Title August 2020

HUDUMA YA WALE MASHAHIDI WAWILI.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, libarikiwe. Nakukaribisha katika kuyatafakari maandiko.

Tunajua kuja kwa Yesu mara ya kwanza, kulibeba siri nyingi za kuja kwake mara ya pili, kwa mfano wakati ule kabla ya Herode, kutaka kumuua Yesu pindi alipozaliwa, kulitangulia kwanza sensa kubwa kwa watu wote wa ulimwengu, ambayo ilimlazimu kila mmoja aende kwenye mji wake aliozaliwa ili ahesabiwe huko..Na ndivyo itakavyokuja kuwa kipindi kifupi kabla ya Yesu kurudi mara ya pili duniani, mpinga-Kristo ataleta utaratibu mpya wa watu wote kuhakikiwa, mfumo huu mpya ndio ile  inayojulikana kama chapa ya Mnyama ambao utamlazimu kila mmoja awe nayo, kama mtu hana basi hataweza kuuza au kununua au kufanya biashara, au kuajiriwa mahali popote..kwa urefu wa somo hilo tutumie ujumbe inbox tukutumie ..

Lakini pia kulikuwa na jambo lingine, ambalo lilichochea kwa haraka sana dhiki kutokea pale Yerusalemu pindi tu Yesu alipozaliwa. Na jambo lenyewe, lilikuwa kwa wale Mamajusi kutoka Mashariki.

Sasa ukiangalia pale, utagundua habari ya kuzaliwa kwa Yesu ilikuwa imeshajulikana hata kabla ya baadha ya watu pale Israeli kujua, utaona kulikuwa na wale wachungaji kule makondeni waliotokewa na malaika na kuambiwa wamfuate mtoto..Ni kweli walienda na kushuhudia waliyoambiwa, na pengine baaada ya pale walisambaza taarifa za kuzaliwa kwa watu wengi vijijini na mijini, lakini habari zao hazikuwa na nguvu sana, wala hazikuleta mabadiliko yoyote kwa Israeli au kwa Herode, Vivyo hivyo, walikuwepo wakina Simoni na Hana, ambao Mungu aliwashuhudia kuwa huyu ndiye mwokozi na mfalme, pengine nao walitangaza, lakini taarifa zao pia hazikufika mbali  sana.

Walikuwepo wakina Zekaria kuhani na mke wake Elisabeti, ambao walitangaza habari za Yesu na Yohana, ambazo kwa habari ya Yohana biblia inasema zilijulikana katika mji wote ule lakini bado hazikuwa na mashiko sana..Lakini tunaona kulikuwa na kundi lingine la watu, toka mbali sana, lililoleta habari,..Hilo halikuwa la watu  wa pale Israeli, bali lilitoka mbali sana, ndio wale mamajusi wa Mashariki, walioina nyota yake na kufunga safari mpaka Israeli, na walipofika moja kwa moja wakamuuliza  mfalme Herode, yupo wapi mfalme wa Wayahudi aliyezaliwa..Sasa kwa taarifa hizo Biblia inatuambia sio tu Herode zilimfadhaisha, bali na Israeli nzima. Hapo ndipo pakawa mwanzo wa sura nyingine kwa taifa la Israeli.

Mathayo 2:1 “Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema,

2 Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.

3 Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye.

4 Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi”?

Sasa kama tunavyoijua habari kilichofuata pale ni Herode kwenda kuwaua watoto wote waliokuwa Bethlehemu wakati ule (kukawa na kilio kikuu Bethlehemu).

Mathayo 2:18 “Sauti ilisikiwa Rama, Kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake, Asikubali kufarijiwa, kwa kuwa hawako”.

 Lakini kabla ya kuwaua, Mama na mtoto walihamishwa, na kupelekwa Misri kuikwepa dhiki.

Sasa, katika siku za mwisho, mambo kama hayo hayo yataenda kujirudia,. Baada ya Unyakuo kupita, dunia itakuwa imebakiwa na miaka 7 tu mpaka iishe kabisa, katika kipindi hicho, Mungu atawanyanyua watu watu wawili ambao watawatenga kwa lengo moja tu, la kwenda kuwatolea Unabii Israeli, juu ya kurudi kwa Kristo ulimwenguni kutawala kama mfalme wa wafalme…ndio mfano wa wale mamajusi wa Mashariki. (Na Huo ndio utakuwa wakati wa neema kuhamia Israeli)

Watu hawa ndio wale mashahidi wawili tunaowasoma katika Ufunuo 11, Watahubiri pale Israeli, kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu kama biblia inavyotuambia,..Na wakati huo mpinga-Kristo, atawasikia, na hiyo ndio itakuwa kama alert yake, kuwa mwisho umefika.Atakachofanya ni kufanya vita na hawa watu, na kuleta dhiki Israeli, na duniani kote, hiyo ndio ile dhiki kuu,

Ufunuo 11:3 “Nami nitawaruhusu mashahidi wangu wawili, nao watatoa unabii siku elfu na mia mbili na sitini, hali wamevikwa magunia.

4 Hao ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili visimamavyo mbele za Bwana wa nchi.

5 Na mtu akitaka kuwadhuru, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwala adui zao. Na mtu akitaka kuwadhuru, hivyo ndivyo impasavyo kuuawa.

6 Hao wana amri ya kuzifunga mbingu, ili mvua isinyeshe katika siku za unabii wao. Nao wana amri juu ya maji kuyageuza kuwa damu, na kuipiga nchi kwa kila pigo, kila watakapo.

7 Hata watakapoumaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika kuzimu atafanya vita nao, naye atawashinda na kuwaua”.

Lakini kabla hajafanikiwa, lipo kundi dogo ambalo litasikia injili ya wale mashahidi wawili, na kuondoshwa na kwenda kufichwa, ndio wale wayahudi 144,000, hao watafichwa na dhiki kuu haitawapata (Ufunuo 7&11).

Ufunuo 12:13 “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.

14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.

15 Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule.

16 Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.

17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari”.

Unaona, Lakini wayahudi wengine wote, waliosalia duniani, pamoja na wale watu ambao hawakuipokea chapa ya mnyama, Watapitia dhiki kubwa isiyokuwa na mfano tangu dunia kuumbwa.

Injili inayohubiriwa sasa hivi haiwezi kutikisa au kuleta matatizo duniani, ila kipindi cha injili za hawa manabii wawili watakaposimama, na kutoa unabii pale Israeli, na kwa yale mapigo yaliyoorodheshwa pale ndipo ulimwengu utakapojua rangi halisi ya mpinga-Kristo.

Hawa watu pengine tayari wapo duniani, kwasababu dalili zote zinaonyesha.. Lakini mpaka hayo yote yatokee sisi tuliookoka ambao tumejiweka tayari, tutakuwa siku nyingi tumeshakwenda utukufuni (kanisa halitashuhudia mambo hayo ya manabii wawili). Jiulize na wewe ndugu ikiwa unyakuo utapita leo, wewe utakuwa wapi? Utajisikiaje kuona wenzako wapo mbinguni, wanaona vitu ambavyo jicho halijawahi kuona, na wewe bado upo hapa duniani, kwenye dhiki za mpinga-Kristo, ukizingatia ulihubiriwa injili mara nyingi na hukutaka kusikia?..

Je! bado unadanganywa na manabii wa uongo? Je bado, unapumbazwa na ulimwengu huu unaopita, Je! bado unasita sita kwenye mawazo mawili. Tubu kama bado hujafanya hivyo, ukabatizwe, dunia hii ipo ukingoni. Hatuna muda mrefu sana.?.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI

https://wingulamashahidi.org/ushirikina-na-madhara-yake/

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya Usiwe mwovu kupita kiasi? (Mhubiri 7:17)

Mhubiri 7:17 “Usiwe mwovu kupita kiasi; Wala usiwe mpumbavu; Kwani ufe kabla ya wakati wako?

Mstari huo haumaanishi kuwa uwe mwovu kiasi, hapana, uovu ni uovu tu, na una hukumu, Uwe unatenda dhambi nyingi au chache, ukifa utahukumiwa na jehanum utaenda..

Lakini kinachomaanishwa, hapo ni kuwa upo uovu unaozidi ambao, unaweza kukusababishia uondoke hapa duniani kabla ya siku zako,..Na aina nyingine ya uovu huu ni ule unaendekezwa kwa muda mrefu, pale unapojua madhara yake lakini hutaki kuacha.

Tengeneza picha unafanya kazi ya ujambazi, wa kuua watu kisa mali, unategemea vipi usipigwe risasi siku moja na polisi?

Wale wahalifu waliosulibiwa na Yesu pale msalabani, walijua kabisa yale yamewapata kwasababu ya makosa yao ya uuaji na wizi, na ndio maana mmojawao akasema.

Luka 23:41 “Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa”.

Au unasafirisha madawa ya kulevya, kimataifa, unategemea vipi usikamatwe na kunyongwa? Au unaiba mali za watu na umeonywa mara nyingi auche lakini husikii unategemea vipi usichomwe moto?

Au unamtukana Mungu unategemea vipi uhai wako usifupishwe? n.k n.k.

Au unauchukua utukufu wa Mungu kupita kiasi unategemea vipi Mungu asikuondoe, kwasababu yeye mwenyewe anasema, mimi ni Mungu mwenye wivu. Mtazame Herode alifanya jambo kama hilo, na Mungu anampiga saa ile ile na chango.

Matendo 12:21 “Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi, akatoa hotuba mbele yao.

22 Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu.

23 Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho”.

Huo ni mifano michache ya maovu yanavuka mipaka, au yanayoendekezwa kwa muda mrefu. Umekuwa mzinzi au uasherati, na unajua kabisa tabia hiyo haimpendezi Mungu lakini bado unaendelea kufanya hivyo, siku baada ya siku, hapo unajitafutia mwenyewe Mungu kukupiga na janga la Ukimwi, na kufa kabla ya siku zako.

Mhubiri 7:17 “Usiwe mwovu kupita kiasi; Wala usiwe mpumbavu; Kwani ufe kabla ya wakati wako”?

Hivyo lililo la msingi, ni kujiepusha na uovu kabisa, kwasababu ouvu wowote uwe hata kama huna adhabu hapa, lakini kule utakutana nayo. ambayo ni ziwa la moto.

Warumi 2:5 “Bali kwa kadiri ya ugumu wako, na kwa moyo wako usio na toba, wajiwekea akiba ya hasira kwa siku ile ya hasira na ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu”,

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.

Yuko mwenye haki apoteaye katika haki yake.

Huyu Azazeli ni nani tunayemsoma katika(Walawi 16:8)

Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, alimaanisha hakuwa na wengine?

Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

UNAZO KILA SABABU ZA KUMSHUKURU MUNGU

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.’

Kama unaishi, basi unayo kila sababu ya kumshukuru Mungu, hata kama huna shilingi 10 mfukoni mwako, unazo kila sababu za kumshukuru Mungu.

Kwasababu dakika hii tunayozungumza, wakati wewe unaumwa kichwa tu!..yupo mtu ICU, kapoteza fahamu, yupo mwingine kalazwa unaugua sana. Na wakati pengine wewe upo kitandani umelazwa, ukitafakari matatizo unayoyapitia, kuna mwingine sehemu nyingine ndio yupo katika hatua ya kukata roho.

Wakati wewe hujala tangu asubuhi, yupo mwingine tangu jana hajala kabisa. Wakati wewe unao wazazi na ndugu, yupo mwingine hana hao, yupo peke yake..

Wakati wewe macho yanakusumbua (unavaa miwani), yupo mwingine hana macho kabisa. Wakati unatembea kwa kuchechemea, yupo mwingine hata hiyo miguu hajawahi kuwa nayo. 

Wakati wewe huna fedha wala mali, lakini unao uhuru wa kuamka asubuhi na kwenda unapotaka, wapo wengine sasahivi wamefungwa magerezani na tena kwa miaka mingi, hawana uhuru kama ulionao wewe, wanatamani wangeupata hata walau kwa siku moja tu, lakini hawana… 

Wakati wewe leo siku yako imeenda vizuri, wapo wengine dakika hii hii wapo misibani, wameamka na taarifa za misiba, wanazika wapendwa wao, watu wao wa thamani na wa muhimu. Na sio kwamba wamemchukiza Mungu ndio maana yamewapata hayo hapana! wengine ni watumishi wa Mungu wa thamani kabisa mbele zake, lakini ni wagonjwa, wengine wamefungwa, wengine wametengwa, na wengine hata hawana chakula n.k Lakini wewe hupitii hayo mazito kama ya kwao..Tafakari mara mbili!!..Mshukuru Mungu wala usiwe mtu wa kulalamika kabisa!.

Kitendo cha wewe kuimaliza siku unaishi, huo tayari ni muujiza mkubwa sana. Hivyo katika hali yoyote ile uliyopo, maadamu unao uzima mshukuru Mungu. Siku zote usijilinganishe na yule aliyenacho, bali jilinganishe na yule asiyenacho, ndipo utakapokuwa na kila sababu za kumshukuru Mungu. 

Tena mshukuru Mungu kwa kumwimbia, kumshangilia na kumtolea. Unapofanya hivyo, unaonyesha kumheshimu Mungu na kutambua uwepo wake katika maisha yako. Na pia ni mapenzi ya Mungu sisi tumshukuru yeye.

1Wathesalonike 5:17  “ombeni bila kukoma;  shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu”.

 

Wakolosai 3:15 “…tena iweni watu wa shukrani”.

Siku hizi za kumalizia, shikilia imani kwa nguvu zaidi, kamwe usiruhusu, taabu za dunia kukukatisha tamaa, Mwisho upo karibu sana.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JIOKOE WEWE NA NYUMBA YAKO.

BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics

BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics

YAKINI NA BOAZI.

BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

AINA ZA MAJINI, MAJINA YAO, KAZI ZAO, NA TIBA ZAKE.

Ndugu Msomaji, nakukaribisha katika ukurasa huu kupata maarifa ya rohoni, Awali ya yote nakutahadharisha kuwa mitandaoni kuna elimu nyingi za uongo, Hivyo uisamini kila kitu mtu anachokuambia, kwasababu wengine, hawana nia njema wapo kwa ajili ya kutangazama biashara zao, na hawana lolote la kukusaidia kiroho.

 Sasa turudi katika kutazama majini, na kazi zao.

Nataka ufahamu kuwa ufalme wa Roho, upo katika pande kuu mbili tu!

  1. Upande wa Mungu.
  2. Upande wa Shetani.

Hakuna upande wa hapo katikati..

Upande wa Mungu yupo Mungu mwenyewe pamoja na malaika zake watakatifu. Na upande wa Shetani, Yupo shetani na malaika zake(Mapepo), Haya mapepo ndio wale malaika walioasi mbinguni, na kwa jina lingine wanaitwa MAJINI.

Usidanganywe na mwanadamu yeyote chini ya jua kukwambia kuwa kuna majini wazuri..Huo ni uongo mkubwa sana. Hakuna majini wazuri, majini wote ni roho za mashetani zinazofanya kazi duniani  kuangamiza roho wa watu, na lengo lao kubwa ni kuwapeleka  watu kuzimu..Na ndio maana nakuambia chukua tahadhari mpendwa. Mafundisho ya mashetani yalitabiriwa kutokea sana katika siku hizi za mwisho

1Timotheo 4:1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;

Pengine ulishawahi kukutana na watu wakikueleza juu ya majini wazuri, na wabaya akakutajia mmojawapo kati ya hawa..

  • Jini subiani,
  • Jini Maimuna,
  • Jini Makata,
  • Jini Ruhani,
  • Jini Kabula,
  • Jini Kajadu,
  • Jini Sharifu,
  • Jini Jabari,
  • Jini bahari,
  • Jini Bedui,
  • Jini Zuhura,
  • Jini Zohari,
  • Jini Zamda n.k. n.k.

Haya yote ni mapepo ya kuzimu, na mbali ya kuwapeleka watu kuzimu huwa yanafanya na kazi nyingine pia za kuiharibu dunia na jamii,

  • mengine yanawafanya watu wawe vichaa na kutembea uchi ..

Mathayo 8:28 “Naye alipofika ng’ambo, katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile”.

  • Mengine yawanawafanya watu wawe na ulemavu wa kudumu.

Luka 13:11 “Na tazama, palikuwa na mwanamke aliyekuwa na pepo wa udhaifu muda wa miaka kumi na minane, naye amepindana, hawezi kujinyosha kabisa.

12 Yesu alipomwona alimwita, akamwambia, Mama, umefunguliwa katika udhaifu wako.

  • Wawe mabubu, na vipofu, na viziwi..

Luka 11:14 “Naye alikuwa akitoa pepo bubu; ikawa pepo alipotoka, yule bubu akanena, makutano wakastaajabu”.

  • Mengine yanawafanya watu wasimpende Mungu, pale wanapotakana kusoma biblia, au kusikia mahubiri wanachukia na kuleta vurugu na kutaka kuondoka maeneo hayo.

Luka 8:2 “na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba”,

  • Mengine yanawafanya watu wasifanikiwe, katika mambo yao; Ndoa, biashara, elimu, n.k. n.k.k

Sasa, watu wanawadanganya watu na kuambiwa , jini(Pepo) ukitaka kulituma au  likikuingia, fauta taratibu Fulani za asili kulitoa, labda aidha chukua majivu changanya na hiki au na kile, au andika maneno kwenye karatasi jeupe fanya hivi au vile, au ukilala angalia juu, au chukua udongo wa makaburini uchanganye na maji ya bahari na hiki au kile…Mambo kibao, Na ukifanya hivyo basi utaweza kulitoa jini hilo, au kulituma kufanya kazi Fulani.

Ndugu kama ulishawahi kufanya hivyo, ujue kuwa hukulitoa wala hukulituma, bali ndio umelikaribisha ndani ya maisha yako kukuharibu.

Idadi ya mapepo ulimwenguni ni kubwa sana, na yapo yanazunguka zunguka duniani kila mahali (Ayubu 1:7), hivyo kwa namna moja au nyingine ikiwa hujafahamu njia ya kufanya yasikukurabie basi utateswa sana. Na wengi wanadhani mpaka yawepo ndani yako, ni mpaka yatakapojidhihirisha..Hilo jambo si kweli, Mapepo ni roho, na yanafanya kazi kwa njia nyingi, mtu anaweza kuwa ni jini ndani yake lakini lisijidhirishe hata kidogo, lakini utamjua tu huyo mtu kwa tabia ya kitofauti aliyonayo.

NIFANYE NINI ILI MAJINI YASINIFUATE?

Lakini habari njema ni kuwa, yupo mmoja tu, anayeweza kumtoa mtu Mapepo/Majini kabisa kabisa, Na NI mmoja TU anayeweza kumzuia mtu asisogelewa na hayo maroho ya mashetani ndani yake kabisa kabisa, na huyo mtu si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.

Ikiwa wewe ni Mkristo/muislamu, huna haja ya kuzunguka kwa waganga, au kwa watu wanaojiita mataalamu wakuondolee,au wakufukuzie mapepo katika maisha yako, hao wanakudanganya tu..unamuhitaji YESU..

Yeye pekee yake ndiye aliyeweza kuyatoa majini kama aliweza kuyatoa majini (zaidi ya 82,000) kwa wakati mmoja, kwa mtu ambaye alishindikana katika mji mzima yeye akayatoa .Na saa ile ile Yule kichaa akawa mzima..

Mathayo 8:28 “Naye alipofika ng’ambo, katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile.

29 Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?

30 Basi, kulikuwako mbali nao kundi la nguruwe wengi wakilisha.

31 Wale pepo wakamsihi, wakisema, Ukitutoa, tuache twende, tukaingie katika lile kundi la nguruwe.

32 Akawaambia, Nendeni. Wakatoka, wakaingia katika nguruwe; na kumbe! Kundi lote wakatelemka kwa kasi gengeni hata baharini, wakafa majini”.

Na wewe hivyo hivyo, ukimpokea Yesu leo katika maisha yako, atakufanya kuwa huru..Biblia inasema hivyo katika Yohana 8:36..

Je! Unataka leo Yesu akuokoe?..Kumbuka wokovu sio dini, wokovu sio fedha..Wokovu ni bure kwa watu wote watakaompokea Yesu, Hivyo, kama upo tayari leo akubadilishe, unachopaswa kwanza kufanya ni kukubali kuacha dhambi zako zote,  Kisha unatubu, na baada ya hapo Yesu atayabadilisha maisha yako.

Sasa kabla sijakwenda kukuombea neema ya Yesu, ikuponye hapo hapo ulipo..Fuatisha kwanza hii sala ya Toba, kwa kumaanisha kabisa..

Hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha sema maneno haya kwa Imani,

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuwa na uhalali kwa kuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako.

Sasa upo tayari kuombewa..

Bwana Yesu, wewe ni yeye Yule jana na leo na hata milele, uliwaponya wale, ukaniponya mimi, utamponya na huyu ndugu aliyetubu leo hii.. Nakuomba Bwana Yesu unyooshe mkono wako umguse, roho yake, uyaguse maisha yako, uuguse mwili wako. Chunguza kiungo kimoja hadi kingine, uone ni wapi, pana kasoro umponye Bwana Yesu kama ulivyomponya Yule kichaa. Nguvu zote za giza zinazomsumbua mwili wake, au familia yake, au biashara yake, au ajira yake, leo hii nazitangazia mwisho wake kwa jina lako YESU KRISTO. Natuma moto wa Roho Mtakatifu ukayafunike maisha yake kama ulivyofunika Ayubu kuanzia leo na hata milele.

Asante Bwana Yesu kwa kumponya. Amen.

Sasa ikiwa umefuatisha maelekezo yote, kuanzia hichi kipindi utaanza kuona jinsi Yesu atakavyotembea na wewe maishani mwako. Hivyo usiache kujifunza Neno la Mungu lililo hai. Mwisho kabisa wa somo hili kuna masomo mengine ya kiroho, anza kuyapitia ujifunze ukue kimaarifa.

Pia kama utahitaji msaada zaidi, wa kupata mafundisho ya mara kwa mara kwa njia ya email. Au whatsapp yako, na ubatizo, basi wasiliana nasi kwa namba hizi : +255789001312

Bwana akubariki sana. Na hongera kwa wokovu.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

MAJINI WAZURI WAPO?

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?

MAPEPO YANATAFUTA HIFADHI NDANI YAKO KWA BIDII SANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Orodha ya mistari ya biblia kuhusu watoto.

Mistari ya biblia kuhusu watoto


Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/F1fZHcuNCB69aZsaGFpe3E

Tazama mistari hii, na chini kabisa utapata orodha ya masomo ya kujifunza kuhusu watoto, kwako wewe kama mzazi/mlezi.

Isaya 54:13 “Na watoto wako wote watafundishwa na Bwana; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi”.

Mathayo 19:14 “Lakini Yesu akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu; wala msiwazuie; kwa maana walio mfano wa hao, ufalme wa mbinguni ni wao”.

Wakolosai 3:20 “Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana”.

Mithali 1:8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,

9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako”.

Waefeso 6:1 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.

2 Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,

3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia”.

Luka 2:52 “Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu”.

3Yohana 1:4 “Sina furaha iliyo kuu kuliko hii, kusikia ya kwamba watoto wangu wanakwenda katika kweli”.

Marko 10:15 “Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa.

16 Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabarikia”.

1Timotheo 4:12 “Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi”.

Zaburi 127:3 “Tazama, wana ndio urithi wa Bwana, Uzao wa tumbo ni thawabu”.

Zaburi 34:11 “Njoni, enyi wana, mnisikilize, Nami nitawafundisha kumcha Bwana”.

Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”.

Mithali 22:15 “Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali”.

Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.

Mithali 13:24 “Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema”.

Mithali 19:18 “Mrudi mwanao, kwa maana liko tumaini; Wala usiikaze nafsi yako kwa kuangamia kwake”.

Waebrania 12:11 “Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani”.

Mithali 29:17 “Mrudi mwanao naye atakustarehesha; Naam, atakufurahisha nafsi yako”.

Mithali 17:6 “Wana wa wana ndio taji ya wazee, Na utukufu wa watoto ni baba zao”.

Waefeso 6:4 “Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana”.

Mafundisho muhimu ya wazazi kwa watoto.

Rudi Nyumbani:

Je! utapenda mafundisho ya Neno la Mungu ya kila siku yawe yanakufikia kwa njia ya whatsapp au email yako? Kama ndio, basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312

Print this post

Atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani? Maana yake nini?

SWALI: Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?”


JIBU: Ili tupate picha kamili tuisome habari yake kuanzia juu kidogo, kwasababu Bwana alichokisema kinategemea hiyo habari iliyokuwa juu yake…

Luka 18 :1-8

“1 Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.

2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.

3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.

4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,

5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.

6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.

7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?

8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani”?

Kama tunavyosoma hapo alipomaliza tu kueleza hiyo habari ya huyo mjane ndipo akaongezea na hicho kipenge mwishoni.. “walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani”? Kumaanisha kuwa siku ya kuja kwake anatazamia kuona imani yenye mfano wa huyo mwanamke, kama kigezo cha mtu kunyakuliwa.

Huyo mwanamke, hakuvunjwa moyo, pale alipoona hakuna dalili yoyote ya kutendewa haki na Yule kadhi dhalimu, lakini aliendelea hivyo hivyo tu kila siku kama kipofu, akiamini siku moja atapatiwa haki yake, na mwisho wa siku akaipata, jaribu kujiweka wewe katika mazingira kama hayo, ni wazi utakata tamaa mapema pale unapoona mtu hata haoneshi dalili ya kukusikiliza, unaweza kusema anadharau, lakini kumbe hujui moyoni mwake unamtesa sana.

Vivyo hivyo, katika nyakati hizi za mwisho, nyakati za masumbufu ya maisha, nyakati ambazo watu wengi wamekata tamaa ya kumngojea Yesu, wengine wamerudi kwenye dunia, wengine wanadhihaki wanasema huyo Yesu mnayemsubiria yupo wapi? Kama biblia inavyosema katika..

2Petro 3:3 “Mkijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki, wafuatao tamaa zao wenyewe,

4 na kusema, Iko wapi ahadi ile ya kuja kwake? Kwa maana, tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa”.

Wengine watasema mnamwomba yeye ambaye hawajali..unaona?

Lakini siku atakapokuja Yesu, jambo la kwanza kama alivyosema ni kuwa ataangalia IMANI kwanza, ataaangalia wale waliokuwa na Imani kwake, ambao hawakukatishwa tamaa kuomba ufalme wake uje, (Mathayo 6:9), japokuwa alionekana kama amechelewa, watu ambao hawakuruhusu kurudi nyuma..hao ndio atakaowaangalia..Na hao ndio kitendo cha kufumba na kufumbua watatoweka duniani siku ile.

Wengine wote watabaki hapa duniani, na wale ambao walikuwa wameshakufa tayari, Jicho la Yesu nalo litatazama mpaka kule makaburini, kama mtu alikufa bila imani hiyo, atabakia pale pale makaburini, watakaofufuliwa ni wale tu ambao mpaka dakika ya mwisho ya maisha yao waliishi kama vile Yesu anarudi muda wao, hao ndio watakaosikia sauti yake mwana wa Adam una wataungana na wale walio hai kwa pamoja kwenda kwenye karama ya mwana-kondoo mbinguni.

Lakini swali ni Je! imani hiyo ipo ndani yetu au imeshakufa siku nyingi?..Jibu unalo. Tunachopaswa kufanya sasa, ni kutungeneza mahusiano yetu na Mungu vizuri katika hichi kipindi kifupi cha maisha tulichobakiwa nacho hapa duniani, tujue kalenda ya Mungu duniani sasa ni ipi?…Pale ulimwengu unapozidi kwenda mbali na Imani na kudhihaki sisi ndio tuzidi kuomba na kumlilia Mungu zaidi kama huyu mjane..

Na siku moja isiyokuwa na jina, kitendo cha kufumba na kufumbua, tutajiona pale mawingu na majeshi ya malaika wengi yamekuja kutulaki, na parapanda ya Mungu. Itakuwa ni raha isiyo na kifani, maneno ya kibinadamu hayawezi kuelezea. Hivyo tuishi kwa Imani Bwana atakapokuja aione ndani yetu.

Jina la Bwana libarikiwe Milele.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

REKEBISHA YAFUATAYO ILI MAMBO YAENDE SAWA.

Uwanda wa dura ni nini?

JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.

Mlima sinai upo nchi gani? Na Je unaijua Sinai yako ya rohoni?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nifanye nini ili niishi maisha ya ushindi siku zote?

Maisha ya ushindi


Shalom,

Awali ya yote ni lazima ufahamu kuwa kupita katika majaribu, kupita katika dhiki, kupita katika mateso, haimaanishi kuwa umeshindwa, hapana hivyo vyote vinaitwa vita,..Kushindwa ni pale, vita hivyo vinapokuzidi nguvu na hatimaye kukuangusha kabisa..hapo ndio umeshindwa.

Kwasababu kama ingekuwa kila anayepitia majaribu au dhiki au shida, au bonde la mauti ni kushindwa, basi Daudi angekuwa wa kwanza, kwasababu yeye, kila kukicha alikuwa anapita katika hali ya kukimbizwa na maadui zake na hatari za kufa, mpaka wakati mwingine anakwenda kuomba msaada kutoka kwa maadui zake wengine ili tu wampe hifadhi kwa muda. Lakini katika yote alikuwa na uhakika kuwa maisha yake ni ya ushindi tu..mpaka akaandika katika Zaburi 23 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu…. Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”. (Zab 23)

Na kweli kama tunavyojua mwisho wa siku aliibuka mshindi, na kuwa mfalme wa Israeli, na mpaka sasa habari zake tunazisoma,

Hata Bwana wetu Yesu,vivyo hivyo alijaribiwa kama sisi tulivyojaribiwa, hata zaidi ya sisi lakini katika majaribu yake yote, hakuwahi kushindwa na hata moja, wala hakuwahi kutenda dhambi.. Na ndio maana akatuambia..

Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.

Unaona? Na watakatifu wengine wote kwenye biblia hivyo hivyo..

Lakini siri ya ushindi wao ilikuwa ni nini?

Je ni nguvu zao? Au bidii zao? Au ni nini.. Biblia imeshatoa jibu na kusema, mtu anayeweza kuushinda ulimwengu,(kuishi maisha ya ushindi) ni mtu Yule ambaye amezaliwa na Mungu tu.

1Yohana 5:4 “Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu”.

Unaona?, Ni mtu tu aliyezaliwa na Mungu ndio anapokea uwezo huo wa kuushinda ulimwengu, si mtu mwingine yeyote, nguvu za mtu binafsi haziwezi, bidii za mtu haziwezi, fedha ya mtu haiwezi, wala kipaji cha mtu hakiwezi kuushinda ulimwengu.

Huwezi kumshinda shetani atakapokuletea majaribu kama hujazaliwa na Mungu (yaani hujazaliwa mara ya pili), haiwezekani kuushinda uzinzi, haiwezekani kuishinda dhambi ile inayokusumbua, ni ngumu kuwashinda wachawi na mapepo, vilevile ni ngumu kuishi maisha ya amani na furaha hapa duniani.

Kwasababu Mungu anakuwa hayupo upande wako kukutia nguvu..Lakini wale ambao Mungu yupo ndani yao..biblia inasema hivi.

Warumi 8:31 “Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?

32 Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?

33 Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.

34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.

35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga”?

Kwa mtu aliyezaliwa mara ya pili kunakuwa na nguvu Fulani ya ajabu kutoka kwa Mungu inayomlinda asitetereke pindi unapopitia majaribu mazito ulimwenguni.

Hivyo ukiwa kama hujaokoka, au ulikuwa upo nusu nusu, (yaani mguu mmoja nje,mwingine ndani) na ndio maana maisha yako yamekuwa ni ya kushindwa kudumu katika wokovu, ya kushindwa kusimama, ya kushindwa kuwa na mahusiano mazuri na Mungu. Basi leo hii fanya uamuzi thabiti wa kumpa Yesu maisha yako upya kwa kumaanisha kabisa.

1Yohana 1:9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote”.

Kama upo tayari kumruhusu Yesu ayaunde upya maisha yako, basi uamuzi huo ni wa busara, sana, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba. Na pia kama unahitaji kubatizwa pia usisite kuwasiliana nasi .>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Ikiwa umefungua na kufuata hayo maelekezo hapo juu, basi mpaka hapo tayari ushindi wa kwanza umepata wa mauti..

1Wakorintho 15:55 “Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako?

Vilevile wachawi na mapepo hawatakuweza, kwa lolote..

Kuanzia huo  wakati utakapobatizwa na kuendelea utaanza kuona mabadiliko ya tofauti katika maisha yako,.Sina mengi ya kusema, wewe mwenyewe utayashuhudia.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye  namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

HIZI NI NYAKATI ZA KUJIINGIZA KWA NGUVU.

OLE WAO WANAOJITAHIDI KUMFICHA BWANA MASHAURI YAO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

KUZIMU NI WAPI

Rudi Nyumbani:

Print this post

JIFUNZE KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo lizidi kubarikiwa.

Karibu tujifunze Neno la Mungu wetu.

Kama ni msomaji mzuri wa Biblia utakuwa unayajua majaribu matatu ya Yesu aliyojaribiwa na Ibilisi kule jangwani. Jambo la ajabu ni kwamba shetani hakwenda kumjaribu Bwana Yesu kwa uchawi, au kwa magonjwa au kwa maneno yake, bali alikwenda kumjaribu kwa kutumia maandiko matakatifu.

 Maana yake ni kwamba kitengo kikubwa cha Majaribu ya shetani kwa mkristo hakipo kwa wachawi, au kwa waganga wa kienyeji kama watu wengi wanavyofikiri,  BALİ KİPO KATİKA NENO LA MUNGU. Na shetani hatumii nguvu nyingi kututumia majeshi ya wachawi wake kama unavyohubiriwa na watu, bali anatumia nguvu kubwa kuhakikisha kwamba hulielewi Neno la Mungu, na hapo akifanikiwa basi unakua umekwisha!.. Bwana wetu Yesu asingekuwa analijua Neno kweli kweli, basi asingemweza shetani kamwe..Lakini shetani hakumweza kwasababu yeye ndio aliyekuwa Neno mwenyewe.

Wengi wetu tunakosa shabaha hapo, Tukidhani uadui mkubwa wa shetani kwetu ni waganga wa kienyeji na wachawi wanaotuzunguka…jambo linalompelekea Mkristo kutwa kuchwa kupambana na wachawi katika maombi.. Na kusahau kuwa silaha yake kubwa ni Neno la Mungu (Ndio upanga) Waefeso 6:17. Na pasipo kujua kuwa asipokuwa na Neno la Mungu la kutosha ndani yake basi tayari anakuwa kalogwa na shetani siku nyingi (Wagalatia 3:1)..Hata kama atakuwa anasali na kupiga maombi ya vita kila siku.

Sasa hebu tusome kwa ufupi jinsi Bwana alivyomjibu shetani katika yale majaribu na kisha tutajifunza kitu cha muhimu sana. Usipite hata kama ulishasoma rudia tena.

Mathayo 4:1  “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi. 

2  Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa. 

3  Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate. 

4  Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu. 

5  Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu

6  akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 

7  Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako. 

8  Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, 

9  akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia. 

10  Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. 

11  Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia”

Kama tunavyojua maneno yote shetani aliyomwambia Bwana Yesu hapo , hayakuwa ya UONGO! Yote yalikuwa ya kweli na yapo katika biblia, yalikuwa ni maneno ya Mungu yenye pumzi ya uhai (hivyo upo ukweli unaopotosha)…na yote shetani aliyatoa katika biblia..Kwamfano hilo Neno “Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua” Ni Neno la Zaburi 91:12.

Lakini shetani aliyapindisha yale maneno na kuyafanya yatumike mahali ambapo sio sahihi, na kwa wakati usio sahihi. Maneno ya Mungu yakitumika mahali ambapo sio sahihi na kwa wakati ambao sio sahihi yanakuwa ni sumu kubwa.

Kwamfano Neno la Mungu ni kweli linasema.. “waume waishi na wake zao kwa akili na kumpa mke heshima (1Petro 3:7)”..Sasa Neno hili linawahusu Wanaume waliooa ndoa halali ya kimaandiko…Na si mtu yeyote tu hata anayeishi na girlfriend wake. Nimewahi kukutana na watu wanaoishi pasipo kuonana na wanautumia huu mstari kwa madai kwamba Mungu amesema “tuishi na wake kwa akili”. Nimewahi kukutana na mwingine akiwashawishi wanawake kufanya nao uzinzi huku akitumia hichi kipengele cha maandiko.. 1Wakorintho 7:5 “Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu”.

Hivyo mwanamke yeyote anayekutana naye anakimbilia kumwonyesha huu mstari, na kusema hata Mungu amesema “tusinyimane” na amefanikiwa kuwanasa mabinti wengi kwa andiko halo…Pasipo kufahamu kuwa hilo andiko linawahusu wana-ndoa tu!(watu ambao tayari wameoana) na sio kila mtu tu!.

Sasa shetani alimjia Yesu kwa njama hiyo hiyo, kuyaweka maneno ya Mungu mahali pasipopaswa na kwa wakati usiofaa.

Anamwambia Bwana ajitupe chini na Mungu atamwagizia malaika waje wamchukue asijikwae…Ni kweli hilo ni Neno la Mungu, lakini huo sio wakati wake..Neno hilo litafaa kutumika wakati ambao tumejikuta tumeingia majaribuni au hatarini pasipo hiari yetu, huo ndio wakati wa Bwana kuwaagiza malaika zake watuchukue. Lakini sio wakati ambao tupo salama halafu tunamjaribu Mungu tuone atafanya nini, tukifanya hivyo tunajitafutia laana badala ya baraka..

Na sisi tunapaswa tujifunze KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU. Na hiyo inakuja kwa kulisoma Neno la Mungu kwa bidii. Ukisoma kijimstari kimoja tu na kwenda kulala! Ni rahisi kushindwa kuyagawanya Maneno ya Mungu ipasavyo..

Na pia usitumie nguvu kubwa kuchunguza mchawi wako ni nani?.. Tumia nguvu kubwa kuyachunguza maandiko!!…Je biblia inasema nini katika hali hiyo unayopitia?..Je katika biblia kuliwahi kutokea kisa kama hicho unachopitia na je kilitatuliwaje?.. Unapoona kuna kitu fulani hakipo sawa, tafuta kujua je! Biblia inasemaje kuhusu hiyo hali.. Usisubiri kufundishwa-fundishwa biblia, jifunze kuisoma mwenyewe..Utakutana na mambo mengi huko, ambayo hata mchungaji wako hawezi kukuhubiria, na pia utagundua ni vitu gani ulikuwa unapotoshwa na vitu gani ulikuwa unaambiwa ukweli.

Lakini ukisubiri tu kila somo unalokutana nalo mitandanoni, ni kulisoma tu, kwasababu mtumishi yule anaaminika na wengi!, au kila hubiri ni kusikiliza tu kwasababu mtumishi yule anasifiwa na wengi. Nataka nikuambie, utaishia kukosa mahali pa kusimamia, utakuwa ni mtu wa kupepesuka daima. Na kutufuta mchawi ni nani kwenye ukoo wako, kumbe uchawi ni kukosa kwako maarifa ya Neno la Mungu.

Hosea 4:6 “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa;..”

Soma Biblia mwenyewe huo ndio uthibitisho wa kwanza wa kwamba umeamua kuanza safari ya kumjua Mungu.

Na Bwana akubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

UPONYAJI WA ASILI

JIOKOE WEWE NA NYUMBA YAKO.

MASOMO MBALIMBALI YA NENO LA MUNGU.

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Jiepushe na tamaa ya Mali/kupenda fedha.

Kwa namna ya kawaida fedha haina ubaya wowote, ni nyezo ambayo Mungu aliiruhusu iwepo na itumiwe ili kuendesha kushughuli zote za kijamii.

Mhubiri 19:19 “…Na fedha huleta jawabu la mambo yote”.

Lakini kitendo cha kupenda fedha, hicho ndicho Mungu amekikatazata, na katika biblia kimekemewa sana, ikiwa wewe ni mtoto wa Mungu, na roho ya kupenda fedha ipo ndani yako, basi upo hatarini sana, kuzama katika maovu mengi..biblia inasema hivyo..

1Timotheo 6:10 “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.”

Ndio maana biblia inawaasa sana watoto wa Mungu na kuwaambia..

Waebrania 13:5 “Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa”.

Mungu ametoa ahadi ya kuwahudumia watoto wake, kiasi kwamba hawatapungukiwa kabisa, hawatakosa kabisa ikiwa tu watakuwa watulivu katika shughuli zao.

Mtu mwenye tabia ya  kupenda fedha ni rahisi kuhonga, ili upate fursa Fulani,ni rahisi kufanya biashara haramu kisa tu ameona  zinamwingizia  fedha nyingi, mwingine atakuwa radhi hata kujiuza mwili wake kisa fedha, wengine wanakwenda kwa waganga, wengine wapo tayari kuikana imani,..n.k.n.k. hapo ndipo unajua ni kwanini biblia inasema kupenda fedha ni shina la mabaya yote ulimwenguni. Wengine wapo tayari hata kuua watu, ili walipwe au waibe.

Mithali 1:19 “Ndivyo zilivyo njia za kila mwenye tamaa ya mali; Huuondoa uhai wao walio nayo”.

Na dalili mojawapo ambayo biblia inasema itatutambulisha kuwa tunaishi katika siku za mwisho, ni kuibuka kwa wimbi kubwa la watu wanaopenda fedha.

2Timotheo 3:1 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.

2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,”

Mpaka sasa, imefikia hatua huduma za rohoni kutolewa kwa fedha,

1Timotheo 6: 5 “na majadiliano ya watu walioharibika akili zao, walioikosa kweli, huku wakidhani ya kuwa utauwa ni njia ya kupata faida”.

Hiyo yote ni matokeo ya wanadamu kupenda fedha..Bwana Yesu alisema..

Mathayo 6:24 “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali”.

Shetani alijua hapa ndipo wanadamu wengi wanapoweza kunaswa, hivyo, akatumia  njia hiyo hiyo kumjaribia pia Yesu, akamwambia nitakupa milki zote za ulimwenguni, nitakupa fedha zote na majumba yote ikiwa utanisujudia tu. Lakini Bwana Yesu alimkemea akamwambia utamsujudia Bwana Mungu wako tu.. Kwasababu alijua kupenda fedha ni kuupenda ulimwengu.

1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake”.

Kama hiyo haitoshi Wenye mali, bado biblia inawapa nafasi ndogo sana ya kuurithi ufalme wa mbinguni;

Mathayo 19:23 “Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni.

24 Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu”.

Vifungu vipo vingi sana kwenye biblia vinavyozungumzia hatari za kupenda fedha., hatuwezi kuviweka vyote hapa, lakini kwa hivyo vichache  kama na wewe ni mmojawapo, basi geuka haraka sana, uridhike na vile Mungu anavyokupa, kwasababu biblia inasema..

Mhubiri 5:10 “Apendaye fedha hatashiba fedha, Wala apendaye wingi hatashiba maongeo. Hayo pia ni ubatili”.

Na pia inasema.

Zaburi 37:16 “Kidogo alicho nacho mwenye haki ni bora Kuliko wingi wa mali wa wasio haki wengi”.

Chuma kidogo kidogo utafanikiwa..

Mithali 13:11 “Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa”.

Lakini kama wewe hujaokoka, ukweli ni kwamba hii roho ya kupenda fedha haiwezi kuondoka ndani yako, hata iweje,  itaondoka, ikiwa tu utamruhusu Bwana Yesu aingie ndani yako aibadilishe Nia yako..

Akishakubadilisha hapo ndipo  Roho ya kuridhika na ya utulivu itaingia ndani yako, na hapo hapo Mungu ataanza kukufundisha njia sahihi na yenye Baraka ya kukusanya..mpaka mwisho wa siku atakufikisha pale anapotaka uwepo. Na zaidi ya yote utaurithi uzima wa milele.

Hivyo kama upo tayari leo hii kutubu dhambi zako, unahitaji kuokoka, uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana basi, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.

YONA: Mlango 1

UNYAKUO.

UTAWALA WA MIAKA 1000.

EPUKA MUHURI WA SHETANI

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mshulami ni msichana gani?

Mshulami ni jina Sulemani alilompa msichana ambaye alikuwa naye katika mahusiano kama tunavyosoma katika kitabu cha wimbo ulio bora, alimwita hivyo kutokana na kuwa eneo alilotokea lilitwa  Shulami,

Wimbo 6:13 “Rudi, rudi, Mshulami, Rudi, rudi, ili sisi tukutazame. Kwani mnataka kumtazama Mshulami, kama kutazama ngoma ya Mahanaimu?


Fahamu zaidi:

Je unajua ni kwa nini Mariamu aliitwa Mariamu magdalene? >>> Mariamu Magdalene

Mlima Sinai upo nchi gani? >> Mlima sinai

Mti wa mlozi ni mti gani>>>> Fimbo ya haruni -mti wa mlozi

Kwanini Yesu alisema wacheni wafu wazike wafu wao? >>> Wafu wazike wafu wao

Amin, Amin, nawaambia kizazi hiki hakitapita >>> Kizazi hiki hakitapita,

Mitume wa Yesu walikufaje >>> Vifo vya mitume wa Yesu

Rudi Nyumbani:

Print this post