu” Atazishika Amri zote na Moyo wake hautakuwa katika mali kama yule kijana aliyekutana na Bwana YESU.

Mathayo 19:16 “Na tazama, mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa milele?

17  Akamwambia Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri.

18  Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo,

19  Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako.

20  Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena?

21  Yesu akamwambia, UKITAKA KUWA MKAMILIFU, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.

22  Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi”.

Hivyo hatuna budi kuutafuta UKAMILIFU na sio UTAKATIFU tu peke yake!!.

Biblia inasema Nuhu alikuwa mtu Mkamilifu katika vizazi vyake ndio maana akapona katika ile gharika (Mwanzo 6:9),  Daudi alikuwa mkamilifu ndio maana alipendwa na Mungu zaidi ya wafalme wote (2Samweli 22:24), Ayubu alikuwa mkamilifu ndio maana alimwona Mungu katikati ya majaribu (Ayubu 1:1).

Na hata sisi tukiwa WAKAMILIFU tutamwona Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MADARAKA YA WAKATI MKAMILIFU.

BABA UWASAMEHE

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

Nini maana ya Mungu amemfanya mwanadamu mnyofu?

NENO LA MUNGU NI UFUNUO MKAMILIFU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Ipi tofauti kati ya KUHANI na MCHUNGAJI.

Jibu: Makuhani ni watu waliokuwa wanahudumu katika “Hema ya Mungu” wakati wana wa Israeli wakiwa jangwani na katika “Hekalu la Mungu” baada ya wana wa Israeli kuingia katika nchi ya ahadi na kumjengea Mungu nyumba.

Kazi ya Makuhani ilikuwa ni “kuwapatanisha watu na Mungu wao” kupitia damu za wanyama. Vile vile Makuhani walikuwa na kazi ya kuwafundisha wana wa Israeli torati, na wote walitoka katika kabila moja lililoitwa Lawi.

Kwa mapana na marefu kuhusu makuhani wa agano la kale, pamoja na kazi zao na tofauti yao na walawi wengine fungua hapa >>>Tofauti kati ya makuhani na walawi ni ipi?

Lakini tunapokuja kwa “Wachungaji” wenyewe ni watu maalumu walioteuliwa na kuchaguliwa na MUNGU kulichunga na kulilisha kundi lake kupitia Mafundisho ya Neno la Mungu, maonyo na Maombi!. (Soma Yohana 21:15-17).

Na hawa wanafanya kazi mfano wa zile za kikuhani katika nyumba ya Mungu. Isipokuwa wenyewe hawawapatanishi watu kwa damu za wanyama bali kwa damu ya BWANA YESU kupitia Neno lake. Hivyo Wachungaji nao ni MAKUHANI WA BWANA.

Lakini si tu wachungaji walio makuhani wa Bwana peke yao, bali hata watu wengine wote waliojazwa Roho Mtakatifu wana sehemu ya huduma ya kikuhani… Kwani ndivyo maandiko yasemavyo kwamba sote tumechaguliwa kuwa MAKUHANI KWA MUNGU WETU.

Ufunuo 1:5 “tena zitokazo kwa Yesu Kristo, shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake,

6  na kutufanya kuwa ufalme, NA MAKUHANI KWA MUNGU, naye ni Baba yake; utukufu na ukuu una Yeye hata milele na milele. Amina”

Hivyo kila mmoja aliyejazwa Roho Mtakatifu anayo huduma ya upatanisho (ambayo ndiyo ya kikuhani) ndani yake kupitia ile karama aliyopewa, ndio maana sote tuna uwezo wa kuhubiri injili na kuchungana sisi kwa sisi kupitia Neno la Mungu.

2Wakorintho 5:18 “Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, naye alitupa huduma ya upatanisho;

19  yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho.

20  Basi tu wajumbe kwa ajili ya Kristo, kana kwamba Mungu anasihi kwa vinywa vyetu; twawaomba ninyi kwa ajili ya Kristo mpatanishwe na Mungu”.

Kama wewe ni Mchungaji, unayesimamia kundi kama kiongozi,  basi simama katika nafasi yako ya kuchunga na kulisha kwani kuna hatari kubwa ya kutokufanya hivyo..

Ezekieli 34:1 “Neno la Bwana likanijia, kusema,

2 Mwanadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli, toa unabii, uwaambie, naam, hao wachungaji, Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao wachungaji wa Israeli, wanaojilisha wenyewe; je! Haiwapasi wachungaji kuwalisha kondoo?

3 Mnawala walionona, mnajivika manyoya, mnawachinja walionona; lakini hamwalishi kondoo.

4 Wagonjwa hamkuwatia nguvu, wala hamkuwaponya wenye maradhi, wala hamkuwafunga waliovunjika, wala hamkuwarudisha waliofukuzwa, wala hamkuwatafuta waliopotea; bali kwa nguvu na kwa ukali mmewatawala.

5 Nao wakatawanyika, kwa sababu hapakuwa na mchungaji; wakawa chakula cha wanyama- mwitu, wakatawanyika.

6 Kondoo zangu walitanga-tanga katika milima yote, na juu ya kila kilima kirefu; naam, kondoo zangu walitawanyika juu ya uso wote wa dunia; wala hapakuwa na mtu aliyewaulizia, wala kuwatafuta.

7 Basi, enyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana;

8 Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, kwa sababu kondoo zangu walikuwa mateka, kondoo zangu wakawa chakula cha wanyama-mwitu wote, kwa sababu hapakuwa na mchungaji, wala wachungaji wangu hawakutafuta kondoo zangu, bali wachungaji walijilisha wenyewe wala hawakuwalisha kondoo zangu;

9 kwa sababu hiyo, enyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana;

10 Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu ya wachungaji; nami nitawataka kondoo zangu mikononi mwao, nami nitawaachisha hiyo kazi ya kuwalisha kondoo; nao wachungaji hawatajilisha wenyewe tena; nami nitawaokoa kondoo zangu vinywani mwao, wasiwe tena chakula chao”.

Bwana YESU atusaidie sana.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WACHUNGAJI WA BWANA MAKONDENI.

TOFAUTI YA MITUME, MANABII, WAINJILISTI, WACHUNGAJI NA WAALIMU NI IPI?

JE! UNAMPENDA BWANA?

Kwa namna gani tumefanyika Makuhani na Ufalme?.(Ufunuo 1:6)

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

Rudi Nyumbani

Print this post

Ipi tofauti kati ya maasi na maovu?

Swali: Kuna tofauti gani ya kufanya maasi na kufanya maovu?


Jibu: Maovu ni mambo yote mabaya mtu anayoyafanya yaliyo kinyume na Mungu, na haya yanatokana na shetani (ndio maana anajulikana kama Mwovu, Mathayo 5:37)…mfano wa maovu ni mauaji, uasherati, dhuluma, wizi, ulawiti, ufiraji, ibada za sanamu na mambo mengine yanayofanana na hayo..

Lakini “Maasi” ni mabaya yote yanayofanywa na watu waliokuwa ndani ya Imani kisha wakatoka!!!. (kwa ufupi ni maovu ya watu waliokwisha kumjua Mungu).

Maana yake kama mtu alikuwa ndani ya Imani, na baadaye akakengeuka na kuisaliti ile Imani au kurudi nyuma kwa kuanza kufanya mambo mabaya… basi mambo hayo maovu ayafanyayo ndiyo yanayoitwa MAASI.

Mtu wa kidunia ambaye hajamjua Mungu bado, huyo hawezi kufanya MAASI!.. Kwasababu hakuna ALICHOKIASI!... Mpaka mtu afanye Maasi ni lazima awe AMEASI!..Sasa mtu ambaye hajamjua Mungu anakuwa anafanya MAOVU tu na si MAASI.. lakini akishamjua Mungu na akamwacha Mungu na kurudia maovu aliyokuwa anayafanya,.. basi yale maovu ayafanyayo ndiyo yanayoitwa MAASI.

Na watu wanaofanya Maasi wana hukumu kubwa kuliko wanaofanya Maovu, kwasababu tayari walishamjua Mungu na kisha wakamwacha kwa kurejea nyuma. Mfano wa watu waliokuwa wanatenda MAOVU na si MAASI katika biblia ni watu wa Sodoma na Gomora.

Mwanzo 19:15 “Hata alfajiri ndipo malaika wakamhimiza Lutu, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika MAOVU YA MJI HUU.”

Na mfano wa watu waliokuwa wanafanya MAASI ni wana wa Israeli (kwasababu walikuwa walianza na Mungu lakini wakakengeuka baadaye)

Yeremia 3:22 “21 Sauti inasikiwa juu ya vilele vya milima, ni kulia kwao na maombi yao wana wa Israeli; kwa kuwa wameipotosha njia yao, wamemsahau Bwana, Mungu wao.

22 RUDINI, ENYI WATOTO WAASI, mimi nitaponya maasi yenu. Tazama, tumekuja kwako; maana wewe u Bwana, Mungu wetu.”

Na katika siku za mwisho biblia inatabiri KUONGEZEKA KWA MAASI!.. Maana yake watakaokuwa wanarudi nyuma na kuisaliti imani na kufanya vitu kwa makusudi watakuwa ni wengi kuliko wale walio wa kudunia wafanyao maovu pasipo kuijua njia ya kweli.

Mathayo 24:12 “Na kwa sababu ya KUONGEZEKA MAASI, upendo wa wengi utapoa”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba “Maasi” ni “Maovu” yanayofanywa na watu waliorudi nyuma au waliomwacha Mungu!… Na watendao MAASI wana hukumu kubwa Zaidi ya watendao Maovu tu.. kwasababu wameyajua mapenzi ya Bwana wao halafu wakaasi.

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.

48  Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na Zaidi”.

Ukitoa mimba na huku unamjua KRISTO na unasema umeokoka ni UASI, ukiiba na huku unajua kabisa wizi ni dhambi na tena unajiita Mkristo huo ni UASI, ukifanya uzinzi na unasema umeokoka wewe ni Muasi, ukiabudu sanamu na huku unajua kabisa si sawa kufanya hivyo ni Uasi!..Na roho ya kuasi ni ROHO YA MPINGA KRISTO! (2Thesalonike 2:7).

Bwana atusaidie tusiwe WAASI wala tusifanye MAASI baada ya kumjua yeye, bali tudumu katika ukamilifu na utakatifu katika Roho wake Mtakatifu.

Lakini ikiwa wewe bado haujaokoka fahamu kuwa pia MAOVU yako uyafanyayo hayatakufikisha popote, mwisho wake ni katika ziwa la Moto..

Ni heri ukayasalimisha maisha yako kwa BWANA YESU ili akusafishe na kukupa uzima wa milele.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MUNGU HAJARIBIWI NA MAOVU BALI MEMA.

IMANI “MAMA” NI IPI?

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Je Adamu na Hawa, walikuwa hawafanyi mema kabla ya kula tunda?

MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.

Rudi Nyumbani

Print this post

TEMBEA KATIKA NJIA KUU

Jina la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe daima. Karibu katika mafundisho ya biblia, Neno la Mungu wetu lililo Taa na Mwanga wa Njia zetu (Zab.119:105).

Zipo njia Mbili tu zilizowekwa mbele ya kila mwanadamu, Nazo ni njia ya UZIMA, na njia ya MAUTI.

Yeremia 21:8 “Nawe waambie watu hawa, Bwana asema hivi, Tazama naweka mbele yenu NJIA YA UZIMA, na NJIA YA MAUTI”.

Njia ya Uzima, inamwongoza mtu “Uzimani”..na Njia ya Mauti inamwongoza mtu “Mautini (ziwa la moto)”.

Njia ya Uzima imenyooka haina migawanyiko mingi (sawasawa na Yohana 14:6), ambapo Bwana YESU alisema yeye ndio hiyo “Njia”, na mtu hafiki kwa Baba isipokuwa kwa njia yake yeye.

Yohana 14:6  “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”

(Maana yake hakuna njia mkato wala njia mbadala ya kumfikia Baba)…Ni moja tu! Tena iliyonyooka, nayo ni YESU KRISTO, na si kupitia mtu mwingine yoyote mashuhuri, au mtakatifu mwingine yoyote aliye hai au aliyekufa au nabii yoyote katika biblia.

Lakini ile ya Mauti inamigawanyiko mingi, inaanza kama njia moja lakini mwisho wake inamigawanyiko,

Mithali 14:12 “IKO NJIA ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni NJIA ZA MAUTI”

Hapo anamaliza na kusema mwisho wake ni “NJIA ZA MAUTI” na si “NJIA YA MAUTI” kana kwamba ni moja, bali nyingi. Na njia ya Mauti si mwingine Zaidi ya “shetani”…Kama jinsi njia ya UZIMA ilivyo Bwana YESU kadhalika njia ya Mauti ni “shetani”.

Na shetani anaabudiwa kupitia vitu vingi, anaweza kuabudiwa kupitia miti, mawe, udongo, au kupitia vitu vitu vingine kama fedha, watu, dini n.k..ndio maana hapo biblia inasema hiyo Njia (shetani) mwisho wake ni “Njia za Mauti” (maana yake zipo nyingi).

Na hiyo ndio sababu pia kwanini biblia inataja uwepo wa milango mingi ya kuzimu (Soma Mathayo 16:18). Milango ya kuzimu ndio hizo njia zote zinazoweza kumpeleka mtu kuzimu.

Nabii Isaya amezidi kuziweza vizuri njia hizi kwa ufunuo wa Roho… Amezitofautisha kama “NJIA” pamoja na “NJIA KUU”..

Isaya 35:8 Na hapo patakuwa na NJIA KUU, na NJIA….”

“Njia Kuu” ni “Njia ya Uzima”…. Na “Njia” pekee yake “Ni njia ya Mauti”..

Lakini anaendelea kusema… hiyo “Njia kuu” itaitwa Njia ya utakatifu, na ya watu wasafirio..

Isaya 35:8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio….”

Maana yake wote wanaiendea hiyo njia ya Uzima (YESU) Ni lazima “utakatifu” uwe muhuri wao sawasawa na kitabu kile cha Waebrani 12:14.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”.

Vile vile ni lazima wawe “wasafiri”.. Tabia ya msafiri huwa anadumu katika chombo cha usafiri awapo safarini, na hawezi kujishikisha na mambo akutanayo njiani au barabarani…. na chombo chetu cha usafiri ni NEEMA YA MUNGU.  Tuwapo katika safari hii ya kwenda mbinguni kupitia njia ya Bwana YESU, mambo ya ulimwengu hayapaswi yashikamane  na sisi.

1Petro 2:11  “Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho”.

Na mwisho anasema.. “wajapokuwa wajinga hawatapotea katika njia hiyo”

Isaya 35:8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio, WAJAPOKUWA WAJINGA, HAWATAPOTEA KATIKA NJIA HIYO”. 

Ikiwa utaonekana mjinga kwa kuwa umeamua kuifuata NJIA KUU ya UTAKATIFU na umeamua kuishi kama MSAFIRI duniani, basi biblia inasema “hautapotea/hatutapotea” katika njia hiyo..

Haijalishi dunia nzima itakuona kama umepotea, umerukwa na akili, umechanganyikiwa…Mungu yeye anakuona upo katika njia sahihi na una hekima nyingi.. kwasababu mwisho wa njia hiyo ni UZIMA WA MILELE, Na Utakutana na Bwana naye atakufuta machozi.

Ufunuo 7:15 “Kwa hiyo wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, nao wanamtumikia mchana na usiku katika hekalu lake, na yeye aketiye katika kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao

16  Hawataona njaa tena, wala hawataona kiu tena, wala jua halitawapiga, wala hari iliyo yote.

17  Kwa maana huyo Mwana-Kondoo, aliye katikati ya kiti cha enzi, atawachunga, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji yenye uhai, na Mungu atayafuta machozi yote katika macho yao.”

Je wewe leo umechagua njia ipi??… Njia kuu ya Uzima? Au Njia ya Mauti..

Kumbukumbu 30:14 “Lakini neno li karibu nawe sana, li katika kinywa chako na moyo wako, upate kulifanya.

15 ANGALIA, NIMEKUWEKEA LEO MBELE YAKO UZIMA NA MEMA, NA MAUTI NA MABAYA”.

CHAGUA NJIA YA UZIMA, na TEMBEA KATIKA NJIA KUU YA UTAKATIFU.

BWANA AKUBARIKI.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

HATARI YA KUTOKUITAFAKARI BIBLIA VIZURI?

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Nardo ni nini? (Yohana 12:3)

Jibu: Turejee..

Yohana 12:3 “Basi Mariamu akatwaa ratli ya marhamu ya NARDO SAFI yenye thamani nyingi, akampaka Yesu miguu, akamfuta miguu kwa nywele zake. Nayo nyumba pia ikajaa harufu ya marhamu.

4  Basi Yuda Iskariote, mmojawapo wa wanafunzi wake, ambaye ndiye atakaye kumsaliti, akasema,

5  Mbona marhamu hii haikuuzwa kwa DINARI MIA TATU, wakapewa maskini”

“Nardo” ni jamii ya mmea mdogo ujulikanao kama “Nardostachys”. Mmea huu hutoa maua madogo ya rangi ya “Pinki” (Tazama picha juu), na vijimatunda vidogo vyeusi ambavyo ndivyo chanzo cha mafuta aina ya “Nardo” yanayotumika kutengenezea madawa ya asili pamoja na marhamu (yaani Perfumes/pafyumu) iliyo ya gharama kubwa kuliko nyingine nyingi.

marhamu ya Nardo

Pafyumu iliyotengenezwa kwa “Nardo”, ilikuwa ni ya gharama kubwa na hata sasa ni ya gharama kubwa kutokana na upatikanani wa mimea hiyo.

Mimea ya Nardostachy, inapatikana katika safu za milima ya Himalaya, iliyopo nchini Nepali, na sehemu chache za “nchi ya India” pamoja na “Uchina”.  Na inamea kuanzia kwenye kimo cha Mita 3,000 mpaka mita 5,000 kutoka katika usawa wa bahari (Mita 5,000 ni karibia na kimo cha Mlima Kilimanjaro).. Hivyo upatikanaji wake ni mgumu sana, kutokana na sehemu chache unazomea na kimo unapopatikana!.

Kutokana na sababu hizo, ndizo zinazoifanya Marhamu ya Nardo kuwa ya gharama. Mpaka hapo tutakuwa tumeshafahamu kuwa ile Marhamu yule mwanamke aliyompaka Bwana iliagizwa kutoka mbali sana (maana yake nje ya Israeli) na ilikuwa ya gharama sana… Dinari 300 ni sawa na shilingi Milioni 6 za kitanzania.

Mistari mingine inayozungumzia Marhamu ya Nardo ni pamoja na Wimbo ulio bora 1:12, na 4:13-14

Sasa kufahamu kwa urefu ni nini tunajifunza kupitia tukio la mwanamke yule kukivunja kile kibweta fungua hapa >>AKAKIVUNJA KIBWETA AKAIMIMINA KICHWANI PAKE.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

AKAZIDI KUENDELEA KATIKA HEKIMA NA KIMO.

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

GHARAMA YA UFALME WA MBINGUNI.

SI KILA KILICHO HALALI KINAFAA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kimiami ni nini? (Wimbo ulio bora 2:9).

Jibu: Turejee,

Wimbo 2:9 “Mpendwa wangu ni kama paa, au ayala. Tazama, asimama nyuma ya ukuta wetu, Achungulia dirishani, atazama kimiani”.

“Kimiami” ni dirisha kubwa lililo katika “ghorofa”..

Madirisha makubwa yaliyo katika maghorofa tofauti na yale yaliyo katika nyumba za chini ndiyo yaliyoitwa “kimiami”.

Mfano wa dirisha la Kimiami ni lile ambalo mfalme Ahazia aliloanguka na kuugua..

2Wafalme 1:2 “Na Ahazia AKAANGUKA KATIKA DIRISHA la chumba chake orofani, katika Samaria, akaugua; akatuma wajumbe, akawaambia, Enendeni mkaulize kwa Baal-zebubu, mungu wa Ekroni, kwamba nitapona ugonjwa huu”.

Na lile ambalo Yezebeli alianguka, baada ya kuangushwa na wale matowashi..

2Wafalme 9:30 “Hata Yehu alipofika Yezreeli, Yezebeli akapata habari; akatia uwanja machoni mwake, akapamba kichwa chake, akachungulia dirishani.

31 Hata Yehu alipoingia lango la mji, alisema, Je! Ni amani, Ewe Zimri, mwenye kumwua bwana wako?  32 AKAINUA USO WAKE KULIELEKEA DIRISHA, akasema, Aliye upande wangu ni nani? Matowashi wawili watatu wakachungulia.

33 Akasema, Mtupeni chini. Basi wakamtupa chini; na damu yake ikamwagika nyingine juu ya ukuta, na nyingine juu ya farasi, naye akamkanyaga-kanyaga”.

Tazama pia shubaka hapa >>>Shubaka ni nini kibiblia? (Mithali 7:6) 

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA.

KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

MUNGU HAJARIBIWI NA MAOVU BALI MEMA.

Rudi Nyumbani

Print this post

JE! UNATAKA UITWE MSOMI NA MUNGU?

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, Karibu katika kuyatafakari maneno ya uzima.

Sulemani, mtoto wa Daudi, katika kitabu chake cha mhubiri, kilichojawa na utafiti wa hali ya juu wa mambo mengi ya kimaisha yamuhusuyo mwanadamu, Tunaona mwishoni kabisa mwa utafiti wake alihitimisha kwa maneno haya;

Mhubiri 12:11 “Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; HAKUNA MWISHO WO WOTE WA KUTUNGA VITABU VINGI; NA KUSOMA SANA HUUCHOSHA MWILI. 

13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.

12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili. 

13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu”.

Sulemani alikuwa ni mtafiti sana, na kama kusoma na kutunga vitabu, basi alitunga vingi sana, na katika vyote (viwe Vya ki-Mungu na visivyo wa ki-Mungu ) alijaribu kutafuta siri, na mwongozo sahihi wa mwanadamu. Lakini tunaona akapata jawabu, ambalo ni rahisi sana kwa wote. Na jawabu lenyewe ni hili “kumcha Mungu na kuzishika amri zake”.

Akasema unaweza ukakesha kusoma vitabu vingi sana katika huu ulimwengu, na matokeo ya kusoma sana, ni kudhoofika, Na bado usipate ukweli mwingine zaidi ya ule ule “kumcha Mungu na kuzishika amri zake”. Ndio maana akahitimisha kwamba Mtu akizingatia sana hilo, laweza kuzidi usomaji mwingi tuuona hapa duniani.

Sasa kumcha Mungu na kuzishika amri zake maana yake ni nini?

Kumbuka biblia nzima inazungumzia habari za Yesu Kristo mwokozi wetu. Hivyo hapo ni sawa na kusema “Kumcha Yesu na kuzishika amri zake”. Hiyo Ni zaidi ya kuwa na maarifa ya vitabu milioni moja, au elimu za shahada elfu,. Ikiwa na maana yule mtu aliyemwamini Yesu, kisha akawa anaishi kwa kulifuata Neno lake, na kuitimiza amri yake kuu, ambayo alisema ni UPENDO. Huyo ni zaidi ya Msomi yoyote aliyewahi kutokea duniani. Au mtunzi yoyote mwenye hekima aliyewahi kuandika vitabu vingi. Ni mtu aliyemaliza kusoma vitabu vyote.

Yohana 13:34  Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.

35  Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.

Hivyo, usisumbukie maarifa  mengi, ukadhani kuwa ndio utamwelewa Mungu, sumbukia Kristo moyoni mwako, sumbukia upendo wa agape moyoni mwako. Kwasababu huko kote utakapokwenda kutakurudisha hapo hapo, ndicho alichokigundua sulemani katika usomaji wake mwingi, hakuna jipya ndani yake Ni kujisumbua tu, ndio maana biblia inasema, yapo mambo mengi aliyoyafanya Yesu na kama yangeandikwa basi vitabu vyote visingetosha duniani.

Yohana 21:25  Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa.

Umeona? Vitabu visingetosha kuandika mambo yote ya Yesu, kwasababu maudhui yake ndio yaleyale, tunayoyasoma katika maneno machache ya kwenye biblia. Ambayo ni wokovu na Upendo wa Mungu. Tukiyatimiza hayo ni sawa na kusoma vitabu vyote duniani.

Hivyo mimi na wewe tuanze kuweka juhudu, kimatendo, kutendea kazi Neno lake, zaidi ya kuhangaika kutafuta maarifa mengi. Kwasababu anasema mwenyewe chanzo cha maarifa ni kumcha yeye, na sio chanzo cha kumcha yeye ni maarifa.

Kumbuka pia asemapo kusoma kwingi huuchosha mwili, hamaanishi uwe mjinga usiwe msomaji kabisa hapana, Lakini anakupa shabaha ni wapi uweke juhudi zako nyingi ili ufanikiwe kuwa na Maarifa ya kweli ya kisomi, Usije ukawa unaufuata upepo.

Tumia nguvu nyingi kuyatendea kazi yale yaliyopo kwenye biblia tu, zaidi ya mihangaiko mingi huku na kule, na elimu nyingi za kidunia.  Utaitwa Msomi na Mungu.

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Uchaji ni nini kama tunavyosoma katika 1Timotheo 2:10?

NI NANI ANAYEUFUNGA MLANGO WA MAARIFA?

Rudi Nyumbani

Print this post