Ndugu, kosa kila kitu, kosa mali, kosa mtoto, kosa uzuri, kosa hata marafiki,potoza hata chochote unachokiona kina thamani, lakini usifikirie hata siku moja kuikosa karamu hiyo, kwasababu mahali popote biblia inapoizunguzia karamu hii inatumia neno HERI..Biblia haina maneno ya kujitosheleza kuelezea maana ya hili Neno heri, yaani tunawezeka kusema, amebahatika sana, au amebarikiwa sana, amependwa bure, yeye atakayepata neema ya kualikwa kwenye karamu hiyo, kwasababu wengi wanaojulikana kama wakristo wataikosa.