Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?

Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?

Je! Ni wakina nani hao katika (Mathayo 16:28) ambao Bwana alisema hawataonja mauti mpaka atakapokuja?


JIBU: Tusome..

Mathayo 16:27 “Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.

28 Amin, nawaambieni, Pana watu katika hawa wasimamao hapa, ambao hawataonja mauti kabisa, hata watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika ufalme wake”

Katika sentensi hiyo tunaona Bwana alikuwa anazungumza habari za kuja kwake jinsi kutakavyokuwa kwamba atakuja katika utukufu wa Baba yake na malaika zake na kufanya hukumu…Lakini wakati anazungumza maneno hayo akaongezea na sentensi moja ya kipekee sana kwamba “kuna watu ambao wamesimama naye pale wakati anaongea nao ambao hawataonja mauti hata watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika ufalme wake”.

Sasa ukianzia juu tena kidogo utaona kuwa Bwana Yesu hakuwa anazungumza maneno hayo mbele ya makutano..utagundua alikuwa anazungumza na wanafunzi wake 12 tu!..Kumbuka si mambo yote Bwana alikuwa anazungumza mbele ya makutano..kuna mambo alikuwa anazungumza mbele ya watu wote na kuna ambayo alikuwa anazungumza na wanafunzi wake tu!..Sasa mojawapo ya aliyokuwa anazungumza na wanafunzi wake tu ndilo hili kwamba “wapo ambao hawataonja mauti mpaka watakapomwona anakuja”…Maana yake ni kwamba miongoni mwa wale wanafunzi 12, kuna ambao hawataonja mauti kabisa.

Sasa swali la kujiuliza ni kweli Bwana alikuwa anamaanisha hivyo kwamba wapo ambao hawatakufa kabisa au alikuwa anamaanisha vingine?

Biblia inataja baadhi ya mitume walikufa..na historia pia inathibitisha vifo vya mitume wengine wote waliosalia…Hivyo hakuna mtume hata Mtume mmoja ambaye hakufa…Kwahiyo maana yake Bwana pale hakumaanisha kuwa hawatakufa kabisa kabla ya kushuhudia kuja kwake kwa mara ya pili(Ingawa huo uwezo wa kumfanya mtu asife kabisa hata atakapokuja anao lakini kwa pale hakumaanisha vile)..Bali alikuwa anamaanisha kuwa wapo ambao hawatakufa mpaka “watakapoonyeshwa jinsi atakavyokuja katika utukufu wake siku za mwisho”..Na kuonyeshwa huko si kwingine bali kwa njia ya maono ya wazi kabisa…Yapo maono yanayokuja kwa mfumo wa ndoto, na yapo yanayokuja kwa njia ya dhahiri kabisa…Haya ya Dhahiri mara nyingine yanajumuisha watu Zaidi ya mmoja wanaona kitu kinachofanana kwa wakati mmoja…lakini pia hayo mengine mara nyingi yanamtokea mtu mmoja mmoja na yanakuwa kwa mfumo kama wa ndoto.

Sasa ni lini walionyeshwa maono hayo ya kuja kwa Bwana kwa nguvu na utukufu?

Ukishuka kidogo sura inayofuata mstari wa kwanza biblia inasema…

Mathayo 17:1 “Na baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani;

2 akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang’aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru.

3 Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye.

4 Petro akajibu akamwambia Yesu, Bwana, ni vizuri sisi kuwapo hapa; ukitaka, nitafanya hapa vibanda vitatu, kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya.

5 Alipokuwa katika kusema, tazama, wingu jeupe likawatia uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile wingu, ikasema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye.

6 Na wale wanafunzi waliposikia, walianguka kifulifuli, wakaogopa sana.

7 Yesu akaja, akawagusa, akasema, Inukeni, wala msiogope.

8 Wakainua macho yao, wasione mtu ila Yesu peke yake.

9 Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, Msimwambie mtu ye yote habari ya maono hayo, hata Mwana wa Adamu atakapofufuka katika wafu”

Umeona hapo mstari wa 2 unasema “AKAGEUKA SURA YAKE MBELE YAO; USO WAKE UKANG’AA KAMA JUA, MAVAZI YAKE YAKAWA MEUPE KAMA NURU.” Huo ndio utukufu ambao atakuja nao mwana wa Adamu siku za mwisho…ambapo kila jicho litamwona wakati huo uso wake utakuwa unang’aa kama jua, na mavazi yake yatakuwa meupi kama Nuru..Mataifa yote wataanguka chini na kuomboleza…naye atawahukumu waovu…

Kwahiyo hawa mitume watatu kati ya wale 12, ndio waliopata neema hiyo/bahati hiyo kuuona utukufu huo wa kuja kwa Yesu kabla hawajafa, na hivyo Neno la Yesu likatimia hapo kwamba wameuona utukufu wake kabla hawajafa. Na haikumaanisha kwamba wataendelea kuwa hai mpaka watakapomwona akija mara ya pili atakapotokea mawinguni hapana!….watakaomwona akitokea mawinguni kwa utukufu huo ni wale wote watakaokuwa wameachwa katika unyakuo, ambao wamebaki duniani na kuipokea chapa…lakini watakatifu wakati huo watakuwa wameshanyakuliwa na watakuja pamoja na Kristo siku hiyo ya utukufu wake…

Sasa tutazidi kujuaje kama hayo yote ni kweli?..Biblia inasema kwa vinywa vya mashahidi wawili, watatu kila neno lithibitike.

Tunaona tena Petro akilishuhudia jambo hilo…Jinsi alivyoona kuja kwake..

Tusome..

2Petro 1:16 “Maana hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, tulipowajulisha ninyi nguvu zake Bwana wetu Yesu Kristo na KUJA KWAKE; bali tulikuwa tumeuona wenyewe ukuu wake.

17 Maana alipata kwa Mungu Baba heshima na utukufu, hapo alipoletewa sauti iliyotoka katika utukufu mkuu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.

18 Na sauti hiyo sisi tuliisikia ikitoka mbinguni tulipokuwa pamoja naye katika mlima ule mtakatifu.”.

Uonaona hapo?..anasema hatukuhadithiwa na mtu kuhusu nguvu zake na KUJA KWAKE..(maana yake siku ile mlimani yeye pamoja na Yohana na Yakobo walionyeshwa KUJA KWAKE) na walishuhudia wenyewe.

Bwana akubariki sana.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

SIKU ILE NA SAA ILE.

Shetani anatolea wapi fedha, angali tunajua Fedha na dhahabu ni mali ya Bwana?.

TAFUTA KUJUA MAMBO YAJAYO

Kuna tofauti gani kati ya SALA na DUA?

MAJINI WAZURI WAPO?

IPO NGUVU ITUVUTAYO KWA KRISTO, ITHAMINI!.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Jackson Mkwasa
Jackson Mkwasa
2 years ago

Jina la bwana wetu YESU KRISTO litukuzwe

Haroldn
Haroldn
3 years ago

Mbarikiwe sana na Bwana wetu YESU KRISTO