Title March 2019

NI NANI ANAYEUFUNGA MLANGO WA MAARIFA?.

Wakati nikiwa shule ya msingi, kuna mwalimu mmoja aliyetufundisha somo lijulikanalo kama “stadi za kazi”, mwalimu huyu wanafunzi wote tulimpenda sana kwasababu alikuwa tofauti kidogo na walimu wengine, kwani yeye kila alipokuwa akija darasani, alituambia watoto tumchangie hela ya karanga atutoe nje michezoni (lakini kiukweli hakuitumia kwa karanga bali alikwenda kununulia pombe).Na kama unavyojua watoto wanavyopenda michezo, hawapendi kukaa muda wote darasani kufundishwa, hivyo suala la kujitolea kila mtu sh.5 au sh.10 halikuwa ni jambo kubwa sana kulinganisha na raha tuliyokwenda kuipata kwenye michezo!.

Hiyo ndio ilikuwa desturi yake, na walimu wengine walipokuwa wanaona watoto wanacheza nje muda wa masomo, walipoulizwa mnafanya nini nje muda huu, wote wanajibu ni sehemu ya somo mwalimu ametutoa nje!, na ni kweli katika somo la stadi za kazi michezo inayo nafasi yake. Lakini baadaye likaja kuleta madhara mengine.

Hiyo ikapelekea watoto kupoteza hamu ya kufundishwa darasani somo lile, na hivyo kutokuwa na maarifa ya mambo mengine muhimu yahusuyo stadi za kazi, mfano ujenzi, ususi, uchongaji, ufugaji, ukulima, ushonaji n.k. wakabakia kufikiri stadi za kazi ni michezo tu ya kuruka ruka nje. Na mwisho wa siku mtihani wa mwisho ukifika watoto wanafeli. Kwasababu wanakuwa wamekosa maarifa ya kutosha juu ya somo lile…Unaona hapo tatizo mama lipo kwa yule mwalimu ambaye angepaswa atimize wajibu wake wa kuwafungulia wanafunzi wake mlango wa maarifa kwa kuwafundisha mambo yote katika uwiano, badala yake yeye ndiye anayekuwa wa kwanza kuufunga mlango huo kwa faida zake mwenyewe.

Jambo la namna hiyo lipo hata katika kanisa la Mungu, biblia inasema katika.

Luka 11:52 “Ole wenu, enyi wana-sheria, kwa kuwa MMEUONDOA UFUNGUO WA MAARIFA; wenyewe hamkuingia, na wale waliokuwa wakiingia mmewazuia”.

Unaona, Mungu alishaweka ufunguo mlangoni, kilichokuwa kimebaki ni kufunguliwa tu na kuingia katika maarifa ya kumjua Mungu kwa mapana na marefu yake na sio kuhangaika hangaika tena, lakini hapa tunaona wana-sheria (yaani watu waliobobea katika kuisoma sheria/torati), au kwasasa tunaweza kusema waalimu wa biblia, wachungaji, maaskofu,manabii n.k. wao ambao ndio wangepaswa wawe wa kwanza kuuzungusha ule ufunguo ili waingie katika maarifa ya kumjua Mungu pamoja na watu wao, badala yake wao ndio wanaokuwa wakwanza kuundoa ule ufunguo na wanafanya hivyo kwa makusudi kabisa,…na mtu akishautoka ufunguo ni nani awezaye kuingia tena?.

Viongozi hawa wanajua kabisa watu wengi hawapendi, kufundishwa maneno ya Mungu katika mapana yake na marefu yake, kwasababu ni wachanga hawajui umuhimu wake kwasasa, na wao bila hata ya kuwahurumia, wanawalazimisha hivyo hivyo wajifunze na hayo mengine hata kama hawataki kwa usalama wa maisha yao,..Wao wanawafundisha yale ambayo watu wanataka tu kusikia, watu wanapenda tu, na kibaya zaidi pale wanapoona matoleo yanaongezeka kwa injili kama hizo, ndipo wanapoamua kutia nanga na kufundisha hizo hizo tu siku zote, na kuacha mambo ya msingi.

Viongozi hawa wanafahamu kuwa injili za mafanikio zinapendwa na watu wengi, lakini kwa makusudi kabisa huku wakijua kabisa hakuna mlevi yoyote atakayeurithi ufalme wa mbinguni, wala mtu yoyote ambaye sio mtakatifu atakayemwona Mungu, (Waebrania 12:14), wala wazinzi, wala muabudu sanamu, lakini wao hawana muda wa kugusia mambo hayo…

Viongozi hawa wanafahamu kabisa kuwa wale watu ni wachanga, na kama ni wachanga ni lazima watapenda vitu vilaini laini tu, na yeye kama mwalimu badala azingatie kuwa mchezo peke yake haitoshi kumpa mtu maarifa yote ya kufaulia mtihani bali achanganye na maarifa mengine yote..Yeye hilo halizingatii na matokeo yake mwisho wa siku watoto wote wanafeli, na ndio huko watu wanaishia shimo la kuzimu.

Ndugu jiulize injili unazozisikia mara kwa mara, JE! ZINAKUJENGA PANDE ZOTE AU UPANDE MMOJA TU WA MAFANIKIO YA KIMWILI?…Unafahamu kuwa haya maisha yatakuwa na mwisho?..ulishawahi kulitafakari hilo?, kama unyakuo hautakukuta basi ujue siku yoyote unaweza ukaondoka hapa duniani, na huko uendako je! utakuwa mgeni wa nani? Huko uendako umejiwekea hazina gani?..BWANA YESU ANASEMA ITAKUFAIDIA NINI UUPATE ULIMWENGU MZIMA, NA HUKU UMEPATA HASARA YA NAFSI YAKO?, upate nyumba nzuri, upate gari, upate umaarufu, upate ukubwa na kila kitu na huku unapata hasara ya nafsi yako kwa kumkosa Kristo moyoni mwako??

Siku ile utakapokufa utasema laiti ningejiwekea huku hazina, nisingekuwa mahali hapa pa taabu, Leo hii unafurahia injili ya kuburudishwa na vichekezo na comedy kwenye madhabahu, na huku unajua kabisa umefarakana na Mungu moyoni mwako, na hata ukifa leo unakwenda kuzimu, hujui kuwa kizazi unachoishi ndio kizazi kilicho katika hatari kubwa sana kuliko vyote vilivyotangulia, ni kizazi kilicho katika hatari ya kuuona uharibifu utakaoijilia dunia nzima, hujui kuwa kulingana na kalenda ya kimbinguni tunaishi katika lile kanisa la Mwisho lijulikanalo kama Laodikia ambalo ndilo litakaloshuhudia kurudi kwa pili kwa Kristo?. Hufahamu kuwa hatua za Unyakuo zimeshakwisha anza, na wewe huna habari, haujui kuwa kazi za mpinga-kristo sasa zipo dhahiri na kiti chake kinajulikana sasa mahali kilipo, wewe upo buzy kukimbilia injili za vichekesho, na kufarijiwa, na huku unadhani upo sawa…Kaa mbali na hao viongozi! Na hizo injili ambazo zimekosa uwiano.

Tunaonywa tuwe makini, huu ni wakati wa kutafuta kwa bidii mahusiano yetu binafsi na Mungu, kupata maarifa ya kina juu ya mapenzi yake kwetu sisi wanadamu, na maarifa haya yanakuja kwa kulitafakari na kuliishi Neno la Mungu.

2Petro 1:4 “Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa WASHIRIKA WA TABIA YA UUNGU, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa.

5 Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu MAARIFA”,

Hivyo ni maombi yangu, tutaanza mwanzo mpya sasa, ikiwa tulishampa Bwana maisha yetu, embu tuongezee na maarifa ya kumjua Mungu na uweza wake..Tutafakari zaidi mambo ya mbinguni kwasababu mtihani mkubwa sana upo mbele yetu, na tusipokuwa na maarifa ya kutosha ya kuyajua mapenzi ya Mungu, basi tujue kufeli kupo mbele yetu, na kufeli kwenyewe ni kuishia kuzimu..Lakini tukiwa na maarifa ya kutosha kuhusu Mungu wetu, hiyo itatusaidia kuishi maisha ya uangalifu sasa katika huu ulimwengu kama wapitaji hapa duniani na mwisho wake tutafaulu na kuishia Mbinguni milele.

Kama hujampa Bwana maisha yako kihakika, au unasita sita katika mambo mawili, au umezamishwa katika hizi injili za mafanikio zisizokuwa na uwiano za kuchuja mbu na kumeza ngamia, hebu tenga muda jaribu kuweka mambo yote kwenye mizani, jaribu kulitilia mkazo lile lenye uzito mkubwa zaidi na hayo mengine yafuate baadaye.

Mathayo 23:23 “Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, na rehema, na imani; hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache.

24 Viongozi vipofu, wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia”.

Hivyo tuwe tayari kuzisikia habari zote, za ufalme wa mbinguni, kwa uwiano wote, na Mungu atatusaidia, La kwanza liwe ufalme wa mbinguni, na hayo mengine yafuate.

Wakolosai 1.9 “Kwa sababu hiyo sisi nasi, tangu siku ile tuliposikia, hatuachi kufanya maombi na dua kwa ajili yenu, ILI MJAZWE MAARIFA YA MAPENZI YAKE KATIKA HEKIMA YOTE NA UFAHAMU WA ROHONI;

10 mwenende kama ulivyo wajibu wenu kwa Bwana, mkimpendeza kabisa; mkizaa matunda kwa kila kazi njema, na kuzidi katika maarifa ya Mungu;”

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

KWANINI KUNA WATU WANAFANYIWA DELIVERANCE (MAOMBI YA KUFUNGULIWA), LAKINI BAADA YA MUDA WANARUDIWA TENA NA HALI ILE ILE SABABU NI NINI?

NGUVU YA HEKIMA NA AKILI

UKWELI UNAOPOTOSHA.


Rudi Nyumbani

Print this post

UPONYAJI WA YESU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, libarikiwe.

Karibu tujifunze Neno la Mungu, na leo tutajikumbusha kazi mojawapo ya Yesu Kristo iliyomleta Duniani…Tukiachilia mbali kazi ya UKOMBOZI na KUTUONYESHA NJIA YA KUMWELEKEA BABA..kazi nyingine iliyomleta Bwana duniani ni UPONYAJI. Na uponyaji upo wa rohoni na mwilini. Leo kwa ufupi tutajifunza juu ya uponyaji wa mwili.

Yesu Kristo sio daktari, ingawa tukimwita ni daktari mkuu tutakuwa hatujakosea sana..lakini yeye ni zaidi ya hapo…yeye ni mwumbaji..daktari atamtibu mtu, lakini litabaki kovu (hana uwezo wa kukirudisha kitu kama kilivyokuwa katika uhalisia wake)..Lakini Mungu ni zaidi ya hapo hatibu bali anaponya..

Katika huduma yake, Tangazo lake la kwanza alilowatangazia wayahudi ni hili.

Luka 4: 18 “ROHO WA BWANA YU JUU YANGU, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,

19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa.

20 Akakifunga chuo, akamrudishia mtumishi, akaketi; na watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.

21 AKAANZA KUWAAMBIA, LEO MAANDIKO HAYA YAMETIMIA MASIKIONI MWENU”.

Huyo ni Bwana Yesu aliyezungumza maneno hayo baada ya miaka mingi wana wa Israeli kusubiria tumaini kutoka kwa Mungu, na sasa tumaini hilo limewafikia, Na tunaona ni Bwana pekee ndiye aliyeanza kufanya miujiza isiyo ya kawaida ambayo haikuwahi kutokea katika historia ya mwanadamu kwa vizazi vyote. Vipofu walikuwa wanaona, viwete wanatembea..na wenye magonjwa ya kila namna yalikuwa yanaponywa.

Ndugu nataka nikuambie Kristo Yesu mpaka leo anaishi, na kazi alizozifanya wakati akiwa hapa duniani bado anazifanya hata leo, kwa kupitia watu wake. Na yeye sio mwongo kama sisi wanadamu. Maneno yake ni ya ukweli wote. Tumeshuhudia mara nyingi kwa macho yetu watu wakiponya papo kwa hapo. Na mimi mwenyewe alishawahi kuniponya papo kwa hapo na sio mara moja.

Nimewahi kusikia shuhuda kadha za watu kuponywa magonjwa ambayo yamewatesa muda mrefu na wamekosa suluhisho kila walikokwenda, nimewahi kuwaombea watu kadhaa na Bwana akawaponya magonjwa ambayo yamewatesa kwa miaka mingi, na nimewahi kusikia shuhuda kadha za watu ambao Mungu kawaponya watu pasipo hata kuombewa. Hayo yote ni kuthibitisha kuwa Yesu Kristo si mwongo.

Sasa ni muhimu kufahamu ni jinsi gani uponyaji wa kimungu unashuka juu ya mtu. Wengi wetu tunadhani Mungu anatuponya au anatupa afya kwa utakatifu wetu tulionao….hiyo kwa sehemu Fulani ina ukweli kwa baadhi ya watu…kwasababu kama mtu anaisikia injili kwa miaka na miaka na hataki kubadilika, na anakuwa ni mtu wa kusitasita, leo anakwenda mbele, kesho anarudi nyuma, leo anakwenda kanisani kesho ni mwasherati, mtu wa namna hiyo ulinzi wa kimungu umeondoka juu yake, hivyo inakuwa ni rahisi kwake kuvamiwa na roho za uharibifu, ndio unakuta zitakazomsababishia magonjwa ya ajabu na hata wakati mwingine mauti.

Lakini kama mtu ni mwaminifu kwa Mungu au hakuwahi kuisikia kabisa INJILI au yupo katika hatua za awali za kumpa Yesu maisha yake halafu baadhi ya mambo yamemtokea, kama vile magonjwa pengine yasiyojulikana hata chanzo chake ni nini, na akaenda kutafuta uponyaji kutoka kwa Mungu kwa moyo wa kumgeukia yeye..Nataka nikuambie Ipo dawa!!, YESU NDIYE DAWA!!. Biblia inasema Yesu ni yeye Yule jana, leo na hata milele ikimaanisha kuwa anao uwezo wa kukirudisha kitu kiwe kama kilivyokuwa jana, na anao uwezo wa kukileta kitu leo kiwe kama kitakavyokuwa miaka 100 mbele au milele ijayo..Kwahiyo yeye hana muda wala hajachelewa…wanadamu sisi ndio tunao usemi unaosema “basi tena haiwezekani” lakini Yesu sio hivyo yeye hana muda, anaponya sasahivi na anarudisha kitu kama kilivyokuwa jana.. aliirudisha ngozi ya Naamani iliyokuwa na ukoma ikawa kama ngozi ya mtoto mchanga….

2 Wafalme 5: 13 “Watumishi wake wakamkaribia, wakamwambia, wakasema, Baba yangu, kama yule nabii angalikuambia kutenda jambo kubwa, usingalilitenda? Je! Si zaidi basi, akikuambia, Jioshe, uwe safi?

14 Ndipo akashuka, akajichovya mara saba katika Yordani, sawasawa na neno lake yule mtu wa Mungu; NAYO NYAMA YA MWILI WAKE IKARUDI IKAWA KAMA NYAMA YA MWILI WA MTOTO MCHANGA, AKAWA SAFI.

15 Akamrudia yule mtu wa Mungu, yeye na mafuatano yake yote. Akaja, akasimama mbele yake;”

Sasa kama wewe ni mgonjwa na huo ugonjwa umekutesa sana kwa muda mrefu, labda ni UKIMWI, au CANCER, au KISUKARI au ugonjwa wowote ule na unakuogopesha na hujui huo ugonjwa sababu yake ni nini, unachotakiwa kufanya sasahivi, ni kutulia, usiogope wala usikuogopeshe wala usipanic, tenga dakika chache mahali ulipo, tubu dhambi zako na maovu yako, na umwahidi Bwana endapo akikuponya huo ugonjwa utamfanyia nini…

Baada ya kutubu na kumwahidi…nataka utafakari mfano huu kisha uutumie huo kupokea uponyaji wako sasahivi. Hebu tafakari siku ulipojikata na kisu na baada ya muda Fulani kile kidonda kikapona..je! ulitumia utakatifu gani hapo kufanya ngozi yako ijirudie kama ilivyokuwa kwanza?…au siku upele ulipokuota kwenye ngozi yako na kesho asubuhi ukaukuta umepotea ulitumia utakatifu gani kuufanya upotee…hebu tafakari siku ulipojisikia kichwa kinauma na baada ya muda kikaisha chenyewe labda baada ya kulala na kuamka asubuhi, ulitumia utakatifu gani kukiponya? Kama hukutumia utakatifu wowote kijiponya kadhalika na ugonjwa ulio nao sasahivi hauhitaji utakatifu wowote…Siku ile ni Mungu alikiponya kichwa chako bure kwa Neema yake pasipo hata wewe kujijua, ukadhani ni mwili wako umejiponya mwenyewe, kumbe hujui ni Mungu ndiye aliyekuponya. na kila siku anauponya mwili wako pasipo hata wewe kujijua wala kumwomba, anakuponya kwa neema zake tu! Bureee…ngozi ya mguu wako kila siku inachubuka lakini kila siku Bwana anakutengenezea ngozi mpya ndio maana kiatu chako kinachakaa na unakibadilisha viatu kila siku lakini mguu wako hauchakai na wala haubadilishi, ndio maana nguo zako zinachakaa lakini mwili wako uko vile vile siku zote. Huo ni uponyaji wa kiMungu unaoendelea mwilini mwako pasipo matendo ya sheria.

Hivyo kwa kanuni hiyo hiyo ya kuponywa pasipo matendo, basi itumie hiyo hiyo kwa ugonjwa ulionao hapo ulipo, kama una HIV, au KISUKARI, au KANSA, au UTASA au Vidonda vya tumbo, au tatizo la figo, au ini, au moyo, au ni kiziwi, au kipofu, au ni kiwete, au tatizo lolote lile katika mwili wako. Kinachohitajika kwako ni IMANI tu!!..Usianze kujishaurishauri wala kuwa na mashaka mashaka, yakatae hayo mashaka, hata kama wakati mwingine bado unaona kuna udhaifu mwilini, hapo ulipo simama juu sema nimeshapona kwa jina la YESU. Kifo kimeshaingia kwenye huo ugonjwa..haupo tena huo ugonjwa, hata kama bado unahisi maumivu yasikuogopeshe tayari kifo kimeshaingia kwenye huo ugonjwa..unaukumbuka ule mtini Bwana Yesu alioulaani?…haukunyauka palepale lakini tayari ulikuwa umeshakufa ndani kwa ndani, hauna uzima tena, mizizi ilikuwa imeshaoza, baada ya masaa kadhaa wanafunzi wanafunzi walipouona umenyauka ndipo wakaelewa kuwa kumbe mti ulikuwa umeshakufa tangu jana Bwana alipoulaani, na sio leo, na ndivyo itakavyokuwa leo kwako na huo ugonjwa ulio ndani yako, usiangalie hali uliyo nayo hapo, amini kwamba tayari kiini cha ugonjwa hakipo…

Sasa kwa ajili ya kuwathibitishia wengine uponyaji wako..Nenda sehemu ambayo unafanyaga check/up ukifika waambie nimekuja kuchukua cheti ya uzima wangu, waambie wakupime na wakupe majibu ili ukatangaze matendo makuu ya Mungu, na watakupa majibu ambayo wao wenyewe watashangaa, yachukue hayo nenda mtaani kwako waonyeshe watu wengine kuwa YESU KRISTO SIO MZIMU YUPO HAI na anatenda kazi zake hadharani.

Nakuombea kwa Mungu, imani yako isitetereke, mwamini Bwana Yesu, fanya kama nilivyokwambia na wewe mwenyewe utashuhudia kwa macho yako matendo makuu ya Mungu. Alifanya kwa wengine, alifanya kwangu, atafanya na kwako, na atafanya kwa wengine kwa kupita ushuhuda wako wewe.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

YESU MPONYAJI WA KWELI.

TUNAYE MWOMBEZI.

ALIFANYIKA SADAKA KWA AJILI YETU!

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.


Rudi Nyumbani

Print this post

NDOA NA HARUSI TAKATIFU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, Mkuu wa Uzima libarikiwe. Karibu tujifunze Neno la Mungu, ikiwa ni mwendelezo wa mafunzo ya ndoa ambapo leo tutajifunza juu ya ndoa takatifu jinsi inavyofungwa ..kwa kufuata misingi ya kimaandiko.

Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa kuna ndoa za aina mbili, kuna ndoa zetu sisi wanadamu, zinazohusu mwanaume na mwanamke, na Pia kuna ndoa ya kimbinguni inayomuhusu Yesu Kristo na Kanisa lake. Na ndoa ni kitu cha kimaandiko kabisa na ni mpango wa Mungu kamili. Na shetani siku zote hapendi ndoa takatifu inayofungishwa na Mungu mwenyewe, kwasababu anajua itamzuilia mambo yake mengi maovu ambayo angeweza kuyafanya kwa mtu husika au jamii kama ndoa isingekuwepo. Na ndio maana biblia inasema katika siku za mwisho “yatatokea mafundisho ya uongo ya kuwazuia watu wasioe” Tutaelewa jambo hili kwa undani zaidi kwa jinsi tunavyoendelea kujifunza.

Tukianza kwa kuzizungumzia kwa ufupi ndoa zetu za kibinadamu; Kwanza ni lazima ziwe na utaratibu, kwasababu Mungu ni wa utaratibu, ndoa ya kwanza ilifungishwa Edeni na Mungu mwenyewe, lakini unaona Mungu alikuwa na utaratibu katika kuifungisha ile ndoa..Tunaona alimwumba kwanza Adamu ambaye ni mwanaume kabla ya Hawa kufunua kuwa mwanamume ndiye kiongozi wa ile ndoa, na kabla hajamwumba Hawa, alimpa Adamu Majukumu ya kuilima na kuitunza Bustani, ili mkewe ajapo akute kila kitu kipo tayari, awe kama ni msaidizi tu, na sio aanze kuteseka nayeye kufanya hivi na vile. Kwahiyo unaona huo ni utaratibu mzuri, kwamba mwanamume akitaka kwenda kuoa ni sharti aandae mazingira ya atakapomweka mke wake na tayari awe ameshajiweka tayari kiakili kwa majukumu yaliyopo mbele yake.

Hivyo baada ya ndoa ya kwanza kufungishwa na Mungu mwenyewe utaratibu ulibadilika haikuwezekana tena ndoa nyingine zinazofuata wanawake watoke kwenye ubavu wa mwanamume, au Mungu atoe maagizo moja kwa moja tena kutoka mbinguni kama hapo kama kwanza, hapana bali ni lazima watu wazaliwe..kwahiyo mwanadamu akapewa jukumu na uwezo wa kutengeneza mwanadamu mwingine kutoka katika tumbo lake na viuno vyake. Hii ikiwa na maana pia azisimamie kwa utaratibu ndoa zote zitakazofuata mbele yake, kwamba zizaliwe kupitia kwenye mikono ya ya watu wa Mungu, kwamba lazima ndoa ihalalishwe mbele za Mungu kwa kupitia watu.

Hivyo huo utaratibu ukaendelea hivyo vizazi na vizazi, mwanamume anapotaka kumwoa mwanamke ni lazima ataratibu ufuatwe, kwanza wazazi washirikishwe, na sheria za Mungu zihusike ndipo hiyo ndo iwe halali. Sio sawa na sio jambo la kimaandiko kabisa watu wawili kuchukuana pasipo utaratibu wowote na kuishi pamoja na kusema wameonganishwa na Mungu, hapo hawajaunganishwa na Mungu bali shetani. Kwasababu Mungu ni Mungu wa utaratibu. Adamu hakumwona Mzazi kwasababu alikuwa hana wazazi, na kadhalika Hawa…Lakini baadaye unaona Mungu anasema “mwanamume atamwacha babaye na mamaye na kuungana na mkewe nao watakuwa mwili mmoja”. Kumwacha pale mzazi sio kumwacha kwa shari bali kwa heri..

Kuna usemi unaosema kuwa Agano la kale hakukuwa na utaratibu wa kuoa..na hivyo watu walikuwa wanajitwalia wake tu! manabii walikuwa wanajitwalia wake, usidanganyike ndugu, utaratibu ulikuwepo. Na leo tutaenda kujifunza huo utaratibu.

Katika desturi za kiyahudi (yaani waisraeli) utaratibu wa ndoa ulikuwa kama ifuatavyo. Kulikuwa na hatua mbili kuu za ndoa, ilikuwa baada ya mwanamume kumpenda mwanamke na kutaka kumwoa, anakwenda kutoa taarifa kwa wazazi wake, na kisha wazazi wake wanakwenda nyumbani kwa mwanamke na kuzungumza na wazazi wa mwanamke, na endapo wazazi wakiridhia hatua nyingine zinafuata.

Hatua ya kwanza ni KUPOSA: Hatua hii inahusisha mwanaume Pamoja na washenga, kutoka kwao na kwenda nyumbani kwa mwanamke, ambapo watatoa mahari, kufanya karamu ndogo, na kikubwa zaidi WATABADILISHANA VIAPO na kuwekeana mkataba kwamba watakuwa waaminifu wote wawili mpaka siku Harusi itakapofungwa. Hivyo baada ya kukamilisha hiyo hatua, mwamume na mwanamke wanakuwa wamefungwa na hicho kiapo, mpaka siku ya Harusi yenyewe itakapofika.

Hapo mwanamume anakuwa huru kurudi kwao, na kuendelea kutengeneza maisha yake, ataendelea kuandaa nyumba ya kumweka mkewe, kama alikuwa hana, na mambo mengine ya muhimu ya kifamilia, na hapaswi kuwa na mahusiano na mwanamke mwingine yeyote, na mwanamke naye ni hivyo hivyo, hapaswi kujihusisha na mahusiano yoyote na mwanamume mwingine, na katika kipindi hichi pia wapendwa hawa wawili hawapaswi kukutana kimwili kabisa (yaani kufanya tendo la ndoa)..Mpaka siku ya harusi itakapofika, ingawa wana ruhusa ya kuitwa mume na mke, Na kipindi hichi cha matengano kinaweza kikadumu kwa miezi kadhaa au hata zaidi ya mwaka, inategemea na hali ya kimaisha ya mwanamume.

Kipindi hichi ndicho kipindi ambacho Mariamu alionekana ana mimba, ya Bwana Yesu Kristo, kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, baada ya kuposwa na Yusufu.

Na hatua ya PILI inayofuata baada ya KUPOSWA Ni Harusi yenyewe. Katika siku hiyo ya arusi, Mwanamume atatoka kwao pamoja na kundi la wanaume wenzake, na ndugu zake wakiume atakwenda kwa matarumbeta na shangwe nyumbani kwa mwanamke, na kisha atamchukua mwanamke na kwenda naye nyumbani kwa mwanamume (kwa Baba wa mwanamume) na kule watakwenda tena kurudia vile VIAPO walivyotoa wakati wa kuposa. Na watakuwepo Marabi ambao watasoma maandiko machache ndani ya TORATI, yanayohusiana na ndoa Na baada ya kufanya hivyo hiyo ndoa inakuwa ni halali na Takatafu na inabarikiwa. Na mfano wa mazungumzo hayo ni huu:

Mwanzo 24: 57 “Wakasema, Na tumwite huyo msichana, tumwulize mwenyewe.

58 Wakamwita Rebeka wakamwuliza, Je! Utakwenda na mtu huyu? Akasema, Nitakwenda.

59 Ndipo wakampeleka Rebeka ndugu yao, na yaya wake, na mtumishi wa Ibrahimu, na watu wake.

60 Wakambarikia Rebeka, wakamwambia, Ndugu yetu, uwe wewe mama wa kumi elfu, mara elfu nyingi, na wazao wako waurithi mlango wa hao wawachukiao.

61 Rebeka akaondoka na vijakazi wake, nao wakapanda juu ya ngamia, wakamfuata yule mtu. Naye huyo mtumishi akamchukua Rebeka akaenda zake”.

Baada ya ndoa hiyo kufungwa, bibiarusi anajitenga na mumewe kwa siri kwa siku saba, ambapo kuanzia hapo wanaruhusiwa kukutana kimwili na kuendelea na mambo mengine.

Huo ndio ulikuwa utaratibu wa ndoa kwa Wayahudi wa agano la Kale, na hakuna mahali popote watu walijitwalia wake kienyeji na kuishi nao, labda tu watu hao wawe si wayahudi.

Sasa Ndoa ya rohoni nayo pia ina utaratibu huo huo.

Bwana Yesu aliacha enzi na Mamlaka mbinguni kwa Baba yake, akalipenda kanisa lake (ambaye ndio mke wake), ubavu wake, akaja duniani ambapo ndio makao ya mke wake yalipo, Na akaliposa kanisa kwa kulitolea mahari, na mahari hiyo ilikuwa ni DAMU yake iliyomwagika pale Kalvari. Na baada ya kulinunua kanisa(ambaye ndio mke wake)..Ilimpasa aondoke arudi nyumbani kwa Baba yake ili kumwandalia mkewe makao, ili baadaye aje kumchukua tena…

Kama ilivyo desturi za wayahudi kwamba ni lazima mwanamume baada ya kuposa aondoke kwa kipindi fulani kwenda kumwandalia mke wake makazi na kisha baadaye aje kumchukua tena kwa shangwe na tarumbeta na nderemo aende kwake, ndivyo Kristo alivyofanya na atakavyofanya, siku atakaporudi mara ya pili kulichukua kanisa lake, naye atarudi kwa parapanda ya Mungu pamoja na kundi la malaika, na kumchukua mkewe kwenda kwenye makao ya Baba yake,(mbinguni) ambapo huko mbinguni kutakuwa na karamu kubwa ambayo haijawahi kutokea..na bibi arusi atakaa na Bwana arusi mbinguni kwa kipindi cha miaka saba, wakati huo duniani kutakuwa na dhiki kuu, na baada ya hiyo miaka saba ya karamu kuisha Bwana Yesu atashuka na kanisa lake, duniani kuja kuitawala dunia na dunia hii itageuka na kuwa mbingu mpya na nchi mpya, wataishi kwa furaha isiyo na kifani milele na milele.

 

Na kama inavyopaswa mwanamke aliyeposwa awe mwaminifu siku zote, wakati mume wake anakwenda kumwandalia makao, ndivyo inavyotupasa na sisi wakristo tunaoishi sasa, wakati tunamngojea Bwana twende mbinguni kwenye karamu tunapaswa kuwa watakatifu na wasafi katika roho zetu, kwa kujiepusha na uzinzi wa kiroho, kama ibada za sanamu, uasherati, ulevi, anasa na mambo mengine yote machafu. Ili ajapo atukute bado ni waaminifu katika lile agano aliloingia nasi pale Kalvari.

Kwahiyo kwa muhtasari huo mfupi unaweza ukaona ndoa iliyo katika utaratibu ni mpango wa Mungu kabisa..kwasababu ndani yake imebeba siri ya Kristo na kanisa lake.

Hivyo katika Ukristo pia, ni lazima hatua za kufunga ndoa zifuatwe, Baada ya mwanamume kumpenda mwanamke, anapaswa awashirikishe wazazi wa pande zote mbili, ili awaache wazazi wake kwa amani, kisha Mahari itolewe kulingana na makubaliano ya pande zote mbili, kama familia ya mwanamke haitaki mahari basi ni sawa, lakini ni lazima wamtoe Binti yao kwa moyo mweupe, Na baada ya mahari mipango ya ndoa inaanza, hapo ni kipindi cha matengenezo inaweza ikawa baada ya wiki,mwezi au hata mwaka inategemea na maamuzi ya upande wa mwanamume, kisha hatua ya mwisho ni kanisani…

Kwaajili ya kubadilishana viapo, sasa viapo vinavyobadilishwa hapa sio viapo vya upumbavu ambavyo biblia imevikataza, kwamba tusiape kabisa, bali viapo vinavyozungumziwa hapa ni viapo vya ahadi, mtu anaahidi kusema ukweli wa moyo wake wote..ambavyo ni lazima mtu aahidi, kuishi na mume wake/mke wake mpaka kifo kitakapowatenganisha, anaahidi kumpenda na kumjali siku zote za maisha yake…viapo hivi ni NADHIRI, na hivyo havina kugeuka nyuma, mtu atakayoyasema kutoka kwenye kinywa chake yanakuwa yanarekodiwa mbinguni, akiyavunja hayo basi atahukumiwa. Baada ya hapo ndipo ndoa hiyo inajulikana mbinguni na kupigwa muhuri.

Lakini ndoa nyingine inayofungwa nje ya utaratibu huo, sio halali mbele za Mungu, wengi hawapendi kuambiwa hivi kwasababu wameshafanya makosa na hawataki kuyarekebisha makosa yao, hivyo wanatetea uovu wao kwa kutumia maneno ambayo hayapo kwenye biblia.

Wewe kama umeishi na mwanamke/mwanamume ambaye mlichukuana tu! pasipo kufuata utaratibu, na ulifanya hivyo kwa kutokujua, ni rahisi tu kujirekebisha, tubu kwa Mungu wako kwa maana yeye anakuhurumia na kukupenda, kisha anza hizo hatua haraka sana, nendeni kwa wazazi wa pande zote, kama huyo mwanamke hana wazazi basi ndugu zake wa karibu,na mwisho kanisani..Mungu atawabariki, lakini kama umesikia na hutaki kutubu kwa kisingizio kuwa ni wapi manabii walifungishwa ndoa..Umekwisha kuusoma hapa utaratibu wa ndoa ulivyokuwa katika agano la kale..kwahiyo siku ile hutasema hukusikia.

Ni maombi yangu kuwa Bwana atakusaidia katika hilo, na pia kama hujampa Bwana maisha yako, nakushauri ufanye hivyo leo, ukubali kujiunganisha na Bwana, Ndoa ya Muhimu na ya msingi ambayo mtu hapaswi kuikosa ni hii ya rohoni (yaani muunganiko wa Kristo na kanisa lake).Kosa hiyo ya mwilini lakini usikose hii ya rohoni, Mpokee leo Kristo na IKUBALI MAHARI YA DAMU YAKE aliyoitoa pale Kalvari, Hakuna mahari kubwa kama hiyo ambayo ilishawahi kutolewa, ni UPENDO WA AJABU SANA, aliouonyesha Bwana, na baada ya hapo ishi katika uaminifu katika hichi kipindi kifupi tunachomngoja arudi, ili atakapokuja tuingie naye karamuni tusifananishwe na wale wanawali wapumbavu ambao Bwana wao alipokuja hawakuwa na mafuta ya ziada na hivyo wakatupwa nje..Hebu kwa kumalizia chukua muda kutafakari mfano huu wa wanawali na ujifunze kitu.

Mathayo 25 : 1-13

“1 Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi.

2 Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara.

3 Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao;

4 bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao.

5 Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.

6 Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.

7 Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.

8 Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.

9 Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.

10 Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.

11 Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.

12 Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi.

13 Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa.”

Bwana akubariki.

Tafadhali “share” ujumbe huu na wengine na Bwana akubariki

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.

UNYAKUO.

ULE MFANO WA WANAWALI 10 (MATHAYO 25), YALE MAFUTA YA ZIADA KATIKA CHUPA ZAO YANAWAKILISHA NINI?


Rudi Nyumbani

Print this post

JE! UNA MHESHIMU MUNGU?

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, Mkuu wa Uzima libarikiwe…Karibu tujifunze Neno la Mungu, na leo kwa Neema zake tutajifunza Maana ya kumheshimu Mungu ni ipi?, Tukijifunza kupitia maandiko matakatifu.

Maana ya kumpa mtu heshima…haina tofauti sana na “kumpandisha mtu hadhi”, Biblia inaposema “waheshimu Baba yako na Mama yako” haina tofauti sana na kusema fanya jambo lolote ambalo likawaletea wazazi wako heshima mbele za Mungu na mbele za jamii inayowazunguka…Kwa kufanya hivyo ni sawa na umewaheshimu wazazi wako.

Kwamfano mtoto anapokuwa ni msafi wa tabia na mwenendo, anasalimia wakubwa, mpole, mtulivu, msikivu, mwelekevu na watu wote wa nje wakamwona..jambo la kwanza watu watakwenda kuwatazama wazazi wake na kuwasifia wazazi kwamba wanajua kumlea mtoto katika maadili, hivyo wazazi wa yule mtoto wanapata heshima kwa kupitia mwanao.Kwahiyo hapo huyo mtoto tayari katimiza amri ya Mungu ya kuwaheshimu mzazi wake, hata kama wazazi wake nyumbani hawajamfundisha hayo maadili.

kadhalika kijana wa kike, anapovaa mavazi ya nusu uchi na anatembea mtaani au barabarani, hata kama kapewa ruhusu ya kuvaa hayo mavazi na wazazi wake mwenyewe lakini bado mbele za Mungu na wanadamu HAJAWAHESHIMU MZAZI WAKE..Ni kwasababu gani?..Ni kwasababu Kwa mavazi yale anasababisha kuwadhalilisha wazazi wake na ndugu zake mbele za watu walio nje na mbele za Mungu. Na hili ndio tatizo kubwa kwa vijana wengi wa kike wanadhani kwasababu tu wazazi wao wanavaa nguo fupi na zaidi ya yote wanapewa ruhusa na wao kuvaa nguo fupi kama za wazazi wao, basi wanadhani mbele za Mungu tayari wanawaheshimu wazazi wao.

Wanaona wazazi wao wanakunywa pombe, na pengine hata wazazi wao wanawaacha na wenyewe wanywe pombe, wanadhani kuwa ndio wanawaheshimu wazazi wao.

Binti usijidanganye kumheshimu mzazi wako sio kumtii tu! bali ni kumpa hadhi kama mzazi, hata kama mzazi wako anakuruhusu au anakuhimiza uvae nguo za nusu uchi, au vimini, au suruali wewe kataa..mwambie Mama/Baba sitaki kukuvunjia heshima kwa kuvaa hizo nguo,.

Na pia kwa kijana wa kiume hata kama mzazi wako anatoboa masikio, au anakuruhusu nawe utoboe masikio, au anafuga rasta au anakunywa pombe hivyo anataka na wewe uwe mlevi kama yeye…wewe usikubali kwani kinyume chake kwa kukataa kwako ndiko utakuwa umemheshimu…ukitii kwa kukubali kuwa mlevi kama yeye, utakuwa hujamheshimu, hivyo kama maandiko yanavyosema “wote wasiowaheshimu wazazi wao watakuwa na siku chache za kuishi duniani”..Na wewe utakuwa ni mmoja wao..Lakini endapo ukakataa na watu wakikuona wewe sio mlevi kama baba yako, hata kama watamdharau baba yako kwa ulevi wake lakini pia kwa sehemu fulani watampa heshima baba yako kwa kulea mtoto mwenye adabu mbele za watu.

Na hivyo wewe kijana utakuwa umempandisha hadhi mzazi wako(umempa heshima yake).N.k Na mambo mengine yote ambayo unaweza kufanya yakampandisha hadhi mzazi wako mbele za Mungu na mbele za wanadamu, ukiyafanya hayo ndio utakuwa umemheshimu mzazi wako na kwa Mungu wa Mbingu na nchi.

pia ni hivyo hivyo, hatumheshimu Mungu wetu kwa KUMPA SHIKAMOO hapana! Mungu haheshimiwi hivyo, Yapo mambo matatu tunayoweza kufanya yakampa Mungu HESHIMA kubwa sana, nayo ni 1) IMANI2)UTAKATIFU…….3)MWONEKANO

Hayo mambo matatu ndio yatakayomfanya Mungu apate heshima kutoka kwetu., Lakini leo hatutazungumzia hayo mawili ya kwanza, bali tutazungumzia hilo moja la mwisho, ambalo ni MWONEKANO, tutaliangalia ni kwa namna gani litampa Mungu heshima.

Mavazi yamekuwa ni tatizo kubwa sana, kwa watu wanaojiita ni watu wa Mungu, hasa hasa kwa wanawake..Utakuta mwanamke hata kwenye Ibada anakwenda na suruali, au kimini, au anakwenda kajipaka uso rangi na mdomoni kaweka kila rangi. Na anaujasiri wote wa kukaa kiti cha mbele kabisa na anapaza sauti yake kwa nguvu akiabudu na kusifu, na ni kila siku anafanya hivyo.

Binti unayesoma haya, nakwambia kwasababu pengine uliambiwa lakini hukuelewa au ulipuuzia…Kwa mwonekano huo HUMWESHIMU MUNGU HATA KIDOGO. Kama tu ni aibu kutembea na Baba yako mzazi njiani ukiwa umevaa hizo nguo, si zaidi KUSIMAMA MBELE YA MUNGU WA MBINGU NA NCHI ukiwa na hizo nguo?..Hebu chukua muda kutafakari hili jambo, usilichukulie kiwepesi tu! Usidhani pale unapokwenda kuabudu hakuna macho ya Mungu, yapo na anaangalia kama tunavyoangalia sisi wanadamu, kwasababu Mungu huyo huyo aliyeuimba roho ndio huyo huyo aliyoumba mwili. Kwahiyo acha kusikiliza Ubeti wa shetani uliotungiwa kuzimu kwamba MUNGU ANAANGALIA ROHO HAANGALII MWILI.

Hebu tujifunze kwenye maandiko kidogo watu waliomheshimu Mungu kwa mwonekano wao.

Yohana 21 : 1-25

“1 Baada ya hayo Yesu alijidhihirisha tena kwa wanafunzi wake, penye bahari ya Tiberia, naye alijidhihirisha hivi.

2 Simoni Petro, na Tomaso aitwaye Pacha, na Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, na wana wa Zebedayo, na wengine wawili wa wanafunzi wake, walikuwapo pamoja.

3 Simoni Petro aliwaambia, Naenda kuvua samaki. Nao wakamwambia, Sisi nasi tutakwenda nawe. Basi wakaondoka, wakapanda chomboni; ila usiku ule hawakupata kitu.

4 Hata asubuhi kulipokucha, Yesu alisimama ufuoni; walakini wanafunzi hawakujua ya kuwa ni Yesu.

5 Basi Yesu akawaambia, Wanangu, mna kitoweo? Wakamjibu, La.

6 Akawaambia, Litupeni jarife upande wa kuume wa chombo, nanyi mtapata. Basi wakatupa; wala sasa hawakuweza kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa samaki.

7 Basi yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akamwambia Petro, Ndiye Bwana. Naye Simoni Petro, aliposikia ya kwamba ni Bwana, akajifunga vazi lake, (maana alikuwa uchi), akajitupa baharini.

8 Na hao wanafunzi wengine wakaja katika mashua; maana hawakuwa mbali na nchi kavu; ila yapata dhiraa mia mbili; huku wakilikokota lile jarife lenye samaki.

9 Basi waliposhuka pwani, wakaona huko moto wa makaa, na juu yake pametiwa samaki, na mkate”.

Ukisoma habari hiyo kwa makini utaona kwamba Petro alikuwa anavua na wenzake akiwa uchi (sasa uchi unaozungumziwa hapo sio uchi kabisa wa kukosa nguo zote, hapana bali ni uchi ambao mtu anakuwa amebakiwa tu na nguo ya ndani). Kutokana na desturi za uvuvi, wavuvi wengi wanapunguza nguo zao wakati wa kuvua ili wawe wepesi wa kuogelea na wanakuwa vile kwasababu wanakuwa wanaenda mbali na makazi ya watu, kwahiyo kwa mwonekano wao hawawezi kuiharibu jamii..

Kwahiyo hapa Petro alikuwa yupo na nguo ya ndani tu, gafla akatokea Bwana ufukweni na hawakumtambua lakini walipomtambua tu! PETRO ALIVAA VAZI LAKE HARAKA NA KISHA AKAJITUPA BAHARINI!.

Hebu tafakari hilo tukio!! Petro huyo ni mwanaume, na akatokea Yesu ambaye pia ni mwanaume kama yeye lakini Petro kwa kumheshimu Bwana akavaa haraka vazi lake, na hata baada ya kuvaa akaona haitoshi, ili kujisitiri zaidi akajitupa kwenye maji. Kwasababu anajua aliyesimama mbele yake ni nani?…alijua kabisa ni zaidi ya mwanadamu ni Mungu, na hivyo mbele zake anapaswa ajisitiri.

Kwa tukio hilo unaweza ukaona kabisa kamwe wanafunzi wa Yesu walikuwa hawajiachii mbele zake, ikiwa na maana kuwa walikuwa wanajisitiri mbele zake kila wakati, walikuwa hata hawadhubutu kubaki kifua wazi mbele zake ingawa wote walikuwa ni wanaume kama yeye.

Sasa kama hawa wanafunzi wa Bwana Yesu walio wanaume walikuwa wanajisitiri hivyo mbele za Bwana, unadhani wale wanawake waliokuwa wanamfuata walikuwaje mbele zake??..unadhani wakina Mariamu Magdalena walikuwa wanavaaje mbele zake, unadhani wangeweza hata kuonyesha vifua vyao mbele yake? walikuwa wanajisitiri kuliko kawaida, pengine hata walikuwa wanaficha wakati mwingine hata nyuso zao mbele zake.

Lakini leo hii unamwambia binti wa Mungu, kwa kumhurumia na kwa upendo, jisitiri unapoingia mbele za Mungu, na sio tu mbele za Mungu bali kila mahali, uendako unamwonyesha na maandiko kuhusiana na yeye kujisitiri (1Timthotheo 2:9)…anakuambia Mungu haangalii mavazi anaangalia roho, Injili ambayo haijulikani ilitoka wapi.

Mwanaume hawezi kwenda kwenye ibada na kaptura, au malapa lazima kuna kitu ndani yake kitamhukumu, na ukiona kaenda na malapa basi ni kweli huyo mtu hana viatu au anamajeraha..Lakini mwanamke ataingia kapaka wanja, lipstick, kapaka uso rangi, kapuliza pafyumu mita 5 mbele watu wanasikia, mgongo wote uko wazi, kavaa sketi fupi ambayo ni aibu kuelezea mfano wake, na ndani hakuna kitu kinamchoma!! Lazima kuna tatizo ndani ya huyo mtu.

1 Samweli 2: 30 “Kwa sababu hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli, asema, Ni kweli, nalisema ya kuwa nyumba yako, na nyumba ya baba yako itakwenda mbele zangu milele; LAKINI SASA BWANA ASEMA, JAMBO HILI NA LIWE MBALI NAMI; KWA MAANA WAO WANAONIHESHIMU NITAWAHESHIMU, NA WAO WANAONIDHARAU WATAHESABIWA KUWA SI KITU”.

Mwanamke unapokwenda kwenye ibada na mwonekano usio wa heshima, jua unakwenda kukutana na Bwana Yesu mwenyewe, unamshushia Yesu Kristo heshima yake, na hivyo na yeye hawezi kukuheshimu ndivyo Neno lake linavyosema, Watu wasio wakristo wanasema dini yenu ni ya namna gani? watu wanamwabudu Mungu uchi. Jina la Mungu linatukanwa kwa ajili yako. Utajikuta unakwenda kujitafutia laana badala ya Baraka..Hata kama hilo kanisa unalokwenda mchungaji wake anawaruhusu wanawake kuvaa hivyo au haongei chochote…wewe usiende kujitafutia laana mbele za Mungu, vaa kwa kujisitiri, vaa nguo za heshima jisitiri mbele za Mfalme Mkuu Yesu Kristo, na mbele za wanadamu Kama Petro aliyeteuliwa na Bwana alijisitiri mbele zake, na alikuwa ni mwanamume alifanya hivyo wewe mwanamke ni nani usifanye hivyo. Vaa nguo yako ndefu, funika kichwa chako, hata watu wasione kifua chako ndivyo utakavyokuwa UMEMHESHIMU MUNGU, na HIVYO MUNGU ATAKUHESHIMU.

Kama wewe umempandisha Mungu hadhi kwa mwonekano wako, na watu wa nje wakamweshimu Mungu wako kwa kupitia wewe, na yeye pia Mungu atakuheshimu, atakupandisha hadhi. Lakini kama ukimshusha na yeye atakushusha.
Kwasababu lolote utakalolifanya liwe baya au jema, Bwana atakulipa hilo hilo.. “alisema mkinionea haya nami nitawaonea haya mbele za Baba yangu, tukimkiri naye atatukiri”.

Ni matumaini yangu kuwa Bwana atakupa macho ya kuyaona hayo ewe mwanaume/mwanamke..kwamba utamheshimu Mungu kwa mwonekano wako ili naye akuheshimu.

Mungu akubariki sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

MAVAZI YAPASAYO NI YAPI?.

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE

WEWE SI MALI YAKO MWENYEWE!

WEWE NI HEKALU LA MUNGU.

TWEKA MPAKA VILINDINI.


Rudi Nyumbani

Print this post

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

Tukiachilia mbali ule waraka wa kwanza ambao Mtume Yohana aliuandika kwa watu wote, zile nyaraka mbili za mwisho zilizosalia hakuzielekezwa kwa watu wote, bali kwa watu husika, na tunaona ndio zimekuwa nyaraka fupi kuliko zote katika biblia nzima, lakini zimebeba ujumbe wa msingi sana, kwa makundi ya watu waliozungumziwa huko..Kwa mfano kama tukiutazama ule waraka wa tatu, tunasoma mtume Yohana aliuelekeza kwa ndugu mmoja anayeitwa GAYO.

Sasa wengi wanaupenda mstari mmoja maarufu sana unaotoka katika kitabu kile unaosema..”MPENZI NAOMBA UFANIKIWE KATIKA MAMBO YOTE NA KUWA NA AFYA YAKO, KAMA VILE ROHO YAKO IFANIKIWAVYO.(3YOHANA 1:2)”..Ni mstari unaopendwa na kila mmoja kwasababu ni mstari unatoa Baraka na mafanikio..Lakini tunashindwa kuelewa kuwa waraka ule haukuandikwa kwa watu wote bali kwa mtu anayeitwa GAYO peke yake ndio aliyeambiwa maneno yale ya baraka, na ni lazima ujue ni kwanini Baraka zile alizistahili yeye na si mwingine kutoka kwa Mungu, na kwa kujifunza kupitia yeye na sisi ndio tunaweza kustahili kupata Baraka kama zile, kwa ufupi kama ukisoma pale utagundua kuwa mtu huyu alikuwa na moyo wa kipekee sana, aliwakaribisha wageni waliokuwa wanasafiri kwa ajili ya kazi ya Mungu, alijitoa kwa ajili ya Bwana kweli kweli, aliwahudumia watumishi wa Mungu waliokwenda kuhubiri nchi za ugenini, kwa hali na mali kiasi cha kwamba hata watumishi hao waliosafirishwa na yeye wakawa hawana mahitaji yoyote kutoka kwa watu wasioamini, Hivyo sifa zake zikavuma katikati ya makanisa yote mpaka kuwafikia mitume..Na ndipo ukija kusoma utaona maneno hayo ya Baraka yanatamkwa mbele yake..

Sasa leo utamwona mtu ni mkristo lakini hata kutoa kitu kidogo kwa Mungu wake anaona shida, na huyo huyo bado ndio wa kwanza kumwambia Mungu, ulisema nifanikiwe katika mambo yote..Hajui kuwa ili Mungu akubariki kwa Baraka kama hizo kuu na nono sio hivi hivi tu..BALI KWA WATU WENYE TABIA KAMA ZA GAYO. Watu ambao hawapo tayari kuona kazi ya Mungu haikwamishwi na kitu chochote.

Vile vile na leo tutaona kwa ufupi juu ya ujumbe ulio katika huu Waraka wa PILI wa Yohana, je! Unamhuhusu nani?. Ni vema ukapata muda wa kuusoma wote peke yako. kwanza ni mfupi na pia itakusaidia tuende pamoja katika uchambuzi huu tunaokwenda kuuangalia..

Tunasoma…

3Yohana 1:1 “Mzee, kwa MAMA MTEULE, na watoto wake niwapendao katika kweli; wala si mimi peke yangu, bali na wote waijuao ile kweli;

Awali ya yote tunaona Hapa mtume Yohana anajitambulisha kama MZEE, na sio kama mtume, au mtumwa wa Kristo, kufikisha ujumbe kama mkomavu, mtu aliyekula chumvi nyingi, anafahamu mambo mengi yahusuyo kanisa na shamba la Mungu kwa ujumla, anayejua jinsi ya kupambanua mitego ya Yule mwovu aliyowahi kuiona katika maisha yake ya kikristo, na jinsi mitego hiyo inavyoweza kunasa makundi mbali mbali ya watu na namna yake, “kijana kwa wazee”, watoto kwa wakubwa, waume kwa wake, n.k.

Hivyo hapa waraka huu tunaona moja kwa moja anaulekeza kwa MAMA MTEULE..Na sio mama tu wa kawaida, Bali anasema mama MTEULE tena pamoja na watoto wake..Hivyo ni wazi kuwa ujumbe huu unawahusu WANAWAKE WOTE, WALE WALIO WATEULE WA KRISTO, ambao wameshaokolewa, ambao walishaoshwa dhambi zao kwa damu ya Yesu Kristo, ambao neema ya Mungu tayari ipo juu yao siku zote, ambao ni watakatifu tena wenye watoto,.

Sasa yapo mambo 3 makuu yalipaswa yazingatiwe au yaonekane katikati wanawake watuelu wa Mungu wa namna hiyo..Na ndio hayo tutayatazama leo katika vipengele vyake. Jambo la kwanza ni..

1) KUWAONGOZA WATOTO KATIKA KWELI:

Kama ukisoma hapo utaona mzee huyu alianza kwanza kwa kuchunguza hali ya watoto wa mama Yule mkristo, katika nyumba yake, na kutamani sana kuona jinsi alivyoweza kuwajali watoto wake au watu wa nyumbani kwake kwa kuhakikisha kuwa wanamcha Mungu, wanadumu katika utakatifu, alitamani kumwona mama huyu jinsi ambavyo angejitoa katika kuangalia hali ya kiroho ya watoto wake kuliko kitu kingine chochote wakifanyacho.. na kama tunavyosoma ni kweli mwanamke huyu mteule alikuwa nacho Tunasoma.

1:1 “Mzee, kwa mama mteule na watoto wake niwapendao katika kweli; wala si mimi peke yangu, bali na wote waijuao ile kweli;

2 kwa ajili ya hiyo kweli ikaayo ndani yetu, nayo itakuwa pamoja nasi hata milele.

3 Neema, na rehema, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo Mwana wa Baba, zitakuwa pamoja nasi katika kweli na upendo.

4 Nalifurahi mno kwa kuwa nimewaona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile tulivyopokea amri kwa Baba”.

Unaona hapo mstari wa 4 anasema.

“4 Nalifurahi mno kwa kuwa nimewaona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile tulivyopokea amri kwa Baba.”

Hivyo ikiwa wewe ni mama, na unataka kuitwa MTEULE wa Kristo, Swali ni je!.unahakikisha watoto wako wanaenenda katika misingi ya kumjua Mungu?, Unawakemea wanapotenda dhambi au unawaangalia tu, je! Unafuatia hali zao za kiroho, au kila wakati upo buzy kufuatilia tu mahudhurio yao ya shuleni na huku mahusiano yao na Mungu yanadorora kila siku. Watoto wako mstari mingapi ya biblia wanaifahamu mpaka sasa, lakini nyimbo za kidunia kila siku unawasikia wakiimba lakini huwasemeshi? Na bado unajiita MAMA MTEULE wa Kristo unayempenda Mungu….Huo sio uteule mama, siku ile hautakuwepo katikati ya wanawake wateule wa Kristo kama wakina SARA na HANA, na wengineo ikiwa utawaona watoto wako wanapotea na wewe huwasemeshi kitu, ikiwa utawaona hawamjui Mungu na wewe hutaki kuwafundisha, unawanunulia kila siku vitabu vipya vya shuleni lakini biblia huwanunulii, unawalipia tution kila siku lakini fellowship na bible study huwapeleki…Huo sio uteule mama…Hali kadhalika na wewe ambaye bado hujawa na watoto, je! Hayo malengo yapo kwenye kichwa chako?

2) KUWA NA UPENDO:

Jambo la pili Mzee huyu alilotamani kuliona katikati ya mwanamke huyu mteule wa Kristo ni UPENDO.

Tunasoma.

“5 Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane.

6 Na huu ndio upendo: tuenende kwa kuzifuata amri zake. Hii ndiyo ile amri, kama mlivyosikia tangu mwanzo kwamba mwenende katika hiyo”.

Unaona hapo? Anasema Hii ndiyo ile amri, kama mlivyosikia tangu mwanzo kwamba mwenende katika hiyo. Sasa Amri hiyo aliyokuwepo tangu mwanzo ni ipi?

Marko 12:29 “Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja;

30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.

31 Na ya pili ndiyo hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.”

Umeona hizo mbili zote alitazamia kuziona kwa mwanamke huyu, ahakikishe kuwa kumpenda Mungu kupo ndani yake siku zote, juu ya kulea watoto katika kweli lakini pia kumcha Mungu kuwepo ndani yake, awe na amani kuwepo uweponi mwa Bwana, awe mwombaji, au msomaji wa Neno.

 

Na pia awapende ndugu, kwa furaha kabisa kama vile biblia isemavyo upendo huvumilia, upendo hauhusudu, upendo haujivuni, upendo hauhesabu mabaya,.

Lakini mwanamke anayesema ameokoka, lakini hana habari na Mungu, hataki kujifunza maneno ya Mungu, hata kusali kwake ni shida, huruma hana, ni msengenyaji wakati wote, hana uvumilivu ndani yake, akiudhiwa kidogo tu, yeye naye anaanza kusengenya. Na suala hili limekuwa hafifu kwa wanawake wengi, na hivyo kimekuwa kikwazo kikubwa sana cha UTEULE WAO pasipo wao kujijua, Hivyo kama wewe ni mwanamke na unajiita mteule fanyia kazi hilo kwa bidii, shindana na usengenyaji huo mpaka uushinde.

3) KUJILINDA NA WADANGANYIFU. 

Hili ndio jambo la tatu na la mwisho mzee huyu mwenye hekima alimwomba mama huyu mteule alizingatie. Hapa anaendelea kusema..

“7 KWA MAANA WADANGANYIFU WENGI WAMETOKEA DUNIANI, wasiokiri ya kuwa Yesu Kristo yuaja katika mwili. Huyo ndiye yule mdanganyifu na mpinga Kristo.

8 Jiangalieni nafsi zenu msiyapoteze mliyoyatenda, BALI MPOKEE THAWABU TIMILIFU.

9 Kila apitaye cheo, wala asidumu katika mafundisho ya Kristo, yeye hana Mungu. Yeyeadumuye katika mafundisho hayo, huyo ana Baba na Mwana pia.

10 Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu.

11 Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu”.

Tazama hapo anasema “KWA MAANA WADANGANYIFU WENGI WAMETOKEA DUNIANI”,…Sasa kumbuka kama wadanganyifu hawa walitokea wakati ule, watatokea na sasa, na pia zingatia jambo hili ili usichanganyikiwe roho ya mpinga-kristo ni ile ile, lakini utendaji wake kazi unabadilika kulingana na nyakati na majira. Wadanganyifu waliokuwepo wakati ule wa mitume walikuwa na kazi moja tu, yaani Kumkana Kristo kuwa hakufufuka..Kwasababu habari ya ukristo ndio kwanza zilikuwa zinaanza kuhubiriwa, Hivyo shetani ili kuuuwa ukristo usiaminiwe na wengi kwa wakati ule, alitumia udanganyifu wa kuwa Kristo hajafufuka, na pia hawezi kurudi katika mwili..Hao ndio walioitwa wapinga-kristo wa wakati ule, na ndio hao Mzee huyu alikuwa anamwonya mama huyu MTEULE ajitenge nao pamoja na mafundisho yao…Kwasababu kwa uzoefu wake wa rohoni Mungu aliompa aliona kuwa wanawake wengi wateule ndio wanaokuwa rahisi kuchuliwa na wimbi hili na wapinga-kristo zaidi ya wanaume wateule,.(sisemi kuwa wanaume hawadanganyiki), hapana bali wengi ni wanawake.

Lakini roho ile ile ya udanganyifu, inatenda kazi hata sasa isipokuwa kwa namna ya ujanja mkubwa zaidi, mpaka kufikia hatua Bwana Yesu kusema wakati huo watawadanganya yamkini hata walio WATEULE…Hivyo roho hii ya udanganyifu haiji tena kwa kusema Yesu hakufufuka, au haikuambii Yesu hatarudi, kwani mpaka sasa shetani anafahamu kuwa hakuna mkristo asiyejua kuwa Kristo alifufuka, na Yesu siku moja atarudi..kila mtu analijua hilo, lakini badala yake anakuja na udanganyifu mwingine nao ndio huu “Kushusha thamani ya wokovu na injili ya YESU KRISTO.”

Kuwafanya watu wasichukulie tena kwa uzito na umakini habari za wokovu, watu wajue kuwa ni kweli Yesu anaokoa lakini maisha yao yasiathiriwe na wokovu huo, anahakikisha kuwa mtu anakuwa vuguvugu, nusu kwa Mungu nusu kwa dunia, injili ya kisasa, injili ya I don’t care, injili ya “haijalishi!”..injili ya kutabiriwa tu mafanikio basi, lakini mambo ya toba yasigusiwe kabisa..Na hali hiyo inawalewesha hata wale ambao walikuwa wamesimama waanze kuwa vuguvugu.

Na roho hii inawakamata sana sana wakina mama, tena hata wale wateule, na ndio maana hapo Mtume Yohana anamwambia. “9 Kila apitaye cheo, wala asidumu katika MAFUNDISHO YA KRISTO, yeye hana Mungu”.

Umeona, njia pekee ya kuwatumbua hao ni kudumu katika mafundisho ya Kristo (Yaani Neno la Mungu)…

Webrania 12: 14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;

Hivyo ikiwa wewe ni mwanamke mteule unayetaka kupokea THAWABU TIMILIFU kama huyu mama, hakikisha unaufanya imara uteule wako kama maandiko yanavyosema, kwa kuzingatia hayo mambo matatu kuwa yapo ndani yako.

2 Petro 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na UTEULE WENU; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe”.

Mungu akubariki. Tafadhali “Share” ujumbe huu kwa wengine. Na Bwana atakubariki zaidi.

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

TWEKA MPAKA VILINDINI.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA TATU WA YOHANA.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU

TOA HUDUMA ILIYO BORA.


Rudi Nyumbani

Print this post

NI NANI ALIYEIDHARAU SIKU YA MAMBO MADOGO?.

Ni nani aliyeidharau siku ya mambo madogo?…Ni swali Bwana alilouliza.

Jina la Bwana Yesu Kristo, libarikiwe, karibu katika kujifunza Neno la Mungu, Leo kwa Neema za Mungu, tutajifunza namna ya  kusimama imara siku ya mambo madogo?.

Najua unajiuliza SIKU YA MAMBO MADOGO NDIO NINI?...Lakini kabla ya kufikia huko kuelezea siku ya mambo madogo, hebu tujikumbushe kidogo historia fupi ya Taifa la Israeli, ambapo kwa kupitia hiyo tutaelewa kwa undani nini maana ya “siku ya mambo madogo”.

Kama wengi wetu tunavyojua Mungu aliwatoa wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri, na kuwaingiza katika nchi ya ahadi, ambapo ndani ya nchi ile aliwaahidia kula mema yote endapo wataishi kwa kuzishika amri zake, na kama ni msomaji mzuri wa biblia utagundua kuwa vipo vizazi vilivyofanya vizuri kwa kwenda katika sheria za Mungu, ambavyo viliishi kwa raha na kwa amani, na vipo pia vizazi vya wana wa Israeli ambavyo havikufanya vizuri, vilikengeuka na kuacha kuyashika maagizo ya Mungu waliyopewa na badala yake  vikapitia vipindi vya tabu sana.

Na utaona pia baada tu ya Israeli kugawanyika na kuwa sehemu mbili yaani YUDA NA ISRAELI …ndio kipindi ambacho wana wa Israeli walipozidi  kukengengeuka kwa viwango vya hali ya juu. Kuanzia kipindi cha Mfalme Yeroboamu mpaka kipindi cha mfalme Hosea wa Israeli kulikuwa hakuna unafuu kabisa, watu waliabudu mabaali na sanamu wazi wazi na kuvukiza uvumba katika sehemu za juu. Na kwasababu ya maasi kuwa mengi, Bwana alituma idadi kubwa sana ya manabii wake katika kipindi hichi kuliko vipindi vyote vilivyotangulia ili kuwaonya wana wa Israeli wageuke na kuacha njia zao mbovu, hivyo kuanzia huo wakati manabii wengi sana walitokea kama wakina Eliya, Elisha, Nathani, Yona, Habakuki,Sefania, Hosea, Mika, Yeremia,Isaya, Obadia, Amosi,Nahumu,Ezekieli,Yoeli,Mika, Zekaria n.k Wote hawa walitokea ndani ya kipindi cha wafalme wa Israeli..Lakini hawakusikia, kinyume chake waliwaua wengine na kuwapiga kwa mawe.

Hivyo maovu yalipozidi hata kufikia kikombe cha ghadhabu ya Mungu kujaa, kukawa hakuna tena kusamehe, Mungu akaahidi kuwa watakwenda utumwani, na Miji yao yote itachomwa moto, na watu wengi sana watauawa kwa upanga, na wengine watakufa kwa njaa, na  wengine kwa Tauni. Na lile hekalu ambalo mfalme Sulemani alilitengeneza kwa gharama nyingi litavunjwa na kuteketezwa kabisa..Na kweli wakati ulipowadia Neno la Bwana lilitimia, Israeli ilichukuliwa utumwani Ashuru na wale waliosalia wa Yusa ,Wakaldayo(yaani watu wa Babeli)..walifika Yerusalemu wakauteketeza mji wao kwa moto, wakalivunja lile hekalu kama Ilivyotabiriwa wakawaua watu wengi kwa upanga; wanawake, kwa watoto na wachache waliobakia waliwachukua utumwani kwenda nao Babeli. Israeli Mji ambao ulipata sifa na kuogopeka na mataifa yote ulimwenguni ukageuka kuwa kama jalala.

Lakini Mungu ni wa rehema aliwaahidi kuwa hawatakaa huko utumwani milele, bali watakaa huko wakimtumikia Mfalme wa Babeli kwa miaka 70 tu! na baada ya hiyo miaka 70 kuisha watarejeshwa tena kwao.

Sasa ndio tunaelekea kwenye kiini cha somo letu, baada tu ya wana wa Israeli kutimiza ile miaka 70, wakiwa Babeli Mungu aliwafungulia mlango wa kurudi tena nchini mwao, lakini waliporudi kule walikuta tayari kuna watu wengine ambao walikuwa wanakaa pale, ambao sio waisraeli, ambao mfalme wa Uajemi aliwaweka wakae kule…Lakini Hao watu walipoona wana wa Israeli wamerudi tena nchini mwao wakaanza kuwapiga vita.

Wakati wana wa Israeli wanapanga kumjengea tena Mungu Hekalu lingine jipya baada ya lile la kwanza kuharibiwa na Mfalme wa Babeli miaka 70 iliyopita, wanakutana tena na changamoto nyingine ya kusumbuliwa…hivyo kwasababu ya hao watu iliwafanya waishiwe nguvu kabisa ya kuijenga tena nyumba ya Mungu, kwasababu pia kwa idadi yao waliorudi Israeli walikuwa ni wachache sana.

Lakini ulipofika wakati Mungu aliwanyanyua manabii wake wawili HAGAI na ZEKARIA kuwatabiria wana wa Israeli kwamba wasimame imara waijenge nyumba ya Mungu wasiogope changamoto zilizopo mbele yao, ijapokuwa hawana fedha wala utajiri lakini Bwana atakuwa nao katika UDOGO WAO. Bwana akamwambia Hagai maneno haya awaambie wana wa Israeli.

Hegai 2: 1 “Katika mwezi wa saba, siku ya ishirini na moja ya mwezi, neno la Bwana lilikuja kwa kinywa cha Hagai nabii, kusema,

2 Sema sasa na Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, liwali wa Yuda, na Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, na hayo mabaki ya watu, ukisema,

3 Miongoni mwenu amebaki nani aliyeiona nyumba hii katika utukufu wake wa kwanza? Nanyi mnaionaje sasa? Je! Mbele ya macho yenu, siyo kama si kitu?

4 Lakini sasa uwe hodari, Ee Zerubabeli, asema Bwana; nawe uwe hodari, Ee Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, nanyi iweni hodari, enyi watu wote wa nchi hii, asema Bwana; MKAFANYE KAZI, kwa kuwa mimi ni pamoja nanyi, asema Bwana wa majeshi;

5 KAMA NENO LILE NILILOAGANA NANYI MLIPOTOKA KATIKA NCHI YA MISRI; NA ROHO YANGU INAKAA KATI YENU; MSIOGOPE.

6 Kwa maana Bwana wa majeshi asema hivi, Mara moja tena, ni kitambo kidogo tu, nami nitazitikisa hizo mbingu, na hii nchi, na bahari, na nchi kavu;

7 nami nitatikisa mataifa yote, na vitu vinavyotamaniwa na mataifa yote vitakuja; nami nitaijaza nyumba hii utukufu, asema Bwana wa majeshi.

8 FEDHA NI MALI YANGU, NA DHAHABU NI MALI YANGU, asema Bwana wa majeshi.

9 Utukufu wa mwisho wa nyumba hii utakuwa mkuu kuliko utukufu wake wa kwanza, asema Bwana wa majeshi; na katika mahali hapa nitawapa amani, asema Bwana wa majeshi”.

Unaona maneno hayo?..Bwana anawatia moyo wana wa Israeli kuwa WASIOGOPE! Utukufu wa hekalu la pili utakuwa mkubwa kuliko utukufu wa lile Hekalu la Kwanza. Hivyo wasonge mbele, wakafanye kazi, wasiangalie umaskini walio nao, wala shida waliyo nayo wasonge mbele kwasababu utukufu wa nyumba ya pili utakuwa ni mkubwa kuliko utukufu wa nyumba ya kwanza, na FEDHA NA DHAHABU NI MALI ya Bwana.. haleluya!! Haleluya!!.

Zaidi ya hayo wakati wana waisraeli wakiongozwa na kiongozi wao aliyeitwa ZERUBABELI wanatazama kuwa kujenga nyumba na uchache wao, na umaskini wao, pamoja na wingi wa maadui uliowazunguka ni jambo lisilowezekana, ni kama mlima mkubwa umewekwa mbele yao halafu uusawazishe kwa beleshi..Lakini jicho la Mungu lilikuwa linaona tofauti..Na ndio Bwana akampa nabii Zekaria maono mengine miezi miwili baada ya yale maono ya Hagai na kusema..

Zekaria 4: 5 “Ndipo malaika aliyesema nami akajibu, akaniambia, Hujui vitu hivi ni nini? Nikasema, La, Bwana wangu.

6 Akajibu akaniambia, akisema, Hili ndilo neno la Bwana kwa Zerubabeli, kusema, SI KWA UWEZO, WALA SI KWA NGUVU, BALI NI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA WA MAJESHI.

7 NANI WEWE, EE MLIMA MKUBWA? MBELE YA ZERUBABELI UTAKUWA NCHI TAMBARARE; NAYE ATALILETA LILE JIWE LA KUWEKWA JUU KABISA PAMOJA NA VIGELEGELE VYA, NEEMA, NEEMA, ILIKALIE.

8 Tena neno la Bwana likanijia, kusema,

9 Mikono yake Zerubabeli imeiweka misingi ya nyumba hii, na mikono yake ndiyo itakayoimaliza; nawe utajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma kwenu

10 MAANA NI NANI ALIYEIDHARAU SIKU YA MAMBO MADOGO? Kwa kuwa watafurahi, nao wataiona timazi katika mkono wa Zerubabeli…..”

Unaona hapo anasema NANI WEWE, EE MLIMA MKUBWA? MBELE YA ZERUBABELI UTAKUWA NCHI TAMBARARE, Mbele ya changamoto zote zinazoonekana kama ni milima, mbele za masihi wa Bwana zitakuwa ni nchi tambarare…na sio kwa uwezo wa Zerubabeli wala kwa nguvu zao bali kwa roho yake Bwana ndio watausawazisha huo mlima.

Na zaidi ya yote Bwana anamwambia Zerubabeli.. “MAANA NI NANI ALIYEIDHARAU SIKU YA MAMBO MADOGO”…

Sasa siku ya mambo madogo ndio ipi?..Ndio hiyo siku ambayo walikuwa hawana chochote, siku ambayo walikuwa wanaona hakuna chochote kinachoweza kufanyika, siku ambayo walikuwa wanaona ndio kwanza mambo bado hata hayajaanza, siku ambazo nguvu zao ni chache, hizo ndio siku za mambo madogo?..Na Bwana anawauliza ni nani anayezidharau siku hizo??…Ni nani anayesema kwamba jambo hilo la kuisimamisha nyumba yenye utukufu mwingi halitafanikiwa?..Ni nani anayesema kuwa katika udhaifu huo hakuna chochote kinachoweza kufanyika?!…sentensi hiyo huwa inamuhuzunisha Mungu sana.

Ndugu somo hili ni la kukutia moyo tu! wewe ambaye upo katika safari ya kwenda mbinguni, kuwa USIIDHARAU SIKU YA MAMBO MADOGO.

Kama ndio kwanza unaanza kumtafuta Mungu, usizidharau siku hizi ambazo unajiona huwezi kuitenda kazi ya Mungu, siku inafika utakayoleta matunda mengi kwa Kristo, endapo hutazimia unachopaswa kufanya ni kuendelea kusonga mbele kwa bidii zote bila kukata tamaa,…Mtaji ulionao moyoni mwako uzalishe, kwasababu ni kama mbegu ndogo, na itakapokuwa itakuletea faida nyingi sana mbeleni. Mwingine aliniambia jana siwezi kumgeukia Mungu kwasasa sina kazi,..ndugu hata ukipata bilioni 100 leo bado utajiona tu hujafika, anza leo na Bwana.

Na pia katika maisha ya kawaida ya kujitafutia riziki, ikiwa wewe ni mkristo na kwanza ndio shughuli  uzifanyazo zinaanza kuchipuka, upo  kama fukara tu! au una mtaji kidogo, au kazi yako ni ya hadhi ya chini sana, na ukiangalia mbele unaona milima mikubwa, hiyo milima isikuogopeshe, ITAKUWA NCHI TAMBARARE…. Usidharau siku ya mambo madogo nenda kakifanyie kazi hicho kidogo, kakizalishe!! Usimvunjie Mungu heshima kwa kutomwamini endelea kutenda haki katika utakatifu wote kwa sababu fedha na dhahabu ni mali yake, mwisho wa siku atakunyanyua tu! kama alivyomnyanyua Zerubabeli na haitakuwa kwa nguvu zako wala kwa uwezo wako bali kwa ROHO WA MUNGU,…NI NANI WEWE UNAYEIDHARAU SIKU YA MAMBO MADOGO! Mungu mwenyewe haidharau wewe ni nani uidharau na mtu mwingine yoyote yeye ni nani hata aidharau siku ya mambo yako madogo!!..Hata kama unauza mchicha usizidharau hizo siku.

Na mwisho kabisa tunaona baada ya Zerubabeli kupata unabii ule kutoka kwa Bwana, kwa vinywa vya Hagai na Zekaria Manabii wa Bwana, alipata nguvu mpya yeye pamoja na Yoshua na wana wa Israeli wote na kwenda kuijenga nyumba ya Mungu, na baada tu ya kutia nia ya kwenda kuijenga nyumba, wakati huo huo vibali vikaanza kufunguka, mara mfalme anatoa amri wapewe ruhusa ya kujenga pasipo kusumbuliwa, mara mfalme anasema wapewe fedha na wasilipishwe kodi yoyote na fursa nyingi na upendeleo mwingi waliupata kutoka kwa watu na mfalme, nyumba ya Mungu ilipatikana na dhahabu nyingi na fedha nyingi, na ikamalizika chini ya mikono ya Zerubabeli salama sawasawa na unabii Bwana alioutoa.

Hivyo ndugu, Bwana ndiye anayenyanyua na ndiye anayeshusha, kama alikushusha chini wakati mwingine ni kwasababu ya maovu yako (ingawa sio kila kushushwa chini ni kwasababu ya maovu, nyingine ni kwa utukufu wa Mungu kama Ayubu), kama ilivyo tu kufanikiwa, sio mafanikio yanatoka kwa Mungu…lakini kama maisha yako yalikuwa hayampendezi Mungu huko nyuma na akakushusha ni kwasababu anakupenda anataka akupe tumaini tena, kama alivyowashusha wana wa Israeli kukaa Babeli miaka 70, na walipotubu aliwarudisha tena katika nchi yao na kuwapa faraja kubwa kama hiyo, na kuwanyanyua tena! Kwanini na wewe asikufanyie hivyo endapo utatubu kabisa kwa kumaanisha kuziacha dhambi zako na kumgeukia yeye. Na kumbuka USITUBU! Kwasababu tu unataka KUPATA UTAJIRI WA ULIMWENGU HUU, tubu kwasababu unataka kwanza kupata UTAJIRI WA ULIMWENGU UNAOKUJA!…..Huo ukiupata hata huu wa ulimwengu hauhitaji kuuhangaikia, Bwana alisema TUTAZIDISHIWA, kuzidishiwa sio kusumbukia, kitu cha kutafuta ni Ufalme wa Mungu, huo ndio tumeambiwa tuutafute kwa bidii zote …“ Mathayo 6:33..utafute kwanza ufalme wake na haki yake, na hayo mengine mtazidishiwa”.

Hivyo Kama hujampa Bwana maisha yako, huu ndio wakati wako wa kufanya hivyo, kabla mlango wa Neema haujafungwa, Roho wa Mungu anataka utii thabiti kutoka ndani ya moyo wako na sio kulazimishwa, anataka utubu kabisa kwa kudhamiria KUACHA, sio KUPUMZIKA, hapana bali kuacha dhambi, unakusudia kuacha kwa vitendo usengenyaji, uasherati, rushwa, utukanaji, ulevi, uvaaji usio na heshima(vimini na suruali kwa wanawake), unakusudia kuacha anasa zote za ulimwengu, na ukisha tubu hatua inayofuata ni ubatizo sahihi, na ubatizo sahihi ni wa maji Mengi na kwa Jina la Yesu Kristo, kulingana na Matendo 2:38, na kisha baada ya ubatizo Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu atakayekusaidia kushinda dhambi. Na hapo utakuwa umezaliwa mara ya pili kwa maji na kwa Roho.

Mungu akubariki sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

SHETANI ANATOLEA WAPI FEDHA, ANGALI TUNAJUA FEDHA NA DHAHABU NI MALI YA BWANA?.

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

JE! KUBET NI DHAMBI?


Rudi Nyumbani

Print this post

IMANI “MAMA” NI IPI?

Moja ya somo pana sana katika biblia ni somo lihusulo IMANI. Imani ni kama Elimu, kama vile watu wasemavyo Elimu haina mwisho hali kadhalika Elimu ya IMANI nayo haina mwisho.

Watu wawili wanaweza wakasema ni wasomi, wamehitimu pamoja, wamepokea shahada kwa pamoja wakajulikana na serikali kama ni watu wasomi wazuri wenye manufaa makubwa katika nchi lakini unajua kuwa mmoja anaweza akawa ni mjinga kwa mwingine sawasawa tu na mtu Yule ambaye hajakwenda shule kabisa, Unauliza ni kivipi?.

Jaribu kufikiria mmoja alipomaliza elimu ya msingi alikwenda kusomea masomo ya urubani, na yule mwingine akaenda kusomea udaktari..sasa na elimu zao embu jaribu kumchukua Yule daktari umpe ndege aendeshe abiria, au umpeleke Yule rubani kwenye chumba cha upasuaji kwa vichwa vya wanadamu awatibu wagonjwa..wewe Unadhani ni jambo gani hapo litatokea?..Ni maafa makubwa sana..Sasa tukiwahukumu hawa wote kwa kutazama maafa yaliyotokea na kusema kuwa ni wajinga, tutakuwa hatujatathmini uhalisia wa mambo….Ukweli ni kwamba Yule daktari ni msomi lakini ni msomi aliyebobea katika mambo ya udaktari hivyo masuala ya Jeografia kwake ni kama maruweruwe, hali kadhalika na yule Rubani.

Na ndivyo ilivyo hata katika mambo ya Imani.. Imani haina mchipuko mmoja kama wengi wadhanivyo, Sio kila imani mtu aliyonayo ndani yake itatenda miujiza, sio kila imani mtu aliyonayo itamwokoa hali kadhalika si imani yoyote tu mtu aliyonayo ITAMPENDEZA MUNGU, vile vile sio kila imani itakuja kwa kulisikia Neno la Mungu, ukiyafahamu hayo vizuri itakujengea ufahamu mzuri wa kupima kiwango chako cha Imani kilipo…. Leo kwa neema za Bwana tutatazama kwa ufupi baadhi ya vipengele hivi vya imani, na kisha tutaangalia ni IMANI ya aina gani, ambayo Mungu anaiona kama ni kiini cha mkristo anapaswa awe nayo.

Embu tuchambue mojawapo ambayo tuliiona ikijitokeza kwa mtu fulani kipindi kile cha Bwana Yesu..Tunasoma:

Luka 7:1 Alipokwisha kuyamaliza maneno yake yote masikioni mwa watu, aliingia Kapernaumu.

2 Na mtumwa wake akida mmoja alikuwa hawezi, karibu na kufa; naye ni mtu aliyempenda sana.

3 Aliposikia habari za Yesu, alituma wazee wa Wayahudi kwake kumwomba aje amponye mtumwa wake.

4 Nao walipofika kwa Yesu, walimsihi sana wakisema, Amestahili huyu umtendee neno hili;

5 maana, analipenda taifa letu, naye alitujengea sinagogi.

6 Basi Yesu akaenda pamoja nao. Hata alipokuwa si mbali na nyumba yake, yule akida alituma rafiki kwake, akamwambia, Bwana, usijisumbue, maana mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu;

7 kwa hiyo nilijiona sistahili mwenyewe kuja kwako; lakini, sema neno tu, na mtumwa wangu atapona.

8 Kwa maana mimi nami ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, mwenye askari chini yangu; nikimwambia huyu, Nenda, huenda; na huyu, Njoo, huja; na mtumwa wangu, Fanya hivi, hufanya.

9 Yesu aliposikia hayo alimstaajabia, akaugeukia mkutano uliokuwa ukimfuata, akasema, Nawaambia, hata katika Israeli sijaona imani kubwa namna hii.

10 Na wale waliotumwa waliporudi nyumbani, wakamkuta yule mtumwa ni mzima”.

Sasa huyu Akida kumbuka hakuwa myahudi, wala hakuijua torati kama wayahudi wenyewe walivyokuwa, kwanza kwa wakati ule ilikuwa ni mwiko wayahudi kuchangamana na watu wa mataifa. Mtu huyu alikuwa ni akida wa kirumi, aliye chini ya utawala wa Kaisari, lakini alikuwa ni mkarimu sana tofauti na maakida wengine waliowekwa kuilinda Israeli,, aliwapenda wayahudi na kuwatendea mema, mpaka kufikia hatua ya kuwajengea Sinagogi, Lakini ikatokea siku moja mtumwa wake aliyempenda sana akaugua karibu na kufa, hivyo akahitaji uponyaji kutoka kwa Yesu, na wayahudi waposikia wakaenda kumwombea kwa Yesu ili aende kumponya. kama tunavyosoma habari ile Bwana akiwa njiani tu yule akida alipata taarifa kuwa YESU anakuja kwake, hivyo akatuma haraka haraka watu kwake na kumwambia atamke Neno tu, na mtumwa wake naye atapona…

Sasa jambo la kutazama hapo, si kawaida mtu kuwa na imani kubwa kiasi kile kama hajaipata kutoka mahali fulani..Imani haiwezi kuja kama haina chanzo..Lakini kumbuka biblia inatuambia Imani chanzo chake ni kusikia na kusikia huja kwa Neno la Kristo.. Lakini huyu mtu hakuwa mkristo, wala hakuwa myahudi, bali mrumi..basi imani kubwa kama ile mpaka YESU kusema hajaiona hata kwa wayahudi, hata kwa kwa makuhani, hata kwa mitume, hata kwa marabi, yeye aliitolea wapi?.

Siri ipo pale pale kwenye maandiko tukisoma mbele kidogo utaona anamwambia Bwana “Kwa maana mimi nami ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, mwenye askari chini yangu; nikimwambia huyu, Nenda, huenda; na huyu, Njoo, huja; na mtumwa wangu, Fanya hivi, hufanya.”

Unaona hapo?, Yeye alitumia experience (au Uzoefu) wa maisha yake kumwesabia Mungu kuwa ni muweza..Yeye mwenyewe alijiona katika hali aliyopo, anao wakuu wengi juu yake ambao wakati wowote wakimwambia fanya hivi hufanya, tenda hili hutenda, hali kadhalika anao watumwa wengi chini yake akiwaamrisha fanya hivi hufanya tenda lile hutenda pasipo hata yeye kuwepo mahali husika na jambo lile hutendeka vile vile kama alivyotoa yale maagizo pasipo kuongezwa wala kupunguza..

Kwahiyo akasema huyu ni YESU naye ni MKUU kuliko sisi wote, mambo yale yale niliyoonyesha kwa watumwa wangu, au niliyoonyeshwa kwa wakuu wangu waliyafanyika bila kasoro yoyote pasipo sisi kuwepo, atashindwaje huyu kutoa tu maagizo na uponyaji kutokea, Kuliko kuja kujitaabisha huku?..Na ndio hapo akawambia Bwana aseme Neno tu!…Hapo hapo Akapokea alichokuwa anakitafuta!!.Haleluya.

Ndugu Imani yoyote ya kupokea chochote kwa Mungu, iwe ni uponyaji, au mahitaji, au mafanikio, au kutendewa miujiza, au kutenda miujiza, hiyo haitegemei Ile IMANI inayozungumziwa katika Warumi 10:17 “(Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.”)..hapana hii Inategemea ni jinsi gani wewe unavyomwelewa Mungu na kumchukulia hata katika hatua ya maisha inayopitia sasa, kwa kutazama tu mazingira yanayokuzunguka, au unayoyaishi unaweza ukaumba mambo makubwa mpaka dunia ikashangaa.

Itafakari tena ile habari ya Yule mwanamke aliyemwendea Yesu ambaye hakuwa myahudi kabisa, alitokea huko Tiro ambapo kwa sasa ni Nchi ya Lebanoni, lakini alipomwendea Yesu ili amponywe binti yake, Bwana alimwambia si vema kutwaa chakula cha watoto na kuwapa mbwa, lakini Yule mwanamke akamwambia Bwana hata mbwa hula makombo yanayondoka mezani pa watoto,.Ndipo Bwana akamwambia mama imani yako ni kubwa na iwe kwako kama utakavyo..(Marko 7:27)

Unaona huyu naye hakusoma mahali popote kwenye maandiko mpaka, awe na imani kubwa kama ile, kiasi cha Bwana kumwambia, Wote hawa wanatumia (uzoefu wao) wa maisha na kumuhesabia Mungu kuwa anaweza pia , na hivyo wanapata majibu ya maombi yao kwa Mungu.

Hata na wewe unaweza kupata lolote kwa Imani ya namna hiyo, uponyaji, kutoa pepo, na vitu vingine kama, gari, nyumba, mafanikio, kuamrisha vitu navyo vikatokea, n.k. na kwa jinsi utakavyoamini sana kwa kumchukulia Mungu kuwa anaweza ndivyo utakavyopokea zaidi. lakini fahamu kuwa Imani ya dizaini hiyo hata kama itafikia hatua ya kuweza kuhamisha milima bado uwezekano wa kwenda Jehanum ya moto ukawa ni mkubwa kwako kama hutafahamu shabaha ya Imani ambayo Mungu anataka kuiona kwa mtu.

Imani hii haiwezi ikakupa faraja, imani hii haiwezi ikakupa tumaini, imani hii haiwezi ikakupa uzima wa milele imani hii haiwezi ikakupa tumaini, Imani hii haiwezi ikakupa MAFUNUO kutoka kwa Mungu…Wengi leo wanaikimbilia hii ambayo kimsingi ni nzuri lakini wanasahau kiini cha imani mama impasayo kila mtu awe nayo kwa mambo yote.

IMANI MAMA NI IPI?

Warumi 10:17 “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa NENO LA KRISTO”.

Sasa nataka ufahamu kuwa ipo imani inajengeka ndani ya mtu si kwa uzoefu fulani hapana, kama alioupata yule akida aliyeponyewa mtumwa wake au aliyoipata yule mama wa Tiro aliyeponyewa binti wake, bali ni kwa kulisikia Neno la Kristo tu, Kumfahamu Kristo tu kwa mapana yake na marefu yake basi, hii ni Imani timilifu katika Neno la Kristo. Si wengi wanayo, na hii haifikiwi hivi hivi labda kwa kusali sana, au kwa kufunga sana, hapana bali inafikiwa kwa kumjua sana Kristo tu katika Neno lake..Tunaposema kufahamu Neno la Mungu hatumaanishi kukariri vifungu vya biblia tu hapana, bali ni kupata ufunuo wa Yesu Kristo ni nani katika maisha yako, na hiyo inakuja kwa kumtafakari sana Bwana Yesu, na kumjua yeye kwa upana wake na urefu wake kwa maana biblia inasema katika “Wakolosai 1:19.. Kwa kuwa katika yeye ilipendeza UTIMILIFU wote ukae;

Sehemu nyingine biblia inasema katika Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia UMOJA WA “IMANI” NA KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo; ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu”.

Shetani hapendi kabisa watu watafute IMANI ya NAMNA HII,..Hapendi kabisa watu wapoteze muda mwingi kufundishwa habari za YESU, bali za mafanikio na uponyaji tu kila wakati..Kwani anajua watu imani yako ikishajengwa katika ufunuo wa kumjua YESU KRISTO ni nani kwao? Basi watamsumbua sana yeye na kuleta madhara makubwa katika ulimwengu kwa roho. Kwahiyo hapendi watu wamjue sana Yesu Kristo, hababaiki watu wawe hata na imani ya kuhamisha mlima, hiyo haimbabaishi inaogopa sana mtu mwenye Imani iliyojengwa katika kumjua Yesu Kristo, nguvu za kufufuka kwake.

Jiulize ni kwanini utakuta mtu ameshakuwa ni mkristo kwa muda mrefu lakini leo hii hana hata Amani katika maisha yake, jiulize ni kwanini hana furaha, ni kwanini anaona kama vile Mungu hamsikii, ni kwanini anayo hofu ya kufa, kwanini anayumbishwa na mafundisho ya uongo, kwanini kila siku ni mchanga kiroho, kwanini hapokei mafunuo yoyote kutoka kwa Mungu, kwanini anawaogopa wachawi? Ni kwanini hata ujasiri kwa Mungu wake hana, na bado ni mkristo wa muda mrefu…

Hajui kuwa tatizo lipo hapo, Imani yake haijajengwa katika misingi ya kumjua YESU KRISTO bali katika misingi mingine..Amekuwa hataki kufundishwa habari za msalaba, yeye anataka tu, atabiriwe ndoa yake, atakata tu aombewe juu ya uponyaji wake, anataka tu aombewe biashara yake, anataka tu afundishe mafundisho laini laini, ya kubembeleza, ya faraja, mafupi, na ya kuchekesha,..Sasa ile Imani inayozungumziwa na Mungu mtu wa dizaini hii asitazamie kama ataipata.

Ndugu tafuta kumjua Yesu na uweza wake, weka uhusiano wako sawa na YESU maishani mwako, jishughulishe sana kumtafuta kwa kumchunguza, na kwa kusoma habari zake zote, na kwa kumtafiti sana, huko huko ndiko utakapopata ufunuo wa kumjua YEYE ni nani kwako. Zipo faida nyingi, na mojawapo ni kuwa wewe utayapata yote utakayotaka, ya mwilini na ya rohoni, ukimwomba Baba vya mwilini atakupa kwasababu tayari utakuwa ameshakuonyesha njia ya kuvipata, halikadhalika rohoni utakuwa ni amani, furaha, utulivu, tumaini, ujasiri,faraja na maji ya mito ya uzima kuyatakuwa yanatiririka moyoni mwako. Kwasababu Imani yako imejengwa katika misingi ya kumjua YESU KRISTO. Umeshapata ufunuo wa Yesu Kristo ni nani kwako, Hivyo shetani hawezi kukusumbua tena. Yesu Kristo ndio siri ya Mungu iliyotabiriwa itafunuliwa katika siku za mwisho, Unabii wote wa biblia unamuhusu yeye, na ushuhuda wake ndio roho ya Unabii (Ufunuo 19:10).

Ndugu ikiwa bado unasua sua katika imani, huu ni wakati wa kuweka mambo yako sawa, Tubu, anza mwanzo mpya na Bwana, badili mfumo wako wa maisha kwa ujumla na wa kumwendea Mungu, angalia Imani yako unaijenga katika Nyanja ipi? Kumbuka hilo eneo la IMANI ni pana kama ilivyo Elimu…Hivyo chaguo ni lako Ni matumaini yangu kuwa sote tutachagua kujenga katika misingi ya Neno lake ili tupate vyote.

Ubarikiwe sana. Tafadhali “Share” ujumbe huu na wengine, na Bwana atakubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

IMANI NI KAMA MOTO.

JE! NI SAHIHI KWA MKRISTO KUOA/KUOLEWA NA MTU WA IMANI NYINGINE?

JE! NI LAZIMA WATU WOTE WANENE KWA LUGHA?

IMANI YENYE MATENDO;

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?


Rudi Nyumbani

Print this post

UTENDAJI KAZI WA MPINGA-KRISTO.

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, natumai u mzima, karibu tushiriki pamoja maneno ya uzima, leo tutazungumzia juu ya ujio wa mpinga-kristo.

Mpaka sasa dunia inatazamia ujio wa watu wawili huko mbeleni kabla ya mambo yote kuisha, wa kwanza ni KRISTO na wa pili ni MPINGA-KRISTO. Na kila mmoja amekuwa akitazamiwa na watu na bado anaendelea kutazamiwa. Lakini kuna mahali ambapo watu wengi wanakosa shabaha hususani katika namna ya kumtambua mpinga-kristo na utendaji kazi wake. Tambua kuwa njia pekee ya kumjua shetani ni kumfahamu Mungu tu, hakuna njia ya mkato, huwezi kusema unamjua vizuri shetani na huku hata mahusiano yako na Mungu ni mabovu, Neno la Mungu halipo ndani yako Roho wa Mungu yupo mbali na wewe, hapo ni sawa na unajidanganya tu hata kama utasema wewe unamjua shetani namna gani, na ndio hapo utamwona mtu anaishia kudhani shetani ni freemason aliyekaa kuzimu anawatajirisha watu na kuwaambia watoe kafara za watu ili awape utajiri, na kusababisha ajali, na mambo mabaya hilo tu,.na utakuta mtu huyo anapoteza muda wake mwingi kuchunguza ishara na alama kila mahali, na kwenye vibao, vya kichawi ili kujiepusha navyo, utakuta anafahamu alama zote wazitumiazo wachawi. Na kwa hilo anajisifu kuwa anamfahamu shetani, lakini hafahamu kuwa hivyo ndivyo shetani anavyotaka afikirie siku zote, apoteze muda mwingi kuwafahamu wachawi na vikundi vyao, lakini asidhubutu hata kidogo kumfahamu Kristo na Neno lake.

Ndugu usipoifahamu noti original utawezaje kuitambua noti feki, watu wengi wanafikiria kuwa Mpinga-kristo atakuja kuwa ni mtu wa ajabu na wa tofauti, mtu katili sana, mtu ambaye ulimwengu mzima utakwenda mbele yake na kumsujudia na mtu yeyote asipomsujudia atauawa kama kuku, mtu ambaye atawalazimisha watu kwa nguvu wapokee chapa na endapo mtu asipopokea atachinjwa hadharani bila huruma yoyote, atakuwa mtu mkali kupindukia, atakuwa anakunywa damu za watu hadharani n.k..Hivyo hiyo inawafanya watu wastarehe wadhani kuwa bado muda mrefu sana, mpaka atokee mtu wa namna hiyo, bado hajaanza kutenda kazi na siku atakapoanza tutajua…

Lakini turudi katika upande wa pili..watu vivyo hivyo wanadhani YESU yupo mbinguni ametulia , na yeye ipo siku moja atakuja, na siku atakayokuja makaburi yatafunguka na watu wote watawaona wafu wakifufuka, atasimama mawinguni, parapanda italia, malaika wataonekana kila pande, hivyo kwasasa bado unyakuo haujaanza siku utakapotekea siku ndiyo tutakapojua.

Kitu ambacho hatukifahamu mpaka sasa ni kwamba Kristo anakuja katika roho na anawanyakua watu wake mbali na watu waovu, Bwana Yesu hajakaa katika kiti fulani huko mbinguni mpaka sasa miaka elfu mbili imepita akisubiria tu siku moja ifike aje kuwachukua wateule wake, hapana badala yake tangu kuondoka kwake amekuwa na AGENDA, na bado anatenda kazi, na agenda hiyo imekuwa akifanyia kazi kizazi baada ya kizazi, amekuwa akizungumza na watu wake katika kipindi kimoja cha kanisa hadi kingine, vipindi hivyo tunaviona katika kitabu cha ufunuo 2&3. Kila nyakati amekuwa akilinyakua kanisa lake na kulihadhi mahali fulani, hata sasa bado anaendelea kuwanyakua watu wake na kuwahifadhi, na kama utakufa na ule mwisho bado haujakukuta unahifadhiwa mahali fulani ukingojea siku ya kujumuika na wengine watakao kuwa hai na kwenda nao mbinguni.

1Wathesalonike 4.13 “Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.

14 Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.

15 Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.

16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele”.

Unaona hapo siku ile unyakuo haimuhusu tu yule atakayekutwa hai hapana bali inawahusu na wale wengine ambao walishakufa wakiwa wanatembea katika mstari wa Kristo kabla ya hapo.

Lakini vigezo vya kunyakuliwa vipo wazi, ni hicho si kingine zaidi ya alama utakayotiwa, au Chapa au Muhuri uliojuu yako..Na muhuri wenyewe si mwingine zaidi ya ROHO MTAKATIFU. Pasipo huo muhuri huwezi Kunyakuliwa ndugu..aidha iwe hai au uwe umekufa..

Waefeso 4.30 “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; AMBAYE KWA YEYE MLITIWA MUHURI HATA SIKU YA UKOMBOZI”.

Hali kadhalika na kwa mpinga-kristo, hangojewi eti mpaka kipindi fulani kitakapofika ndio adhihirishe kazi zake, ni kweli kwasasa hajatokea lakini biblia ipo wazi kabisa kuwa utendaji kazi wake upo tangu zamani na ile roho inazidi kuendelea kufanya kazi hata sasa,..na kama vile Bwana alivyokuwa na Muhuri au chapa yake, Halikadhalika ibilisi naye anayo chapa yake au Muhuri wake,.Na chapa hiyo ni KU-MPINGA-KRISTO, na mtu anampingaje Kristo? Ni kwa kumkataa Roho Mtakatifu ndani yake..Kuupinga wokovu ndani ya moyo wako..Kuzipinga-kazi za Mungu ndani ya moyo wako…Kwenda kinyume na njia za Bwana, kukaidi maagizo ya Mungu kama shetani mwenyewe alivyo. Kuutua msalaba, kulikosoa Neno la Mungu, kuipuuzia injili na kuona kama ni hadithi za kizee, kuwatukana watu wote wanaoutumainia msalaba. N.k. sasa mtu ukishajiona upo katika hali hiyo basi ujue tayari ulishapokea chapa ya mnyama..Hivyo mtu yeyote atakayekufa leo katika hali hiyo yeye naye atahifadhiwa mahali pa mateso panapoitwa, akisubiria siku ya kukamilishwa kwa wapinga-Kristo wenzake, na kwa pamoja wote wataungana na kwenda kuhukumiwa kwa kupokea chapa ya mnyama, na wote kwa pamoja watatupwa katika lile ziwa la moto.

1Yohana 2: 18 “Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo YUAJA, HATA SASA WAPINGA KRISTO WENGI WAMEKWISHA KUWAPO. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho.

2Wathesalonike 2:5 “Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?

6 Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.

7 MAANA ILE SIRI YA KUASI HIVI SASA INATENDA KAZI; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.

8 Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake;

9 yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo;

10 na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa”.

Hivyo usidanganyike kuwa ukifa sasa bila kuufika wakati wa mpinga-kristo umeotea, kwamba umeikwepa chapa yake..fahamu kuwa chapa inapigwa hata sasa, na jua kuwa chapa ile ipo katika roho na si mwili kama vile biblia inavyosema wale watakaokutwa hai wakati wa Bwana hawatawatangulia wale waliokufa siku ile ya unyakuo..Hali kadhalika wale watakaopokea chapa ya mnyama wakati ule wa dhiki kuu, hawatawatangulia wale waliokwisha kuipokea zamani kabla ya dhiki kufika;..Watakaosalia katika ile siku ya dhiki kuu, kwa kupitia kitambulisho cha dini na udhehebu wataithibitisha chapa ya mnyama ambayo tayari imo katika roho zao.

Pia biblia inatueleza kuwa Bwana alikuja, akaondoka, na atarudi tena, halikadhalika na yule mnyama biblia inasema, alikuwako, naye hayuko naye yu tayari kupanda kutoka kuzimu na kwenda kwenye uharibifu..Hii inatuweka wazi kuwa kazi zilishaanza zamani sambamba na za Bwana wetu Yesu Kristo.

Ufunuo 17:8 “Yule mnyama uliyemwona alikuwako, naye hayuko, naye yu tayari kupanda kutoka kuzimu na kwenda kwenye uharibifu. Na hao wakaao juu ya nchi, wasioandikwa majina yao katika kitabu cha uzima tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, watastaajabu wamwonapo yule mnyama, ya kwamba alikuwako, naye hayuko, naye atakuwako”.

Unaona?, Sasa ni vizuri kufahamu pia Mpinga-Kristo mwenyewe atatokea wapi..Biblia inatueleza atatokea RUMI, katika ule utawala wa mwisho kabisa wa chuma..VATICAN ndiyo yatakayokuwa makao yake makuu, katika kiti cha KI-PAPA…Mpinga-Kristo hatashika bunduki, wala visu, anashika biblia, na anahubiri..lakini injili yake ni ya uongo.

Kwanini usifanye uamuzi sasa wa kumgeukia muumba wako?, hatari uliyonayo ni kubwa kama hutageuka sasa, mambo yote yanakaribia kuisha, ukifa leo katika dhambi huko utaenda kuwa mgeni wa nani. Tafakari hilo, usiishi tu ilimradi siku zinapita, Neema inapatikana bure, uamuzi ni wako, Ni matumaini yangu utatubu leo na kumgeukia muumba wako angali muda upo, saa zaja utakazotamani huu wakati wa sasa lakini utaukosa.

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

CHAPA YA MNYAMA

MPINGA-KRISTO NI NANI?

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

UFUNUO: Mlango wa 13

UFUNUO: Mlango wa 17


Rudi Nyumbani

Print this post