Orodha ya mistari ya biblia kuhusu watoto.

by Admin | 30 August 2020 08:46 am08

Mistari ya biblia kuhusu watoto


Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/F1fZHcuNCB69aZsaGFpe3E

Tazama mistari hii, na chini kabisa utapata orodha ya masomo ya kujifunza kuhusu watoto, kwako wewe kama mzazi/mlezi.

Isaya 54:13 “Na watoto wako wote watafundishwa na Bwana; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi”.

Mathayo 19:14 “Lakini Yesu akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu; wala msiwazuie; kwa maana walio mfano wa hao, ufalme wa mbinguni ni wao”.

Wakolosai 3:20 “Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana”.

Mithali 1:8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,

9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako”.

Waefeso 6:1 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.

2 Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,

3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia”.

Luka 2:52 “Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu”.

3Yohana 1:4 “Sina furaha iliyo kuu kuliko hii, kusikia ya kwamba watoto wangu wanakwenda katika kweli”.

Marko 10:15 “Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa.

16 Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabarikia”.

1Timotheo 4:12 “Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi”.

Zaburi 127:3 “Tazama, wana ndio urithi wa Bwana, Uzao wa tumbo ni thawabu”.

Zaburi 34:11 “Njoni, enyi wana, mnisikilize, Nami nitawafundisha kumcha Bwana”.

Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”.

Mithali 22:15 “Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali”.

Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.

Mithali 13:24 “Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema”.

Mithali 19:18 “Mrudi mwanao, kwa maana liko tumaini; Wala usiikaze nafsi yako kwa kuangamia kwake”.

Waebrania 12:11 “Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani”.

Mithali 29:17 “Mrudi mwanao naye atakustarehesha; Naam, atakufurahisha nafsi yako”.

Mithali 17:6 “Wana wa wana ndio taji ya wazee, Na utukufu wa watoto ni baba zao”.

Waefeso 6:4 “Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana”.

Mafundisho muhimu ya wazazi kwa watoto.

Rudi Nyumbani:

Je! utapenda mafundisho ya Neno la Mungu ya kila siku yawe yanakufikia kwa njia ya whatsapp au email yako? Kama ndio, basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/08/30/orodha-ya-mistari-ya-biblia-kuhusu-watoto/