Category Archive Mafundisho ya msingi

MWONGOZO WA MAOMBI YA KUJIKUZA KIROHO.

Ikiwa wewe umeokoka, na una kiu kweli ya kumkaribia Mungu wako katika viwango vya juu. Basi fahamu huna budi ujikuze kiroho. Na ukuaji huo hutegemea mambo mawili makuu “Neno pamoja na maombi”. Katika tovuti hii yapo mafundisho mbalimbali yatakayokusaidia kupiga hatua hizo.

Makala hii imeegemea zaidi katika Maombi. Hivyo huu ni mwongozo wa Wiki kwa Wiki, mfululizo wa vipengele muhimu vya kuombea. Uwapo nyumbani, uwapo kanisani. Jiwekee ratiba Kisha kuwa mwombaji. Na hakika baada ya wakati fulani utaona matokeo makubwa sana ndani yako.

Wiki ya Kwanza:

Wiki ya pili:

Wiki ya Tatu:

Wiki ya Nne:

Wiki ya Tano:

Wiki ya Sita:

Wiki ya Saba:

Wiki ya Nane:

Mwendelezo utakuja…

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MASOMO MBALIMBALI YA NENO LA MUNGU.

MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Orodha ya mafundisho yote.

KUONGOZWA SALA YA TOBA

Rudi nyumbani

Print this post

Nchi ya “Kabuli” ndio nchi gani kwasasa, na kwanini iliitwa hivyo? (1Wafalme 9:13).

Jibu: Tusome,

1 Wafalme 9:12 “Naye Hiramu akatoka Tiro kuitazama hiyo miji Sulemani aliyompa; wala haikumpendeza.

13 Akasema, Miji gani hii uliyonipa, ndugu yangu? Akaiita NCHI YA KABULI, hata leo”.

Nchi hiyo iliitwa “Nchi ya Kabuli” na sio “Nchi ya Kaburi”.Kuna tofauti ya “Kabuli” na “Kaburi”.

Maana ya “kaburi” ni shimo la kuzikia mtu aliyekufa, lakini “Kabuli” maana yake ni “isiyofaa kitu”. Kwahiyo hapo inaposema Nchi ya Kabuli, maana yake ni nchi isiyofaa kitu.

Sasa kwanini nchi hiyo iliitwa hivyo na huyu Hiramu?. Na ni funzo gani tunapata?.

Kipindi Sulemani anaijenga nyumba ya Mungu pamoja na nyumba yake mwenyewe, aliingia makubaliano na Mfalme wa Tiro kwamba Mfalme wa Tiro atampa Sulemani Malighafi za ujenzi (Miti ya Mierezi na mawe pamoja na malighafi nyingine baadhi, 1Wafalme 5:17-18), kwa makubaliano ya kwamba Mfalme Sulemani atampa Hirimu, mfalme wa Tiro ardhi kama malipo.

Sasa baada ya Sulemani kukamilisha ujenzi wa nyumba hizo mbili, ambapo alitumia miaka 20 (1Wafalme 9:10), aliazimu kumlipa Hirimu malipo yake.

Hivyo Sulemani akaamua kumpa Mfalme wa Tiro miji 20, (maana yake kila mji mmoja kwa mwaka mmoja aliotumikiwa). Zaidi ya hayo Sulemani alimpa Hiramu mwaka kwa mwaka kori nyingi za mafuta na ngano.

1Wafalme 5:10 “Basi Hiramu akampa Sulemani miti ya mierezi na miti ya miberoshi kadiri alivyotaka. 

11 Sulemani akampa Hiramu kori ishirini elfu za ngano, chakula cha watu wake, na kori ishirini za mafuta safi. Ndizo Sulemani alizompa Hiramu mwaka kwa mwaka”.

Lakini tunasoma Hiramu, Mfalme wa Tiro hakupendezwa na miji hiyo 20 iliyokuwa kaskazini mwa Israeli (Galilaya, mpakani na Tiro), na biblia haijataja sababu za yeye kutopendezwa na miji hiyo, huenda pengine aliona si mizuri na yeye alitegemea kupewa miji mingine mizuri yenye kupendeza, ambayo huenda ipo katikati ya Israeli.

Na kwasababu hakupendezwa nayo, aliipokea tu hivyo hivyo, na kuiita “miji isiyo na faida” yaani “Kabuli”

Lakini yote katika yote biblia haijaelezea kwa kina sababu ya Sulemani kufanya vile, au sababu ya Hiramu, Mfalme wa Tiro kutopendezwa nayo na hata kuiita nchi ya Kabuli (Maana yake isiyofaa kitu).

Ni nini tujajifunza kupitia habari hiyo na miji hiyo?.

Tunachoweza kujifunza ni kuwa tunapotenda wema “tusitegemee malipo kutoka kwa wanadamu, bali kutoka kwa Mungu”. Malipo ya wanadamu siku zote yana mapungufu mengi.

Mfalme huyu wa Tiro, alikuwa ni mtu mwema sana kuliko wafalme wote waliowahi kutokea Tiro, na zaidi sana alikuwa ni rafiki yake Mfalme Daudi, baba yake Sulemani, na hata alivyosikia kuwa Sulemani anataka kumjengea Mungu nyumba alifurahi sana na kumtukuza Mungu wa Israeli, (1Wafalme 5:7) hivyo akamtia nguvu Sulemani kwa sehemu kubwa sana, lakini pamoja na hayo alitazamia kupewa thawabu nyingi (malipo mengi) kutoka kwa Sulemani, kwasababu alijua Sulemani alikuwa Tajiri sana, Zaidi ya wafalme wote duniani, lakini kinyume chake akapewa vichache tofauti na alivyotegemea, hivyo moyo wake ukauma!, lakini Laiti kama angetegemea vichache ni wazi kuwa asingeumia kwa vile alivyopewa badala yake angeshukuru na thawabu yake ingezidi kuwa kubwa mbele za Mungu.

Hivyo na sisi hatupaswi kutegemea malipo kutoka kwa watu, pale tunapotenda wema bali tunapaswa tuwe na nia ya kiasi, ili wakati wa Bwana ukifika tupate thawabu kulingana na kile tulichokitenda.

Bwana atubariki.

Maran atha.

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mafundisho mengine:

Miji ya Tiro na Sidoni ni miji gani kwasasa?

Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)

Je! Sulemani alienda mbinguni?

Je Mungu anaketi katika giza? (1Wafalme 8:12)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 14 (Yoeli, na Obadia).

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inaposema Yesu ameketi mkono wa kuume inamaana gani?

Mungu mara nyingi huwa anatumia lugha ya picha au maumbo, ili kutupa sisi uelewa mzuri kuhusiana na mambo ya rohoni. Kama tunavyojua inapotokea mtawala, labda raisi amekualika uketi pamoja naye meza moja ule chakula, ni wazi kuwa kwa tendo hilo litakuwa limekupandisha hadhi sana.

Sasa zamani, za wafalme ilikuwa mtu aliyepewa heshima kubwa aliwekewa kiti chake kidogo pembeni mwa mfalme upande wake wa kuume. Na hiyo ilikuwa inamaana kubwa zaidi ya heshima peke yake, bali pia ilimaanisha kupewa mamlaka.

Hivyo katika biblia unapokutana na “mkono wa kuume” Mungu ametumia picha hiyo kumaanisha aidha mambo haya makuu matatu;

  1. Heshima
  2. Mamlaka
  3. Ulinzi

1. HESHIMA.

Maandiko kutuambia Kristo, ameketi mkono wa kuume wa Mungu, ni kutuonyesha, hadhi na ukuu alionao sasa. Mbinguni wapo malaika wengi wenye nguvu, wapo wenye uhai wanne, wapo maserafi na mamilioni ya malaika, lakini hakuna hata mmoja alipewa hadhi ya kuwa karibu/sawa na Mungu zaidi ya Kristo, Bwana wetu.

Waebrania 1:13  Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? 14  Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?

Kwahiyo, aliyepokea heshima, ya juu zaidi ya viumbe vyote ni Kristo Yesu Bwana wetu. Na ndio maana tunamwabudu na kumtukuza. Na heshima zote na shukrani zinamwelekea yeye tu peke yake. Ndiye Mfalme wa Wafalme, na Bwana wa Mabwana. Hafananishwi na mwanadamu yoyote duniani, au malaika yoyote mbinguni.

2. MAMLAKA.

Lakini pia mkono wa kuume sio tu heshima bali pia huwakilisha mamlaka, Kuketi kwake kule, ni kuonyesha mamlaka ya kumiliki na kutenda jambo lolote na kutiisha vitu vyote chini yake anayo.

Waefeso 1:20  aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; 21  juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; 22  akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo 23  ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote

> Vilevile anayo mamlaka ya kutuombea na kutuondolea dhambi, kama kuhani mkuu,

Warumi 8:34  Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.

>Mamlaka ya kutumwagia vipawa vya rohoni na nguvu ya kushuhudia habari njema.

Matendo 2:33  Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia,

Luka 16:19  Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kuume wa Mungu. 20  Nao wale wakatoka, wakahubiri kotekote, Bwana akitenda kazi pamoja nao, na kulithibitisha lile neno kwa ishara zilizofuatana nalo

3. ULINZI.

Uwapo karibu na mfalme, maana yake upo salama, chini ya mfumo wa ulinzi wake. Hivyo Mungu kumweka Kristo kuumeni mwake ni kutuonyesha sisi,ufalme wa Kristo hauhasiki. Na wanaompinga kazi yao ni bure. Na Mungu atawaweka maadui zake chini ya miguu yake.

Zaburi 110:1 Neno la Bwana kwa Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwafanyapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako.

Lakini jambo ambalo watu wengi hawajua ni kwamba Bwana anataka na sisi tumweke yeye mkono wetu wa kuume, maana yake tumpe heshima yake, katika mambo yetu, na yeye, atatuheshimisha, atatuinua, na atatulinda.

Matendo 2:25  Maana Daudi ataja habari zake, Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote, Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.

Usiweke Mali kuumeni kwako, usiweke elimu, au mwanadamu kuumeni kwako. Bali Kristo tu peke yake.

Unaweza pia kupitia vifungu hivi Kwa maarifa zaidi; Mathayo 22:44 , Matendo 7:55, Wakolosai 3:1, Waebrania 1:3,13, 10:12, 1Petro 3:22.

Bwana akubariki.

Je! Kristo yupo kuumeni kwako? Fahamu tu ili Kristo awe pembeni yako, na wewe pembeni yake wakati wote, ni sharti uwe umeokoka. Na wokovu unakuja kwanza kwa kutubu (, yaani kukubali kuacha njia mbaya), na hapo hapo unaupokea msamaha wa dhambi, kisha Kristo anaingia moyoni mwako. Na baada ya hapo unaitimiza haki yote kwa kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi, wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu, na Roho atakuwa tayari ameshakuja ndani yako kuanzia huo wakati na kuendelea. Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu leo akusamehe dhambi zako, basi fungua hapa kwa mwongozo mfupi wa sala ya toba>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Ubarikiwe.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume, maana yake nini?

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

Nini maana ya.. “Utoapo sadaka mkono wako wa kuume usijue ufanyalo mkono wako wa kushoto”

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

Je! waliokufa kabla ya Bwana Yesu wataokolewaje?

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

Rudi nyumbani

Print this post

NDOA NA IHESHIMIWE NA WATU WOTE.

Karibu tujifunze biblia.

(Masomo maalumu  kw wanandoa).

Waebrania 13:4 “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu”.

Hapa biblia inataja vitu viwili; 1) NDOA NA IHESHIMIWE NA WATU WOTE, na 2) MALAZI YAWE SAFI.

Tutazame moja baada ya lingine.

1.NDOA NA IHESHIMIWE NA WATU WOTE.

Hapa anasema “Na iheshimiwe na watu wote”..maana yake si mtu mmoja tu au wawili au watatu, bali wote. Sasa swali ni makundi gani ya watu wanaopaswa kuiheshimu ndoa, na ndoa inaheshimiwaje.

Kundi la kwanza la watu wanaopaswa kuiheshimu ndoa, ni wanandoa wenyewe!..(Na kumbuka ndoa ni ile ya mume mmoja na mke mmoja). Na kundi la pili ni watu wa nje, wasiohusiana na hiyo ndoa.

Kwa wanandoa wanapaswa kuiheshimu ndoa yao kwa kuzuia kitu chochote ambacho kinaweza kuifanya ndoa hiyo iwe ndaifu au ivunjike. Na vitu vinavyoweza kufanya ndoa iwe ndaifu au kuvunjika kabisa ni pamoja na kukosa maelewano, Ugomvi, mafarakano, kukosa utii na upendo,uvumilivu, na uaminifu..haya ni baadhi ya mambo yanayodhoofisha ndoa na hata kuivunja kabisa.

Hivyo wanandoa ni lazima wafanya wawezavyo kutunza upendo wao wa kwanza walipokutana, Amani yao kwanza, furaha yao kwanza, maelewano yao kwanza, na mengineyo mazuri waliyokuwa nayo kipindi wanakutana. Kwa kufanya hivyo watakuwa wameiheshimu ndoa yao na itadumu daima.

Na kwa namna gani wanandoa wanaweza kurudisha upendo wao wa kwanza?…si kwanjia nyingine bali ile ya kutubu na kunyenyekea, na kujazwa Roho Mtakatifu, kwamaana yeye pekee (Roho wa Mungu) ndiye mwenye kutoa matunda yanayohitajika katika ndoa..

Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.

Kundi la pili la watu linalopasa kuheshimu Ndoa, ni watu wa nje wasio wanandoa. Ikiwa na maana kuwa mtu yeyote wa nje iwe ndugu, au rafiki, au jamaa, au jirani, au mpita njia, hapaswi kuwa sababu ya ndoa ya mwingine kudhoofika au kuvunjika.

Maana yake kama huhusiki na ndio hiyo, basi hupaswi kupanda mbegu za fitina katika hiyo ndoa, hupaswi kufanya wanandoa wachukiane, watengane, waumizane, au wafanye lolote litakalowatolea heshima wanandoa hao. Unachopaswa kufanya ni kuwaombea na kuwashauri ikiwa wamefungua mlango huo!, na ushauri unaopaswa kuwapa ni ule wa kibiblia na si wa kidunia.

Vile vile wewe kama mtu usiyehusika na ile ndoa, hupaswi kumtamani mke/mume wa jirani yako, wala kujaribu kumshawishi uwe naye!..ni lazima uiheshimu ndoa yake, vile vile hupaswi kuanzisha mahusiano yoyote yenye viashiria vya kukushuku, au kuleta tashwishi kuhusu uhusiano wako na yeyote katika ndoa, ni lazima ukae mbali kwa kadiri uwezavyo, isipokuwa kwa sababu maalumu ambazo zitaweza kueleweka katika pande zote mbili. (Kwa kufanya hivyo utakuwa umeiheshimu ndoa ya mwingine).

2.MALAZI YAWE SAFI.

Hili ni jambo la Pili: Malazi yawe masafi.

Malazi yanayozungumziwa hapa ni mahali wanandoa wanapokutana kimwili, maana yake mahali hapo panapaswa pawe pasafi daima, pasiwe pachafu!. Na uchafu unaozungumziwa hapo si usafi ule wa vumbi katika kitanda, au jasho la mwili, (huo unafaa lakini sio unaozungumziwa hapo).

Uchafu unaozungumziwa hapo ambao ni najisi ni uchafu wa Zinaa, pamoja na kukutana kimwili kinyume na maumbile kwa wanandoa.

Unapokuwa mwanandoa ni amri kutokutana  kimwili na mwanamke/mwingine  tofauti na uliyefunga naye ndoa!, unapolala na mtu mwingine hapo umefanya malazi kuwa machafu, na ni dhambi kubwa!. Vile vile katika kukutana ni lazima iwe kwa namna ya asili. Na si kinyume na maumbile!. Biblia inasema wafiraji hawataurithi uzima wa milele.

1Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, WALA WAFIRAJI, WALA WALAWITI”

Soma pia 1Timotheo 1:10.

Iheshimu ndoa yako, vile vile heshimu ndoa za wengine.

Je umeokoka?..Fahamu kuwa Kristo anarudi!, na tupo nyakati za hatari.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mafundisho mengine:

MAFUNDISHO YA NDOA.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

FAMILIA TAKATIFU: Marimu na Yusufu.

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?

SWALI: Kikombe cha maji ya baridi ni  kipi Bwana alichokitaja katika;

Mathayo 10:42  Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia, haitampotea kamwe thawabu yake


JIBU: Ni kawaida mtu anayetoka kufanya kazi ngumu, labda ya shamba, au wanaoshiriki katika michezo labda riadha au mipira, utaona huduma ya kwanza wanayoihitaji, sio chakula, bali ni maji, kwasababu mwili huwa unapoteza maji mengi sana pale jasho linapotoka. Na gharama ya maji sikuzote ni ndogo kuliko chakula. Hivyo mtu yeyote huwa ni rahisi kupata huduma hiyo, kwani mtu anaweza kumtolea ndani mwake kwenye pipa lake la kutunzia maji masafi, au kuchota kisimani, na kumpa n.k. Na pale anapompa ya baridi kabisa basi humfanya mtu yule ayanywe yale maji sio tu kwa kukata kiu lakini pia kwa burudiko.

Vivyo hivyo na Bwana naye anawafananisha watu wake, na watenda kazi waliotoka kufanya kazi ya kuchosha, hivyo na wenyewe huwa wanakuwa na kiu chao, wanahitaji maji yao. Lakini zaidi sana maji baridi. Na mtu anayefanya hivyo Mungu amemuahidia kumpa thawabu yake.

Maji ya mwaminio ni yapi?

Yanaweza kuwa ni vyakula: Kwamfano umuonapo, mtumishi wa Mungu labda anahudumu au anahubiri pengine kwenye masoko, au mahali fulani kwa muda mrefu, na wewe ukathamini kumpatia chakula au hata chupa ya maji. Akanywa au akala ashiba akamshukuru Mungu. Hiyo ni thawabu kwako kwa Mungu.

Yaweza pia kuwa sadaka yako: Kile kidogo, kinachoweza kumtunza hata kwa siku hiyo, kwa ajili ya usafiri, au sabuni, au vocha kwa ajili ya mahitaji yake madogo madogo. Bwana amekuahidia pia thawabu yako hata kama utakiona ni kidogo, si zaidi  ukampa vya ziada? Kinabadilika kuwa kikombe cha maji ya baridi.

Yaweza kuwa pia ni “vitu”: Mfano mwingine hana fedha au chakula, lakini ana kitu Fulani cha kumpa, labda nguo, au kiatu, au simu, au huduma n.k. Hicho nacho Bwana anakihesabu kama kikombe cha maji ya baridi.

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa zipo thawabu mbalimbali ambazo Bwana anatoa, kwa kutenda mema, zipo thawabu za kuwasaidia maskini, zipo thawabu za kuwasaidia ndugu, lakini zaidi pia Bwana ameahidi thawabu kwa wale wote wanaowajali watumishi wake.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mafundisho mengine:

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA.

JE NI KIKOMBE KIPI UTAKINYWEA SIKU ILE?

YESU ANA KIU NA WEWE.

UWE KIKOMBE SAFI 

AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.

MAJI YA UZIMA.

Rudi nyumbani

Print this post

Je agano la kale litatoweka kabisa kulingana na Wabrania 8:13?

Jibu: Tusome,

Waebrania 8:13 “Kwa kule kusema, Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka”.

Neno “kuukuu” maana yake ni “kitu kilichochakaa/ kilichoisha muda wake”.. Hivyo hapo biblia inaposema kuwa Agano la kwanza amelifanya kuwa kuukuu tafsiri yake rahisi ni kwamba “Agano la kwanza yaani lile la kale amelifanya kuwa chakavu (lililoisha muda wake)/ lisilofaa tena”.

Lakini swali ni je!.. kupitia mstari huo inamaanisha kuwa Agano la kale litapotea kabisa na halitatumika?…kiasi kwamba halifai tena wala halitatumika?

Jibu ni la! Bwana Yesu alisema mwenyewe kuwa “hakuna yodi moja wala nukta moja ya torati itakayoondoka (soma Mathayo 5:18)”… Na Zaidi sana alisema hakuja kuitangua torati bali kuitimiliza.

Mathayo 5:17 “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza.

18  Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie”.

Sasa swali linarudi pale pale kama hivyo ndivyo kwamba Bwana YESU hakuja kuitangua torati bali kuitimiliza, na kwamba agano la kale bado litaendelea kuwepo, ni kwanini hapo katika Waebrania 8:13 biblia iseme kuwa litatoweka kabisa?. Je! Biblia inajichanganya??

Jibu ni La! biblia haijichanganyi bali tafakari zetu ndizo zinazojichanganya!.

Ili tuelewe vizuri tutafakari mfano ufuatao.

Kampuni moja limetoa aina Fulani la gari, na aina hiyo ya gari ikatumika kwa miaka kadhaa, lakini baada ya miaka 10 ikatoa toleo lingine jipya la aina ile ile ya gari, na hivyo kampuni hilo likaacha kuzalisha lile toleo la kwanza lililo dhaifu na kujikita katika uzalishaji wa toleo jipya.

Sasa ni wazi kuwa kwa jinsi miaka inavyozidi kwenda lile toleo la kwanza litaenda kupotea kabisa na kubaki hili la pili… kwa lugha nyepesi tunaweza kusema kuwa… “Kampuni lile limelifanya toleo la kwanza kuwa kuu, na hivyo lipo karibuni kutoweka kabisa”.

Lakini kwa kutoa toleo jipya haimaanishi kuwa limelipinga lile la kwanza, kwamba badala ya kuzalisha magari sasa linazalisha treni. Hapana! Bali kinyume chake limeliimarisha lile la kwanza, ikiwa na maana kuwa kama tairi za toleo la kwanza zilikuwa dhaifu, basi toleo la pili limeziongezea uimara, lakini gari ni lile lile, vile vile  kama mwonekano wa toleo la kwanza ulikuwa si mzuri basi toleo la pili limeongeza uzuri wa kimwonekano lakini gari ni lile lile.

Na ndivyo katika habari ya agano jipya na lile la kale, Hakuna kilichoondolewa, na kuletwa kingine kipya, bali ni kile kile kilichokuwepo kimeimarishwa Zaidi, kuwa bora Zaidi, kuwa imara Zaidi, kuwa chenye uwezo Zaidi n.k

Kwamfano biblia inasema katika mojawapo wa amri katika agano la kale kuwa “usizini” ikaishia hapo… Sasa hii amri ilikuwa ni dhaifu, kwasababu inasema usizini tu!, mtu anaweza asizini kweli lakini moyoni mwake akalipuka tamaa..

Lakini sasa Bwana YESU aliye mjumbe wa agano jipya anakuja kuitimiliza amri hiyo kuwa “mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha kuzini naye nafsini mwake”. Hata kabla ya kwenda kufanya kile kitendo.

Mathayo 5:27  “Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini;

28  lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake”

Na vile vile katika amri ya “kuua” ni hivyo hivyo…(soma Mathayo 5:21-22).

Kwahiyo kwa lugha nyepesi ni kwamba Agano la pili ni toleo jipya la Agano la kwanza. Lakini mambo ni yale yale.

Sasa ni swali lingine.. Ni wakati gani ambapo agano la kale lilianza kuwa kuu kuu?

Jibu: Ni wakati wa kuja kwa Bwana Yesu kwa mara ya kwanza.

Kipindi Bwana Yesu alipokuja, yeye ndiye wa mwanzilishi wa agano jipya, na kuanzia huo wakati ndio agano la kale katika maarifa yake machanga lilipoanza kuisha muda wake, na mpaka leo hatulitumii tena, limetoweka! Na nguvu katika damu ya Yesu ndani ya agano jipya inatawala.

Ndio maana maarifa machanga ya agano la kale, mfano matumizi ya damu za wanyama kama sadaka za kafara zimebaki kutumiwa na watumishi wa shetani, na katika ukristo Damu ya Yesu ndio utimilifu wa Torati za kafara. Na yeyote anayetumia kafara za wanyama leo hii, awe anajiita mtumishi wa Mungu au mtu yeyote yule anafanya ibada za miungu.

Kwahiyo leo hii katika ukristo hatuna matambiko, wala kafara za wanyama, wala utakaso kupitia damu za wanyama, wala hatuishi kwa kujizuia kuua lakini mioyoni tuna hasira, au tamaa.. bali tunaishi kwa Roho mtakatifu na tunamuabudu Mungu katika roho na kweli.

Bwana atubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MJUMBE WA AGANO.

Je! waliokufa kabla ya Bwana Yesu wataokolewaje?

LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.

Tofauti kati ya ufalme wa mbinguni na ufalme wa Mungu ni ipi?

Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)

Rudi nyumbani

Print this post

Je! fedha ni jawabu la mambo yote? (Mhubiri 10:19).

Jibu: Tusome,

Mhubiri 10:19 “Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, Na divai huyafurahisha maisha; NA FEDHA HULETA JAWABU LA MAMBO YOTE”.

Kulingana na huu mstari je ni kweli fedha ni jawabu la kila kitu?.

Jibu ni La! Fedha haitoi jawabu la mambo yote, kama ndio basi fedha ingeweza kununua uzima wa milele, hivyo kusingekuwa na haja ya Bwana Yesu kutoa uhai wake kwaajili ya uzima wa roho zetu.

Lakini biblia inatufundisha kuwa tumekombolewa kwa damu ya Yesu na si kwa fedha.

1 Petro 1:18 “Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu

19 bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo”.

Vile vile fedha haiwezi kutibu kifo, wala kununua amani, kwasababu wapo watu wenye pesa nyingi lakini hawana amani n.k.

Lakini kama hivyo ndivyo kwamba fedha si jawabu la mambo yote, kwanini bi lia iseme no jawabu la mambo yote?.

Ili kupata jibu la swali hili ni vizuri tukausoma mstari huo kwa kutafakari kwa kina sehemu za kwanza za mstari huo na zile za mwisho.

Mstari huo unaanza kwa kusema.. “Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko” na unandelea kwa kusema… “Na divai huyafurahisha maisha”…na unamalizika kwa kusema “NA FEDHA HULETA JAWABU LA MAMBO YOTE”.

Sasa swali ni mambo gani hayo ambayo fedha inaleta majibu yake?.

Jibu: Ni mambo hayo yanayotajwa hapo juu, maana yake yahusuyo karamu hizo ziletazo kicheko zenye ulevi…. na si mambo mengine tofauti na hayo.

Na kweli mambo ya kidunia karibia yote jawabu lake ni fedha, maana yake ukiwa na fedha utaweza kuyafanya au kuyapata, na ukizikosa fedha pia unaweza kuyakosa.

Anasa zote za kidunia zinahitaji pesa, na wanaotaka anasa wanazitafuta pesa kwasababu hilo ndio jibu lake.

Lakini wana wa Mungu, hawaishi kwa fedha wala fedha si jawabu la mambo yao yote…bali Damu ya Yesu ndio jawabu la mambo yao yote.

Wana wa Mungu hata pasipo pesa wanaweza kuishi vizuri kabisa, na pia hawana tabia ya kupenda fedha, bali fedha yao ni Damu ya Yesu katika Roho Mtakatifu.

Je upo ndani ya agano la damu ya Yesu au Mungu wako ni fedha?.

Waebrania 13:5 “Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Aibusu midomo atoaye jawabu la haki (Mithali 24:26)

KUOTA UNAPEWA PESA, KUNA MAANISHA NINI?

Pesa za bindoni ni nini?(Marko 6:8)

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

Rudi nyumbani

Print this post

SHUGHULIKA NA TABIA ZA KURITHI.

Zipo tabia au mienendo ambayo inaweza kurithishwa kutoka kwa wazazi au mababu/mabibi kwenda kwa watoto au wajukuu. Kama vile jinsi sura, maumbile, rangi, kimo, na mwonekano vinavyoweza kurithishwa kutoka kwa mzazi kwenda kwa mtoto, kiasi cha kwamba mtoto anazaliwa na anakuwa amefanana na baba yake vile vile au bibia yake au mama yake….halikadhalika mambo ya ndani kama vile tabia au mienendo, mtu anaweza kurithi kutoka kwa wazazi wake au mababu zake/mabibi zake.

Ikiwa na maana kuwa kama Mzazi alikuwa na tabia ya ulevi kuna uwezekano na mwana wake naye akaja kuichukua hiyo tabia kama hatashughulika nayo, vile vile kama Mama alikuwa ni kahaba kuna uwezekano na binti naye akaja kuwa kahaba vile vile.

Ezekieli 16:44 “….KAMA MAMA YA MTU ALIVYO, NDIVYO ALIVYO BINTI YAKE”.

Kama mzazi alikuwa ni mtu wa hasira, au mwuaji ni rahisi na mwanae kuja kuwa mtu wa namna hiyo hiyo, kama mzazi au babu alikuwa mwizi, au mkorofi ni rahisi na mtoto wake au mjukuu wake kuja kuchukua hiyo tabia.

Hivyo ni muhimu sana kushughulika na Mienendo ya kurithi!… Ukiona una tabia fulani ambayo pia ipo au ilikuwepo kwa wazazi wako basi shughulika na hiyo tabia mapema.

Zifuatazo ni njia za kushughulika na tabia za Kurithi.

1. ZAMA KATIKA AGANO LA DAMU YA YESU.

Damu ya Yesu pekee ndio inayovunja na kufuta maagano yote ya ukoo na tabia zote za kurithi. Utauliza kivipi?..tusome maandiko yafuatayo..

1Petro 1:18  “Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; MPATE KUTOKA KATIKA MWENENDO WENU USIOFAA MLIOUPOKEA KWA BABA ZENU;

19  bali kwa DAMU YA THAMANI, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo”.

Hapo anasema “MPATE KUTOKA KATIKA MWENENDO USIOFAA MLIOPOKEA KWA BABA ZENU”..Kumbe kuna mienendo inatoka kwa mababa na si yetu!, bali tumepokea!.. na sasa ni kitu gani kinaweza kuifuta hiyo mienendo?..si kingine bali ni Damu ya Yesu pekee sawasawa na huo mstari wa 19.

Na tunaoshwaje kwa Damu ya Yesu?..

Si kwa njia nyingine bali ile ya KUTUBU, kwa kumaanisha kuacha hiyo mienendo tuliyoirithi na hatua ya pili ni KUBATIZWA katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu na hatua ya tatu nay a mwisho ni  KUPOKEA ROHO MTAKATIFU. (sawasawa na Matendo 2:38).

Baada ya hapo ile damu ya Yesu ambayo mpaka leo inatiririka pale Kalvari katika ulimwengu wa Roho, itakutakasa kwa namna isiyoweza kuonekana kwa macho na utakuwa safi, na mizizi ya tabia zote za kurithi itakuwa imekufa hapo..tabia za hasira, vinyongo, chuki, ukahaba, uhuni, vita, wizi, ulevi, uchoyo, ubinafsi n.k zitakuwa zimeondoka.

2.DUMU KATIKA UTAKASO

Baada ya kupokea utakaso wa Damu ya Yesu kwa njia ya kutubu na  kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu sawasawa na Matendo 2:38, hatua inayofuata si kulala tu!, na kusubiria matokeo!!…bali ni kudumu katika agano hilo la Damu ya Yesu, kwanjia ya kuomba mara kwa mara na kuondokana na vichocheo vyote vya dhambi, pamoja na kumtumikia Mungu.

Usitubu na kubatizwa halafu ukaendelea kwenda kwa waganga, au kufanya matambiko ya ukoo, au kutenda dhambi..(hapo zile tabia hazitakuondoka bali ndio zitakita mizizi zaidi)

Lakini ukizingatia hayo maandiko yanayotufundisha kwa moyo wote, basi fahamu kuwa hakuna tabia yoyote ya kurithi itakayosalia ndani yako, bali utakuwa safi daima na hivyo hata kufanyika baraka kwa vizazi vyako vilivyopo na vitakavyokuja. Na Zaidi sana badala ya watoto wako kurithi tabia za kishetani kutoka kwako watarithi tabia za kiungu, kwasababu  tabia za kurithi zinakuwa pia zinabeba laana na baraka nyuma yake..

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

UMUHIMU WA KUZALIWA MARA YA PILI.

TABIA KUU TATU ZA WAHUBIRI WALIORUDI NYUMA NA KUMWACHA MUNGU.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

MAZUNGUMZO MABAYA HUHARIBU TABIA NJEMA.

Rudi nyumbani

Print this post

USIKWEPE CHUO CHA UTAKATIFU.

Zawadi kubwa Mungu aliyompa mwaminio ni UTAKATIFU. 

Utakatifu ni ile hali kuwa mkamilifu kama Mungu, kutokuwa na dosari au kasoro yoyote, msafi asilimia mia moja, bila kosa lolote ndani yako. 

Sasa heshima hii tumetunukiwa na Mungu, jambo ambalo hapo zamani halikwepo, ilihitaji matendo ya haki ya Mtu kuufikia, lakini hapakuwahi kutokea mwanadamu yoyote aliyeweza kufikia cheo hicho cha juu sana cha Mungu, yaani kutokuwa na dhambi kabisa.

Lakini pale tunapomwamini Bwana Yesu, siku hiyo hiyo, Mungu anatufanya Watakatifu kama yeye, haijalishi bado tutakuwa na asili ya dhambi nyingi kiasi gani. Hiyo ndio maana ya neema. Tunaitwa watakatifu bila ya kujisumbua kwa lolote.

Lakini sasa lengo la Mungu sio tuwe “watakatifu katika dhambi” Bali “tuwe watakatifu katika utakatifu”. Hivyo kuanzia huo wakati anaanza kumfundisha mtu kuusomea hadi kuuhitimu Utakatifu wake,aliopewa ili aendane na cheo alichotunukiwa tangu mwanzo.

Na hapo mtu akishindwa kupiga hatua, basi anaondolewa heshima hiyo kwake, na hivyo hawezi tena kuwa kama Mungu, na matokeo yake wokovu unampotea.

Mwaka Fulani hapa nchini kwetu kulikuwa na askari mmoja aliyeonyesha kitendo cha kishujaa kukataa rushwa ya milioni 10, ambapo alishawishiwa aipokee ili aifute kesi ya watuhumiwa wawili waliokuwa wanakabiliwa na mashtaka,. Lakini yeye hakukubali, na ilipokuja kubainika, mkuu wa jeshi la polisi (IGP) akafurahishwa naye, Akampandisha cheo (kwani alikuwa ni askari wa chini). Lakini cha kushangaza baada ya kama miaka mwilini tukaja kusikia Yule askari aliyepandishwa cheo ameshushwa cheo kile. Kufuatilia ni kwanini imekuwa hivyo? Jeshi la polisi likatoa taarifa kuwa alionyesha utovu wa nidhani, wa kukataa kwenda kwenye mafunzo ya cheo chake kipya.  Akidhani kwasababu IGP amempandisha basi inatosha hakuna haja ya mafunzo tena. Akasahau kuwa ufahamu wake wa kielimu ni lazima uendane na cheo chake, kwamba akiwa bado na cheo kikubwa, wakati huo huo anapaswa aendelee kusoma,na kujifunza kimatendo, ili aweze kutumika ipasavyo. Lakini akashushwa cheo na kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa kukataa kutii amri ya jeshi.

Ndivyo ilivyo katika UTAKATIFU tunaopewa na Mungu bure, ni lazima tuutendee kazi kwa kila siku kupiga hatua mpya ya mabadiliko. Huwezi kusema umeokoka (wewe ni mtakatifu), halafu maisha yako ya mwaka jana na mwaka huu ni yaleyale wewe sio mtakatifu.  Kila siku lazima uwe na mabadiliko, ulikuwa unabeti, unaacha kubeti, ulikuwa unavaa mavazi ya uchi uchi, unayachoma moto, ulikuwa unajichubua, unaacha, ulikuwa unasengenya unakaa mbali na wasengenyaji, ulikuwa unakesha kwenye muvi usiku kucha unaacha hayo, unatumia muda wako mwingi kwenye kujisomea biblia, ulikuwa ni mtu wa rushwa unaanza kuondoa vitendo hivyo kwenye biashara yako. Ulikuwa huwezi kufunga na kuomba unaanza kujizoeza kuwa mtu wa rohoni, unafunga, unaomba, na kukesha, Huko ndiko Mungu anakokutaka. Anaona umekiheshimu cheo alichokupa.

Ukiwa ni mtu wa kupiga hatua kila siku, basi Mungu atazidi kukuona wewe ni MTAKATIFU na hivyo utakuwa karibu na yeye. Lakini ukiishi hoe hae, hutambuliki kama umeokoka, au vipi, tabia zilezile za zamani unaendelea nazo, wala hujihangaishi kuziondoa. Usijindanganye wewe umeokoka.

Bwana atusaidie..

Je! Upo ndani ya Kristo? Je unataarifa kuwa hizi ni siku za mwisho? Yesu amekaribia kurudi? Ni nini utamweleza Mungu siku ile endapo leo utaukataa wokovu unaoletwa kwako bure..  Tubu dhambi zako, mgeukie Bwana, akupe Roho Mtakatifu, akupe heshimu hiyo ya utakatifu. Hivyo Ikiwa upo tayari kufanya hivyo basi fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa sala ya toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

FUNDISHO KUU LA NEEMA YA MUNGU KWETU.

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.

USITAZAME NYUMA!

Kwanini hatuirithi neema kama tunavyoirithi dhambi?

HATARI YA KUHUBIRI INJILI TOFAUTI NA ILIYOANDIKWA KWENYE BIBLIA.

Wakili ni nani kibiblia? Uwakili ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Wapalestina ni watu gani, na sehemu yao katika biblia ni ipi?

Jina Palestina limetoka na Neno la kiyunani Filistia,  lenye maana ya ardhi ya wafilisti. Kwahiyo ile Filisti inayotajwa kwenye biblia ndio Palestina unayoisikia sasa.

Lakini Jambo ambalo wengi wanachanganya ni kudhani kuwa wafilisti walikuwa ni waarabu. Si kweli, kwani waarabu walikuwa ni watoto wa Ishmaeli kutoka kwa Ibrahimu, lakini wafilisti walikuwepo kabla hata ya Ibrahimu, na walitokea katika uzao wa Hamu.

Mwanzo10:14 na Wapathrusi, na Wakasluhi; huko ndiko walikotoka Wafilisti na Wakaftori.

Watu hawa walikuwa ni wapagani moja kwa moja, na waliabudu miungu yao mikuu mitatu iliyoitwa Ashtorethi, Baal-zebubu, na Dagoni.(Waamuzi 16:23, 2Wafalme 1:2, 1Samweli 31:10,)

Wafilisti walikwenda kuweka makazi yao, katika nchi ya Kaanani. Upande wa kusini, kutoka mto Yordani mpaka ule wa ile habari kubwa (Bahari ya Mediterenia). Na baadaye kipindi cha akina Samweli wakawa na miji yao mitano imara iliyoitwa Gaza, Ashdodi, Gathi, Ashkeloni, Ekroni (1Samweli 6:17, Yoshua 13:3)

Hivyo Ibrahimu alipoitwa na Mungu na kuambiwa aindee nchi ile aliwakuta tayari wapo, na wameshajiwekea ngome zao (Mwanzo 21:32, 34, 26:1).

Na wana wa Israeli walipokuwa wanavuka kuingia nchi yao ya ahadi Waliambiwa wawaangamize wakaanani wote, kwasababu wamepewa nchi yote. Lakini tunaona walipuuzia, na kule kukawia kawia kwao na kuridhika, Mungu akawaambia watu hawa watakuwa “mwiba” kwao .  

Waamuzi 2:1 Kisha malaika wa Bwana alikwea juu kutoka Gilgali kwenda Bokimu. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi;  2 nanyi msifanye agano lo lote na hawa wenyeji wa nchi hii; zipomosheni nchi madhabahu zao; lakini hamkuisikia sauti yangu; je! Mmefanya haya kwa sababu gani?  3 Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni tanzi kwenu.

Na ndivyo ilivyokuwa Yoshua hakuweza kuwatoa wenyeji wote wa Filisti(Yoshua 11:20-23). Na ndio hao wakaja kuwasumbua baadaye.

Ni wazi kuwa Israeli walipigana vita vingi, lakini moja wa maadui zao waliokuwa wanawasumbua sana basi ni hawa wafilisti, kwasababu walikuja kupata nguvu, sio tu ya wingi wa watu, bali pia ya kiteknolojia katika silaha, kiasi kwamba Israeli ilitegemea kunolewa silaha zao kutoka Filisti.(1Samweli 13:19-23). Na zaidi sana waliwazidi Israeli hata kimaendeleo, kwa kipindi kirefu hawakuweza kuwashinda

Na wana wa Israeli walipomkosea Mungu aliwaweka kwenye mikono yao, wakataabishwa kwa muda mrefu, kisha walipomlilia Bwana, walinyanyuliwa mkombozi. Ndio hapo tunawaona waamuzi kama wakina Samsoni, Shamgari, Samweli, Sauli, Daudi.Wakipigana vita vingi sana na watu hawa.Ambavyo tunavyosoma katika biblia (Waamuzi, Samweli 1&2, Wafalme 1&2,)

Kuanguka kwa wafilisti.

Lakini wakati Israeli inachukuliwa utumwani taifa hili nalo halikupona lilianguka, katika mkono wa mfalme Nebukreza wa Babeli, na kupotea kabisa. (Yeremia 47:47, Ezekieli 25:15-17, Sefania 2:4-7).

Tangu huo wakati hakukuwa na taifa rasmi la wafilisti, wala haikuwa rahisi kuwatambua kwa miaka zaidi ya 2500.  Mpaka ilipofikia mwaka 1948, Taifa la Israeli kuundwa tena kwa mara ya kwanza, eneo hilo la wafilisti, kusini mwa Israeli, lilikuwa tayari linajulikana kama “Palestina”

Palestina ya leo ni mahali palipo na mchanganyiko wa jamii mbalimbali za watu, walio wa asili ya kifilisti wakiwa ni wachache sana, lakini wengi wao sasa ni waislamu waliohamishiwa hapo na waturuki, kutoka katika mataifa mbalimbali kati ya karne ya 16-19, pamoja waarabu katika karne ya 20 ambao nao waliletwa na waingereza.

Hivyo mpaka sasa tunavyoona, ni kwamba Palestina imemezwa zaidi na dini ya kiislamu na jamii kubwa ya waharabu. Na cha kushangaza ni kwamba ijapokuwa  jamii ya sasa ni tofauti kabisa,na wafilisti wa zamani, bado migororo ile ile ya zamani inanyunyuka tena. Kuonyesha kuwa Neno la Mungu halipiti milele.

Ule mwiba bado utawasumbua wayahudi.

Nini kinaendelea rohoni?

Lakini ipo sababu nyingine ya Rohoni. Kumbuka kuwa hatma ya huu ulimwengu, itakuwa ni Dunia nzima kusimama kinyume na taifa teule la Mungu Israeli. Ili Yesu Kristo atokee mawinguni na kuwapigania watu (Matendo 1:6, Ufunuo 19) .  Na tayari Mungu alishaahidi kuwa atafanya mataifa yote kuwa kama kikombe cha kulemea,. Ili tu ayachonganishe, kisha mwisho wake uwe ni yeye kulitetea taifa lake, ndipo huo mwisho ufike.

Wewe huoni mvuragano huu, unayagusa mataifa yote duniani.

Zekaria 12:3 Tena itakuwa siku hiyo, nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote; wote watakaojitwika jiwe hilo watapata jeraha nyingi; na mataifa yote ya dunia watakusanyika pamoja juu yake

Unaweza kuona ni jinsi gani tupo mwishoni kabisa mwa dunia. Hii neema tuliyonayo huku katika mataifa, ndio inafikia ukomo wake, na kurejea Israeli. Maana Mungu anasema atawarudia watu wake (Warumi 10&11), na kuwaokoa, wakati huo yatakapokuwa yanatendeka unyakuo utakuwa umeshapita huku kwetu.

Zekaria 12:9 Hata itakuwa siku hiyo, ya kwamba nitatafuta kuwaangamiza mataifa yote watakaokuja kupigana na Yerusalemu.  10 Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.  11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido

Je! Unaishije sasa hivi, Umehubiriwa injili mara ngapi, bado unashupaza shingo yango? Huko uendako unatarajia ukawe mgeni wa nani. Na ukweli umeshaujua kuwa tunaishi katika siku za kumalizia, Unyukuo wa kanisa ni wakati wowote. Huu ni wakati sasa ya kuyathimini maisha yako ya rohoni, angalia dunia inapoelekea, kufumba na kufumbua mambo yanabadilika. Uamuzi ni wako. Lakini ikiwa utapenda Yesu akuokoe, akufanye kiumbe kipya basi fungua hapa upate mwongozo wa sala ya toba. >>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

NIMEAZIMIA KUWAKUSANYA MATAIFA. NIPATE KUWAMWAGIA GHADHABU YANGU

KUNA NGUVU YA ZIADA KATIKA KULING’ANG’ANIA KUSUDI LA MUNGU.

Konzo la Ng’ombe ni nini? (Waamuzi 3:31).

Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.

USIMPE NGUVU SHETANI.

Mataifa ni nini katika Biblia?

UAMINIFU NI KIGEZO KIKUBWA CHA KUTUMIWA NA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post